Inaendelea
Samahani kwa kuchelewa Kuweka muendelezo ubize wa utafutaji unasababisha niwe free wikendi ila tajitahidi niwezavyo tumalize hii stori
Tuendelee.........
Ndani ya huo mwaka 2011 Kaka angu ( mtoto wa Bamkubwa) aliharibu huko bush alipokua anakaa alitorokea home kwetu Mzee wangu alimpokea vzr tu.Bro na Sister Walienda kusomea kwa ndugu zetu mmoja Dom mwingine Tanga,Me ndo nilibaki kijana mkubwa mpk alipokuja huyo broh wangu mwingine ( mtoto wa bamkubwa ) nilifurahi kubaki me ndo mkubwa ila pia nifurahi zaidi kwa ujio wa huyu bro maana damu zilkua zinapata kinoma tofauti na bro wangu wa damu kwanza nilifurahi alivyoondoka.
Huyu bro wangu ( mtoto wa bamkubwa) alikua anavuta ndumu,sigara na tungi anakunywa japo ilikua kisiri baadae akazoea mpk leo bado anatumia hivyo vitu.Nilijikuta me nae naanza kuvuta ndumu alizokuwa akinipa nimuashie.Tulikua tunalala nae chumba kimoja ko muda mwingi nilkua nae alafu hicho chumba kilikua kimejitenga na kilikua na mlango wa nje.
Mdogo mdogo nikawa mzoefu kwenye ndumu lakin ckuta wazazi wajue wadogo zangu walikua wanajua lakin walikua sio WANAA.Shule ikawa kwa machale ila nilijitahid nikafanya mtihani wa Taifa form 2 majibu yalikuja vizur tu maisha yakasonga.
Mwaka 2012 nikiwa form 3 ndo mambo yalikua yanazid kuharibika, hapo home kulikua kuna banda moja lilitumika kwa ajili ya parking ya gari.Kipindi hicho sio mzee wa yule mtoto wa mwenye alie kuwa na gari ko banda lilikua tu lipo free.Bro wangu aliamua kulifanya liwe Jim ( gym) siku moja alileta nondo ( ckujua hata alitoa wapi ) ko tukawa tunapigiapo tizi mida ya jioni.Kuna siku moja alikuja na muhuni mmoja wa kundi la JAMAICA MOCKERS pale gym.Huyo muhuni walikua wamehamia pale Mtaani kwetu japokua nyumba zetu zilkua mbali kidogo.Huyo muhuni alikua na tabia chafu balaa ( yaani kwa kifupi familia yake walinyanyua mikono juu.) kuiba na kujeruhi watu ndo ilkua raha yake.Nilkua nikipiga nae story anasimulia tu matukio yake ya kukata watu sime ( zuna ) na kupora.Nilikua na vutiwa na story zake sana ( Huyo muhuni now ni marehemu 2014 ndo alifariki ).
Nakumbuka tukio la kwanza kushirikiana nae huyo muhuni tulimwibia bishoo mmoja simu ( dingi ake alikua ni mfanyakazi wa TRA ).Huyo bishoo tulimchorea ramani me na huyo muhuni maana ilikua kila jioni anapita home kwetu kwenda kwa manzi ake.
Tulimchorea ramani vizuri tu me muhuni alinambia nimdanganye huyo bishoo aingie King ( yaani nimlete gym ) na kweli hatukuchukua siku nyingi nikawa nimemleta bishoo gym.ilikua saa 12 kuelekea saa Moja jioni.Muhuni alimwomba bishoo simu aione ilivyo, Alivyopewa tu Akasepa nayo mazima.Bishoo alisubir wap mtu atokei ( wakati huo niko nae ) alivyoona muhuni atokei akasepa huku akisema atamkomesha.Basi bna mida ya Saa Tano usiku muhuni alikuja yeye na Bro wangu wakaniamsha walinipa 10k kwa kazi niliyoifanya
Kesho yake tukiwa hatuna hili wala lile tunavuta zetu ndumu, mara Baba ake na huyo bishoo wako na wazee wakazi mbele yetu.Muhuni yeye aliwai kusepa tukawa tumebaki me na bro wakatushika ilikua ni purukushani siku bro anakataa yeye ajaiba me nilishikwa na Baba ake huyo bishoo nilkua sileti usumbufu wakati huo najitetea kuwa sikuiba mimi.Na kweli bishoo alinitetea kuwa me sikushiriki wakaniachia wakabaki na broh wanamlazimisha awapeleke kwao na huyo muhuni, cjui alifanyaje akawachoropoka maafande mbio alizotoka angefaa awakilishe taifa kwenye Olympic


.
Hili tukio Wazazi walivyopata taarifa walinipiga marufuku kutembea na huyo muhuni na hyo gym wakaipiga marufuku.Ila hata baada ya hilo tukio kuisha bado niliendelea kutembea na huyo muhuni sasa hapo ndo kuteka watu simu n.k ilikua imeshamiri.kipindi cha Umiseta tumewachuklia Wanafunzi simu sana tunauza bei ya hasara.Ilifikia mahala hata nilipokua mwenyewe mazingira yakiniruhusu kukuteka nakuteka vizuri na kusepa.Mzee wangu alinikanya mpaka kuna siku alitufukuza kwake mimi na huyo bro angu ila tena akaturudisha home ( alikua na huruma sometimes )
matukio ni mengi tuliyoyafanya kipindi hicho lakini hili sitokuja kulisahau ilikua kidogo tufe.
Siku hyo tumeenda Club Club House ( Metro ) kama kawaida yetu tulikua wanne ikiwe bro wqngu na huyo muhuni na jamaa mmoja hivi.Sasa midaa ya saa 9 usiku tuliamua kurudi magheton kulala, kilindi tunatoka huyo muhuni alimuona kuna mdada kasimama pekee ake karibu na wanapouza magazet.Muhuni alisema tu nisubirin nikaongee na yule demu ( alikua anamjua ) sisi tulimsubir pembeni tulikua na pikipiki ( XL ) bro aliazima alipokua anafanyia kibarua chake.zilipita kama dakika kadhaa muhuni bado anaongea na yule demu mara ghafla wakaanza kuzozana, Muhuni alimchukilia yule demu kimkoba chake......acha yule demu apige kelele za mwizi, muhuni akaanza kukimbia tulipo bahati nzuri aliwai kukalia pikipiki mapema, bro akaiwasha ili tukimbie kucheki nyumba mabodaboda walikuwa wanatufata wako kwenye boda zao.tulifukuzana nao walikua bampa to bampa nasisi.Hapo sasa mimi mpk tungi imeisha kichwani nawaza tu mazishi yangu na wakati huo namuomba Mungu kimoyomoyo atusaidie.
Tulikimbilia barabara ya kwenda Majita road ila hatufika kabisa Majita road kuna sehem panaitwa kwa ILIJi ndo dereva wetu alikatiapo kona ( kuna njia hapo inaenda mtaani kwetu ) Pikiki ilimshinda dereva ( kinjia kilikua ni chembamba sana pikipik kupita ) bahat nzuri tulianguka kwenye bustani ya mboga mboga.Wale boda walitukosa maana tuliwaacha hatua nyingi sana ndo ikawa pona yetu.pikipiki iliharibika hand cater moja.Ila me peke angu niliumia ( niliumia mguu wa kushoto sehemu ya ugoko ckumbuki hata ni nini kiliniumiza vibaya vile).Wazazi niliwadanganya tu nimeanguka kwenye Jiwe wakakubali na maisha ykazid kusonga.
Nitaendelea