Hadithi ya kweli ya maisha yangu

Hadithi ya kweli ya maisha yangu

Awa jamaa kwenye matangazo yao wanavutia sana ukisoma unaweza kuta mshahara laki 5 na posho zipo ukiwa na bidii tunakupandsha cheo utaona bonge la kazi,
Sasa nenda utakuta kubebeshwa masufuria tena kichwan au kwenye li mfuko khaaaa
Na walivyokua wanatupatia maelekezo na kuisifia Company yao mara makao makuu ni USA mpk SA wapo ila nilivyosikia kulipwa nikutokana na ulivyouza nikajua hapa amna kitu
 
Big up mkuu,nilipitia uninja kama wako ila at some point nilikuja kubadilika mpaka leo..Nimecheka sana kila niliposoma matukio yako
 
Inaendelea


Basi bna Jumapili ilifika saa moja nikawa nipo Nyamiongo ( Tenki la Maji lilipokuwa lina Jengwa ) nikamkuta huyo boss wetu fundi kashafika mapema tu pamoja na yule rafiki angu aliyejipigia promo mwenyewe ( kwanza alishangaa kuniona pale hata ckumjali ).Boss alitupa maelekezo kuhusu malipo na aina ya kazi ( 10k kwa siku ila tunalipwa kwa wiki kila jumamosi ).Nilimwambia jumamosi sitokua nafanya kazi akanielewa ila akasema utakua unakuja kuchukua hela maana ndo siku mshahara unatoka nikasema poa.

Kazi tuliokuwa tunafanya sisi ilikua ni kusuka nondo juu ya Tenki ili Zege imwage juu yake.Siku ya kwanza kazi ilkua nyepesi sana kama mimi waliniona ni lazy wakanipa kufagia viuchafu vilivyokua juu ya Tenk.Vibarua wenzangu wakawa waona wivu eti hela tunalipwa sawa ila kazi ni tofauti kuna siku Boss aliwamaind sana akawaambia Wanawe wasubir hela yao wasirud tena ko wakawa wapole ila bado wakawa wananitenga ( hasa foremen wetu alikua anajikuta sana huyu jamaa eti nae ananipelekesha nikawa nampuuza tu maana komesha yake ilikua ni Boss )

Siku zilienda hatimae nikapewa kazi ya kunyoosha Nondo na kuzipandisha Juu ya Tenki, kazi ilkuwa ni ngumu kinoma yaani hadi nilkua nasema kesho sirudi ng' oo ..ila nikazoea kibishi.Hiyo kazi ilinifanya nikawa nakula chakula kingi balaa asubui napiga chai ya buku jero,mchana sahani mbili za Wali mpk tatu na usiku nyumbani nilkua nakula hadi wananishangaa maana me nilikua sio mpenzi wa kula sana.

Kunyoosha Nondo na kuzi Kunja kusikieni tu nilikua naenyeka juani wengine wapo juu ya Tenki ni order tu wanatoa kwangu " Nondo hamsini mara miambili " yaani mgongo ulikua sio wangu kwa sababu ya kuinama kunyoosha nondo na Bender.Chini kukiwa hakuna kazi napanda juu ya Tenki Kusuka na mimi Jamvi la nondo kwa vile vi Pisa kama mnavijua viko kama plyis.....Mshahara wangu wa kwanza nilitoa 25k tu zilizobaki nilimpa Mama atumie 25k hyo nilinunulia kasimu kangu ka kwanza kununua binafsi ka Aitel ka batani ila kalikua na Java ko vigemu nilikua nacheza sana.

Siku zilienda niko hapo kibaruani Tamaa zikanishika, kwanza huo mradi kuna Wazungu ndo walipewa Tenda na serikali alafu na wao wakawapa Tenda Wahindi ko makampuni yalikua mawili tofauti.Nilicheza kamchezo akilini mwangu ya jinsi gani nitaiba Nondo pale niuze.Nilianza kuwa nitawezaje maana ilikua ni ngumu kidogo.

Nilianza kuweka mazoea na Mlinzi wa mchana na kweli aliingia King tulizoena sana na kuna siku nilimshirikisha mpango wangu akakubali ( yeye nae alikua njaa tu ) ila akasema nikishikwa yeye hayumo nikamwambie fresh tu.Ila bado nilkua sijui ni jinsi gani nitaiba nondo maana zilikua zina hesabiwa asubui na jioni mbele ya walinzi.

