Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 153,421
- 455,435
Sawa mkuuOk...ngoja nije pm
Sawa mkuuOk...ngoja nije pm
Haina shida mkuu! Ngoja nilifanyie kazi..nitakapokwama nitakushtua inboxMkuu Nyemo nimefurahi kukuona uku mara nyingi inabid niingie fb kusoma simulizi zako nadhan kwa sasa nitakuwa mubashara...
Ombi langu ni moja fanya mpango account yako iwe verified na uwe na uzi maalumu wa story zako wafuatiliaji wengi huku...
Japo na wajuaji wapo pia
Ya hiza iko wapihuku Bazoka kule Hiza,ni mtafutano.Big up sana bro.
Duuh balaah kubwaaUCHAWI WA BILIONEA BAZOKA.
IMEANDIKWA: NYEMO CHILONGANI.
0756362035
Sehemu ya 05.
Ilikuwa kazi ngumu, kila aliponunua kilo mia moja, alipoondoka, alikaa nusu saa, mchele ulikwisha na kurudia kilo mia moja.
Ni ndani ya saa tatu tu, zile tani moja za mchele kwenye gari lile zilimalizika, zote aliuza Bazoka kitu kilichokuwa kimemshangaza sana.
“Bazoka!” aliita Hamisi.
“Niambie mshikaji wangu!”
“Umeanza lini kuuza mchele?”
“Leo! Yaani mpaka nimeshangaa, mchele umekwisha fasta sana,” alisema Bazoka.
“Kila mtu ameshangaa, imekuwaje?” aliuliza Hamisi.
Alipouliza hivyo ndipo alipokumbuka kile alichoambiwa usiku uliopita, ule utajiri alioambiwa ndiyo ambao ulikuwa ukimnyemelea. Hakujibu swali hilo, akajifanya akipuuzia na kuondoka sokoni hapo na kurudi nyumbani.
Alikuwa na kiasi kikubwa cha pesa, alijishangaa, katika maisha yake hakuwahi kushika kiasi kikubwa kama kile alichokuwanacho. Alipofika nyumbani, akamgawia Asha ile pesa aliyoazimwa na baba yake na kumpelekea.
Asha alishangaa, hakuamini alichokiona, hakujua mahali ambapo mpenzi wake alizipata pesa nyingi kiasi kile, alimuuliza na kitu pekee alichoweza kujibu Bazoka ni kwamba alifanya biashara.
Huo ndiyo ukawa mwanzo wa utajiri wake, akawa mfanyabiashara wa mchele, kila siku aliuza kiasi kikubwa mno, alipata pesa kupita kawaida, kila mtu alikuwa akimshangaa huku wengine wakimwambia alikuwa na kismati kuliko hata wao walioanza.
Baada ya mwezi mzima, akaamua kukodi gari ambapo akawa na kazi ya kuufuata mchele yeye mwenyewe mkoani Mbeya. Hilo likampa mafanikio makubwa, akaingiza kiasi kikubwa cha pesa na hivyo kuhama Kwa Ally Maua na kuhamia Mwenge ambapo bado aliendelea kufanya biashara zake kama kawaida.
Maisha yalibadilika, akapanga nyumba nzima, akaanzisha biashara nyingine, mafanikio yake yalikuja kwa kasi sana kiasi kwamba akawa anashangaa tu.
Akanunua gari la kwanza katika maisha yake. Aliyafurahia maisha yake, hakutaka kuishi peke yake, alichokifanya ni kumchukua Asha ambaye alibakiza mwezi mmoja kabla ya kujifungua.
Mara kwa mara alikuwa akikutana na marafiki zake, Sultani na Bonge na kwenda kuabudu kama kawaida yao. Maisha yake aliyakabidhi kwa shetani, hakutaka kurudi nyuma kwani kumuabudu shetani kulimpa mafanikio makubwa ambayo hakuwa akitegemea kuyapata.
Baada ya mwaka mmoja wa mafanikio makubwa huku akiwa ametengeneza jina kubwa nchini Tanzania, akapata kipele katika mguu wake wa kushoto. Kilikuwa kidogo na kilichokuwa kikiwasha sana.
Alikikuna, kadiri alivyokuwa akikikuna ndivyo kilivyokuwa kikiongezeka. Kiliendelea kuwa hivyo mpaka alipoamua kwenda hospitalini kuangalia tatizo lilikuwa nini.
“Ni kipele, inaonekana damu imechafuka eneo hili, chukua hizi dawa zitakusaidia,” alisema nesi huku akimpa dawa.
“Nashukuru sana!” alisema Bazoka na kuondoka.
Alipofika nyumbani, kitu cha kwanza kilikuwa ni kumwambia Asha kilichokuwa kimetokea hospitalini kwamba alipewa dawa na hivyo kuanza kuzitumia.
Wakati huo alikuwa na mtoto wa kiume aliyempa jina la Edward, mtoto mzuri ambaye alichukua sura yake, alimpenda, kwake, mtoto huyo alikuwa kila kitu na kila alipokuwa akimuona, alizidi kupambana zaidi na zaidi.
Siku ziliendelea kukatika, kipele kile hakikuacha kuuma, kilimpa maumivu makali, alipewa dawa mbalimbali kwa ajili ya kukitibu lakini hakikuacha kuwasha na kuuma.
Aliendelea kwenda katika hospitali mbalimbali lakini bado matokeo yalikuwa yaleyale, alichokifanya ni kusafiri mpaka nchini Kenya lakini napo huko kukagonga mwamba, kipele kikaiva na kupasuka, kukatokea kidonda kilichokuwa na maumivu makali.
“Tatizo nini lakini?” alijiuliza lakini hakuwa na jibu lolote lile.
Baada ya mwezi mmoja wa maumivu, akaamua kumwambia Sultani kile kilichokuwa kikiendelea, mwanaume huyo akamuita Bonge na kuanza kumwambia kidonda kile kilitokana na utajiri aliokuwanao.
“Unasemaje?” aliuliza Bazoka huku akionekana kushtuka.
“Kadiri kinavyozidi kuongezeka na kuuma ndivyo utajiri wako utakavyokuwa ukiongezeka,” alisema Bonge.
“Kwa maana hiyo hakitopona?”
“Mpaka unaingia kaburini!”
“Kwa nini?”
“Unakumbuka ulivyoambiwa utajiri huo utaambatana na maumivu makali?” aliuliza Sultan.
“Ndiyo! Nakumbuka niliambiwa na mungu wetu!”
“Hayo ndiyo maumivu yenyewe. Hautoweza kupona, kitaendelea kuuma mpaka kifo chako,” alisema Bonge huku akimwangalia Bazoka.
Bazoka alihuzunika, hakuamini kama yale maneno aliyoambiwa na mungu wake ndiyo yangekuwa maumivu ya namna ile.
Ili kumuonyesha hakuwa peke yake, Bonge akavua shati lake, alikuwa na kidonda kikubwa chini ya kwapa lake, kilikuwa kidonda kilichotisha kuliko hata alichokuwanacho.
Bazoka akashtuka, hakutegemea kuona mtu akiwa na kidonda kile halafu akawa mzima na kuzungumza kana kwamba hakukuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea. Alimwangalia mwanaume huyo, kwake, alionekana kuwa jasiri kuliko wanaume wote ndani ya dunia hii.
“Na wewe Sultan?” aliuliza Bazoka huku akimwangalia Sultan.
“Mimi sina kidonda!”
“Una nini?”
“Sitoweza kupata mtoto maisha yangu yote!” alijibu Sultan huku akimwangalia Bazoka.
Hapo ndipo akagundua utajiri ule ulikuwa na maumivu makali mno. Ulikuwa mtamu, alifanya kitu chochote alichokitaka lakini kila siku alipokiangalia kidonda chake, moyo wake ulimuuma mno.
Asha alimpeleka katika hospitali mbalimbali kutibiwa, Bazoka hakuwa akikataa, alikubaliana na Asha lakini hakuwa radhi kumwambia ukweli kile kilichokuwa kikiendelea.
“Kidonda chako kinaonekana kuwa na bakteria wakali ambao kitaalamu wanaitwa Bicorture,” alisema daktari mmoja baada ya kukiangalia kidonda cha Bazoka.
“Na dawa yake?” aliuliza Asha.
“Naomba akatumie hii, nadhani anaweza kupata nafuu na kupona kabisa,” alisema daktari na kuwapa dawa.
Wakaichukua na kuondoka mahali hapo, moyoni mwa Asha aliamini mpenzi wake angeweza kupona kidonda kile lakini Bazooka alifahamu kila kitu na hakutaka kuweka wazi hata kidogo.
Wakarudi nyumbani na kuanza tiba kama alivyoambiwa lakini hakukuwa na mafanikio yoyote yale. Siku ziliendelea kukatika kama kawaida
Biashara zake ziliendelea kumuingizia kiasi kikubwa cha pesa. Akawa bilionea mkubwa na mwenye makamuni mengi, alikuwa na kazi ya kuuza nafaka ambazo alikuwa akizitoa vijijini na kuzipeleka katika masoko makubwa jijini Dar es Salaam.
Alifanikiwa, akanunua nyumba nyingi jijini Dar es Salaam. Yalikuwa ni mafanikio makubwa na ya haraka sana lakini cha ajabu hapakuwa na mtu aliyetilia shaka kwa kile kilichokuwa kikiendelea.
Walimuona mwanaume huyo kuwa mpambanaji, alijua kupambana kwa ajili ya mafanikio yake. Kila siku aliamka asubuhi na mapema na kuwahi kazini hata kabla ya wafanyakazi wake. Hilo likawafanya watu wengi kuona mafanikio yote aliyokuwa akiyapata ni kwa sababu alijitolea kupambana.
Baada ya miaka miwili, akaitwa katika nyumba ile ya ibada na kuambiwa huo ulikuwa muda wa kutoa kafara kwa mungu wao. Kwanza hakuamini, alichojua walimalizana baada ya kupewa kile kidonda.
Aliogopa, hakujua ni kafara ya aina gani alitakiwa kuitoa. Alikuwa radhi kutoa damu ya mnyama au kitu chochote kile lakini si kuua. Hakuona kama kweli mungu wao angewaambia watoe kafara ya mnyama, alichokiona walitakiwa kutoa kafara ya damu ya mtu.
Alikuwa na hofu, alitetemeka kiasi kwamba kijasho chembamba kikaanza kumtoka. Alikuwa na hofu moyoni mwake na kuhisi kabisa huo haukuwa muda mzuri, piga ua kulikuwa na tatizo mbele yake.
“Inakuwaje tena kutoa kafara,” alimuuliza Sultani huku akionekana kushangaa.
“Huo ndiyo utaratibu tuliyowekewa, kila baada ya miaka miwili, kafara inahitajika,” alisema Sultani huku akimwangalia Bazoka, uso wake ulikuwa na tabasamu pana kana kwamba hakukuwa na tatizo lolote lile.
“Lakini si tuna vidonda?”
“Bado haitoshi, suala la kafara lipo palepale,” alijibu mwanaume huyo.
Jibu hilo lilimchosha, alimwangalia Sultani kwa kumkazia macho, alitamani kumsikia akimwambia alikuwa akimtania. Hakutaka kutoa kafara yoyote ile, moyo wake ulimwambia kile kidonda alichokuwanacho ndiyo kilikuwa kafara yenyewe.
Je, nini kitaendelea?
Namba ya whatsap plz nataka niwe nanunua hukoHii ni kama series ya Breaking Bad...inaanza unaichukulia poa kumbe mbele ni kimbembe.