Chilojnr
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 308
- 1,354
- Thread starter
- #41
UCHAWI WA BILIONEA BAZOKA
MSIMULIAJI: HUSSEIN SANURA
IMEANDIKWA: NYEMO CHILONGANI
0718069269
Sehemu ya 07.
Alikaa kwa wiki nzima huku akiwasiliana na wenzake, Bonge na Sultani ambao walimwambia kuwa kutoa kafara halikuwa jambo gumu, katika kipindi cha kwanza kama hicho angeona kuna ugumu lakini baada ya kuzoea, kusingekuwa na ugumu wowote ule.
Walimtia moyo ili aone kile alichokuwa akienda kukifanya ni cha kawaida sana. Maneno yao yakamuingia, hofu aliyokuwanayo ikaanza kupungua na kujiaminisha kweli kile alichotakiwa kukifanya kilikuwa cha kawaida sana.
Baada ya siku mbili, akachukua kisu kile alichopewa, akakiweka ndani ya gari na kuondoka nyumbani. Siku hiyo alidhamiria kufanya mauaji aliyoambiwa kufanya. Hakutaka kujifikiria mara mbili, alilazimishwa kwa kuwa ndiyo ilikuwa njia mojawapo ya kumfanya kuwa na utajiri ule aliokuwanao.
Akaondoka na kuelekea Manzese, moyo wake ulidhamiria siku hiyo ni lazima atoe kafara ya kwanza na baada ya hiyo angezimalizia zile zilizokuwa zimebaki.
Alipofika maeneo ya Manzese Midizini akalipaki gari lake mbali kabisa na kuanza kutembea kuelekea mahali walipokuwa watoto wanacheza mpira.
Kabla ya kufanya kitu chochote kile akasimama na kuanza kuwaangalia watoto hao huku akiyasoma mazingira ya mahali hapo. Hakutaka kukurupuka, hakutaka kufanya vitu pasipo mahesabu.
Ilikuwa ni lazima auone urahisi ulikuwa mahali gani na kama angeamua kumchukua mtoto mmoja, je, kungekuwa na mtu aliyekuwa akimfuatilia au la? Alikuwa makini na kugundua mahali pale palikuwa na usalama mkubwa hivyo kusingekuwa na mtu yeyote ambaye angemfuatilia.
“Kupo salama, ngoja nimfuate yule pale,” alisema na kuanza kumfuata mtoto mmoja aliyekuwa pembeni huku akiwaangalia wenzake wakicheza mpira.
Alipomfikia, akamsalimia, akaamkiwa na kusimama pembeni yake. Kwa kumwangalia mtoto yule, hakuwa na miaka zaidi ya kumi, akaanza kuongea naye stori za kitoto lakini mwisho wa siku alihitaji kutengeneza urafiki naye.
Hilo alifanikiwa, akaanza kuongea naye mfululizo huku akimuuliza maswali mengi tu ambayo mtoto huyo aliyajibu kitoto sana.
Hiyo ilikuwa mbinu ya kwanza lakini pia alihitaji kutumia pesa kwa kuamini kwa mtoto yeyote ingekuwa ni rahisi kuuteka moyo wake. Akaingiza mkono mfukoni na kutoa shilingi elfu tano.
“Unaishi na nani nyumbani?” alimuuliza huku akijitahidi kuachia tabasamu.
“Mama na baba!” alijibu mtoto yule.
“Unasoma wapi?”
“Magomeni!”
“Darasa la ngapi?”
“Darasa la nne,” alijibu mtoto yule huku naye akitabasamu, kila alipomwangalia Bazoka, akili yake ilimwambia alikuwa rafiki mzuri tu.
“Na unaitwa nani?” aliuliza.
“Hussein Madebe.”
Alizungumza naye kwa dakika kumi, wakawa marafiki wakubwa hivyo kumpa ile noti ya shilingi elfu tano na kuondoka zake. Alichohitaji ni mazoea tu, alijua fika inawezekana kabisa mtoto huyo alikuwa na rafiki yake aliyekuwa albino, alimuhitaji huyo hivyo kumpata kwa urahisi ilikuwa ni lazima kumtumia mtoto ambaye angekwenda kumwambia kuhusu yeye.
Akaondoka na kuelekea nyumbani kwake, kichwa chake kilikuwa na mawazo tele, mtihani aliopewa ulikuwa mkubwa lakini ilikuwa ni lazima afanikishe kwa kuwa hakuwa na jinsi.
Yalikuwa ni masharti makubwa ambayo yangeufanya utajiri wake kuchipukia na kuendelea kuwa mkubwa kila siku. Alijipa moyo kwamba kila kitu kingekuwa vizuri kabisa hivyo hakutakiwa kuwa na hofu hata kidogo.
Nyumbani hakuwa mzungumzaji sana, alimwambia mke wake kulikuwa na vitu vingi ambavyo kipindi hicho alikuwa akivishughulikia hivyo alikuwa bize sana.
Mkewe hakuwa na wasiwasi hata kidogo, ubize wake aliuona, hakuwa mtu wa kutulia hata kidogo, alipokuwa akifika nyumbani, alikaa kwa dakika kadhaa na kuondoka zake huku akionekana kuwa na haraka kupita kawaida.
Siku hiyo hakulala kwa raha kama siku nyingine, kichwa chake kilikuwa kikifikiria mtihani uliokuwa mbele yake. Siku iliyofuatia, akaamka na kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kufuatilia biashara zake.
Ziliendelea kuingiza pesa nyingi, alishangaa, mafanikio ambayo alikuwa akiyapata kipindi hicho yalikuwa makubwa mno. Aliheshimiwa, alikuwa na umri mdogo lakini kila alipopita alisalimiwa kwa heshima kama alikuwa mtu mzima.
Hilo ndilo alilokuwa akilitaka, kwake, alitamani kuona siku moja watu wakimuheshimu kama walivyokuwa wakifanya siku hiyo. Kila alipopita, aliitwa bosi na hakuchungulia mfuko wake, kila mtu ambaye alikuja kulia shida mbele yake, alimsaidia pasipo kuangalia alikuwa nani.
Wakati akiendelea kufanya hayo yote, akiheshimiwa kila alipokuwa akipita bado mguu wake uliendelea kuuma. Ulimkosesha furaha kabisa, kidonda chake kilikuwa kikubwa sana na wakati mwingine alipokuwa peke yake alikuwa akilia kwa maumivu makali.
Kidonda hicho hakikupona, kilitakiwa kuwa hivyohivyo mpaka siku ambayo alikuwa akiingia kaburini. Hakutaka kuhangaikia tena matibabu, aliamua kuachana nacho japokuwa mke wake mara kwa mara alimwambia kwamba wajaribu kwenda katika hospitali kubwa lakini hakutaka kabisa.
Ilipofika jioni ya siku hiyo, haraka sana akaingia ndani ya gari lake na kuelekea kule Manzese Midizini ambapo jana yake alijaribu kutengeneza urafiki na mtoto mmoja kwa kuzungumza naye na hata kumpa pesa.
Alipofika karibu na huko akatafuta sehemu ya kupaki gari lake, alipoipata na kufanya hivyo akaanza kuondoka kuelekea kule uwanjani. Alipofika, hakutaka kumfuata mtu yeyote, aliwaangalia watoto ambao walikuwa wakicheza mpira, akafanikiwa kumuona akiwa peke yake pembeni kabisa.
Akamfuata, alipomfikia, akaanza kuongea naye huku akijitahidi kutoa tabasamu pana. Mtoto yule alipomuona, akafurahi kwani alijua rafiki yake wa jana ambaye alimfuata na kumpa pesa alirudi tena.
Walikaa na kuzungumza mambo mengi, Bazoka alimwambia jinsi alivyofurahi kuonana naye lakini pia akamdanganya kwamba alitaka kukutana na rafiki yake mwingine ambaye alikuwa albino.
“Una rafiki yako albino?” alimuuliza.
“Ninaye! Anaitwa Yusufu! Unamtaka nikamuite?’ aliuliza Hussein.
“Hapana! Ila unaye?”
“Ndiyo!”
“Ni rafiki mzuri kwani?”
“Ni mzuri ila nyumbani kwao wanamkatazaga kutoka!”
“Kwa nini?”
“Eti watamuiba!”
“Ila wewe ukimwambia mtoke si mtatoka?”
“Eeeeh! Atakubali!”
“Basi njoo naye kesho! Halafu nitakupa hela na zawadi nyingine,” alisema Bazoka huku akiachia tabasamu kwani hakutaka kuonekana adui hata kidogo.
Alichokifanya ni kuondoka na kumwambia kesho yake aende naye pale kwani kulikuwa na sehemu alitaka kumpeleka ili wakifika huko wachukue zawadi nyingine na kurudi nyumbani.
Kwa kuwa mtoto Hussen hakuwa akielewa kilichokuwa kikiendelea, akakubaliana naye na kuondoka huku akimwambia afanye liwezekanalo wazazi wake wasijue kitu chochote kile.
Siku iliyofuata, akarudi mahali hapo na kukutana na Hussein, mtoto huyo alikuwa na mwenzake, albino ambaye alimwambia Bazoka kwamba huyo ndiye aliitwa Yusufu aliyekuwa akimuulizia na kumwambia kwamba leo aende naye mahali hapo.
Bazoka akaachia tabasamu pana kwani tayari aliona kufanikiwa kwa kile alichokitaka hivyo kazi ilikuwa kwake kuwachukua na kuwapeleka kule kulipokuwa na gari lake na kuondoka nao.
Hakutaka kwenda nao muda huo kwani kulikuwa na mwanga hivyo kama angefanya hivyo ilikuwa ni lazima kuonekana na watu wengine na hivyo kumtilia shaka. Akasubiri mpaka giza liingie ndiyo akawachukua na kuondoka nao.
Kwa sababu hakukuwa na mwanga wa kutosha, kwake ilikuwa ni afadhali kabisa kwani alifanikiwa kuwafikisha mpaka ndani ya gari na kitu cha kushangaza hakukuwa na mtu yeyote yule ambaye alishtukia kitu chochote.
Akaliwasha, kabla ya kuondoka, akamwambia Hussein akamnunulie maji dukani kwani alikuwa na kiu, kwa sababu mtoto huyo hakujua kitu chochote kilichokuwa kikiendelea akilini mwa mwanaume huyo na tayari alimuona kuwa rafiki, akakubaliana naye na kuelekea dukani.
Huku nyuma, Bazoka hakutaka kubaki, akaliwasha gari na kuondoka mahali hapo akiwa na Yusufu kuelekea njia ya Kigogo huku akimwambia mtoto huyo kwamba Hussein angekwenda kule walipokuwa wakienda wao.
“Atakuja! Huwa anakujaga pale mbele, tutamsubiri,” alisema Bazoka huku akionekana kushinda vita ya kile kilichokuwa kimempeleka mahali hapo, mtu wa kwanza ambaye alikuwa ni albino alikuwa ndani ya gari lake, kilichotakiwa kufanyika ni kumuua kama alivyoambiwa ili aendelee na mtu mwingine, bibi kizee.
Je, nini kitaendelea?
Je, Bazoka alifanikiwa kila kitu?
Tuonane siku Jumatano.
MSIMULIAJI: HUSSEIN SANURA
IMEANDIKWA: NYEMO CHILONGANI
0718069269
Sehemu ya 07.
Alikaa kwa wiki nzima huku akiwasiliana na wenzake, Bonge na Sultani ambao walimwambia kuwa kutoa kafara halikuwa jambo gumu, katika kipindi cha kwanza kama hicho angeona kuna ugumu lakini baada ya kuzoea, kusingekuwa na ugumu wowote ule.
Walimtia moyo ili aone kile alichokuwa akienda kukifanya ni cha kawaida sana. Maneno yao yakamuingia, hofu aliyokuwanayo ikaanza kupungua na kujiaminisha kweli kile alichotakiwa kukifanya kilikuwa cha kawaida sana.
Baada ya siku mbili, akachukua kisu kile alichopewa, akakiweka ndani ya gari na kuondoka nyumbani. Siku hiyo alidhamiria kufanya mauaji aliyoambiwa kufanya. Hakutaka kujifikiria mara mbili, alilazimishwa kwa kuwa ndiyo ilikuwa njia mojawapo ya kumfanya kuwa na utajiri ule aliokuwanao.
Akaondoka na kuelekea Manzese, moyo wake ulidhamiria siku hiyo ni lazima atoe kafara ya kwanza na baada ya hiyo angezimalizia zile zilizokuwa zimebaki.
Alipofika maeneo ya Manzese Midizini akalipaki gari lake mbali kabisa na kuanza kutembea kuelekea mahali walipokuwa watoto wanacheza mpira.
Kabla ya kufanya kitu chochote kile akasimama na kuanza kuwaangalia watoto hao huku akiyasoma mazingira ya mahali hapo. Hakutaka kukurupuka, hakutaka kufanya vitu pasipo mahesabu.
Ilikuwa ni lazima auone urahisi ulikuwa mahali gani na kama angeamua kumchukua mtoto mmoja, je, kungekuwa na mtu aliyekuwa akimfuatilia au la? Alikuwa makini na kugundua mahali pale palikuwa na usalama mkubwa hivyo kusingekuwa na mtu yeyote ambaye angemfuatilia.
“Kupo salama, ngoja nimfuate yule pale,” alisema na kuanza kumfuata mtoto mmoja aliyekuwa pembeni huku akiwaangalia wenzake wakicheza mpira.
Alipomfikia, akamsalimia, akaamkiwa na kusimama pembeni yake. Kwa kumwangalia mtoto yule, hakuwa na miaka zaidi ya kumi, akaanza kuongea naye stori za kitoto lakini mwisho wa siku alihitaji kutengeneza urafiki naye.
Hilo alifanikiwa, akaanza kuongea naye mfululizo huku akimuuliza maswali mengi tu ambayo mtoto huyo aliyajibu kitoto sana.
Hiyo ilikuwa mbinu ya kwanza lakini pia alihitaji kutumia pesa kwa kuamini kwa mtoto yeyote ingekuwa ni rahisi kuuteka moyo wake. Akaingiza mkono mfukoni na kutoa shilingi elfu tano.
“Unaishi na nani nyumbani?” alimuuliza huku akijitahidi kuachia tabasamu.
“Mama na baba!” alijibu mtoto yule.
“Unasoma wapi?”
“Magomeni!”
“Darasa la ngapi?”
“Darasa la nne,” alijibu mtoto yule huku naye akitabasamu, kila alipomwangalia Bazoka, akili yake ilimwambia alikuwa rafiki mzuri tu.
“Na unaitwa nani?” aliuliza.
“Hussein Madebe.”
Alizungumza naye kwa dakika kumi, wakawa marafiki wakubwa hivyo kumpa ile noti ya shilingi elfu tano na kuondoka zake. Alichohitaji ni mazoea tu, alijua fika inawezekana kabisa mtoto huyo alikuwa na rafiki yake aliyekuwa albino, alimuhitaji huyo hivyo kumpata kwa urahisi ilikuwa ni lazima kumtumia mtoto ambaye angekwenda kumwambia kuhusu yeye.
Akaondoka na kuelekea nyumbani kwake, kichwa chake kilikuwa na mawazo tele, mtihani aliopewa ulikuwa mkubwa lakini ilikuwa ni lazima afanikishe kwa kuwa hakuwa na jinsi.
Yalikuwa ni masharti makubwa ambayo yangeufanya utajiri wake kuchipukia na kuendelea kuwa mkubwa kila siku. Alijipa moyo kwamba kila kitu kingekuwa vizuri kabisa hivyo hakutakiwa kuwa na hofu hata kidogo.
Nyumbani hakuwa mzungumzaji sana, alimwambia mke wake kulikuwa na vitu vingi ambavyo kipindi hicho alikuwa akivishughulikia hivyo alikuwa bize sana.
Mkewe hakuwa na wasiwasi hata kidogo, ubize wake aliuona, hakuwa mtu wa kutulia hata kidogo, alipokuwa akifika nyumbani, alikaa kwa dakika kadhaa na kuondoka zake huku akionekana kuwa na haraka kupita kawaida.
Siku hiyo hakulala kwa raha kama siku nyingine, kichwa chake kilikuwa kikifikiria mtihani uliokuwa mbele yake. Siku iliyofuatia, akaamka na kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kufuatilia biashara zake.
Ziliendelea kuingiza pesa nyingi, alishangaa, mafanikio ambayo alikuwa akiyapata kipindi hicho yalikuwa makubwa mno. Aliheshimiwa, alikuwa na umri mdogo lakini kila alipopita alisalimiwa kwa heshima kama alikuwa mtu mzima.
Hilo ndilo alilokuwa akilitaka, kwake, alitamani kuona siku moja watu wakimuheshimu kama walivyokuwa wakifanya siku hiyo. Kila alipopita, aliitwa bosi na hakuchungulia mfuko wake, kila mtu ambaye alikuja kulia shida mbele yake, alimsaidia pasipo kuangalia alikuwa nani.
Wakati akiendelea kufanya hayo yote, akiheshimiwa kila alipokuwa akipita bado mguu wake uliendelea kuuma. Ulimkosesha furaha kabisa, kidonda chake kilikuwa kikubwa sana na wakati mwingine alipokuwa peke yake alikuwa akilia kwa maumivu makali.
Kidonda hicho hakikupona, kilitakiwa kuwa hivyohivyo mpaka siku ambayo alikuwa akiingia kaburini. Hakutaka kuhangaikia tena matibabu, aliamua kuachana nacho japokuwa mke wake mara kwa mara alimwambia kwamba wajaribu kwenda katika hospitali kubwa lakini hakutaka kabisa.
Ilipofika jioni ya siku hiyo, haraka sana akaingia ndani ya gari lake na kuelekea kule Manzese Midizini ambapo jana yake alijaribu kutengeneza urafiki na mtoto mmoja kwa kuzungumza naye na hata kumpa pesa.
Alipofika karibu na huko akatafuta sehemu ya kupaki gari lake, alipoipata na kufanya hivyo akaanza kuondoka kuelekea kule uwanjani. Alipofika, hakutaka kumfuata mtu yeyote, aliwaangalia watoto ambao walikuwa wakicheza mpira, akafanikiwa kumuona akiwa peke yake pembeni kabisa.
Akamfuata, alipomfikia, akaanza kuongea naye huku akijitahidi kutoa tabasamu pana. Mtoto yule alipomuona, akafurahi kwani alijua rafiki yake wa jana ambaye alimfuata na kumpa pesa alirudi tena.
Walikaa na kuzungumza mambo mengi, Bazoka alimwambia jinsi alivyofurahi kuonana naye lakini pia akamdanganya kwamba alitaka kukutana na rafiki yake mwingine ambaye alikuwa albino.
“Una rafiki yako albino?” alimuuliza.
“Ninaye! Anaitwa Yusufu! Unamtaka nikamuite?’ aliuliza Hussein.
“Hapana! Ila unaye?”
“Ndiyo!”
“Ni rafiki mzuri kwani?”
“Ni mzuri ila nyumbani kwao wanamkatazaga kutoka!”
“Kwa nini?”
“Eti watamuiba!”
“Ila wewe ukimwambia mtoke si mtatoka?”
“Eeeeh! Atakubali!”
“Basi njoo naye kesho! Halafu nitakupa hela na zawadi nyingine,” alisema Bazoka huku akiachia tabasamu kwani hakutaka kuonekana adui hata kidogo.
Alichokifanya ni kuondoka na kumwambia kesho yake aende naye pale kwani kulikuwa na sehemu alitaka kumpeleka ili wakifika huko wachukue zawadi nyingine na kurudi nyumbani.
Kwa kuwa mtoto Hussen hakuwa akielewa kilichokuwa kikiendelea, akakubaliana naye na kuondoka huku akimwambia afanye liwezekanalo wazazi wake wasijue kitu chochote kile.
Siku iliyofuata, akarudi mahali hapo na kukutana na Hussein, mtoto huyo alikuwa na mwenzake, albino ambaye alimwambia Bazoka kwamba huyo ndiye aliitwa Yusufu aliyekuwa akimuulizia na kumwambia kwamba leo aende naye mahali hapo.
Bazoka akaachia tabasamu pana kwani tayari aliona kufanikiwa kwa kile alichokitaka hivyo kazi ilikuwa kwake kuwachukua na kuwapeleka kule kulipokuwa na gari lake na kuondoka nao.
Hakutaka kwenda nao muda huo kwani kulikuwa na mwanga hivyo kama angefanya hivyo ilikuwa ni lazima kuonekana na watu wengine na hivyo kumtilia shaka. Akasubiri mpaka giza liingie ndiyo akawachukua na kuondoka nao.
Kwa sababu hakukuwa na mwanga wa kutosha, kwake ilikuwa ni afadhali kabisa kwani alifanikiwa kuwafikisha mpaka ndani ya gari na kitu cha kushangaza hakukuwa na mtu yeyote yule ambaye alishtukia kitu chochote.
Akaliwasha, kabla ya kuondoka, akamwambia Hussein akamnunulie maji dukani kwani alikuwa na kiu, kwa sababu mtoto huyo hakujua kitu chochote kilichokuwa kikiendelea akilini mwa mwanaume huyo na tayari alimuona kuwa rafiki, akakubaliana naye na kuelekea dukani.
Huku nyuma, Bazoka hakutaka kubaki, akaliwasha gari na kuondoka mahali hapo akiwa na Yusufu kuelekea njia ya Kigogo huku akimwambia mtoto huyo kwamba Hussein angekwenda kule walipokuwa wakienda wao.
“Atakuja! Huwa anakujaga pale mbele, tutamsubiri,” alisema Bazoka huku akionekana kushinda vita ya kile kilichokuwa kimempeleka mahali hapo, mtu wa kwanza ambaye alikuwa ni albino alikuwa ndani ya gari lake, kilichotakiwa kufanyika ni kumuua kama alivyoambiwa ili aendelee na mtu mwingine, bibi kizee.
Je, nini kitaendelea?
Je, Bazoka alifanikiwa kila kitu?
Tuonane siku Jumatano.
