Nakuonea huruma tu. Hukustahili kuelekezwa cha kufanya baada ya kujitumbukiza kwenye taasisi hii ya ndoa. Ndoa ni taasisi, haiwezi kushaurika tena ukiisha ingia. Haswa ka ni ya Kikristo. Ukiisha ingia dawa pekee ni kifo tu. Je, unataka tukushauri kuua? Hapana. Vumilia tu tena acha kelele nje ya mlango wenu wa chumbani. Za chumbani zibaki humo humo, mgeni ma mkwe asijue hilo.
Kuhusu ufanye nini; Sasa umeshamfahamu mwenzio, ukitaka kupona, usijaribu kumuwaza yulee wa kale tena haswa wakati upo kwenye mitikisiko ile yenu na huyu Mr wako. Huyu ndo mwenye hiyo kitu, hairuhusiwi kumuwazia mwingine tena kwani hairuhusiwi hata kuiona kwa mbali.
Hebu weka mawazo na fikara zako kwa huyu Mr.
Mpe yote mpaka ajisahau apagawe. Kweli kipo kimoja tu lakini cha kukutoa jasho. Kipo kimoja lakini hakikufikishi kwa kuwa upo mbali hapo ni tundu tu lipo mwenye tundu yuko kwa Johnnnnn kulee mwaka juzi uleee. Huu ni Ukangi kabisa. Mavi ya kale hayanuki tena?
Mfurahiye mumeo tena usithubutu kumwita "bure kabisaa" angekuwa bure ungekaa hapo? Mwandae, mvalie hata vinguo lainiiii, mshawishi mapema kabla ya usingizi wala usimpe stress za hunitoshelezi. Atakuwa chuma siku si nyingi. Kwa heri. We ulivyo hata ungekuwa jirani yangu, sikutaki kwani ulishawapa wengi na kazi yako ni kuwapima wanaume