Hadithi ya kusisimua- Mimba ya Jini

Hadithi ya kusisimua- Mimba ya Jini

Samahani mkuu Mzizimkavu, unawanyima watt raha, story in a sehemu 3 mpya ambazo hujaziweka humu. Ila kwa kuheshimu thread yako, I won't spoil it by posting them here, you go ahead the way you want it to be.
 
Samahani Mzizi Mkavu! Umekuwa ukitutesa sana kwa kiu ya kujua nini kiliendelea baada ya sehemu ya 49. Kutokana na hilo, naomba nichukue wasaa huu kubandika sehemu iliyofuata ili kuwasaidia wenzangu wenye kiu kama mimi! Narudia tena kuomba samahani usije ukanifurusha!

Mimba ya Jini - 50
ILIPOISHIA:
"Shehna."
"A...abeee," aliitikia kwa sauti ya kilio.
"Nisamehe mpenzi wangu."
"Huna kosa, nisamehe mimi."
"Kwa kosa gani mpenzi?"
"Nimekutia kwenye mateso bila kosa."
"Shehna huna kosa bali mimi ndiye niliyeshindwa kukusikiliza."
"Hapana Mustafa mwenye makosa ni mimi kushindwa kukueleza ukweli mapema."
SASA ENDELEA...
"Shehna nimekuelewa, najua una wasiwasi lakini ulitakiwa kunieleza mapema, nilikuwa na wasiwasi wewe labda nani lakini akili yangu ilikataa."
"Kwa hiyo umenielewa mimi ni nani?"
"Ndiyo."
"Hutaniacha?"
"Nilikueleza mapema sitakuacha maishani mwangu wewe ni kiumbe muhimu sana. Najuta kutaka kukupoteza wewe, mimi mwenyewe na watoto wetu watarajiwa."
"Mustafa ukitoka hapa hutaitoa siri hii kwa watu?"
"Sitatoa, nimejua makosa yangu sitarudia, Shehna wewe ni kiumbe mwenye huruma sana na mapenzi mazito."
"Kesho utarudi katika hali yako, ukiamka rudi kazini kama kawaida, usihoji kitu chochote ukifika endelea na kazi zako."
"Sawa nimekuelewa."
"Mustafa nitafanya kila kitu ili maisha yako yawe juu baada ya kujifungua nitakubadilishia kazi nataka uwe mmoja wa matajiri duniani."
"Asante mpenzi wangu," Mustafa alimkumbatia Shehna kwa furaha.
"Naomba usiniogope kwa vile ushanijua."
"Siwezi, nakupenda Shehna."
"Baada ya kunipa zawadi ya mtoto baada ya mimi kujifungua mkeo naye atapata mtoto. Nisingempa dawa ya ujauzito mkeo kwa sasa kwa vile nisingeweza kujifungua mpaka ajifungue yeye hivyo ningeteseka kwa uchungu kwa muda mrefu."
"Nimekuelewa mpenzi."
Baada ya mazungumzo ya kimabaha walilala kwa Shehna kuzima taa na kuondoa nguo zote kumuachia Mustafa kulichezea tumbo lililokuwa zimezidi kuwa kubwa. Ilikuwa ni siku ya furaha kwake. Alipanga siku nyingine amuombee Sara msamaha ili atolewe kwenye umbile la kimbwa.
***
Siku ya pili Mustafa aliposhtuka asubuhi alijaribu kumwita mkewe sauti ilitoka.
"Mke wangu."
"Ha! Jamani Mungu mkubwa umepona mume wangu?" Husna alikurupuka usingizini baada ya kusikia sauti ya mumewe.
"Ndiyo."
"Jamani Mungu mkubwa, siamini kama mume wangu leo ukizungumza sauti inatoka!"
"Niandalie maji nioge ili niwahi kazini."
"Unataka kwenda kazini?"
"Ndiyo."
"Kwani unajua ulikuwa kwenye hali gani?"
"Najua, si sauti ilikuwa haitoki sasa naweza kuwasiliana na wateja kama kawaida."
"Si ungeiangalia hali yako kwa wiki ndipo uende kazini?"
"Ni kweli, lakini naamini nimepona."
"Mmh! Haya."
Mkewe Husna alinyanyuka kitandani na kwenda kumwandalia maji mumewe, baada ya kuoga na kupata kifungua kinywa aliondoka kwenda ofisini. Mlinzi alipomuona alishtuka.
"Ha! Bosi."
"Vipi John."
"Umepona?"
"Ndiyo, nipo ofisini," Mustafa hakutaka mazungumzo mengi aliingia moja kwa moja ofisini na aliikuta ipo katika hali ya usafi aliouzoea japo hakuwepo kwa muda mrefu. Hakukuwa na mabadiliko yoyote naye hakuhoji kitu kama alivyoelekezwa na mpenzi wake Shehna. Alifanya kazi kama kawaida mpaka jioni na kurudi nyumbani.
Husna alizidi kumshangaa mumewe na kutaka kujua tatizo lile lilitokana na nini. Baada ya chakula cha usiku wakiwa kitandani alitumia nafasi ile kumuuliza mumewe kilichomsibu.
"Mume wangu pole kwa matatizo, maana asubuhi sikuweza kuzungumza na wewe baada ya kutoka kuwa na haraka ya kuwahi kazini."
"Asante."
"Hivi nini kilichokusibu kupoteza uwezo wa kuzungumza mpaka mganga akasema hutakiwi kutumia dawa yoyote?"
"Mke wangu tuacheni na hayo."
"Hapana mume wangu, ni mimi ndiye nilikuwa nateseka kuishi na wewe muda wote ukiwa bubu. Lazima kuna kitu kilichosababisha hali ile, hata mlinzi alishtuka kuona ukibadilika ghafla wakati mlikuwa mkizungumza."
"Naomba uachane na hayo mke wangu kwa vile nimepona."
"Kwa nini?"
"Kuwa mwelewa au unataka nirudi katika hali niliyokuwa nayo?"
"Hapana."
"Basi tuachane na hayo."
"Nimekuelewa mume wangu."
Mustafa aligeukia upande wa pili na kuvuta shuka, mkewe naye alijisogeza karibu na mumewe na kumkumbatia kuitafuta siku ya pili.
***
Kama kawaida Mustafa alishtuka na kujikuta akiwa pembeni ya mpenzi wake, uso wa Shehna ulikuwa na tabasamu pana na kuzidi kuongeza uzuri wake. Alimuangalia sana Mustafa kama anataka kusema kitu na kufanya aulize.
"Vipi mpenzi?"
"Najua kuna kitu kinakuumiza akili siku nzima."
"Kitu gani?"
"Kuhusu Sara."
"Ni kweli, nilipanga kumuombea msamaha, nina imani wote tumekukosea."
"Mustafa wewe hujanikosea lakini Sara kanikosea sana kafikia hatua ya kutaka kuniua!" Shehna alisema kwa sauti ya kilio.
"Adhabu aliyopata nina imani hawezi kurudia tena."
"Mustafa nitamleta mbele yako aseme siku akirudia sitampa adhabu bali kumuua, nimefanya hivyo kwa ajili ya mapenzi yangu kwako."
"Nakuahidi kuusemea moyo wake hatarudia tena."
"Sawa."
Shehna alinyanyuka na kutoka nje na kupiga makofi, vijakazi na watwana walifika haraka mbele yake kumsikiliza.
"Naam binti wa mfalme wa bahari ya dhahabu unasemaje?"
"Kamleteni Sara mbele yangu."
"Sawa binti mfalme."
Alitoweka ghafla na kumuacha Shehna akirudi ndani, kabla hajaweka makalio chini Sara alikuwa mbele yake katika umbile la kimbwa. Mustafa alishtuka kumuona mbwa mbele yao.
"Mustafa usishtuke huyu ndiye Sara."
"Ha! Usishangae, sijawahi kuona kiumbe mwenye kiburi kama huyu mwanamke."
Sara yote aliyasikia lakini aliogopa kusema kuomba msamaha kwa kuogopa kubweka na kuwatisha.
Itaendelea.

