Hadthi : Sundi

Hadthi : Sundi

SEHEMU: 14

ILIPOISHIA:
"Mama nilikuwa kwa ma mdogo na pia nilipitia kwa kaka Lyasi."
"oooh kumbe ulikuwa na safari ndefu hawajambo wote?"
"Wazima wa afya njema."
"Mhu wanasemaje?"
"Wanakusalimia ila mama ma mdogo amenituma kesho niende kwa dada Cathy."
"Wapi? Dar?"
"Ndiyo mama."
"kuna nini tena?"
"Sijui amesema atanijulisha hiyo kesho kutwa."
"Mimi sina tatizo mjulishe na baba yako tu nisije nikaulizwa."
Jioni baba yake aliporudi alisubiri mpaka usiku baada ya chakula cha usiku ndipo alipomweleza. Lakini baba yake alisema ameisha pata taarifa la muhimu awahi kurudi.
"Mume wangu mwache mtoto akapumzike hata wiki ili aone na jiji."
"Na kazi za hapa?"
"Na akiolewa atafanya nani?"
"Mpaka akiolewa."
"Lazima tujifunze kukaa peke yetu ili akiolewa tusiwe wakiwa."
SASA ENDELEA…

"Haya kaa hata mwaka mzima."
"Hapana baba siku mbili tu siendi kukaa nimetumwa na ma mdogo."
"Ahaa kumbe haya mama uende salama."
Siku ilipotimu Sundi alikwenda Dar kwa dada yake Catheline, alipata siti ya dirishani upande wa siti ya watu wawili. Alikaa na mwanamke mmoja makamo ya dada yake mkubwa anayefuatwa na Cathy na yeye ameolewa Dar na ndiye alikaa na Cathy na kuolewa mikononi mwake.
Baada ya kusalimiana kila mmoja alipenda kuongea na mwenzie, kabla ya basi kuondoka yule dada wa jirani na Sundi alinunua gazeti na kusoma. Lilikuwa gazeti la udaku baada ya kusoma kwa muda alilikunja, ndipo Sundi na yeye alipoomba kusoma.
Yule mama alimpa na kuanza kusoma, alilisoma gazeti lote na kukutana na kitangazo kilichokuwa kukusema kuwa kuna mganga anayeweza kuokoa ndoa za watu. Kuimalisha ndoa zinazoyumba hata kumrudisha mke au mume aliyehasi nyumba yake.
Baada ya kusoma alijikuta akiguna kitu kilichomfanya yule mama wa jirani yake kuhoji:
"Vipi mdogo wangu unaguna nini?"
"Yaani unajua dada waganga wa kienyeji waongo sana."
"Kwa nini unasema hivyo mdogo wangu?"
"Eti wanawadanganya watu wana uwezo wa kuokoa ndoa za watu, hivi kweli duniani kuna dawa ya kubadili tabia ya mtu?"
"Mmmh kweli hakuna mdogo wangu."
"Sasa kama sio uongo ni nini?"
"Sikiliza mdogo wangu dawa zipo za kumfanya mwanaume atulie ndani au aachane na tabia chafu."
"Lakini kwa upeo wangu mdogo japo sijakuwa sana japo sijaolewa lakini naamini dawa ya mapenzi ni wewe mwenyewe."
"Nakubaliana na wewe kwa asilimia mia, lakini mdogo wangu ukiona hivyo ujue Simba kazidi inabidi amloge mtu na pale hakuna mapenzi zaidi ya mmoja kugeuzwa ndondocha."
"Unazidiwa vipi na wewe unafanya yote kwa mumeo ikiwa tabia mpaka kauli njema."
"Mdogo wangu unajua ndoa ni jumba lililo na pande mbili yaani nje na ndani aliye nje anatamani kuingia ndani na walio ndani wapo wanaofurahia kubakia lakini wengine kwao kama jehanamu wanatamani kutoka na waliotoka hawataki kurudi tena na wengine waliotoka kwa uzembe wao ndio hao huenda kwa watalamu kama hawa na kuwapa dawa ambazo huwarudisha ndani. Vilevile wapo walio nje ambao wanatamani kuingia ndani lakini bahati hiyo hawa ndio huenda kwa wataalamu kama hawa ambao huwasaidia."
"Una amini zinasaidia?"
"Zinasaidia sana mdogo wangu."
"Mmh. Siamini."
"Bado mdogo ukikuwa utayajua haya unaweza kuwa unayafanya yote haya tabia nzuri au kauli tamu kama kinanda lakini mumeo akawa ndani hakai lazima utajua uangaike vipi kuiokoa ndoa yako hasa pale unapompenda mumeo na kutokutaka ndoa yako ivunjike."
"Wewe unaamini vipi?"
"Mimi ninaye kuelezea hivi yamenikuta," kauli ile ilimfanya Sundi ajiweke vizuri kupata kisa kingine kabla ya kumfikia dada yake. Kabla ya kuongea alitulia tuli kwa muda kisha alitoa kitambaa kwenye mkoba wake na kufuta machozi ikionyesha machozi yalikuwa yakimtoka kisha kwa sauti ya upole alisema:
"Mdogo wangu katika maisha yako usipoteze muda wako."
"Kivipi dada?"Sundi alimuuliza huku akiwa amemkazia macho.
"Mdogo wangu wakati ukuta na ukitimu hugota na vilevile hakuna marefu yasiyo na ncha na ngoma ikivuma sana hupasuka."
"Dada yangu yote uliyosema nimetoka kapa."
"Ni kweli lakini unakuwa na wakubwa hawakukosea kusema kuwa uyaone."
"Ni kweli dada yangu na sisi wadogo hujifunza kupitia ninyi wakubwa zetu mlio tutangulia."
"Ni kweli kabisa, ila nakuomba chondechonde mdogo wangu usiipige teke tunu uliyopewa na Mungu hasa huu uzuri wako ukajiona huwezi kuufuja kwa kuolewa na kutaka kuponda maisha...
Mimi mdogo wangu enzi zangu nilikuwa ni utatanishi kwa wanaume si kwa wanaume hata mwenyewe nilijijua ni mzuri. Nilikataa kuolewa kwa kujua ndoa ni utumwa na kujifuja. Hata elimu niliiona haina mpango kwa kuendekeza starehe.
Na siku zote mdogo wangu jiepushe na kuzionja starehe za kidunia zitakupoteza na kuona ndio maisha kumbe unapotea. Nilikuwa sishikiki enzi zangu lakini ipo siku nilibakia kama nyani mzee wanaume wakawa wananikimbia hapo ndipo nilikimbilia kwa wataalamu na kubahatika kupata bwana kwa vile sikuwa na uwezo wa kumshawishi mtu.
"Mmh ilikuwaje dada yangu mpaka kufikia hivyo?"
"Ni hivi baada ya siku moja kupata dhahama ambayo ni Mungu aliyeokoa maisha yangu. Siku hiyo nakumbuka vizuri ilikuwa baada ya kutoka hospitali na kusimama mbele ya kioo na kuiangalia sura yangu iliyopoteza haiba sikuwa mimi tena wa miaka ile iliyopita niliyekuwa nikitumia muda mwingi kwenye kioo lakini sasa uso wangu hauna tofauti na kibaka aliyekwapua mkoba kwenye kituo cha basi.
Sasa hivi mdogo wangu nimekuwa adui mkubwa na kioo kuna kipindi huuogopa uso wangu kwa kujiona nimekutana na kiumbe cha ajabu. Uso wangu nimekuwa kama dudu la kutishia watoto vikojozi.
Kila aliyeniona muda huu hawezi kuamini kuwa ni mimi mtu niliye kuwa tishio kwa wanawake wenzangu ni gari gani litakalopita bila kusimama na kuniulizia ninakwenda wapi kutembea kwa miguu kutaka mwenyewe.
Leo hii uso wangu umekuwa kama ubao wa shabaha ambao umebondeka kwa wale wenye shabaha ambao upiga nje ya duara mdomoni maskini sikuwa na meno ya kuchekea ambayo siku za nyuma nilicheka muda wote tena nilionyesha meno yangu matatu ya dhahabu na mwanya wangu mwembamba ulioongeza uzuri wangu.
Sikuwa radhi kuolewa raha za dunia ningezifaidi saa ngapi kwanza mwanamke mzuri kama mimi sikuumbwa ili nifungwe ndani kama mfungwa. Nilijua Mungu aliniumba ili nile raha za dunia na kutembea mitaani kuonyesha uwezo wake wa uumbaji, nikikaa ndani nani ambaye ataniona.
Halafu nivae nguo ndefu hayo maumbile niliyoumbwa nayo nani atayaona tena sikuvaa nguo nzito nilivaa nguo za wanaita za trans palent zilizo onyesha mpaka ndani. Wapo walionikufuru nilijua wananionea gere kwa sababu hawakuwa na maumbile wala sura ya mvuto kama yangu.
Lakini sasa imebakia simulizi na majuto ya nafsi na kuusemea moyo wangu ningejua lakini ni wakati huo. Hapo nyuma nilikuwa kimbelembele kuonekana mbele ya macho ya watu kwa sababu nilikuwa nikijiamini kwa kila kitu. Hata wanawake wenzangu walijua kwa kunisifia bila aibu wala choyo, ukiona mwanamke mwenzio anakusifia ujue wewe ni mzuri ni nadra mwanamke mwenzio kukusifia hata uwe mzuri vipi.
Najua una shauku mdogo wangu kuyajua ila nakuomba kupitia simulizi hii iwe fundisho kwako hata kwa mashoga zako sipendi kosa langu lirudiwe na mtu mwingine, kisa hiki ambacho kilinifanya nitake kujiua zaidi ya mara mbili.
Kwa jina mdogo wangu naitwa Konsolata nimezaliwa miaka 32 iliyopita ni mtoto wa nne katika familia ya watu watano nikiwa ni mmoja wa watoto wa kike wa famili ya mzee Jonasani na mama yangu Magdalena.
Kwanza lazima nimshukuru Mungu kwa kuzaliwa familia iliyompokea Bwana.Wazazi wetu walikuwa wacha Mungu wazuri sana. Lakini ilikuwa tofauti na sisi watoto wao kwenda kanisani ilikuwa mbinde au kusingizia tunakwenda kanisani kumbe kwenye mambo yetu.
Siku zote tulijua ukimuona mtu anamfuata sana Mungu ujue maisha ya kidunia yamemshinda hasa wazee ambao wakiona wamekaribia kufa hapo ndipo humrudia Mungu.
Pamoja na wazazi wetu kuwa wacha Mungu tulikuwa hatukosi kwenye matamasha hasa kumbi za starehe majira ya usiku kwa kutoroka.
Baada ya kumaliza kidato cha sita nilibahatika kwenda chuo kikuu, kwa kweli kwa upande wangu nilikuwa kama mfungwa aliyefunguliwa kifungoni kwa kupata muda wa kufanya mambo yangu ambayo wazazi wangu walikuwa wakinibana.
Nilikutana na shoga yangu ambaye tulikuwa tunakaa naye chumba kimoja kwa kweli mwanzo mavazi yake yalinishinda yalikuwa ya nusu uchi alinishangaa mimi kuvaa nguo ndefu kama mtawa.
"Konso utakatifu gani huo?"
"Kwa nini unasema hivyo?"
"Mavazi gani hayo yaani umbile kama lako ningekuwa nalo mimi kila mtu angelisoma namba Mungu amekupa ili uutangaze uwezo wake wa uumbaji ukilificha usije shangaa siku moja ukasikia umekuwa mremavu kwa kushindwa kuvitangaza..kwanza unajijua wewe mzuri."
"Nitajijuaje mwenyewe."
"Ina maana kote uliko soma hukuwahi kusifiwa?"
"Hiyo hali nimeisha izoea."
"Basi Konso wewe ni mzuri chuo kizima yaani ningekuwa kama wewe mbona wangenikoma."
Suzy msichana ambaye alionekana ni mjanja kuliko mimi starehe kwake kilikuwa kitu cha kawaida eti hata wazazi wake walilijua hilo kwa kumuachi kujirusha la muhimu akili yake ilikuwa ikichaji.
Ushawishi wa Suzy haukuwa mkubwa kwa sababu hata mimi starehe nilikuwa nazipenda lakini ndio hivyo ni nilikuwa kwenye geti kali. Kwa kweli nilijikuta naungana na Suzy kwenda kwenye kumbi za starehe usiku. Huku nako Suzy alikuwa na rafiki yake wa kiume na mimi alinitafutia rafiki yangu.
Basi mdogo wangu mabwana tulio wapata walikuwa na pesa za kumwaga, ilifikia hatua ya kusafiri nje ya mkoa kwenda kwenye miji ya starehe. Ajabu bwana wa Suzy alifanya mapinduzi kwa kunitangazia dau kubwa kwa kuwa mimi nilikuwa mzuri kuliko Suzy kibaya niliyekuwa natembea naye ni rafiki yake na pesa alikuwa akitoa yeye.
Yule bwana alisababisha mimi na shoga yangu tuwe maaduni na kuwa kama chui na paka hata kufikia hatua ya kutengana chumba na kununiana hatukuwa tukiongea ulikuwa uhasama mkubwa.
Yule bwana aliyefahamika kwa jina la Afidh Bantu au kama alivyokuwa akipenda kujiita 'Bishanga'. Aliamua kunihamisha shule na kunipangishia uswahilini lakini sehemu ya watu wenye uwezo.
Aliniwekea kila kitu ambacho ni muhimu kwa kweli nilijikuta nayasahau maisha ya chuo na kuishi maisha ya starehe ya kila wiki lazima tutoke kwenye kumbi za starehe. Bishanga aliniambia niache kusoma kwa kuwa anataka kunioa na kunipa maisha mazuri.
Nilikubali kuacha shule bila wazazi wangu kujua niliamua liwalo na liwe hata kama wakijua watasema mwisho watalala. Bishanga alikuwa tayari kuwalipa kiasi chochote cha gharama ya masomo yangu kuanzia chekechea.
Niliishi na Bishanga kwa mwaka mmoja nikiwa sijui kupika wala kufua, niliishi kama malkia na yeye aliniita malkia wake. Kwa kweli kila sehemu tuliyokwenda walimuuliza amenitoa wapi malaika ambaye hawaamini kama nimezaliwa bali nimeshushwa kwa uzi wa buibui.
Sehemu zote nilikuwa nakwenda naye katika mavazi ya ajabu ya nusu uchi nilipomgomea alisema kama Suzy.
"Lazima niutangaze utaalamu wa Mungu kwa utundu alioufanya kukuumba nina imani siku aliyo kuumba aliacha shughuli zote na kukuumba kwa utundu wa hali ya juu."
Mwanzo nilikuwa naona kazi lakini nilikuja kuyazoea na kuona kutembea uchi au nusu uchi ni jambo la kawaida. Pamoja na kuwa na pesa nyingi lakini nilikuwa sijui kazi ya Bishanga. Siku moja tukiwa tumelala majira ya saa saba za usiku nyumba yetu ilivamiwa na askari.
Afidh Bantu pamoja na mimi tulichukuliwa juujuu na kupelekwa polisi usiku huohuo, kwa upande wangu sikujua tumechukuliwa kwa sababu gani. Huko nyuma tuliacha nyumba kwenye upekuzi mzito.
Tulipofika polisi tulitenganishwa kila mmoja aliwekwa sehemu yake, tulilala palepale hadi asubuhi. Kesho yake majira ya saa saa tano tulitolewa kwa dhamana na rafiki zake na Bishanga, walikuwa na watu wenye pesa.
Mpaka tunarudi nyumbani sikujua jana yake tulichukuliwa na polisi kila nikimuuliza anasema achana nayo. Pamoja na kukaa kimya bado nilikuwa kwenye maswali mazito juu ya kuvamiwa na jeshi zito la Polisi na siraha nzito na mbwa kama jambazi au mhaini.
Jioni ya siku ile Bishanga alinieleza kuwa tatizo lake ni zito kwa hiyo anatakiwa kuondoka nchini usiku ule, nilijiuliza ni tatizo gani linalo mkimbiza nchi.
"Sasa utarudi lini?"
"Kwa kweli haijulikana ikiwezekana kuonana majaliwa."
"Ooh! Mungu wangu na mimi itakuwaje?"
"Sina jinsi itanibidi nikuache kwa sababu tatizo lenyewe limetokea ghafla."
"Mimi nitaishi vipi kwa kuwa wewe ndiye umeniachisha shule?"
"Siwezi kukuacha kwenye hali mbaya bali nitakuachia pesa nina imani itakutosha kununua nyumba na gari moja dogo na za kutumia kwa miaka mwili."
"Kiasi gani."
"Milioni 50 ila ndani ya nyumba hii unatakiwa kuanzia kesho uondoke nyumba si mali yetu tena nimeiuza ili kupata nauli na pesa ya kukuachia."
Nilitamani kulia kwa kujua sasa ndipo wakati wa kuadhirika mtoto wa kike kwa sababu Afidh Bantu alikuwa amenizoesha vibaya sana. Sikuwa na jinsi nilimuagia palepale kwa sharti hatakiwi kusindikizwa na mtu.
Baada ya Bishanga kuondoka nilirudi kwenye chumba changu ambacho nilikuwa bado sijakirudisha. niliyaanza maisha mapya nikiwa peke yangu niliwaza kurudi nyumbani lakini nilijiuliza nitawaeleza nini. Niliamua maisha yangu yatakuwa mbele kwa mbele sirudi nyuma.
Kama pesa nilikuwa nayo ya kuishi maisha yoyote ninayotaka, nilisimama mbele ya kioo kuthibitisha uzuri wangu, kweli nilithibitisha mimi mzuri tena sana. Nilikuwa nikiona fahari kusimama kwenye kioo kwa muda mrefu kwa kuuangalia uzuri wangu.
Basi mdogo wangu nilichukua muda wa mwezi mmoja na kuolewa na bwana mmoja wa kiarabu. Kwa kweli ilikuwa harusi kubwa sana ambayo nina imani mpaka Mungu ananichukua haitatokea. Bwana huyu pesa alikuwa nayo alikuwa akimiliki magari na vituo zaidi ya kumi vya mafuta jijini.
Mwanzo ndoa niifurahia kwa kuona napendwa na ndugu na jamaa wa mume wangu. Lakini ndoa ilinitumbukia nyongo kwa kujiona nipo kizuizini. Yaani nilikuwa mimi na ndani, ndani na mimi. Kwa kweli ndoa niligundua ni utumwa haina nafasi ya kujitawala.
Nilijifikilia kama pesa ninayo tatizo nini maisha ya kufungwa yalinishinda na kuamua kuomba talaka japo mume wangu alinipenda sana. Lakini nilimlazimisha kunipa na kumtishia asiponipa atanipea mahakamani.
Mume wangu hakuwa na jinsi alinipa talaka baada ya talaka niliapa sitaolewa tena na mwanaume nitaishi maisha yangu kwa kumchagua mwanaume atakaye kubali masharti yangu.
Mdogo wangu ujinga mzigo nilijiona mzuri na kusahau kuna wazuri wengi wanao hangaika kwa waganga bila mafanikio lakini mimi nilijiona mimi ndio mimi, nisiye kubali kubabaishwa na mwanaume yeyote kwa kujijua wanaume wananigombea kama mpira wa kona.
Niliyaanza maisha yangu kwa staili nyingine kwa kila jioni kwenda kwenye kumbi za starehe na kurudi nyumbani majira ya usiku wa manane. Siku moja nikiwa kwenye moja ya kumbi za starehe nilimuona kijana mmoja ambaye nilivutiwa naye.

