Hadithi tamu: Hisia zangu

Hadithi tamu: Hisia zangu

Hivi jamani hakuna adhabu nyingine anayoweza kupata aliyeshindwa kuwa mwaminifu badala ya hii award ya HIV? Bro mleta maada naomba contact za Lily tumpime tena yumkini majibu aliyopewa sio yake!
Nadhani kuna funzo kubwa sana linakuja mbele ya hadithi hii, ndio kwanza imeanza, hebu fuatilia utaona nn kitatokea.
 
Nadhani kuna funzo kubwa sana linakuja mbele ya hadithi hii, ndio kwanza imeanza, hebu fuatilia utaona nn kitatokea.

Bro! Please, make sure Lilian ni mzima bwana na kwamba yaliyotokea yote yalikuwa ndoto na kwamba maisha yataendelea kama kawaida..nakwa kuwa muda ni ukuta basi wakiwa tayari kuoana ukumbi na Vinywaji ni juu yangu...PAM,Lucy & Laila wasifike! Ni amri!
 
Bro! Please, make sure Lilian ni mzima bwana na kwamba yaliyotokea yote yalikuwa ndoto na kwamba maisha yataendelea kama kawaida..nakwa kuwa muda ni ukuta basi wakiwa tayari kuoana ukumbi na Vinywaji ni juu yangu...PAM,Lucy & Laila wasifike! Ni amri!

Hahahaha laiti mkuu ungekuwa Mungu... Hakika dunia ingebaki tupu
 
Bro! Please, make sure Lilian ni mzima bwana na kwamba yaliyotokea yote yalikuwa ndoto na kwamba maisha yataendelea kama kawaida..nakwa kuwa muda ni ukuta basi wakiwa tayari kuoana ukumbi na Vinywaji ni juu yangu...PAM,Lucy & Laila wasifike! Ni amri!

Ha ha ha ha pole maana unaonekana umeumizwa na hii story, pole mkuu
 
Bro! Please, make sure Lilian ni mzima bwana na kwamba yaliyotokea yote yalikuwa ndoto na kwamba maisha yataendelea kama kawaida..nakwa kuwa muda ni ukuta basi wakiwa tayari kuoana ukumbi na Vinywaji ni juu yangu...PAM,Lucy & Laila wasifike! Ni amri!

Kwani si stori inaendelea mbona mna papara subirini msitake kupredict mambo yajayo na do kwanza hujaambiwa mwisho wa hadithi
 
Mommadou Keita, vipi mbona kimya kimekuwa kirefu sana
Kuja pande hii please
 
Last edited by a moderator:
Nadhani kuna funzo kubwa sana linakuja mbele ya hadithi hii, ndio kwanza imeanza, hebu fuatilia utaona nn kitatokea.

hivi ndo nini kutusubirisha muda mrefu kusoma muendelezo wa hii hadithi????kama hujajipanga kuileta kila wiki nakushauri ni bora kuacha kabisa kutuletea hadithi...hebu amka ulipolala njoo utupie vitu.......
 
Hisia Zangu sehemu ya 23
ILIPOISHIA...
Uamuzi alioufikia ulikuwa ni kuandika barua ya kuomba kuhairisha mwaka wa masomo hadi mwaka uliofuata. Katika barua yake, alieleza sababu mbalimbali za kutunga, uongozi wa chuo ukakubaliana naye.
“Sitakwenda nyumbani, nitakuwa hapahapa Dar,” alijisemea Lilian akiwa kitandani, akisoma barua ya majibu aliyopewa na uongozi wa chuo ambao ulikubaliana na maombi yake.
SASA ENDELEA...