Mimba ya Jini - 50

ILIPOISHIA:
Alitoweka ghafla na kumuacha Shehna akirudi ndani. Kabla hajaweka makalio chini, Sara alikuwa mbele yake katika umbile la ki-mbwa. Mustafa alishtuka kumuona mbwa mbele yao.
"Mustafa usishtuke huyu ndiye Sara."
"Ha! Usishangae, sijawahi kuona kiumbe mwenye kiburi kama huyu mwanamke.
SASA ENDELEA...
Sara yote aliyasikia lakini aliogopa kusema kuomba msamaha kwa kuogopa kubweka na kuwatisha. Machozi yalimtoka na kupiga magoti kuomba msamaha kwani mateso aliyopata asingeyasahau mpaka anakufa. Mustafa machozi ya uchungu yalimtoka kumuonea huruma Sara anavyotaabika.
Shehna alimshika Sara kichwani, ghafla alirudi katika umbile la kibinadamu. Hakusubiri maelezo, Sara alijitupa chini ya miguu ya Shehna kuomba msamaha.
"Shehna shoga yangu najua jinsi gani nilivyokukosea, nipo chini ya miguu yako haki ya Mungu, sitarudia tena kukufuatilia wala kufuatilia mambo yasiyonihusu. Nimeamini sisi wanadamu ndiyo wabaya, pamoja na mabaya yote niliyokutendea, hukuniacha nilale na njaa wala nile jalalani.
Nakuahidi kama utanibakiza na umbile langu la kibinadamu, nitakuwa kiumbe kipya, sitajiingiza tena katika mambo yasiyonihusu."
"Nina imani sasa unanijua, mimi ni nani?" Shehna alimuuliza huku akimtazama kwa jicho kali.
"Shehna."
"Nilipokuja kwako ulinionaje?"
Sara alishindwa kujibu alibakia kimya, Shehna alimuuliza tena.
"Ulikwenda kwa waganga ili kuchunguza kama mimi ni nani?"
"Ji.." hakumalizia, aliogopa kusema.
"Malizia tu, kwani nilipokuja kwako nilikuambia mimi ni nani?"
"Jini."
"Baada ya kunijua?"
"Shehna, nimekukosea naomba unisamehe sitarudia tena, najutia nafsi yangu," Sara alilia kilio cha majuto.
"Mustafa elewaneni na Sara ili likitokea, mimi simo tena," Shehna alijitoa kwenye kiburi cha Sara.
"Sara, ukitoka hapa, ya hapa yaache hapahapa ukiropoka litakalokukuta utalia na nafsi yako."
"Kaka Mustafa sirudii tena, nimejifunza kiburi si maungwana."
"Nina imani mmeelewana leo sitazungumza chochote siku ukinitibua, nitakufanya kiumbe cha ajabu, siwezi kukuua tu ila cha moto utakiona."
"Shehna nakuapia sitathubutu kusema chochote wala kufanya lolote."
"Kesho utaamka asubuhi nyumbani kwako, majirani wakikuona lazima utakutana na maswali mengi, usiwajibu kitu, oga wahi kazini."
"Nimekuelewa shoga yangu."
Shehna alimshika Sara kichwa na kujikuta akipitiwa usingizi mzito, aliwaita wasaizidi wake wamrudishe nyumbani kwake ili asubuhi aamkie kitandani kwake.
Baada ya Sara kuondoka, Shehna alimgeukia Mustafa aliyekuwa ametulia akimtazama na kumwambia:
"Mustafa, kuanzia leo sitaonekana mchana wala kufika kazini kwako."
"Kwa nini?"
"Sina tena uhuru wa awali, najiuliza atakaponiona mchana utanionaje au Sara akiniona ofisini atanionaje?"
"Nina imani kila kitu kimeisha, nimesha kuelewa, siwezi kukushangaa."
"Kwako, lakini kwangu itachukuwa muda kujionesha wazi kwako."
"Sasa nikiwa na shida na wewe?"
"Utaniona mara moja lakini si kama mwanzo."
"Mmh! Sawa," Mustafa alikubali kwa shingo upande.
"Mustafa naomba ukubaliane na mimi ili twende sawa."
"Nimekubali mpenzi."

***
Siku iliyofuata Sara alishtuka asubuhi na kujikuta kitandani kwake, aliamka na kwenda kuoga. Alipotoka nje, majirani zake walimshangaa na kumuuliza alikuwa wapi. Aliwajibu alikuwa safari ila wangezungumza vizuri jioni akirudi kazini. Alikwenda kazini kama kawaida.
Akiwa kazini alijawa na mawazo mengi juu ya maswali ya majirani zake, alijiuliza akirudi atawaeleza alikuwa wapi baada ya kuondoka ghafla. Mawazo yalipokuwa mengi, aliamua kwenda kwa bosi wake kuomba ushauri, baada ya kumsikiliza alimwambia:
"We wanyamazie tu."
"Wasumbufu sana watataka kunichimba, nitashindwa kuwajibu."
"Ulikuwa na wazo gani?"
"Kuhama pale."
"Hakuna tatizo."
Mara simu iliita Mustafa alipoangalia alikuta ni Shehna, alisema kwa sauti.
"Shehna."
"Anasemaje shoga yangu," Sara alisema kwa tabasamu.
Alipokea simu:
"Haloo mpenzi."
"Nipe Sara." Mustafa alimpa simu Sara.
"Haloo shoga," Sara alisema baada ya kuchukua simu.
"Ni hivi, ukitoka hapo usirudi nyumbani, umeshahamishwa."
"Nimehamishiwa wapi?"
"Masaki, nyumba inatazamana na duka la jumla, nina imani hayo yatakuwa maisha yako mapya."
"Asante shoga, ufunguo?"
"Mustafa atakupeleka sehemu yako mpya."
"Asante shoga."
"Haya kwaheri."
Sara alimpa Mustafa simu, baada ya kupokea alipewa maelekezo na Shehna, baada ya kukata simu alimgeukia Sara na kumueleza.
"Ukimaliza kazi nitakupeleka."
"Duh! Siamini nikitoka kazini nakwenda Masaki, siamini nami nimekuwa mtu wa matawi ya juu!" Sara alisema akishika kifua.
"Hongera, ulitaka kumtibua bure kumbe mambo mazuri yalikuwa yakija."
"Mbona nimekoma."
"Nina imani tatizo lako limekwisha, kaendelee na kazi."
"Sawa bosi," Sara alirudi kuendelea na kazi.
Muda wa kutoka Mustafa alimpeleka Msaki kwenye nyumba aliyoelekezwa na Shehna. Ilikuwa nyumba nzuri iliyokuwa na kila kitu ndani, hakukuwa na kitu chochote kutoka chumbani kwake zaidi ya vitu vyake vyote muhimu. Sara aliendelea kumshukuru Shehna na kuona kumbe jini ni umbile lakini wapo wenye roho nzuri kushinda hata wanadamu.
***
Mwezi moja kabla ya kujifungua, Shehna alimweleza Mustafa kuwa muda ule anatakiwa kuwa sehemu maalum ambayo hatakiwi mtu yeyote kuingiza zaidi ya mzazi wake na mkunga tu.
Pia alimweleza kuonana naye itakuwa baada ya miaka mitatu. Mustafa alikubaliana naye, hakuwa na kipingamizi.
Itaendelea wiki ijayo
 
hii hadithi ni nzuri ila mwendelezo wake unachelewa mno
tasavali mkuu usikawie kuiendeleza
 
HADITHI YA KUSISIMUWA MIMBA YA JINI-50

ILIPOISHIA:
“Shehna.”
“A...abeee,” aliitikia kwa sauti ya kilio.
“Nisamehe mpenzi wangu.”
“Huna kosa, nisamehe mimi.”

