Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,339
- 51,863
HAKI HAIPO CHADEMA WALA CCM, JAMII IPO GIZANI.
Kwa Mkono wa, Robert Heriel.
Haki hutofautiana baina ya nchi na Nchi. Ingawaje zipo haki za ujumla za kila mwanadamu Kama vile Haki ya kuishi na kupata nyezo zinazomfanya mtu aishi.
Haki hutofautiana baina ya nchi na Nchi kutokana na utashi, utamaduni, elimu, mazingira, Aina ya jamii husika, miongoni mwa mambo mengine.
Pengine ili nieleweke zaidi, napaswa Kueleza Kwa kifupi maana ya HAKI;
Neno Haki kwa tafsiri ya kamusi ya Kiswahili sanifu lina maana ya ‘jambo ambalo mtu anastahiki au kitu anachostahili kuwa nacho.
Kwa tafsiri ya kamusi ya kisheria neno Haki lina maana ‘ kile mtu anachostahili kuwa nacho au kile anachoruhusiwa kufanya, au kile anachostahili kupokea kutoka kwa wengine kwa mujibu wa sheria’.
Kwa maana hizo zote mbili, tunaona kuwa Haki imejikita zaidi katika Utashi wa watu, mtazamo, elimu na utamaduni wa jamii.
Haki ya Zama hizi haiwezi kuwa Haki ya zama zijazo.
Hii ni kusema, haki huathiriwa na Wakati pia.
Haki huathiriwa na Wakati kutokana na sababu kuwa Mitazamo, utashi na utamaduni wa watu hubadilika kulingana na wakati.
Msingi wa haki kidunia umejikita zaidi katika Sheria za jamii husika, sheria za nchi. Hata hivyo sheria za nchi ni matokeo ya utashi na Mitazamo ya watu katika kipindi husika.
Katika Siasa za nchi yetu, haki hutafsiriwa kulingana na mtu yupo upande gani, utashi na mtazamo wake.
Mwana CCM anatafsiri yake ya HAKI, halikadhalika na mwana CHADEMA na watu wa vyama vingine, sio ajabu kila chama kinakatiba na sheria zake. Kumaanisha vile kinavyoona na kutafsiri haki.
CCM ambayo ilikuwa TANU baada ya TAA, ilipata ngekewa ya kuwa kiranja wa kupigana Uhuru wa nchi hii ikiwa Kama haki namba moja wanayoipigania. Sio kwamba hakukuwa na vyama vingine kama sivyo nisingalisema TANU ilikuwa kiranja.
Baada ya Uhuru, CCM ya zamani (TANU) iliunda katiba (pengine kufanya amendment Kwa baadhi ya vifungu kutoka katiba iliyorithiwa Kwa wakoloni) na kutengeneza katiba na sheria kadiri ya utashi wa viongozi wa wakati ule.
Haki ndio msingi wa sheria, lakini huongozwa na utashi ambapo kwenye utashi sharti ubinafsi(maslahi) yazingatiwe.
Kuondolewa Kwa vyama vingi miaka ya 1967 ni mwendelezo wa utashi wa viongozi wa wakati huo. Mpaka kufikia 1992 kulipofufuliwa tena vyama vingi ambapo kimsingi wafufuaji na waanzilishi wa vyama pinzani walitokea chama tawala Kwa sehemu kubwa.
CCM wengi huamini kuwa kuongoza nchi ni haki yao. Wakati vyama pinzani nao huona kuwa kuongoza nchi ni haki yao.
Kila mmoja anahaki kulingana na utashi, mtazamo na uelewa wake. Hata hivyo huwezi tenga mbali haki na maslahi.
CCM hawaioni kasoro ya Katiba mpya kwa sababu inalinda Haki(Maslahi) Yao. Pia Katiba hiyo waliiratibu vile ilivyo kulinda maslahi Yao ya kushika Dola na kuendelea kuwepo Dolani.
CHADEMA lazima wahitaji katiba mpya itakayolinda Haki zao(maslahi Yao), kwani maslahi ya chama cha Siasa ni yapo; Msingi WA uwepo wa chama cha Siasa ni Kushika Dola.
Ikiwa ni hivyo, lazima chama kiangalie njia zitakazo kisaidia Kushika Dola. Njia moja wapo ni uwepo wa Katiba na sheria nzuri zinazokiwezesha Kushika Dola Kama vile UWEPO WA TUME HURU YA UCHAGUZI.
CHADEMA Kama ilivyo CCM au vyama vingine inalinda maslahi ya chama na Wanachama kabla ya maslahi ya wananchi.
Ukiingalia jamii ya Watanzania walio wengi, Kwa kweli haina mpango wowote na wala haina mpango na masuala ya Siasa, jamii ya kitanzania wengi wao hata hawana mpango na Katiba mpya kwani hata yazamani hawalijui.
Katika uchunguzi huru nilioufanya Maeneo kadhaa ya nchi hii, nilibaini kuwa Watanzania waliowengi wapo gizani kabisa.
Watanzania wengi ni Bora liende, yote Sawa, ilimradi tunaishi na Kula ugali matembele.
Haki kuu ya Watanzania Kwa uchunguzi wangu, ni kuishi Kwa usalama bila kujali wanaishi maisha ya umasikini au Utajiri.
Pia nilibaini kuwa, Watanzania wengi hawapendi kujiingiza katika mkondo wa mambo ya Siasa, pia hawapendi marafiki wanaojihusisha na mambo ya Siasa.
Endapo utajiingiza kwenye Siasa, sio ajabu rafiki na watu wanaokuzunguka wakakuambia shauri yako, unakihere here, na mambo mengine Kama hayo.
Ikiwa Watanzania wengi hawataki kuisikia wala kujiingiza kwenye Siasa ni dhahiri hawana maslahi na Siasa,
Ni ngumu kuwaingiza Watanzania kwenye Katiba mpya ati waidai, wakati hawataki kujiingiza kwenye Siasa, na uhitaji wa Katiba ndio msingi Mkuu wa Siasa.
Haki za CHADEMA ni uwepo wa Katiba mpya itakayowapa fursa nao Kushika Dola.
Haki ya CCM ni kuendelea Kwa Katiba iliyopo itakayowafanya waendelee Kushika Dola.
Haki ya wananchi sio Katiba mpya wala Katiba iliyopo. Kwani wananchi hawana Uelewa na hawataki Uelewa wa mambo ya Katiba.
Wananchi wengi huwa na mtazamo kuwa iwe CCM iwe CHADEMA au ACT, itakayoshika Dola, hawatapata maslahi ya moja Kwa moja isipokuwa lazima waendelee kusota na kuhangaika na maisha Kama ilivyosiku zote.
CCM hawaioni haja ya Katiba mpya Kwa sababu wameshapima kina cha maji ya wananchi WA taifa hili kuwa wao hawapo upande wowote ule. Katiba sio kipaumbele cha wananchi. Hata hivyo hawajui hata hiyo Katiba ni nini.
Wananchi wa Tanzania wengi wao Wana mtazamo kuwa Maendeleo kuletwa ni hisani ya Viongozi, sio ajabu wakiwasujudia na kuwaogopa.
Katiba mpya itakuwa muhimu na yalazima pale jamii itakapobadili mtazamo, utashi, elimu, maarifa.
Ukosefu wa elimu miongoni mwa Watanzania imeathiri Kwa kiasi kikubwa utambuzi wa haki zenye manufaa kwa wananchi.
Wananchi wasio na elimu huona ni haki Yao kuishi vile waishivyo bila kujali wanaumia au law. Hii ni tofauti na Wale wenye elimu.
Katiba mpya itakuwa haki ya jamii siku jamii yenyewe ikipata Uelewa wa kile kinachohitajika ndani ya Katiba mpya na jinsi kitakavyoathiri maisha yao Kwa namna chanya.
Katiba mpya haitapatikana ikiwa sio hitaji la jamii, ikiwa itakuwa hitaji la chama Fulani hasa kisichokuwepo madarakani basi bado itakuwa ni ndoto kuipata.
Nafikiri,
Elimu ya maisha itolewe,
Jamii ielezwe Kwa nini wanamaisha mabovu,
Na Kwa nini wanapaswa wabadili maisha yao yawe Bora,
CHADEMA na vyama vingine havipaswi kutumia harakati Kali katika masuala haya.
Katika jamii ambayo elimu ya uraia bado ni changamoto,
Katika jamii ambayo ushabiki wa mambo ya udaku ni mkubwa mno,
Katika jamii ambayo huamini maisha ni bahati,
Katika jamii ambayo huona Siasa ni mchezo hatari,
Katika jamii ambayo uchawi na Ushirikina ni mkubwa,
Katika jamii ambayo ujenzi wa makanisa ya kuombea miujiza yanajengwa kila uchwao badala ya kujenga mashule na hospital.
Katika jamii ambayo ukiwapigania unaitwa kihere here,
Nafikiri namna Bora ya kuibadili jamii yoyote Ile sio kuwatetea Bali kuwapa Hali ngumu ya kiuchumi, kimaisha na kila Nyanja ya maisha.
Mabadiliko hutokea kwenye Hali ngumu.
Jamii ipo GIZANi,
Wenye Nuru hawataki Nuru iwafikie wanajamii.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Morogoro
Kwa Mkono wa, Robert Heriel.
Haki hutofautiana baina ya nchi na Nchi. Ingawaje zipo haki za ujumla za kila mwanadamu Kama vile Haki ya kuishi na kupata nyezo zinazomfanya mtu aishi.
Haki hutofautiana baina ya nchi na Nchi kutokana na utashi, utamaduni, elimu, mazingira, Aina ya jamii husika, miongoni mwa mambo mengine.
Pengine ili nieleweke zaidi, napaswa Kueleza Kwa kifupi maana ya HAKI;
Neno Haki kwa tafsiri ya kamusi ya Kiswahili sanifu lina maana ya ‘jambo ambalo mtu anastahiki au kitu anachostahili kuwa nacho.
Kwa tafsiri ya kamusi ya kisheria neno Haki lina maana ‘ kile mtu anachostahili kuwa nacho au kile anachoruhusiwa kufanya, au kile anachostahili kupokea kutoka kwa wengine kwa mujibu wa sheria’.
Kwa maana hizo zote mbili, tunaona kuwa Haki imejikita zaidi katika Utashi wa watu, mtazamo, elimu na utamaduni wa jamii.
Haki ya Zama hizi haiwezi kuwa Haki ya zama zijazo.
Hii ni kusema, haki huathiriwa na Wakati pia.
Haki huathiriwa na Wakati kutokana na sababu kuwa Mitazamo, utashi na utamaduni wa watu hubadilika kulingana na wakati.
Msingi wa haki kidunia umejikita zaidi katika Sheria za jamii husika, sheria za nchi. Hata hivyo sheria za nchi ni matokeo ya utashi na Mitazamo ya watu katika kipindi husika.
Katika Siasa za nchi yetu, haki hutafsiriwa kulingana na mtu yupo upande gani, utashi na mtazamo wake.
Mwana CCM anatafsiri yake ya HAKI, halikadhalika na mwana CHADEMA na watu wa vyama vingine, sio ajabu kila chama kinakatiba na sheria zake. Kumaanisha vile kinavyoona na kutafsiri haki.
CCM ambayo ilikuwa TANU baada ya TAA, ilipata ngekewa ya kuwa kiranja wa kupigana Uhuru wa nchi hii ikiwa Kama haki namba moja wanayoipigania. Sio kwamba hakukuwa na vyama vingine kama sivyo nisingalisema TANU ilikuwa kiranja.
Baada ya Uhuru, CCM ya zamani (TANU) iliunda katiba (pengine kufanya amendment Kwa baadhi ya vifungu kutoka katiba iliyorithiwa Kwa wakoloni) na kutengeneza katiba na sheria kadiri ya utashi wa viongozi wa wakati ule.
Haki ndio msingi wa sheria, lakini huongozwa na utashi ambapo kwenye utashi sharti ubinafsi(maslahi) yazingatiwe.
Kuondolewa Kwa vyama vingi miaka ya 1967 ni mwendelezo wa utashi wa viongozi wa wakati huo. Mpaka kufikia 1992 kulipofufuliwa tena vyama vingi ambapo kimsingi wafufuaji na waanzilishi wa vyama pinzani walitokea chama tawala Kwa sehemu kubwa.
CCM wengi huamini kuwa kuongoza nchi ni haki yao. Wakati vyama pinzani nao huona kuwa kuongoza nchi ni haki yao.
Kila mmoja anahaki kulingana na utashi, mtazamo na uelewa wake. Hata hivyo huwezi tenga mbali haki na maslahi.
CCM hawaioni kasoro ya Katiba mpya kwa sababu inalinda Haki(Maslahi) Yao. Pia Katiba hiyo waliiratibu vile ilivyo kulinda maslahi Yao ya kushika Dola na kuendelea kuwepo Dolani.
CHADEMA lazima wahitaji katiba mpya itakayolinda Haki zao(maslahi Yao), kwani maslahi ya chama cha Siasa ni yapo; Msingi WA uwepo wa chama cha Siasa ni Kushika Dola.
Ikiwa ni hivyo, lazima chama kiangalie njia zitakazo kisaidia Kushika Dola. Njia moja wapo ni uwepo wa Katiba na sheria nzuri zinazokiwezesha Kushika Dola Kama vile UWEPO WA TUME HURU YA UCHAGUZI.
CHADEMA Kama ilivyo CCM au vyama vingine inalinda maslahi ya chama na Wanachama kabla ya maslahi ya wananchi.
Ukiingalia jamii ya Watanzania walio wengi, Kwa kweli haina mpango wowote na wala haina mpango na masuala ya Siasa, jamii ya kitanzania wengi wao hata hawana mpango na Katiba mpya kwani hata yazamani hawalijui.
Katika uchunguzi huru nilioufanya Maeneo kadhaa ya nchi hii, nilibaini kuwa Watanzania waliowengi wapo gizani kabisa.
Watanzania wengi ni Bora liende, yote Sawa, ilimradi tunaishi na Kula ugali matembele.
Haki kuu ya Watanzania Kwa uchunguzi wangu, ni kuishi Kwa usalama bila kujali wanaishi maisha ya umasikini au Utajiri.
Pia nilibaini kuwa, Watanzania wengi hawapendi kujiingiza katika mkondo wa mambo ya Siasa, pia hawapendi marafiki wanaojihusisha na mambo ya Siasa.
Endapo utajiingiza kwenye Siasa, sio ajabu rafiki na watu wanaokuzunguka wakakuambia shauri yako, unakihere here, na mambo mengine Kama hayo.
Ikiwa Watanzania wengi hawataki kuisikia wala kujiingiza kwenye Siasa ni dhahiri hawana maslahi na Siasa,
Ni ngumu kuwaingiza Watanzania kwenye Katiba mpya ati waidai, wakati hawataki kujiingiza kwenye Siasa, na uhitaji wa Katiba ndio msingi Mkuu wa Siasa.
Haki za CHADEMA ni uwepo wa Katiba mpya itakayowapa fursa nao Kushika Dola.
Haki ya CCM ni kuendelea Kwa Katiba iliyopo itakayowafanya waendelee Kushika Dola.
Haki ya wananchi sio Katiba mpya wala Katiba iliyopo. Kwani wananchi hawana Uelewa na hawataki Uelewa wa mambo ya Katiba.
Wananchi wengi huwa na mtazamo kuwa iwe CCM iwe CHADEMA au ACT, itakayoshika Dola, hawatapata maslahi ya moja Kwa moja isipokuwa lazima waendelee kusota na kuhangaika na maisha Kama ilivyosiku zote.
CCM hawaioni haja ya Katiba mpya Kwa sababu wameshapima kina cha maji ya wananchi WA taifa hili kuwa wao hawapo upande wowote ule. Katiba sio kipaumbele cha wananchi. Hata hivyo hawajui hata hiyo Katiba ni nini.
Wananchi wa Tanzania wengi wao Wana mtazamo kuwa Maendeleo kuletwa ni hisani ya Viongozi, sio ajabu wakiwasujudia na kuwaogopa.
Katiba mpya itakuwa muhimu na yalazima pale jamii itakapobadili mtazamo, utashi, elimu, maarifa.
Ukosefu wa elimu miongoni mwa Watanzania imeathiri Kwa kiasi kikubwa utambuzi wa haki zenye manufaa kwa wananchi.
Wananchi wasio na elimu huona ni haki Yao kuishi vile waishivyo bila kujali wanaumia au law. Hii ni tofauti na Wale wenye elimu.
Katiba mpya itakuwa haki ya jamii siku jamii yenyewe ikipata Uelewa wa kile kinachohitajika ndani ya Katiba mpya na jinsi kitakavyoathiri maisha yao Kwa namna chanya.
Katiba mpya haitapatikana ikiwa sio hitaji la jamii, ikiwa itakuwa hitaji la chama Fulani hasa kisichokuwepo madarakani basi bado itakuwa ni ndoto kuipata.
Nafikiri,
Elimu ya maisha itolewe,
Jamii ielezwe Kwa nini wanamaisha mabovu,
Na Kwa nini wanapaswa wabadili maisha yao yawe Bora,
CHADEMA na vyama vingine havipaswi kutumia harakati Kali katika masuala haya.
Katika jamii ambayo elimu ya uraia bado ni changamoto,
Katika jamii ambayo ushabiki wa mambo ya udaku ni mkubwa mno,
Katika jamii ambayo huamini maisha ni bahati,
Katika jamii ambayo huona Siasa ni mchezo hatari,
Katika jamii ambayo uchawi na Ushirikina ni mkubwa,
Katika jamii ambayo ujenzi wa makanisa ya kuombea miujiza yanajengwa kila uchwao badala ya kujenga mashule na hospital.
Katika jamii ambayo ukiwapigania unaitwa kihere here,
Nafikiri namna Bora ya kuibadili jamii yoyote Ile sio kuwatetea Bali kuwapa Hali ngumu ya kiuchumi, kimaisha na kila Nyanja ya maisha.
Mabadiliko hutokea kwenye Hali ngumu.
Jamii ipo GIZANi,
Wenye Nuru hawataki Nuru iwafikie wanajamii.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Morogoro