Haika Lawere wa 'Mbezi Garden' apewa Talaka

Haika Lawere wa 'Mbezi Garden' apewa Talaka

kakutana na bomba ya maana itakuwa
...napitatu

yaan hii dunia watu wanakaa miaka 21 wanaachana na kuna watu wanajazana kwa mwamposa kuhan MUSA
SUGUYE

" WANAOMBA MUNGU AWARUDISHE WAUME ZAO WAMEKIMBIA AISEEEE^^
Japo wameachana mpaka kutalakiana leo ndo niliona hiyo post ya mzee magesa na bibiye Haika naye sijawahi sikia akizungumzia ndoa yake udhaifu wake kama wafanyavyo wnawake walio wengi,

Kwa kiasi kikubwa nilivyosoma post ya magesa nimeona ukuaji na utu uzima wenye hekima akili na busara though wameachana watoto ni watu wazima sasa

Kuna mtu mmoja kasema wameachana kisomi nimeipenda hiyo 😂 ingekuwa Mimi kilio kingesikika mpka kwa chalamila
 
Kulingana na maelezo yako basi mambo ya wananwake magumu sana. (Unakuta ni bikra au wewe ndio mwanaume wa pili). Sasa uwe wa ngapi ndio salama?!
Suala mtambuka, jiandae kisaikolojia kupata mwanamke kwa wastani wa chini kishatembea na wanaume 5, hakika utakuwa na amani kwenye ndoa, ila ukisha muoa, hakikisha unamlinda tu wale waliomtoa bikra wasirudi maana hawezi kusahau aliyemtoa bikra mpaka anaingia kaburini na aliyemtoa akija hatongozi, mwanamke analegea kama mbwa kwa chatu.
 
Suala mtambuka, jiandae kisaikolojia kupata mwanamke kwa wastani wa chini kishatembea na wanaume 5, hakika utakuwa na amani kwenye ndoa, ila ukisha muoa, hakikisha unamlinda tu wale waliomtoa bikra wasirudi maana hawezi kusahau aliyemtoa bikra mpaka anaingia kaburini na aliyemtoa akija hatongozi, mwanamke analegea kama mbwa kwa chatu.
Sasa uoe mwanamke ambae ashatumika na minimum approximation ya wanaume watano halafu ufanye kazi ya kumlinda asifuatwe na maex wake, kwanini usioe tu bikira kuondoa huo usumbufu. Maelezo yako yanaonyesha mwanamke used ana uwezekano mkubwa zaidi wa kuchepuka kwa sababu bado ana kumbukumbu za mambo aliyoyafanya na maex wake
 
Anaandika MUME (Phares Magesa):

Watu wengi kwa muda mrefu zaidi ya miaka 4 sasa wamekuwa wakiuliza maswali katika baadhi ya posts zangu mama wa watoto hawa mbona hawamuoni ? kwenye picha nyingi ukiacha chache chache sana za matukio muhimu au labda hata kwenye posts za mama yao pia labda baadhi ya watu nao wanauliza/wanajiuliza swali kama hilo .

Ukweli upo hivi;

Mwaka 2001 Phares Magesa na Haika tulioana na ndoa ilifungwa katika Kanisa la Mennonite Tanzania (KMT), mtaa wa Ally Khan, Upanga karibu na DIT au Regency Hospital, sherehe ya harusi baadae ilifanyika ukumbi wa Diamond Jubilee na kuhudhuriwa na watu takribani 1,000 wakati ule, sherehe ilifana sana MC alikuwa FomaFoma.

Wakati namuoa Haika alikuwa ni Mwanafunzi anasomea Shahada ya kwanza Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) na akamaliza vizuri licha ya kuwa kwenye ndoa akiwa mwanafunzi, na tukiwa ndani ya ndoa nikamshauri asiridhike na elimu aliyoapata na nikamruhusu akasome Shahada ya Uzamili, akaenda Salford University, Uingereza nako pia akamaliza vizuri masomo yake na kwa neema ya Mungu baada ya hapo tukajaliwa watoto wazuri watatu, wawili wa kiume Paxton na Haris na mmoja wa kike Princess.

Mungu amekuwa mwema sana kwetu ametusaidia sana kwa kutuwezesha kufanya kazi na biashara zetu kila mmoja kwa bidii, maarifa, nidhamu na kujituma kwa hali ya juu na kufanikiwa kadri Mungu alivyotujalia.

Baada ya kuwa katika ndoa kwa miaka 21, yaani 2001 hadi 2022 Mahakama ya Mwanzo, Kawe, Kinondoni ilihitimisha shauri la talaka lililokuwa mahakamani hapo kwa takribani mwaka mmoja na kuanzia 2022 kila mmoja akawa huru na kwa sasa tunashirikiana vizuri kulea watoto wetu (Co-Parenting) na tunashukuru Mungu kwa yote.

Ushauri kama hakuna sababu ya msingi ya kuachana na mwenza wako, sishauri wanandoa wowote hasa kama mkiwa na watoto kufikia kirahisi uamuzi wa kuvunja ndoa ni mpaka pale itakapokuwa hiyo ndio njia salama na ya lazima kwa mustakabali mwema wa pande zote tatu yaani Mke, Mme na Watoto.

Usiingie kwenye ndoa kwa nia ya kutaka kuonekana na wewe umo au kwa nia ya ku trend, pia usiachane na mtu kwa sababu hizo hizo.

Mbarikiwe wote mlio kwenye ndoa zidumu na mnaotaka kuingia pia ndoa zidumu,tumtangulize Mungu na kujali famlia zetu.
Ahmad Issa Michuzi on Instagram: "Msikilize kijana huyu Haris Phares Magesa ambaye ni mto wa Nguli wa mambo ya 'IT' kitaifa na Kimataifa @pmagesa akishangaa wanaofeli mitihani ya @nectatz,@nactvet haris_with_one_r_"
View attachment 3561971


Upuuzi tu. Hatumjui na hatuhitaji kuyajua mambo yake. Anatuambia iweje?
 
Back
Top Bottom