“Kwa kosa gani mpenzi?”
“Nimekutia kwenye mateso bila kosa.”
“Shehna huna kosa bali mimi ndiye niliyeshindwa kukusikiliza.”
“Hapana Mustafa mwenye makosa ni mimi kushindwa kukueleza ukweli mapema.”
SASA ENDELEA...

“Shehna nimekuelewa, najua una wasiwasi lakini ulitakiwa kunieleza mapema, nilikuwa na wasiwasi wewe labda nani lakini akili yangu ilikataa.”
“Kwa hiyo umenielewa mimi ni nani?”
“Ndiyo.”
“Hutaniacha?”

“Nilikueleza mapema sitakuacha maishani mwangu wewe ni kiumbe muhimu sana. Najuta kutaka kukupoteza wewe, mimi mwenyewe na watoto wetu watarajiwa.”
“Mustafa ukitoka hapa hutaitoa siri hii kwa watu?”
“Sitatoa, nimejua makosa yangu sitarudia, Shehna wewe ni kiumbe mwenye huruma sana na mapenzi mazito.”

“Kesho utarudi katika hali yako, ukiamka rudi kazini kama kawaida, usihoji kitu chochote ukifika endelea na kazi zako.”
“Sawa nimekuelewa.”
“Mustafa nitafanya kila kitu ili maisha yako yawe juu baada ya kujifungua nitakubadilishia kazi nataka uwe mmoja wa matajiri duniani.”

“Asante mpenzi wangu,” Mustafa alimkumbatia Shehna kwa furaha.
“Naomba usiniogope kwa vile ushanijua.”
“Siwezi, nakupenda Shehna.”
“Baada ya kunipa zawadi ya mtoto baada ya mimi kujifungua mkeo naye atapata mtoto. Nisingempa dawa ya ujauzito mkeo kwa sasa kwa vile nisingeweza kujifungua mpaka ajifungue yeye hivyo ningeteseka kwa uchungu kwa muda mrefu.”

“Nimekuelewa mpenzi.”
Baada ya mazungumzo ya kimabaha walilala kwa Shehna kuzima taa na kuondoa nguo zote kumuachia Mustafa kulichezea tumbo lililokuwa zimezidi kuwa kubwa. Ilikuwa ni siku ya furaha kwake. Alipanga siku nyingine amuombee Sara msamaha ili atolewe kwenye umbile la kimbwa.
***
Siku ya pili Mustafa aliposhtuka asubuhi alijaribu kumwita mkewe sauti ilitoka.
“Mke wangu.”
“Ha! Jamani Mungu mkubwa umepona mume wangu?” Husna alikurupuka usingizini baada ya kusikia sauti ya mumewe.
“Ndiyo.”

“Jamani Mungu mkubwa, siamini kama mume wangu leo ukizungumza sauti inatoka!”
“Niandalie maji nioge ili niwahi kazini.”
“Unataka kwenda kazini?”
“Ndiyo.”
“Kwani unajua ulikuwa kwenye hali gani?”

“Najua, si sauti ilikuwa haitoki sasa naweza kuwasiliana na wateja kama kawaida.”
“Si ungeiangalia hali yako kwa wiki ndipo uende kazini?”
“Ni kweli, lakini naamini nimepona.”
“Mmh! Haya.”
Mkewe Husna alinyanyuka kitandani na kwenda kumwandalia maji mumewe, baada ya kuoga na kupata kifungua kinywa aliondoka kwenda ofisini. Mlinzi alipomuona alishtuka.

“Ha! Bosi.”
“Vipi John.”
“Umepona?”
“Ndiyo, nipo ofisini,” Mustafa hakutaka mazungumzo mengi aliingia moja kwa moja ofisini na aliikuta ipo katika hali ya usafi aliouzoea japo hakuwepo kwa muda mrefu. Hakukuwa na mabadiliko yoyote naye hakuhoji kitu kama alivyoelekezwa na mpenzi wake Shehna. Alifanya kazi kama kawaida mpaka jioni na kurudi nyumbani.

Husna alizidi kumshangaa mumewe na kutaka kujua tatizo lile lilitokana na nini. Baada ya chakula cha usiku wakiwa kitandani alitumia nafasi ile kumuuliza mumewe kilichomsibu.
“Mume wangu pole kwa matatizo, maana asubuhi sikuweza kuzungumza na wewe baada ya kutoka kuwa na haraka ya kuwahi kazini.”
“Asante.”

“Hivi nini kilichokusibu kupoteza uwezo wa kuzungumza mpaka mganga akasema hutakiwi kutumia dawa yoyote?”
“Mke wangu tuacheni na hayo.”
“Hapana mume wangu, ni mimi ndiye nilikuwa nateseka kuishi na wewe muda wote ukiwa bubu. Lazima kuna kitu kilichosababisha hali ile, hata mlinzi alishtuka kuona ukibadilika ghafla wakati mlikuwa mkizungumza.”

“Naomba uachane na hayo mke wangu kwa vile nimepona.”
“Kwa nini?”
“Kuwa mwelewa au unataka nirudi katika hali niliyokuwa nayo?”
“Hapana.”
“Basi tuachane na hayo.”

“Nimekuelewa mume wangu.”
Mustafa aligeukia upande wa pili na kuvuta shuka, mkewe naye alijisogeza karibu na mumewe na kumkumbatia kuitafuta siku ya pili.
***
Kama kawaida Mustafa alishtuka na kujikuta akiwa pembeni ya mpenzi wake, uso wa Shehna ulikuwa na tabasamu pana na kuzidi kuongeza uzuri wake. Alimuangalia sana Mustafa kama anataka kusema kitu na kufanya aulize.
“Vipi mpenzi?”
“Najua kuna kitu kinakuumiza akili siku nzima.”
“Kitu gani?”

“Kuhusu Sara.”
“Ni kweli, nilipanga kumuombea msamaha, nina imani wote tumekukosea.”
“Mustafa wewe hujanikosea lakini Sara kanikosea sana kafikia hatua ya kutaka kuniua!” Shehna alisema kwa sauti ya kilio.

“Adhabu aliyopata nina imani hawezi kurudia tena.”
“Mustafa nitamleta mbele yako aseme siku akirudia sitampa adhabu bali kumuua, nimefanya hivyo kwa ajili ya mapenzi yangu kwako.”
“Nakuahidi kuusemea moyo wake hatarudia tena.”
“Sawa.”

Shehna alinyanyuka na kutoka nje na kupiga makofi, vijakazi na watwana walifika haraka mbele yake kumsikiliza.
“Naam binti wa mfalme wa bahari ya dhahabu unasemaje?”
“Kamleteni Sara mbele yangu.”
“Sawa binti mfalme.”

Alitoweka ghafla na kumuacha Shehna akirudi ndani, kabla hajaweka makalio chini Sara alikuwa mbele yake katika umbile la kimbwa. Mustafa alishtuka kumuona mbwa mbele yao.
“Mustafa usishtuke huyu ndiye Sara.”

“Ha! Usishangae, sijawahi kuona kiumbe mwenye kiburi kama huyu mwanamke.”
Sara yote aliyasikia lakini aliogopa kusema kuomba msamaha kwa kuogopa kubweka na kuwatisha.