Kuna siku Boss alinambia mimi na kibarua mwenzangu tupande lori twende Bukanga tukafate mzigo wa Nondo maana pale zilikua zimeeisha.Tulifika bukanga fresh tu boss akanambia niende kwa storekeeper ni mwambie tumefata nondo.Nilifika kwa storekeeper alikua ana malingo jamaa yule kama demu, alinambia tu nikazitoe nondo ( tulikua tunahitaji nondo 400 ) alafu tuje tuhesabu wote, na kweli nilizitoa zilipokua nyingi tu maana nilikua zisihebu kwa wakati huo nilimsubir storekeeper aje tuhesabu nae ila akanambia ni hesabu mwenyewe alafu ni mpeleke hesabu stoo ( nilifurahi sana kusikia hivo mpk nikawa natetemeka kwa furaha ) nilizihesabu pekee yangu yule kibarua mwenzangu yeye alikua mvivu anazurula cjui wapi...nilikuta nondo 441 ko nikapeleka hesabu ya 400 jamaa akaindika akanambia nisepe nikasepa kwenda kuzipakia kwenye Lori.Tulizipakia tukisaidia na huyo kibarua mwenzangu baada kumaliza Boss akaja tukasepa kuelekea site.kichwani nawaza nitawezaje kuzitorosha hizi nondo 41?.

Tulivyofika tu site niliongea na mlinzi kipindi tena na hesabu nae nikamwambia kuna Nondo ishirinina tano zimezidi yeye aliandika 400 ndo zimeletwa hata boss alikua anajua hivyo.

Basi Boss alinambia ninyooshe nondo hamsini za fasta fasta kulkua na kazi ndogo siku hyo.Nilimuonya mlinzi kuwa wakihesabu nondo jioni wakati anakabidhi Lindo afanye kila njia hao walinz wasijue nikampa na ten ( 10k ) akafurahi...niljua tu hii inshu haifanikiwi nikasema hata kama haito fanikiwa sawa tu ila nilivyofika home nilimpigia simu bro wangu ( mtoto wa bamkubwa ) nikamwambia anitafutie wateja wa nondo 40 ( nililapanga kuziuza kwa 10k kila nondo.Bro akasema poa aliniuliza unazitoa wap sikumwambia nkakata simu.

Kesho nikaenda job nikijua tu inshu imebuma nilimkuta mlinzi ndo snakabidhiwa lindo nikajua tu basi hizi nondo watakua wamezihesabu vizuri.niliongea na mlinzi akanambia mambo ni mazuri nifanye haraka kabla ya ukaguzi ( Wazungu walikua wanakuja kukagua tenki siku mbili mbele) basi nikpanga mchana wake ndo nitaziiba mlinzi hakuamini ( kumbe alikua hanijui ).kuna Wamama wawili waliokua wanatupikia chakula niliwafata bila kupepesa macho nikawaambia mpango wangu bahat nzur mmama mmoja alikua anaishi jirani huo mradi.Niliwaambia tiwapa 20k kila mtu kama nitafanikiwa hyo kazi walifurahi.Huyo mmama alikuana Shamba la mihogo karibia na choo tulichokuwa tunatumia vibarua alafu Uzuri na nondo ndo zikuepo basi nikaona kama mambo ni mazuri kidogo.

Baada ya mapumziko ya chakula cha Mchana kama kawaida niliambiwa ninyooshe Nondo mia 50 nikasema hapa ndl pennyewe nilimfuata mlinzi kamwambia avunge anioni na wale Wamama.Nilitumia lile shamba la mihogo kufichia nondo.Mtashangaa niliwezaje ilikua ni kwa spid ya ajabu maana watu wote walikua juu ya tenki wakifukuzana na siku ya ukaguzi had wahindi walikua juu ya tenk kasoro babu mmoja wa kihindi ndo alibaki kwenye Kontena kapumzika.

Roho ilkua inaniuma plus hofu ya kushikwa lakin sikujali nilivyokua naiona 400k kwenye mawazo yangu.nilisoma mchezo nikaona sionwi basi nilikua nashika nondo tano tano nazipitisha chini ya Fence za wire alafu mtoto wa yule mama mpishi alikua anazipokea anazitandaza shambani.Kulikua na majan mengi shambani ko kuziona ilkua ni tizi sana.Baada ya kufanikiwa kuzificha nilivunga kama natoka chooni kisha nikaendelea na kazi yakunyoosha Nondo kama kawa.Siku hyo jioni sikupanda gari la kuturudisha home.Nilisubir watu wakaisha mimi na yule kijana midaa ya usiku tukaingia shambani kuchukua Nondo zetu tulzificha nyumba moja ilikua chini kabisa na huo mradi.Nilirud home nikampigia simu bro wangu akasema mambk yako mazur ko akachukua Bajaj za mzigo tuakaenda kuchukua mali usiku huo huo ilikua kwenye saa 7 usiku.Nilipewa hela yangu na huyo Mbaba tulie muuzia nondo ( tulizingua nae kidogo maana alikua anataka tumuuzie nondo moja kwa 8000 ).nilimpa 30k bro wangu kesho yake nikawapa wale wamama 60k wamgawie na yule kijana wao mlinzi nilimpa 100k iliyobaki nilitunza siku hyo nilimnunulia mpka boss msosi akawa anafurahi tu.Siku zilisonga mlinzi alikubali uwezo wangu akawa anataka niibe tena Mbao fulani hivi zilkuwa hapo ila nilikataa, akawa analalamika eti " Dogo we muoga sana " nilikua na mkwepa tu mpk walimbadilishia eneo la kazi.Siku tuliyokua tunamaliza kazi baada ya kulipwa tu na boss kurudi Kwao Dar nilimpigia simu nikamwambia mkasa mzima alicheka tu.

Hela nilizopata hapo kibaruani niliplan ni lisiti mtihan na nyingine nilimpa Bimkubwa atumie me nilikua sina bado matumizi makubwa ya pesa kwa wakat huo....

Itaendelea tena bado mikasa ni mingi sana niliyokumbana nayo ila bahati mara nyingi ilikua upande wangu.
 
ndo ivo unakuta nature inatumlia hatima yetu duniani
 
Big up mkuu,nilipitia uninja kama wako ila at some point nilikuja kubadilika mpaka leo..Nimecheka sana kila niliposoma matukio yako
ndo ivo mkuu nature ndo inatumlia hatima yetu maishan
 
Inaendelea.....

Mwanzoni mwa mwaka wa 2015 mahusiano kati ya Mzee wangu na Mama angu hayakuwa mazuri walikua wanarumbana sana mpk Mama akawa anatwambia kua ataondoka.Na kweli Mwez wa Tatu aliondoka bila kumtaarifu Mzee.

Mama angu alikua yupo kwenye kikundi cha vikoba bahat nzur alikua ndo mtunza hazina wao.sasa siku wanakorofishana na Mzee hii pia ilikua ni sababu, mzee alikua hataki kabisa Mama awe kwenye kikundi.Na siku Mama ana plan kusepa alitushirikisha Wanae ila akatwambia tusimwambie Mzee.Alisepa na hela ya wanakikundi m 2.8 pamoja na hela ya Ticha mmoja hivi alikua anafundisha shule moja na Mzee sh 400k.

Siku anaondoka alituita wanae tuliopo akatupatia kila mtu 50k na 300k kwa ajili ya matumizi ya home ila alitusihi sana tusije tukatoe no ya simu yake kwa watu ( hasa wanakikundi ) maana alibadili no ya simu.Hakubeba Nguo zake aliondoka na mkoba wake tu, me binafsi sikutaka kujua ni wapi anaenda ila nilikua na muhurumia sana.Baada ya yeye kuondoka na Kutokupatikana kwenye simu Wanakikundi walitaka kuzimia,Walienda Police wakachukua RB ya kumkamata ambapo mpaka Leo hawajawi kumkamata.Ila pesa alilipa Mzee ila Mzee alilaani sana hicho kitendo akaapa mbe yetu kuwa Mama ndo basi tena ( lakini leo hii wapo pamoja tena ).

Nyumbani nilibaki mimi wadogo zangu wa tatu na bro wangu ( mtoto wa Bamkubwa lakin yeye ni tofauti na yule wa mwanzo.Huyu alikua home kuishi baada kumaliza chuo wa walimu ko alikua anasubiria Ajira ambayo alipata mwezi wa Tano 2015 kama nitakua sahihi ).Bro wangu kabisa yeye alikua chuo pamoja sister angu.

Mwezi wa Tano Sister angu alirud home baada ya kumaliza Chuo Ualimu walipishana na huyo bro wangu ( mtoto wa bamkubwa ) yaani huyu anatoka huyu anaingia.Mimi wakati huo nime lisiti mtihani wa Form four.Nilikua nasoma Tuition jioni huku asubui nakuwa kwenye harakati zangu.

Kipindi cha kampeni za Uchaguzi kuna tukio nililifanya...

Me binafsi na Familia yangu tupo Chadema sasa kipindi hicho cha Kampeni harakat nilipunguza hii ni kutokana kulisit Pepa.Kuna siku moja Mzee alikuja Home na mgombea udiwani wa Chadema kutuomba kura.Tuliokuwa tunasifa za kupiga kura nilikua mimi na Sister.Sasa baada ya Huyo mgombea udiwani kuondoka aliniachia Picha ya Lowasa kubwa zile za kubandika kwenye mabango.kwa vile nyumba yeti ilikua karibu na barabara nikaamua niibandike kwenye ukuta nyuma ya Nyumba.Sasa hapo tulipokuwa tunaishi tulikua tunaishi na jamaa mmoja hivi alikua amepanga kagheto kake yaan alikua ni jirani yetu.

Huyo jamaa alikua ni mwendesha bajaji za Mizigo alafu ana ubaunsa fulani hivi kingine ni mwana Ccm damu damu.Siku ya tukio nilibandika picha ya Lowasa vizur tu kwenye ukuta wa nyumba yetu nikaondoka kwenda Kigera kwenye kampeni za Mbunge.Nilivyorudi nakuta picha ya Lowasa imechanwa na kutolewa pale ukutani alafu kuna picha ya Magufuli ( Hapa kazi tu ).nilipandwa na hasira kishenzi nikaulizia nani kafanya vile watoto wakanambie ni yule dereva bajaj ndo kafanya vile.nilimfuata gheto lake hakuepo kwa muda huo ko nikamsubir mpk usiku kwenye saa mbili hivi alivyokuja.Nilimuuliza kiupole tu " mbona umechana picha yangu " akanijibu kunya nikamuacha nikaenda nikachana picha Jiwe na mimi.Kesho yake asubui alivyokuta picha imechanika akamaindi sana.Alinifuata mpk ndani akanivuta mpk nje ( jamaa alikua ana ubaunsa na me nilikua kimbaumbau ) tulivyofika njee ananiuliza kwanini nimechana picha, nikamwambia kidharau kwani ajaona pakueka hiyo picha mpk aweke kwenye ukuta wetu.Akaanza kuiponda nyumba na mawe akidai lazima anishikishe adabu me na Ukoo wangu.Alimtukana Mzee mpk Mama ambao hawa usiki na Sister angu alipigwa kofi alivyo hoji tatizo.Sister alikua anafua ko nilichukua ndo iliyokua na maji yalio suuza nguo nika ya mwaga kisha nikampiga nayo kichwani huyo fala.

Na ilitua vizuri pembeni mwa kichwa chake mpk alianguka chini, aliinuka na kuanza kunifukuza nilikimbila ndani chumbani kwangu nikachukua Nondo ( zile za kunyooshea Nondo zinaitwa bender ) alivyoona ivo akaanza kukimbia lakin alikosea kuanguka, nilimpiga nayo mgongoni na shingon mpk nikaona mtu ametulia tiiii....damu ndo zina mtoka sikioni.Nilivyoona hivo nilikimbilia Iringo kwa bibi yangu nikijua kuwa nimeua.Simu, ndala vyote niliacha home.

Mzee alijulishwa hilo tukio ko aliwai home kuona nini kinaendelea.Jamaa alienda police lakin Mzee alimazana nao na jamaa akalipwa fidia ( 170k ) hata siku naambiwa kuwa mambo yameisha nilkua siamini kama ni kweli.Tokea hapo huyo dereva bajaji alikua ananiogopa kisenge yaani nilkua nikikutana nae hajiamini ila me pia nilikua na taadhari nae mpk siku anahama pale mtaani.

Maisha yalisonga na Kura nilipiga na Mtihani nikafanya fresh majibu yalikuja sio mabaya sana

Tutaendelea bado safari ni ndefu...
 
Inaendelea.....

Mwanzoni mwa mwaka wa 2015 mahusiano kati ya Mzee wangu na Mama angu hayakuwa mazuri walikua wanarumbana sana mpk Mama akawa anatwambia kua ataondoka.Na kweli Mwez wa Tatu aliondoka bila kumtaarifu Mzee.

Mama angu alikua yupo kwenye kikundi cha vikoba bahat nzur alikua ndo mtunza hazina wao.sasa siku wanakorofishana na Mzee hii pia ilikua ni sababu, mzee alikua hataki kabisa Mama awe kwenye kikundi.Na siku Mama ana plan kusepa alitushirikisha Wanae ila akatwambia tusimwambie Mzee.Alisepa na hela ya wanakikundi m 2.8 pamoja na hela ya Ticha mmoja hivi alikua anafundisha shule moja na Mzee sh 400k.

Siku anaondoka alituita wanae tuliopo akatupatia kila mtu 50k na 300k kwa ajili ya matumizi ya home ila alitusihi sana tusije tukatoe no ya simu yake kwa watu ( hasa wanakikundi ) maana alibadili no ya simu.Hakubeba Nguo zake aliondoka na mkoba wake tu, me binafsi sikutaka kujua ni wapi anaenda ila nilikua na muhurumia sana.Baada ya yeye kuondoka na Kutokupatikana kwenye simu Wanakikundi walitaka kuzimia,Walienda Police wakachukua RB ya kumkamata ambapo mpaka Leo hawajawi kumkamata.Ila pesa alilipa Mzee ila Mzee alilaani sana hicho kitendo akaapa mbe yetu kuwa Mama ndo basi tena ( lakini leo hii wapo pamoja tena ).

Nyumbani nilibaki mimi wadogo zangu wa tatu na bro wangu ( mtoto wa Bamkubwa lakin yeye ni tofauti na yule wa mwanzo.Huyu alikua home kuishi baada kumaliza chuo wa walimu ko alikua anasubiria Ajira ambayo alipata mwezi wa Tano 2015 kama nitakua sahihi ).Bro wangu kabisa yeye alikua chuo pamoja sister angu.

Mwezi wa Tano Sister angu alirud home baada ya kumaliza Chuo Ualimu walipishana na huyo bro wangu ( mtoto wa bamkubwa ) yaani huyu anatoka huyu anaingia.Mimi wakati huo nime lisiti mtihani wa Form four.Nilikua nasoma Tuition jioni huku asubui nakuwa kwenye harakati zangu.

Kipindi cha kampeni za Uchaguzi kuna tukio nililifanya...

Me binafsi na Familia yangu tupo Chadema sasa kipindi hicho cha Kampeni harakat nilipunguza hii ni kutokana kulisit Pepa.Kuna siku moja Mzee alikuja Home na mgombea udiwani wa Chadema kutuomba kura.Tuliokuwa tunasifa za kupiga kura nilikua mimi na Sister.Sasa baada ya Huyo mgombea udiwani kuondoka aliniachia Picha ya Lowasa kubwa zile za kubandika kwenye mabango.kwa vile nyumba yeti ilikua karibu na barabara nikaamua niibandike kwenye ukuta nyuma ya Nyumba.Sasa hapo tulipokuwa tunaishi tulikua tunaishi na jamaa mmoja hivi alikua amepanga kagheto kake yaan alikua ni jirani yetu.

Huyo jamaa alikua ni mwendesha bajaji za Mizigo alafu ana ubaunsa fulani hivi kingine ni mwana Ccm damu damu.Siku ya tukio nilibandika picha ya Lowasa vizur tu kwenye ukuta wa nyumba yetu nikaondoka kwenda Kigera kwenye kampeni za Mbunge.Nilivyorudi nakuta picha ya Lowasa imechanwa na kutolewa pale ukutani alafu kuna picha ya Magufuli ( Hapa kazi tu ).nilipandwa na hasira kishenzi nikaulizia nani kafanya vile watoto wakanambie ni yule dereva bajaj ndo kafanya vile.nilimfuata gheto lake hakuepo kwa muda huo ko nikamsubir mpk usiku kwenye saa mbili hivi alivyokuja.Nilimuuliza kiupole tu " mbona umechana picha yangu " akanijibu kunya nikamuacha nikaenda nikachana picha Jiwe na mimi.Kesho yake asubui alivyokuta picha imechanika akamaindi sana.Alinifuata mpk ndani akanivuta mpk nje ( jamaa alikua ana ubaunsa na me nilikua kimbaumbau ) tulivyofika njee ananiuliza kwanini nimechana picha, nikamwambia kidharau kwani ajaona pakueka hiyo picha mpk aweke kwenye ukuta wetu.Akaanza kuiponda nyumba na mawe akidai lazima anishikishe adabu me na Ukoo wangu.Alimtukana Mzee mpk Mama ambao hawa usiki na Sister angu alipigwa kofi alivyo hoji tatizo.Sister alikua anafua ko nilichukua ndo iliyokua na maji yalio suuza nguo nika ya mwaga kisha nikampiga nayo kichwani huyo fala.

Na ilitua vizuri pembeni mwa kichwa chake mpk alianguka chini, aliinuka na kuanza kunifukuza nilikimbila ndani chumbani kwangu nikachukua Nondo ( zile za kunyooshea Nondo zinaitwa bender ) alivyoona ivo akaanza kukimbia lakin alikosea kuanguka, nilimpiga nayo mgongoni na shingon mpk nikaona mtu ametulia tiiii....damu ndo zina mtoka sikioni.Nilivyoona hivo nilikimbilia Iringo kwa bibi yangu nikijua kuwa nimeua.Simu, ndala vyote niliacha home.

Mzee alijulishwa hilo tukio ko aliwai home kuona nini kinaendelea.Jamaa alienda police lakin Mzee alimazana nao na jamaa akalipwa fidia ( 170k ) hata siku naambiwa kuwa mambo yameisha nilkua siamini kama ni kweli.Tokea hapo huyo dereva bajaji alikua ananiogopa kisenge yaani nilkua nikikutana nae hajiamini ila me pia nilikua na taadhari nae mpk siku anahama pale mtaani.

Maisha yalisonga na Kura nilipiga na Mtihani nikafanya fresh majibu yalikuja sio mabaya sana

Tutaendelea bado safari ni ndefu...
Mtoto wa Nyoka ni Nyoka, mother nae kawapiga wanakikundi
 
Inaendelea.....

Maisha huwa hayaeleweki kimtindo baada ya me Kuachana na Sugar mumy wangu 2014 nilikaa bila mahusiano.Nilikua natafuta wakunifaa ni mani lakin mara nyingi nilkua nashindwa ( uoga nao ulinitesa sometimes ) mpaka mwaka 2015 mwezi December kwenye Mahubiri ya Setilite kanisani ya UHURU HATIMAYE yalikua yanarushwa Jioni saa 12 mpk usiku saa 2 ( Wasabato wenzangu mtayakumbuka kabla hayajaailishwa mpaka mwezi wa 2 mwaka 2016 ).Siku hiyo nakumbuka nilikaa viti vya nyuma kabisa na kasimu kangu nachati,sina hili wala lile, Mara akaja mtoto mmoja kisu balaa alinipa hi alafu akakaa pembeni yangu kulikua na kiti kina mtu ila alitoka lakin me nilimwambia kaa tu kiti hakina mtu .Nilishindwa kuongea siku hiyo nikawa namuangalia kiwizi wizi jinsi mtoto alivyo pisi kali.Alikua ni mrembo yaan alipita vigezo vyote nilivyokua navihitaji kimwili lakin kiroho ckujua kwa muda huo.

Siku hiyo sikuongea nae sana mpk alivyoondoka nikajilaumu nikajua bahat haiji mara mbili.Lakin kesho yake tena alikuja kwenye mahubiri tena akakaa ile line ya mstari niliyokua nimekaa sasa nilisema lazima leo nikuongeleshe baada mkutano kuisha, lakin aliwai kuondoka hata mkutano hujaisha niliumia kimtindo.Kesho yake tena Akaja siku hiyo aliwai sana maana nilimkuta kashakaa alafu pembeni kuna mabishoo wa kanisa, roho iliniuma plus wivu nahuku mtu hata cjamsemesha ...siku hyo nilikaa nyuma sana nikiwachora tu wale mabishoo na kweli baada ya mahubir kuisha wakamsindikiza sasa hapo ndo hasira zilinishika balaa ila sikua nalakufanya.

Kesho yake tena alikuja akanikuta nimekaa zangu Nyuma kabisa hata sikumwongelesha nilimuona ananipita na kwenda kuchukua kiti akarudi nacho nilipokua nimekaa nae akakaa pembeni yangu.Moyo ulidunda sana mpk joto nilisikia na kulikua na kaubaridi.Mtoto alinipa hi nikamjibu alafu nikaendelea ku concentrate kwenye somo.muda wa mahubir ulivyoisha tulianza kukusanya viti kuvipeleka ndani ya kanisa Demu nilimuona anaongea na Rafiki angu mmoja, mara nikaitwa na huyo rafiki angu.Nilienda kama sitaki vile, nilifika tukaongea kidogo tukiwa watatu Manzi ikadai isindikizwe kwao ( nilifurahi kinoma ).Tulimsindikiza na njiani rafiki angu aliitwa na manzi yake nikabaki na huyo mrembo.alivyokaribia kufika kwao nilimuomba No zake akanipa, usiku huo huo nikamsaundisha kwanza akavunga kuleta kaugumu kidogo nisimuone yuko cheap sana ila alikubali siku hiyo hiyo ukurasa wetu wa Mapenzi ukaanza.

Penzi likiwa jipya aisee lina raha sana ngoja niweke nukta hapa kwa leo.

Nitaendelea baadae
 
Inaendelea.....

Maisha huwa hayaeleweki kimtindo baada ya me Kuachana na Sugar mumy wangu 2014 nilikaa bila mahusiano.Nilikua natafuta wakunifaa ni mani lakin mara nyingi nilkua nashindwa ( uoga nao ulinitesa sometimes ) mpaka mwaka 2015 mwezi December kwenye Mahubiri ya Setilite kanisani ya UHURU HATIMAYE yalikua yanarushwa Jioni saa 12 mpk usiku saa 2 ( Wasabato wenzangu mtayakumbuka kabla hayajaailishwa mpaka mwezi wa 2 mwaka 2016 ).Siku hiyo nakumbuka nilikaa viti vya nyuma kabisa na kasimu kangu nachati,sina hili wala lile, Mara akaja mtoto mmoja kisu balaa alinipa hi alafu akakaa pembeni yangu kulikua na kiti kina mtu ila alitoka lakin me nilimwambia kaa tu kiti hakina mtu .Nilishindwa kuongea siku hiyo nikawa namuangalia kiwizi wizi jinsi mtoto alivyo pisi kali.Alikua ni mrembo yaan alipita vigezo vyote nilivyokua navihitaji kimwili lakin kiroho ckujua kwa muda huo.

Siku hiyo sikuongea nae sana mpk alivyoondoka nikajilaumu nikajua bahat haiji mara mbili.Lakin kesho yake tena alikuja kwenye mahubiri tena akakaa ile line ya mstari niliyokua nimekaa sasa nilisema lazima leo nikuongeleshe baada mkutano kuisha, lakin aliwai kuondoka hata mkutano hujaisha niliumia kimtindo.Kesho yake tena Akaja siku hiyo aliwai sana maana nilimkuta kashakaa alafu pembeni kuna mabishoo wa kanisa, roho iliniuma plus wivu nahuku mtu hata cjamsemesha ...siku hyo nilikaa nyuma sana nikiwachora tu wale mabishoo na kweli baada ya mahubir kuisha wakamsindikiza sasa hapo ndo hasira zilinishika balaa ila sikua nalakufanya.

Kesho yake tena alikuja akanikuta nimekaa zangu Nyuma kabisa hata sikumwongelesha nilimuona ananipita na kwenda kuchukua kiti akarudi nacho nilipokua nimekaa nae akakaa pembeni yangu.Moyo ulidunda sana mpk joto nilisikia na kulikua na kaubaridi.Mtoto alinipa hi nikamjibu alafu nikaendelea ku concentrate kwenye somo.muda wa mahubir ulivyoisha tulianza kukusanya viti kuvipeleka ndani ya kanisa Demu nilimuona anaongea na Rafiki angu mmoja, mara nikaitwa na huyo rafiki angu.Nilienda kama sitaki vile, nilifika tukaongea kidogo tukiwa watatu Manzi ikadai isindikizwe kwao ( nilifurahi kinoma ).Tulimsindikiza na njiani rafiki angu aliitwa na manzi yake nikabaki na huyo mrembo.alivyokaribia kufika kwao nilimuomba No zake akanipa, usiku huo huo nikamsaundisha kwanza akavunga kuleta kaugumu kidogo nisimuone yuko cheap sana ila alikubali siku hiyo hiyo ukurasa wetu wa Mapenzi ukaanza.

Penzi likiwa jipya aisee lina raha sana ngoja niweke nukta hapa kwa leo.

Nitaendelea baadae
Oya endelea madomo zege kumbe tupo wengi
 
Back
Top Bottom