blackstarline
JF-Expert Member
- Sep 19, 2016
- 3,517
- 8,872
- Thread starter
- #121
Pole sana mkuu, naweka muda siyo mrefu.Aisee alostoo imezidi mkuu fanya fikra
Pole sana mkuu, naweka muda siyo mrefu.Aisee alostoo imezidi mkuu fanya fikra
Mkuu ni kwamba nimeona tangu hayo mapendekezo yatokewe hakujakua na muendelezo nadhani kwa siku 2 sasa tangu uweke chapter iliyopita.Hahaah kwa nini mkuu?

Hata humu ipo tafuta uzi wa mshana jr unaitwa nani anamkumbuka umslopogaaz jamiiforum utaipata hiyo English version tena mpaka audio ipo ila sikumbuki wapi nilisikiaMkuu unayo hiyo version kwa PDF unitumie?
Andika Allan quartemain pdf utaipata hiyo English versionMkuu unayo hiyo version kwa PDF unitumie?
Pana kipande umekisahau hapo pale inkubu aliposema basi tujaribu kuwa shambulia ndipo yule mtu mkubwa alipo sema "umesema kama mwanamume inkubu ya nini kuogopa yule mtoto amesema watachinja ng'ombe na kufanya karamu? basi na iwe karamu yao ya mazikoni yule mbwa ninae tumaini kumuumbua kutakapo pambazuka alisema haogopi kuwa tutawashambulia sababu tu wachache walijua boma walilowewaliloweka kambi?Yule Mjivuni akautikisa mkuki wake mrefu, akacheka sana kwa muda mrefu, akajibu, ‘’Laiti tungeweza kushindana mimi na wewe peke yetu, ningekuonyesha kazi.’’ Aligeuka aende zake huku anacheka.
Umslopogaas akajibu, na ‘sauti yake ingali ikinguruma,’
‘’Usiwe na shaka, tutashindana peke yetu mimi na wewe.’’
‘’Utashindana uso kwa uso na Umslopogaas, wa damu ya Chaka, wa kabila la Wazulu, mkuu wa jeshi la Nkomabakosi, kama wengi wengine walivyofanya; nawe utajisalimisha mbele ya Inkosikazi kama walivyofanya wengi wengine. Ndiyo, cheka, cheka ila mwisho wako nakuhakikishia fisi watakuwa wanacheka na huku wanavunja mifupa na kuzitafuna mbavu zako.’’
Tuendelee....
SURA YA SITA
Alipokwisha kwenda Yule Mjivuni, mmoja wetu alilifungua lile kapu. Ua zuri sana lilionekana ndani yake, tena barua ndogo iliyoandikwa katika karatasi iliyofungiwa chakula alichokichukuwa, maneno ya barua hiyo ni haya:
‘’Wapenzi Baba na Mama, Wajivuni wametukamata tulipokuwa tukirudi pamoja na ua hili. Nilijaribu kukimbia nisiweze, Hawakunizuru wala yaya, lakini wamesema watanibadilisha kwa mmoja wapo wa rafiki za Bwana Quatermain, Mimi sikubali shauri hili.
Usimwache mtu yeyote atoe maisha yake kuniokoa mimi. Jaribu kuwashambulia usiku; wanafanya karamu ya ng’ombe watatu walioiba na kuchinja. Ninaogopa sana, lakini namtumaini Mungu. Siwezi kuandika zaidi, maana wanaanza kunitazama.
Kwa herini
Flossie.’’
Kwa nje ya karatasi iliandikwa, ‘’Nisalimie Bwana Quatermain. Wanachukua kapu, basi atalipata lile ua.’’
Nilipoyasoma maneno yaliyoandikwa na Yule mtoto mwanamke shujaa wakati wa hatari ambayo ilitosha kumtia wazimu mtu mzima mwenye nguvu, nakiri ya kuwa nililia machozi, tena, katika moyo wangu nilinuia hafi kabisa ya kuwa hafi ikiwa maisha yangu yanaweza kumuokoa.
Basi, hapa tulianza kuzungumza kwa bidii juu ya shauri la kufanya.
Nikasema tena ya kuwa nitakwenda, na tena Bwana Mackenzie alikataa, na Sir Henry na Bwana Good kama watu wema na waaminifu walivyo, walisema nikienda, basi na wao watakwenda pamoja nami na kufa pamoja nami.