Itaendelea Jumapili ijayo
 
HADITHI YA KUSISIMUWA MIMBA YA JINI-51-

ILIPOISHIA:
Alitoweka ghafla na kumuacha Shehna akirudi ndani. Kabla hajaweka makalio chini, Sara alikuwa mbele yake katika umbile la ki-mbwa. Mustafa alishtuka kumuona mbwa mbele yao.
"Mustafa usishtuke huyu ndiye Sara."
"Ha! Usishangae, sijawahi kuona kiumbe mwenye kiburi kama huyu mwanamke.

SASA ENDELEA...

Sara yote aliyasikia lakini aliogopa kusema kuomba msamaha kwa kuogopa kubweka na kuwatisha. Machozi yalimtoka na kupiga magoti kuomba msamaha kwani mateso aliyopata asingeyasahau mpaka anakufa. Mustafa machozi ya uchungu yalimtoka kumuonea huruma Sara anavyotaabika.

Shehna alimshika Sara kichwani, ghafla alirudi katika umbile la kibinadamu. Hakusubiri maelezo, Sara alijitupa chini ya miguu ya Shehna kuomba msamaha.
"Shehna shoga yangu najua jinsi gani nilivyokukosea, nipo chini ya miguu yako haki ya Mungu, sitarudia tena kukufuatilia wala kufuatilia mambo yasiyonihusu. Nimeamini sisi wanadamu ndiyo wabaya, pamoja na mabaya yote niliyokutendea, hukuniacha nilale na njaa wala nile jalalani.
Nakuahidi kama utanibakiza na umbile langu la kibinadamu, nitakuwa kiumbe kipya, sitajiingiza tena katika mambo yasiyonihusu."
"Nina imani sasa unanijua, mimi ni nani?" Shehna alimuuliza huku akimtazama kwa jicho kali.
"Shehna."
"Nilipokuja kwako ulinionaje?"

Sara alishindwa kujibu alibakia kimya, Shehna alimuuliza tena.
"Ulikwenda kwa waganga ili kuchunguza kama mimi ni nani?"
"Ji.." hakumalizia, aliogopa kusema.

"Malizia tu, kwani nilipokuja kwako nilikuambia mimi ni nani?"
"Jini."
"Baada ya kunijua?"

"Shehna, nimekukosea naomba unisamehe sitarudia tena, najutia nafsi yangu," Sara alilia kilio cha majuto.
"Mustafa elewaneni na Sara ili likitokea, mimi simo tena," Shehna alijitoa kwenye kiburi cha Sara.
"Sara, ukitoka hapa, ya hapa yaache hapahapa ukiropoka litakalokukuta utalia na nafsi yako."

"Kaka Mustafa sirudii tena, nimejifunza kiburi si maungwana."
"Nina imani mmeelewana leo sitazungumza chochote siku ukinitibua, nitakufanya kiumbe cha ajabu, siwezi kukuua tu ila cha moto utakiona."

"Shehna nakuapia sitathubutu kusema chochote wala kufanya lolote."
"Kesho utaamka asubuhi nyumbani kwako, majirani wakikuona lazima utakutana na maswali mengi, usiwajibu kitu, oga wahi kazini."
"Nimekuelewa shoga yangu."

Shehna alimshika Sara kichwa na kujikuta akipitiwa usingizi mzito, aliwaita wasaizidi wake wamrudishe nyumbani kwake ili asubuhi aamkie kitandani kwake.
Baada ya Sara kuondoka, Shehna alimgeukia Mustafa aliyekuwa ametulia akimtazama na kumwambia:
"Mustafa, kuanzia leo sitaonekana mchana wala kufika kazini kwako."
"Kwa nini?"

"Sina tena uhuru wa awali, najiuliza atakaponiona mchana utanionaje au Sara akiniona ofisini atanionaje?"
"Nina imani kila kitu kimeisha, nimesha kuelewa, siwezi kukushangaa."

"Kwako, lakini kwangu itachukuwa muda kujionesha wazi kwako."
"Sasa nikiwa na shida na wewe?"

"Utaniona mara moja lakini si kama mwanzo."
"Mmh! Sawa," Mustafa alikubali kwa shingo upande.
"Mustafa naomba ukubaliane na mimi ili twende sawa."
"Nimekubali mpenzi."

***
Siku iliyofuata Sara alishtuka asubuhi na kujikuta kitandani kwake, aliamka na kwenda kuoga. Alipotoka nje, majirani zake walimshangaa na kumuuliza alikuwa wapi. Aliwajibu alikuwa safari ila wangezungumza vizuri jioni akirudi kazini. Alikwenda kazini kama kawaida.

Akiwa kazini alijawa na mawazo mengi juu ya maswali ya majirani zake, alijiuliza akirudi atawaeleza alikuwa wapi baada ya kuondoka ghafla. Mawazo yalipokuwa mengi, aliamua kwenda kwa bosi wake kuomba ushauri, baada ya kumsikiliza alimwambia:
"We wanyamazie tu."

"Wasumbufu sana watataka kunichimba, nitashindwa kuwajibu."
"Ulikuwa na wazo gani?"
"Kuhama pale."

"Hakuna tatizo."
Mara simu iliita Mustafa alipoangalia alikuta ni Shehna, alisema kwa sauti.
"Shehna."

"Anasemaje shoga yangu," Sara alisema kwa tabasamu.
Alipokea simu:
"Haloo mpenzi."

"Nipe Sara." Mustafa alimpa simu Sara.
"Haloo shoga," Sara alisema baada ya kuchukua simu.
"Ni hivi, ukitoka hapo usirudi nyumbani, umeshahamishwa."
"Nimehamishiwa wapi?"

"Masaki, nyumba inatazamana na duka la jumla, nina imani hayo yatakuwa maisha yako mapya."
"Asante shoga, ufunguo?"

"Mustafa atakupeleka sehemu yako mpya."
"Asante shoga."
"Haya kwaheri."

Sara alimpa Mustafa simu, baada ya kupokea alipewa maelekezo na Shehna, baada ya kukata simu alimgeukia Sara na kumueleza.
"Ukimaliza kazi nitakupeleka."

"Duh! Siamini nikitoka kazini nakwenda Masaki, siamini nami nimekuwa mtu wa matawi ya juu!" Sara alisema akishika kifua.
"Hongera, ulitaka kumtibua bure kumbe mambo mazuri yalikuwa yakija."
"Mbona nimekoma."

"Nina imani tatizo lako limekwisha, kaendelee na kazi."
"Sawa bosi," Sara alirudi kuendelea na kazi.

Muda wa kutoka Mustafa alimpeleka Msaki kwenye nyumba aliyoelekezwa na Shehna. Ilikuwa nyumba nzuri iliyokuwa na kila kitu ndani, hakukuwa na kitu chochote kutoka chumbani kwake zaidi ya vitu vyake vyote muhimu. Sara aliendelea kumshukuru Shehna na kuona kumbe jini ni umbile lakini wapo wenye roho nzuri kushinda hata wanadamu.
***
Mwezi moja kabla ya kujifungua, Shehna alimweleza Mustafa kuwa muda ule anatakiwa kuwa sehemu maalum ambayo hatakiwi mtu yeyote kuingiza zaidi ya mzazi wake na mkunga tu.

Pia alimweleza kuonana naye itakuwa baada ya miaka mitatu. Mustafa alikubaliana naye, hakuwa na kipingamizi.

Itaendelea siku ya Jumatano
 
Kaka nimeamua kuisambaza hadithi kwenye group la tanuru la fikra na kwenye wall yangu ili isomwe na wengi na nimekuandika kama wewe mwandishi wa habari hiyoo nimeipenda na nitaasambaza naomba unisamehe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom