Hadithi tamu: Hisia zangu

Hadithi tamu: Hisia zangu

duhhhhhhhhhhhhhhh..kazi kwelikweli.......mpaka lin tena..???
 
Miaka miwili si mchezo!!!!!!


Jamaa watabandua kizibo tu..........
 
duhhhhhhhhhhhhhhh..kazi kwelikweli.......mpaka lin tena..???
Nitajitahidi niwe naiwweka Jumapili maana Ijumaa na Jumamosi nimepata kazi inayoniweka bize sana, samahani sana kwa wote niliowakera.
 
Njoo endelea bac na hii kitu bac maana naona unatuacha na genye muda mrefu sana..








ILIPOISHIA...
Hipsi zilikuwa kivutio kingine, mwisho ni milima ya haja iliyokuwa nyuma ya viuno yao! Hakika walifungasha. Kufungashia huko hakukuwa na maana kuwa walifanana na majimama, la hasha!
Milima yao iliendana kabisa na maumbo yao. Kwa mifanano ya maumbo walikuwa sawa, tatizo likawa kwenye tabia. Hasa kwenye maisha yao ya kimapenzi.
Leila na Lilian walikuwa na misimamo inayofanana. Leila alikuwa na mpenzi wake mmoja anayejulikana aliyeitwa Michael, maarufu zaidi kama Mike, Lilian yeye alitoka na Edo ambaye awali alikuwa akisoma naye chuoni hapo.
Latifa na Lucy wao habari zao zilikuwa nyingi! Hawakutulia na wanaume kabisa. Mikesha na kwenda klabu ilikuwa ndiyo michezo yao. Pamoja na yote hayo, bado wote kwa pamoja walikuwa na juhudi sana darasani na walikimbiza wenzao katika masomo yote.
Lilian alikuwa akitembea kwa pozi kama vile alikuwa akizionea huruma ngazi alizokuwa akitembea. Bado alishindwa kuondoa Edo kichwani mwake.
SASA ENDELEA...