Mwisho, nilisema, ‘’Ni lazima kabisa tufanye jambo kabla ya kufika mapambazuko.’’
Tulikaa pamoja na bwana Mackenzie na kupanga shauri, mwisho tulikubaliana kuwa tuwavamie kijeshi ifikapo muda wa mapambazuko kwa kujua muda huo ulikuwa ni mzuri kwani watakuwa wapo kwenye usingizi mzito.
Pamoja na kuwa hatukuwa na jeshi la kutosha kwani walinzi wengi wa pale mission walikuwa wamesafiri mbali lakini hatukukata tamaa.
Hao hao wachache waliokuwepo tuliona kuwa wanatosha kabisa kuwaunganisha pamoja na kwenda kupambana na wale Wajivuni.
Cha kwanza tuliunda kundi dogo la wapelelezi waende kule kwenye boma la ng’ombe walipoweka kambi yao kwa ajili ya kuwapeleleza na kutupatia ripoti ya nini kinaendelea kila waonapo inafaa kufanya hivyo.
Basi, tulipokwisha weka mambo yote tayari, ilikuwa karibu saa saba ya usiku, tukasubiri. Wapeleleze wetu walituambia kuwa Wajivuni wamekwisha kunywa damu ya ng’ombe na kula nyama nyingi sana, na sasa wamelala kuizunguka mioto yao, lakini watu wakulinda zamu wamewekwa kila mlango.
Flossie, Yule mtoto mdogo alikuwa amewekwa karibu ya ukuta katikati ya upande wa magharibi ya boma, na yaya wake yu karibu naye, na punda weupe amefungiwa kigingi.
Miguu ya mtoto imefungwa kwa kamba, na Wajivuni wamelala huko na huko kumzunguka.
Basi kwa kuwa hakuna jambo tena la kufanya, tulikula kidogo, tukalala kwa muda wa saa mbili.
Niliona ajabu jinsi mzee Umslopogaas alivyoweza kujitupa chini na kupata usingizi mara ile, ingawa mambo makubwa yanamngojea.
Sijui habari za wale wenzangu, lakini mimi sikuweza kulala usingizi. Kwa hakika niliogopa, na sasa kwa kuwa nilikaa kimya, nilianza kufikiri juu ya mambo tunayojaribu kuyafanya, nami sikuyapenda hata kidogo.
Tulikuwa watu thelathini jumla na hawakosi wengine hawakuzoea kupigana, nasi tunakwenda kuwashambulia watu wakali mia mbili na hamsini, watu hodari na stadi wa vita kuliko wenyeji wote wa Afrika, na zaidi ya hayo, walikuwa wamelindwa kwa boma la mawe.
Kweli ni jambo la hatari, na hasa kwa sababu hatuna budi kupafikia mahali petu bila kufanya kelele zozote, tena bila kuonekana na wale Wajivuni waliowekwa kulinda zamu.
Hakika, tukiwaamsha kwa jambo lolote kama vile bunduki ikifyatuka kwa habahati mbaya basi, tumekwisha potea wote, maana Wajivuni wote wataamka mara ile, na tumaini letu la kushinda ni kuwatokea ghafla.
Baada ya kupita muda, nilimsikia Bwana Mackenzie akinong’ona nje ya chumba changu, maana kila jambo lazima lifanywe kimya sana, akaniambia kuwa ni saa tisa, nasi hatuna budi kuanza kazi yetu saa tisa na nusu.
Basi, nilimwambia aingie chumbani, na wakati huo kila mtu alikuwa akivaa na kujitengeneza tayari.
Huku nyuma Umslopogaas alikuwa akiwakusanya watu kiwanjani chini ya ule mti mrefu, akawakagua kuona kama kila mtu ana silaha zake tayari.
Mwisho tulibadili shauri kidogo, tulitoa watu wawili katika wale waliokuwa na bunduki, tukawapa ngao na mikuki ya Kijivuni, tukawaambia wafuatane na Sir Henry na Umslopogaas na Yule Mkazi kuulinda mlango mkubwa wa boma lote tuliona kwa dhahiri ya kuwa watu watatu, hatakama ni hodari na wenye nguvu namna gani, hawatoshi kwa kazi ile.