Itaendelea...
 
SEHEMU: 15

ILIPOISHIA:
Basi mdogo wangu nilichukua muda wa mwezi mmoja na kuolewa na bwana mmoja wa kiarabu. Kwa kweli ilikuwa harusi kubwa sana ambayo nina imani mpaka Mungu ananichukua haitatokea. Bwana huyu pesa alikuwa nayo alikuwa akimiliki magari na vituo zaidi ya kumi vya mafuta jijini.
Mwanzo ndoa niifurahia kwa kuona napendwa na ndugu na jamaa wa mume wangu. Lakini ndoa ilinitumbukia nyongo kwa kujiona nipo kizuizini. Yaani nilikuwa mimi na ndani, ndani na mimi. Kwa kweli ndoa niligundua ni utumwa haina nafasi ya kujitawala.
Nilijifikilia kama pesa ninayo tatizo nini maisha ya kufungwa yalinishinda na kuamua kuomba talaka japo mume wangu alinipenda sana. Lakini nilimlazimisha kunipa na kumtishia asiponipa atanipea mahakamani.
Mume wangu hakuwa na jinsi alinipa talaka baada ya talaka niliapa sitaolewa tena na mwanaume nitaishi maisha yangu kwa kumchagua mwanaume atakaye kubali masharti yangu.
Mdogo wangu ujinga mzigo nilijiona mzuri na kusahau kuna wazuri wengi wanao hangaika kwa waganga bila mafanikio lakini mimi nilijiona mimi ndio mimi, nisiye kubali kubabaishwa na mwanaume yeyote kwa kujijua wanaume wananigombea kama mpira wa kona.
Niliyaanza maisha yangu kwa staili nyingine kwa kila jioni kwenda kwenye kumbi za starehe na kurudi nyumbani majira ya usiku wa manane. Siku moja nikiwa kwenye moja ya kumbi za starehe nilimuona kijana mmoja ambaye nilivutiwa naye.
SASA ENDELEA…

Niliamua kumtongoza na yeye alikubali bila kipingamizi kuanzia hapo nikawa na yule kijana ambaye nilikuwa natanua naye kumbi za starehe. Mmh, kweli usichokijua ni usiku wa giza, kumbe yule kijana alikuwa na akili nyingi alinizidi akili na kuniibia kiasi kikubwa cha pesa ilikuwa ni nusu ya pesa niliyoachiwa na Bishanga kwa kunidanganya amepata nyumba na mimi mapenzi yaliniziba macho nilimuamini kwa kumpa pesa za kulipia nyumba kumbe ndio nilimpa nauli ya kunitoroka.
“Hilo mdogo wangu halikunila mawazo sana kwa kuwa benki nilikuwa na milioni nane niliamua nusu ya pesa kununua vito vya dhahabu kwa kuja hali mbaya ipo njia lazima niwe na vitu vya kumvutia mwanaume.
Japo mwanzo nilikuwa mgumu lakini nilijikuta nakubali ofa za wanaume, lakini nilichagu wanaume wenye pesa kutokana na umbile na uzuri niliokuwa nao hakuna mwanaume aliyekaa dau nilililo mwambia.
Maisha yangu hayakutetereka lakini kila mwanaume niliyekutana naye alitaka kunioa, lakini nilikataa kwa kuhofia kuingizwa kizuizini. Nilijua ndoa ni utumwa na kuwaonea huruma wote walio ndani ya ndoa kwa kukosa uhuru na kukosa kufurahia maisha sijui uzeeni kwao watahadithia nini, nilikuwa sikai na mwanaume mmoja zaidi ya wiki.
Niliyaanza maisha ya kujiuza kimwili kwa kwenda kwenye klabu za starehe usiku.Kutokana na umbile langu wanaume walinikimbilia kama mpira wa kona.Wapo niliokwenda nao muda mfupi na kunilipa malipo yangu na wapo niliokwenda nao kulala nao mpaka asubuhi.
Mradi ule kidogo ulinisaidi baada ya kuanza wizi wa kuwasachi wanaume tukiwa tumelala, kuna siku nililala na mzungu na kufanikiwa kumuibia pesa nyingi na kutimka usiku. Asingeweza kunitafuta kwa sababu hakuwa na ushahidi wa kunifunga.
Baada ya kupata pesa niliamua kuachana na kazi ya kujidhalilisha na kuanzisha biashara ya saluni na duka la vipodozi. Amini usiamini kwa muda mfupi hali yangu ya maisha ilibadilika.
Wakati huo nilikuwa nimekuja na mtindo mwingine ambao nilijua mimi ndiye msemaji mkuu kwa kuchukua mwanaume kijana na kumfuga kwa kumpa kila kitu ili tu aniridhishe kimapenzi.
Kijana Riziwani Bantu kwa kweli nilitokea kumpenda hasa alikuwa na jina kama mpenzi wangu Afidh Bantu nilipomuuliza kuwa na ndugu au jamaa yake alisema majina yanafanana kwa vile wote walikuwa wakitokea Bukoba toka siku ya kwanza nilipomuona. Nilitupa chambo na yeye akakimeza chote na kumfanya mpenzi wangu.
Nilimpa kila kitu alichotaka mpaka gari la kutembelea, kwa kweli nilijikuta nayainjoi maisha kwa kupata kijana shababi ambaye alikuwa akinikata kiu ya mapenzi kisawasawa.Wakati huo shughuli zangu zilikuwa zikienda vizuri.
Riziwani Bantu mwanzo alikuwa akinisikiliza muda wowote niliokuwa nikimtaka nilimpata. Lakini ghafla yakatokea mabadiliko kila nikiwa na shida naye simpati kwa wakati muafaka.
Taarifa zilinifikia kuwa mmoja wa wafanyakazi wangu wa saluni ndio siku hizo wanatumbua pesa ninazompa. Roho iliniuma kwa kukumbuka nilipo mtoa Riziwani kwenye matalo wa kuoshea magari.
Nakumbuka siku ya kwanza kukutana na kijana yule alikuwa pembeni akiwa mwenye njaa na kwa bahati mbaya hakupata kazi kwa siku ile kwa kuwahiwa na wenzake.
Nikiwa nje nasubili gari langu lisafishwe nilimuona Riziwani kwenye mavazi machakavu. Japo mavazi yake yalikuwa machakavu lakini umbile lake lilikuwa limekakamaa kiume haswa. Nilijikuta nikimwangalia kwa matamanio kwa kuwaza kuwa kama nitamiliki yule kijana nitafaidi.
Nilipo mwita alinisogelea kwa wasiwasi:
"Vipi sister kuna issue? Maana mambo mabaya."
"Wewe tu..unaitwa nani?"
"Bantu," Kusikia jina Bantu moyo ulinilipuka nikajua ni ndugu na kipenzi changu Bishanga.
"Ooh! Bantu jina zuri unakaa wapi?"
"Temeke mikoroshoni."
"Sasa Bantu tukitoka hapa tuongozane kuna kazi ikiifanya kwa usanifu nitakupa zawadi nzuri."
"Yaani sister nilivyo na usongo utafurahi mwenyewe."
"Hiyo ndiyo shida yangu."
Baada ya kusafishiwa gari niliongozana na Bantu kuelekea nyumbani kwangu. Moyoni niliona kwa mtindo ule siwezi kuwekewa mipaka hata kama nitakuwa na mwanaume wa nje hawezi kuniziwia.
Tukiwa njiani nilimuuliza maswali mawili matatu juu ya maisha yake.
"Bantu inamaana hii ndiyo kazi yako?"
"Sister ndiyo hii kazi za kuajiliwa zinakwenda kwa majina bilakuwa na refarii satifiketi yako utafungia mandazi"
"Unajua kuendesha gari?"
"Ndiyo"
"Umejifunzia wapi?"
"Hapa hapa kila tukimaliza kuosha tunawageuzia magari yao"
"Umesoma"
"Ndiyo."
"Mpaka darasa la ngapi?"
"Kidato cha nne."
"Ha! kidato cha nne unaosha magari?"
"Kazi hakuna ukisubiri uajiliwe serikalini utakufa na njaa wenye digilii wanalia itakuwa sisi."
"Una vuta sigara?"
"Hapana?"
"Pombe unatumia?"
"Hapana..mimi starehe yangu mpira jioni hujichanganya kwenye mazoezi."
Tulipofika nyumbani nilimpeleka hadi sebuleni, cha kwanza nilimpeleka bafuni kuoga kisha nilimpa nguo ambazo aliziacha yule kijana aliyenitapeli mwanzo. Kwa muda mfupi Bantu alipendeza kweli nguo humfanya mtu aonekane duni au aonekane kiumbe kipya machoni mwa watu.
Tokea hapo mdogo wangu tukawa tupo pamoja mimi na Bantu popote alipokwenda. Pamoja na kuwa na Bantu lakini nilikuwa na wazee wenzangu ambao nilifanya nao starehe kwa nafasi kwa kujua Bantu nilimpa mipaka yake.
Taarifa za Bantu kuwa na mahusiano na mmoja wa wafanyakazi wangu wa saluni yalininyima raha japo hata mimi sikuwa muaminifu kwake lakini yeye nilikuwa kama nimemuoa nampa kila kitu alichotaka siku zote mtenda akitendewa uhisi kaonewa.
Nilimweleza ukweli Bantu kama atafanya upuuzi wake nitamrudisha kijiweni kwake. Bantu alisema kuwa hayo ni maneno yua uzushi kwa kuwa nilikuwa nampenda nilimkubalia.
Siku moja nikiwa kwenye moja ya saluni zangu nilipigiwa simu na mtu nisiyemjua na kunieleza kuwa Bantu ameonekana sehemu na mmoja wa wafanyakazi wangu na kunielekeza niende sehemu ile.
Niliondoka nikiwa nimechanganyikiwa na kwenda sehemu niliyo elekezwa mpaka chumba waliokuwemo niliambiwa. Nilikwenda moja kwa moja hadi chumba nilicho elekezwa. Niligonga baada ya muda mlango ulifunguliwa nilikutana uso kwa uso na mfanyakazi wangu akiwa kwenye taulo bila kitu chochote mwilini ilionyesha si muda mrefu wamemaliza kufanya uchafu wao.
Aliponiona alishtuka nusra azirai kwa mshtuko nilimsukuma ndani na kuingia kama polisi. Nilimkuta Bantu akiwa amejifunika shuka mwisho kiunoni kifua kilikuwa wazi nguo zake zilikuwa zipo juu ya kochi.
"Ha! Bantu unafanya nini?"
Bantu alishtuka na kujikuta akinyanyuka bila kujielewa na kubakia mtupu na kuja kuniomba msamaha, kwa hasira nilimwambia:
"Nilikwambia nini umerudia nini?"
"Nisamehe anti Konso."
"Bantu huna tofauti na jini lililotolewa kwenye chupa ambalo baada ya kushukuru linataka kukumeza huna budi kurudishwa kwenye chupa kijiweni kwako."
"Hapana anti Konso ni shetani tu, ukiniacha nitakuwa mgeni wa nani?"
"Utajijua nipe funguo za gari langu, "nilikwenda hadi kwenye suruali ya Bantu na kuchukua funguo za gari langu kisha niliondoka kwa ghadhabu nikiwa nimevimba kama nataka kupasuka.
Nikiwa njiani niliwaza mengi juu ya tukio nilililoliona muda mfupi nilijiuliza nini anachokikosa kwangu mpaka aamue kutoka nje. Nilijiuliza nina mapungufu gani ambayo siyajui mbona wanaume wananiganda kama luba na kutangaza ndoa wanapo nionja au Bantu amenikinai mbona mapema au kuna kidudu mtu anayetaka kunihujumu.
Kumbe mdogo wangu yanauma ukitendea kwangu kuwafanyia wanaume nilikuwa naona sawa. Sikuwa na haja ya kwenda saluni nilirudi nyumbani moja kwa moja nilipofika nilikwenda moja kwa moja kwenye kabati ya pombe kali na kumimina glasi nzima na kunywa sio siri japo nimemfukuza Bantu nilikuwa bado nampenda.
Nilimimina glasi nzima iliyokuwa imejaa mvinyo mkali kwenye mdomo nilimeza kwa kukunja uso kisha nilijaza nyingine ambayo nilikunywa taratibu huku machozi yakinitoka.
Pamoja na ujasiri wangu wa kutobabaikia wanaume kitendo cha Bantu kiliniuma sana hasa nikizingatia alitakiwa anishukuru kumtoa kwenye maisha mabaya kweli mbuzi kamba ni yake mnyororo unamuonea.
Nikiwa bado naendelea kunywa pombe kwa fujo Bantu aliingia na kuja kunipigia magoti mbele yangu kuniomba msamaha
"Anti Konso naomba unisamehe sirudii tena."
"Bantu au kwa vile nimeonyesha nakupenda ndio umeamua kunifanyia upuuzi kama ule?" nilimuuliza huku nikilia kwa uchungu.
"Hapana anti Konso ni shetani siku zote watu wanatafuta sababu za kututenganisha ni maneno mengi juu yako nimeyavumilia eti wanasema kukaa na wewe na sawa na kujivundika kwa kuwa hata nikikuoa huwezi kuzaa watoto wote umewaua."
Mmh, mbona mapya yaani kumbe kulikuwa na watu wananichimba, ni kweli mdogo wangu sina kizazi baada ya kukitoa pale nilipotaka kuyafaidi maisha. Sasa hivi najuta na bwana niliye naye anataka mtoto mbona kimbembe. Na hii ilikuja baada ya kutoa mimba zaidi ya nne ambazo kidogo zinitoe roho yangu ndipo daktari wangu ambaye ndiye mtaalamu wa kutoa mimba za wake za watu ambao mimba huingia nje ya ndoa au hata wanafunzi," Kauli ile ilimkumbusha Sundi kitendo alicho fanyiwa na wifi yake Waridi kwa kukifunga kizazi kwa ajili ya starehe. Bado alirudiwa na kauli ileile kuwa matatizo ya maisha yanajirudia au kufanana.
Konso alinyamaza kwanza baada ya basi kusimama na kuagiza maji ya chupa, chupa mbili moja yake na nyingine ya Sundi baada ya kumpa alimshukuru. Konso alikunywa maji yote kulainisha koo baada ya kuongea kwa kipindi kirefu na kuitupa chupa tupu nje ya gari kisha alifuta maji kwa kipande cha mtandio aliokuwa amejitanda na kuendelea kuzungumza.
"Basi mdogo wangu Daktari yule alinipa siri nyingi na za watu wengi mashuhuri au wake za watu mashuhuli ambao si waaminifu kwenye ndoa zao ambao wanapopata ujauzito wa nje ya ndoa hukimbilia kwa yule daktari na kuichomoa hasa baada ya kuingia hiki kipimo cha DNA kimewafanya wanawake wengi wawe roho juu na utoaji wa mimba umeongezeka kwa kiasi kikubwa kwa watu kuhofia ndoa zao. Pia wanafunzi wengi wa vyuo vikuu shule za sekondari hata wa shule ya msingi.
Kama kuna siku nilikutana na kisichana cha miaka kumi na moja kilichokuwa darasa la sita shule ya msingi kwa kweli sikujua kimefika pale kufanya nini. Taafifa za kile kibinti kiliniacha mdomo wazi eti kimetoka kuchomoa mimba ya kigogo mmoja mtu mwenye wadhifa wake serikalini.
Halafu kilichonitisha zaidi ni kwamba ile ni mimba ya tatu kuitoa. Mmh, mbona hali inatisha kweli dunia imekaa tenge yaani hata watoto wetu tunapishana nao kutoa mimba.
Daktari wangu alinishauri nifunge kizazi baada ya kuponea kwenye tundu la sindano, lakini cha ajabu mbona ile ilikuwa siri yangu mimi na daktari wao wamejuaje au ndio kazi ya daktari kuuza siri za watu kama anafanya hivyo atakuwa hafai.
Maneno ya Bantu yaliifanya akili yangu ikae sawa na kujikuta nikimsikiliza vizuri.

Itaendelea...
 