ILIKUWA ndiyo kwanza siku ya pili inakatika baada ya kuagana na Edo. Hadi muda huo hakuwa na mawasiliano yoyote na Edo ingawa alimtumia waraka pepe tatu na zote hakujibu. Kwa mbali akawaona rafiki zake akina L wakiwa wamekaa kivulini wanajisomea.
Ni palepale pa siku zote!
Kwa kawaida walizoea kusomea sehemu moja. Lilian alikazana na kuwafikia. Lilikuwa kundi zuri sana la majadiliano kutokana na namna wote walivyokuwa na mtazamo mkubwa na uwezo wa kuelewa.
"Mambo zenu warembo?" Lilian akasalimia.
"Poa Lilian, vipi mwenzetu?" Leila alikuwa wa kwanza kuitikia salamu.
"Safi tu."
"Karibu mrembo, tunatengeneza maisha hapa, hatupo tayari kuendelea kunyanyaswa na wanaume, elimu ndiyo mkombozi wetu wa kweli," Latifa naye akasema.
"Kweli kabisa," akajibu Lilian kisha akaketi na kutoa vitabu vyake.
Jambo lililomshangaza ni kwamba, muda wote aliofika hapo, Lucy hakusema kitu chochote! Lilian hakumfikiria vibaya, aliamini ni masomo ndiyo yaliyokuwa yamembana. Akanyamaza kimya na kuanza kupiga kitabu.
Wote wakawa kimya!
Dakika tano baadaye, Lucy alionekana kuchukua bahasha kwenye begi lake la vitabu na kumkabidhi Lilian. Alipokea kwa mshangao. Ilikuwa bahasha ndogo kiasi lakini iliyonona. Ilionekana ndani yake kuwa na makabrasha muhimu ila yaliyojaa.
"Ni nini?"
"Utafungua baadaye."
"Kama ni bomu je?"
"Mh! Wewe naye, nani wa kukuwekea bomu sasa mtoto wa kike?"
"Niambie ni nini basi?"
"Mtoto una haraka sana wewe. Haya fungua!" akasema Lucy.
Lilian akafungua. Alikutana na burungutu la noti za elfu kumikumi!
Bahasha ilikuwa imejaa kiasi kwamba haikuwa rahisi kufungika vizuri.
"Zimetoka wapi?"
"Hapo sasa tutazungumza baadaye."
"Hapana Lucy, chukua pesa zako."
"Acha upuuzi wewe, lini utakuwa na akili? Huyo Edo unayemn'ang'ania, unajuaje kuwa naye hakusaliti? Kwanza sasa hivi hayupo nchini, una wasiwasi gani? Tumia urembo wako vizuri mtoto, la sivyo utabaki unang'aa macho tu mjini hapa," akasema Lucy kwa msisitizo.
Lilian hakuwa mtoto, alishajua kuwa zile fedha zilitoka kwa mwanaume. Kwa Lucy na Latifa, kubadilisha wanaume lilikuwa jambo la kawaida kabisa.
"Lucy tunaheshimiana sana mimi na wewe, kumbuka kinachotukutanisha hapa ni masomo tena ni kwa vile hili ni kundi letu la kujisomea na ni zuri. Tuishi kwa kuelewana na kuheshimiana.
"Ni vyema kila mmoja akaheshimu hisia za mwenzake. Kwanini unataka kunilazimisha nifanye kitu ambacho sikipendi? Chukua pesa zako," Lilian akasema kwa ukali sana.
"Sitaki, kama unaweza kuzichoma labda ufanye hivyo. Huo ushamba utakutoka lini? Kwani kula pesa ya mtu ndiyo kumkubali? Acha ujinga, kula maisha hayo, mambo mengine baadaye," akasema Lucy akijiandaa kuinuka.
Ni kweli aliinuka.
Alikusanya vitabu vyake na makabrasha mengine, akaondoka zake. Pale akawaacha Latifa, Leila na Lilian wakimshangaa.
Ama kweli alishangaza!
"Sikia shosti, kwani wewe umeomba hela?" akasema Leila.
"Ndiyo nashangaa!"
"Sasa huna haja ya kushangaa, chukua mzigo utumie. Ni nani anaweza kukufuata kukudai? Kwani umekopeshwa? Tumia lakini akikuambia mambo ya wanaume kataa," akasema Leila na kuungwa mkono na Latifa:
"Kweli kabisa, sioni tatizo."
"Wewe na yeye ni walewale tu!" akasema Leila.
"Jamani hebu tusomeni basi, kwani Lilian ni mtoto? Kwanini tunatofautina kwa mambo binafsi? Yeye ni mtu mzima na anaweza kuamua chochote kwa utashi wake," akasema Latifa.
Lilian alikuwa kwenye mzigo mzito wa mawazo lakini alipotafakari sana, hakuona sababu ya kukataa hizo fedha. Akaziweka kwenye mkoba wake na kuendelea kujisomea.
"Kibaya ni kumsaliti Edo, kama ni pesa sioni tatizo lake," akajisemea moyoni mwake akiendelea kujisomea.
***
Edo alifika jijini Kuala Lumpur, nchini Malaysia salama kabisa. Alikuwa na maelekezo yote, hivyo haikuwa vigumu kwake kufika chuoni. Alipokelewa vizuri na kuelekezwa chumbani kwake kisha taratibu nyingine zikafuata.
Alikuwa mchovu sana kutokana na safari ndefu ya kutoka Tanzania hadi Malaysia. Siku tatu baadaye ndipo alipopata utulivu wa akili kidogo. Akiwa chumbani kwake, akakumbuka kuwasiliana na mpenzi wake.
Bado hakuwa na mawasiliano ya simu ya mkononi, simu alikuwa nayo lakini alikuwa bado hajapata usajili wa namba kutoka moja ya kampuni za simu nchini humo.
Alifungua laptop yake na kuingia kwenye akaunti yake ya waraka pepe. Alikutana na ujumbe kutoka kwa watu wengi sana, akiwemo Lilian ambaye alimwandikia mara tatu. Akaanza kusoma mmoja baada ya mwingine.
Hello,
Edo. Najua umefika salama mpenzi wangu. Pole na safari baba. Napenda kukuhakikishia kuwa, moyoni mwangu umejaa wewe pekee na hakuna nafasi ya mwingine zaidi yako. Nakupenda sana.
Ukipata ujumbe wangu, tafadhali unijibu.
Lilian.

Edo akavuta pumzi ndefu sana kisha akazishusha taratibu kabisa. Akatulia kwa muda. Baadaye kidogo akafungua ujumbe unaoufuata.
Ujumbe huo ndiyo uliomshtua sana moyo wake. Aliuma meno kwa nguvu, akarudi kuangalia jina na anwani ya mtu aliyemtumia ili ajiridhishe kuwa Lilian ndiye aliyemtumia.
Ni kweli alikuwa ni Lilian!
Akazidi kuchanganyikiwa!
Itaendelea…
 
[MENTION]
Mommadou Keita[/MENTION]

Mbona hivyo tena kimya kinatisha!!!!!!!!


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Achana na huyu wewe twende tukamalizie kule kwa kina cecy na colin


[MENTION]
Mommadou Keita[/MENTION]

Mbona hivyo tena kimya kinatisha!!!!!!!!


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Achana na huyu wewe twende tukamalizie kule kwa kina cecy na colin


Sawa Mkuu;

Nilikuwa namfuatilia huyu nijue kijana EDO amefikia wapi;


Kwa kweli mtu kuahidiwa miaka miwili ni ngumu sana kumuamini kulinda penzi.
 
Edo, pole yako ungekomaa ukakata seal mwenyewe, ningekuwa mimi ningelia mpaka nikaikata. ona sasa!
 
Inaonekana itakuwa nzuri,hebu ngoja nianze kuifatilia
 
daaah! kiukwe hadithi hizi zinanifanya nipoteze mawazo kabisa
 
ILIPOISHIA...
Hello,
Edo. Najua umefika salama mpenzi wangu. Pole na safari baba. Napenda kukuhakikishia kuwa, moyoni mwangu umejaa wewe pekee na hakuna nafasi ya mwingine zaidi yako. Nakupenda sana.
Ukipata ujumbe wangu, tafadhali unijibu.
Lilian.
Edo akavuta pumzi ndefu sana kisha akazishusha taratibu kabisa. Akatulia kwa muda. Baadaye kidogo akafungua ujumbe unaoufuata.
Ujumbe huo ndiyo uliomshtua sana moyo wake. Aliuma meno kwa nguvu, akarudi kuangalia jina na anwani ya mtu aliyemtumia ili ajiridhishe kuwa Lilian ndiye aliyemtumia.
Ni kweli alikuwa ni Lilian!
Akazidi kuchanganyikiwa!
SASA ENDELEA...

ALITEMBEA kwa maringo yaliyoonekana wazi. Hayakuwa ya kutafuta. Lucy alijua alivyo mrembo, hivyo kuonyesha maringo ilikuwa kichagizo cha jinsi alivyo.
Wanafunzi wengine walikuwa wakimkodolea macho wakati akitembea taratibu akionekana asivyo na haraka na alipokuwa akielekea. Ni kweli hakuwa na haraka maana safari yake ilikuwa inaishia hosteli.
Pamoja na uzuri wa umbo lake, pia mavazi yake yalimshawishi kila mwanaume aliyekamilika kumwangalia kwa uchu wa mahaba mazito.
Kwa mwanaume mkamilifu, ingekuwa vigumu sana kwa Lucy kupita mbele yake bila kukata shingo kumwangalia. Lucy alizawadiwa urembo wa kutosha!
Alitembea hadi alipofika kwenye barabara kubwa ya lami, akasimama kupisha magari yapite kisha akavuka na kupanda kijimlima kidogo kuelekea hosteli.
Alipofika chumbani kwake, alijitupa kitandani, kisha akajilaza kwa mgongo na kuyarusha mcho yake juu ya dari na kuanza kuwaza...
“Siwezi kushindwa kumshawishi Lilian. Ni mtoto mdogo sana. Mimi namuweza. Hanishindi kwa lolote,” akawaza.
“Lazima aingie kingi,” akajisemea kwa sauti.
“Huyu mtoto mdogo tu kwangu, anajifanya ana msimamo. Itakuwa yeye...hapa Bongo akili kichwani.”
Lucy alikuwa kwenye lindi zito la mawazo. Kikubwa kilichokuwa akilini mwake ni milioni tano alizoahidiwa na mzee mwenye fedha zake, mfanyabiashara mkubwa jijini Dar es Salaam, Pamseck Kinga.
Kinga hujulikana zaidi kwa jina la Pam. Kazi aliyopewa na Pam ni kuhakikisha anamuingiza Lilian kwenye himaya yake. Kwa kuanzia Pam alimpa shilingi milioni moja kwenye bahasha ili ampelekee Lilian.
Fedha kwake ilikuwa siyo shida, tatizo kubwa lilikuwa matumizi tu!
Lucy akiwa bado yupo mawazoni, akifikiria mbinu nyingine mpya ya kumnasa Lilian kiulaini, simu yake iliita. Alipoangalia kwenye kioo akakutana na jina la Pam. Haraka akapokea.
“Nategemea kusikia kitu kizuri kutoka kwako, haya niambie,” sauti ya Pam iliunguruma simuni.
“Mh! Pam mbona una haraka sana baba?”
“Lazima niwe na haraka. Namtamani sana huyo mtoto. Niambie umefikia wapi?”
“Hatua nzuri.”
“Hatua nzuri siyo?”
“Kabisa.”
“Nataka kujua kitu kimoja kwanza; amechukua huo mzigo?”
“Ndiyo lakini kwa kumlazimisha sana.”
“Anajua ulipotoka?”
“Hapana, lakini lazima atakuwa anahisi, kwani yeye mtoto? Kuna pesa inaweza kujipeleka yenyewe?”
“Kweli lakini, dalili unazionaje?”
“Pam usiwe na wasiwasi, niachie mimi hii shoo nitaisimamia mpaka mwisho.”
“Nakuamini Lucy, ni mtihani wako mdogo sana. Ukiufaulu milioni moja itakuwa halali yako.”
“Sema.”
“Nataka wikiendi hii uje naye club, utaweza?”
“Milioni ipo?”
“Kumbuka mimi ndiyo nimekuahidi.”
“Sawa, niachie mimi.”
“Nakutumia laki tano baadaye kidogo, ukifanikiwa kuja naye, laki tano yako nitakumalizia. Kumbuka matumizi mengine yote ambayo utakayotumia wewe na rafiki zako kutokana na ujio wenu nitalipia mimi.
“Hapo namaanisha kuanzia mambo ya salon na mengineyo nitarudisha. Kazi yako ni moja tu; kuhakikisha Lilian unakuja naye disko. Mambo mengine niachie mimi.”
“Kazi ndogo, tuma pesa hiyo kwa namba zangu za simu.”
“Robo saa ijayo fedha itakuwa tayari imeshakufikia.”
“Poa Pam.”
“Usiniangushe Lucy.”
“Umenisahau mara hii?” akasema Lucy huku akisindikiza na kicheko cha nguvu.
“Sawa.”
Pam akakata simu.
Lucy aliendelea kuisikiliza simu yake. Alipogundua ilikuwa imekatwa, akaitoa sikioni.
“Nitajua cha kufanya,” akasema.
Palepale akamtumia meseji Latifa iliyosomeka: “Shoga, Pam amenipa dili lingine, amesema kama nikifanikiwa kwenda na Lilian club wikiendi hii, atanipa milioni moja.
“Sasa nakupa dili, na wewe hapa nakushirikisha, utakula laki mbili. Naomba uanze kulianzisha.”
“Poa shoga yangu, miye tena? Huku huku naanza mambo,” akajibu Latifa.
***
Wiki moja bila Edo nchini Tanzania ilikuwa ngumu kwa Lilian. Chuo kilianza kuwa na ugumu kidogo. Kwa namna alivyojizoesha matumizi makubwa, bila Edo ilikuwa ni wakati mgumu sana kwake.
Pamoja na fedha wanayopewa wanafunzi wote kwa ajili ya matumizi, bado haikuweza kukidhi mahitaji yake ipasavyo. Umuhimu wa milioni aliyopewa na Lucy akiwa hajui ilipotokea ulionekana dhahiri.
Kwa kutumia hila na maneno laghai, Latifa na Lucy walifanikiwa kuwateka mawazo Leila na Lilian na kukubali kwenda disko, kichwani wakiamini walikuwa wanakwenda kwenye berthday.
Walipofika Masaki, kibao kikageuka. Wakaambiwa wanakwenda Klabu Maisha. Lilian aligoma, kwa ushawishi wa Lucy na Latifa, Leila akajikuta akiunga mkono, Lilian akajikuta akikubali kuingia. Lucy aliwalipia wote.
Disko lilikuwa limechangamka sana. Lilian alionekana kuwa mpole, akiwa amekaa kwenye kiti muda wote akinywa juisi. Latifa na Lucy walikuwa wamekolea kilevi, wakicheza kwa madaha muziki uliokuwa ukirindima.
Leila alijikuta akifuata mkumbo na kwenda kucheza na wenzake. Muziki ulipokolea, Lucy alikwenda kumvuta Lilian na kuelekea naye kwenye sehemu maalumu ya kuchezea muziki.
Kwa shingo upande, Lilian alijikuta akienda. Hakujua kuwa alikuwa akienda kukutana na Pam!
***
Edo aliendelea kusoma ujumbe ule zaidi ya mara tatu; maneno yalikuwa yaleyale. Safari hii aliamua kusoma kwa sauti:
Edo
Nilijua lazima hili lingetokea. Ni wiki tu tangu umeondoka, lakini tayari hisia za usaliti zimeanza kunukia. Nakuomba baada ya kusoma ujumbe huu, tafadhali endelea na maisha yako, nami niache na maisha yangu.
Siwezi kuendelea kulazimisha mapenzi mahali nisipopendwa. Kwa taarifa yako kwa sasa natafuta mwanaume mwingine ambaye ataweza kunithamini na kujua umuhimu wangu.
Kutokea muda utakaosoma ujumbe huu, ondoa kichwani mwako kuwa una mwanamke Tanzania anayeitwa Lilian.
Lilian.
Edo akaamua kujiridhisha tena kujua kama aliyetuma alikuwa ni Lilian. Ni kweli ulikuwa ujumbe kutoka kwa Lilian. Hilo alijihakikishia kwa asimilia mia moja!
Itaendelea.
 
af mbona haditj ya wakil hutoi mizambwa tunakuda epusode km tano iv tuwekee bas cz hadith zako ni nzur mno hongera
 
Last edited by a moderator:
Nani ameingilia account ya Lilian jamani, Lily hawezi kuandika hivyo kwa edo, haiwezekani!
 
Back
Top Bottom