SONONEKO lilijaa moyoni mwa Lilian, aliingia katika historia mpya kabisa ambayo katu hakuitegemea kama angeipitia. Kichwa chake kilikuwa kizito sana. Hakuwa na uwezo wa kufanya chochote tena.
Aliamini kuhairisha mwaka mmoja wa masomo, pengine kungeweza kuwa dawa. Alijihisi mzito kuliko kawaida. Kwa uchovu mkuu, woga moyoni na hofu isiyo na kifani, aliburuza begi lake akatokea kwenye lango kuu la hosteli yao.
Alikuwa na mawazo mengi sana. Bado aliendelea kufikiria kukaa Dar es Salaam. Isingekuwa rahisi kwake kwenda nyumbani kwao ambapo angekutana na maswali mengi ambayo asingekuwa na majibu yake.
“Siwezi kwenda nyumbani kabisa, siwezi,” aliwaza.
Mawazo yake yalikuwa sahihi kwa hakika. Isingekuwa rahisi kwake kwenda nyumbani kwao. Akawaambie nini? Hakuwa na la kusema.
Bado aliwaza: “Sawa, nitakaa hapa Dar, nitakaa kwa nani?”
Mawazo hayo ndiyo yaliyosababisha safari yake ya kwenda kusipojulikana iishie katika Bar ya Udasa pale chuoni ambapo kwa kutuliza kichwa chake, akaagiza mvinyo mweupe na kuanza kunywa!
Pengine kweli bwana, huenda pombe huwa inasaidia kwa kiasi fulani hivi....mara akili yake ikafunguka...mawazo yake yakamtuma kwenye kitu kipya kabisa ambacho kwake aliona ahueni kubwa. Alimkumbuka shangazi yake, Juliana!
“Nitakwenda kwa anti. Bora niende kwake.”
Wazo hilo lilipita moja kwa moja. Akajiinua kitini na kuchukua begi lake la magurudumu kisha akaanza kulikokota!
Alipofika nje ya baa hiyo, alivuka barabara na kusimama kituoni, upande wa pili. Mara daladala likitokea Makumbusho kuelekea Ubungo likasimama mbele yake. Akajipakia na kwenda kukaa siti ya nyuma kabisa. Mawazo tele kichwani mwake.
“Maisha haya mpaka lini?” akawaza.
Alishuka Ubungo na kupanda daladala la Gongo la Mboto, hapo angetafuta usafiri wa kwenda kwa shangazi yake Juliana, Pugu – Kajiungeni.
***
Alikuwa na umri wa miaka 29. Binti mbichi kabisa, akiwa mtoto wa mwisho kuzaliwa katika uzao wa babu yake na Lilian. Ni shangazi yake, lakini alikuwa na umri unaokaribiana kabisa na wake.
Wote walikuwa wadada wa kadiri. Juliana alipomaliza masomo yake ya kidato cha sita, Shule ya Sekondari Mkwawa, Iringa alikwenda kusoma uhasibu katika Chuo Kikuu cha Uhasibu Arusha (Institute of Accountancy Arusha – AII) kilichopo jijini Arusha. Alipohitimu, kwa bahati nzuri akafanikiwa kupata kazi katika Kampuni ya Think Big Production ya jijini Dar es Salaam. Kwa uwezo wake kazini, miaka mitatu tu ya kufanya kazi katika kampuni hiyo, aliteuliwa kuwa mhasibu mkuu.
Akahama Tabata alipokuwa akiishi awali na kupewa nyumba ya ofisi, Pugu – Kajiungeni, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Kwa kuzingatia shida ya usafiri, Juliana alipewa gari na ofisi yake ili limsaidie kumwahisha ofisini.
