Hadithi ya kweli ya maisha yangu

Hadithi ya kweli ya maisha yangu

Inaendelea.....

NILIVYOANZA KUIBA NA KUTEKA WATU VITU

Siyo kwamba ndo nilikua naanza wizi, hapana sema nilkua nimepumzika sasa ndo nikawanimerudi tena rasmi kwenye wizi.

Twende kazi sasa.....

Mwaka 2011 Yule jamaa mtoto wa mwenye nyumba alikua kashamaliza chuo nakurudi home.Alitaka tumuachie chumba kimoja aanzie maisha na kimoja kwa ajili ya wazazi wake wakiwa wanakuja wanafikiapo.Hilo jambo lilitufedhehesha sana hasa mimi lakin tayar jamaa alishaamua nyumba c yao bna tutafanyaje sisi wapangaji....basi jamaa alichagua chumba alichokua analala sister na young sister ndo watoke kusudi yeye ahamie.Sister alimpisha akahamia chumba walichokuwa wanafikia wageni wetu ( kumbuka hiyo nyumba ilikua na vyumba vitano ) ko sisi tukabaki na vyumba vitatu.

Hicho kitendo kilifanya ni mchukie huyo jamaa ila ckuonesha kama namchukia nilijisemea moyoni ni lazima nimkomoe,ckujua na mkomoa vipi ilanilisema cku akijiset tu ataumia.

Basi bna jamaa hata hakukaa sana home akawa amepata kazi idara ya Maji ( Mzee wake ndo alimfanyia connection akawai kupata kazi )

Kabla hatujampa funguo za chumba alichokua anataka nilichomoa funguo mbili, moja ya hicho chumba chake nyingine ya chumba cha wazazi wake.Nilifanya kisiri hakuna alie jua kama nimechomoa funguo.

Wakati huo ndo kwanza nipo form 2 ila jamaa yeye alikua anaongea nasisi vizuri alikua hana noma ila sema alikua ana majivuno sana hicho ndo nilikua simpendei.Siku moja kuna pick up ilikuja hapo homee ikiwa imebeba maboksi yalikua 30.Yale maboksi yalikua yamebeba vitabu vya secondary.Vitabu vilkua vya Chemistry, Physics na Mathematics form 1,2 na 3.

Usiku wa siku aliniita chumbani kwake akanipa vitabu vitatu cha Physic, Chemistry na Mathematics vya form two.Nilimshukuru nikaondoka ila hata nilkua sivisomi.Kuna siku niko darasani kuna jamaa mmoja ( john kisomo wa darasa ) alitaka nimuuzie kitabu cha physic nilimuuliza unashingap akasema buku tano nikasema poa, akanipa nikampa kitabu ila nilimwambia ninavyo vingi anitaftie wateja akasema frsh

Kuna siku sikwenda shule nilikua home tu huyo John kisomo alikuja home ule muda wa wanafunzi kutawanyika.Alikua anataka kitabu cha mathe nikampa kwa ileile bei niliyomuuzia mara kwanza akasepa.Siku hyo nikawaza nikasema kumbe humu ndani nakaaa na mali tu burebure.

Basi nilimtafuta rafiki angu mmoja tulikua tunasoma nae nikamweleza hyo inshu yeye akasema atakua anatafuta wateja kisha hela tunagawana.Na kweli alikua anapata wateja me nampa mali anauza.

Nilikua natumia zile funguo nilizochukua kisiri kuingia chumbani mwa huyo jamaa na kuchukua vitabu kisha tunaenda kuuza.Niliafanya kwa Umakini mkubwa na usiri ckutaka home wajue kitu nachokifanya, kuingia tu nilikua nahakikisha hakuna anaye niona.Nilikua naona ni fresh tu kwa niliyokua nafanya, na tulipiga sana hela me na huyo muhuni wangu tukawa madoni shuleni 🙃🙃 .
Jamaa wala hata alikua hashituki kama namcheza vitabu vyake na ckuwai kujua leengo lake la kuleta vile vitabu ni nini.Nilifurahi maana vilikuwa vinanipa hela za buree.

Siku moja huyo muhuni wangu alipata dili kubwa tu kuna maticha fulani wa shule za private walikua wanaitaji vitabu vya kutosha walitaka vitabu 20 Chemistry na Mathematics kwa Buku 4 kwa kila kitabu.Nilifurahi sana nikaona mambo cndo hayo muhuni wangu alinambia kuwa atavifata jioni home kwetu me nikampanga muda wa kuja nilimwambia ni saa moja ndo atokee tuchukue mzigo tukauhifadhi kwao then kesho yake tukafanye biashara na hao Maticha.

Niliingia chumba cha huyo jamaa kama kawa nikachkua mzigo nikatoka sikuonwa na yoyote nilivificha chini ya godoro langu madogo wasivione nikawa subir saa moja ifike muhuni aje tuvihamishe.Na kweli Muhuni alitimba na Rafiki ake hata nilikua cmjui ila hilo halikua likinihusu kwanza nifurahi maana kazi ilikua imerahisishwa, Tuliviweka kwenye limfuko la Rambo yale Makubwa safari ikaanza kuelekea Maeneo ya buhare ( ndo muhuni alikua anaishi ) tulipitia barabara ya kuelekea Makoko.Tulifika Eneo moja linaitwa Boda 2 Boda darajani ( Mwisenge ) kwa mbele kidogo barabara ilikua ni yavumbi kuna kamto kalikua kanapita chini ya daraja kana mwaga maji kuelea ziwani.

Ghafla tulikutana Kundi la Wahuni nahisi walikua wanatokea Makoko, walikua zaidi ya kumi.Walituteka bna wakaanza kutupiga sachi bahati nzuri ckua na chochote mfukoni mee nilikua mpole ila wale wahuni wangu wawili walikua wabishi kinoma waliparanganya nao ikawa ni vita ni vita Mura 🤣🤣.Hao wahuni walikua wanadai eti tulifanyia Fujo makaburini nilikataa kuwa sio sisi nilichezea bapa za Panga mgongoni walinambia nikae chini.katika zile harakati za kupigana wale wahuni wangu walipata upenyo wakakimbia vitabu vingi viliangukia darajani na baadh vilichanika ko biashara ikawa imeishia hapo.Baada ya wale wahuni wangu kukimbia na kuniachw pale mwenyewe hasira zao zikikahamia kwangu nilipigwa bapa.Huwez amini nilikua napiga kelele za msaada lakini raia walikua wanaogopa kuja kunisaidia.Waliamua tu kunisamehe wenyewe, walinambia nikimbie nilitoka baru sendo ckujua hata zilipoangukia 🤣🤣🤣🤣.Nilikimbia mpk nikawa nasema kumbe kuna kipaji ndani yangu cha riadha ila me ndo ckitumii.

Basi bna biashara ilikufa cku hyo ckujutia sana maana vitu vilikua vya wizi nikaacha maisha yasonge Ila nilistop kuingia kwenye hicho chumba kwa muda.

Nitaendelea tena....
 
Inaendelea


Samahani kwa kuchelewa Kuweka muendelezo ubize wa utafutaji unasababisha niwe free wikendi ila tajitahidi niwezavyo tumalize hii stori

Tuendelee.........

Ndani ya huo mwaka 2011 Kaka angu ( mtoto wa Bamkubwa) aliharibu huko bush alipokua anakaa alitorokea home kwetu Mzee wangu alimpokea vzr tu.Bro na Sister Walienda kusomea kwa ndugu zetu mmoja Dom mwingine Tanga,Me ndo nilibaki kijana mkubwa mpk alipokuja huyo broh wangu mwingine ( mtoto wa bamkubwa ) nilifurahi kubaki me ndo mkubwa ila pia nifurahi zaidi kwa ujio wa huyu bro maana damu zilkua zinapata kinoma tofauti na bro wangu wa damu kwanza nilifurahi alivyoondoka.

Huyu bro wangu ( mtoto wa bamkubwa) alikua anavuta ndumu,sigara na tungi anakunywa japo ilikua kisiri baadae akazoea mpk leo bado anatumia hivyo vitu.Nilijikuta me nae naanza kuvuta ndumu alizokuwa akinipa nimuashie.Tulikua tunalala nae chumba kimoja ko muda mwingi nilkua nae alafu hicho chumba kilikua kimejitenga na kilikua na mlango wa nje.

Mdogo mdogo nikawa mzoefu kwenye ndumu lakin ckuta wazazi wajue wadogo zangu walikua wanajua lakin walikua sio WANAA.Shule ikawa kwa machale ila nilijitahid nikafanya mtihani wa Taifa form 2 majibu yalikuja vizur tu maisha yakasonga.

Mwaka 2012 nikiwa form 3 ndo mambo yalikua yanazid kuharibika, hapo home kulikua kuna banda moja lilitumika kwa ajili ya parking ya gari.Kipindi hicho sio mzee wa yule mtoto wa mwenye alie kuwa na gari ko banda lilikua tu lipo free.Bro wangu aliamua kulifanya liwe Jim ( gym) siku moja alileta nondo ( ckujua hata alitoa wapi ) ko tukawa tunapigiapo tizi mida ya jioni.Kuna siku moja alikuja na muhuni mmoja wa kundi la JAMAICA MOCKERS pale gym.Huyo muhuni walikua wamehamia pale Mtaani kwetu japokua nyumba zetu zilkua mbali kidogo.Huyo muhuni alikua na tabia chafu balaa ( yaani kwa kifupi familia yake walinyanyua mikono juu.) kuiba na kujeruhi watu ndo ilkua raha yake.Nilkua nikipiga nae story anasimulia tu matukio yake ya kukata watu sime ( zuna ) na kupora.Nilikua na vutiwa na story zake sana ( Huyo muhuni now ni marehemu 2014 ndo alifariki ).

Nakumbuka tukio la kwanza kushirikiana nae huyo muhuni tulimwibia bishoo mmoja simu ( dingi ake alikua ni mfanyakazi wa TRA ).Huyo bishoo tulimchorea ramani me na huyo muhuni maana ilikua kila jioni anapita home kwetu kwenda kwa manzi ake.

Tulimchorea ramani vizuri tu me muhuni alinambia nimdanganye huyo bishoo aingie King ( yaani nimlete gym ) na kweli hatukuchukua siku nyingi nikawa nimemleta bishoo gym.ilikua saa 12 kuelekea saa Moja jioni.Muhuni alimwomba bishoo simu aione ilivyo, Alivyopewa tu Akasepa nayo mazima.Bishoo alisubir wap mtu atokei ( wakati huo niko nae ) alivyoona muhuni atokei akasepa huku akisema atamkomesha.Basi bna mida ya Saa Tano usiku muhuni alikuja yeye na Bro wangu wakaniamsha walinipa 10k kwa kazi niliyoifanya

Kesho yake tukiwa hatuna hili wala lile tunavuta zetu ndumu, mara Baba ake na huyo bishoo wako na wazee wakazi mbele yetu.Muhuni yeye aliwai kusepa tukawa tumebaki me na bro wakatushika ilikua ni purukushani siku bro anakataa yeye ajaiba me nilishikwa na Baba ake huyo bishoo nilkua sileti usumbufu wakati huo najitetea kuwa sikuiba mimi.Na kweli bishoo alinitetea kuwa me sikushiriki wakaniachia wakabaki na broh wanamlazimisha awapeleke kwao na huyo muhuni, cjui alifanyaje akawachoropoka maafande mbio alizotoka angefaa awakilishe taifa kwenye Olympic .

Hili tukio Wazazi walivyopata taarifa walinipiga marufuku kutembea na huyo muhuni na hyo gym wakaipiga marufuku.Ila hata baada ya hilo tukio kuisha bado niliendelea kutembea na huyo muhuni sasa hapo ndo kuteka watu simu n.k ilikua imeshamiri.kipindi cha Umiseta tumewachuklia Wanafunzi simu sana tunauza bei ya hasara.Ilifikia mahala hata nilipokua mwenyewe mazingira yakiniruhusu kukuteka nakuteka vizuri na kusepa.Mzee wangu alinikanya mpaka kuna siku alitufukuza kwake mimi na huyo bro angu ila tena akaturudisha home ( alikua na huruma sometimes )

matukio ni mengi tuliyoyafanya kipindi hicho lakini hili sitokuja kulisahau ilikua kidogo tufe.

Siku hyo tumeenda Club Club House ( Metro ) kama kawaida yetu tulikua wanne ikiwe bro wqngu na huyo muhuni na jamaa mmoja hivi.Sasa midaa ya saa 9 usiku tuliamua kurudi magheton kulala, kilindi tunatoka huyo muhuni alimuona kuna mdada kasimama pekee ake karibu na wanapouza magazet.Muhuni alisema tu nisubirin nikaongee na yule demu ( alikua anamjua ) sisi tulimsubir pembeni tulikua na pikipiki ( XL ) bro aliazima alipokua anafanyia kibarua chake.zilipita kama dakika kadhaa muhuni bado anaongea na yule demu mara ghafla wakaanza kuzozana, Muhuni alimchukilia yule demu kimkoba chake......acha yule demu apige kelele za mwizi, muhuni akaanza kukimbia tulipo bahati nzuri aliwai kukalia pikipiki mapema, bro akaiwasha ili tukimbie kucheki nyumba mabodaboda walikuwa wanatufata wako kwenye boda zao.tulifukuzana nao walikua bampa to bampa nasisi.Hapo sasa mimi mpk tungi imeisha kichwani nawaza tu mazishi yangu na wakati huo namuomba Mungu kimoyomoyo atusaidie.

Tulikimbilia barabara ya kwenda Majita road ila hatufika kabisa Majita road kuna sehem panaitwa kwa ILIJi ndo dereva wetu alikatiapo kona ( kuna njia hapo inaenda mtaani kwetu ) Pikiki ilimshinda dereva ( kinjia kilikua ni chembamba sana pikipik kupita ) bahat nzuri tulianguka kwenye bustani ya mboga mboga.Wale boda walitukosa maana tuliwaacha hatua nyingi sana ndo ikawa pona yetu.pikipiki iliharibika hand cater moja.Ila me peke angu niliumia ( niliumia mguu wa kushoto sehemu ya ugoko ckumbuki hata ni nini kiliniumiza vibaya vile).Wazazi niliwadanganya tu nimeanguka kwenye Jiwe wakakubali na maisha ykazid kusonga.

Nitaendelea
 
Back
Top Bottom