SEHEMU: 16

ILIPOISHIA:
Kama kuna siku nilikutana na kisichana cha miaka kumi na moja kilichokuwa darasa la sita shule ya msingi kwa kweli sikujua kimefika pale kufanya nini. Taafifa za kile kibinti kiliniacha mdomo wazi eti kimetoka kuchomoa mimba ya kigogo mmoja mtu mwenye wadhifa wake serikalini.
Halafu kilichonitisha zaidi ni kwamba ile ni mimba ya tatu kuitoa. Mmh, mbona hali inatisha kweli dunia imekaa tenge yaani hata watoto wetu tunapishana nao kutoa mimba.
Daktari wangu alinishauri nifunge kizazi baada ya kuponea kwenye tundu la sindano, lakini cha ajabu mbona ile ilikuwa siri yangu mimi na daktari wao wamejuaje au ndio kazi ya daktari kuuza siri za watu kama anafanya hivyo atakuwa hafai.
Maneno ya Bantu yaliifanya akili yangu ikae sawa na kujikuta nikimsikiliza vizuri.
SASA ENDELEA…

"Wewe nani kakwambia?"
"Kuna mama mmoja ambaye naye alinitaka kimapenzi."
"Wewe ulimuamini?"
"Siwezi kumuamini bila kupata uthibitisho."
"Basi Bantu jichunge na watu hao hawakutakii mema,"sikuwa na haja kuyakumbusha yaliyopita niliamua kumsamehe kwa kujua kumuacha bantu wapo watu wanaosubili kwa hamu ili wanicheke.
Nilirudisha mahusiano na Bantu ambaye kweli alionyesha kunielewa tabia za mwanzo zilirudi kitu kilichonipa faraja moyoni na kumpa kila alichotaka ili kuhakikisha hababaishwi na vishawishi vya nje.
Baada ya kumdhibiti Bantu niliendelea na kurusha roho na wazee wenzangu kwa kweli Bantu alikuwa nimempangia sehemu gani za kwenda ili tusije kutana nikiwa na wazee wenzangu ambao ndio wanao nilea mjini.
Siku moja usiku ilikuwa majira ya saa nne tukiwa tunajiandaa kulala na kipenzi changu Bantu. Mara nilipigiwa simu ambayo ilikuwa ya bwana yangu mmoja wa kiarabu Abdul akinijulisha kuwa ameingia jijini usiku ile na ndege na hayupo tayari kulala peke yake kwa hiyo alinitaka usiku ile ili tulale pamoja.
Kwa kweli katika wanaume zangu ambao hunipa pesa nyingi ni Abdul ambaye hata gari la kifahari nililotembea amenipa yeye na alikuwa nampango wa kuninunulia nyumba kubwa ambayo amesema ndiyo inalingana na hadhi yangu.
Sikuwa na jinsi kuondoka usiku ile japo toka niwe na Bantu nililala nje mara nyingi kwa kisingizio cha kazi nyingi. Bantu hakuwa na neno lakini nilikuwa sijawahi kuondoka nyumbani usiku tukiwa tumelala wanaume wote wanaonipigia simu usiku huwakatalia kwa kumheshimu Bantu.
Sikuwa na shaka nilinyanyuka na kwenda bafuni kuoga na kujipamba manukato siku zote Abdul hupenda manukato aliyoninunulia kila tukutanapo. Wakati huo Bantu alikuwa bado amelala, nilipanga kama ataamka mwenyewe nitamuaga lakini akikuta sipo tungeongea asubuhi dawa yake ni kurudi na zawadi ambayo itamziba mdomo.
Baada ya kujiandaa kila kitu wakati naweka mkoba wangu kwapani Bantu alishtuka usingizini na kunikuta mtu aliyelala naye akiwa katika hali ya kutoka.
"Vipi mwenzangu mbona hivyo?"
"A.a.aah kuna simu nimepigiwa sasa hivi kuna mzigo umeingia unatakiwa kupakuliwa usiku huu."
"Mmh,"aliguna Bantu.
"Kweli Bantu usinifikilie vibaya siwezi kukusaliti," bila kuelewa nilijikuta nikijiingiza kizimbani mwenyewe.
"Sio sikuamini bali muda mbaya kwa nini usiende kesho alfajiri?"
"Yaani muda huu ndio wameanza kupakuwa kibaya nimewaeleza kuwa naenda."
"Basi wacha nikusindikize usiku mkubwa huu si vizuri uende peke yako," Bantu alisema huku akinyanyuka kitandani ili anisindikize niliona mambo yameharibika kuongozana na Bantu. Hiyo mizigo nitamuonyesha ipi na kweli Abdul atanielewa nisipokwenda wakati nilimuhakikishia nipo peke yangu na kumwambia atanipata muda wowote. Nilijikuta njia panda bila kutegemea nilipata wazo
"Unajua nini Bantu?"
"Hata sijui."
"Hizi dili zetu ni za magendo kwa hiyo huwa hatuendi na watu kwa kuogopa polisi."
"Kwa maana hiyo unaniambiaje?"
"Wacha niende peke yangu hakuna tatizo nitafika salama na kurudi salama."
"Hayaa kama umesema mwenyewe mimi sina neno."
Nilimshukuru Mungu kwa kuweza kumdanganya Bantu wakati huo simu ya Abdul ililia niliipokea na kuongea kwa sauti bila kuhofu kwa kujua lazima Bantu atajua ndio hao tunao fanya nao dili.
"Nakuja sasa hivi."
"Wahi usije chelewa au kukuta vitu nusu si unajua raha ya kitu kipakuliwe ukiwepo."
"Wacha niwahi," nilimpiga busu Bantu na kumuwahi Abdul nilikuwa nimempiga changa la macho kama wasemavyi watoto wa mjini.
Nilikwenda hadi nje kwenye gari langu na kwenda hotel aliyofikia Abdul, nilipofika alifurahi kuniona.
"Ndiyo maana nakuamini Konso kwa mtindo huu siwezi kukunyima chochote ukitakacho."
"Nilikueleza ukweli kuwa nipo kwa ajili yako."
"Basi nikuoe kabisa."
"Haiwezekani labda ubadili dini wewe."
"Ulisikia wapi mwanaume anabadili dini?"
"Mara nyingi tu kama kweli unanipenda badili dini unioe."
"Mmh! Kwa mtindo huo itakuwa ngumu."
"Basi tuendelee kila mmoja na dini yake."
"Lakini Konso ungekubali nikuoe nitakupa zawadi kubwa sana ambayo ni zaidi ya kile ukifilkiliacho kukipata maishani mwako."
"Nipe muda."
Siku hiyo tulilala mpaka asubuhi huku tukifurahia maisha, kwa kweli sio siri uwezo wa Bantu kimapenzi uliwazidi wanaume wote niliokutanana nao.Wengi niliwapendea pesa zao wala si mapenzi.Ila Abdul yeye nilimpendea mapenzi ya moyoni mwake na kunipa chochote nikitakacho pia alikuwa mwanaume muelewa hakuwa na tofauti sana na Bantu tofauti yao ni pesa Abdul anazo na Bantu hana kitu. Kingine bantu ana uwezo wa kimapenzi ila Abdul huwahi kuchoka upesi.
Siku ya pili nilimuacha Abdul na kumwahi Bantu ambaye nilimkuta amelala, siku hiyo usiku tulipanga kukutana tena na Abdul mapema. Sikuwa na wasi nilijua nitamdanganya vipi Bantu, alikuwa kama ndondocha asiyejua kitu kila kitu kwake sawa .
Kama kawaida nilimweleza Bantu kuwa jioni nitakuwa kwenye biashara kwa hiyo naweza kurudi kesho kwa kujua hata kama Abdul hata ondoka bado Bantu nitamdanganya, kikubwa nilipanga kumnunulia gari dogo ambalo nitamuahidi pale anapoweka vizingiti vya mimi kutoka.
Japo mara nyingi huwa haniziwii lakini lazima niweke taadhali, siku zote kuti la mazoea ndilo linalo muangusha mgema. Kama kawaida ilipofika majira ya mchana wakati huo tulikuwa tumelala nilimjulisha Bantu mtoko wangu wa usiku.
"Mpenzi leo jioni ndio siku ya kufanya biashara ile ya jana usiku."
"Mmh, mbona hii imekuwa ya usiku?"
"Unakuwa kama mgeni cha usiku mara nyingi huuzwa usiku ukiona mchana ujue hata kupatikana kwake ni mchana."
"Lakini mpenzi mbona kuna biashara uliisha wahi kufanya usiku na kuiuza mchana?"
"Ukiona biashara ya usiku mimi sikwenda lazima kuna mtu nimemwamini...alafu unajua nini dear?"
"Hata sijui"
"Lile gari nililokuahidi lipo njiani"
"Wawooo siamini dear."
"Mwanzo huwezi amini nilikuwa nawaogopa kuwaamini wanaume kwa sababu ya kijana wa kwanza alivyotaka kunitia umaskini."
"Sio wote wenye roho ya nyoka ukimfuga akiwa mkubwa anakumeza."
Nilimpiga mabusu ya uongo na ukweli yaliyompumbaza na kujiona yeye ndiye yeye kumbe..."
Majira ya jioni nilijiandaa kama kawaida yangu nilijifukiza manukato anayoyapenda Abdul. Nikiwa namalizia kujikwatua Bantu aliniuliza swali.
"Dear manukato mazuri kama haya kwa nini upenda kupulizia kwa nadra sana?"
"Aah, si unajua waswahili ukipenda kujipulizia kila siku utasikia ninaringa ndio mara nyingi hujipulizia siku moja moja."
"Mmh, na kweli hawachelewi kukuroga."
Kama kawaida nilimpiga busu zito na kutoka nikimwacha akinisindikiza kwa macho. Mara nyingi ninapokuwa na Abdul huwa situmii gari langu zaidi ya magari ya kukodi. Nilikodi gari hadi kwenye hoteli aliyofikia Abdul na kumkuta akinisubiri kwa hamu kubwa.
Hatukuwa na muda wa kukaa tuliingia kwenye gari lingine la kukodi hadi kwenye kumbi ya starehe. Kila mmoja alipata kinywaji kilichomtoa nishai na kujimwaga kwenye ukumbi kusakata mziki.
Sikuwa nyuma nilisakata kisawasawa na kumpagawisha Abdul ambaye muda wote aliishia kunikumbati japo hatukuwa tukicheza blues. Pombe zikiwa zimepanda kichwani sikukubali kukaa chini nilicheza muda wote na Abdul.
Ilifikia hatua ya sisi wawili kubakia ukumbini tukisakata mziki uwezo wangu wa kuzungusha nyonga uliwafanya watu wasimame na kunishangilia. Hapo mimi nikawa siambiwi nilizidisha kujinyonga kama sina mfupa.
Baada ya mziki kuisha nilikumbatiana na Abdul na kuelekea kwenye viti vyetu huku watu wakiendelea kushangilia wengine wakiomba nirudie tena.Lakini Abdul alikataa kwa kusema hatukuja kutoa shoo bali kuja kujifurahisha kwa kucheza na kunywa pombe.
Nikiwa nimemkumbatia kwa mahaba mazito macho yangu yaliona kitu lakini hayakuamini kwa kuwa nilikuwa na uhakika kutokiona sehemu ile. Mbele yetu alikuwa amesimama Bantu akiwa kama anashangaa kama haamini macho yake kwa kile alichokiona.
Nilijikuta nguvu zikiniishia na kushindwa kwenda mbele kitu kilichomshtua Abdul na kutaka kujua kulikoni.
"Honey vipi mbona hauendi au pombe imekuzidia?"
Sikuwa na jibu nilijiuliza nitamwambia nini Bantu kwa kumdanganya kuwa nipo kwenye biashara ni wazi uaminifu wake kwangu ndio siku yake ya mwisho. Sikutaka kujua pale amefikaje japo nammiliki lakini sidhani kama nina haki ya kumuuliza pale amefuata nini, lakini nilijikaza kike na kumuuliza:
"Bantu huku umekuja kufanya nini?"
"Kabla sijakujibu huyu ni nani?"
"Bantu siku hizi huniheshimu yaani unatoka bila idhini yangu?"
"Bado hujanijibu huyu ni nani?"
"Kwani dear huyu ni nani?" Abdul aliuliza.
"Abdul usiingilie we kaa pembeni."
"Hapana honey lazima nimjue huyu ni nani."
"Konso hapa ndio kwenye biashara inamaana kila siku unanila kisogo kwa kunidanganya kwa mtindo huu," Bantu aliongea kwa sauti ya kilio.

Itaendelea….
 
SEHEMU: 17

ILIPOISHIA:
Sikuwa na jibu nilijiuliza nitamwambia nini Bantu kwa kumdanganya kuwa nipo kwenye biashara ni wazi uaminifu wake kwangu ndio siku yake ya mwisho. Sikutaka kujua pale amefikaje japo nammiliki lakini sidhani kama nina haki ya kumuuliza pale amefuata nini, lakini nilijikaza kike na kumuuliza:
"Bantu huku umekuja kufanya nini?"
"Kabla sijakujibu huyu ni nani?"
"Bantu siku hizi huniheshimu yaani unatoka bila idhini yangu?"
"Bado hujanijibu huyu ni nani?"
"Kwani dear huyu ni nani?" Abdul aliuliza.
"Abdul usiingilie we kaa pembeni."
"Hapana honey lazima nimjue huyu ni nani."
"Konso hapa ndio kwenye biashara inamaana kila siku unanila kisogo kwa kunidanganya kwa mtindo huu," Bantu aliongea kwa sauti ya kilio.
SASA ENDELEA…

