Hadithi: Uchawi wa bilionea Bazoka

Mkuu Nyemo nimefurahi kukuona uku mara nyingi inabid niingie fb kusoma simulizi zako nadhan kwa sasa nitakuwa mubashara...
Ombi langu ni moja fanya mpango account yako iwe verified na uwe na uzi maalumu wa story zako wafuatiliaji wengi huku...
Japo na wajuaji wapo pia
Haina shida mkuu! Ngoja nilifanyie kazi..nitakapokwama nitakushtua inbox
 
NYEMO CHILONGANI
UCHAWI WA BILIONEA BAZOKA
0718069269

SEHEMU YA 11.

Frank akaogopa, mwili wake ulimsisimka, hakuamini alichokuwa akikiona, lilikuwa jambo lisilowezekana hata kidogo mahali hapo kuwa na makaburi. Alilifahamu hilo eneo, kulijengwa nyumba nyingi ikiwemo ya Bi. Semeni ambaye ndiye alitumwa kwake kwenda kuichimbia dawa ile, cha ajabu sana kuwahi kukiona maishani mwake, eti mahali hapo hapakuwa na nyumba.
Alibaki akitetemeka, moyo wake ulikuwa na hofu na wakati mwingine alihisi kabisa mwili kusisimka kama alikuwa akiangalia jambo fulani la kutisha mno. Alitamani kukimbia lakini akahisi miguu yake kuwa mizito kufanya hivyo.
“Nyumba haipo! Inawezekana vipi?” lilikuwa swali lililojirudia kichwani mwake bila kuwa na jibu lolote lile.
Huku akiwa amezubaa mahali hapo ndipo wazo la kurudi alipotoka lilipokuja kichwani mwake, hakutaka kusubiri tena, haraka sana akaondoka mahali hapo na kurudi nyumbani kwake, alipofika tu, akaingia chumbani na kujifungia.
Kijasho chembamba kilikuwa kikimtoka mfululizo, kulikuwa na mambo mengi ya kishirikina aliyokuwa akiyasikia na kuyaona alipokuwa mdogo lakini siku hiyo, kwa lile aliloliona halikuelezeka hata kidogo.
“Hivi ilikuwaje?” alijiuliza huku akiwa kitandani mwake.
Wakati akijiuliza hivyo akahisi mwili wake ukisisimka kwa mara nyingine ila mara hii ilikuwakwa kiasi kikubwa, aliyasikia mafeni ya majirani yakinguruma, wengine wakiangalia televisheni lakini ghaflatu mahali pote hapo kukawa na ukimya wa ajabu, yaani kama kwenye dunia hii alibaki peke yake.
Haikuwa kawaida, akasimama kutoka kitandani kwa lengo la kuelekea nje, akaanza kuusogelea mlango ili aufungue, maajabu yaliyotokea hakuwa akiufikia mlango, yaani ulionekana kuwa mbali kabisa. Alipiga hatua kama mia moja na ishirini na hakuweza kuufikia mlango huo.
Ilikuwa ni ajabu mno, alijua kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea, akarudi kitandani na kukaa kitako, sasa akaanza kujuta sababu iliyomfanya kutaka kupambana na Bi. Semeni, mwanamke aliyekuwa hatari sana.
Akiwa anajifikiria sana, mara akasikia mlango ukigongwa, hakujua alikuwa nani, ilikuwa ni usiku sana na hakuwahi kupata ugeni wowote ule hasa kwa muda kama huo, akasimama na kuanza kuusogelea mlango, kilichotokea, aliufikia mlango, haikuwa kama sekunde chache zilizopita, akaufungua.
Macho yake yakagongana na ya mtu aliyesimama nje ya mlango ule, alikuwa mke wake, Sarah. Alishangaa, ilikuwaje mwanamke huyo aruhusiwe kutoka peke yake hospitalini na wakati alimuacha akipatiwa matibabu?
“Mke wangu!” aliita huku akionekana kushtuka.
“Mbona uliniacha?” aliuliza Sara huku akimwangalia Frank kwa macho ya mshangao.
“Kwa nini upo hapa?” aliuliza huku akiweweseka.
“Si kwetu ama? Ulitaka niendelee kubaki hospitalini?” aliuliza Sarah huku akiingia ndani.
Frank hakuzungumza kitu, alibaki akiwa amesimama kama mtu aliyepigwa misumali pale mlangoni, alimshangaa mke wake, haikuwa hali ya kawaida, alimwacha hospitalini tena akiwa kwenye maumivu makali, sasa iweje mwanamke huyo awe mahali hapo? Tena akionekana kuwa mzima kabisa.
“Unajua unanichanganya sana mke wangu!” alisema Frank, sasa akapata nguvu ya kumsogelea pale kitandani.
“Wewe ndiye unanishangaza! Kwa nini uliniacha hospitalini na wakati daktari alisema unisubiri?” aliuliza Sarah huku akimwangalia mume wake.
‘Daktari alisema nikusubiri?”
“Ndiyo! Wewe ukachukua Bajaj na kuondoka zako! Kwa nini?” aliuliza.
“Daktari alisema nikusubiri muda gani? Halafu....Halafu mbona kama unaonekana mzima wa afya?” aliuliza Frank, yaani mpaka muda huo hakuwa akijua kilichokuwa kikiendelea.
“Frank mume wangu!” alimwambia.
“Unasemaje?”
“Kwanza kwa nini unataka kumuua bibi wa watu? Amekukosea nini?” aliuliza Sarah.
“Kumuua bibi wa watu? Bibi yupi?”
“Bi. Semeni!”
“Mimi nimuue Bi. Semeni, ili?”
“Sasa kwa nini ulitaka kwenda kuchimba dawa nyumbani kwake?” aliuliza Sarah huku akimwangalia.
Frank akashtuka, suala la kwenda kuchukua dawa kwa mganga ilikuwa siri, hapakuwa na mtu aliyekuwa akifahamu zaidi yake yeye na dereva Bajaj aliyekuwa ameondoka mahali hapo.
Sarah alirudi nyumbani na kumwambia alichukua dawa na alitaka kwenda kuifukia kwa Bi. Semeni, alijuaje na wakati mwanamke huyo alimuacha hospitalini? Akahisi kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea mahali hapo, na kama mwanaume ilikuwa ni lazima akigundue ni kitu gani.
“Sarah mke wangu!”
“Naomba maji ninywe kwanza,” alisema mwanaume huyo.
Frank hakutaka kujali, akachukua kikombe, akafungua friji na kuanza kumimina maji huku akiwa amempa mgongo mke wake, alipomaliza na kugeuka nyuma, Sarah hakumuona, yaani chumbani kwake alikuwa peke yake.
Alishangaa, lilikuwa ni ajabu jingine kabisa. Mlango ulifungwa, haukufunguliwa, huyo Sarah alikuwa nyuma yake wakati akimimina maji kwenye glasi, ghafla tu mwanamke huyo hakuonekana.
Mshtuko alioupata mpaka glasi ya maji ikdondoka na kupasuka vipande vipande. Nyumba hiyo ikaonekana kuwa na mauzauza, kitu kilichokuja kichwani mwake kwa haraka sana ni kuchukua ile dawa aliyopewa akaichimbe kwa Bi. Semeni, alipoanza kuitafuta, ajabu ni kwamba hakuipata na wakati aliiweka kwenye mfuko wa nailoni.
“Ilikuwa hapa! Dawa iko wapi?” alijiuliza huku akiupekua mfuko ule kwa zaidi ya mara tano.
Kwa kuchanganyikiwa hivyo akatoka ndani ya chumba chake na kuanza kuelekea kule kwa Bi. Semeni, cha ajabu kabisa kipindi hiki aliiona nyumba ile, yaani yale makaburi aliyoyaona kipindi kilichopita hayakuwepo tena.
Ilimshangaza sana, aliiangalia nyumba hiyo kwa dakika kadhaa, akaamua kuanza kuelekea nyuma ya nyumba hiyo. Hali ilikuwa ni ya ukimya kabisa, hapakuwa na sauti yoyote ile, hakutembea kwa kujiamini kwani aliamini endapo mtu yeyote angemuona mahali hapo, angejua alikuwa mwizi aliyetaka kuvunja nyumba hiyo na kuingia ndani.
Taa zote ndani ya nyumba hiyo zilikuwa zimezimwa isipokuwa chumba kimoja tu ambacho kwa mawazo yake yalimwambia kilikuwa chumba cha mwanamke huyo alichokitumia kulala, akaanza kusogea dirishani ili asikie kama kulikuwa na mtu ama kulikuwa na kitu gani kilichokuwa kikiendelea.
Aliposogea, alisikia sauti za watu wawili wakicheka na kuongea, sauti hizo alizigundua dhahiri, hazikuwa ngeni masikioni mwake, sauti moja ya mwanaume ilikuwa yake na nyingine ya kike ilikuwa ya mke wake.
Ilimshangaza mno! Ilikuwa yeye na mke wake wawe ndani ya nyumba ile, tena wakiongea na kucheka sana kana kwamba hapakuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea. Alipigwa ganzi pale dirishani, mwili wake alihisi kama umepooza, kwenye mauzauza aliyokuwa akiyaona kwa usiku huo, aliamini mwanamke huyo alikuwa mchawi kuliko wote waliowahi kuumbwa kwenye dunia hii.
Wakati akiwa amesimama tu hapo dirishani, mara akaanza kusikia vishindo vya mtu vikija kutoka nyuma yake, alishtuka, hakuwa amelitegemea hilo, haraka sana akageuka na macho yake kutua kwa Bi. Semeni, mwanamke huyo alikuwa uchi wa mnyama, wakabaki wakiangaliana kama watu waliotaka kufahamiana zaidi.
“Unafanya nini hapo?” lilikuwa swali alilouliza mwanamke huyo.
Ghafla tu Frank akashtuka na kujikuta akiwa katika makaburi ya Mburahati, alizungukwa na watu wengi, alikuwa uchi wa mnyama, na kila mtu aliyekuwa mahali hapo alikuwa akimshangaa, ilikuwa ni asubuhi ya saa mbili.
***
Moyo wa Bazoka haukuwa kama ulivyokuwa kipindi cha nyuma, alifanya mauaji ya mtoto kwa mara ya kwanza kwenye maisha yake, aliumia lakini hakuwa na jinsi, ili kuendelea kuwa na utajiri aliokuwanao ilikuwa ni lazima afanye kile alichokuwa amekifanya.
Biashara zakezilizidi kuchanganya, kafara ya mtoto aliyokuwa ameitoa iliwavuta wateja wengi na kuendelea kuingiza pesa nyingi. Alifanikiwa kufanya mauaji hayo na mtu mwingine ambaye alitakiwa kummaliza alikuwa mwanamke mzee, hakujua angempata wapi lakini alikuwa na uhakika ilikuwa ni lazima ampate mtu huyo.
Siku hiyo akaondoka zake na kuelekea mitaani, alikuwa na kazi kubwa ya kumtafuta mwanamke mzee, alikuwa akiangalia huku na kule, mara nyingi alipokuwa kwenye safari zake ilikuwa ni rahisi sana kuwaona wazee lakini cha kushangaza siku hiyo ni kama wazee wote waliambiwa wakae ndani kwa kuwa alikuwa akipita.
Aliendesha gari lake kwa mwendo wa taratibu, alikuwa akipita mitaa ya Manzese ambapo aliamini kulikuwa na wazee wengi, na ilikuwa rahisi kuwateka tofauti na mitaa mingine ya watu waliokuwa na pesa kama Osterbay ama Upanga.
Huku akiwa amefika maeneo ya Mburahati karibu na makaburi macho yake yakatua kwa watu wengi waliokuwa wamesimama kwenye makaburi huku wakionekana wakiwa wamezunguka kukiangalia kitu fulani.
Hakutaka kujali sana, akataka kuondoka lakini akawa na msukumo mkubwa moyoni mwake ukimwambia ilikuwa ni lazima ateremke na kwenda kuangalia ili kujua kulikuwana nini, na kwa jinsi watu walivyozidi kwenda kule, akahamasika kufanya hivyo.
Akalipaki gari lake, akaufungua mlango na kuteremka, akaanza kuelekea kule makaburini, akapenyapenya na macho yake kutua kwa mwanaume aliyekuwa amelala chini, alimwangalia, hakuwa akimfahamu, ghafla akayafumbua macho yake na kuanza kuangalia mahali hapo.
Ni kama alishangaa, hakujua kilichokuwa kikiendelea, hapakuwa na mtualiyecheka, jambo hilo halikuwa la kawaida hata kidogo. Alichokifanya Bazoka ni kumuinua, akavua fulana yake na kumfunga kwa chini kuficha sehemu zake za siri na kuanza kuondoka naye kwenda ndani ya gari.
Bado Frank alikuwa akishangaa, hakujua kilichokuwa kikiendelea, alikumbuka vilivyo kwamba mara ya mwisho alikuwa nje ya nyumba ya Bi. Semeni ambapo alijisikia yeye na mke wake wakiwa wanacheka ndani ya nyumba hiyo, mara ghafla tu akajikuta akiwa makaburini huku akiwa amezungukwa na watu, mbaya zaidi alikuwa uchi wa mnyama.
Hakujua kilichotokea lakini alihisi alirogwa kwani haikuwa hali ya kawaida hata kidogo. Mwanaume aliyemchukua akamuingiza ndani ya gari na kuondoka mahali hapo pasipo kusema lolote lile.
“Mzee mwenzangu imekuwaje kulala makaburini?” aliuliza Bazoka huku akimwangalia Frank aliyeonekana kutokuwa sawa kabisa.
“Yaani acha tu!”
“Kwani imekuwaje?”
“Nadhani nilirogwa!”
“Ulirogwa? Na nani?” aliuliza.
“Yaani daah! Kweli uchawi upo!”
“Kwani ilikuwaje?” aliuliza Bazoka.
Frank akaanza kumsimulia Bazoka kila kitu kilichokuwa kimetokea, mwanaume huyo alikuwa kimya huku akimsikiliza. Kwa jinsi alivyosimulia, Bazoka akaamini kweli kulikuwa na watu waliokuwa na nguvu za kichawi.
Aliambiwa kuhusu Bi. Semeni, jinsi alivyomfanya mpaka kujikuta akiwa makaburini huku amelala. Bazoka akakenua, hakuamini kama kazi ingekuwa nyepesi kiasi hicho.
Alikuwa safarini kumtafuta mwanamke mzee kwa lengo la kumtoa kafara, kitendo cha kuambiwa kulikuwa na bibi aliyeitwa Semeni kwake ilikuwa ni bora zaidi, kwa kumtumia huyo Frank ilikuwa ni lazima afanikishe kumpata bibi huyo.
“Umesema anaishi wapi?” aliuliza.
“Magomeni!”
“Sawa! Twende ukanionyeshe hata nyumba yake,” alisema Bazoka.
Hawakuchukua dakika nyingi wakafika maeneo hayo, Frank akamuonyesha nyumba aliyokuwa akiishi Bi. Semeni na kumwambia alikuwa mwanamke hatari sana, kupambana naye ilikuwa ni vigumu kwa kuwa alikuwa mwanga, aliyeroga na kufanya lolote alilotaka kufanya.
Mtaa mzima ulimuogopa, wengi walimgwaya kutokana na mauzauza yake hivyo kama kweli alitaka kuonana naye ama kumfanyia kitu chochote kile, alitakiwa kuwa makini mno.
“Haina shida. Ahsante sana kwa kunionyesha, mengine niachie mimi,” alisema Bazoka, hakutaka kumuacha mwanaume huyo hivyohivyo, akampa suruali yake avae na yeye kubaki na pensi, akaondoka zake huku akiwa na hamu ya kukutana na Bi. Semeni ili apambane naye, ilikuwa ni lazima amtoe kafara kama alivyoambiwa.

Je, nini kitaendelea?
 
UCHAWI WA BILIONEA BAZOKA.
IMEANDIKWA: NYEMO CHILONGANI.
0756362035

Sehemu ya 05.

Ilikuwa kazi ngumu, kila aliponunua kilo mia moja, alipoondoka, alikaa nusu saa, mchele ulikwisha na kurudia kilo mia moja.
Ni ndani ya saa tatu tu, zile tani moja za mchele kwenye gari lile zilimalizika, zote aliuza Bazoka kitu kilichokuwa kimemshangaza sana.
“Bazoka!” aliita Hamisi.
“Niambie mshikaji wangu!”
“Umeanza lini kuuza mchele?”
“Leo! Yaani mpaka nimeshangaa, mchele umekwisha fasta sana,” alisema Bazoka.
“Kila mtu ameshangaa, imekuwaje?” aliuliza Hamisi.
Alipouliza hivyo ndipo alipokumbuka kile alichoambiwa usiku uliopita, ule utajiri alioambiwa ndiyo ambao ulikuwa ukimnyemelea. Hakujibu swali hilo, akajifanya akipuuzia na kuondoka sokoni hapo na kurudi nyumbani.
Alikuwa na kiasi kikubwa cha pesa, alijishangaa, katika maisha yake hakuwahi kushika kiasi kikubwa kama kile alichokuwanacho. Alipofika nyumbani, akamgawia Asha ile pesa aliyoazimwa na baba yake na kumpelekea.
Asha alishangaa, hakuamini alichokiona, hakujua mahali ambapo mpenzi wake alizipata pesa nyingi kiasi kile, alimuuliza na kitu pekee alichoweza kujibu Bazoka ni kwamba alifanya biashara.
Huo ndiyo ukawa mwanzo wa utajiri wake, akawa mfanyabiashara wa mchele, kila siku aliuza kiasi kikubwa mno, alipata pesa kupita kawaida, kila mtu alikuwa akimshangaa huku wengine wakimwambia alikuwa na kismati kuliko hata wao walioanza.
Baada ya mwezi mzima, akaamua kukodi gari ambapo akawa na kazi ya kuufuata mchele yeye mwenyewe mkoani Mbeya. Hilo likampa mafanikio makubwa, akaingiza kiasi kikubwa cha pesa na hivyo kuhama Kwa Ally Maua na kuhamia Mwenge ambapo bado aliendelea kufanya biashara zake kama kawaida.
Maisha yalibadilika, akapanga nyumba nzima, akaanzisha biashara nyingine, mafanikio yake yalikuja kwa kasi sana kiasi kwamba akawa anashangaa tu.
Akanunua gari la kwanza katika maisha yake. Aliyafurahia maisha yake, hakutaka kuishi peke yake, alichokifanya ni kumchukua Asha ambaye alibakiza mwezi mmoja kabla ya kujifungua.
Mara kwa mara alikuwa akikutana na marafiki zake, Sultani na Bonge na kwenda kuabudu kama kawaida yao. Maisha yake aliyakabidhi kwa shetani, hakutaka kurudi nyuma kwani kumuabudu shetani kulimpa mafanikio makubwa ambayo hakuwa akitegemea kuyapata.
Baada ya mwaka mmoja wa mafanikio makubwa huku akiwa ametengeneza jina kubwa nchini Tanzania, akapata kipele katika mguu wake wa kushoto. Kilikuwa kidogo na kilichokuwa kikiwasha sana.
Alikikuna, kadiri alivyokuwa akikikuna ndivyo kilivyokuwa kikiongezeka. Kiliendelea kuwa hivyo mpaka alipoamua kwenda hospitalini kuangalia tatizo lilikuwa nini.
“Ni kipele, inaonekana damu imechafuka eneo hili, chukua hizi dawa zitakusaidia,” alisema nesi huku akimpa dawa.
“Nashukuru sana!” alisema Bazoka na kuondoka.
Alipofika nyumbani, kitu cha kwanza kilikuwa ni kumwambia Asha kilichokuwa kimetokea hospitalini kwamba alipewa dawa na hivyo kuanza kuzitumia.
Wakati huo alikuwa na mtoto wa kiume aliyempa jina la Edward, mtoto mzuri ambaye alichukua sura yake, alimpenda, kwake, mtoto huyo alikuwa kila kitu na kila alipokuwa akimuona, alizidi kupambana zaidi na zaidi.
Siku ziliendelea kukatika, kipele kile hakikuacha kuuma, kilimpa maumivu makali, alipewa dawa mbalimbali kwa ajili ya kukitibu lakini hakikuacha kuwasha na kuuma.
Aliendelea kwenda katika hospitali mbalimbali lakini bado matokeo yalikuwa yaleyale, alichokifanya ni kusafiri mpaka nchini Kenya lakini napo huko kukagonga mwamba, kipele kikaiva na kupasuka, kukatokea kidonda kilichokuwa na maumivu makali.
“Tatizo nini lakini?” alijiuliza lakini hakuwa na jibu lolote lile.
Baada ya mwezi mmoja wa maumivu, akaamua kumwambia Sultani kile kilichokuwa kikiendelea, mwanaume huyo akamuita Bonge na kuanza kumwambia kidonda kile kilitokana na utajiri aliokuwanao.
“Unasemaje?” aliuliza Bazoka huku akionekana kushtuka.
“Kadiri kinavyozidi kuongezeka na kuuma ndivyo utajiri wako utakavyokuwa ukiongezeka,” alisema Bonge.
“Kwa maana hiyo hakitopona?”
“Mpaka unaingia kaburini!”
“Kwa nini?”
“Unakumbuka ulivyoambiwa utajiri huo utaambatana na maumivu makali?” aliuliza Sultan.
“Ndiyo! Nakumbuka niliambiwa na mungu wetu!”
“Hayo ndiyo maumivu yenyewe. Hautoweza kupona, kitaendelea kuuma mpaka kifo chako,” alisema Bonge huku akimwangalia Bazoka.
Bazoka alihuzunika, hakuamini kama yale maneno aliyoambiwa na mungu wake ndiyo yangekuwa maumivu ya namna ile.
Ili kumuonyesha hakuwa peke yake, Bonge akavua shati lake, alikuwa na kidonda kikubwa chini ya kwapa lake, kilikuwa kidonda kilichotisha kuliko hata alichokuwanacho.
Bazoka akashtuka, hakutegemea kuona mtu akiwa na kidonda kile halafu akawa mzima na kuzungumza kana kwamba hakukuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea. Alimwangalia mwanaume huyo, kwake, alionekana kuwa jasiri kuliko wanaume wote ndani ya dunia hii.
“Na wewe Sultan?” aliuliza Bazoka huku akimwangalia Sultan.
“Mimi sina kidonda!”
“Una nini?”
“Sitoweza kupata mtoto maisha yangu yote!” alijibu Sultan huku akimwangalia Bazoka.
Hapo ndipo akagundua utajiri ule ulikuwa na maumivu makali mno. Ulikuwa mtamu, alifanya kitu chochote alichokitaka lakini kila siku alipokiangalia kidonda chake, moyo wake ulimuuma mno.
Asha alimpeleka katika hospitali mbalimbali kutibiwa, Bazoka hakuwa akikataa, alikubaliana na Asha lakini hakuwa radhi kumwambia ukweli kile kilichokuwa kikiendelea.
“Kidonda chako kinaonekana kuwa na bakteria wakali ambao kitaalamu wanaitwa Bicorture,” alisema daktari mmoja baada ya kukiangalia kidonda cha Bazoka.
“Na dawa yake?” aliuliza Asha.
“Naomba akatumie hii, nadhani anaweza kupata nafuu na kupona kabisa,” alisema daktari na kuwapa dawa.
Wakaichukua na kuondoka mahali hapo, moyoni mwa Asha aliamini mpenzi wake angeweza kupona kidonda kile lakini Bazooka alifahamu kila kitu na hakutaka kuweka wazi hata kidogo.
Wakarudi nyumbani na kuanza tiba kama alivyoambiwa lakini hakukuwa na mafanikio yoyote yale. Siku ziliendelea kukatika kama kawaida
Biashara zake ziliendelea kumuingizia kiasi kikubwa cha pesa. Akawa bilionea mkubwa na mwenye makamuni mengi, alikuwa na kazi ya kuuza nafaka ambazo alikuwa akizitoa vijijini na kuzipeleka katika masoko makubwa jijini Dar es Salaam.
Alifanikiwa, akanunua nyumba nyingi jijini Dar es Salaam. Yalikuwa ni mafanikio makubwa na ya haraka sana lakini cha ajabu hapakuwa na mtu aliyetilia shaka kwa kile kilichokuwa kikiendelea.
Walimuona mwanaume huyo kuwa mpambanaji, alijua kupambana kwa ajili ya mafanikio yake. Kila siku aliamka asubuhi na mapema na kuwahi kazini hata kabla ya wafanyakazi wake. Hilo likawafanya watu wengi kuona mafanikio yote aliyokuwa akiyapata ni kwa sababu alijitolea kupambana.
Baada ya miaka miwili, akaitwa katika nyumba ile ya ibada na kuambiwa huo ulikuwa muda wa kutoa kafara kwa mungu wao. Kwanza hakuamini, alichojua walimalizana baada ya kupewa kile kidonda.
Aliogopa, hakujua ni kafara ya aina gani alitakiwa kuitoa. Alikuwa radhi kutoa damu ya mnyama au kitu chochote kile lakini si kuua. Hakuona kama kweli mungu wao angewaambia watoe kafara ya mnyama, alichokiona walitakiwa kutoa kafara ya damu ya mtu.
Alikuwa na hofu, alitetemeka kiasi kwamba kijasho chembamba kikaanza kumtoka. Alikuwa na hofu moyoni mwake na kuhisi kabisa huo haukuwa muda mzuri, piga ua kulikuwa na tatizo mbele yake.
“Inakuwaje tena kutoa kafara,” alimuuliza Sultani huku akionekana kushangaa.
“Huo ndiyo utaratibu tuliyowekewa, kila baada ya miaka miwili, kafara inahitajika,” alisema Sultani huku akimwangalia Bazoka, uso wake ulikuwa na tabasamu pana kana kwamba hakukuwa na tatizo lolote lile.
“Lakini si tuna vidonda?”
“Bado haitoshi, suala la kafara lipo palepale,” alijibu mwanaume huyo.
Jibu hilo lilimchosha, alimwangalia Sultani kwa kumkazia macho, alitamani kumsikia akimwambia alikuwa akimtania. Hakutaka kutoa kafara yoyote ile, moyo wake ulimwambia kile kidonda alichokuwanacho ndiyo kilikuwa kafara yenyewe.

Je, nini kitaendelea?
Duuh balaah kubwaa
 
NYEMO CHILONGANI
UTAJIRI WA BILIONEA BAZOKA
0718069269

Sehemu ya 12

Mpelelezi Maganza alisimamisha gari lake maeneo ya Manzese karibu kabisa na nyumba aliyokuwa akiishi Iddi na mkewe, Amina. Kulikuwa na idadi ya watu kadhaa ambao walikuwa wakijadili ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.
Ilikuwa ni siku ya pili, mtoto Yusufu hakuwa amepatikana, kila mmoja alionekana kuguswa na tukio hilo kiasi cha kuonyesha dhahiri kuhitaji kusaidia lakini hawakujua ni kwa namna gani wangetoa msaada huo.
Waliwaambia polisi ambao walisema walikuwa wakilifuatilia kwa ukaribu zaidi, ilikuwa ni lazima ndani ya muda mfupi kugundua ni nani hasa ambaye alifanya utekaji huo na kuondoka na mtoto.
Kwa jinsi Maganza alivyowaangalia watu waliokuwa mahali hapo walionekana kuwa na mawazo tele, waliguswa kwa kile kilichotokea, aliwasalimia na kuelekea ndani ambapo alimkuta Amina akiwa amekaa huku akifarijiwa na wanawake kadhaa waliokuwa humo.
“Poleni sana kwa matatizo!” alisema baada ya kuwasalimia.
“Tunashukuru sana baba!” alijibu mwanamke mmoja.
“Naweza kuzungumza na Amina kidogo?” aliuliza.
“Haina shida!”
Amina akasimama na kuanza kumfuata Maganza ambaye alikwenda pembeni na kusimama. Kabla ya kuzungumza na mwanamke huyo, alimwangalia kwa umakini zaidi, sura yake ilionyesha maumivu makali yaliyokuwa moyoni mwake, alionekana kuvunjika moyo na hakuwa na matumaini hata kidogo.
“Unahisi ni nani alimchukua mtoto wako?” aliuliza Maganza.
“Kwa kweli sijui! Alikuwa akicheza na marafiki zake, halafu ghafla akapotea!” alijibu.
“Alikuwa akicheza nao wapi?”
“Uwanjani!”
“Hapakuwa na mtu aliyekuja kumchukua?” aliuliza huku akiwa makini kabisa.
“Yaani sifahamu ila inasemekana kuna mtoto mmoja alimuona mwanaume aliyemchukua!” alijibu.
“Mtoto gani?”
“Anaitwa Hussein!” alijibu.
Alichotaka Maganza ni kuzungumza na huyo mtoto, ilikuwa ni lazima apate mwanga wa pa kuanzia kumtafuta mtu ambaye alimteka mtoto huyo na kupotea naye.
Alimuuliza alipokuwa akiishi, akaambiwa na kwenda huko, alipofika, alikutana na wazazi wake na kuanza kuzungumza nao, aliwaambia alichoambiwa na Amina hivyo ilikuwa ni lazima kumuuliza mtoto huyo maswali kadhaa.
“Eti nani alimchukua rafki yako?” alimuuliza Hussein.
“Kuna kaka alikuja, alikuwa ndani ya gari, akamchukua,” alijibu mtoto huyo.
“Wakati yeye anamchukua wewe ulikuwa wapi?”
“Alinituma dukani. Basi nikaenda, niliporudi nikaona wanaondoka,” alijibu.
“Walikuwa wakitembea?”
“Walikuwa ndani ya gari!”
“Gari gani?”
“Kama ya mzee Setebe!” alijibu.
Maganza akawageukia wazazi wa mtoto yule.
“Hilo gari la mzee Setebe ni la aina gani?” aliuliza.
“Noah!”
Akamgeukia Hussein.
“Lilikuwa na rangi gani?”
“Nyeupe...gari nzuriiiiiiii...” alijibu.
“Sawa.”
Kidogo Maganza akapata mahali pa kuanzia, hapo ilionyesha kuwa mtoto Yusufu alitekwa na mwanaume aliyekuwa na gari aina ya Noah nyeupe na kutokomea zake, kwenye uchunguzi huo ilikuwa ni lazima kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha anampata mwanaume huyo.
Kwa jiji kama la Dar es Salaam kulikuwa na magari mengi kama hayo hivyo ilikuwa ni vigumu kugundua kwamba hili ndilo ambalo lilihusika kwenye utekaji ama la.
Alichokifanya ni kupiga simu kwenye vituo mbalimbali ndani ya jiji na hata mikoa mingine na kuwaambia kuhusu gari hilo, ilikuwa ni lazima ipatikane kwa kuwa ndilo lililokuwa limembeba mtoto huyo na kutokomea zake.
Walichoongezewa ni kupekua kila gari ambalo lingepita kwenda kwenye mikoa mingine, Yusufu alikuwa ni albino hivyo walitakiwa kuhakikisha magari yote hayo yanapekuliwa na kuangaliwa ndani.
Baada ya kumaliza, akaondoka na kuelekea kule uwanjani ambapo kulikuwa na watu waliokuwa wafanya mazoezi na kuangalia mazingira ya hapo. Alikuwa na uhakika wakati tukio lilipotokea ilikuwa ni lazima baadhi ya watu wawe wameliona lakini hawakutulia shaka yoyote ile.
Ndivyo inavyokuwa, mahali popote pale ambapo kunakuwa na tukio fulani ni lazima watu walione lakini wanakuwa hawajalitolea macho mpaka pale ambapo wangeulizwa kuhusu tukio hilo lilikuwa muhimu kiasi gani.
Hilo ndilo lililomfanya kulisogelea duka moja lililokuwa pembeni na uwanja huo na kuhitaji kuzungumza na muuza duka. Alihitaji muda wake wa dakika kama kumi, muuza duka akakataa kwa kuwa alikuwa bize, hakumtolea kitambulisho, alichomuuliza, ndani ya dakika kumi alikuwa na uwezo wa kutengeneza kiasi gani?
“Elfu tatu!” alijibu. Akamgawia na kuomba kumuuliza baadhi ya maswali, hivyo akakubali.
Wakakaa na kuanza kuongea, alichomuuliza ni kuhusu lile gari aina ya Noah ambalo siku iliyopita lilifika hapo uwanjani majira ya jioni, yeye kama muuza duka alikuwa na uhakika aliliona gari hilo, alihitaji kujua zaidi.
“Noah?” aliuliza huku akionekana kujifikiria.
“Ndiyo! Ilikuwa nyeupe, uliiona mahali hapa?” aliuliza Maganza huku akimwangalia.
“Kwa jana?”
“Ndiyo!”
“Kama nililiona! Unasema lilisimama wapi?”
“Sijajua! Ila nahisi ni maeneo ya hapa karibu!”
“Yeah! Nakumbuka nililiona...Ilikuwa Noah nadhani, ilisimama pale mbele!” alijibu huku akionekana kukumbuka zaidi.
“Baada ya kusimama, unachokumbuka kuna mtu aliteremka?”
“Hapana! Ila kulikuwa na mtoto aliingia, alikuwa albino hivi! Halafu nilishangaa, nakumbuka nilikuwa na Lyimo hapa, tena tukawa tunaulizana ilikuwaje? Ama jamaa alikuwa akimteka...halafu tukacheka sana tulijiona wajinga, utekaji gani ufanyike wazi namna hiyo, tukapuuzia....kwani kuna nini bro?” alielezea muuza duka huyo na kuuliza.
“Huyu albino alitekwa!”
“Na nani? Yule mwenye Noah?” aliuliza.
“Yeah! Ndiye aliyemteka! Unasema kwamba hukumuona mwanaume akishuka?”
“Hapana! Sikumuona kabisa.”
“Na ulibahatika kuona hata namba za gari?”
“Hapana! Ila nakumbuka namba ilikuwa D,” alijibu.
Maganza alizungumza naye kwa dakika kadhaa baada ya kumaliza, akaomba kuondoka, akiwa amekwishampa kisogo, muuza duka akamuita na kumuongezea jingine. Alichomwambia ni kwamba siku iliyopita kulikuwa na mechi hapo hivyo kulikuwa na jamaa alikuwa akiirusha mechi hiyo kwenye Mtandao wake wa Youtube, hivyo ilikuwa ni lazima amtafute kama kweli alitaka kuliona hilo gari.
“Sasa atakuwa alilipiga picha kwa video?” aliuliza.
“Yaani kwa mahali liliposimama, ilikuwa ni lazima lionekane,” alisema kijana huyo.
Maganza akakubaliana naye na hivyo kumuomba namba ya huyo jamaa aliyeitwa kwa jina la Stefano. Na kweli akawasiliana naye na mwanaume huyo kumwambia ni kweli alipiga video, mbali na mechi hiyo pia alilipiga picha gari hilo, yaani lilionekana kabisa.
“Nataka kuja kuona hiyo video!”
“Haina noma. Njoo home,” alisema na kuanza kumuelekeza.
Ni ndani ya dakika kadhaa, Maganza akafika nyumbani kwa Stefano na kuanza kuongea naye, alichomwambia ni kutaka kuna hiyo video, alihitaji kuliona gari hilo kwani lilifanya utekaji mahali hapo.
Halikuwa tatizo, haraka sana kijana huyo akamuwekea video hiyo na kuanza kuangalia. Maganza aliitolea macho, aliangalia video nzima, tena kwa uangalifu kabisa, kitu cha ajabu kilichomshangaza, si yeye tu bali hata Stefano mwenyewe, gari lile halikuonekana hata kidogo kwenye hiyo video.
“Sasa mbona hakuna hilo gari?” aliuliza Maganza.
“Nashangaa! Gari lilikuwepo, tena jana nilipokuwa naiangalia video, nilijisemea hili gari limependezesha mechi kishenzi, sasa nashangaa eti sasa hivi halionekani!” alisema Stefano.
“Una uhakika ulilipiga picha?”
“Ndiyo! Tena kwa karibu zaidi.”
“Sasa mbona silioni? Au uliedit picha kipande cha gari ukafuta?” aliuliza Maganza huku akionekana kushangaa.
“Kaka sijaanza kuedit, nilipanga niifanye kazi hiyo leo usiku!” alijibu kijana huyo huku akionekana kuwa na uhakika na alichokisema.
“Sasa gari liko wapi?”
“Hata mimi nashangaa!”

JE, nini kitaendelea?
 
