Hadithi ya kweli ya maisha yangu

Nakumbuka kwenye story yake nilisoma mahali amenunua Kitanda na Godoro akavipeleka kwa rafiki ,.baadae sikujua alivipeleka wapi,.nahisi kuna mahali nimeruka.
Itakua umeruka mkuu au ckuelezea vzr kuhusu hilo.

Asante sana kwa umakin wako kwenye huu uzi big up sana.
 
Me nili lelewa na wazaz ambao walikua busy na kusaka maisha, hawakua care sana na sisi.Kama mdogo wangu wa tano na wa sita ni kama hawajalelewa na Mama.Alikua busy sana kusafir na biashara zake.

Asante sana kwa kufuatilia story yangu Mkuu
Mkuu story yako ni nzuri,inatisha pia inachekesha sana kwa baadhi ya matukio ulofanya. Namna ya usimuliaji na matukio yako ya kibabe ndio imepelekea story izidi kuvutia kuifatilia mpaka mwisho.
Kuna FUNZO kubwa katika Story yako.

Sent from my Redmi 8A using JamiiForums mobile app
 
Inaendelea.....

NILIVYOANZA KUIBA NA KUTEKA WATU VITU

Siyo kwamba ndo nilikua naanza wizi, hapana sema nilkua nimepumzika sasa ndo nikawanimerudi tena rasmi kwenye wizi.

Twende kazi sasa.....

Mwaka 2011 Yule jamaa mtoto wa mwenye nyumba alikua kashamaliza chuo nakurudi home.Alitaka tumuachie chumba kimoja aanzie maisha na kimoja kwa ajili ya wazazi wake wakiwa wanakuja wanafikiapo.Hilo jambo lilitufedhehesha sana hasa mimi lakin tayar jamaa alishaamua nyumba c yao bna tutafanyaje sisi wapangaji....basi jamaa alichagua chumba alichokua analala sister na young sister ndo watoke kusudi yeye ahamie.Sister alimpisha akahamia chumba walichokuwa wanafikia wageni wetu ( kumbuka hiyo nyumba ilikua na vyumba vitano ) ko sisi tukabaki na vyumba vitatu.

Hicho kitendo kilifanya ni mchukie huyo jamaa ila ckuonesha kama namchukia nilijisemea moyoni ni lazima nimkomoe,ckujua na mkomoa vipi ilanilisema cku akijiset tu ataumia.

Basi bna jamaa hata hakukaa sana home akawa amepata kazi idara ya Maji ( Mzee wake ndo alimfanyia connection akawai kupata kazi )

Kabla hatujampa funguo za chumba alichokua anataka nilichomoa funguo mbili, moja ya hicho chumba chake nyingine ya chumba cha wazazi wake.Nilifanya kisiri hakuna alie jua kama nimechomoa funguo.

Wakati huo ndo kwanza nipo form 2 ila jamaa yeye alikua anaongea nasisi vizuri alikua hana noma ila sema alikua ana majivuno sana hicho ndo nilikua simpendei.Siku moja kuna pick up ilikuja hapo homee ikiwa imebeba maboksi yalikua 30.Yale maboksi yalikua yamebeba vitabu vya secondary.Vitabu vilkua vya Chemistry, Physics na Mathematics form 1,2 na 3.

Usiku wa siku aliniita chumbani kwake akanipa vitabu vitatu cha Physic, Chemistry na Mathematics vya form two.Nilimshukuru nikaondoka ila hata nilkua sivisomi.Kuna siku niko darasani kuna jamaa mmoja ( john kisomo wa darasa ) alitaka nimuuzie kitabu cha physic nilimuuliza unashingap akasema buku tano nikasema poa, akanipa nikampa kitabu ila nilimwambia ninavyo vingi anitaftie wateja akasema frsh

Kuna siku sikwenda shule nilikua home tu huyo John kisomo alikuja home ule muda wa wanafunzi kutawanyika.Alikua anataka kitabu cha mathe nikampa kwa ileile bei niliyomuuzia mara kwanza akasepa.Siku hyo nikawaza nikasema kumbe humu ndani nakaaa na mali tu burebure.

Basi nilimtafuta rafiki angu mmoja tulikua tunasoma nae nikamweleza hyo inshu yeye akasema atakua anatafuta wateja kisha hela tunagawana.Na kweli alikua anapata wateja me nampa mali anauza.

Nilikua natumia zile funguo nilizochukua kisiri kuingia chumbani mwa huyo jamaa na kuchukua vitabu kisha tunaenda kuuza.Niliafanya kwa Umakini mkubwa na usiri ckutaka home wajue kitu nachokifanya, kuingia tu nilikua nahakikisha hakuna anaye niona.Nilikua naona ni fresh tu kwa niliyokua nafanya, na tulipiga sana hela me na huyo muhuni wangu tukawa madoni shuleni 🙃🙃 .
Jamaa wala hata alikua hashituki kama namcheza vitabu vyake na ckuwai kujua leengo lake la kuleta vile vitabu ni nini.Nilifurahi maana vilikuwa vinanipa hela za buree.

Siku moja huyo muhuni wangu alipata dili kubwa tu kuna maticha fulani wa shule za private walikua wanaitaji vitabu vya kutosha walitaka vitabu 20 Chemistry na Mathematics kwa Buku 4 kwa kila kitabu.Nilifurahi sana nikaona mambo cndo hayo muhuni wangu alinambia kuwa atavifata jioni home kwetu me nikampanga muda wa kuja nilimwambia ni saa moja ndo atokee tuchukue mzigo tukauhifadhi kwao then kesho yake tukafanye biashara na hao Maticha.

Niliingia chumba cha huyo jamaa kama kawa nikachkua mzigo nikatoka sikuonwa na yoyote nilivificha chini ya godoro langu madogo wasivione nikawa subir saa moja ifike muhuni aje tuvihamishe.Na kweli Muhuni alitimba na Rafiki ake hata nilikua cmjui ila hilo halikua likinihusu kwanza nifurahi maana kazi ilikua imerahisishwa, Tuliviweka kwenye limfuko la Rambo yale Makubwa safari ikaanza kuelekea Maeneo ya buhare ( ndo muhuni alikua anaishi ) tulipitia barabara ya kuelekea Makoko.Tulifika Eneo moja linaitwa Boda 2 Boda darajani ( Mwisenge ) kwa mbele kidogo barabara ilikua ni yavumbi kuna kamto kalikua kanapita chini ya daraja kana mwaga maji kuelea ziwani.

Ghafla tulikutana Kundi la Wahuni nahisi walikua wanatokea Makoko, walikua zaidi ya kumi.Walituteka bna wakaanza kutupiga sachi bahati nzuri ckua na chochote mfukoni mee nilikua mpole ila wale wahuni wangu wawili walikua wabishi kinoma waliparanganya nao ikawa ni vita ni vita Mura 🤣🤣.Hao wahuni walikua wanadai eti tulifanyia Fujo makaburini nilikataa kuwa sio sisi nilichezea bapa za Panga mgongoni walinambia nikae chini.katika zile harakati za kupigana wale wahuni wangu walipata upenyo wakakimbia vitabu vingi viliangukia darajani na baadh vilichanika ko biashara ikawa imeishia hapo.Baada ya wale wahuni wangu kukimbia na kuniachw pale mwenyewe hasira zao zikikahamia kwangu nilipigwa bapa.Huwez amini nilikua napiga kelele za msaada lakini raia walikua wanaogopa kuja kunisaidia.Waliamua tu kunisamehe wenyewe, walinambia nikimbie nilitoka baru sendo ckujua hata zilipoangukia 🤣🤣🤣🤣.Nilikimbia mpk nikawa nasema kumbe kuna kipaji ndani yangu cha riadha ila me ndo ckitumii.

Basi bna biashara ilikufa cku hyo ckujutia sana maana vitu vilikua vya wizi nikaacha maisha yasonge Ila nilistop kuingia kwenye hicho chumba kwa muda.

Nitaendelea tena....
Imetulia
 
Hongera sana home boy kwa kusimulia maisha yako. Nimefatilia simulizi mwanzo mpaka mwisho, bahati nzuri nimeisoma ikiwa imefika tamati. Simulizi yako ni harisi kabsa haijatiwa chumvi wala ndimu, kuna code za kitaa umezitumia katika simuliz yako ambao wenyeji wa Musoma tunazifaham. Ulivyoelezea maisha ya visiwani yako hvyo hivyo, ni ngono, ujambazi(bahati nzuri kwako hukukutana nao ukiwa huko) pombe na maladhi yote ya ngono utayakuta huko.

Aisee simulizi yako kila kipande nilikua siachi kucheka mwenyewe..

Mwisho nimekumaind ulivyowapiga wasimbiti wenzangu tukio nami ntakutafte nikupige tukio😂😂😂😂

BOY HAKIKISHA UMEUACHA WIZI, UTAPELI, NA UKIBAKA. Hakikisha sana tena sana unakaa mbali na hivyo vitu.
 
Hongera sana home boy kwa kusimulia maisha yako. Nimefatilia simulizi mwanzo mpaka mwisho, bahati nzuri nimeisoma ikiwa imefika tamati. Simulizi yako ni harisi kabsa haijatiwa chumvi wala ndimu, kuna code za kitaa umezitumia katika simuliz yako ambao wenyeji wa Musoma tunazifaham. Ulivyoelezea maisha ya visiwani yako hvyo hivyo, ni ngono, ujambazi(bahati nzuri kwako hukukutana nao ukiwa huko) pombe na maladhi yote ya ngono utayakuta huko.

Aisee simulizi yako kila kipande nilikua siachi kucheka mwenyewe..

Mwisho nimekumaind ulivyowapiga wasimbiti wenzangu tukio nami ntakutafte nikupige tukio😂😂😂😂

BOY HAKIKISHA UMEUACHA WIZI, UTAPELI, NA UKIBAKA. Hakikisha sana tena sana unakaa mbali na hivyo vitu.
pamoja sana hommie, tupo pamoja now nime change sana me cyo yule mtu wa zamani kabisa.

Mungu ikua na mimi toka enzi mpk leo kanipa mwanamke makini sana nafurahi kwa hilo.

Pole sana kwa kuwapiga wasimbiti wenzako 😂😂😂 niko radhi unilipizie kisasi ila sio kikubwa sana 😂😂 .

Na karbu sana Mkuu.
 
Hongera kwa kupata mke, nakumbuka mke wangu naye nilimpata kwa staili inayofanana.... Demu alileta bag akakomaa haondoki huku alisisitiza yeye ndio mke Mungu kanipa, nikawa mkali nikampa mateso yote aliyashinda
Basi tupe na ww story yako ilikuwaje kuwaje mpka akawa mke kwa lazima. ukisjaandika tupe link hukuhuku kweny huu uzi tuisome

Sent from my Redmi Note 3 using JamiiForums mobile app
 
Unakipaji kikubwa Sana Cha uandishi tangu nimejiunga jf 2014 ni wewe tu ndio nimesoma story yako na ukafika mwisho tena simulizi ya kweli bila blah blah ...

Fanyia kazi huo uandishi usiache kipawa kipotee.
Yaani mm mwenyewe nilipokiwa nasoma nikajisemea moyoni, huyu mtu si tu MUNGU amempa kipawa cha mziki lakin ana kipawa cha UANDISHI mzuri, maana jinsi ulivyokuwa ukipangilia matukio, asiee nimependa sana, umejua kuzigusa hisia za watu na kuwashika hisia zao wapate kuendelea kukufuatilia sana kwa ukaribu.

Ni makosa madogo madogo ambayo nimeyaona kweny uandishi wake, kama kuweka nukta na koma, hivi ni vitu vidogo sana kweny uandishi lakin vina thamani sana. Yaani unakuta umeanza sentensi ghafla unajikuta umeshaanza kusimulia kitu kingine, kwahiyo ule mtiririko unapotea kwa ghafla, na hii si kwa sana umefanya lakin kama akipata shule nzuri yeyote ile iwe Youtube au mafundisho yoyote online au hata vitabu akienda bookshop yaan atakuwa ni mtu bora sana, anaweza akawa mtunzi mzuri sana hata akapata ajira ya kuandika makala mbalimbali kwenye magazeti.



Sent from my Redmi Note 3 using JamiiForums mobile app
 
Yaani mm mwenyewe nilipokiwa nasoma nikajisemea moyoni, huyu mtu si tu MUNGU amempa kipawa cha mziki lakin ana kipawa cha UANDISHI mzuri, maana jinsi ulivyokuwa ukipangilia matukio, asiee nimependa sana, umejua kuzigusa hisia za watu na kuwashika hisia zao wapate kuendelea kukufuatilia sana kwa ukaribu.

Ni makosa madogo madogo ambayo nimeyaona kweny uandishi wake, kama kuweka nukta na koma, hivi ni vitu vidogo sana kweny uandishi lakin vina thamani sana. Yaani unakuta umeanza sentensi ghafla unajikuta umeshaanza kusimulia kitu kingine, kwahiyo ule mtiririko unapotea kwa ghafla, na hii si kwa sana umefanya lakin kama akipata shule nzuri yeyote ile iwe Youtube au mafundisho yoyote online au hata vitabu akienda bookshop yaan atakuwa ni mtu bora sana, anaweza akawa mtunzi mzuri sana hata akapata ajira ya kuandika makala mbalimbali kwenye magazeti.



Sent from my Redmi Note 3 using JamiiForums mobile app
Nashukuru sana Mkuu wangu kwa ushauri mzuri.
 
Back
Top Bottom