Mmh, nilijua nimevaa mkenge Bantu nitamueleza nini ili anielewe na Abdul nitamweleza nini ili anielewe.
Kimasilahi Abdul ni muhimu na kimapenzi Bantu ni muhimu swali linakuja nitumie lugha gani wote wanielewe, nilijikuta naongea lililokuja akilini.
"Bantu hebu njoo."
"Konso unanipeleka wapi?"
"Hapana Bantu hebu njooo huku tuongee."
"Honey huyu nani...kaka yako?"
Nilijikuta nanyanyua kichwa bila kujibu neno kumbe Bantu ameona, Mungu wangu hapo ndipo alipokuja juu kama moto wa kifuu.
"Konso kweli umenichoka yaani mimi ni kaka yako?"
"Mbona sikuelewi...vipi bwana mdogo una tatizo gani kama dada yako ametoka bila ruksa ni kiasi cha kuelewana," Abdul alimsogelea Bantu na kumpoza.
"Basi bwana shemeji hapa ni sehemu ya starehe hakuna haja ya kupigizana kelele na dada yak...."
He! hakumalizia sentesi ngumi nzito ya mkono wa kushoto ya Bantu ilitua kwenye shavu la mkono wa kulia kwa Abdul lililomtupa kwa nyuma. Nilijikuita napiga ukelele.
"Ha! Bantu unafanya niniii?" kumbe kipigo kile hakikuwa cha Abdul peke yake kiligeukia kwangu huku nikifuatia na matusi mazito juu yangu. Kwa kuitwa mwanamke malaya fagio la chooni jamvi la wageni basi kila aliloliona linanifaa kutukanwa.
Kipigo nilichopewa na Bantu kilinifanya nipoteze fahamu na kuzinduka siku ya pili na kujikuta nipo hospitali nimelazwa. Muuguzi alinieleza kuwa jana usiku tuliletwa na mume wangu tukiwa tumepoteza fahamu ila mume wangu ndiye mwenye hali mbaya kwa kuwa alikuwa na majeraha mengi.
Japo najua ni Bantu ndiye aliyetoa kipigo ni nani niliyeletwa naye hospitali ni Abdul au Bantu. Kutokana na matibabu mazuri niliweza kunyanyuka mwenyewe na kuweza kutembea japo mwli ulikuwa ukiniiuma kwa mbali, nilijua bila dawa za maumivu maumivu yangekuwa makubwa.
Nilikwenda ofisi ya wauguzi na kuwaomba wanionyeshe bwana niliyeletwa naye usiku.Tuliongozana na yule muuguzi hadi kwenye wodi ya wanaume na kuingia. Mmh, kumbe alikuwa ni Abdul ambaye alikuiwa kwenye plasta ikionyesha aliumizwa sana.
Nilikwenda hadi kwenye kitanda chake aliponiona alianza kulia.
"Konso kosa langu nini mpaka utake kuniua?"
"Pole Abdul yule ni kaka yangu."
"Muongo mkubwa mwanamke mbaya wewe, kwa nini Konso ukuniambia ukweli kuliko kunifanya hivi ona sasa mambo yangu yote yamevurugika...kwa nini ukuniambia ukweli kama una bwana?"
"Nisamehe Abdul."
"Siwezi kukusamehe wewe ni muuaji yaani kila ulichotaka nilikupa matokeo yake unanifanya hivi hata sijui nitakuwa kwenye hali gani nikitoka nimeambiwa mbavu zimeteguka."
"Lazima nimshtaki."
"Haitasaidia nimeishaumia ana haki kwa vile ni mumeo."
"Abdul sijaolewa yule ni rafiki yangu wa zamani lakini tulikwisha achana."
"Leo hivi kesho nitegemee mauti...kwa mtindo huo mimi basi."
"Usiniache Abdul usiniache bado nakupenda lazima mshenzi yule nitamshikisha adabu."
"Haitasaidi kitu inatosha kweli shukrani ya punda nimeiona."
"Abdul...Abdul,” nilianza kulia kwa kweli kumkosa Abdul kwa ajili ya kula kulala Bantu sikubali lazima nimshtaki ikibidi nimfunge.
Kilio changu kilimfanya Abdul awaite wauguzi ili wanirudishe chumbani kwangu.
Niliondoka huku nikilia na kumchukia Bantu hata kama sikumuaga hakuwa na haki ya kunipiga kwa sababu maisha yake niliyamiliki mimi hakuwa tofauti na mwanamke. Upande mwingine wanawake wengi wameamka kila mtu siku hizi anajitafutia.
Nilirudi hadi chumbani kwangu na kuanza kulia kwa hali aliyokuwa nayo Abdul kama kweli angekuwa ameumia kama alivyonieleza basi lazima hakutakuwa na mapenzi na mimi hawezi kunisamehe.
Siku ile ilipita hakukuwa na mtu wa kuja kunijulia hali mpaka siku ya pili nilipopata ruhusa ya kwenda nyumbani. Japo bado nilikuwa naumwa lakini nilikuwa na afadhali kubwa, kabla ya kuondoka nilikwenda chumba alicholazwa Abdul ajabu nilikuta shuka tupu kitandani wazo langu lilikimbilia kuwa Abdul amekufa na kuanza kulia kwa sauti ya juu iliyowavuta wauguzi kutaka kujua kulikoni
"Vipi da’ Konso mbona unalia?"
"Jamani Abdul yupo wapi..au ameisha kufa?"
"Hapana dada hajafa."
"Sasa atakuwa wapi au amezidiwa sana yupo chumba cha wagonjwa mahututi?"
"Hapana hayupo chumba cha wagonjwa mahututi."
"Sasa atakuwa wapi?"
"Ametolewa hospitali."
"Amepona?"
"Hapana."
"Kwa nini basi ametoka?"
"Amehamishwa hospitali na ndugu zake."
"Ha! kwa nini hamkuniambia?"
"Alikataa tusikuambie," kauli ile ilinikata maini niliongea kwa sauti ya kukata tamaa.
"Ooh, maskini."
Sikuwa na jinsi zaidi ya kugeuka na kuondoka, nilikodi gari hadi nyumbani. Nijani nilikuwa na wazo nikifika nyumbani nikimkuta Bantu namfukuza kama mbwa aliyekula mayai. Nilikwenda hadi nyumbani lakini ajabu sikumkuta mtu nilijiuliza Bantu atakuwa amekwenda wapi. Ilibidi nimuulize mlinzi wa getini.
"Eti Chodo Bantu yupo wapi?"
"Mmh, na siku ya pili sijamuona..mmh nakumbuka siku ya mwisho kama sikosei aliniaga kuwa anatoka mara moja lakini sikumuona kurudi mpaka leo hii."
"Atakuwa amekwenda wapi?"
"Hata mimi nashangaa."
"Ina maana ndiyo tabia yake kuondoka kwa muda wa siku nyingi ninapokuwa nimetoka?"
"Mmmh .ha.ha.pana yaani Bantu bwana siku hizi huwa hatoki akitoka sana huja hapa kupiga stori na kisha hurudi ndani hata chakula akinunua kama haupo huwa tunakula pamoja...Yaani Bantu mtu freshi sana."
"Mm..mmh sasa atakuwa amekwenda wapi lakini Chodo utakuwa unajua vizuri kama Bantu rafiki yako lazima utajua yupo wapi."
"Ukweli sijui mama mara nyingi hata siku ambazo hutoka usiku huwa hachelewi kuja na akirudi huniletea mzinga wa pombe kali husema siku moja moja hujichanganya viwanja..alafu alisema eti wewe ulimpiga mkwala juu ya wanamke."
"Mmh,"nilishusha pumzi ndefu na kuinama huku nikiwaza bila kupata majibu nilijiuliza inamaana baada ya ugomvi ule kaamua kuondoka moja kwa moja kwa nini basi asichukue nguo zake ambazo zote zilikuwemo au ndio kaenda kwa mashoga zangu waliokuwa wakimfuata fuata kama fisi mwenye njaa.
"Chodo hebu nieleze vizuri inamaana Bantu alipoondoka juzi usiku hajarudi tena"
"Sijamuona"
"Aliondoka saa ngapi?"
"Majira ya saa moja na nusu jioni"
"Acha utani yaani saa moja juzi mpaka leo hajarudi"
"Ni kweli mama kwani kuna nini?"
"Mmmh shuguli ipo"nilisema huku nikiingia ndani
"Mama kwani kuna nini?"mlinzi aliniuliza sikumjibu niliingia ndani na kwenda moja kwa moja hadi kitandani na kujilaza chali macho nikiwa nimetizama juu kwa mawazo mazito niliwaza
"Inamaana Bantu lazima kitendo changu cha kumdanganya kimemuuma sana na kuona kila siku nilikuwa namdanganya..mmh ni nani aliye mwambia mimi nipo kule lazima kuna wachawi wanao niwangia kila siku na kutaka kujua maisha yagu hyanavyo kwenda ili wayaalibu.
Nilijikuta nimepoteza watu wawili muhimu kwa wakati mmoja lilikuwa pigo kubwa moyoni mwangu.Niliamua kupiga moyo konde kwa kujua maji yamekwisha mwagika siwezi kuyazoa japo kumpoteza Abdul ni hasara kwa maisha yangu mwanaume aliyenijali kama mkewe wa kumuoa.
Tukio lile japo lilinishtua halikunichanganya akili kwa kujua nitapata mtu wa kuziba nafasi za watu wote siku zote nilijifananisha na ulezi chakula cha njiwa kila njiwa akionaye lazima atue.
Niliyaanza maisha yangu ambayo hayakuwa na mapungufu naweza sema Bantu lilikuwa ni pengo nilifananisha na mchungwa wa uani ambao sikupata tabu kuchuma matunda yake kila nilipo kuwa na hamu ya machungwa nilijua yatanighalimu kumpata mwanaume shababi awezae kunikata kiu ya mapenzi.
Hakuchukua muda nilipata bwana mmoja afisa wa jeshi ambaye aliingia kichwakichwa, mmh nilishangaa uwezo wake wa pesa alinipa kila nilichokitaka. Mapenzi yetu yalikuwa kukutana naye kwa wiki mara mbili.
Lakini alijikuta akinogewa na kuongeza siku zilikuwa mbili zikaja tatu mara nne ooh kila siku. Kukutana kila siku sio tatizo kilichoniudhi ni wivu wa kijinga hapo ndipo nilipoamua kuvunja mapenzi na yeye hakuwa tayari kuvunja mapenzi alinipiga mkwala asinione na mwanaume yoyote atamuua.
Mbona makubwa yaani mapenzi yalikuwa lazima nilimwambia mapenzi sio lazima masharti aliyonipa yanachekesha pale aliponiambia kama simtaki yeye basi niwakatae wanaume wote.
Nilijua ni maneno ya kuchanganyikiwa si mchezo mwanaume akiingia kichwa aliniganda kama luba.
Tatizo kubwa upande wangu ni kuwekewa wivu wa kijinga wakati hujanioa,baada ya kuacha na mwanajeshi nilijikuta nachagua mabwana wastaarabu nilipenda waume za watu ambao hawafanyi mapenzi kama chakula wao mapenzi ni starehe. Nilijikuta napata bwana mmoja ambaye alikuwa ni afisa katika kampuni ya mafuta kwa kweli pamoja na kuwa na pesa nyingi lakini alikuwa mstaarabu.
Siku za kukutana huniuliza kama nina nafasi na ninapo kuwa sina nafasi huwa hakasiriki lakini nilijitahidi kutokumuudhi. Nilipanga mipango yangu ambayo haikuingilia na mtu, nilipata wanaume za watu wanne ambao wote hawakujuana.
Niliweza kuwahudumia wote bila kujuana na kila mmoja alifurahia huduma niliyompa. Nilipata kila nilichokitaka kwa kweli ulikuwa mradi mzuri ambao ulikuwa haunighalimu nguvu nyingi.
Siku moja nikiwa nipo kumbi moja ya Hotel ambayo huenda na mmoja wa mabuzi zangu nikiwa nimemuacha chumbani baada ya starehe, nilitoka nje kufuata nyama ya kuchoma ambayo ilicheleweshwa na muhudumu niliamua kuifuata jikoni.
Baada ya kutoka nje nikielekea jikoni nilisikia nikishikwa mkono na mtu nilipogeuka nilikuta ni yule bwana yangu mwanajeshi.
"Hebu niachie we vipi?"
"Konso nilikuambia nini?"
"Kuhusu nini?"
"Ulifikiri nakutania basi leo ndio nitakuonyesha mimi ni mwanajeshi kuua kwangu ni jambo kawaida kama kupiga mswaki."

Itaendelea...
 
SEHEMU: 18

ILIPOISHIA:
Niliweza kuwahudumia wote bila kujuana na kila mmoja alifurahia huduma niliyompa. Nilipata kila nilichokitaka kwa kweli ulikuwa mradi mzuri ambao ulikuwa haunighalimu nguvu nyingi.
Siku moja nikiwa nipo kumbi moja ya Hotel ambayo huenda na mmoja wa mabuzi zangu nikiwa nimemuacha chumbani baada ya starehe, nilitoka nje kufuata nyama ya kuchoma ambayo ilicheleweshwa na muhudumu niliamua kuifuata jikoni.
Baada ya kutoka nje nikielekea jikoni nilisikia nikishikwa mkono na mtu nilipogeuka nilikuta ni yule bwana yangu mwanajeshi.
"Hebu niachie we vipi?"
"Konso nilikuambia nini?"
"Kuhusu nini?"
"Ulifikiri nakutania basi leo ndio nitakuonyesha mimi ni mwanajeshi kuua kwangu ni jambo kawaida kama kupiga mswaki."
SASA ENDELEA…

"Kwani mapenzi lazima?"
"Yaani umenifilisi ndio umeniaacha sio?"
"Nilikuita?"
"Sasa nasema nipeleke alipo huyo mwanaume ili ushuhudie namwaga ubongo."
"Siende popote."
Aliponishika kwa nguvu niligoma kwenda yule bwana alinishushia makofi mawili yaliyofanya masikio yazibe na kuona kizunguzungu akiwa amenishika kama kibaka aliyemtoroka askari hivyo kamshika makini nisimkimbie huku kashikilia bastora mkononi ili nimpeleke kwa yule bwana ambaye alikuwa chumbani akinisubiri nipeleke nyama choma.
Nilijua lazima bwana yule atafanya kweli kutokana na taarifa za matukio ya wanajeshi utasikia mwanajeshi amemuua mke wake na yeye kujilipua. Ilibidi niwe mpole ili nitunge uongo wa kumuokoa yule bwana. Kibaya zaidi yule mwanajeshi alikuwa amelewa lazima angefanya alichokidhamilia.
"Basi mpenzi taratibu."
"Pumbavu mpenzi wako nani?" makubwa, nilijibiwa huku nikipigwa kofi zito la kisogoni lililonifanya nione kiza mbele, nilisikia akisema:
"Unataka kunichezea leo ndio utanijua mimi ni nani wanangu walikuwa wanalala na njaa kwa ajili yako wengine wapo nyumbani kwa kukosa ada ya shule wewe unaleta mchezo..."
Mmh, shughuli ilikuwa pevu lazima nilijua amepania kuua, sikukata tamaa na kusema:
"Sikuja na mtu nipo peke yangu."
"Konso..Konso unataka nikumwage ubongo sasa hivi yule uliyeingia ndani ni nani unafikiri sijakuona kwa usalama wako nipeleke kwa hijali bila kutumia nguvu."
Nilijua mpaka kufikia hatua ile maneno aliyokuwa akiyaongea na pombe alizo kunywa lazima atafanya kitendo cha kihistori cha kumuua yule bwana na kuniua mimi kisha kujimaliza mwenyewe.
Sikuwa na jinsi nilijikuta nikisema kwa sauti ya upole baada ya kuona kuwa nimepatikana.
"Basi niache nikupeleke."
"Haya tangulia ukifanya ujanja nakumwaga ubongo."
Nilianza kuongoza chumba tulichokuwa kwa kuogopa kufanya ujanja wowote nitaambulia kipigo.Tukiwa tunakata kona kuingia upande wa vyumba tulikutana na watu wakikimbizana.
Walikuja na kupita katikati yetu na kutusukuma kitu kilichofanya bastora ya yule mwanajeshi kumuanguka wazo bila haraka bila kuchelewa nilitimua mbio kukimbilia nje kupitia katikati ya kundi la watu.
Nilikimbia kwa nguvu zote huku nyuma nilisikia mlio wa risasi sikugeuka hata nilipotoka nje ya hotel niliendelea kutimua mbio kwa mwendo wa robo saa wakati huo nilikuwa peku peku miguu yote ilikuwa na majeraha kwa kujikwaa njia.
Pamoja na kukimbia umbali urefu bado nilikuwa siamini kama nimeokoka, nikiwa nahema ovyo niliona gari likija niliamua kulipungia mkono ili linipeleke nyumbani. Lilisimama na kumwambia anipeleke nyumbani dereva aliniuliza:
"Vipi sister kuna usalama?"
"Sio muhimu kujua la muhimu niwahishe nyumbani."
"Pesa unayo?"
"Hata ya kukulisha wewe na mkeo."
"Ni majibu gani hayo sister?" majibu yangu hayakumfurahisha dereva.
"Umeyataka mwenyewe," jibu lilimziba mdomo na kukaa kimya aliponifikisha nyumbani nilimchukulia pesa ndani baada ya kuliacha pochi langu hotelini."
Siku hiyo sikulala mawazo yote yalikuwa juu ya tukio lililonitokea lilikuwa tukio la pili la kwanza nilipata kipigo na mpenzi wangu ambaye alivunjwa mbavu. Pia hapo nilimpoteza mtu muhimu kama Abdul. Ila ya muda ule kubwa ilikuwa napoteza maisha ya bwana yangu ambaye najua familia yake ingeathirika kwa namna moja au nyingine.
Nilijua mwendo kama nitaendelea kwenda nao lazima mwisho wake ni mauti, ilibidi nibadili tabia yangu ambayo mwenendo wake unatishia maisha yangu. Lakini sikutaka kuachana na waume za watu kwa kujua wengi niliokuwa nao ni wastaarabu.
Niliamua kubadili mtindo wa kukutana nao nyumbani kwangu kwa kujua nitakuwa nimejipusha na yule mwanajeshi ambaye dhamila yake ni mbaya kumkataa imekuwa nongwa kama angekuwa mstaarabu kama wenzake nisingekuwa na haja ya kumkataa. Eti nimesababisha maisha yake yayumbe nilimwita kama sio alipima injini ya pikipiki kwenye samitella kama sio kuipasua injini.
Mpango wangu wa kukutana na mabuzi yangu kwangu ulikwenda vizuri kwa kila mmoja kuja kwa wakati wake na siku ambayo atakayopangiwa. Kwa kweli nilijikuta kumbe mpango ule ningeutumia mapema mbona maswahibu ya kutokea kwenye tundu la sindano.
Mambo yaliniendea vizuri sikuwa na presha tena pesa ziliingia nina imani mwanajeshi atabung'aa macho mpaka yaote kengeza kwa kunitafuta kumbi za starehe.Tena nilifanya vizuri kutokumuonyesha kwangu.
Siku moja nikiwa natoka kufanya shoping super market nilivamiwa na watu ambao waliniteka na kuniingiza kwenye gari na kuondoka na mimi.Mmh, moyoni nilijua lazima watakuwa wametumwa na mwanajeshi kama itakuwa yeye nitakuwa nimekwisha.
Nilifungwa kitambaa usoni na kushindwa kuelewa wapi ninapo pelekwa na kwa nini wameniteka, kila nikiwauliza kosa langu nini niliambiwa.
"Kelele utalijua muda si mrefu."
Sikuwa na la kuongeza zaidi ya kutulia kusubiri kujua kilichofanya wanitendee kitendo cha kigaidi.Baada ya mwendo mfupi gari lilisimama na kuamliwa kuteremka.Baada ya kutelemka nilishikwa mkono na kupelekwa ndani ya nyumba.
Nilipofikishwa ndani nilifunguliwa kitambaa usoni na kuona nilipopelekwa.Mbele yangu kulikowa na kina mama zaidi ya watano waliokuwa wageni machoni mwangu. Nilikalishwa chini kwenye zuria.
Baada ya kimya kifupi mmoja wa wale kina mama alisema:
"Vijana mmefanya kazi nzuri..leo ndio siku ambayo atajua kuwa mume wa mtu ni sumu"baada ya kuongea vile hapo ndipo nilipopata wazo huenda hawa ni wake wa wale wanaume ninaowachuna.
"Konso"alinigeukia na kulitaja jina langu
"Abee"niliitika
"Unatujua sisi?"
"Hapana"
"Basi sisi ni wake wenzio ambao tunashea bwana mmoja"
sikujibu kitu kusikia vile moyo ulinipasuka na kujua leo ipo kazi.
"Sasa leo najua itakuwa mwanzo na mwisho wa kuchukua waume zetu na kujua maana halisi ya cha mtu mavi ukikiona kiteme mate"
"Jamani sikujua kama waume zenu naomba mnisamehe"
"Sisi waongeaji ila vijana watakupa zawadi nzuri...vijana kazi kwenu"
Baada ya kusema vile waliondoka wale wanawake watano na kuniacha na kundi la wanaume zaidi ya sita ambao bila kuchelewa walinivamia na kunivua nguo zote na kubakia mtupu na kuanza kunibaka kwa zamu.
Baada ya kumaliza kunibaka walinishushia kipigo kitakatifu ambacho kilinifanya nipoteze fahamu.Nilizinduka siku ya tatu na kujikuta nipo hospitali nikiwa nimefungwa bandeji kila kona ya mwili wangu.
Meno yoye ta mbele sikuwa nayo uso wote ulikuwa na mishono kama nguo ya maskini. Kwa kweli nilinitenda vibaya hata sijui ile ilikuwa ni laana ya wazazi wangu au nini. Maana matukio ya hatari yalikuwa yameongozana.
Nilitoka hospitali baada ya mwezi moja na nusu na kuruhusiwa kurudi nyumbani. Nikiwa nyumbani nilipata nafasi ya kujiangalia kwenye kuoo kikubwa ambacho mara nyingi hutumia muda mwingi kusimama kuusifia uzuri wangu lakini siku ile nusra nijikimbie mwenyewe.
Konso mimi nilikuwa na sura mbaya kama mzimu uliofufuka kila kona ya uso wangu ulikuwa na mshono wa jeraha. Meno sikuwa nayo lilikuwa pigo kweli mwanajeshi na yeye alikuwa na kila sababu ya kutaka kuniua au mkewe angejua ni mimi niliyesababisha nyumba yake kuyumba lazima angenitafuta na kunishikisha adabu.
Sikuwa tena Konso niliyekuwa nikitetemesha jiji lakini nilikuwa kama kinyago cha kutishia watoto vikojozi. Sikuwa na thamani tena mbele ya wanaume wote walinisababishia niwe vile walinikumbia.
Nilibakia kama Gendaheka dume la nyani lisilo na rafiki, mji niliuona mgumu sikuwa na hamu tena ya kuendelea kuwepo mjini. Wazo lililoniijia ni kurudi kwa wazazi wangu ili niwaombe msamaha japo niliondoka nyumbani zaidi ya miaka saba.
Nilifunga safari hadi nyumbani baada ya kuuza vitu vyangu vyote hadi kwa wazazi wangu. Ambao kwanza walinisahau lakini baada ya kujieleza hapo ndipo mama aliponikumbuka. Hali niliyokuwa nayo ilimfanya mama yangu na ndugu zangu kuangu kilio.
Niliwaomba msamaha wazazi wangu ambao walikuwa wameshiba dini walinisamehe na kuniona ni mwana mpotevu aliyerudi nyumbani. Konso mimi niliyaanza maisha mapya ya kuishi na wazazi wangu nikiwa mwana niliye zaliwa upya japo nilikuwa na sura mbaya lakini niliyafurahia maisha yangu kwa kushibishwa neno la Bwana.
Siku zote la kuvunda halina ubani maisha ya kuishi kwa wazazi yalinishinda na kuamua kuhama na kuanza maisha yangu mwenyewe yenye uhuru. Nilipata shoga ambaye nilishibana naye langu lake lake langu.
Siku moja alinipa wazo la kupata mwanaume nitaishi vile mpaka lini nilimkubalia na kunionyesha mbinu za kumpata mwanaume nimtakaye. Kuna bwana mmoja nilikuwa nampenda sana, basi nilipelekwa kwa mtaalamu. Kweli mdogo wangu yule bwana alinikubali bila kutegemea na sasa ndiye shemeji yako..
Ndio maana nakwambia ukimuona Simba anakula majani kazidiwa si hiyari yake na usiseme sifanyi muombe Mungu akuepushe na balaa ili kama si kwako basi kwa mumeo atakaye kuoa.
Lakini namshukuru Mungu sasa hivi sijambo hata uso wangu una nuru kidogo na haya meno ya bandia na kunifanya nionekane mtu kidogo mbele za watu kama huamini angalia picha hii na sasa nilivyo. Kila nikiangalia picha zangu za zamani na kuiangalia sura yangu ya sasa moyo uliniuma lakini sikuwa na jinsi maji yamekwisha mwagika. Kila aliyeziona picha zangu za zamani hakuiacha kunisifia
"Da Konso ulikuwa bomba."
Alitoa picha kipande kwenye mkoba na kumpa Sundi ambayo aliiangalia wakati huo Konso alikuwa amevua kabisa ushungi na uso wake kuonekana kwa uwazi. Sundi aliiangalia na kugundua mapungufu makubwa kwenye uso wa Konso baada ya kuridhika alimrudishia picha yake na kusema:
"Pole da Konso."
"Asante lakini nataka pole yako iwe yenye kujifunza jambo sio siku moja uwaze da Konso alinieleza."
Nitazingatia yote nashukuru kwa kunipa fundisho zito kwenye maisha yangu."
Wakati huo gari lilikuwa limefika Kibaha ambako Konso alikuwa amefika.
"Mdogo wangu mi ndio nimefika, lakini siku yoyote ukija Dar tena nitafute huku ndiko kujuana.”
"Da Konso usihofu nitakuja siku moja hata kulala kwako najua ni mengi uliyonayo yaliyokutokea mwenyewe au kusikia hata kuona."
"Karibu sana," walikumbatiana na Konso aliteremka.

