Jamaani mimi hapa ninatoa ushuhuda wangu jinsi nilivyokua kipindi cha nyuma, nilifanya makosa nakiri ndio nilifanya, ila watu washaanza kuni judge as if me nimewaambia bado ni mwizi,
Nitoe rai kwenu tuwe wavumilivu tu subir story iishe ndo uni judge vizuri.
Inaendelea
Tabia yangu ya kuiba ilikua inaendelea niliendelea kuiba nguo kama kawa mpk huyo jamaa alianza kustuka kuwa nguo zake zinapotea sana.
Kuna siku moja jamaa alileta begi flani hivi lilikua na nguo mbali mbali za kuuzwa, hizo nguo zilikua amemuagizia mchumba wake kwa ajili ya kuziuza ( kwa mujibu wake alivyoniambia )...basi kuna siku niliingia kutafuta chochote kama kawaida yangu ila siku hyo niliingia na bro wangu ( mtoto wa bamkubwa )....



jamaa huyu alikua hana ustarabu kabisa nilijuta kuingia nae.
Jamaa vitu alikua ana vivuruga balaa vingine anavitupa tupa yaani nilichoka, alivyokosa alivyokua anataka aliamua kuchukua Vitasa vya mlango ni vipya, me nilifungua lile begi la nguo nikachukua vinguo vya kike viwili vya kumpa Manzi angu....tulivyo maliza ilibid nianze kupanga vitu vilivyo vurugwa

.
Jamaa alijua kuwa kaibiwa aliniita akanambia me nikaruka futi mia....Jamaa aliamua kumleta pale home binti mmoja hivi ni ndugu yake awe ana muangalizia mji.
Niliona mambo ni mabaya kwa ujio wa huyo binti nilichukia ila sikutaka kuonesha chuki yangu,huo ndo ulikua ni mwanzo wa anguko langu.maana huyo binti alikua anakaza kinoma.Ilibidi nianzishe mazoea nae ya kinafki.na kweli tulizoena nae mpk kuna siku moja nili sex nae ( na alivyokua bonge )...licha ya kumla bado alikua ni kikwazo kwangu yaan kutoka kwake ilikua ni kidogo sana.
Nilipanga nitaibaje asee...kuna siku aliingia king alinitext kuwa niko wap nikamwambia niko town akanambia njoo na chips basi....nikasema poa na kweli nikamletea chips akadai ana nyege hatare nilimgonga siku ( kwenye gheto langu ) wakat huo dogo aliingia chumban kwa jamaa akachukua hela na nguo.
Kuna siku nimeenda Shirati na kwaya tulialikwa kutoa huduma ya uimbaji, safari ilikua ni ya kwenda na kurudi, nilivyokua Shirati kwenye huduma dogo alinipigia simu kuniambia kuwa jamaa kaiba nguo zangu ( nilifua nguo ijumaa usiku, jumamos alfajir niliamka nikazianika nje )....sasa kumbe yule jamaa alichukua hizo nguo.Nilichukia mpk ibada ilikua haipandi kabisa natamani tuwai kuondoka.
Saa mbili usiku tulikua tumesharud kutoka shirati nilifika home nikavua sare yangu, dogo akanipa mkasa mzima nikachukua kisu nikamfuata chumbani kwake,alikua anaona tv pamoja na yule demu ( ndugu yake )...nilifika nikaanzisha moto kwa huyo jamaa nikidai anipe nguo zangu nilimkaba huku nimekitoa kisu kumwelekezea usoni, yule demu ( ndugu yake ) alipiga yowe majirani wakaja kuamua, nilishikwa kutolewa nje yule jamaa akafunga mlango, barozi aliitwa ndo jamaa akatoka lkn alikua kakaa mbali na mimi.
Alidai hizo nguo ni zake na ameshazisafirisha kwenda Butiama ( kwao na Mzee wake ) ila kama na dai ni zangu basi ataagiza ziletwe ili kuondoa utata...nilikubali na ikapangwa siku za hizo nguo kuja.
Nilijua kuumbuka kwangu kuna karibia niliwaza nitafanyaje au nikimbie Musoma...ila niliamua kujikaza kukabir hilo tatizo lililo mbele yangu.
Siku ya tukio ilifika jamaa siku hyo hakwenda kazini siku hyo nilikua na hofu lakin sikua na jinsi...nilimwambia dogo achelewe kutoka shule siku hyo.nikachukua kisu nikakiweka chini ya godoro ili muda ukifika niende nacho kwa ajili ya lolote litakalo tokea.
Mchana gari lilikuja ( range ) wakashuka watu na begi la nguo...walikua ni Mama ake, bro wake na mjomba wake..mngeniona siku hyo nilivyokua


tulisalimiana vizur wakaingia ndani.
Mama ake aliniita na kuniagiza dukani duh...niliona viela kwenye pochi yake tamaa ikaniingia...nilizuga kama nimeenda dukan aliponiagiza maana walitoka nje kuangalia mazingira ya nyumba yao.nilizama chumban speed nikachukua hela kwenye ile pochi ya Mama ( roho inaniuma sana kwa nilio fanya ) 40k tu ndo nilichukua, alafu nikatoka kwa kunyata nikapita kinjia flan ivi nikaenda dukan nilipoagizwa....nilirud kuleta walicho niagiza hata yule Mama hakujua kama nimemcheza.
Barozi aliitwa na nguo kutolewa lakin nilipelewa na maneno nikawa mdogo ko jamaa alishinda yule Mama ni mtu smart sana alinishaur sana niache hyo tabia kama ni kweli nafanya..walilala kesho yake wakarud makwao.Siku fanya baya lolote na kile kisu nilichokificha
Niliendelea kumtafuna yule binti maana muda mwingi tulikua nae pale home tu.
Mzee alipewa notice ya kuhama ikifika mwezi December kwa kisingizio kuwa Nyumba inabak ya Familia..Mzee aliwalaumu bila kujua kuwa chanzo ni mimi.
Nitarejea.