Dah! Mkuu hichi kipande sina kama unacho kiunganishie tu hapo, utakuwa umetusaidia sana.Pana kipande umekisahau hapo pale inkubu aliposema basi tujaribu kuwa shambulia ndipo yule mtu mkubwa alipo sema "umesema kama mwanamume inkubu ya nini kuogopa yule mtoto amesema watachinja ng'ombe na kufanya karamu? basi na iwe karamu yao ya mazikoni yule mbwa ninae tumaini kumuumbua kutakapo pambazuka alisema haogopi kuwa tutawashambulia sababu tu wachache walijua boma walilowewaliloweka kambi?
Dah, shukran sana mkuu kwa kutusaidia kwa kutuletea hizi story mubasharaMAAJABU YALIYOWAPATA ALLAN QUATERMAIN NA WENZAKE
HADITHI YA UMSLOPAGAAS
SURA YA KWANZA
SIKU saba zilikuwa, zimepita tangu mwana wangu mpenzi alipozikwa na jioni ilipofika, nilikuwa Nikitembea huko na huko chumbani mwangu nikifikiri, mara mlango unabishwa, Nikaenda nikaufungua mlango mwenyewe, Kumbe rafiki zangu wa zamani Sir Henry Curts na Bwana John Good wapo nje.
Niliwakaribisha ndani wakaingiaa chumbani. Wakakaa mbele ya moto uliokuwa ukiwaka humo.
‘’Mmefanya vyema kuja kunitazama.’’
Hawakujibu neno, ila Sir Henry alishindilia tumbako katika kiko chake akakiwasha kwa kaa alilolitoa motoni, Alipokuwa akiinama mbele kufanya hivyo moto, uliwaka zaidi ukaangaza chumbani, nikafikiri jinsi alivyo mtu mzuri mno.
Uso wake mtulivu wenye nguvu, sura yake thabiti, macho yake makubwa ya kijivu ndevu na nywele zake rangi ya manjano.
Sura yake yote ilikuwa ya mtu aliye bora, tena umbo lake halikuwa kinyume cha uso wake, Sijapata kuona mabega mapana, zaidi wala kifua kinene kama chake.
Umbo la Sir Henry ni pana, ingawa ni mrefu wa futi sita na inchi mbili lakini haonekani kuwa mrefu nilipokuwa nikimtazama hivi, sikuweza kujizuia nisifiri namna mimi nilivyo mwembamba mfupi na namna nilivyohitilafiana na uso wake mzuri, na umbo lake bora.
Embu wazeni basi juu ya mtu mfupi aliyesinyaa, mwenye uso wa rangi ya manjano na umri wa miaka sitini na mitatu mwenye mikono membamba, macho makubwa ya kahawia, kichwa kimefunikwa na nywele zinazoingia mvi na kusimama wima kama brashi iliyotumika, kiasi uzani wake pamoja na mavazi aliyovaa ratili mia moja thelathini na mbili tu.
Basi hapo ndipo mtakapofahamu namna alivyo Allan Quatermain, ambaye kwa desturi huitwa Mwindaji Quatermain, na Waafrika humwita ‘’Makumazahn,’’ maana yake akeshaye usiku, yaani mtu mwerevu asiyedanganyika.
Tena, yupo Bwana Good ambaye hafanani na Sir Henry wala na mimi maana ni mfupi, mweusi kidogo, mnene mnene sana ana macho meusi yang’aayo na katika jicho moja siku zote huvaa rodi, yaani miwani ya jicho moja.
Nilisema yeye ni mnene, lakini neno hilo halitoshi kueleza namna alivyo mnene. Sir Henry humwambia ya kuwa amenenepa hivi kwa sababu yu mvivu, tena anakula sana, ingawa Bwana Good hapendezwi kwa maneno yake , lakini hawezi kuyakana.
Tulikaa kwa muda mfupi, kisha niilichuka kiberiti ili niiwashe taa, kwa sababu niiona giza linachosha, maana ndivyo inavyoelekea hasa ikiwa muda wa siku saba tu umepita tangu mtu alipozika tumaini la maisha yake.
Huku nyuma Sir Henry na Bwana Good walikuwa wamekaa kimya, wakiona nadhani, ya kuwa hawana la kusema linaloweza kunifariji, wakaridhika kunifariji kwa kuwapo kwao ni rambirambi zao za kimya.