Itaendelea...
 
SEHEMU: 19

ILIPOISHIA:
Alitoa picha kipande kwenye mkoba na kumpa Sundi ambayo aliiangalia wakati huo Konso alikuwa amevua kabisa ushungi na uso wake kuonekana kwa uwazi. Sundi aliiangalia na kugundua mapungufu makubwa kwenye uso wa Konso baada ya kuridhika alimrudishia picha yake na kusema:
"Pole da Konso."
"Asante lakini nataka pole yako iwe yenye kujifunza jambo sio siku moja uwaze da Konso alinieleza."
Nitazingatia yote nashukuru kwa kunipa fundisho zito kwenye maisha yangu."
Wakati huo gari lilikuwa limefika Kibaha ambako Konso alikuwa amefika.
"Mdogo wangu mi ndio nimefika, lakini siku yoyote ukija Dar tena nitafute huku ndiko kujuana.”
"Da Konso usihofu nitakuja siku moja hata kulala kwako najua ni mengi uliyonayo yaliyokutokea mwenyewe au kusikia hata kuona."
"Karibu sana," walikumbatiana na Konso aliteremka.
SASA ENDELEA…

Gari liliendelea na safari yake huku Konso na Sundi wakipungiana mikono.
***
Sundi aliwasiri majira ya alasiri na kukuta dada yake Cathy na mumewe ambao walikuwa wakimsubili kwa hamu kubwa. Alipoteremka hakuchelewa kuwaona kwa kuwa walikuwa usawa na mlango wa kutokea, alipowaona aliwakimbulia na kuwavamia kwa furaha.
"Wawoooo mdodo wangu karibu sana."
"Asante, shikamoni."
"Marahaba," waliitikia kwa pamoja huku wakimpokea mizigo na kuelekea kwenye gari.
Baada ya kuingia kwenye gari Cathy aliliondoa gari kitu kilicho mshtua Sundi na kuhoji.
"Ha! da Chathy na wewe unajua kuendesha gari?"
"Kwani mdogo wangu ni ajabu," alijibu huku akibadili gia.
"Sio ajabu ni maendeleo hata mimi mdogo wako utanifundisha?"
"Muda wako."
"Vipi bibie za nyumbani?"shemeji yake alimuuliza,
"Mmh, nzuri sijui ya nyuma."
"Karibu sana maana ulitususa."
"Shemu masomo si unajua kidato cha nne kilikuwa mshikemshike."
"Una matumaini kiasi gani?"
"Mmh sijui," Sundi alijibu huku akipandisha mabega juu.
"Basi nataka kidato cha tano na sita usomee huku."
"Shemu sasa hivi kusoma basi."
"Kwa nini?"
"Basi tu kusoma kunataka kuyapenda uyasomayo."
"Hapana kusoma kunatakiwa kusukumwa mnataka wote muishie kidato cha nne."
"Basi shemu nitasoma ngoja tusubiri matokeo," Sundi alikubali yaishe ili kuepuka maswali mazito ya shemeji yake ambayo yalimfanya akose jibu la maana.
Wakati huo gari lilikuwa linaingia nyumbani kwenye uzio wa nyumba, baada ya kuliingiza ndani alilisimamisha na wote waliteremka na kuingia ndani. Baada ya kuoga na kupata chakula Sundi aliongea na wenyeji zake habari zingine hakupenda shemeji yake ajue.
Siku ya pili baada ya shemeji yake kwenda kazini alishangaa kumuona dada yake naye akijiandaa kutoka ilibidi amuhoji.
"Da na wewe asubuhi asubuhi unakwenda wapi?"
"Mdogo wangu huu si wakati wa mwanamke kukaa bila shughuli hasa pale inapopatikana."
"Siku hizi unafanya kazi wapi?"
"Nina duka langu la vipodozi nimelifungua si mbali na hapa."
"Hongera, lina muda gani?"
"Sasa mwezi wa sita."
"Maendeleo?"
"Mmmh mazuri, mbona nilikuwa nimechelewa kazi nzuri na sasa hivi nipo kwenye hatua za mwisho kumalizia saluni ya kike."
"Usiniambie dada!"
"Tena nilikuwa nina mpango nikuite ili uisimamie kwa kuwa tuna mpango wa kufungua miradi mingi. Kwa vile umekubali kuendelea na masomo sio mbaya shida kubwa ya shemeji yako ni kukusomesha masuala ya kompyuta ili baadae usimamie Stationary anayotaka kufungua katikati ya jiji."
Zilikuwa habari zenye faraja kwa Sundi lakini sizo zilizompeleka pale zaidi ya akili yake ya kuolewa, kwa vile alikuwa amekwenda kwa sababu maalumu aliamua kumweleza ukweli dada yake ambaye kabla ya kutoa jibu alijikuta njia panda.
"Mmh, mazito yaani kumbe sisi tunakufikiria vingine na wewe nafikiria yako kweli mawazo hayafanani."
"Ni kweli na mimi natamani siku moja niishi kama wewe na kufikia kuwa kama mama na baba tena niwe mwalimu mwema kama wazazi wetu kwa watoto tunao wazaa."
"Ni kweli mdogo wangu,siwezi kukuingilia kwenye maamuzi yako kwa kuwa kila mwanadamu hujipangia jinsi ya kuishi kwa kuutegemea msaada wa Mungu."
"Sawa kabisa, kote nimepita mengi nimeyasikia japo hayapishani sana lakini hizo kasoro ndizo somo kubwa."
"Sawa mdogo wangu kwa vile umetaka kujua na mimi sitaacha hata moja kukueleza ukweli tukifika Saluni nitaangalia kazi kisha tutarudi nyumbani tuzungumze kwa kituo si unajua huu ndio muda muafaka shemejio hayupo."
Waliongozana hadi Saluni ambayo haikuwa mbali na wanapoishi ni mwendo wa dakika ishirini.Walipofika saluni alikuta tayari usafi umemalizika na kuwa katika hali ya kuanza kazi, baada ya kuwasalimia wafanyakazi wake ambao aliishi nao kama wadogo zake.
"Jamani kwanza kabla ya yote nilikuwa nawatambulisha mdogo wangu ambaye amefika jana."
"Ooh! Karibu sana dada jisikie upo nyumbani."
"Asante sana."
"Tena da Cathy mnafanana kama mapacha yaani mtu haulizi inaonekana mama yenu alikuwa muaminifu sana."
"Kwa nini Rehema unasema hivyo?" Cathy aliuliza.
"Da Cathy unaweza kukuta watoto wa baba na mama mmoja lakini kila mmoja ana sura yake.”
"Kwa hiyo unataka kusemaje kuhusu familia isipo fanana?"
"Mmh, hapo lazima ujue mama kamzidi akili baba."
"Mmh ni fikira potofu tu."
"Unasema tu dada, basi jana ndio nimepata picha ya mauaji yale ya kutisha ya jamaa aliyeua familia yake na yeye kujiua."
"Ray utanihadithia siku nyingine kwa sababu tuna haraka kidogo."
Sundi alijikuta akimlaumu dada yake kimoyomoyo kwa kumfanya akose kisa kingine ambacho alijua lazima kinamafundisho. Kwake aliamini si rahisi mtu kuua familia yake yote na kujimaliza mwenyewe.
Siku zote mficha uchi hazai, hakukubali kukaa kimya alijikuta ameingilia mazungumzo yale.
"Dada wacha atusimulie kwa sababu nina imani kulikuwa na jambo ambalo ni zito.Yaani mtu kuua familia yake yote na yeye kujiua lazima kuna sababu.
"Mmh, sawa nilikuwa na wasiwasi na wewe kwa vile umekubali hakuna shaka Ray unaweza kutupa kisa hicho."
"Basi da Cathy kama nilivyosema unakuta mtoto anazaliwa kwenye familia hafanani na mtu yoyote. Mama akiulizwa eti anafanana na babu yake kumbe mbegu kaiokota nje, basi nasikia yule jamaa baada ya kumuoa mkewe na kukaa naye kwa muda kumbe hakuwa muaminifu kwenye ndoa yake.
Alikuwa na bwana wa pembeni ambaye ndiye aliyekuwa amemfanya mumewe, hata kumuona mumewe si mali kitu. Basi yule mwanamke baada ya muda alibeba ujauzito na kujifungua mtoto wa kiume.Tena Mungu aliamua kumuheleleza yaani mtoto alitoka kopi laiti na baba wa pembeni.
Basi nasikia yaani yule bwana akapakwa mafuta kwa mgongo wa chupa kwa kuambiwa mtoto anafanana na marehemu babu yake kizaa mama mkwe. Kwa vile kitanda hakizai haramu baba alikubali kuwa kweli damu yake na kumuhudumia huduma zote.
Maisha yaliendelea watu wa pembeni wakijua kila kitu yaani kila jamaa alipokuwa akienda kazini mkewe alikuwa akimleta mtu wake ndani. Jamaa alikuwa mlinzi wa usiku, siku zilikatika wakababatika kupata mtoto wa pili mwenye sura kama wa kwanza.
Kwa vile alikuwa amekwisha ambiwa wanawe wanafanana na marehemu babu yao kizaa mama mkwe alikubali bila kuhoji na kuendelea kuhudumia kwa moyo mmoja bila kinyongo kumbe anahudumia sio damu yake.
Siku moja kwa maelezo ya watu yule bwana baada ya kutoka kazini katika tembea tembea yake alikutana na mke wake akiwa na bwana mmoja kwenye mazingira sio mazuri.Yule bwana hakuonyesha kushtuka japo wasiwasi wake ulionekana.
Hapo mkewe kwa kumfanya bwege mumewe alimtambulisha yule bwana kuwa mtoto wa mama yake mdogo upande wa mama yao. Japo alikuwa na wasiwasi aliamua kumchangamkia mtu aliyeambiwa ni ndugu ni vibaya kumdhani kumbe kweli na kupata aibu.
"Ndio shemeji za siku?"
"Nzuri tu, nilikuwa napita nikakutana na dada na kunieleza anakaa maeneo ya jirani."
"Ooh, vizuri karibu nyumbani basi."
"Siku nyingine nimeelekezwa nitakuja."
Basi kwa maelezo ya wadaku, msiniulize nilikuwepo, siku ya pili unaambiwa yule bwana alifika pale yaani bila aibu. Kwa vile jamaa alikwisha elekezwa yule ni nani, ikawa shemeji shemeji kumbe mume mwenzake. Yaani kuna wanawake huwafanya wanaume vipofu kwa kujiona wanayoyafanya watu hawajui."
Maneno yale yalimfanya Sundi kuendelea kuamini mambo mengi kwenye maisha yanafanana na kujirudia. Kwa mara nyingine amesikia neno likirudiwa tena yaani wanawake kuwageuza wanaume vipofu pale wanapoona wamewadhibiti, alijifikiria kwa kijisemea moyoni "au kwa sababu ya nguvu ya ushirikina.
"Basi yule mwanamke alifanya mambo kama mnyama mpaka yakawa yanawaudhi majirani. Siku zote wanadamu wanaweza kukunyima chakula sio neno. Basi mtu mmoja aliamua kumueleza ukweli mumewe juu ya tabia za mkewe.
Siku hiyo jamaa alikosa raha na kuamua kufanya uchunguzi wa kina pale alipowaangalia watoto wake wanafanana na nani. Baada ya uchunguzi wa kina alikubaliana na maelezo aliyopewa na mdaku mkeleketwa yaliyomshinda kuyaweka moyoni.
Jamaa alimuhoji mkewe ukweli juu ya yule bwana kuna ukweli gani juu yake na wale watoto. Mkewe alimjia juu na kumwambia kama amekubali kuwasikiliza watu wa pembeni yeye anaondoka hawezi kumdhalilisha kwa kumfanya kaka yake ndiye mzazi wa wale watoto.
Mkewe kwa kuona ameumbuka aliamua kuondoka pale nyumbani, kama unavyojua mazoea yana tabu, jamaa uvumilivu ilimshinda baada ya siku mbili mkewe kuondoka alimfuata na kumpigia magoti kwamba arudi nyumbani.
Mkewe kujua anapendwa si ndio alipozidisha manyanyaso na masharti mazito kwa mumewe. Kwa vile mumewe alikuwa akimpenda alikubaliana na kila alichotaka mkewe. Kwa vile alikuwa ameisha julikana alibadili sehemu ya kukutana kwa yule mwanamke.
Sharti kubwa lilikuwa anapoondoka nyumbani hakuna kumuuliza alikuwa wapi, hilo alikubaliwa bila tatizo si unajua kupenda ugonjwa. Mwanamke alizidisha dharau kwa mume wake hata kufikia kumnyima haki yake ya ndoa.
Kwa kweli jamaa aliishi kwa manyanyaso chini ya amri kali za mkewe, kwa vituko alivyofanyiwa na mkewe bila kuchukua uamuzi wowote ilionyeshwa jinsi alivyodhibitiwa na madawa ya kienyeji. Ilifikia hatua yule mwanamke kumjibu lolote mumewe bila kuhofia lolote.
Siku moja nasikia mumewe alikuwa amekaa uani na mkewe na mama mmoja wa jirani wakiongea. Mara mtoto wa yule mama alitumwa na baba yake na kukataa kwenda ndipo yule baba alipo mpiga yule mtoto aliyelia kwa sauti ya juu iliyomfanya yule mkewe kuja juu.
"Ukome kunipigia wanangu unajua uchungu wake?"
"Kwani bila mimi watoto hawa ungewapata?"
"Heheheeeeh Usinichekeshe mie,una uwezo kuzaa watoto wazuri kama hawa?"
"Kama sio mimi nani baba yao?"
"Utawahi! Watoto wa mwanaume mwenzako anaye ijua shughuli nazae na wewe nimerogwa."
"Aaah mama John ni maneno gani hayo umwambia mumewe,"ilibidi aingilie kati jirani.

Itaendelea...
 
SEHEMU: 20

ILIPOISHIA:
Siku moja nasikia mumewe alikuwa amekaa uani na mkewe na mama mmoja wa jirani wakiongea. Mara mtoto wa yule mama alitumwa na baba yake na kukataa kwenda ndipo yule baba alipo mpiga yule mtoto aliyelia kwa sauti ya juu iliyomfanya yule mkewe kuja juu.
"Ukome kunipigia wanangu unajua uchungu wake?"
"Kwani bila mimi watoto hawa ungewapata?"
"Heheheeeeh Usinichekeshe mie,una uwezo kuzaa watoto wazuri kama hawa?"
"Kama sio mimi nani baba yao?"
"Utawahi! Watoto wa mwanaume mwenzako anaye ijua shughuli nazae na wewe nimerogwa."
"Aaah mama John ni maneno gani hayo umwambia mumewe,"ilibidi aingilie kati jirani.
SASA ENDELEA….

"Mama Ashura kwani siri hata yeye anajua watoto hawa wa mwanaume mwenzie, niliondoka amenifuata."
"Ma Ashura yaache tumezoeana na mke wangu," alijibu yule mwanaume kwa sauti ya unyonge.
"Lakini sio majibu mazuri unaweza kufikiria kweli."
"Ni kweli atafanya nini kwanza nakaa naye kwa basi na nikiondoka nisikuone unanifuata."
"Jamani yamekuwa hayo ni kwa ajili ya mtoto tu au kuna mengine?" jirani aliuliza.
"Mama Ashura ondoka ya hapa uyawezi,"mwanamke alimwambia jirani ambaye aliondoka na kuacha zogo likiendelea. Basi tokea siku ile jamaa alikuwa mkimya kupita kiasi kila mtu alimuonea huruma kwa tabia chafu za yule mwanamke na kuwapa sifa mbaya wanawake wote.
Ndio siku moja jirani mama Ashura alifuatwa na yule mwanaume na kumuaga kuwa wana safari na familia yake. Ajabu mchana ule alisikia vilio ndani ya nyumba ile kwa kweli vilikuwa vya kutisha. Wengi walifurahi wakijua yule mwanamke amepatikana yaani unyonge umemwisha yule mwanaume.
Baada ya muda pakawa kimya na kufanya watu waliokuwa jirani kufuatilia tukio kuondoka wakijua yule mwanamke kwa kipigo alichokipata lazima atashika adabu. Kama kawaida mama Ashura baada ya kimya cha zaidi ya masaa matano akitaka kujua mama John yupo kwenye hali gani baada ya kipigo kikali.
Alipopiga hodi si ndio alipokutana na michirizi ya damu, kwa ujasiri mkubwa aliingia ndani picha aliyokuta ndani ilimfanya apike kelele na kutoka mbio lakini hakufika mbali alianguka chini na kupoteza fahamu.
Ndipo watu walimpa huduma ya kwanza na kuelezea aliyoyaona ndani.Watu hawakuamini mpaka walipoingia na kukuta mauaji ya kutisha ya watu kuuawa kwa kukatwa katwa kama nyama ya bucha. Mama John na wanae wakikuwa wameuawa kwa kutenganishwa viungo kwa shoka lililokuwa pembeni na yule mwanaume alikuwa amekufa kwa kujinyonga na kamba ya katani na kuacha ujumbe.
Ujumbe ulisema hivi:
Kwanza kabisa namuomba Mungu anisamehe kwa kitendo nilichokifanya cha kinyama ambacho kitaiweka jamii kwenye maswali mzito na kunijengea chuki mioyoni mwao. Lakini jamii nzima iliyonizunguka inatambua tabia chafu za mke wangu.
Niliweza kuvumilia japo walimwengu lililowachoma walinieleza ukweli. Nilishindwa kutoa maamuzi kwa kuwa mke wangu nilikuwa nampenda vilevile nilijua ni makosa ya kibinaadamu yanayorekebishika.
Niliamua kumuonyesha mke wangu mapenzi ya dhati ili aachane na upumbavu, kumbe nilikuwa nimejichongea hapo ndipo alipoonyesha dharau za wazi tena mbele za watu. Sawa nilijua watoto sio wangu lakini nilijua siku zote kitanda hakizai haramu.
Nimeamini ukicheka na nyani utavuna mabua au ukicheza na mbwa atakufuata mpaka msikitini. Mke wangu ilifikia hatua ya kuniambia upumbavu wake mbele za watu eti watoto sio wangu ni wa wanaume wenzangu.
Kwa kweli ilikuwa imevuka mipaka kwa kauli aliyoitoa mbele ya jirani yetu mama Ashura ambaye ndiye shahidi wetu mzuri. Ilinikosesha raha na kuona nimevuliwa utu wangu na sina thamani ya kuendelea kuishi.
Nilitaka kujiua mwenyewe lakini moyo wangu ulikataa kwa kuona sikuutendea haki ni heri tuondoke wote, ningeweza kumuua mke wangu tu na kuwaacha watoto najua lazima mtasema hawana hatia. Lakini moyoni mwangu walikuwa na hatia kubwa kwa kula jasho langu na kuwapatia kila kitu, lakini msaada wangu haukuonekana una faida kwao.
Hivyo niliamua na wao kuwaua baada ya kuonyesha na mama yao lao moja nao kufikia hatua ya kunidharau. Sikuwa na budi kuwaua na wao ili nikahukumiwe kwa hesabu kamili. Kwa kitendo changu naomba jamii ichukulie kama fundisho kwa wana ndoa kuheshimu ndoa zao. Si kwa wanawake kutoka nje ya ndoa hata wanaume nao. Mama yangu alimuua baba yangu pale alipogundua amezaa nje ya ndoa.
Ila naomba nililolifanya mimi au mama yangu la kumuua baba yangu lisirudiwe na mwingine na hii itatokana na maelewano upendo na uaminifu katika ndoa. Ni mimi baba John wa bandia.

Huwezi kuamini watu wote waliozipata habari zile walimlaumu mwanamke kuwa ndiye chanzo cha yale yote. Basi dada sisi tulikuwa tukiongea tofauti kwa kusema labda mwanaume alikuwa anavuta bangi au unga."
Baada ya maelezo yale Cathy aliguna kisha alivuta pumzi na kusema:
"Mmh, kwenye majumba kuna mambo ya ya ajabu ambayo ufanyiwa mwana ndoa mmoja wa kiume au wa kike. Kwa mtindo huu watu watazidi kumalizana Ray si unakumbuka juzi kumetokea msiba mzito nao kwa ajili ya mapenzi tena wana ndoa wa muda mrefu."
"Kile cha mchezaji wa Simba wa zamani?"
"Hicho hicho."
"Na chenyewe kimetokana na nini?"Sundi aliuliza.
"Kwenye magazeti wamesema kwa ajili ya wivu wa kimapenzi."
"Kibaya zaidi wamewaacha watoto ambao hawana mlezi."
"Kwani hawana ndugu?"
"Hata kama wapo malezi ya wazazi ni tofauti na ndugu siku zote tembo hashindwi na mkonga wake."
Maneno yale yalimfanya Sundi kuona ugumu wa ndoa, ni kweli ndoa nzito kwa nje ina rangi nzuri lakini ndani ni matatizo makubwa. Alikatishwa na sauti ya dada yake iliposema:
"Lakini siku zote ndoa unaijenga mwenyewe na kuibomoa mwenyewe hata matatizo mengine tunajitakia japo mengine hulazimishwa kufanya."
"Una maana gani?"Sundi alimuuliza dada yake amabaye wakati huo alikuwa ameisha simama na kuitengeneza gauni lake.
"Kwa mfano mama John matatizo kayatengeneza mwenyewe na mumewe amelazimishwa kufanya jambo ambalo akulikusudia kuifanya amelazimishwa na hali."
Baada ya maongezi yale Sundi na dada yake walielekea nyumbani kwa ajili ya maongezi yaliyokusudiwa. Baada ya kufika nyumbani dada yake kabla ya maongezi alikwenda bafuni kuoga na kuvaa upande wa kanga na mdogo wake alifanya vilevile.
Baada ya kukaa kwenye sofa ya mtu mmoja kila mmoja alimwelekea mwenzi, kabla ya maongezi kila mmoja alishikilia glasi ya juisi. Hapo ndipo maongezi yalipoanza.
"Ndio mdogo wangu nina imani ndoa yako itakuwa nzuri nakuombea kwa Mungu umpate mume kama wangu. Nina imani kwa jinsi ninavyokufahamu mtazeeka na kutenganishwa na kifo. Mdogo wangu huwezi kuamini toka niolewe na mume wangu simjui mwanaume wa nje.
Siwezi kusema kanikuta msichana sijaguswa, nilikuwa nimeisha wahi kufanya mapenzi na wanaume zaidi ya watano kwa vipindi tofauti kabla ya kuolewa. Lakini toka nimeolewa nimekuwa naishishimu ndoa yangu, nina imani mama yetu hili alilijua na ndio maana alituhusia tuwe waaminifu kwenye ndoa zetu kuepuka matatizo yaliyomkuta mama John.
Siku zote huwezi kutumikia mabwana wawili lazima mmoja atazidi nguvu na mara nyingi bwana wa pembeni huzidi nguvu wa ndani. Hapo lazima dharau hutawara ndoa yako na kufikia hatua ya kumuona bwana wa nje ni bora kulko mumeo wa ndoa," Cathy alinyamaza kidogo ili kunywa kidogo juisi ili kulegeza koo kisha aliendelea.
"Nina imani yote uliyopitia ni tofauti kubwa na maisha ya mwanzo wa ndoa yangu, mi mdogo wangu sijui niseme ushamba au nilikuwa na pupa ya mapenzi kama si ulimbukeni wa kupenda. Pale nilipoona mume wangu anapokuwa mbali nami basi nilijua naibiwa.
“Kwa pupa zangu nilijikuta nasahau yote au kuamua kuishi nitakavyo tofauti nilivyohusiwa na mama na dada juu ya maisha ndoa. Hapo ndipo nilipopotea mdogo wangu baada ya ndoa basi mdogo wangu katika vitu ninavyo vipenda duniani kama ningeulizwa ningejibu mume wangu, nampenda mume wangu mpaka mwenyewe najichukia.
“Najua utaona utani lakini kwa mwenye kujua kupenda maana yake nini, atakubaliana na haya nitakayo yasema leo. Basi mdogo wangu baada ya kumaliza kidato cha nne na matokeo yangu kuwa mabaya nilimuomba mama nije kwa dada huku Dar. Mama baada ya kushauriana na baba walikubaliana na hii ilikuja baada ya dada kuniomba niende Dar.
“Nilifika jijini mwaka wa kumi na mbili sasa wakati huo wewe sijui ulikuwa na miaka mingapi mmh, kama sikosei ulikuwa na miaka sita hata shule ya msingi ulikuwa hujaanza. Nilikuwa nimekuja kwa dada kumsaidia kazi za nyumbani kutokana na kutumia muda mwingi kazini.
Aliamua kunichukua baada ya kuibiwa na mtumishi wa ndani hivyo aliamua kuniita mdogo wake ambaye muda huo nilikuwa nimemaliza elimu yangu ya kidato cha nne na kupata matokeo mabaya. Sio siri ujio wa jijini ulinifanya nijisikie furaha isiyo kifani, hasa kutokana na sifa za jiji la Dar. Nilipokelewa na dada pamoja na shemeji na kuelekezwa majukumu yangu muhimu.Tokea hapo nilikuwa mtumishi mzuri wa ndani kitu kilichofanya shemeji na dada wanipe sifa nyingi na zawadi kibao.
“Tabia yangu haikuwa ndani ya nyumba bali hata kwa majirani, japo dada hakupenda kuwa nao karibu lakini hao ndio waliokuwa wakiniondoa ukiwa. Jumba lote ningewezaje kukaa peke yangu, lazima ningekosa raha na kutamani kulikimbia jiji.
“Katika maisha waliokuwa wakiishi shemeji na dada yalinifanya nisikie wivu na mimi kuomba Mungu anijalie mume kama shemeji. Niliuahidi moyo wangu kuwa nitampenda mume wangu zaidi ya dada na upendo wangu hautajificha lazima nimuonyeshe ninavyo mpenda na yeye hatambue nampenda.
“Siku moja nikiwa na dada tukiwa wawili nilimuuliza siri ya ndoa yake hasa tukizingatia ndoa nyingi zimejaa migogoro na zilizobaki kukosa uaminifu na zingine kuvunjika kabisa na kuwaacha watoto wakikosa mwelekeo wa kimaisha au kuangukia kuwa watoto wa mitaani.
Dada alinieleza kuwa:
"Mdogo wangu ndoa zina siri nyingi usione watu wametulia wengi wamepitia mitihani mizito yenye kukatisha tamaa," kauli ile ilinishtua kidogo na kutaka kujua mitihani gani hiyo.
"Dada mbona unanitisha?"
"Sikutishi mdogo wangu siku zote sala zako muombe Mungu akupe ndoa yenye baraka mume mwenye mapenzi na wewe mwenye kukujali."
"Una maana gani kusema hivyo?"
"Nina maana unaweza kupata mume mwema lakini mashetani wa kidunia wakamuhadaa na kuisaliti ndoa yake, lakini kama Mungu atakuwa ameibaliki ndoa yako basi lazima atailinda."
"Mmh, dada mbona kama nauona uzito mbele yangu kuhusu ndoa."
"Hakuna uzito ni kumuomba Mungu kama nilivyo kwambia."
"Na mitihani hiyo ni ipi?"
"Huwezi kuamini leo mimi na shemeji yako tunaongea na kucheka kuwa kuna kipindi tulikuwa kama chui na paka. Ilifika hatua hatuongei na tunalala vitanda mbalimbali au kulala kwa kupeana migongo kitu kilichokuwa kikiipeleka pabaya ndoa yetu...
Lakini nilikutana na mama mmoja wa makamo mwenye hekima zake na kumweleza tatizo lililo nikabili cha kwanza aliniomba niwe mvumilivu kwani aliniambia uvumilivu ndio njia pekee ya kuinusuru ndoa ambayo imeingia matatizo. Hasa pale mwanaume anapokuwa amekumbana na mashetani wa kike ambao mara nyingi ndio vyanzo vya matatizo ya ndoa nyingi," maneno ya dada yalinifanya nitulie tuli kusikiliza kwa makini, aliendelea.
"Basi mdogo wangu yule mama aliendelea kuniambia siku zote mjenzi wa nyumba yenye ufa ni wewe mwenyewe na siri ya ujenzi huo ni wewe kukubali matokeo kwa kushuka chini kuonyesha upendo kwa mume wako kutokuwa mbishi wala mkaidi bila kusahau kumuomba Mungu usiku na mchana ili amrudishe kundini mumeo aliyepotea.
“Nilifanya hivyo na kutopunguza mapenzi kwa mume wangu hatimaye Mungu alimrudisha na kutambua makosa yake ndio maana mpaka leo hii unatuona tupo kwenye hali hii, Cathy dada yako nilikonda na kubakia mfupa na ngozi."
"Kwa hiyo dada unataka kuniambia nini pindi nipatapo mume wa kunioa?"

Itaendelea...
 
SEHEMU: 21

ILIPOISHIA:
"Huwezi kuamini leo mimi na shemeji yako tunaongea na kucheka kuwa kuna kipindi tulikuwa kama chui na paka. Ilifika hatua hatuongei na tunalala vitanda mbalimbali au kulala kwa kupeana migongo kitu kilichokuwa kikiipeleka pabaya ndoa yetu...
Lakini nilikutana na mama mmoja wa makamo mwenye hekima zake na kumweleza tatizo lililo nikabili cha kwanza aliniomba niwe mvumilivu kwani aliniambia uvumilivu ndio njia pekee ya kuinusuru ndoa ambayo imeingia matatizo. Hasa pale mwanaume anapokuwa amekumbana na mashetani wa kike ambao mara nyingi ndio vyanzo vya matatizo ya ndoa nyingi," maneno ya dada yalinifanya nitulie tuli kusikiliza kwa makini, aliendelea.
"Basi mdogo wangu yule mama aliendelea kuniambia siku zote mjenzi wa nyumba yenye ufa ni wewe mwenyewe na siri ya ujenzi huo ni wewe kukubali matokeo kwa kushuka chini kuonyesha upendo kwa mume wako kutokuwa mbishi wala mkaidi bila kusahau kumuomba Mungu usiku na mchana ili amrudishe kundini mumeo aliyepotea.
“Nilifanya hivyo na kutopunguza mapenzi kwa mume wangu hatimaye Mungu alimrudisha na kutambua makosa yake ndio maana mpaka leo hii unatuona tupo kwenye hali hii, Cathy dada yako nilikonda na kubakia mfupa na ngozi."
"Kwa hiyo dada unataka kuniambia nini pindi nipatapo mume wa kunioa?"
SASA ENDELEA….