Alifanya kazi kwa juhudi sana. Akawa na heshima kubwa kwenye kampuni hiyo iliyokuwa na ofisi zake Barabara ya Nyerere, mbele kidogo ya Tazara jijini Dar es Salaam.
Aliishi na msichana wake wa kazi katika nyumba hiyo kubwa. Aliitwa Neema.
***
Ilikuwa Jumamosi, moja kati ya siku zake mbili za mapumziko ya mwisho wa juma. Juliana hupumzika Jumamosi na Jumapili. Akiwa hana hili wala lile, alisikia kengele ikipigwa kutokea geti kubwa la kuingilia nyumbani kwake.
Neema aliamka haraka na kwenda kufungua. Lilian akaingia. Juliana alishangaa sana, maana si tu hakuwa na taarifa ya ugeni wake, bali hawakuwasiliana kwa simu kwa zaidi ya miezi miwili.
“Karibu, mwenzetu mbona kimyakimya?” Juliana alisema wakati akimpokea Lilian.
“Ahsante anti, we acha tu, tutazungumza.”
“Kuna tatizo?” Juliana aliuliza.
Alikuwa na kila sababu ya kuuliza kutokana na namna Lilian alivyoonekana usoni. Ni wazi alikuwa na jambo zito lililokuwa likimsumbua.
“Tupo anti, usijali tutazungumza tu.” Begi lake likapelekwa ndani, Lilian akafikia kwenye bustani nzuri, nje ya nyumba hiyo. Ni hapo walikuwa wamepumzika Juliana na Neema. Walikuwa kama mtu na ndugu yake – Juliana mwenyewe hakupenda kabisa ijulikane kuwa, Neema alikuwa msichana wake wa kazi.
Alimpenda sana kwa bidii yake ya kazi.
***
“Haya niambie anti yangu, kuna tatizo gani?” Juliana alimwuliza akiwa na hakika kabisa kuwa Lilian alikuwa na tatizo lililomsumbua.
“Nimeahirisha mwaka wa masomo anti, nakuomba sana...sitaki kwenda nyumbani. Naomba nipumzike hapa kwako kwa mwaka mmoja, mpaka nitakaporejea chuoni,” akasema Lilian.
“Ni sawa, lakini kuna nini? Nini kimekufanya uhairishe masomo?”
“Anti ngoja niwe mkweli kwako. Wewe ni zaidi ya shangazi kwangu. Wewe ni rafiki yangu na ninategemea utakuwa msiri wangu.”
“Sawa, niambie una nini?”
“Anti tatizo ni mapenzi. Kuna mtu amenivuruga sana kichwa changu,” akadanganya Lilian.
Alizungumza ukweli kiasi, maana ni kweli mapenzi ndiyo yaliyomtibua, lakini kuna alichoacha!
“Mh! Nilijua tu,” akasema Juliana akitabasamu.
“Lakini ni ujinga kuyapa nafasi mapenzi katika maisha yako, kiasi cha kuhairisha masomo. Uamuzi wako nadhani haupo sawa na sidhani kama jambo hilo linaniingia akilini,” akasema Juliana kwa sauti yake ya taratibu lakini ikionekana wazi kuwa na hasira kidogo ndani yake.
Lilian akachanganyikiwa!
Kulikuwa na dalili zote za kufukuzwa na shangazi yake. Moyoni, aliapa kabisa kutomwambia siri iliyosababisha afikie uamuzi huo. Alitaka kuifanya siri yake ya moyoni.
Juliana hakujua kilichokuwa ndani ya moyo wa shangazi yake. Alichukulia suala lake kama uzembe tu wa fikra katika uhusiano. Laiti angeingia moyoni mwake na kujua siri aliyokuwa nayo!
Angejua!!!
Je, nini kitatokea? Usikose kufuatilia.
 
Samahani waungwana kwa kuchelewesha kuiweka hadithi hii humu ndani, si kwa kukusudia, samahani leo nimejitahidi kuiweka hapa. samahani sana.
 
Inaedeleeaa... Kibishi ngoja niimalize
edo baada ya kumaliza chuo alifungua campun ya vifaa vya magari na hii campuni ilikwa ya watu wawili edo pamoja na baba yake mdogo pam, edo ndiye alikuwa akisafiri mara kwa mara kwenda malaysia kuchukua vifaa vya campuni yao.. Ehee sasa kama edo na pam ni ndugu ilikuwaje hadi pam amzunguke edo na kwenda kumuambukiza lilian h.i.v
.. Kuwa makini sasa hapa kuelewa jinsi ilivyo kuwa.. Jioni moja edo akiwa na baba mdogo wake walikuwa wakiongelea kuhusu lilian edo alimweleza pam mambo mengi sana kuhusu lilian jinsi alivyo mnyima papuch kwa miaka zaidi ya mitatu. Na jinsi ambavyo lilian ni mwaminifu na kuwa hata iweje liliani asingeweze kuwa na mwanaume mwingine zaidi yake.. Pam alicheka sana na alimuahidi edo kuwa ampe mwezi mmoja tu atakuwa amesha maliza mamboo.. Kwaiyo dili lilichezwa kati ya edo, pam, na room mate wa liliani ( kwahiyo yote yaliyotokea ni game?) ndiyo! Unakumbuka siku ile ambayo ilikuwa ni birthday ya lilian.. (Tazama visuri hii scine hapa ndipo movie inapochanganya siku iyo ilikuwa hivi) early that day.. Edo vipii? Pam hapa leo ndiyo inatakiwa tukamalize game letu.... sawa wapii? Nimeshaanda venue kwahiyo kama tulivyokubaliana mimi nitamnywesha alafu baadye sana akiwa amechoka na taa kuzimwa wewe utakuja kumaliza na asubuhi sana nitakuja...
poa kaka basi fanya hivyoo. Siku hiyo jioni edo alikuja na alimwingila lilian na kuutoa usichana wake.. Baada ya kumaliza shughuli hiyo ndiyo siku ambayo edo anakumbuka aliwahi kulia kuliko siku zote .. Inamaaana kweli lili anaweza kunisalitii hapana sikubalii lazima nimwonyeshe mimi ni nani lazima nimwonyeshee kuwa alicho kifanya ni kosa la kujutia.. (mtazame edo eti baada ya kumwingilia lili aliapa kwakosa lili alilofanya lazima amfanye alie na kusaga meno) siku hiyo pam na edo walipanga kuwa wamtumie mpenzi wake na pam ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye hospitali ya binafsi tabata kufeki majibu nakweli tunaona ilikuja kufanikiwa.. Kama unakumbuka siku mbili tu baada ya lile tukio edo alitokea kama sapuraizi na kama unakumbuka edo pale hotelin alikataaa kabisa pale lili alipompa papuchi hata baada ya kumwambiaa kuwa bado yupo nabikiraa yaani sildi.. Na aling'ang'ania kuwa lazima akapime..
Kwahiyo sasa kumbe zile ishu zote za edo kutumiwa email, kwenda kusoma chuoni malysia zilikuwa ni dilii.. Mhuuuu twende hii scene nyingine ya ambayo inaweza inaweza ikawa inakuchanganya. Edo anaelewa kila kinachoendelea kwa lili na hadi alipo lakini kwanini edoo amuache lilian aendelee kuteseka kiasi kile na hata kuahirisha masomo.. Je edo yupo wapi kwasasa .. Je mipango ya edo kwa lili ni ipii ... Malizia mwenyewe ndugu msomaji mimi sina kipaji cha uandishi wa hadithi alafu pia mimi ni mvivu sana wakuandika
nihayo tu najua kila mmoja anatamani ingekuwa hivi alafu wewe jamaa habari za kukaa wiki mbimbili uache
 
  • Thanks
Reactions: ram
Inaedeleeaa... Kibishi ngoja niimalize
edo baada ya kumaliza chuo alifungua campun ya vifaa vya magari na hii campuni ilikwa ya watu wawili edo pamoja na baba yake mdogo pam, edo ndiye alikuwa akisafiri mara kwa mara kwenda malaysia kuchukua vifaa vya campuni yao.. Ehee sasa kama edo na pam ni ndugu ilikuwaje hadi pam amzunguke edo na kwenda kumuambukiza lilian h.i.v
.. Kuwa makini sasa hapa kuelewa jinsi ilivyo kuwa.. Jioni moja edo akiwa na baba mdogo wake walikuwa wakiongelea kuhusu lilian edo alimweleza pam mambo mengi sana kuhusu lilian jinsi alivyo mnyima papuch kwa miaka zaidi ya mitatu. Na jinsi ambavyo lilian ni mwaminifu na kuwa hata iweje liliani asingeweze kuwa na mwanaume mwingine zaidi yake.. Pam alicheka sana na alimuahidi edo kuwa ampe mwezi mmoja tu atakuwa amesha maliza mamboo.. Kwaiyo dili lilichezwa kati ya edo, pam, na room mate wa liliani ( kwahiyo yote yaliyotokea ni game?) ndiyo! Unakumbuka siku ile ambayo ilikuwa ni birthday ya lilian.. (Tazama visuri hii scine hapa ndipo movie inapochanganya siku iyo ilikuwa hivi) early that day.. Edo vipii? Pam hapa leo ndiyo inatakiwa tukamalize game letu.... sawa wapii? Nimeshaanda venue kwahiyo kama tulivyokubaliana mimi nitamnywesha alafu baadye sana akiwa amechoka na taa kuzimwa wewe utakuja kumaliza na asubuhi sana nitakuja...
poa kaka basi fanya hivyoo. Siku hiyo jioni edo alikuja na alimwingila lilian na kuutoa usichana wake.. Baada ya kumaliza shughuli hiyo ndiyo siku ambayo edo anakumbuka aliwahi kulia kuliko siku zote .. Inamaaana kweli lili anaweza kunisalitii hapana sikubalii lazima nimwonyeshe mimi ni nani lazima nimwonyeshee kuwa alicho kifanya ni kosa la kujutia.. (mtazame edo eti baada ya kumwingilia lili aliapa kwakosa lili alilofanya lazima amfanye alie na kusaga meno) siku hiyo pam na edo walipanga kuwa wamtumie mpenzi wake na pam ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye hospitali ya binafsi tabata kufeki majibu nakweli tunaona ilikuja kufanikiwa.. Kama unakumbuka siku mbili tu baada ya lile tukio edo alitokea kama sapuraizi na kama unakumbuka edo pale hotelin alikataaa kabisa pale lili alipompa papuchi hata baada ya kumwambiaa kuwa bado yupo nabikiraa yaani sildi.. Na aling'ang'ania kuwa lazima akapime..
Kwahiyo sasa kumbe zile ishu zote za edo kutumiwa email, kwenda kusoma chuoni malysia zilikuwa ni dilii.. Mhuuuu twende hii scene nyingine ya ambayo inaweza inaweza ikawa inakuchanganya. Edo anaelewa kila kinachoendelea kwa lili na hadi alipo lakini kwanini edoo amuache lilian aendelee kuteseka kiasi kile na hata kuahirisha masomo.. Je edo yupo wapi kwasasa .. Je mipango ya edo kwa lili ni ipii ... Malizia mwenyewe ndugu msomaji mimi sina kipaji cha uandishi wa hadithi alafu pia mimi ni mvivu sana wakuandika
nihayo tu najua kila mmoja anatamani ingekuwa hivi alafu wewe jamaa habari za kukaa wiki mbimbili uache

hahahhahaha we jamaa hapo mwisho nimecheka sana
 
ILIPOISHIA...
Juliana hakujua kilichokuwa ndani ya moyo wa shangazi yake. Alichukulia suala lake kama uzembe tu wa fikra katika uhusiano. Laiti angeingia moyoni mwake na kujua siri aliyokuwa nayo!
Angejua!!!
SASA ENDELEA...

SIRI ilitulia ndani ya moyo wa Lilian. Aliificha ndani ya kifua chake na hakuwa tayari hata kidogo kufungua kinywa chake kueleza ukweli.
Alijua ni kwa namna gani angejizidishia mateso ya kihisia ndani ya moyo wake. Alibaki kuwa mwenye mawazo lakini akijiapiza kufa na siri hiyo moyoni mwake.
“Anti,” akaita Lilian.
“Unasemaje? Una nini kipya cha kuniambia?” sasa Juliana alionekana dhahiri kuwa na hasira isiyo na kifani.
“Usinifanyie hivyo anti.”
“Ni kitu gani nisichokijua kuhusu mapenzi? Kipi kigeni kwangu kuhusu uhusiano? Najua kila kitu, ndiyo maana nakushangaa, eti unakuwa tayari kuhairisha mwaka wako wa masomo kwa sababu kuna mpumbavu tu amekuvuruga.
“Sikia... wewe una maisha yako, yeye naye ana maisha yake. Si mume wako huyo. Ingekuwa mmeoana, labda ungepaswa kuumia lakini boyfriend tu. Hebu get serious bwana. Sitaki kusikia upuuzi wako hapa,” akasema tena anti yake kwa hasira ileile.
Lilian akamwaga machozi!
Ilikuwa ni haki yake kulia. Afanye nini sasa? Amwambie ukweli? Nani kasema?
“Siwezi kusema, itakuwa tatizo mara mbili ya hivi, lazima nitumie akili zaidi,” akawaza Lilian.
Juliana alijaribu kuzungumza kama mzazi, akichukua nafasi ya kaka yake, kumshauri Lilian akiwa hajui kabisa kuwa nguvu aliyokuwa akiitumia ilikuwa siyo mahali pake. Hilo hakulijua kabisa.
“Nina ombi moja kwako anti.”
“Ndiyo.”
“Naomba nikae hapa kwa wiki mbili tu nikitafakari, kisha nitakujibu cha kufanya.”
Juliana alikaa kimya kwa muda.
Alionekana amezama kwenye tafakuri ya muda akimfikiria shangazi yake. Kidogo ombi lile lilionekana kumwingia.
“Na ninataka iwe wiki mbili kweli. Sikia... sina tatizo lolote kwa wewe kuishi hapa kwangu. Nina nyumba kubwa, kuna kila kitu ndani. Utakula, utalala, utavaa na kufanya kila kitu. Kwa hiki Mungu alichonijalia, sina tatizo kabisa ndugu zangu wakikitumia.
“Lakini kumbuka, naumizwa na uamuzi wako. Sitaki kuona mapenzi yanaharibu maisha yako. Umeshapita vizingiti vingi Lilian. Kwa nini uje kuharibu mwishoni?”
“Nakuelewa anti, najua ni kwa kiasi gani unaumia, nisamehe tafadhali.”
“Yamekwisha.”
“Ahsante shangazi,” akajibu Lilian alijitahidi kuachia tabasamu usoni mwake.
Tabasamu lilikuwa zito lakini kwa sababu ya vijishimo mashavuni mwake, liliweza kuonekana sawasawa.
***
Kutokana na upweke mara nyingi alipenda kwenda kushinda kwenye saluni ya kike iliyokuwa jirani na nyumbani kwa shangazi yake. Alipenda kwenda pale kwa sababu ya ucheshi wa dada aliyekuwa akihudumia katika saluni hiyo.
Aliitwa Maimuna lakini rafiki zake walimkatishia na kumwita Mai. Alikuwa msichana mrembo kwelikweli. Mwenye kila kitu kizuri mwilini mwake. Nyama za mwili wake zilikuwa zimeshikana vyema.
Alikuwa mrefu kiasi, mwenye shepu sawasawa, umbo likionekana kufanana kabisa na tarakimu namba nane. Alikuwa na makalio makubwa. Hipsi pana, miguu minene, mizuri na kiuno chembamba kama cha nyigu!
Kifupi alikuwa mrembo kupitiliza. Pamoja na urembo wake, hakuwahi kuonekana akiwa karibu na wanaume. Wanaume wengi mtaani walimmezea mate. Wenye roho za kupenda haraka, walijaribu kutupa ndoano zao, wakaambulia patupu!
Mai alikuwa na msimamo sana!
Urafiki wake na Mai ulishamiri kwa wiki moja tu. Lakini Mai hakufurahishwa na ukimya kupitiliza wa shoga yake. Kwa alivyomuona, haraka sana aligundua alikuwa kwenye tatizo kubwa ambalo hakutaka kumshirikisha mtu.
Leo hii hayupo tayari kumuona shoga yake akiendelea kuwa mwenye mawazo wakati yeye yupo. Wakiwa wawili tu saluni, mchana huu. Mai ameamua kuvunja ukimya.
“Lilian...” akaita Mai.
“Abee...”
“Mimi ni rafiki yako siyo?”
“Ndiyo.”
“Tunaaminiana siyo?”
“Hakika.”
“Kwa ninavyokuona, naona una mzigo wa mawazo. Kuna kitu kinakusumbua na kinakutesa, lakini kwa bahati mbaya, inaonekana huna mpango wa kumweleza mtu yeyote jambo hilo.
“Sidhani kama uamuzi huo ni sahihi. Acha kujikondesha mtoto wa kike. Mimi ni shoga’ko kama ulivyosema na umesema unaniamini, nakuamini pia. So please, tell me, what’s wrong with you my dear?” akasema Mai kwa sauti tulivu, yenye kusihi na ushawishi wa hali ya juu.
Kama Mai angesomea masomo ya saikolojia, bila ya shaka angeifanya kazi hiyo kwa ubora wa hali ya juu sana. Aliweza kuwa mshauri mzuri.
“Mbona hakuna tatizo? Nipo sawa kabisa Mai, I’m absolutely okay, nothing wrong with me... please be happy my sister,” akasema Lilian akitengeneza tabasamu ambalo Mai aliligundua haraka kuwa halikuwa halisi.
“Your smile is not real Lilian. Tafadhali niambie, unasumbuliwa na nini? Nipo hapa kwa ajili yako,” akasema Mai kwa sauti tulivu.
“Let me tell you the truth... it’s true that a have a big problem. Angalia....” akasema Lilian machozi yakimlenga, huku akijionyesha mwili wake kwa Mai.
“I’m HIV Positive.... you think what is next to me? I’m finished Mai. I’m nothing....” (Nina virusi vya ukimwi... unafikiri nini kinafuata? Nimekwisha Mai. Mimi si lolote...).
“Hapana... pole sana kwa kusumbuliwa na tatizo kubwa kihisia lakini lisilo kubwa kinadharia. Tuliza moyo. Ishu yako ni ndogo sana...” akasema Mai.
“Unamaanisha nini? Kuwa na ukimwi ni tatizo dogo?”
“Matatizo ni matatizo tu Lilian, ila ukimwi umepewa sifa ya kuwa tatizo kubwa, lakini si kweli. Ngoja... nitakuambia ukweli leo na nitakusaidia uishi maisha safi. Subiri kidogo,” akasema Mai akifuata pochi yake.
Aliporejea, alikuwa na simu. Akaonekana akitafuta kitu katika simu yake, kisha akamkabidhi Lilian. Juu ya kioo cha simu hiyo, kulikuwa na mwanaume mtu mzima, amesimama kando ya gari la kifahari.
“Ni nani huyu? Na kwa nini umenionyesha hii picha?” akauliza Lilian.
“Huyu ni Sadick Kisummi. Ni marehemu kwa sasa. Amefariki miaka nane iliyopita. Mwaka mmoja baadaye, alifuata mkewe. Alikuwa mpenzi wangu. Huyu ndiye chanzo cha matatizo yangu. Ndiyo sababu mpaka sasa sihitaji kuolewa.
“Mzee Kisummi alinipa ukimwi. Hivi ninavyozungumza na wewe, ninaishi na virusi vya ukimwi takribani miaka kumi sasa. Awali niliogopa kama wewe, niliishi kwa mawazo na mashaka kama wewe, lakini kumbe nilikuwa najiumiza tu. Yupo sista anaweza kukusaidia.
“Utaishi kwa amani na utarudi kwenye masomo yako kama kawaida. Kifupi utakuwa Lilian mpya, pengine mwenye furaha zaidi kuliko Lilian ninayezungumza naye sasa hivi hapa.”
“Kweli?”
“Kabisa.”
Lilian akatabasamu!
Mwanga wa maisha mapya ukafunguka. Alimwamini sana Mai. Alimsogelea na kumvutia kwake. Wakakumbatiana.
Machozi hayakuwa hiyari yake tena, yakamwagika kama maji! Mashavu yake yakawa tepetepe!
Je, nini kitatokea? Usikose kufuatilia.
 
Ahsante Mommadou Keita1 But unapotea sana mkuu hadi simulizi inakosa mvuto
Jitahidi kutuwekea angalau kwa siku mara moja, simulizi imeanza mwezi wa April hadi leo Momma..... please!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom