Wildlifer
JF-Expert Member
- May 12, 2021
- 1,883
- 5,190
Wapenzi wa simulizi, hii ni Simulizi iliyotoka mwaka 1886 huko Urusi iliyotungwa na Nguli wa Fasihi, Leo Tolstoy. Mwanafasihi huyu ameandika Riwaya na Hadithi fupi fupi nyingi sana. Riwaya zake Maarufu ni Anna Karenina na War and Peace.
Hadithi hii fupi iliitwa : WHAT AMOUNT OF LAND DOES A MAN NEED. Ni simulizi kumuhusu Mkulima aliyeitwa Pahom aliyekuwa ni mwenye tamaa ya Kumiliki ardhi kwa ajili ya shughuli zake za kilimo na ufugaji.
Licha ya kuwa ni Simulizi yenye umri wa takribani miaka 150, ujumbe wake bado unaishi.
Enjoy!
Dada Mkubwa alikuja kumtembelea mdogo wake aliyekuwa akiishi kijijini. Yeye alikuwa anaishi mjini na ameolewa na mfanyabiashara, huku mdogo wake alikuwa ameolewa na mkulima. Jioni wakiwa wamekaa na kupata chai, dada mtu akaanza kujisifu kuhusu uzuri wa maisha ya mjini; akijinasibu namna wanaishi kwa starehe, nguo nzuri ambazo watoto wao walivaa, vyakula na vinywaji vizuri walivyokuwa wakila na kunywa na namna alivyokwenda kwenye makumbi ya sinema, starehe na burudani.
Mdogowe, kwa ghadhabu, alimjibu kwa kuyapondea maisha ya shemeji yake mfanyabiashara na kuyasifu yale ya mmewe mkulima.
'kamwe siwezi badilisha maisha yangu na yako', alimueleza. 'Tunaweza kuwa tunaishi duni, lakini hatuna wasiwasi. Mnaweza kuwa mnaishi kisasa, lakini siku zote mnapata zaidi ya mnachohitaji, mko kwenye uwezekano mkubwa wa kufirisika kuliko sisi, unafahamu ule msemo kuwa 'kupata na kupoteza ni mapacha'. Mara nyingi hutokea, matajiri leo, kesho wanaomba chakula. Maisha yetu ni salama. Ingawa maisha ya mkulima sio ya kifahari, lakini ni marefu. Kamwe hatuwezi tajirika, lakini siku zote tunapata chakula cha kututosheleza'
Dada mtu, kwa hamaki kubwa alimjibu;
'Umemaliza? Ndio, kama unamaanisha kula pamoja na nguruwe na ndama! Mnajua nini kuhusu usafi au kanuni za kula? Hata mmeo afanye kazi za kitumwa namna gani, mtakufa kama mnaoishi kwenye lundo la samadi, wewe na wanao pia'.
'Ni kweli, lakini kwa kipi?' aliuliza mdogowe, 'Ni kweli kazi zetu ni ngumu na chafu, lakini hatusujudii watu. Nyie wa mjini mmezungukwa na vishawishi wakati wote. Leo kila kitu kinaweza kuwa sawa ila kesho yake Shetani akmashawishi mmeo kwa pombe, au kamali au wanawake na vyote vikapotea? Je, hayatokei hayo?'
Pahom, mwenye nyumba aliyekuwa chumba jirani, alikuwa akiyasikiliza na kuyafuatilia mazungumzo ya wanawake hao.
'Kuna ukweli', alijiwazia. 'sisi wakulima toka tukiwa watoto tumekuwa bize na kulima, haturuhusu upuuzi utawale akili zetu. Tatizo letu ni moja, hatuna ardhi ya kutosha. Ningekuwa na ardhi ya kutosha, hata shetani mwenyewe nisingemuogopa'.
Wale wanawake walimaliza chai zao, wakazungumza kidogo kuhusu mavazi, wakatoa vyombo vya chai, kisha wakalala.
Lakini shetani alikuwa nyumba ya nyumba, na alikuwa ameyasikia mazungumzo yote. Alifurahi kuona namna mke wa mkulima alivyomsifia mmewe, kiasi cha kujinasibu kuwa akiwa na ardhi ya kutosha, hatomuogopa shetani.
'Haina shida', aliwaza shetani. 'Tutaingia kwenye ushindani'. Nitakupa ardhi ya kutosha, na kupitia ardhi hiyo hiyo, nitahakikisha umeingia kwenye himaya yangu'.
Hadithi hii fupi iliitwa : WHAT AMOUNT OF LAND DOES A MAN NEED. Ni simulizi kumuhusu Mkulima aliyeitwa Pahom aliyekuwa ni mwenye tamaa ya Kumiliki ardhi kwa ajili ya shughuli zake za kilimo na ufugaji.
Licha ya kuwa ni Simulizi yenye umri wa takribani miaka 150, ujumbe wake bado unaishi.
Enjoy!
Dada Mkubwa alikuja kumtembelea mdogo wake aliyekuwa akiishi kijijini. Yeye alikuwa anaishi mjini na ameolewa na mfanyabiashara, huku mdogo wake alikuwa ameolewa na mkulima. Jioni wakiwa wamekaa na kupata chai, dada mtu akaanza kujisifu kuhusu uzuri wa maisha ya mjini; akijinasibu namna wanaishi kwa starehe, nguo nzuri ambazo watoto wao walivaa, vyakula na vinywaji vizuri walivyokuwa wakila na kunywa na namna alivyokwenda kwenye makumbi ya sinema, starehe na burudani.
Mdogowe, kwa ghadhabu, alimjibu kwa kuyapondea maisha ya shemeji yake mfanyabiashara na kuyasifu yale ya mmewe mkulima.
'kamwe siwezi badilisha maisha yangu na yako', alimueleza. 'Tunaweza kuwa tunaishi duni, lakini hatuna wasiwasi. Mnaweza kuwa mnaishi kisasa, lakini siku zote mnapata zaidi ya mnachohitaji, mko kwenye uwezekano mkubwa wa kufirisika kuliko sisi, unafahamu ule msemo kuwa 'kupata na kupoteza ni mapacha'. Mara nyingi hutokea, matajiri leo, kesho wanaomba chakula. Maisha yetu ni salama. Ingawa maisha ya mkulima sio ya kifahari, lakini ni marefu. Kamwe hatuwezi tajirika, lakini siku zote tunapata chakula cha kututosheleza'
Dada mtu, kwa hamaki kubwa alimjibu;
'Umemaliza? Ndio, kama unamaanisha kula pamoja na nguruwe na ndama! Mnajua nini kuhusu usafi au kanuni za kula? Hata mmeo afanye kazi za kitumwa namna gani, mtakufa kama mnaoishi kwenye lundo la samadi, wewe na wanao pia'.
'Ni kweli, lakini kwa kipi?' aliuliza mdogowe, 'Ni kweli kazi zetu ni ngumu na chafu, lakini hatusujudii watu. Nyie wa mjini mmezungukwa na vishawishi wakati wote. Leo kila kitu kinaweza kuwa sawa ila kesho yake Shetani akmashawishi mmeo kwa pombe, au kamali au wanawake na vyote vikapotea? Je, hayatokei hayo?'
Pahom, mwenye nyumba aliyekuwa chumba jirani, alikuwa akiyasikiliza na kuyafuatilia mazungumzo ya wanawake hao.
'Kuna ukweli', alijiwazia. 'sisi wakulima toka tukiwa watoto tumekuwa bize na kulima, haturuhusu upuuzi utawale akili zetu. Tatizo letu ni moja, hatuna ardhi ya kutosha. Ningekuwa na ardhi ya kutosha, hata shetani mwenyewe nisingemuogopa'.
Wale wanawake walimaliza chai zao, wakazungumza kidogo kuhusu mavazi, wakatoa vyombo vya chai, kisha wakalala.
Lakini shetani alikuwa nyumba ya nyumba, na alikuwa ameyasikia mazungumzo yote. Alifurahi kuona namna mke wa mkulima alivyomsifia mmewe, kiasi cha kujinasibu kuwa akiwa na ardhi ya kutosha, hatomuogopa shetani.
'Haina shida', aliwaza shetani. 'Tutaingia kwenye ushindani'. Nitakupa ardhi ya kutosha, na kupitia ardhi hiyo hiyo, nitahakikisha umeingia kwenye himaya yangu'.