Nyetk
JF-Expert Member
- Feb 28, 2012
- 1,648
- 1,696
Nilikuwa na timu ya wenzangu kikazi mikoa ya kusini - Lindi na Mtwara kwa siku mbili, sasa tukiwa tunarejea Dar usiku wa kuamkia tarehe 3 August 2012 tuliingia Dar tumechelewa kidogo (kama majira ya saa tano hivi usiku). Wenzangu wakapendekeza kuegeshe mahali fula tupate chakula kabisa kabla gari haijatusambaza kila mtu kwake. "Good idea!", wote tuliunga mkono. Hapo tulishaingia mitaa ya Keko, na mwenzetu mmoja mwenyeji wa mitaa hiyo akatuongoza hadi "National Hotel".
Wow! tukakuta kikundi cha promotion ya bia ya "Windhoek" wakiwa jukwaani. tukakaa, tukaagiza chakula. Meza ya jirani yetu palikuwepo watu watatu: wanaume wawili na kabinti kamoja, na mmoja wao alionekana anatawala meza kwa jinsi alivyokuwa anazimwaga windhock. Mkuu wa meza ndo alionekana anamawasiliano ya karibu na yule binti pekee kwenye meza.
Ghafla akaingia kwa kasi binti/mama mmoja kabeba mtoto mgongoni (anayeonekana si mtoto wa kubebwa na mamaye mgongoni kwa ukubwa wake katika hali ya kawaida), na ndipo picha ikaanza. Akaenda moja kwa moja kwa mkuu wa meza na kumshushia valangati!
"Unafanya nini hapa?" Jamaa kimya, kaduwaa!
"Nakuuliza unafanya nini hapa?" Kamwasha kibao!
"Mbona hunijibu, unafanya nini hapa?" Kibao kingine cha nguvu zaidi; jamaa bado kimya tu. Yule mama akachukua glasi ya pombe ya yule binti aliyemkuta mezani akamwagia mumewe yote. Jama kimya tu utadhani yupo kwenye friji!
"Wewe nakupigia tangu saa kumi na mbili jioni hupokei unajua nakupigia kwa sababu gani? Mbwa wee!" Kibao kingine! Yule rafiki wa mkuu wa meza kaamka, anamtuliza huyo mama.
"Shemeji, huyu anamwaga ofa hapa, ebu muulize nyumbani ameacha hata elfu moja, mbwa huyu?" Kibao kingine - na jamaa amekaa tu kwenye kiti! "Mshenzi mkubwa! Badala ya kuwaza mambo ya maeneleo unakaa kuwaza ujinga tu!" (Hii sentesi ya mwisho aliirudia mara nyingi).
Picha iliendelea kwa muda na wakati wote jamaa yuko kwenye kiti. Huyu mama mtoto pamoja na vurumai zote alionyesha kufanya kwa stara kubwa bila kupiga makelele, ila alikuwa anaongea kwa sauti ya chini bila kuvuruga amani ya wasiohusika (ku-attract attention); hakumtukana wala kumpiga yue binti aliyemkuta na bwana wake (ingawa huyo binti aliepaniki sana), kitu kilichonipa kufikiri kuwa huyu mama mtoto kimsingi si mtu mkorofi kwa asili. Hatimaye yule kijana mwingine akawatuliza na akamudu kuwashawishi wakaondoka wote.
Jina la mfumaniwa halikujulikana ila yule rafiki yake alikuwa anatajwa na mfumaniaji kwa jina la Mwita.
MY TAKE:
Wadau, najua kesi za namna hii na kuzidi ni za kawaida sana kwenye jamii, hata mimi nimeshuhudia senema nzito kuliko hii. Ninachojiuliza ni kwamba, ni nini huwa kinatokea kwa wamaume kisaikolojia wanapokuwa wamefumaniwa hata wakose uwezo wa kujitetea hata kwa ku-act au kudanganya???? Leo nashuhudia rafiki ya "Mwita" anapigwa makofi sita, anamwagiwa pombe na kutukwanwa "mbwa" mara sita, "mshenzi" mara nyingi, "mpumbavu" mara nyingi..... na binti ambaye kwa mwonekano si mmbabe (alikuwa anaonekana mpole sana kwa kweli) na njemba haiwezi hata kujibu kivyovyote?
Najua wanaume wenzangu wengi mmekumbwa na balaa la kufumaniwa; na akinadada/mama wengi mmewafumania/mmewabamba waume zenu na wanaume daima walikuwa wapole. Ebu mwagikeni; ni nini huwa kinawafanya wanaume wawe hivi?
Wow! tukakuta kikundi cha promotion ya bia ya "Windhoek" wakiwa jukwaani. tukakaa, tukaagiza chakula. Meza ya jirani yetu palikuwepo watu watatu: wanaume wawili na kabinti kamoja, na mmoja wao alionekana anatawala meza kwa jinsi alivyokuwa anazimwaga windhock. Mkuu wa meza ndo alionekana anamawasiliano ya karibu na yule binti pekee kwenye meza.
Ghafla akaingia kwa kasi binti/mama mmoja kabeba mtoto mgongoni (anayeonekana si mtoto wa kubebwa na mamaye mgongoni kwa ukubwa wake katika hali ya kawaida), na ndipo picha ikaanza. Akaenda moja kwa moja kwa mkuu wa meza na kumshushia valangati!
"Unafanya nini hapa?" Jamaa kimya, kaduwaa!
"Nakuuliza unafanya nini hapa?" Kamwasha kibao!
"Mbona hunijibu, unafanya nini hapa?" Kibao kingine cha nguvu zaidi; jamaa bado kimya tu. Yule mama akachukua glasi ya pombe ya yule binti aliyemkuta mezani akamwagia mumewe yote. Jama kimya tu utadhani yupo kwenye friji!
"Wewe nakupigia tangu saa kumi na mbili jioni hupokei unajua nakupigia kwa sababu gani? Mbwa wee!" Kibao kingine! Yule rafiki wa mkuu wa meza kaamka, anamtuliza huyo mama.
"Shemeji, huyu anamwaga ofa hapa, ebu muulize nyumbani ameacha hata elfu moja, mbwa huyu?" Kibao kingine - na jamaa amekaa tu kwenye kiti! "Mshenzi mkubwa! Badala ya kuwaza mambo ya maeneleo unakaa kuwaza ujinga tu!" (Hii sentesi ya mwisho aliirudia mara nyingi).
Picha iliendelea kwa muda na wakati wote jamaa yuko kwenye kiti. Huyu mama mtoto pamoja na vurumai zote alionyesha kufanya kwa stara kubwa bila kupiga makelele, ila alikuwa anaongea kwa sauti ya chini bila kuvuruga amani ya wasiohusika (ku-attract attention); hakumtukana wala kumpiga yue binti aliyemkuta na bwana wake (ingawa huyo binti aliepaniki sana), kitu kilichonipa kufikiri kuwa huyu mama mtoto kimsingi si mtu mkorofi kwa asili. Hatimaye yule kijana mwingine akawatuliza na akamudu kuwashawishi wakaondoka wote.
Jina la mfumaniwa halikujulikana ila yule rafiki yake alikuwa anatajwa na mfumaniaji kwa jina la Mwita.
MY TAKE:
Wadau, najua kesi za namna hii na kuzidi ni za kawaida sana kwenye jamii, hata mimi nimeshuhudia senema nzito kuliko hii. Ninachojiuliza ni kwamba, ni nini huwa kinatokea kwa wamaume kisaikolojia wanapokuwa wamefumaniwa hata wakose uwezo wa kujitetea hata kwa ku-act au kudanganya???? Leo nashuhudia rafiki ya "Mwita" anapigwa makofi sita, anamwagiwa pombe na kutukwanwa "mbwa" mara sita, "mshenzi" mara nyingi, "mpumbavu" mara nyingi..... na binti ambaye kwa mwonekano si mmbabe (alikuwa anaonekana mpole sana kwa kweli) na njemba haiwezi hata kujibu kivyovyote?
Najua wanaume wenzangu wengi mmekumbwa na balaa la kufumaniwa; na akinadada/mama wengi mmewafumania/mmewabamba waume zenu na wanaume daima walikuwa wapole. Ebu mwagikeni; ni nini huwa kinawafanya wanaume wawe hivi?