"Cha kwanza kutambua mumeo mpaka amekuchagua kukuoa basi ujijue wewe ndiye chaguo la moyo wake na wewe lazima umpende na kuhakikisha hajutii uchaguzi wake na kumfanya umteke kiakili na kimawazo na kukuona wewe na bora kuliko wanawake wote.
Mheshimu na kumpenda ikiwa pamoja na kuwa mbunifu kuhakikisha kila siku mumeo akuone kiumbe kipya, usafi vilevile ni muhimu mwanamke kuwa msafi wakati wote hata mumeo akirudi kazini akukute umeishaoga unanukia vijifuta sio lazima viwe vya bei mbaya bali kulingana na hali yenu ya maisha. Usiwe karaha kwa mumeo kwa kulazimisha vitu vilivyopo nje ya uwezo wake.
Lazima umsome mumeo anataka nini ili ukifanye muda wote na kukiacha kinacho muudhi. Siku zote mumeo atakupenda na kukujali hata kama umepotoka ni rahisi kurudi kundini."
"Mmh, dada nitajitahidi, unajua dada siwapendi wezi wa waume za watu."
"Hao ndio wabaya wapo kama mamba wanameza bila kutafuna."
Baada ya maongezi na dada tuliachana na kumwacha apumzike na mimi kumalizia kazi ndogo ndogo zilizokuwa zimebakia. Muda wote nilikuwa nikiwaza yote niliyo ambiwa na dada na kuapa kumlinda mume wangu muda wote.
“Siku zote nyota njema huonekana asubuhi na mapem mmoja wa waumini wanaosali kanisa moja na shemeji ambaye mara nyingi alikuwa akija pale nyumbani alivutiwa na mimi na kutaka kunioa. Ombi alilifikisha kwa shemeji na yeye alimwambia dada na mimi kuulizwa nilikubali mara moja.
Kilifanyika kikao cha harusi na hatimaye ndoa ilikubaliwa na matayarisho yalianza. Wazazi wetu toka Mbeya walihudhuria harusi ambayo ilikuwa kubwa kiasi, japo kwa upande wangu niliona bonge la sherehe. Kama kawaida wazazi wangu baada ya harusi waliniita nakuniasa juu ya ndoa na jinsi ya kuishi na mwanaume, hayakuwa na tofauti na yale aliyoyaeleza dada, wao waliongezea kuwa:
"Mumeo mlee kama mwanao ni wewe wa kumtuliza na ni wewe wa kumkimbiza ndani. Kauli njema itawale mdomoni mwako muda wote kwa kuwa wimbo mbaya habembelezewi mtoto." Baada ya yote wazazi kurudi nyumbani Mbeya, niliyaanza maisha mapya ya uchanga kwenye ndoa. Kwa kuyazingatia yote niliyoelezwa na wazazi wangu. Nilijitahidi kuonyesha mapenzi mazito kwa mume wangu na yeye aliyaonyesha kwangu.
Miezi sita ilikatika bila tatizo lolote kwenye ndoa yangu nami nilinenepeana mpaka nilishauriwa nifanye mazoezi kwa kuhofia kupata presha. Kutokana na shughuli za mume wangu yakaanza mabadiliko ya kuchelewa kurudi kazini.
Mwanzoni nilijua ni jambo la kawaida, lakini kila siku likawa la kawaida mume wangu kurudi saa mbili mpaka tatu usiku. Kila nikimuuliza mume wangu alinijibu ni kutingwa na kazi za kiofisi.
"Mume wangu ni kazi gani hizo za kuchelewa kila siku?"
"Mke wangu hiki ni kipindi cha mahesabu ya kufunga mwaka lazima tutumie muda mwingi kufunga mahesabu."
Nilimkubalia kishingo upande lakini moyoni nilijua ndio yaleyale ya dada tayari shetani wa kike kaisha mkamata mume wangu. Nilijikuta nakosa raha hata hamu ya chakula sikuwa nayo nilianza kukonda mtoto wa kike kitu kilicho mshtua mume wangu.
Alipotaka kujua nimekumbwa na kitu gani nilimjibu kwa mkato:
"Hakuna tatizo."
"Hapana mke wangu kuna tatizo hebu niweke wazi."
"Ningekuwa na tatizo ningekuambia nipo sawa."
Nilijikuta naingia kwenye maumivu ya moyo kila muda ambao mume wangu alipochelewa kurudi, hujikuta nalia peke yangu kwa kuona ndoa yangu imekalia kuti kavu kuanguka si ajabu. Basi mdogo wangu siku moja nikiwa nimejilaza kwenye mkeka majira ya saa tisa alasiri. Niliijiwa na njozi mume wangu yupo na mwanamke wakipapasana ofisini mwake.
Nilijikuta nashtuka usingizini na kuanza kuhema kwa kutweta na jasho jingi lilinitoka. Nilijikuta nakosa raha wazo lililo nipata nimfuate huko huko ofisini. Nilikwenda bafuni kuoga haraka haraka na kubadili nguo nilikodi gari hadi kazini kwa mume wangu. Nilipofika nilikwenda moja kwa moja hadi ofisini kwake na kukutana na secretary wake, alipo niona alinikaribisha kwa heshima zote.
"Karibu dada."
"Asante, huyu bwana yupo?"
"Yupo, mbona hivyo kuna tatizo?"
"Hakuna tatizo, naweza kumuona?"
"Subiri nimjulishe."
"Umjulishe ili iweje?" nilijua anataka kumshtua ili ajiandae nisiweze kumfumania sikumsilikiza nilikwenda moja kwa moja na kuufungua mlango wa ofisi ya mume wangu. Kitu kilichomshangaza secretary wake.
Nilishangaa kumkuta mume wangu peke yake akiwa bize kwenye lap top yake ambayo hata nyumbani hurudi nayo. Aliponiona ajabu hakushangaa zaidi ya kunikaribisha kwa kuacha ile computer mpakato na kuja kunilaki.
"Ooh, mpenzi karibu sana, mbona saa hizi?"
"Kwako mimi nina muda maalumu wakukufuata ofisi?" nilijikuta nikimuuliza kwa hasira.
"Hakuna, lakini ni muhimu kunijulisha simu ina kazi gani?"
"Ooo..ooh ili upate kufanya ufisadi wako kwa taadhari!"
"Mbona sikuelewi?"
"Bahati yako."
Nilijibu vile huku nikitoka ofisini bila kusema neno lingine kitu kilichomfanya mume wangu anifuate na kutaka kujua maneno yangu yana maana gani. Sikumjibu neno lolote zaidi ya kulia, mume wangu alinibembeleza na kutaka kujua nilikuwa na maana gani na yote niliyoyasema:
"Mke wangu kwa kweli una mabadiliko makubwa hasa toka niwe kwenye shughuli za mahesabu, najua huniamini lakini amini ni wewe peke yako moyoni mwangu. Sitakwenda kinyume na ahadi yetu."
Sikumjibu mume niliendelea kulia kitu kilichomfanya mume wangu aache kufanya mahesabu na kuondoka na mimi hadi nyumbani. Nilipofika nyumbani nilimweleza kuwa siku hizi amekuwa si muaminifu kwenye ndoa yetu.
Yeye alikataa katakata na kusema:
"Cathy huu si wakati wa kurukaruka nina kosa nini kwako kila sifa ya mwanamke mwema unayo tena na kuzidi niamini mke wangu."
Nilikubaliana na mume wangu kwa mdomo lakini nilipanga lazima nimfumanie, roho yangu ilinituma ni yule secretary wake ndiye mwanamke wake. Nilianza tabia ambazo japo zilikuwa zikuimuudhi mume wangu lakini nilijua zinanisadia kuokoa ndoa yangu kwa kwenda ofisini kwa mume wangu bila taarifa na siku zote nilitoka patupu.
Niliona tabia ya kwenda mchana ameigungua niliamua kumfuatilia muda wa kutoka. Nilikodi gari hadi ofisi kwake majira ya saa moja na nusu usiku na kujificha kumsubiri ni kweli akitoka kazini anakuja moja kwa moja nyumbani au anapitia nyumba ndogo.
Kama kawaida niliwasili muda huo na kukaa kwenye gari macho yakiwa kwenye ofisi ya mume wangu, baada ya nusu saa nilimuona mume wangu akitoka ofisini koti na mkoba akiwa ameshikilia yule secretary wake. Moyo ulinipasuka na kuwa na uhakika kuwa yule ndiye kidudu mtu.
Nilimuona akiingia kwenye gari la mume wangu na kisha kuondoka pamoja, nilimwambia dereva aifuate ile gari ili nijue wanakwenda wapi. Wakati huo moyo ulikuwa ukinidunda na kunifanya nipumue kwa shida.
Dereva wa teksi alilifuata gari la mume wangu kwa nyuma, nalo lilielekea sehemu nisiyo ijua. Baada ya mwendo wa dakika kumi gari nililopanda liliishiwa mafuta, ilisababisha tuingie kituo cha mafuta tuongeze kwa vile palikuwa na foreni tulichelewa kuweka mafuta na kupotezana na mume wangu kitendo ambacho kiliniumiza roho na kujikuta nikimgombeza dereva.
"Ni uzembe gani ulionifanyia, tulikuwa na umuhimu gani kusubiri muda wote?"
"Samahani dada sikuangalia mapema mafuta yapo kiasi gani."
"Huna maana nirudishe nyumbani."
Dereva aligeuza gari na kunirudisha nyumbani niliwa nimefura kwa uzembe wake. Bahati nzuri nilifika nyumbani kabla mume wangu hajarudi, nilimsubiri kwa hamu kubwa ili anieleze amepitia wapi.
Baada ya dakika tano mume wangu aliwasili nyumbani na kunikuta nikiwa nimevimba nusu ya kupasuka. Hata sikuwa na haja ya kumpokea nilijiinamia na kuanza kulia, mume wangu hata bila kutua vitu vyake alinisogelea na kuanza kunishika begani.
Niliteremsha bega chini na kuuondoa mkono wake,lakini hakuchoka:
"Mke wangu ni nini kilichokusibu siku hizi au ndio hivyo vikao vyako vya pembeni angalia vitavunja nyumba yetu kisha watucheke."
"Niambiwe na nani zaidi ya kukuona kwa macho yangu."
"Mke wangu umeniona nafanya nini?"
"Ulipotoka kazini umekwenda wapi?"

Itaendelea
 
SEHEMU: 22

ILIPOISHIA:
Baada ya dakika tano mume wangu aliwasili nyumbani na kunikuta nikiwa nimevimba nusu ya kupasuka. Hata sikuwa na haja ya kumpokea nilijiinamia na kuanza kulia, mume wangu hata bila kutua vitu vyake alinisogelea na kuanza kunishika begani.
Niliteremsha bega chini na kuuondoa mkono wake,lakini hakuchoka:
"Mke wangu ni nini kilichokusibu siku hizi au ndio hivyo vikao vyako vya pembeni angalia vitavunja nyumba yetu kisha watucheke."
"Niambiwe na nani zaidi ya kukuona kwa macho yangu."
"Mke wangu umeniona nafanya nini?"
"Ulipotoka kazini umekwenda wapi?"
SASA ENDELEA…

"Si nimerudi nyumbani," maneno yale yalifanya niamini mume wangu ni muongo kwa kuniongopea kila siku.
"Yaani mume wangu umeisha niona mimi ni mtoto mdogo?"
"Kwa vipi?"
"Kwa nini umenidanganya?"
"Kukudanganya kwa vipi mke wangu?"
"Siku zote kumbe huwa uchelewi kwa kazi bali kwenye upuuzi wako."
"Mke wangu ni upuuzi gani huo?"
"Yule secretary wako uko naye vipi?"
"Ni mfanya kazi kama wafanyakazi wengine."
"Na kila siku unampeleka wapi?"
Kauli yangu ilimfanya mume wangu acheke kidogo kisha alisema kwa sauti ya upole:
"Mke wangu suala la kazi halipo unavyofikilia hasa tukizingatia mimi ni mkubwa lazima niwe karibu na watu wote."
"Basi ili tuelewana naomba umfute kazi yule secretary wako."
"Mmh itakuwa ngumu kwa sababu hana kosa lolote."
"Basi ni mwanamke wako."
"Sivyo ufikiliavyo."
"Basi nitamkomesha hawezi kuniharibia nyumba yangu hivi hivi ninamwachia."
"Utakuwa unamuonea sivyo unavyo mfikilia."
Siku ya pili nilikwenda ofisini kwa mume wangu nikiwa na nia moja ya kumfunza adabu secretary wa mume wangu. Niliwasiri ofisini na kwenda moja kwa moja kwenye ofisi ya mume wangu na bahati nzuri nilikuta yule secretary, aliponiona tu alinikaribisha kwa tabasamu pana.
"Karibu dada," Sikumjibu nilimkata jicho lililomfanya aangalie chini, nilijua ni aibu ameisha jua kuwa nimemgungua.
"Karibu dada pita mzee yumo ndani," alijibu huku akinyanyuka kitini na kubeba mafaili ili aingie nayo kwa bosi. Nilimwacha apite na kumshika nywele zake ndefu na kumvuta kwa nyuma, bila kuchelewa nilianza kumshushia kipigo kitakatifu huku nikimkanya.
"Ukome kufuata wanaume wa watu."
Wakati huo watumishi wengine walikuwa wameishafika akiwemo mume wangu ambaye alionyesha kushtuka na kitendo changu. Wapo walioamini kuwa yule secretary ni mpenzi wa mume wangu na wapo waliosema namuonea.
Baada ya kuniamua mume wangu alinichukua na kunirudisha nyumbani, baada ya kurudishwa nyumbani nilimwambia mume wangu kuwa huo ni mwanzo.
"Mke wangu ni kitendo gani kile cha aibu ilichokifanya ofisi ambacho kinaweza kunifukuzisha kazi."
"Bora ufukuzwe kuliko kukosa uaminifu."
Kauli ile ilimfanya mume wangu amwite dada ya shemeji na kuwaeleza tabia zangu alizozisema ni chafu zisizoweza kuvumilika. Kwa tabia zile mume wangu aliamua kunirudisha nyumbani ili nikajifunze upya tabia.
Kitendo cha kurudishwa nyumbani kilinifanya nijione kama nimepasuliwa moyo wangu kwa kisu butu bila ganzi. Sikuona kosa langu kwani niliamini nilikuwa naitetea ndoa yangu, Pamoja na kumuomba msamaha mume wangu kuwa sitarudia tena kufanya niliyoyafanya. Mume wangu alisema:
"Nimekusamehe ila lazima urudi kwenu upigwe msasa upya mke wangu bado nakupenda lakini kwa mtindo huu hatufiki mbali pia ni hatari kwa upande wangu wa kazi yangu. Dunia ya leo bila kazi tutaishi vipi?"
"Ni kweli shemeji, Cathy nenda kwanza nyumbani," dada aliongezea.
Sikuwa na jisi niliondoka kurudi nyumbani nikiwa nalia njia nzima mpaka nafika nyumbani na kupokelewa na wazazi. Nilipofika nyumbani niliwaeleza wazazi wangu yote yaliyotokea hapo ndipo wazazi wangu walipo niweka chini na kunieleza.
"Cathy nyumba hailindwi hivyo, kwa kitendo chako umemkosea heshima mume wako na kumkosea hata yupo msaidizi wake. Siku zote mume hachungwi kwa kumfuatilia bali tabia nzuri maneno matamu na kuonyesha upendo wako kwa uwazi."
"Vyote hivyo nimevifanya."
"Umekosa subira."
"Kwa hilo naweza kusema kweli nimekosa subira kwa sababu mume wangu nampenda sana."
"Hicho ni kichaa cha mapenzi ambacho ni karaha kwa mwenzio, usifikiri mumeo anafurahia upuuzi wako hata yeye anakosa raha huwezi kujiuliza pamoja na kufanya upuuzi wako mumeo hajakufokea wala kukupiga huoni ni kiasi gani anavyo kupenda."
"Ni kweli wazazi wangu kwa hilo nimemkosea mume wangu."
"Kwanza kuolewa lazima ujione mwenye bahati ni wangapi amewaacha mpaka kukuchagua wewe, kama uhuni angeufanya kabla ya kukuoa lakini mpaka kuamua kukuoa ameridhika na tabia zako vilevile hapendi tabia za kihuni."
"Nakubali yote nimemkosea mume wangu."
"Lazima ukubali na analokueleza, mara ngapi umekwenda ofisi bila taarifa na kumkuta akifanya kazi bila hilo unalo lifikilia. Kwanza ulikuwa ukifanya makosa kumfuata mumeo kazini sio sheria zetu ni nani aliyekufundisha kuondoka nyumbani bila ruhusa ya mumeo? Mama yako pamoja na uzee wake hawezi kwenda sehemu bila ruhusa yangu."
"Ni kweli baba kwa hilo nakubali nimemkosea mume wangu."
"Sio kumkosea bali kumvunjia adabu kwa kujiamulia kufanya mambo kama umejioa huoni umetutukanisha wote tuliokulea?"
"Wazazi wangu naomba mnisamehe."
"Wa kwanza kumuomba msamaha ni mumeo na wa pili msaidizi wake kisha jamii iliyokuzunguka."
"Mwanangu huo ni wasiwasi wa mapenzi na ulimbukeni wa kupenda siku zote ukiolewa huona wanawake wote ni wizi wa mumeo na kuona kila anapochelewa mumeo lazima atakuwa na wanawake," mama aliongezea.
"Mama moyo hushindwa kijizuia."
"Basi ingekuwa hivyo ndoa wengi zingetushinda, yangekukuta yaliyomkuta dada yako si ungeua mtu kabisa."
Maneno ya wazazi wangu yalinifanya nijutie maamuzi yangu, muda wote niliokuwa nyumbani nilijikuta kama mchawi niliyekamatwa mchana kweupe. Nilijiuliza kweli mume wangu atanirudisha japo wazazi wangu walinipa moyo wa kurudi.
Swali lingine lililoniumiza akili ni kuhusu mume wangu kweli atanipenda kama mwanzo. Kilichoniumiza moyo wangu na kuitamani ahera ni pale nilipoelezwa kuwa mume wangu amesimamishwa kazi kutokana na kitendo nilichokifanya. Muda ule alikuwa yupo chini ya uchunguzi na akikutwa na kosa anafukuzwa kazi.
Habari zile zilinikata maini na kujikuta kila siku nikilia na kujilaumu kwa yote niliyoyafanya yaliyopelekea kusimamishwa kazi mume wangu. Hali yangu ilikuwa mbaya hata kula y angu ilikuwa ya matatizo, nilikonda kila siku ya Mungu.
Nilimuomba Mungu usiku na mchana mume wangu arudishwe kazini, nilikuta nikipata vidonda vya tumbo kwa kutokula na mawazo. Roho iliniuma kukaa mbali na mume wangu nilikuwa tayari kuwa naye kipindi hiki cha matatizo, kwani ndio muda mzuri wa kuwa pamoja kupeana moyo.
Nina imani dua zangu Mungu alizipokea, mume wangu alirudishwa kazini na kuanza kazi mara moja. Wakati huo nilikuwa namaliza mwezi wa nne nyumbani, sikuwa dada yako Cathy yule aliyemzoea hata wewe nina imani ulikuwa shahidi wangu nilikuwa Cathy ambaye ukimtupa hata jalalani mbwa hamli kwa jinsi nilivyo kuwa nimepoteza mwelekeo.
Ambao hawakujua yaliyonisibu walijua nina ng'weng'we, wapo waliosema nimeyakanyaga na kurudishwa kwetu. Siku moja nikiwa nyumbani nilipata wazo la kumuandikia barua mume wangu na kumuomba msamaha baada ya kuona kimya kimezidi. Nilikwenda dukani na kununua kalatasi zangu mbili na kalamu zangu na kujifungia chumbani na kuanza kuandika barua kwa mume wangu:
Kwako mume wangu kwanza kabla ya yote napenda kutanguliza samahani yenye kila kitu cha kujutia na majuto yaliyo mazito ndani ya moyo wangu. Ni kweli mume wangu nimekukosea nimekukwaza kwa kipindi kirefu.
Ni ukweli uliowazi mapenzi yako kwangu ndiyo yaliyopelekea kunivumilia na kuwa tayari kunisamehe, najua uamuzi wako wa kunirudisha nyumbani si mapenzi yako bali maji yalikufika shingoni.
Mpaka muda huu sijui ni nini kilichonisibu na kufanya yote niliyofanya mpaka kufikia kukughalimu kimaisha. Huwezi kuamini nilifanya vile ili kulilinda penzi langu, kumbe nilikuwa nahalibu.
Mume wangu mimi ni mchanga katika mapenzi vilevile ndoa, hakuna kitu nilichokuwa nakiogopa kama mashetani wa kike wanaovunja ndoa za watu. Na dalili za mwanaume kutoka nje ya ndoa ndio iliyonifanya niamini nawe tayari umeisha tekwa na mashetani wa kike ambao ni sumu kali katika ndoa za watu.
Kilichonisumbua ni ahadi niliyoiweka moyoni mwangu kuwa nitalilinda penzi langu na kuwa mtumwa wa mapenzi ya mume wangu. Amini mume wangu nakupenda mpaka mwenyewe najichukia.
Siku zote humuomba Mungu kama kumchukua mmoja wetu basi nianze kufa mimi kwa kuwa kufa kwako nina imani litakuwa pigo kubwa maishani. Nitakuwa sawa kuondokewa na moyo sidhani kama nitaweza kuishi.
Mume wangu hiki ni kichaa cha mapenzi nimepanda mpaka nikapoteza akili ya ziada ambayo inaweza kunishawishi pale ninapotaka kufanya jambo mbaya. Kilichoniponza ni kupokea vibaya matatizo ndani ya ndoa na kuwa tayari kukabiliana kumbe sivyo.
Mume wangu hali yangu ni mbaya usishangae kusikia leo hii nimekufa kwa ajili ya kukupoteza wewe ambaye nilitegemea kifo ndicho pekee kitakacho tutenganisha. Kama mafunzo nimeyapata mume wangu nakuahidi nitakuwa mke mwema tena mwenye kukutii na kukueelewa na kuwa tayari kuyafuata yote uyatakayo.
Mume wangu amini nakupenda sina mwingine aliye na thamani chini ya jua zaidi yako hata wazazi wangu siwapendi kama ninavyo kupenda. Nisamehe mume wangu nipo chini ya miguu yako na kuyajutia yote niliyo yafanya.
Nirudishe mume wangu rudisha tumaini langu lililopotea, amini bila wewe sina maisha. Kumbuka uhai wangu ni wewe ndiye uliyeubeba nakupenda mume wangu. Nimejifunza na kuyachukua yote yawezayo kustawisha ndoa yetu.
Ni mimi mkeo Catheline Mwaipyana.

Baada ya kuiandika ile barua nilikuagiza mdogo wangu uende hadi kwa dada kisha akuelekeze kwa mume wangu ili umpe ile barua. Pamoja ya kutengana na mume wangu, hakuacha kuniletea pesa za matumizi baada ya kurudishwa kazini.
Siku ya pili nilikutuma mdogo kwenda Dar kwa dada na kukuomba ukishampa usisubiri majibu bali urudi tu. Baada ya kuondoka sikuacha kumuomba Mungu mume wangu arudiwe na moyo wa imani ili anirudie kwa sababu hali yangu ilikuwa mbaya sana.
Itaendelea
 
SEHEMU: 23

ILIPOISHIA:
Baada ya kuiandika ile barua nilikuagiza mdogo wangu uende hadi kwa dada kisha akuelekeze kwa mume wangu ili umpe ile barua. Pamoja ya kutengana na mume wangu, hakuacha kuniletea pesa za matumizi baada ya kurudishwa kazini.
Siku ya pili nilikutuma mdogo kwenda Dar kwa dada na kukuomba ukishampa usisubiri majibu bali urudi tu. Baada ya kuondoka sikuacha kumuomba Mungu mume wangu arudiwe na moyo wa imani ili anirudie kwa sababu hali yangu ilikuwa mbaya sana.
SASA ENDELEA…

Nilikuwa na tofauti kubwa na wanawake wa kabila yetu, siku zote wanawake wa mkoa wa Mbeya huwa hatuwabembelezi wanaume. Akiachika anarudi nyumbani na kuanza shughuli zake mwenyewe kama alivyofanya ma mdogo, tofauti na mimi kurudishwa nyumbani niliugua kidogo ya kufa.
Wenzangu wote niliokuwa nao wengi walikuwa hawajaolewa na walio olewa na kuachika hawakupoteza muda wao kumbembeleza mwanaume au kuumia mioyo yao zaidi ya kuona sawa maisha popote. Nilikuwa na tofauti kubwa na hao, mimi nilimpenda mume wangu na nilipenda maisha yangu yote niishi kwenye ndoa ndio maana nimekuwa mkali sana kwenye ndoa yangu kama nyuki kwenye asali yake.
Siku zote wenzangu walinicheka eti naliaibisha kabila yangu ambalo siku zote mwanamke amekuwa mtu wa kujiamini na asiyekubali kuendeshwa na mwanaume kwa kujua hata wao wana uwezo wa kutafuta pengine kuwazidi hao wanaume.
Sikuwa tayari kusikiliza maneno yao hakuna maisha mazuri duniani kama ya ndoa Mungu si mjinga kuwaumba Adamu na Hawa. Alikuwa na maana yake, kwa kujua umuhimu ya watu wawili wa jinsia tofauti. Kama kujifunza kwa kweli nilikuwa nimejifunza mengi nina imani ile kauli ya mume wangu nirudi nyumbani nikajifunze tena nimeifanyia kazi.
Siku ya pili nilisubiri kwa shauku kuu kupata majibu yako mdogo wangu toka kwa mume wangu. Lakini ajabu hadi usiku unaingia sikupata jibu lolote toka kwa mume wangu. Nilijikuta naingia kwenye ugonjwa mwingine wa kuwaza nisiyo yajua.
Siku ya tatu nayo ilikuwa inakatika, huwezi kuamini toka niwe nasubiri majibu lala yangu ilikuwa ya mang'amung'amu na kila siku nilishinda kwenye msingi wa nyumba kuangalia wanaotoka barabara kuu huenda nitakuona mdogo wangu.
Jamani kupenda kubaya ni ugonjwa usio na tiba mbadala zaidi ya ile iliyokusudiwa, mpaka kigiza kinaingia na kufanya macho yasione anayekuja mbele ndipo nilipohama kwenye usingi wa nyumba na kurudi ndani.
Moyoni wivu ulinitawala huenda ndio mume wangu amenipiga chini kwa ajili ya hawala yake yule Secretaly. Nilijikuta nakosa raha hata chakula cha usiku kilinishinda, niliamua kulala hivyohivyo bila kula wala kuoga. Sikuwa na haja ya kubadili nguo na kuvaa za kulalia, nililala na nilizoshinda nazo siku nzima.
Nikiwa nimelala nilishtushwa kama mlango unagongwa, lakini sikuamka niliendelea kusubiri nijue nani anagonga au nipo ndotoni. Baada ya kutulia kwa muda nilisikia mlango ukigongwa na sauti ikiita kama yako mdogo wangu niliye kutuma kwa mume wangu.
Nilikurupuka kitandani na kufungua mlango, nilishangaa kukuta ukiwa umesimama mlangoni.
"Dada mbona umelala mapema," uliniuliza.
"Nikae muda wote nina raha gani, mbona umechelewa?"
"Nilikuwa nasubiri jibu."
"Sundiiii nilikwambia ukimpa urudi."
"Dada kwa hali yako nisingeweza kurudi mtupu bila jibu la uhakika na kumweleza mhusika mateso huyapatayo juu yake."
"Aaaah Sundi kwa nini umefanya hivyo?"
"Dada kuumia kwako si kwako tu hata kwetu sisi vilevile tunaumia,vile vile hata baba na mama wapo kwenye wakati mgumu kutokana na hali yako."
"Ni kweli lakini haikuwa na haja ya kumlazimisha."
"Umuhimu wa kumweleza ukweli ulikuwepo na si kumlazimisha," baada ya kusikia yale nilishusha pumzi na kujikuta nikikulaumu mdogo wangu kwenye mawazo na kujua anaweza kuharibu kila kitu.
"Mmhu, amesemaje?"
"Amenipa jibu."
"Jibu! jibu gani hilo tena mdogo wangu hapa nilipo matumbo yote yananicheza."
"Kwanza pole najua unaumia japo na mimi nipo kwenye safari ya kuja huku uliongea yale kama ulijua kuna siku tutayaongea haya, baada ya kumpa ile barua na kumuomba aisome na anipe jibu. Aliisoma kwa kweli dada shemeji anakupenda sana ile barua ilimuumiza sana na mimi niliongeza msumali wa moyo wa kumuomba aokoe maisha yako ambayo nilikuwa na uhakika yapo mikononi mwake."
Kauli ile mdogo wangu ilinishtua na kukuangalia mara mbili mbili msichana mdogo kama wewe amepata wapi maneno mazito kama yale, nilitaka kujua baada ya maneno mazito kama yale mume wangu alijibu nini.
"Ehe yeye akasemaje?"
"Alisema ujumbe umefika na yeye alipanga kuja siku ile ambayo ilikuwa ya pili na wewe utangulie kunijulisha yupo njiani, moyo wangu haukuamini maneno yake na kumwambia: Shemeji yako kuwa yeye ni muhimu kuliko wewe ni muda mrefu mimi nilikuwa nateseka kukuona wewe ni kuongeza mateso ya moyo wangu kwa kubakia na swali yatakayo uumiza moyo wangu kama siku ya pili atakuja nyumbani si vibaya mkaongozana na wewe nimechoka kuona mtu akiteseka kila kukicha.
Hapo ndipo ulipokubaliana na shemeji yako muongozane pamoja kuja huku na ndiyo asubuhi mlipoamka mlipanda gari ambalo kwa bahati mbaya liliharibika njiani na kuwafanya muingie usiku.
Maneno yako mdogo wangu yalikuwa kama wimbo mmoja mzuri uliopenya kwenye ngoma za sikio zangu na kufanya mwili usisimke, lakini nilijiona kama bado nipo ndotoni na kujiuliza mara mbilimbili ni kweli usemayo mdogo wangu au kunipa moyo.
"Sundi usemayo ni kweli au?"
"Ni kweli dada," ulijibu.
"Shemeji yako yupo wapi?"
"Yupo nje anazungumza na wazazi."
Sikusubiri maneno mengine nilikurupuka na kutoka nje na kumkuta mume wangu yupo anaongea na mama, bila kumsalimia nilijikuta nimemparamia na kutufanya tuanguke wote. Mume wangu hakuamini hali yangu.
"Catheline mke wangu ulikuwa unaumwa nini?"
"Maradhi ya kukukosa wewe mume wangu."
"Pole sana mke wangu nina imani umepata mafunzo mazuri yatakayoimalisha ndoa yetu."
"Mume wangu nimekoma sirudii tena ni mapenzi mazito yamenifanya nione kila mwanamke aliye mbele yako ni mwizi wangu."
"Hilo nalijua na mapenzi yangu kwako hayatapungua ila lazima ujifunze maisha ya ndoa ili tuishi vizuri bila kuumizana mioyo yetu."
"Mume wangu nakuahidi kila alilolitaka nimelifanya, sasa hivi si Sofia yule mwenye akili za kitoto."
Siku ule kama unakumbuka shemeji yako alilala palepale kwetu na siku ya pili tulirudi wote Dar. Baada ya kurudi kwangu na kuyaanza maisha mapya yenye kila aina ya woga wa kumkorofisha mume wangu. Sikuwa mtu wa kuhoji hata mume wangu akirudi saa ngapi, lakini hata mume wangu alionyesha mapenzi mazito kwangu pamoja na kuijali familia yangu. Kwa muda mfupi nilinenepeana na kurudia kuwa Cathy tipwatipwa na kulazimishwa kufanya mazoezi ili kuepuka presha.
Mpaka sasa hivi mimi na shemejio tunaishi maisha ya kuelewana na kuaminiana. Ninapo kuwa mbali naye huna kwenye wakati mgumu hufikia kukoda na niumwapo hata niwe Mbeya lazima nirudi Dar kwa mume wangu.
Niwapo kwa mume wangu maumivu hupungua hasa anaponipa pole na kunikanda mwili hujiona kama nipo peponi. Siku zote humuomba Mungu kuwa kama kumchukua mmoja kati yetu basi mimi ningekuwa wa kwanza kufa. Huwa najiuliza kama mume wangu atakufa kabla yangu nitakuwa kwenye hali gani. mdogo wangu ndoa tamu hasa umpate akupendae kama mimi na Mume wangu.
Mwisho nakuomba mdogo wangu pindi utakapo olewa umpende mumeo kwa kuonyesha mapenzi ya kweli na kuwa muaminifu katika ndoa yako hii itasaidia kupunguza mayatima. Mdogo wangu kutoka nje ya ndoa ndio mwanzo wa kuutafuta UKIMWI ambao upo na unaua kwa wasio waaminifu wa ndoa zao.
Kutokana na busara zako mdogo wangu mume wangu alipanga baada ya kumaliza elimu yako lazima uje umalizie maisha yako kwetu na ndio mkakati tulioupanga baada ya kumaliza kidato cha nne uje huku. Lakini kwa vile umepata mipango yako ya maisha sina budi kukubaliana na matakwa yako.
Lakini sitamwambia shemeji yako sasa hivi lazima atapinga kwa kutaka usome zaidi."
Sundi alitulia kutafakari yote aliyoambiwa na dada yake na kuyakumbuka yote aliyoambiwa. Kwa mara ya kwanza aliona tofauti kubwa ya maisha ya ndoa ambayo aliyosimuliwa tokea mama yake mdogo mpaka dada yake.
Alishusha pumzi na kutulia kwa muda kuyatafakari yote aliyoelezwa na wote aliowasikiliza. Akili yake alijifunza vitu vingi na kujua kibaya kipi na kizuri kipi na kuamua kuchukua yote mazuri na kuyaacha mabaya.
Lakini alimuomba Mungu ampate mwanaume asiye utesa moyo wake kwa kuwa mapenzi au mahusiano ni bahati nasibu ule au uliwe. Baada ya kuwaza sana alishusha pumzi na kumshukuru dada yake kwa yote aliyomweleza na kumuahidi kuyatekeleza yote yatayodumisha ndoa yake.
Siku ya pili alikwenda kwa dada yao mkubwa ambaye ndiye aliyempokea dada yake Cathy na pale vilevile alitaka kujua siri ya ndoa ya dada yake kama alivyoelezwa na Cathy. Dada yake yake mkubwa alimwambia maelezo mafupi kuwa:
"Yangu si makubwa sana kama ya mama mdogo, yangu sanasana ni pale mume wangu alipopata mwanamke wa pembeni na kuanza kunidharau hata kufikia hatua ya kunipiga ikiwa pamoja na kuacha kunipa huduma za muhimu hata watoto walikosa ada za shule kufikia hatua ya kusimamishwa shule..
Shemeji yako alikuwa amepagawa na mwanamke wake wa nje na kumuona ndiye bora kuliko familia yake. Hukuwepo mdogo wangu nilipitia kipindi kigumu, kurudi nyumbani nataka ndoa nayo naitaka. Lakini sijui nani alimueleza mama ambaye alikuja na vyakula vingi na kuniweka kitako juu ya mitihani ya maisha na kuniomba nimuombee mume wangu kwa Mungu ili arudi kundini.
Nilifanya nilivyoelekezwa na mama pamoja na mama mmoja wa makamo niliyemweleza hata kabla mama hajaja. Mungu ana nguvu sikuamini mume wangu alirudi nyumbani kwake na kuniomba msamaha ndio mpaka leo tupo pamoja na kulifurahia penzi letu na watoto kama hawa tunao.
La muhimu kuliko yote si muhimu kujua shemeji yako alininyanyasa vipi zaidi ya kujua kuwa ndoa iko kama jumba kubwa ambalo lina muonekano wa picha mbili walio nje wana muono wao na walio ndani wana muono wao.
Sasa kila mwanadamu ameumbwa na hulka yake ya mume wangu haiwezi kuwa kama ya wa kwako. Vilevile sio kila mmoja huumia kwenye ndoa au kuona wanaume ndio wakorofi au kusema wanawake ndio wakorofi.
Kikubwa katika ndoa ni sawa na maji yenye kina kirefu yanahitaji ujasiri wa hali ya juu kuyaepuka bila hivyo unaweza kufa maji. Wapo waliojiua kwa ajili ya mapenzi tena wengine hata ladha yake hawaijui ni papara tu.
Mapenzi kama ya shuleni wanafunzi wengi wamejiua kwa ajili ya mapenzi, kwa vile ameyaingia kwa pupa akiachwa uona kama ameachwa na dunia nzima. Huwa hana tofauti na mtu aliyepata majibu ya damu na kuonekana damu yake chafu.
Kutokana na ufinyu wa mawazo huona huo ndio mwisho wa maisha yake au kuona ugonjwa ule ni aibu na kuamua kujiua na kusahau ugonjwa ule ni sawa na magonjwa mengine la muhimu kufuata ushauri na kuishi vizuri tena hakuna wa kukudhani mpaka uwaambie napo wataona uongo.
Ndio hata katika mapenzi wengi hukimbilia kujiua kama dada yako unafikiri kama kweli shemeji yako angemuacha angekuwa kwenye hali gani kama sio kumzika kabisa. Ni kweli inauma lakini uvumilivu ndio kinga pekee ya kukufanya uweze kuushinda moyo na kuyasahau yote japo itachukua muda kuyasahau.

Itaendelea...
 
Back
Top Bottom