Ni kweli ya kuwa twapata tumaini na faraja katika saa za majonzi kwa kuwapo wengine, wala si kwa maongezi yao ambayo huelekea kutuudhi tu. Wakakaa wakivuta tumbako, na mimi nilisimama mbele ya moto nikivuta tumbako pia na kuwaangalia.
Halafu kidogo nilisema, ‘’Je rafiki zangu wa zamani, tangu tuliporudi toka nchi ya Ukukuana hata leo, miaka mingapi imepita? ‘’Bwana Good akasema, ‘’Miaka mitatu. Kwa nini unauliza?’’.
Nikajibu, ‘’Nauliza kwa sababu nafikiri ya kuwa muda niiokaa pamoja na watu mijini umenitosha kabisa, Nitarudi mwituni tena.’’
Hapa Sir Henry alikipeleka nyuma kichwa chake, akacheka mcheko wake wa kindani, akasema, ‘’Ama ni ajabu sana, sivyo Good?’’
Bwana Good akaniangalia, na huku anacheka katika rodi yake, kama kwamba anaficha siri, akasema, ‘’Ndiyo, ajabu sana ajabu kweli kweli.’’
Mimi ni mtu asiyependa mafumbo na mambo ya sirisiri, basi niliwatazama mmoja mmoja, kishanikasema, ‘’Siwezi kufahamu vizuri,’’
Sir Henry akasema, ‘’Hufahamu? Basi, nitaeleza. Good na Mimi tulipokuwa tukija hapa tuliongea.’’
Nikayakatiza maneno yake kwa ukali kidogo, nikasema, ‘’Nadhali kama Good alikuwapo, hamkosi mliongea maana Good ni mtu apendaye sana maongezi. Je, mliongea habari gani?’’
Sir Henry, akauliza, ‘’Ee wafikiri tuliongea habari gani?’’
Nikatikisa kichwa changu.
Haiwezekani nikajua Good aliongea nini, maana mara nyingi huongea habari za mambo mengi.
Sir Henry akasema, ‘’Tuliongea juu ya shauri dogo nililoliwaza yaani kama wewe utakubali tutafunga mizigo yetu na kuiendea nchi ya Afrika kufanya safari nyingine,’’
Nilipoyasikia maneno yake, nilishtuka sana, nikasema, ‘’Ni kweli usemayo?’’ akajibu, ‘’Ni kweli, na Good naye amekubali pia, sivyo Good?’’
Na yeye akaitikia, ‘’Ndiyo.’’
Basi, Sir Henry akaendelea, na sauti yake ilionyesha namna anavyoona hamu, akasema, ‘’Nami pia nimechoka kukaa bure kiubwana katika nchi iliyokinai mabwana.
Kwa muda wa mwaka mzima na zaidi nimekuwa nikitukutika kama tembo mzee anusaye batari.
Kila mara ninaota ndoto za nchi ya Ukukuana, na bibi kichawi Gagula, na Mashimo ya Mfalme Sulemani. Nakuambia ya kuwa nimenaswa na hamu nisiyoweza kuieleza.
Mkuu unaweza kunipa link ya Mashimo ya Mfalme SuleimanMkuu blackstarline naona hili shauri la kuiweka yote lime slow process, tafadhali usipate tabu, twende tu kwa mfumo ule ule tulioenda nao tukamaliza Mashimo ya mfalme Suleiman bila tatizo, sura moja kwa siku
Kunradhi kama nimemkwaza yeyote
Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani - JamiiForumsMkuu unaweza kunipa link ya Mashimo ya Mfalme Suleiman
nashukuru mkuu kwa ufafanuzi,nategemea upo sahihi,lakini nakuwekea hapa screenshot ya english version pamoja na plot summary kutoka wikipedia,kote wametumia masai sehemu ya wajivuni kwenye swahili version.In most cases hadithi za kubuni is from reality au maisha ya maeneo flani. James Hadley chase novel zake zote zilitokana na miji na maisha ya eneo flani. Mfano ni kweli kwamba Kenya kuna Mto Tana kama ilivyozungumziwa hapa. Pia wamasai niliowaona Kenya tamaduni zao ni sawa kabisa na walioko Tanzanian, kuna kipindi wamasai wa Tanzania wakiiba mifugo walikuwa wanaipeleka Kenya.
Dah mkuu thanks for sharing this English version, na labda yawezekana am wrong. Nimejifunza kitu kimoja hapo hao Masai outcast ambao babu yangu pia aliwahi nisimulia wanaitwa WAKWAVI ni kweli kabisa.nashukuru mkuu kwa ufafanuzi,nategemea upo sahihi,lakini nakuwekea hapa screenshot ya english version pamoja na plot summary kutoka wikipedia,kote wametumia masai sehemu ya wajivuni kwenye swahili version.
Salute mkuuYule Mjivuni akautikisa mkuki wake mrefu, akacheka sana kwa muda mrefu, akajibu, ‘’Laiti tungeweza kushindana mimi na wewe peke yetu, ningekuonyesha kazi.’’ Aligeuka aende zake huku anacheka.
Umslopogaas akajibu, na ‘sauti yake ingali ikinguruma,’
‘’Usiwe na shaka, tutashindana peke yetu mimi na wewe.’’
‘’Utashindana uso kwa uso na Umslopogaas, wa damu ya Chaka, wa kabila la Wazulu, mkuu wa jeshi la Nkomabakosi, kama wengi wengine walivyofanya; nawe utajisalimisha mbele ya Inkosikazi kama walivyofanya wengi wengine. Ndiyo, cheka, cheka ila mwisho wako nakuhakikishia fisi watakuwa wanacheka na huku wanavunja mifupa na kuzitafuna mbavu zako.’’
Tuendelee....
SURA YA SITA
Alipokwisha kwenda Yule Mjivuni, mmoja wetu alilifungua lile kapu. Ua zuri sana lilionekana ndani yake, tena barua ndogo iliyoandikwa katika karatasi iliyofungiwa chakula alichokichukuwa, maneno ya barua hiyo ni haya:
‘’Wapenzi Baba na Mama, Wajivuni wametukamata tulipokuwa tukirudi pamoja na ua hili. Nilijaribu kukimbia nisiweze, Hawakunizuru wala yaya, lakini wamesema watanibadilisha kwa mmoja wapo wa rafiki za Bwana Quatermain, Mimi sikubali shauri hili.
Usimwache mtu yeyote atoe maisha yake kuniokoa mimi. Jaribu kuwashambulia usiku; wanafanya karamu ya ng’ombe watatu walioiba na kuchinja. Ninaogopa sana, lakini namtumaini Mungu. Siwezi kuandika zaidi, maana wanaanza kunitazama.
Kwa herini
Flossie.’’
Kwa nje ya karatasi iliandikwa, ‘’Nisalimie Bwana Quatermain. Wanachukua kapu, basi atalipata lile ua.’’
Nilipoyasoma maneno yaliyoandikwa na Yule mtoto mwanamke shujaa wakati wa hatari ambayo ilitosha kumtia wazimu mtu mzima mwenye nguvu, nakiri ya kuwa nililia machozi, tena, katika moyo wangu nilinuia hafi kabisa ya kuwa hafi ikiwa maisha yangu yanaweza kumuokoa.
Basi, hapa tulianza kuzungumza kwa bidii juu ya shauri la kufanya.
Nikasema tena ya kuwa nitakwenda, na tena Bwana Mackenzie alikataa, na Sir Henry na Bwana Good kama watu wema na waaminifu walivyo, walisema nikienda, basi na wao watakwenda pamoja nami na kufa pamoja nami.
Mwisho, nilisema, ‘’Ni lazima kabisa tufanye jambo kabla ya kufika mapambazuko.’’
Tulikaa pamoja na bwana Mackenzie na kupanga shauri, mwisho tulikubaliana kuwa tuwavamie kijeshi ifikapo muda wa mapambazuko kwa kujua muda huo ulikuwa ni mzuri kwani watakuwa wapo kwenye usingizi mzito.
Pamoja na kuwa hatukuwa na jeshi la kutosha kwani walinzi wengi wa pale mission walikuwa wamesafiri mbali lakini hatukukata tamaa.
Hao hao wachache waliokuwepo tuliona kuwa wanatosha kabisa kuwaunganisha pamoja na kwenda kupambana na wale Wajivuni.
Cha kwanza tuliunda kundi dogo la wapelelezi waende kule kwenye boma la ng’ombe walipoweka kambi yao kwa ajili ya kuwapeleleza na kutupatia ripoti ya nini kinaendelea kila waonapo inafaa kufanya hivyo.
Basi, tulipokwisha weka mambo yote tayari, ilikuwa karibu saa saba ya usiku, tukasubiri. Wapeleleze wetu walituambia kuwa Wajivuni wamekwisha kunywa damu ya ng’ombe na kula nyama nyingi sana, na sasa wamelala kuizunguka mioto yao, lakini watu wakulinda zamu wamewekwa kila mlango.
Flossie, Yule mtoto mdogo alikuwa amewekwa karibu ya ukuta katikati ya upande wa magharibi ya boma, na yaya wake yu karibu naye, na punda weupe amefungiwa kigingi.
Miguu ya mtoto imefungwa kwa kamba, na Wajivuni wamelala huko na huko kumzunguka.
Basi kwa kuwa hakuna jambo tena la kufanya, tulikula kidogo, tukalala kwa muda wa saa mbili.
Niliona ajabu jinsi mzee Umslopogaas alivyoweza kujitupa chini na kupata usingizi mara ile, ingawa mambo makubwa yanamngojea.
Sijui habari za wale wenzangu, lakini mimi sikuweza kulala usingizi. Kwa hakika niliogopa, na sasa kwa kuwa nilikaa kimya, nilianza kufikiri juu ya mambo tunayojaribu kuyafanya, nami sikuyapenda hata kidogo.
Tulikuwa watu thelathini jumla na hawakosi wengine hawakuzoea kupigana, nasi tunakwenda kuwashambulia watu wakali mia mbili na hamsini, watu hodari na stadi wa vita kuliko wenyeji wote wa Afrika, na zaidi ya hayo, walikuwa wamelindwa kwa boma la mawe.
Kweli ni jambo la hatari, na hasa kwa sababu hatuna budi kupafikia mahali petu bila kufanya kelele zozote, tena bila kuonekana na wale Wajivuni waliowekwa kulinda zamu.
Hakika, tukiwaamsha kwa jambo lolote kama vile bunduki ikifyatuka kwa habahati mbaya basi, tumekwisha potea wote, maana Wajivuni wote wataamka mara ile, na tumaini letu la kushinda ni kuwatokea ghafla.
Baada ya kupita muda, nilimsikia Bwana Mackenzie akinong’ona nje ya chumba changu, maana kila jambo lazima lifanywe kimya sana, akaniambia kuwa ni saa tisa, nasi hatuna budi kuanza kazi yetu saa tisa na nusu.
Basi, nilimwambia aingie chumbani, na wakati huo kila mtu alikuwa akivaa na kujitengeneza tayari.
Huku nyuma Umslopogaas alikuwa akiwakusanya watu kiwanjani chini ya ule mti mrefu, akawakagua kuona kama kila mtu ana silaha zake tayari.
Mwisho tulibadili shauri kidogo, tulitoa watu wawili katika wale waliokuwa na bunduki, tukawapa ngao na mikuki ya Kijivuni, tukawaambia wafuatane na Sir Henry na Umslopogaas na Yule Mkazi kuulinda mlango mkubwa wa boma lote tuliona kwa dhahiri ya kuwa watu watatu, hatakama ni hodari na wenye nguvu namna gani, hawatoshi kwa kazi ile.
Kitabu kipo mbali nami ila hukumbuka sana hapo kwani yule mzee mzulu alipanga mashambulizi si mchezo. Siwezi kwenda neno kwa neno ila kifupi ilikuwa hivi. Basi tubahatishe kuwashambulia usiku alisema inkubu. "Ndio umesema kama mwanamume inkubu ya nini kuogopa bwana mkubwa (mackenzie anao watu 20 na kuna watu weupe hawa tunatosha yule mtoto alisema watakula na kufanya karamu kwa ng'ombe waliowaiba basi na iwe karamu yao ya mazikoni yule mbwa ninae tumaini kumuumbua kutakapo pambazuka alisema haogopi kuwa tutawashambulia sababu tu wachache walijua boma walilowekaDah! Mkuu hichi kipande sina kama unacho kiunganishie tu hapo, utakuwa umetusaidia sana.