NYEMO CHILONGANI
UCHAWI WA BILIONEA BAZOKA
SEHEMU YA 13

Mtu ambaye alimtaka kwa udi na uvumba alimuona, alikuwa Bibi Semeni ambaye kwa stori za mtaani hapo aliambiwa alikuwa mwanamke mchawi, aliyeogopwa kila kona.
Hakutaka kukubali, hapakuwa na kitu ambacho Bazoka alikuwa akikiamini kama uchawi aliokuwa akiutumia, ulikuwa mkubwa, kutoka kuzimu ambapo aliamini kwa mwanamke huyo hakuwa amefika huko.
Ilikuwa ni lazima kummaliza kwa kuwa alihitaji sana kufanikiwa zaidi kwenye mambo yake. Aliwaambia wenzake, yaani Bonge na Sultani kuhusu Bibi Semeni, jinsi alivyokuwa akisifika kwa uchawi, walichomwambia ni kuwa alitakiwa kuhakikisha anammaliza kwani kwa uchawi waliokuwa wakiutumia ulikuwa mkubwa mno.
Ili kumpata mwanamke huyo ilikuwa ni lazima awe anakwenda huk kumuona, ilikuwa ni lazima kuomba naye ukaribu lakini mwisho wa siku afanikiwe kwa kile alichokuwa akikitaka.
Alihitaji kufahamu mengi kuhusu Bi. Semeni hivyo alitakiwa kuongeza ukaribu wake na Frank ambaye ndiye angemwambia mengi kuhusu mwanamke huyo. Kwa jinsi alivyokuwa akimuuliza, hata Frank mwenyewe alishangaa, hakuamini mtu kama Bazoka angehitaji kufahamu mengi kuhusu mwanamke huyo, alikuwa mchawi, mtu aliyeogopwa na watu wote katika mtaa huo, sasa kwa sababu gani alitaka kumfahamu zaidi mwanamke huyo?
“Kwani wewe wa nini?” aliuliza Frank, macho yake yalikuwa yakimshangaa Bazoka.
“Ninataka nimzoee, nahisi anaweza kunisaidia mengi tu hapo baadaye, si unajua mambo yetu ya upande wa pili haya,” alimjibu huku akijitahidi kuonyesha tabasamu kumdanganya Frank kwaba kila kilikuwa sawa kabisa.
“Yule bibi mchawi sana!”
“Umejuaje? Huwezi kumuita mtu mchawi kama wewe si mchawi,” alimwambia.
“Aliwahi kuniroga, alimuwangia sana mke wangu!” alimjibu.
“Na una uhakika gani kwamba yeye ndiye alifanya hivyo?” alimuuliza, alihitaji kujua ukweli.
“Nilikwenda kwake!”
“Kufanya nini?”
“Kuweka dawa, aisee nilichokutana nacho sikuamini macho yangu,” alimwambia.
“Ulikutana na nini?”
“Makaburi!”
“Makaburi?”
“Ndiyo! Nilikutana na makaburi, tena yakiwa kwenye eneo la nyumba yake, unaweza kuamini hilo?” alijibu na kuuliza kwa mshangao.
Bazoka alikaa kimya huku akimwangalia Frank, kwa yale aliyomwambia yalionyesha jinsi bibi huyo alivyokuwa hatari kwenye mambo ya ulozi lakini hakutaka kuacha, ilikuwa ni lazima afanye kila linalowezekana kuhakikisha anaonana na mwanamke huyo, amzoee lakini mwisho wa siku amuue kama alivyotaka kufanya.
Kwa kuwa ilikuwa ni mchana, akaondoka nyumbani kwa Frank na kuelekea kwa Bi. Semeni, alipoingia kwenye uwanja huo tu, kila mtu aliyekuwa jirani akaanza kumwangalia, hapakuwa na aliyeamini kama kweli kungekuwa na mtu ambaye angeingia ndani ya eneo la nyumba hiyo, bibi huyo alitisha, alikuwa mtu hatari ambaye hakutakiwa hata kusogelewa, sasa ilikuwaje mwanaume huyo aingie ndani ya nyumba hiyo na kujiaminisha kabisa.
Bazoka akaanza kuusogelea mlango, alipoufikia, akagonga, baada ya dakika kama moja, ukafunguliwa na Bi. Semeni ambaye alimshangaa Bazoka, hakuwahi kupokea ugeni, ndugu zake, marafiki zake wote walimtenga kwa kuwa alikuwa mchawi, sasa huyo alihitaji nini?
Inawezekana alitaka kupanga chumba lakini pia alijua kila mtu aliyetaka kwenda kupanga hapo kabla ya kuifikia nyumba hiyo, aliwahiwa na majirani na kuambiwa asiende kupanga kwa kuwa alikuwa mchawi, sasa huyo mwanaume alihitaji nini?
“Karibu!” alimkaribisha nyumbani hapo.
“Naruhusiwa kuingia ndani?” aliuliza.
“Unahitaji nini?”
“Kuzungumza na wewe!” alijibu.
“Kuhusu nini?”
“Kwanza ningeingia ndani,” alimwambia.
Kwa Bi. Semeni hapakuwa na tatizo, akamkaribisha mpaka ndani, akaingia huku akiangalia mandhari ya nyumba hiyo, alijifanya kuwa rafiki lakini upande wa pili kulikuwa na kitu alichokuwa akihitaji.
Ilikuwa ni lazima kujenga urafiki mkubwa na mwanamke huyo, amwamini lakini mwisho wa siku akamilishe kile alichokuwa akikihitaji, kwenye kufikiria hayo yote, akapata jibu kwamba ili awe karibu naye zaidi ilikuwa ni lazima amwambie alihitaji chumba na aliambiwa aende katika nyumba ile.
Hilo likaonekana kufaa na kumwambia mwanamke huyo. Bi. Semeni alishangaa, ilikuwa kirahisi mno, alimwambia Bazoka kwa jinsi alivyokuwa na wasiwasi kwamba kweli alihitaji chumba ama kulikuwa na jambo jingine, akamsisitizia ni kweli alihitaji chumba.
“Nimehangaika sana! Tena sana mama yangu!” alimwambia huku akimwangalia.
“Nani alikuelekeza hapa?”
“Kuna mwanaume nilionana naye hapo mtaa wa nyuma, cha ajabu kila dalali niliyemtaka anilete kwenye nyumba hii nzuri, alikataa,” alimwambia.
“Hukuuliza kwa nini walikataa?”
“Sikuuliza! Labda uniambie wewe!” alimwambia.
Bi. Semeni akatoa tabasamu la mbali kabisa huku akimwangalia Bazoka, alihisi kabisa alikuwa akidanganywa na mwanaume huyo, kulikuwa na jambo jingine ambalo hakutaka kumwambia, alihitaji kulifahamu jambo hilo, lilikuwa ni lipi hasa?
Haikuwa kawaida kuja tu kutoka huko ulipokuwa na kwenda nyumbani hapo, eti ulihitaji chumba, nani alikwambia kulikuwa na chumba? Alihitaji kufahamu mengi.
Bazoka alipoona mwanamke huyo anakuwa na hofu sana, akaamua kumdanganya kuwa alihitaji sana kukaa karibu na mke wake, walipendana lakini kwa kipindi hicho waligombana kwa kuwa hakuwa akimwamini.
Nyumbani kwake kulikuwa kama jehanamu, muda wote walikuwa wakigombana, alipotoka kazini na kwenda nyumbani hapo, hakuwa akipata furaha, alikutana na maneno makubwa na malalamiko kutoka kwa mkewe, hivyo aliamua kuondoka nyumbani hapo na kwenda kupanga.
“Unaishi wapi?” aliuliza Bi. Semeni.
“Kijitonyama!”
Walizungumza kwa dakika kadhaa na mwisho kabisa Bi. Semeni akakubali kumpangisha chumba mwanaume huyo, hakuwa amemjua, hakujua lengo lake lakini kwa kuwa alijiamini alikuwa mchawi, basi hakuhofu kama mtu huyo angembabaisha kwa lolote lile.
Siku hiyohiyo Bazoka akaenda kununua baadhi ya vitu vya ndani na kuviingiza, kila mtu aliyekuwa akimuona alishangaa, ilikuwa ajiamini kwenda kuishi ndani ya nyumba hiyo? Tena kwa mwanamke mshirikina kama alivyokuwa Bi. Semeni, hakika kila mtu akataka kufahamu ni kwa namna gani mwanaume huyo alikuwa amechanganyikiwa.
“Sitokuwa nalala siku zote, mara chache nitakuwa nakuja kulala hapa,” alisema Bazoka.
“Haina shida.”
“Ila kwa wiki hii nitalala siku zote, nitamwambia nimesafiri! Hizi ndoa zina majanga sana,” alisema Bazoka na kucheka kidogo.
Siku hiyohiyo Bazoka akarudi nyumbani kwake na kuzungumza na mke wake, alichomwambia ni kuwa alipata safari ya Ghafla kuelekea nchini Uganda hivyo alitakiwa kuondoka siku hiyohiyo kwani kulikuwa na mambo yake alikuwa akienda kuyarekebisha.
Mkewe hakuwa na tatizo hata kidogo, hakuwahi kumfumania mume wake ama hata kuhisi kwa lolote lile, alikuwa mwanaume mwamifu sana, akakubaliana naye na kuondoka zake, safari yake iliishia Magomeni ndani ya chumba chake kipya.
Mpaka muda huo bado Bi. Semeni hakuwa akiamini kama kweli mpangaji wake aliyekuwa kupanga kwake alikuja kupanga kama wapangaji wengine kwenye nyumba nyingine ama kulikuwa na kitu.
Alitaka kujua kama kulikuwa na kitu ni kitu gani lakini hakupata jibu kabisa. Akaamua kukubaliana naye ila kama ilivyokuwa hata kwa wachawi mwengine ilikuwa ni lazima kumjaribu usiku kuona kama alikuwa na kinga yoyote ile.
Alijipanga vilivyo, alicheka mbele ya macho ya Bazoka lakini moyoni mwake alipanga mambo yake kwa lengo la kuhakikisha anafanya lolote lile kuhakikisha anamloga kijana huyo, amtingishe kwanza ili kuuona uwezo wake.
“Nitaanza kazi hiyo leo,” alisema Bi. Semeni, moyo wake ulikuwa na kiu kubwa kuhakikisha anamloga Bazoka usiku huo.Mtu ambaye alimtaka kwa udi na uvumba alimuona, alikuwa Bibi Semeni ambaye kwa stori za mtaani hapo aliambiwa alikuwa mwanamke mchawi, aliyeogopwa kila kona.
Hakutaka kukubali, hapakuwa na kitu ambacho Bazoka alikuwa akikiamini kama uchawi aliokuwa akiutumia, ulikuwa mkubwa, kutoka kuzimu ambapo aliamini kwa mwanamke huyo hakuwa amefika huko.
Ilikuwa ni lazima kummaliza kwa kuwa alihitaji sana kufanikiwa zaidi kwenye mambo yake. Aliwaambia wenzake, yaani Bonge na Sultani kuhusu Bibi Semeni, jinsi alivyokuwa akisifika kwa uchawi, walichomwambia ni kuwa alitakiwa kuhakikisha anammaliza kwani kwa uchawi waliokuwa wakiutumia ulikuwa mkubwa mno.
Ili kumpata mwanamke huyo ilikuwa ni lazima awe anakwenda huk kumuona, ilikuwa ni lazima kuomba naye ukaribu lakini mwisho wa siku afanikiwe kwa kile alichokuwa akikitaka.
Alihitaji kufahamu mengi kuhusu Bi. Semeni hivyo alitakiwa kuongeza ukaribu wake na Frank ambaye ndiye angemwambia mengi kuhusu mwanamke huyo. Kwa jinsi alivyokuwa akimuuliza, hata Frank mwenyewe alishangaa, hakuamini mtu kama Bazoka angehitaji kufahamu mengi kuhusu mwanamke huyo, alikuwa mchawi, mtu aliyeogopwa na watu wote katika mtaa huo, sasa kwa sababu gani alitaka kumfahamu zaidi mwanamke huyo?
“Kwani wewe wa nini?” aliuliza Frank, macho yake yalikuwa yakimshangaa Bazoka.
“Ninataka nimzoee, nahisi anaweza kunisaidia mengi tu hapo baadaye, si unajua mambo yetu ya upande wa pili haya,” alimjibu huku akijitahidi kuonyesha tabasamu kumdanganya Frank kwaba kila kilikuwa sawa kabisa.
“Yule bibi mchawi sana!”
“Umejuaje? Huwezi kumuita mtu mchawi kama wewe si mchawi,” alimwambia.
“Aliwahi kuniroga, alimuwangia sana mke wangu!” alimjibu.
“Na una uhakika gani kwamba yeye ndiye alifanya hivyo?” alimuuliza, alihitaji kujua ukweli.
“Nilikwenda kwake!”
“Kufanya nini?”
“Kuweka dawa, aisee nilichokutana nacho sikuamini macho yangu,” alimwambia.
“Ulikutana na nini?”
“Makaburi!”
“Makaburi?”
“Ndiyo! Nilikutana na makaburi, tena yakiwa kwenye eneo la nyumba yake, unaweza kuamini hilo?” alijibu na kuuliza kwa mshangao.
Bazoka alikaa kimya huku akimwangalia Frank, kwa yale aliyomwambia yalionyesha jinsi bibi huyo alivyokuwa hatari kwenye mambo ya ulozi lakini hakutaka kuacha, ilikuwa ni lazima afanye kila linalowezekana kuhakikisha anaonana na mwanamke huyo, amzoee lakini mwisho wa siku amuue kama alivyotaka kufanya.
Kwa kuwa ilikuwa ni mchana, akaondoka nyumbani kwa Frank na kuelekea kwa Bi. Semeni, alipoingia kwenye uwanja huo tu, kila mtu aliyekuwa jirani akaanza kumwangalia, hapakuwa na aliyeamini kama kweli kungekuwa na mtu ambaye angeingia ndani ya eneo la nyumba hiyo, bibi huyo alitisha, alikuwa mtu hatari ambaye hakutakiwa hata kusogelewa, sasa ilikuwaje mwanaume huyo aingie ndani ya nyumba hiyo na kujiaminisha kabisa.
Bazoka akaanza kuusogelea mlango, alipoufikia, akagonga, baada ya dakika kama moja, ukafunguliwa na Bi. Semeni ambaye alimshangaa Bazoka, hakuwahi kupokea ugeni, ndugu zake, marafiki zake wote walimtenga kwa kuwa alikuwa mchawi, sasa huyo alihitaji nini?
Inawezekana alitaka kupanga chumba lakini pia alijua kila mtu aliyetaka kwenda kupanga hapo kabla ya kuifikia nyumba hiyo, aliwahiwa na majirani na kuambiwa asiende kupanga kwa kuwa alikuwa mchawi, sasa huyo mwanaume alihitaji nini?
“Karibu!” alimkaribisha nyumbani hapo.
“Naruhusiwa kuingia ndani?” aliuliza.
“Unahitaji nini?”
“Kuzungumza na wewe!” alijibu.
“Kuhusu nini?”
“Kwanza ningeingia ndani,” alimwambia.
Kwa Bi. Semeni hapakuwa na tatizo, akamkaribisha mpaka ndani, akaingia huku akiangalia mandhari ya nyumba hiyo, alijifanya kuwa rafiki lakini upande wa pili kulikuwa na kitu alichokuwa akihitaji.
Ilikuwa ni lazima kujenga urafiki mkubwa na mwanamke huyo, amwamini lakini mwisho wa siku akamilishe kile alichokuwa akikihitaji, kwenye kufikiria hayo yote, akapata jibu kwamba ili awe karibu naye zaidi ilikuwa ni lazima amwambie alihitaji chumba na aliambiwa aende katika nyumba ile.
Hilo likaonekana kufaa na kumwambia mwanamke huyo. Bi. Semeni alishangaa, ilikuwa kirahisi mno, alimwambia Bazoka kwa jinsi alivyokuwa na wasiwasi kwamba kweli alihitaji chumba ama kulikuwa na jambo jingine, akamsisitizia ni kweli alihitaji chumba.
“Nimehangaika sana! Tena sana mama yangu!” alimwambia huku akimwangalia.
“Nani alikuelekeza hapa?”
“Kuna mwanaume nilionana naye hapo mtaa wa nyuma, cha ajabu kila dalali niliyemtaka anilete kwenye nyumba hii nzuri, alikataa,” alimwambia.
“Hukuuliza kwa nini walikataa?”
“Sikuuliza! Labda uniambie wewe!” alimwambia.
Bi. Semeni akatoa tabasamu la mbali kabisa huku akimwangalia Bazoka, alihisi kabisa alikuwa akidanganywa na mwanaume huyo, kulikuwa na jambo jingine ambalo hakutaka kumwambia, alihitaji kulifahamu jambo hilo, lilikuwa ni lipi hasa?
Haikuwa kawaida kuja tu kutoka huko ulipokuwa na kwenda nyumbani hapo, eti ulihitaji chumba, nani alikwambia kulikuwa na chumba? Alihitaji kufahamu mengi.
Bazoka alipoona mwanamke huyo anakuwa na hofu sana, akaamua kumdanganya kuwa alihitaji sana kukaa karibu na mke wake, walipendana lakini kwa kipindi hicho waligombana kwa kuwa hakuwa akimwamini.
Nyumbani kwake kulikuwa kama jehanamu, muda wote walikuwa wakigombana, alipotoka kazini na kwenda nyumbani hapo, hakuwa akipata furaha, alikutana na maneno makubwa na malalamiko kutoka kwa mkewe, hivyo aliamua kuondoka nyumbani hapo na kwenda kupanga.
“Unaishi wapi?” aliuliza Bi. Semeni.
“Kijitonyama!”
Walizungumza kwa dakika kadhaa na mwisho kabisa Bi. Semeni akakubali kumpangisha chumba mwanaume huyo, hakuwa amemjua, hakujua lengo lake lakini kwa kuwa alijiamini alikuwa mchawi, basi hakuhofu kama mtu huyo angembabaisha kwa lolote lile.
Siku hiyohiyo Bazoka akaenda kununua baadhi ya vitu vya ndani na kuviingiza, kila mtu aliyekuwa akimuona alishangaa, ilikuwa ajiamini kwenda kuishi ndani ya nyumba hiyo? Tena kwa mwanamke mshirikina kama alivyokuwa Bi. Semeni, hakika kila mtu akataka kufahamu ni kwa namna gani mwanaume huyo alikuwa amechanganyikiwa.
“Sitokuwa nalala siku zote, mara chache nitakuwa nakuja kulala hapa,” alisema Bazoka.
“Haina shida.”
“Ila kwa wiki hii nitalala siku zote, nitamwambia nimesafiri! Hizi ndoa zina majanga sana,” alisema Bazoka na kucheka kidogo.
Siku hiyohiyo Bazoka akarudi nyumbani kwake na kuzungumza na mke wake, alichomwambia ni kuwa alipata safari ya Ghafla kuelekea nchini Uganda hivyo alitakiwa kuondoka siku hiyohiyo kwani kulikuwa na mambo yake alikuwa akienda kuyarekebisha.
Mkewe hakuwa na tatizo hata kidogo, hakuwahi kumfumania mume wake ama hata kuhisi kwa lolote lile, alikuwa mwanaume mwamifu sana, akakubaliana naye na kuondoka zake, safari yake iliishia Magomeni ndani ya chumba chake kipya.
Mpaka muda huo bado Bi. Semeni hakuwa akiamini kama kweli mpangaji wake aliyekuwa kupanga kwake alikuja kupanga kama wapangaji wengine kwenye nyumba nyingine ama kulikuwa na kitu.
Alitaka kujua kama kulikuwa na kitu ni kitu gani lakini hakupata jibu kabisa. Akaamua kukubaliana naye ila kama ilivyokuwa hata kwa wachawi mwengine ilikuwa ni lazima kumjaribu usiku kuona kama alikuwa na kinga yoyote ile.
Alijipanga vilivyo, alicheka mbele ya macho ya Bazoka lakini moyoni mwake alipanga mambo yake kwa lengo la kuhakikisha anafanya lolote lile kuhakikisha anamloga kijana huyo, amtingishe kwanza ili kuuona uwezo wake.
“Nitaanza kazi hiyo leo,” alisema Bi. Semeni, moyo wake ulikuwa na kiu kubwa kuhakikisha anamloga Bazoka usiku huo.
Mtu ambaye alimtaka kwa udi na uvumba alimuona, alikuwa Bibi Semeni ambaye kwa stori za mtaani hapo aliambiwa alikuwa mwanamke mchawi, aliyeogopwa kila kona.
Hakutaka kukubali, hapakuwa na kitu ambacho Bazoka alikuwa akikiamini kama uchawi aliokuwa akiutumia, ulikuwa mkubwa, kutoka kuzimu ambapo aliamini kwa mwanamke huyo hakuwa amefika huko.
Ilikuwa ni lazima kummaliza kwa kuwa alihitaji sana kufanikiwa zaidi kwenye mambo yake. Aliwaambia wenzake, yaani Bonge na Sultani kuhusu Bibi Semeni, jinsi alivyokuwa akisifika kwa uchawi, walichomwambia ni kuwa alitakiwa kuhakikisha anammaliza kwani kwa uchawi waliokuwa wakiutumia ulikuwa mkubwa mno.
Ili kumpata mwanamke huyo ilikuwa ni lazima awe anakwenda huk kumuona, ilikuwa ni lazima kuomba naye ukaribu lakini mwisho wa siku afanikiwe kwa kile alichokuwa akikitaka.
Alihitaji kufahamu mengi kuhusu Bi. Semeni hivyo alitakiwa kuongeza ukaribu wake na Frank ambaye ndiye angemwambia mengi kuhusu mwanamke huyo. Kwa jinsi alivyokuwa akimuuliza, hata Frank mwenyewe alishangaa, hakuamini mtu kama Bazoka angehitaji kufahamu mengi kuhusu mwanamke huyo, alikuwa mchawi, mtu aliyeogopwa na watu wote katika mtaa huo, sasa kwa sababu gani alitaka kumfahamu zaidi mwanamke huyo?
“Kwani wewe wa nini?” aliuliza Frank, macho yake yalikuwa yakimshangaa Bazoka.
“Ninataka nimzoee, nahisi anaweza kunisaidia mengi tu hapo baadaye, si unajua mambo yetu ya upande wa pili haya,” alimjibu huku akijitahidi kuonyesha tabasamu kumdanganya Frank kwaba kila kilikuwa sawa kabisa.
“Yule bibi mchawi sana!”
“Umejuaje? Huwezi kumuita mtu mchawi kama wewe si mchawi,” alimwambia.
“Aliwahi kuniroga, alimuwangia sana mke wangu!” alimjibu.
“Na una uhakika gani kwamba yeye ndiye alifanya hivyo?” alimuuliza, alihitaji kujua ukweli.
“Nilikwenda kwake!”
“Kufanya nini?”
“Kuweka dawa, aisee nilichokutana nacho sikuamini macho yangu,” alimwambia.
“Ulikutana na nini?”
“Makaburi!”
“Makaburi?”
“Ndiyo! Nilikutana na makaburi, tena yakiwa kwenye eneo la nyumba yake, unaweza kuamini hilo?” alijibu na kuuliza kwa mshangao.
Bazoka alikaa kimya huku akimwangalia Frank, kwa yale aliyomwambia yalionyesha jinsi bibi huyo alivyokuwa hatari kwenye mambo ya ulozi lakini hakutaka kuacha, ilikuwa ni lazima afanye kila linalowezekana kuhakikisha anaonana na mwanamke huyo, amzoee lakini mwisho wa siku amuue kama alivyotaka kufanya.
Kwa kuwa ilikuwa ni mchana, akaondoka nyumbani kwa Frank na kuelekea kwa Bi. Semeni, alipoingia kwenye uwanja huo tu, kila mtu aliyekuwa jirani akaanza kumwangalia, hapakuwa na aliyeamini kama kweli kungekuwa na mtu ambaye angeingia ndani ya eneo la nyumba hiyo, bibi huyo alitisha, alikuwa mtu hatari ambaye hakutakiwa hata kusogelewa, sasa ilikuwaje mwanaume huyo aingie ndani ya nyumba hiyo na kujiaminisha kabisa.
Bazoka akaanza kuusogelea mlango, alipoufikia, akagonga, baada ya dakika kama moja, ukafunguliwa na Bi. Semeni ambaye alimshangaa Bazoka, hakuwahi kupokea ugeni, ndugu zake, marafiki zake wote walimtenga kwa kuwa alikuwa mchawi, sasa huyo alihitaji nini?
Inawezekana alitaka kupanga chumba lakini pia alijua kila mtu aliyetaka kwenda kupanga hapo kabla ya kuifikia nyumba hiyo, aliwahiwa na majirani na kuambiwa asiende kupanga kwa kuwa alikuwa mchawi, sasa huyo mwanaume alihitaji nini?
“Karibu!” alimkaribisha nyumbani hapo.
“Naruhusiwa kuingia ndani?” aliuliza.
“Unahitaji nini?”
“Kuzungumza na wewe!” alijibu.
“Kuhusu nini?”
“Kwanza ningeingia ndani,” alimwambia.
Kwa Bi. Semeni hapakuwa na tatizo, akamkaribisha mpaka ndani, akaingia huku akiangalia mandhari ya nyumba hiyo, alijifanya kuwa rafiki lakini upande wa pili kulikuwa na kitu alichokuwa akihitaji.
Ilikuwa ni lazima kujenga urafiki mkubwa na mwanamke huyo, amwamini lakini mwisho wa siku akamilishe kile alichokuwa akikihitaji, kwenye kufikiria hayo yote, akapata jibu kwamba ili awe karibu naye zaidi ilikuwa ni lazima amwambie alihitaji chumba na aliambiwa aende katika nyumba ile.
Hilo likaonekana kufaa na kumwambia mwanamke huyo. Bi. Semeni alishangaa, ilikuwa kirahisi mno, alimwambia Bazoka kwa jinsi alivyokuwa na wasiwasi kwamba kweli alihitaji chumba ama kulikuwa na jambo jingine, akamsisitizia ni kweli alihitaji chumba.
“Nimehangaika sana! Tena sana mama yangu!” alimwambia huku akimwangalia.
“Nani alikuelekeza hapa?”
“Kuna mwanaume nilionana naye hapo mtaa wa nyuma, cha ajabu kila dalali niliyemtaka anilete kwenye nyumba hii nzuri, alikataa,” alimwambia.
“Hukuuliza kwa nini walikataa?”
“Sikuuliza! Labda uniambie wewe!” alimwambia.
Bi. Semeni akatoa tabasamu la mbali kabisa huku akimwangalia Bazoka, alihisi kabisa alikuwa akidanganywa na mwanaume huyo, kulikuwa na jambo jingine ambalo hakutaka kumwambia, alihitaji kulifahamu jambo hilo, lilikuwa ni lipi hasa?
Haikuwa kawaida kuja tu kutoka huko ulipokuwa na kwenda nyumbani hapo, eti ulihitaji chumba, nani alikwambia kulikuwa na chumba? Alihitaji kufahamu mengi.
Bazoka alipoona mwanamke huyo anakuwa na hofu sana, akaamua kumdanganya kuwa alihitaji sana kukaa karibu na mke wake, walipendana lakini kwa kipindi hicho waligombana kwa kuwa hakuwa akimwamini.
Nyumbani kwake kulikuwa kama jehanamu, muda wote walikuwa wakigombana, alipotoka kazini na kwenda nyumbani hapo, hakuwa akipata furaha, alikutana na maneno makubwa na malalamiko kutoka kwa mkewe, hivyo aliamua kuondoka nyumbani hapo na kwenda kupanga.
“Unaishi wapi?” aliuliza Bi. Semeni.
“Kijitonyama!”
Walizungumza kwa dakika kadhaa na mwisho kabisa Bi. Semeni akakubali kumpangisha chumba mwanaume huyo, hakuwa amemjua, hakujua lengo lake lakini kwa kuwa alijiamini alikuwa mchawi, basi hakuhofu kama mtu huyo angembabaisha kwa lolote lile.
Siku hiyohiyo Bazoka akaenda kununua baadhi ya vitu vya ndani na kuviingiza, kila mtu aliyekuwa akimuona alishangaa, ilikuwa ajiamini kwenda kuishi ndani ya nyumba hiyo? Tena kwa mwanamke mshirikina kama alivyokuwa Bi. Semeni, hakika kila mtu akataka kufahamu ni kwa namna gani mwanaume huyo alikuwa amechanganyikiwa.
“Sitokuwa nalala siku zote, mara chache nitakuwa nakuja kulala hapa,” alisema Bazoka.
“Haina shida.”
“Ila kwa wiki hii nitalala siku zote, nitamwambia nimesafiri! Hizi ndoa zina majanga sana,” alisema Bazoka na kucheka kidogo.
Siku hiyohiyo Bazoka akarudi nyumbani kwake na kuzungumza na mke wake, alichomwambia ni kuwa alipata safari ya Ghafla kuelekea nchini Uganda hivyo alitakiwa kuondoka siku hiyohiyo kwani kulikuwa na mambo yake alikuwa akienda kuyarekebisha.
Mkewe hakuwa na tatizo hata kidogo, hakuwahi kumfumania mume wake ama hata kuhisi kwa lolote lile, alikuwa mwanaume mwamifu sana, akakubaliana naye na kuondoka zake, safari yake iliishia Magomeni ndani ya chumba chake kipya.
Mpaka muda huo bado Bi. Semeni hakuwa akiamini kama kweli mpangaji wake aliyekuwa kupanga kwake alikuja kupanga kama wapangaji wengine kwenye nyumba nyingine ama kulikuwa na kitu.
Alitaka kujua kama kulikuwa na kitu ni kitu gani lakini hakupata jibu kabisa. Akaamua kukubaliana naye ila kama ilivyokuwa hata kwa wachawi mwengine ilikuwa ni lazima kumjaribu usiku kuona kama alikuwa na kinga yoyote ile.
Alijipanga vilivyo, alicheka mbele ya macho ya Bazoka lakini moyoni mwake alipanga mambo yake kwa lengo la kuhakikisha anafanya lolote lile kuhakikisha anamloga kijana huyo, amtingishe kwanza ili kuuona uwezo wake.
“Nitaanza kazi hiyo leo,” alisema Bi. Semeni, moyo wake ulikuwa na kiu kubwa kuhakikisha anamloga Bazoka usiku huo.
Mtu ambaye alimtaka kwa udi na uvumba alimuona, alikuwa Bibi Semeni ambaye kwa stori za mtaani hapo aliambiwa alikuwa mwanamke mchawi, aliyeogopwa kila kona.
Hakutaka kukubali, hapakuwa na kitu ambacho Bazoka alikuwa akikiamini kama uchawi aliokuwa akiutumia, ulikuwa mkubwa, kutoka kuzimu ambapo aliamini kwa mwanamke huyo hakuwa amefika huko.
Ilikuwa ni lazima kummaliza kwa kuwa alihitaji sana kufanikiwa zaidi kwenye mambo yake. Aliwaambia wenzake, yaani Bonge na Sultani kuhusu Bibi Semeni, jinsi alivyokuwa akisifika kwa uchawi, walichomwambia ni kuwa alitakiwa kuhakikisha anammaliza kwani kwa uchawi waliokuwa wakiutumia ulikuwa mkubwa mno.
Ili kumpata mwanamke huyo ilikuwa ni lazima awe anakwenda huk kumuona, ilikuwa ni lazima kuomba naye ukaribu lakini mwisho wa siku afanikiwe kwa kile alichokuwa akikitaka.
Alihitaji kufahamu mengi kuhusu Bi. Semeni hivyo alitakiwa kuongeza ukaribu wake na Frank ambaye ndiye angemwambia mengi kuhusu mwanamke huyo. Kwa jinsi alivyokuwa akimuuliza, hata Frank mwenyewe alishangaa, hakuamini mtu kama Bazoka angehitaji kufahamu mengi kuhusu mwanamke huyo, alikuwa mchawi, mtu aliyeogopwa na watu wote katika mtaa huo, sasa kwa sababu gani alitaka kumfahamu zaidi mwanamke huyo?
“Kwani wewe wa nini?” aliuliza Frank, macho yake yalikuwa yakimshangaa Bazoka.
“Ninataka nimzoee, nahisi anaweza kunisaidia mengi tu hapo baadaye, si unajua mambo yetu ya upande wa pili haya,” alimjibu huku akijitahidi kuonyesha tabasamu kumdanganya Frank kwaba kila kilikuwa sawa kabisa.
“Yule bibi mchawi sana!”
“Umejuaje? Huwezi kumuita mtu mchawi kama wewe si mchawi,” alimwambia.
“Aliwahi kuniroga, alimuwangia sana mke wangu!” alimjibu.
“Na una uhakika gani kwamba yeye ndiye alifanya hivyo?” alimuuliza, alihitaji kujua ukweli.
“Nilikwenda kwake!”
“Kufanya nini?”
“Kuweka dawa, aisee nilichokutana nacho sikuamini macho yangu,” alimwambia.
“Ulikutana na nini?”
“Makaburi!”
“Makaburi?”
“Ndiyo! Nilikutana na makaburi, tena yakiwa kwenye eneo la nyumba yake, unaweza kuamini hilo?” alijibu na kuuliza kwa mshangao.
Bazoka alikaa kimya huku akimwangalia Frank, kwa yale aliyomwambia yalionyesha jinsi bibi huyo alivyokuwa hatari kwenye mambo ya ulozi lakini hakutaka kuacha, ilikuwa ni lazima afanye kila linalowezekana kuhakikisha anaonana na mwanamke huyo, amzoee lakini mwisho wa siku amuue kama alivyotaka kufanya.
Kwa kuwa ilikuwa ni mchana, akaondoka nyumbani kwa Frank na kuelekea kwa Bi. Semeni, alipoingia kwenye uwanja huo tu, kila mtu aliyekuwa jirani akaanza kumwangalia, hapakuwa na aliyeamini kama kweli kungekuwa na mtu ambaye angeingia ndani ya eneo la nyumba hiyo, bibi huyo alitisha, alikuwa mtu hatari ambaye hakutakiwa hata kusogelewa, sasa ilikuwaje mwanaume huyo aingie ndani ya nyumba hiyo na kujiaminisha kabisa.
Bazoka akaanza kuusogelea mlango, alipoufikia, akagonga, baada ya dakika kama moja, ukafunguliwa na Bi. Semeni ambaye alimshangaa Bazoka, hakuwahi kupokea ugeni, ndugu zake, marafiki zake wote walimtenga kwa kuwa alikuwa mchawi, sasa huyo alihitaji nini?
Inawezekana alitaka kupanga chumba lakini pia alijua kila mtu aliyetaka kwenda kupanga hapo kabla ya kuifikia nyumba hiyo, aliwahiwa na majirani na kuambiwa asiende kupanga kwa kuwa alikuwa mchawi, sasa huyo mwanaume alihitaji nini?
“Karibu!” alimkaribisha nyumbani hapo.
“Naruhusiwa kuingia ndani?” aliuliza.
“Unahitaji nini?”
“Kuzungumza na wewe!” alijibu.
“Kuhusu nini?”
“Kwanza ningeingia ndani,” alimwambia.
Kwa Bi. Semeni hapakuwa na tatizo, akamkaribisha mpaka ndani, akaingia huku akiangalia mandhari ya nyumba hiyo, alijifanya kuwa rafiki lakini upande wa pili kulikuwa na kitu alichokuwa akihitaji.
Ilikuwa ni lazima kujenga urafiki mkubwa na mwanamke huyo, amwamini lakini mwisho wa siku akamilishe kile alichokuwa akikihitaji, kwenye kufikiria hayo yote, akapata jibu kwamba ili awe karibu naye zaidi ilikuwa ni lazima amwambie alihitaji chumba na aliambiwa aende katika nyumba ile.
Hilo likaonekana kufaa na kumwambia mwanamke huyo. Bi. Semeni alishangaa, ilikuwa kirahisi mno, alimwambia Bazoka kwa jinsi alivyokuwa na wasiwasi kwamba kweli alihitaji chumba ama kulikuwa na jambo jingine, akamsisitizia ni kweli alihitaji chumba.
“Nimehangaika sana! Tena sana mama yangu!” alimwambia huku akimwangalia.
“Nani alikuelekeza hapa?”
“Kuna mwanaume nilionana naye hapo mtaa wa nyuma, cha ajabu kila dalali niliyemtaka anilete kwenye nyumba hii nzuri, alikataa,” alimwambia.
“Hukuuliza kwa nini walikataa?”
“Sikuuliza! Labda uniambie wewe!” alimwambia.
Bi. Semeni akatoa tabasamu la mbali kabisa huku akimwangalia Bazoka, alihisi kabisa alikuwa akidanganywa na mwanaume huyo, kulikuwa na jambo jingine ambalo hakutaka kumwambia, alihitaji kulifahamu jambo hilo, lilikuwa ni lipi hasa?
Haikuwa kawaida kuja tu kutoka huko ulipokuwa na kwenda nyumbani hapo, eti ulihitaji chumba, nani alikwambia kulikuwa na chumba? Alihitaji kufahamu mengi.
Bazoka alipoona mwanamke huyo anakuwa na hofu sana, akaamua kumdanganya kuwa alihitaji sana kukaa karibu na mke wake, walipendana lakini kwa kipindi hicho waligombana kwa kuwa hakuwa akimwamini.
Nyumbani kwake kulikuwa kama jehanamu, muda wote walikuwa wakigombana, alipotoka kazini na kwenda nyumbani hapo, hakuwa akipata furaha, alikutana na maneno makubwa na malalamiko kutoka kwa mkewe, hivyo aliamua kuondoka nyumbani hapo na kwenda kupanga.
“Unaishi wapi?” aliuliza Bi. Semeni.
“Kijitonyama!”
Walizungumza kwa dakika kadhaa na mwisho kabisa Bi. Semeni akakubali kumpangisha chumba mwanaume huyo, hakuwa amemjua, hakujua lengo lake lakini kwa kuwa alijiamini alikuwa mchawi, basi hakuhofu kama mtu huyo angembabaisha kwa lolote lile.
Siku hiyohiyo Bazoka akaenda kununua baadhi ya vitu vya ndani na kuviingiza, kila mtu aliyekuwa akimuona alishangaa, ilikuwa ajiamini kwenda kuishi ndani ya nyumba hiyo? Tena kwa mwanamke mshirikina kama alivyokuwa Bi. Semeni, hakika kila mtu akataka kufahamu ni kwa namna gani mwanaume huyo alikuwa amechanganyikiwa.
“Sitokuwa nalala siku zote, mara chache nitakuwa nakuja kulala hapa,” alisema Bazoka.
“Haina shida.”
“Ila kwa wiki hii nitalala siku zote, nitamwambia nimesafiri! Hizi ndoa zina majanga sana,” alisema Bazoka na kucheka kidogo.
Siku hiyohiyo Bazoka akarudi nyumbani kwake na kuzungumza na mke wake, alichomwambia ni kuwa alipata safari ya Ghafla kuelekea nchini Uganda hivyo alitakiwa kuondoka siku hiyohiyo kwani kulikuwa na mambo yake alikuwa akienda kuyarekebisha.
Mkewe hakuwa na tatizo hata kidogo, hakuwahi kumfumania mume wake ama hata kuhisi kwa lolote lile, alikuwa mwanaume mwamifu sana, akakubaliana naye na kuondoka zake, safari yake iliishia Magomeni ndani ya chumba chake kipya.
Mpaka muda huo bado Bi. Semeni hakuwa akiamini kama kweli mpangaji wake aliyekuwa kupanga kwake alikuja kupanga kama wapangaji wengine kwenye nyumba nyingine ama kulikuwa na kitu.
Alitaka kujua kama kulikuwa na kitu ni kitu gani lakini hakupata jibu kabisa. Akaamua kukubaliana naye ila kama ilivyokuwa hata kwa wachawi mwengine ilikuwa ni lazima kumjaribu usiku kuona kama alikuwa na kinga yoyote ile.
Alijipanga vilivyo, alicheka mbele ya macho ya Bazoka lakini moyoni mwake alipanga mambo yake kwa lengo la kuhakikisha anafanya lolote lile kuhakikisha anamloga kijana huyo, amtingishe kwanza ili kuuona uwezo wake.
“Nitaanza kazi hiyo leo,” alisema Bi. Semeni, moyo wake ulikuwa na kiu kubwa kuhakikisha anamloga Bazoka usiku huo.
Mtu ambaye alimtaka kwa udi na uvumba alimuona, alikuwa Bibi Semeni ambaye kwa stori za mtaani hapo aliambiwa alikuwa mwanamke mchawi, aliyeogopwa kila kona.
Hakutaka kukubali, hapakuwa na kitu ambacho Bazoka alikuwa akikiamini kama uchawi aliokuwa akiutumia, ulikuwa mkubwa, kutoka kuzimu ambapo aliamini kwa mwanamke huyo hakuwa amefika huko.
Ilikuwa ni lazima kummaliza kwa kuwa alihitaji sana kufanikiwa zaidi kwenye mambo yake. Aliwaambia wenzake, yaani Bonge na Sultani kuhusu Bibi Semeni, jinsi alivyokuwa akisifika kwa uchawi, walichomwambia ni kuwa alitakiwa kuhakikisha anammaliza kwani kwa uchawi waliokuwa wakiutumia ulikuwa mkubwa mno.
Ili kumpata mwanamke huyo ilikuwa ni lazima awe anakwenda huk kumuona, ilikuwa ni lazima kuomba naye ukaribu lakini mwisho wa siku afanikiwe kwa kile alichokuwa akikitaka.
Alihitaji kufahamu mengi kuhusu Bi. Semeni hivyo alitakiwa kuongeza ukaribu wake na Frank ambaye ndiye angemwambia mengi kuhusu mwanamke huyo. Kwa jinsi alivyokuwa akimuuliza, hata Frank mwenyewe alishangaa, hakuamini mtu kama Bazoka angehitaji kufahamu mengi kuhusu mwanamke huyo, alikuwa mchawi, mtu aliyeogopwa na watu wote katika mtaa huo, sasa kwa sababu gani alitaka kumfahamu zaidi mwanamke huyo?
“Kwani wewe wa nini?” aliuliza Frank, macho yake yalikuwa yakimshangaa Bazoka.
“Ninataka nimzoee, nahisi anaweza kunisaidia mengi tu hapo baadaye, si unajua mambo yetu ya upande wa pili haya,” alimjibu huku akijitahidi kuonyesha tabasamu kumdanganya Frank kwaba kila kilikuwa sawa kabisa.
“Yule bibi mchawi sana!”
“Umejuaje? Huwezi kumuita mtu mchawi kama wewe si mchawi,” alimwambia.
“Aliwahi kuniroga, alimuwangia sana mke wangu!” alimjibu.
“Na una uhakika gani kwamba yeye ndiye alifanya hivyo?” alimuuliza, alihitaji kujua ukweli.
“Nilikwenda kwake!”
“Kufanya nini?”
“Kuweka dawa, aisee nilichokutana nacho sikuamini macho yangu,” alimwambia.
“Ulikutana na nini?”
“Makaburi!”
“Makaburi?”
“Ndiyo! Nilikutana na makaburi, tena yakiwa kwenye eneo la nyumba yake, unaweza kuamini hilo?” alijibu na kuuliza kwa mshangao.
Bazoka alikaa kimya huku akimwangalia Frank, kwa yale aliyomwambia yalionyesha jinsi bibi huyo alivyokuwa hatari kwenye mambo ya ulozi lakini hakutaka kuacha, ilikuwa ni lazima afanye kila linalowezekana kuhakikisha anaonana na mwanamke huyo, amzoee lakini mwisho wa siku amuue kama alivyotaka kufanya.
Kwa kuwa ilikuwa ni mchana, akaondoka nyumbani kwa Frank na kuelekea kwa Bi. Semeni, alipoingia kwenye uwanja huo tu, kila mtu aliyekuwa jirani akaanza kumwangalia, hapakuwa na aliyeamini kama kweli kungekuwa na mtu ambaye angeingia ndani ya eneo la nyumba hiyo, bibi huyo alitisha, alikuwa mtu hatari ambaye hakutakiwa hata kusogelewa, sasa ilikuwaje mwanaume huyo aingie ndani ya nyumba hiyo na kujiaminisha kabisa.
Bazoka akaanza kuusogelea mlango, alipoufikia, akagonga, baada ya dakika kama moja, ukafunguliwa na Bi. Semeni ambaye alimshangaa Bazoka, hakuwahi kupokea ugeni, ndugu zake, marafiki zake wote walimtenga kwa kuwa alikuwa mchawi, sasa huyo alihitaji nini?
Inawezekana alitaka kupanga chumba lakini pia alijua kila mtu aliyetaka kwenda kupanga hapo kabla ya kuifikia nyumba hiyo, aliwahiwa na majirani na kuambiwa asiende kupanga kwa kuwa alikuwa mchawi, sasa huyo mwanaume alihitaji nini?
“Karibu!” alimkaribisha nyumbani hapo.
“Naruhusiwa kuingia ndani?” aliuliza.
“Unahitaji nini?”
“Kuzungumza na wewe!” alijibu.
“Kuhusu nini?”
“Kwanza ningeingia ndani,” alimwambia.
Kwa Bi. Semeni hapakuwa na tatizo, akamkaribisha mpaka ndani, akaingia huku akiangalia mandhari ya nyumba hiyo, alijifanya kuwa rafiki lakini upande wa pili kulikuwa na kitu alichokuwa akihitaji.
Ilikuwa ni lazima kujenga urafiki mkubwa na mwanamke huyo, amwamini lakini mwisho wa siku akamilishe kile alichokuwa akikihitaji, kwenye kufikiria hayo yote, akapata jibu kwamba ili awe karibu naye zaidi ilikuwa ni lazima amwambie alihitaji chumba na aliambiwa aende katika nyumba ile.
Hilo likaonekana kufaa na kumwambia mwanamke huyo. Bi. Semeni alishangaa, ilikuwa kirahisi mno, alimwambia Bazoka kwa jinsi alivyokuwa na wasiwasi kwamba kweli alihitaji chumba ama kulikuwa na jambo jingine, akamsisitizia ni kweli alihitaji chumba.
“Nimehangaika sana! Tena sana mama yangu!” alimwambia huku akimwangalia.
“Nani alikuelekeza hapa?”
“Kuna mwanaume nilionana naye hapo mtaa wa nyuma, cha ajabu kila dalali niliyemtaka anilete kwenye nyumba hii nzuri, alikataa,” alimwambia.
“Hukuuliza kwa nini walikataa?”
“Sikuuliza! Labda uniambie wewe!” alimwambia.
Bi. Semeni akatoa tabasamu la mbali kabisa huku akimwangalia Bazoka, alihisi kabisa alikuwa akidanganywa na mwanaume huyo, kulikuwa na jambo jingine ambalo hakutaka kumwambia, alihitaji kulifahamu jambo hilo, lilikuwa ni lipi hasa?
Haikuwa kawaida kuja tu kutoka huko ulipokuwa na kwenda nyumbani hapo, eti ulihitaji chumba, nani alikwambia kulikuwa na chumba? Alihitaji kufahamu mengi.
Bazoka alipoona mwanamke huyo anakuwa na hofu sana, akaamua kumdanganya kuwa alihitaji sana kukaa karibu na mke wake, walipendana lakini kwa kipindi hicho waligombana kwa kuwa hakuwa akimwamini.
Nyumbani kwake kulikuwa kama jehanamu, muda wote walikuwa wakigombana, alipotoka kazini na kwenda nyumbani hapo, hakuwa akipata furaha, alikutana na maneno makubwa na malalamiko kutoka kwa mkewe, hivyo aliamua kuondoka nyumbani hapo na kwenda kupanga.
“Unaishi wapi?” aliuliza Bi. Semeni.
“Kijitonyama!”
Walizungumza kwa dakika kadhaa na mwisho kabisa Bi. Semeni akakubali kumpangisha chumba mwanaume huyo, hakuwa amemjua, hakujua lengo lake lakini kwa kuwa alijiamini alikuwa mchawi, basi hakuhofu kama mtu huyo angembabaisha kwa lolote lile.
Siku hiyohiyo Bazoka akaenda kununua baadhi ya vitu vya ndani na kuviingiza, kila mtu aliyekuwa akimuona alishangaa, ilikuwa ajiamini kwenda kuishi ndani ya nyumba hiyo? Tena kwa mwanamke mshirikina kama alivyokuwa Bi. Semeni, hakika kila mtu akataka kufahamu ni kwa namna gani mwanaume huyo alikuwa amechanganyikiwa.
“Sitokuwa nalala siku zote, mara chache nitakuwa nakuja kulala hapa,” alisema Bazoka.
“Haina shida.”
“Ila kwa wiki hii nitalala siku zote, nitamwambia nimesafiri! Hizi ndoa zina majanga sana,” alisema Bazoka na kucheka kidogo.
Siku hiyohiyo Bazoka akarudi nyumbani kwake na kuzungumza na mke wake, alichomwambia ni kuwa alipata safari ya Ghafla kuelekea nchini Uganda hivyo alitakiwa kuondoka siku hiyohiyo kwani kulikuwa na mambo yake alikuwa akienda kuyarekebisha.
Mkewe hakuwa na tatizo hata kidogo, hakuwahi kumfumania mume wake ama hata kuhisi kwa lolote lile, alikuwa mwanaume mwamifu sana, akakubaliana naye na kuondoka zake, safari yake iliishia Magomeni ndani ya chumba chake kipya.
Mpaka muda huo bado Bi. Semeni hakuwa akiamini kama kweli mpangaji wake aliyekuwa kupanga kwake alikuja kupanga kama wapangaji wengine kwenye nyumba nyingine ama kulikuwa na kitu.
Alitaka kujua kama kulikuwa na kitu ni kitu gani lakini hakupata jibu kabisa. Akaamua kukubaliana naye ila kama ilivyokuwa hata kwa wachawi mwengine ilikuwa ni lazima kumjaribu usiku kuona kama alikuwa na kinga yoyote ile.
Alijipanga vilivyo, alicheka mbele ya macho ya Bazoka lakini moyoni mwake alipanga mambo yake kwa lengo la kuhakikisha anafanya lolote lile kuhakikisha anamloga kijana huyo, amtingishe kwanza ili kuuona uwezo wake.
“Nitaanza kazi hiyo leo,” alisema Bi. Semeni, moyo wake ulikuwa na kiu kubwa kuhakikisha anamloga Bazoka usiku huo.
Mtu ambaye alimtaka kwa udi na uvumba alimuona, alikuwa Bibi Semeni ambaye kwa stori za mtaani hapo aliambiwa alikuwa mwanamke mchawi, aliyeogopwa kila kona.
Hakutaka kukubali, hapakuwa na kitu ambacho Bazoka alikuwa akikiamini kama uchawi aliokuwa akiutumia, ulikuwa mkubwa, kutoka kuzimu ambapo aliamini kwa mwanamke huyo hakuwa amefika huko.
Ilikuwa ni lazima kummaliza kwa kuwa alihitaji sana kufanikiwa zaidi kwenye mambo yake. Aliwaambia wenzake, yaani Bonge na Sultani kuhusu Bibi Semeni, jinsi alivyokuwa akisifika kwa uchawi, walichomwambia ni kuwa alitakiwa kuhakikisha anammaliza kwani kwa uchawi waliokuwa wakiutumia ulikuwa mkubwa mno.
Ili kumpata mwanamke huyo ilikuwa ni lazima awe anakwenda huk kumuona, ilikuwa ni lazima kuomba naye ukaribu lakini mwisho wa siku afanikiwe kwa kile alichokuwa akikitaka.
Alihitaji kufahamu mengi kuhusu Bi. Semeni hivyo alitakiwa kuongeza ukaribu wake na Frank ambaye ndiye angemwambia mengi kuhusu mwanamke huyo. Kwa jinsi alivyokuwa akimuuliza, hata Frank mwenyewe alishangaa, hakuamini mtu kama Bazoka angehitaji kufahamu mengi kuhusu mwanamke huyo, alikuwa mchawi, mtu aliyeogopwa na watu wote katika mtaa huo, sasa kwa sababu gani alitaka kumfahamu zaidi mwanamke huyo?
“Kwani wewe wa nini?” aliuliza Frank, macho yake yalikuwa yakimshangaa Bazoka.
“Ninataka nimzoee, nahisi anaweza kunisaidia mengi tu hapo baadaye, si unajua mambo yetu ya upande wa pili haya,” alimjibu huku akijitahidi kuonyesha tabasamu kumdanganya Frank kwaba kila kilikuwa sawa kabisa.
“Yule bibi mchawi sana!”
“Umejuaje? Huwezi kumuita mtu mchawi kama wewe si mchawi,” alimwambia.
“Aliwahi kuniroga, alimuwangia sana mke wangu!” alimjibu.
“Na una uhakika gani kwamba yeye ndiye alifanya hivyo?” alimuuliza, alihitaji kujua ukweli.
“Nilikwenda kwake!”
“Kufanya nini?”
“Kuweka dawa, aisee nilichokutana nacho sikuamini macho yangu,” alimwambia.
“Ulikutana na nini?”
“Makaburi!”
“Makaburi?”
“Ndiyo! Nilikutana na makaburi, tena yakiwa kwenye eneo la nyumba yake, unaweza kuamini hilo?” alijibu na kuuliza kwa mshangao.
Bazoka alikaa kimya huku akimwangalia Frank, kwa yale aliyomwambia yalionyesha jinsi bibi huyo alivyokuwa hatari kwenye mambo ya ulozi lakini hakutaka kuacha, ilikuwa ni lazima afanye kila linalowezekana kuhakikisha anaonana na mwanamke huyo, amzoee lakini mwisho wa siku amuue kama alivyotaka kufanya.
Kwa kuwa ilikuwa ni mchana, akaondoka nyumbani kwa Frank na kuelekea kwa Bi. Semeni, alipoingia kwenye uwanja huo tu, kila mtu aliyekuwa jirani akaanza kumwangalia, hapakuwa na aliyeamini kama kweli kungekuwa na mtu ambaye angeingia ndani ya eneo la nyumba hiyo, bibi huyo alitisha, alikuwa mtu hatari ambaye hakutakiwa hata kusogelewa, sasa ilikuwaje mwanaume huyo aingie ndani ya nyumba hiyo na kujiaminisha kabisa.
Bazoka akaanza kuusogelea mlango, alipoufikia, akagonga, baada ya dakika kama moja, ukafunguliwa na Bi. Semeni ambaye alimshangaa Bazoka, hakuwahi kupokea ugeni, ndugu zake, marafiki zake wote walimtenga kwa kuwa alikuwa mchawi, sasa huyo alihitaji nini?
Inawezekana alitaka kupanga chumba lakini pia alijua kila mtu aliyetaka kwenda kupanga hapo kabla ya kuifikia nyumba hiyo, aliwahiwa na majirani na kuambiwa asiende kupanga kwa kuwa alikuwa mchawi, sasa huyo mwanaume alihitaji nini?
“Karibu!” alimkaribisha nyumbani hapo.
“Naruhusiwa kuingia ndani?” aliuliza.
“Unahitaji nini?”
“Kuzungumza na wewe!” alijibu.
“Kuhusu nini?”
“Kwanza ningeingia ndani,” alimwambia.
Kwa Bi. Semeni hapakuwa na tatizo, akamkaribisha mpaka ndani, akaingia huku akiangalia mandhari ya nyumba hiyo, alijifanya kuwa rafiki lakini upande wa pili kulikuwa na kitu alichokuwa akihitaji.
Ilikuwa ni lazima kujenga urafiki mkubwa na mwanamke huyo, amwamini lakini mwisho wa siku akamilishe kile alichokuwa akikihitaji, kwenye kufikiria hayo yote, akapata jibu kwamba ili awe karibu naye zaidi ilikuwa ni lazima amwambie alihitaji chumba na aliambiwa aende katika nyumba ile.
Hilo likaonekana kufaa na kumwambia mwanamke huyo. Bi. Semeni alishangaa, ilikuwa kirahisi mno, alimwambia Bazoka kwa jinsi alivyokuwa na wasiwasi kwamba kweli alihitaji chumba ama kulikuwa na jambo jingine, akamsisitizia ni kweli alihitaji chumba.
“Nimehangaika sana! Tena sana mama yangu!” alimwambia huku akimwangalia.
“Nani alikuelekeza hapa?”
“Kuna mwanaume nilionana naye hapo mtaa wa nyuma, cha ajabu kila dalali niliyemtaka anilete kwenye nyumba hii nzuri, alikataa,” alimwambia.
“Hukuuliza kwa nini walikataa?”
“Sikuuliza! Labda uniambie wewe!” alimwambia.
Bi. Semeni akatoa tabasamu la mbali kabisa huku akimwangalia Bazoka, alihisi kabisa alikuwa akidanganywa na mwanaume huyo, kulikuwa na jambo jingine ambalo hakutaka kumwambia, alihitaji kulifahamu jambo hilo, lilikuwa ni lipi hasa?
Haikuwa kawaida kuja tu kutoka huko ulipokuwa na kwenda nyumbani hapo, eti ulihitaji chumba, nani alikwambia kulikuwa na chumba? Alihitaji kufahamu mengi.
Bazoka alipoona mwanamke huyo anakuwa na hofu sana, akaamua kumdanganya kuwa alihitaji sana kukaa karibu na mke wake, walipendana lakini kwa kipindi hicho waligombana kwa kuwa hakuwa akimwamini.
Nyumbani kwake kulikuwa kama jehanamu, muda wote walikuwa wakigombana, alipotoka kazini na kwenda nyumbani hapo, hakuwa akipata furaha, alikutana na maneno makubwa na malalamiko kutoka kwa mkewe, hivyo aliamua kuondoka nyumbani hapo na kwenda kupanga.
“Unaishi wapi?” aliuliza Bi. Semeni.
“Kijitonyama!”
Walizungumza kwa dakika kadhaa na mwisho kabisa Bi. Semeni akakubali kumpangisha chumba mwanaume huyo, hakuwa amemjua, hakujua lengo lake lakini kwa kuwa alijiamini alikuwa mchawi, basi hakuhofu kama mtu huyo angembabaisha kwa lolote lile.
Siku hiyohiyo Bazoka akaenda kununua baadhi ya vitu vya ndani na kuviingiza, kila mtu aliyekuwa akimuona alishangaa, ilikuwa ajiamini kwenda kuishi ndani ya nyumba hiyo? Tena kwa mwanamke mshirikina kama alivyokuwa Bi. Semeni, hakika kila mtu akataka kufahamu ni kwa namna gani mwanaume huyo alikuwa amechanganyikiwa.
“Sitokuwa nalala siku zote, mara chache nitakuwa nakuja kulala hapa,” alisema Bazoka.
“Haina shida.”
“Ila kwa wiki hii nitalala siku zote, nitamwambia nimesafiri! Hizi ndoa zina majanga sana,” alisema Bazoka na kucheka kidogo.
Siku hiyohiyo Bazoka akarudi nyumbani kwake na kuzungumza na mke wake, alichomwambia ni kuwa alipata safari ya Ghafla kuelekea nchini Uganda hivyo alitakiwa kuondoka siku hiyohiyo kwani kulikuwa na mambo yake alikuwa akienda kuyarekebisha.
Mkewe hakuwa na tatizo hata kidogo, hakuwahi kumfumania mume wake ama hata kuhisi kwa lolote lile, alikuwa mwanaume mwamifu sana, akakubaliana naye na kuondoka zake, safari yake iliishia Magomeni ndani ya chumba chake kipya.
Mpaka muda huo bado Bi. Semeni hakuwa akiamini kama kweli mpangaji wake aliyekuwa kupanga kwake alikuja kupanga kama wapangaji wengine kwenye nyumba nyingine ama kulikuwa na kitu.
Alitaka kujua kama kulikuwa na kitu ni kitu gani lakini hakupata jibu kabisa. Akaamua kukubaliana naye ila kama ilivyokuwa hata kwa wachawi mwengine ilikuwa ni lazima kumjaribu usiku kuona kama alikuwa na kinga yoyote ile.
Alijipanga vilivyo, alicheka mbele ya macho ya Bazoka lakini moyoni mwake alipanga mambo yake kwa lengo la kuhakikisha anafanya lolote lile kuhakikisha anamloga kijana huyo, amtingishe kwanza ili kuuona uwezo wake.
“Nitaanza kazi hiyo leo,” alisema Bi. Semeni, moyo wake ulikuwa na kiu kubwa kuhakikisha anamloga Bazoka usiku huo.

Je, nini kitaendelea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom