Inaendelea
Kati ya watu ambao walikua hawanipendi Basi Bonge alikua ni wa kwanza tulikua hata tukikutana barabaran hatusalimiani.
Basi siku ile nilivyoona lile geti pale nilimlaani bonge nilijua tu ni yeye ndo kamshaur bro wake waweke lile grill mlango wa nje ila nilisema fresh tu njia itapatikana siku moja.
Ilipita kama wiki tena hivi siku moja nilimtext yule manzi ( wa kwao bonge ) nilimwambia kimatani tu kuwa nime mmiss hatare..lakin hakujibu kitu nikatuma text nyingine nikamwambia namtakia maisha mema akajibu
sawa niliumia kidogo nikasema hata hivyo nina mademu sio yeye tu anisumbue kichwa.
Licha ya hyo nyumba kuwa na vyumba vingi lakin nilikua silali home sana, kuna mshikaj wangu mmoja ni mwanasheria alikua ana gheto lake ko ndo nilikua nalalapo kwake cku moja moja kama hayupo.
Kama zali bana kuna siku natoka kulala kwa huyo mshikaji wangu ilikua saa 2 asubui naelekea home sasa...nilipitia pale kwao na bonge nikaona mlango wa nje uko wazi cku jali niliendelea na safar zangu za kwenda home....jirani na pensula hotel kuna viduka flani hivi vipo hua kuna watu wengi wengi hasa wavuvi na wasio na ramani town hua wapo kupiga umbea.
Nilimkuta bonge alikua na yule mdogo ake wapo dukani cjui walikua wananunua nini....niliwaona na wao wakaniona cku wasemesha ila niliona hyo ni fursa pekee kwangu kulipiza kisasi changu ili roho itulie kwa Amani, nilijifanya kama naendelea zangu na safar kumbe nilikua na hesabu zangu na wachora tu nilimuona yule mdogo wake bonge anaelekea ziwani na mvuvi mmoja ( labda alienda kununua samaki wabichi )..nilimcheki bonge yeye alikua kabaki pale anapiga umbea tu baadh ya wadau pale.
Nilipita kanjia flani hivi kako mliman ili nirud kwao bonge nilikua speed hatare ( hakukua mbali sana ni kama dakika tano hivi unakua umefika )...nilifika kwao bonge nikaangalia angalia pembeni nikahakikisha hakuna mtu maeneo yale moja kwa moja ndani, bahat nzur milango ya chumbani nayo ilikua iko wazi, moja kwa moja mpk kabatin kwenye ile briefcase nilikua speed hatar huku naangalia dirishani kama wanakuja watu, nilikuta kwenye briefcase kuna viela nikavichukua bila hata kuhesabu, nikafungua kabat la nguo nilibeba nguo nyingi.
Nilichukua kadet tatu ya maroon moja, nyeusi moja na kaki moja pia nilichukua staff Jean's 2 zilikua mpya kwenye makaratasi yake.Boksa nazo nilichukua tatu mpya kabisa, shati nilichukua mbili na tishet mbili kali kinoma.Niliingia chumbani kwa yule demu ckukuta cha maana sana nilichukua wigi la huyo demu na spray ili nikaonge manzi angu.sikua na cha kubebea nilichukua begi humohumo cjuo lilikua la nani ila me nilichukua tu nikaweka vitu nikatoka nje kwa haraka sana nilichungulia nikaona hakuna tena mtu huyo nikasepa na beg mgongoni nikarud na ileile njia ya mkato mpk home.
Nilifika home madogo walini shangaa Mzee alikua job kwake na yule mdogo wangu wa kike yeye alikua shule.nilifunga mlango nikatoa vile vitu, madogo niliwapa mgao ma wenyewe ila walini sifu kinoma ( ilo tukio nikikaa kuliwaza nacheka na kuhuzunika cjui bonge angenishika ingekuaje ).
Nilitoa vile vipesa zilikua ni 80k nikawapa madogo 50k watumie nikabaki na 30k ya kutanua nayo.
Zilipita cku nikawa hata siendi kulala kule kwa mshikaji kuna siku yule dogo langu ametoka shule akaja akanambia kuwa bonge amemwambia kuwa ani peleleze kama nina begi jeusi akamwambie, niliona bonge ni fala sana yani anamwambia huyo dogo siri


dogo mwenyewe muongo kama mimi.
nitarejea kidogo.