BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
Usiku huu nimeshindwa kuomba! Nimejikuta nikitokwa na machozi! Si machozi ya huzuni wala si machozi ya furaha! Ni machozi ya mshangao nikimshangaa Mungu! Nilikuwa nikitaka kuwaombea baadhi ya viongozi akiwemo Rais mpya wa Zambia! Ilipofika zamu yake nihimizwa moyoni kuwa niangalie kwanza taarifa za Zambia kabla sijaomba! Macho yangu yamekutana na taarifa iliyonigusa.
Taarifa hiyo imenifanya nishindwe kuendelea kuomba kutokana na mshangao. Macho yangu yameshuhudia Rais Hakainde Hichilema akimuapisha Naibu Kamishina Generali wa Jeshi la Magereza nchini Zambia! Hichilema alipokuwa Kiongozi wa Chama cha Upinzani, alikamatwa na kutupwa Gerezani. Alifunguliwa Mashtaka ya ugaidi/uhaini. Alipokuwa Gerezani, wakati Wakuu wengi wa vyombo vya dola wakimnyanyasa, kulikuwa na kijana mmoja Afisa wa Jeshi la Magereza aliyeamua kutenda haki. Katika mazingira yale magumu yule Afisa Magereza alijitofautisha na wengine waliokuwa 'wanauabudu' mfumo kandamizi!
Sasa Hichilema ndiye Rais wa Zambia! Amempandisha cheo yule kijana kuwa Naibu Kamishina Generali wa Jeshi la Magereza, cheo kinachofuata baada ya Kamishina Generali. Kabla ya kumuapisha, Rais Hichilema alisimulia mazingira magumu ya Gerezani. Simulizi yake ndiyo iliyoniliza! Kwa kiasi ninaelewa maana ya kuwekwa nyuma ya kuta. Ingawa sikuwahi kulala Magereza, lakini nimelala katika Mahabusu za Polisi. Nililala Central Police Dar es Salaam na nililala Kituo cha Polisi Kirumba, Mwanza. Pia, nimekuwa nikipata taarifa za mahabusu wa kisiasa kutoka sehemu nyingi nchini na kuwapazia sauti.
Natamani ujumbe huu uwafikie Askari wa Jeshi la Polisi na Jeshi la Magereza nchini Tanzania. Hivi wanaelewa kuwa hao wanaopita mikononi mwao kama watuhumiwa, mahabusu au wafungwa siku moja baadhi yao wanaweza kuwa wakuu wao? Wakijua hivyo watakuwa na utu katika kutimiza majukumu yao! Ukiamka kesho, hakikisha ujumbe huu anasoma kila aliye Askari katika Majeshi tajwa, kuanzia mdogo hadi mkubwa. Wakuu wanaoshika nafasi za utukufu katika Wilaya, Mikoa, Wizara na hata Ikulu wasiache kusoma nao wasome!
Wekeni ujumbe huu kwenye magrupu yenu ili kila mtu ausome. Hivi utamuangaliaje yule uliyemnyanyasa endapo ndiye atakayekuja kuwa kiongozi na mkuu wako kesho baada ya mapambazuko? Hivi utajisikiaje Kama yule uliyemsingizia na kumbambikia Kesi endapo ndiye atakayekuja kuwa na mamlaka juu yako?
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula
Taarifa hiyo imenifanya nishindwe kuendelea kuomba kutokana na mshangao. Macho yangu yameshuhudia Rais Hakainde Hichilema akimuapisha Naibu Kamishina Generali wa Jeshi la Magereza nchini Zambia! Hichilema alipokuwa Kiongozi wa Chama cha Upinzani, alikamatwa na kutupwa Gerezani. Alifunguliwa Mashtaka ya ugaidi/uhaini. Alipokuwa Gerezani, wakati Wakuu wengi wa vyombo vya dola wakimnyanyasa, kulikuwa na kijana mmoja Afisa wa Jeshi la Magereza aliyeamua kutenda haki. Katika mazingira yale magumu yule Afisa Magereza alijitofautisha na wengine waliokuwa 'wanauabudu' mfumo kandamizi!
Sasa Hichilema ndiye Rais wa Zambia! Amempandisha cheo yule kijana kuwa Naibu Kamishina Generali wa Jeshi la Magereza, cheo kinachofuata baada ya Kamishina Generali. Kabla ya kumuapisha, Rais Hichilema alisimulia mazingira magumu ya Gerezani. Simulizi yake ndiyo iliyoniliza! Kwa kiasi ninaelewa maana ya kuwekwa nyuma ya kuta. Ingawa sikuwahi kulala Magereza, lakini nimelala katika Mahabusu za Polisi. Nililala Central Police Dar es Salaam na nililala Kituo cha Polisi Kirumba, Mwanza. Pia, nimekuwa nikipata taarifa za mahabusu wa kisiasa kutoka sehemu nyingi nchini na kuwapazia sauti.
Natamani ujumbe huu uwafikie Askari wa Jeshi la Polisi na Jeshi la Magereza nchini Tanzania. Hivi wanaelewa kuwa hao wanaopita mikononi mwao kama watuhumiwa, mahabusu au wafungwa siku moja baadhi yao wanaweza kuwa wakuu wao? Wakijua hivyo watakuwa na utu katika kutimiza majukumu yao! Ukiamka kesho, hakikisha ujumbe huu anasoma kila aliye Askari katika Majeshi tajwa, kuanzia mdogo hadi mkubwa. Wakuu wanaoshika nafasi za utukufu katika Wilaya, Mikoa, Wizara na hata Ikulu wasiache kusoma nao wasome!
Wekeni ujumbe huu kwenye magrupu yenu ili kila mtu ausome. Hivi utamuangaliaje yule uliyemnyanyasa endapo ndiye atakayekuja kuwa kiongozi na mkuu wako kesho baada ya mapambazuko? Hivi utajisikiaje Kama yule uliyemsingizia na kumbambikia Kesi endapo ndiye atakayekuja kuwa na mamlaka juu yako?
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula