nameless girl
JF-Expert Member
- Apr 22, 2012
- 4,195
- 2,685
- Thread starter
- #161
taratibu na Powel mwingine kuingia ghafla kama kivuli na kuketi kwenye kiti kilichomuelekea Kombora.
Kombora alimfikiria kama Powel mwingine, kwa jinsi walivyofanana kimaumbile na kimavazi.Yeye pia alikuwa ameungua uso na sehemu mbalimbali za mikono yake. Yeye pia alikuwa na jicho moja, ingawaje lake lililoungua lilikuwa wazi nyuma ya kovu kana kwamba linaona. Badala ya mkono wa bandia yeye alikuwa na mguu mmoja wa mbao. Hilo Kombora aliligundua wakati alipoukunja kwa mikono yake yote miwili pindi akiketi chini, vinginevyo isingekuwa rahisi kugundua.
Powel aliyaona macho ya Kombora yakitembelea uso huu hadi ule kana kwamba yanadai maelezo. Kwa sauti ilelile inayocheka Powel alisema, “Watu wengi wanasema tumefanana. Wengine wanadhani tu mapacha. Lakini wanakosea sana. Hatujafanana hata kidogo. Ukishatuzoea, utagundua kuwa huyu mwenzangu ni mrefu kuliko mimi, mnene kuliko mimi.” Alipoona maelezo hayo hayajamridhisha Kombora aliongeza, “ kinachotufanya tufikiriwe ndugu ni haya masahibu yaliyotukuta, siku moja, saa moja, kwa bomu moja. Ilikuwa tufe pamoja, kwa bahati mungu alitunusuru pamoja. Tungeweza kuwa ombaomba barabarani, lakini mungu ametusaidia vilevile na kutuwezesha kuwa wafanyabiashara wakubwa duniani…”
“Hujaniambia mwenzako anaitwa nani,” Kombora alimkatiza
“Oh kweli anaitwa Philip Benjamin. Yeye ni Mkurugenzi wa Fedha” alimgeukia mwenzake huyo na kumwambia, “Philip, huyu hapa ni Inspekta Kombora bila shaka umepata kumsikia”
Philip alitikisa kichwa kukubali.
Powel aliendelea “Inspekta Kombora anadhani kuna mwizi ambaye amejificha katika jengo hili. Unadhani inawezekana Philip?”
Badala ya kujibu Philip aliangua kicheko.
“Unaona Inspekta? Unapoteza muda wako bure.”
Kombora alianza kupandwa na hasira juu ya watu hawa. Aliona wazi kuwa ama walikuwa punguani wa akili kama ilivyokuwa kwa baadhi ya viungo vyao, ama walikuwa wakimdhihaki. Akaamua kucheza mchezo waliotaka wao. Aliinuka akawashukuru na kutoka nje huku akihisi kila jicho linaloona, la kila mmoja kati yao, likiwa limemganda mgongoni huku linamcheka.
Alipanda gari na kuamuru liondoke. Baada ya kupinda kona moja alisimamisha gari na kumwamuru kachero mmoja arejee na kutafuta uwezekano wa kuilinda ofisi hiyo kwa makini bila ya yeye mwenyewe kuonekana.
11
Ilikaribia saa kumi na mbili Kombora aliporejea ofisini kwake kama mgonjwa aliyeruhusiwa kutoka hospitali baada ya kukata tamaa ya kuendelea kuishi. Alijibweteka juu ya kiti chake na kujiinamia kwa muda, mikono yake yote miwili ikiwa imekilea kichwa chake.
‘Msichana mzuri, asiye na hatia yuko mikononi mwa muuaji wa hatari, aliwaza kwa uchungu, mbele ya macho yangu mwenyewe jambazi huyohuyo ameua watu wawili wasio na hatia… Na ametoweka…mbele ya macho yangu mwenyewe. Mimi … ambaye najiita mkuu wa kikosi hiki…’ alishindwa kuendelea kufikiri. Hasira zilikuwa zimefura katika kichwa chake kiasi cha kufanya ubongo wake ukitishia kuchemka. ‘Lazima nitunze kichwa changu,’ alinong’ona kimoyomoyo huku akiiitoa mikono yake kichwani na kuipeleka mezani ambako ilirudi na faili ambalo hakulihitaji. Alilitupa mezani hapo na kuiingiza mikono mfukoni ambamo alitoka na kile kijitabu cha maelezo ya kampuni ya Kangaroo. Alikipekuapekua kwa dakika chache kabla hajainua simu na kumpigia mmoja wa wasaidizi wake, ambaye alifika mbele yake mara moja na kupiga saluti ambayo haikujibiwa.
“Fanya kila unaloweza nipate taarifa za kampuni hiyo kabla ya saa mbili,” alimwamuru akimwonyesha kijitabu hicho. “Nataka kujua imeanzishwa lini na wapi, hapa nchini imeingia lini, nani hasa mwenye kampuni hiyo, shughuli zake hasa ni zipi na kila unachoweza kupata. Zaidi, jitahidi nipate kila ambalo linaweza kupatikana juu ya wakurugenzi wake wawili walioko hapa, Paul Powel na Philip Benjamin. Tumia watu wote unaoweza kuwapata. Upo?
“Nipo afande.”
“Haya! Bado unasubiri nini zaidi?”
Amri ya pili ambayo Kombora aliitoa na kumtaka Sajin Kangura mwenyewe kuhakikisha inatekelezwa mara moja ni ile ya kupata ramani ya majengo ya Sunrise Modern Club na Kangaroo Enterprises katika muda wa saa mbili.
“Ni zaidi ya saa mbili sasa, afande. Ofisi ya Ardhi na jiji zitakuwa zimefungwa…”
“Zinaweza kufunguliwa. Kama wanaohusika hawapatikani mtafute waziri wao azifungue. Na kama hana funguo mwambie azivunje.”
“Ndiyo, afande.”
Kombora alipobaki peke yake alijaribu tena kukisoma kijitabu cha maelezo ya kampuni ya Kangaroo. Maelezo yalikuwa mengi, marefu yaliyowekwa katika mpangilio ambao ungemfanya msomaji yeyote ahisi kuwa kampuni hiyo ilikuwa moja ya makampuni makubwa sana duniani. Yalitaja matawi yake katikasehemu mbalimbali za dunia. Hata hivyo, ilimshangaza Kombora kuona kuwa anuani za matawi hayo hazikutajwa wala makao makuu, ambayo yalidaiwa kuwa yako New York, Marekani. Hali kadhalika, zaidi ya Powel na Philip, kijitabu hicho hakikuwa na jina jingine la Mkurugenzi yeyote.
Hayo yaliyoongeza mashaka ya Kombora juu ya kampuni hiyo, mashaka ambayo yalianza tangu alipowatia machoni wakurugenzi hao wawili, ambao pamoja na kutojiweza kwao hawakuonekana kuwa na lugha ya biashara hata chembe. Kwa ujumla, Kombora hakuwaona kama wafanyabiashara. ‘Kama wanafanya biashara, lazima biashara hizo zitakuwa haramu,’ aliwaza. ‘Si biashara walizoziorodhesha hapa.’
Kombora alijua ambacho angefanya kesho. Alijua kuwa angehitajika kuwataka msaada polisi wa kimataifa, Interpol, toka nchi zote ambazo Kangaroo ilizitaja kuwa ina matawi yake na kumwomba juu ya uhalali wa makampuni hayo, biashara halisi wanazozifanya na taarifa kamili za wakurugenzi wake.
Hilo lilikuwa la kesho. La leo ambalo lilikuwa likimsumbua Kombora na ambalo lisingesubiri kesho lilikuwa la kumtoa Nuru mikononi mwa Kakakuona, akiwa hai. Alitazama saa yake na kuona ikikaribia moja na nusu usiku; lakini hajapata bado jibu toka kwa watu aliowataarifu kupata taarifa za Kangaroo, jengo lao na lile la Sunrise. ‘Wako wapi hawa’ alinung’una akiinua uso wake kutazama mlangoni.
Juu ya meza yake Kombora alishukuru kuona kuwa mtu mmoja alimwekea chupa ya chai au kahawa na mayai matatu ya kuchemsha. Ndio kwanza akahisi kuwa alikuwa na njaa kali. Akavunja yai moja na kulitafuna. Yai la pili vilevile alilila kavukavu. La tatu ndilo aliloshusha kwa chai nzito ya maziwa toka katika chupa. Baadaye, aliinuka na kuukamilisha mlo wake kwa glasi mbili za maji toka katika friji yake ndogo ya ofisini. Wakati akirudi mezani simu ililia. Kombora aliinyakua na kuidaka masikioni mwake.
“Afande, Kabweka hapa.”
“Najua, uko wapi?”
“Napiga toka bandarini, nilikuwa katika kuhakikisha kama kweli hawa Kangaroo wanaingiza vitu toka nje.”
“Enhe!”
“Ni waingizaji maarufu wa vitu vya nje, Mzee, nimeona mizigo yao mingi ambayo haijatolewa. Nimeambiwa pia kuwa safari hii wamekodi meli mbili. Moja inatarajiwa kuanza kushusha mali zao wakati wowote. Ya pili haijapata nafasi ya kuingia bandarini, imetia nanga nje kidogo ya pwani.”
Hazikuwa habari nzuri sana kwa Kombora. “Ni hayo tu uliyoyapata?” Kombora aliuliza akitaka kuthibitisha kama hakukuwa na habari nzuri zaidi.
“Ndiyo mzee, lakini…”
“Lakini nini?”
“Kuna jambo moja ambalo limenitatanisha.”
“Lipi?”
“Hawa wakurugenzi wake. Idara yetu inayoshughulikia taarifa za wageni haina lolote kabisa juu ya Philip na Powel. Hakuna kinachofahamika zaidi ya kuwa ni raia wa Urusi ambao walikwenda Angola kuwasaidia wazalendo dhidi ya Wareno, wakati walipokuwa wakipigania uhuru wao. Taarifa hizo hazionyeshi maisha yao huko Urusi, waliondoka lini na walikuwa wakipigana kikosi kipi. Zinaonyesha kuwa MPLA tayari wameulizwa juu ya watu hawa na wakashindwa kutoa majibu. Wanasema kwa kuwa watu wengi vitani hupenda kutumia majina ya bandia huenda watu hao walishiriki. Urusi nako, kikosi chao cha KGBkimesema hakina majina hayo katika kumbukumbu zao.”
Kombora alimsikiliza kwa makini, “Kwa hiyo, unawafikiriaje watu hawa, Kabweka?” Kombora alimwambia.
“Nahisi kuna kitu wanaficha na kuna kitu zaidi wanafanya. Inawezekana hawa ni wanachama wa kikundi cha Mafia ambao wanajishughulisha na biashara haramu za dawa za kulevya au nyara za serikali,” alieleza na kuongeza kwa sauti ya kujiamini. “Inawezekana mzee, hawa ni maadui wa Joram Kiango.”
“Ahsante kwa mchango wako. Endelea na usikose kuniarifu kila utakapopata kitu kipya,” Kombora alisema akiitua simu chini.
Papo hapo ikaita tena. Safari hii aliyepiga alikuwa Sajin Kangura. Alikuwa akipiga toka Halmashauri ya jiji. Alimwarifu Kombora habari ambazo zilimsisimua zaidi. “Inashangaza, afande. Si wizara ya Ardhi wala jiji ambao wana nakala ya ramani ya majengo hayo yote mawili.”
“Kwanini?”
“Haieleweki. Jiji wanadai kuwa wana hakika walikuwa na nakala za majengo hayo lakini hawazioni. Hata hivyo, mmoja wa maafisa wa jiji ananieleza kuwa jengo la Sunrise lilikuwa dogo la ghorofa moja lakini liliibuka ghafla na kupanuliwa hata kabla ya kukamilisha taratibu za ujenzi. Kuwa waliingia katika mgogoro na mwenye jengo hilo ambapo baadae ulitatuliwa na akaruhusiwa kundelea.”
“Hamkuweza kumpata mwenye jengo hili awapeni ramani hiyo?” Kombora alimwuliza.
“Yeye pia yalimkuta makubwa,” Kombora aliambiwa “Inadaiwa kuwa huu mwaka wa tatu tangu alipotoweka”
“Katoweka!”
“Ndiyo, afande. Tumeambiwa kuwa bwana huyo, Fabian Kalila, ambaye alikuwa maarufu kwa ujenzi mara tu baada ya kukamilisha jengo hilo la Sunrise aliaga siku moja kuwa anakwenda Kigamboni kukagua uwanja mpya ambao ulihitajiwa kujengwa nyumba ya pili. Bwana huyo alifika hadi Ferry ambapo alionekana akizungumza na watu anaofahamiana naye.Watu waliomwona kwa mara ya mwisho walidai alipanda na kwenda ng’ambo. Lakini huko ng’ambo hakuna aliyemwona, yametolewa matangazo magazetini na maredioni lakini hazijafika taarifa zozote juu yake, wala maiti yake.”
“Naam, iko namna,” Kombora aliropoka kwa namna ya mtu anayezungumza peke yake.
Kangura alikuwa akiendelea, “pamoja na hayo, afande, tumefanya upekuzi mkubwa katika makabrasha yake yote, tumeweza kuona karibu nakala za majengo yote aliyowahi kushughulikia isipokuwa hili la Sunrise na Kangaroo. Hatukuweza kupata hata zile za majaribio.”
“Ni yeye aliyeshughulikia jengo lile pia?”
“Ndio, afande”
Kombora hakujua afanye nini zaidi. Alichanganyikiwa kupita kiasi. Kwa ujumla, hakujua kama anakwenda mbele au anarudi nyuma katika suala hilo. Alitua simu chini bila kusema neno lolote zaidi.
***
Mtu mwingine aliyekuwa jengo Fulani mtaa fulani, wa jijini hapo, baada ya kuyasikiliza maongezi hayo ya Kombora na wasaidizi wake aliitua simu yake chini taratibu. Kisha, akakichunguza chombo chake cha kunasia sauti kuona kama kilikuwa kinafanya kazi vizuri.
“Not so bad” alitamka, akitabasamu. Aliitoa kanda hiyo na kuitia mfukoni mwake. Akategesha upya chombo chake na kisha kuondoka zake toka chumbani humo, tabasamu likiwa bado usoni mwake.
***
Mtaa wa tatu toka hapa mtu mwingine alikuwa akitabasamu. Lakini hili lilikuwa tabasamu lake la kwanza kwa siku hiyo, na pengine kwa wiki hiyo. Mtu huyo aliitwa Joram Kiango.
Kama ungemtazama harakaharaka alivyoketi juu ya kochi, ndani ya chumba alichokodi katika hoteli hii ya Mawenzi usingemfikiria kabisa kuwa alikuwa na tatizo kubwa la kutisha ambalo lingetosha kabisa kumtia kichaa. Badala yake ungemwona kijana mtanashati, aliyevaa suti yake nyeusi iliyomkubali vilivyo; akiwa ameketi juu ya kochi pana glasi ya wiski ikiwa mbele yake, sigara mkono mmoja na simu mkono wa pili.
Hali hii ilimrejea joram baada ya kujiaminisha tena na tena kuwa alihitaji kutuliza kichwa chake ili kupambana kikamilifu na janga hilo. ‘wewe ni Joram Kiango’ nafsi yake ilimwambia, ‘Endelea kuwa Joram Kiango vinginevyo Nuru utampoteza na maisha yako yatapotea.’
Hakujali sana juu ya maisha yake lakini alipomkumbuka Nuru na ukatili wa watu wanaomshikilia, alituliza akili yake na kuwa Joram Kiango. Na kwa mshangao wake alikuta akili yake ikichemka kwa ukamilifu kama betri zilizochajiwa upya.
Aliwakumbuka marafiki zake wote, wa nje na ndani. Namba zao za simu teleksi na faksi ziliibuka kama chemichemi akilini mwake. Akiwa na pesa za kutosha haikumchukua muda kukifanya chumba hicho kidogo kigeuke ofisi kubwa ya mawasiliano ambayo yalitoka huku na huko.
Simu yake ya kwanza ilimwendea rafiki yake mmoja anayemiliki kampuni yake binafsi jijini. Huyu akiwa ni mtu ambaye kila kitu kwake ni biashara, alikuwa anafahamu kila mtu na kila kampuni jijini Dar es Salaam. Hivyo, Joram alipomwuliza anafahamu nini juu ya Kangaroo Enterprises rafiki yake aliangua kicheko.
“Vipi? Sioni kama jina hilo linachekesha,” Jorama alimsaliti.
“Sio jina braza, ni pesa” Sauti ilijibu toka upande wa pili.
“Pesa?”
“Pesa hazina macho,” alieleza na kuongeza “pesa, kwa kweli mara nyingine inapotea njia.”
“Sijakuelewa?” Joram alimkumbusha.
“Kwani hujawaona wakurugenzi wa kampuni hiyo?”
“Wakurugenzi gani?”
“Powel na Philip.”
“Wanakasoro gani?”
“Swali sio wana kasoro gani , ila kasoro gani hawana” kicheko “Wale mabwana ukiwaona utafikiri pacha. Wenyewe wanadai hawana undugu wowote. Ukiwaona utadhani ndio kwanza wanaibuka toka kaburini; utafikiri waliwekwa katika pipa wakachemshwa na kisha kutolewa kabla ya kukata roho. Mmoja ni nusu kipofu asiye na mkono wa pili, mwingine nadhani kiziwi na hana mkono mmoja. Kwakweli mabwana wale ni watu wa kuchekesha sana.”
“Sioni wamewezaje kupata pesa,” Joram alichochea.
Baada ya maswali mengi alibaini kuwa kampuni ya Kangaroo Enterprises ni mpya inayoongozwa na watu wasiojiweza, Paul powel na Philip Benjamin. Pamoja na kwamba kampuni hiyo ilidai inajishughulisha na mambo mengi, lakini taarifa alizozipata ni kuwa kazi kubwa ambayo kampuni hiyo imekwishafanya ni uingizaji wa pickup, bidhaa toka nje na kuzisambaza kwa wauzaji mbalimbali wa jumla jijini. Bidhaa yao kubwa, Joram aliarifiwa, ni vipodozi vya aina kwa aina, hasa kwa kina mama.
Alifahamishwa kuwa kampuni hiyo ilijenga maghara yake kando ya barabara ya Nelson Mandela katika eneo la Tabata.
Joram alimshukuru rafiki huyo na kumtaka amwarifu kila atakachokipata juu ya wakurugenzi hao wawili.
Rafiki yake mwingine alikuwa miongoni mwa vijana wa Inspekta Kombora. Kila alipopata wasaa aliwatoroka wenzake na kumdokeza Joram juu ya kila tukio. Alimfahamisha jinsi ambavyo Inspekta Kombora alikuwa taabani baada ya watu wawili wasio na hatia kuuawa mbele yake na Nuru kutoweka mbele ya macho yake. Aidha, alimfahamisha juu ya harakati zote ambazo zilifanyika kulikagua jengo hilo na majengo yote ya jirani bila mafanikio yoyote.
“Sasa hivi ukimwona mzee Kombora utadhani ana umri wa miaka mia moja, kwa jinsi alivyozeeka ghafla,” Rafiki huyo alidokeza katika maongezi hayo.
Baada ya Joram kuuliza kwa makini ukubwa wa jengo la Sunrise Modern Club, Kangaroo Enterprises zilivyojengwa ndani na nje, sehemu ambayo Kakakuona alimwua dereva wa taksi na alipomwua msichana wa mapokezi, na mengine mengi, alipatiwa majibu yote aliyoyahitaji kwa kiwango cha kuridhisha. Maelezo hayo yalifuatwa na onyo, “Joram kama unakusudia kufuata nyayo za Kakakuona, lazima ujihadhari sana. Huyu sio mtu wa kawaida. Mambo aliyoyafanya hapa ambayo nimeyaona kwa macho yangu sio mambo ya kawaida. Labda tunayoona katika filamu baada ya watu wa studio kuweka utaalamu wao. Huyu si binadamu ningekushauri ufikirie mara mbili.”
Ni hilo ambalo lilimfanya Joram atabasamu kwa mara ya kwanza siku hiyo. Yalimchekesha mengi. Moja likiwa lile la kujua kuwa nje ya maadui, ni yeye peke yake ambaye alifahamu kuwa Kakakuona hayuko duniani tena. Jingine alipoona rafiki yake huyo asivyomwelewa kikamilifu kwa kumtahadharisha kumfuata Kakakuona. Laiti angejua kuwa alikuwa tayari kumfata hadi kuzimu, na kuhakikisha akirejea na Nuru, akiwa hai au salama! Hata hivyo, Joram alimshukuru rafiki huyo na kumtaka aendelee kuwa macho.
Joram alipata msaada mkubwa zaidi toka kwa rafiki yake mmoja wa kampuni ya simu. Huyu, alimwezesha kupata moja kwa moja mawasiliano yote ya simu yaliyokuwa yakiendelea katika ofisi ya Kombora kwa kuiunganisha na laini moja ya hoteli ambayo Joram aliikodi kwa bei mbaya.
Mawasiliano hayo yalimpunguzia Joram kazi kwa kiasi kikubwa. Hakuhitaji tena kujishughulisha na uraia wa watu hao kwa wakati huo kutokana maongezi baina ya Kombora na msaidizi wake. Hakuwa na haja tena ya kutafuta ramani ya majengo hayo wala ujenzi wake kutokana na taarifa hizohizo. Hali kadhalika, asingepoteza muda wa kutafuta habari za kampuni hiyo huko nje kwani tayari ilionyesha kuwa taarifa zao sio za kweli. Zaidi, Joram hakuwa na wasiwasi juu ya Nuru kuhamishwa toka jengo hilo kwa kujua kuwa vijana wa Kombora walikuwa wakilinda doria na kumtaarifu juu ya kila tukio lililotendeka, taarifa ambazo yeye pia alikuwa akizipata.
Kitu ambacho kwa sasa kilisumbua sana akili ya Joram Kiango kilikuwa kushindwa kuoanisha maelezo juu ya maumbile ya wakurugenzi hao wa Kangaroo na mkasa huu mzima. Kama kweli ni watu wasiojiweza,wenye biashara zao halali, vipi wajihusishe na ujasusi huo wa kimachomacho? Watakuwa wanajiamini nini?
Kitendo chao cha kumteketeza Kakakuona hata kabla hajakamilisha jukumu alilopewa pia lilimtatiza. Kama wangemwua Kakakuona na kisha kumwachia Nuru angeweza kuelewa. Ingekuwa ishara ya kukubali kushindwa. Lakini kumwua Kakakuona, na kuendelea kumshikilia Nuru kwa vyovyote vile ni dalili ya kutangaza shari zaidi, shari ambayo kwa maumbile yao yalivyo, wasingeweza kuitekeleza bila msaada wa mtu mwingine mwenye uwezo na akili timamu zaidi ya Kakakuona.
Joram alihitaji kumfahamu mtu huyo kwa gharama yoyote ile kwani ni yeye tu aliyekuwa kipingamizi baina yake na Nuru. Vinginevyo, angeweza kwenda zake, mchana kweupe, na kumpokonya Nuru toka mikononi mwao.
Simu ililia. Akaipokea na kuisikiliza, kisha akaitua, haikuwa na kitu cha muhimu.
Teksi ikapata uhai. Taarifa ilitoka katika tawi moja wapo la NBC mjini hapo, ilimtajia namba ya akaunti ya Kangaroo Enterprises na kitita cha pesa kilichokuwemo. Kwa kampuni kama hiyo, bilioni moja na nusu si ela nyingi. Kilichomsisimua Joram ni habari kuwa pesa hizo ziliingia toka katika akaunti moja ya mjini New York, Marekani.
Joram aliitazama saa yake. Ilikuwa saa kumi kasoro. Aliandika ujumbe harakaharaka na kuutuma kwa faksi kwenda kwa rafiki yake mmoja mwenye kampuni ya upelelezi wa kujitegemea mjini humo, akimtaka kuichunguza akaunti hiyo kuona ina pesa kiasi gani na nani anamiliki. Ujumbe ulichukua nusu dakika kufika na baadaye kupata jibu ambalo lilimfahamisha kuwa anashughulikiwa.
Nusu saa baadaye alipata majibu ya maswali yake. Benki hiyo haikuwa na akaunti yoyote yenye jina la Kangaroo wala namba zilizotajwa si za benki hiyo.
‘Haya.’ Joram aliwaza baada ya kuisoma faksi hiyo, ambayo pia iliandikwa kwa mkono, kazi ndio kwanza inaanza! Hata hivyo, hilo alikumsumbua sana Joram. Kitendo cha kuficha ukweli wa pesa zao ni jambo la kawaida kwa wafanyabiashara kote duniani. Alipoitazama tena saa yake aligutuka kugundua kuwa imetimia saa tatu za usiku akiwa ameketi kwenye kochi hilohilo. Akiwa si mtu wa kuketi alifurahi kuona usiku umeingia. Kwake giza ni mali, giza ni uhai; hali ambayo alihitaji sana.
Akavuta kabati na kutoa vifaa vyake vyote muhimu alivyokuwa ameviandaa kwa safari yake ya Zanzibar; bastola moja, visu viwili, funguo zake Malaya, bomu moja la mkono alilolitengeneza mwenyewe na vikorokoro vingine vingi. Vyote alivifutika katika mifuko ya siri baada ya hapo alichukua kitita cha pesa na kukifutika mifukoni. Kabla ya kutoka alitegesha chombo cha kupokelea simu ambazo angepigiwa. Wakati akikamilisha kufanya hivyo, simu iliyomwunga na redio call ya Kombora ilipata uhai. Joram akainua chombo cha kusikilizia na kulitegesha sikio lake.
“Ni mimi afande koplo Shomari. Bado nilikuwa nikilinda ofisi ya Kangaroo ninamashaka kuna kitu wanafanya mzee…”
“Kitu gani?”
“Ni sanduku kubwa ambalo linatosha kupakia watu watatu wazima. Sioni kwanini mzigo huo usafirishwe saa hizi…”
“Nisubiri nakuja.” Sauti ya Kombora ilisikika. “Usiache mzigo huo ukupotee machoni. Kadhalika, usiruhusu wajue kuwa unawatazama.”
“Sawa, afande…”
Jibu hilo la mwisho halikumfikia Joram. Alikuwa tayari amekwisha funga mlango na kukimbia hadi nje ambako alimwomba dereva wa teksi bubu moja, aina ya Toyota Corolla, aliyekuwa amepaki nje ya hotel hiyo, amwazime gari. Ili mtu huyo asiwe na shaka Joram alimkabidhi laki tano. “Nikirudisha gari salama laki mbili zako, laki tatu utanirejeshea,” alimwambia baada ya kumwelekeza namba ya chumba chake na kumtajia jina lake la bandia.
Dakika tano baadaye gari hilo likawa limepaki jengo moja toka ilipo ofisi ya Kangaroo, boneti ikiwa imefunguliwa huku dereva wake akihangaika, mara achungulie ndani ya injini mara aingie ndani na kujaribu kuwasha, mara ajitie kulisukuma. Lakini wakati wote huo macho yake yalikuwa yakiangalia kwa umakini kila kinachoendelea katika ofisi hiyo.
Utulivu wake na jinsi alivyokuwa akiitazama saa yake mara kwa mara vilimfanya Joram aanze kuhisi kuwa chochote kilichomo ndani ya sanduku hilo hakikuwa na thamani yoyote kama alivyotarajia. Hakuamini kama Nuru alikuwa ndani ya sanduku hilo. Badala yake alihisi kuwa zilikuwa zinafanyika njama za kuwaita polisi nje ya eneo hilo ili aweze kuhamishwa kwa utulivu zaidi.
Wakati Joram alipokuwa akiwaza hayo, aliona gari ya Inspekta Kombora likifika katika eneo hilo. Lilikuwa Rangerover lenye namba za kiraia. Lilijipitisha katika eneo hilo kama ambalo halina shughuli yoyote na jengo hilo, kwa mwendo wa taratibu na kutokomea mitaani.
Kana kwamba dereva wa pickup yenye ‘mzigo’ alikuwa akisubiri ishara hiyo, aliingia ndani ya gari lake na kulitia moto. Alifuata barabara ya UWT na baadaye kuingia ya Morogoro. Dakika mbili baadaye Joram aliona gari ya Kombora, likiwa na watu wawili zaidi, waliovaa sare za polisi wakilifuata gari hilo.
Joram alisita kabla ya kuamua kulifuata gari hilo au la. Lakini, shingo upande alilifanya gari lake Lionekane kama limepona, akaliwasha na kuyafuata magari ambayo yalikuwa yakitokomea mbele yake.
Saa hizo, magari yakiwa yamepungua barabarani, haikumchukua muda kuyapata magari hayo. Aliacha magari mawili, moja likiwa daladala yamtenganishe na Kombora ambalo lilikuwa nyuma ya ile pickup. Waliipata kariakoo wakaivuka jangwani na kuingia magomeni ambapo pia waliinuka hadi Manzese.
Wakati wakikaribia kiwanda cha urafiki, Joram alimwona Inspekta Kombora akilipita gari hilo na kisha kulisimamisha kwa mkono. Liliposimama yeye na wenzake wawili, bastola zikiwa wazi mikononi, walishuka na kumfuata dereva wa pickup hiyo.
“Una nini ndani ya sanduku…? Joram alimsikia Kombora akiuliza alipokuwa akiwapita taratibu.
Asingeweza kusimama hapo. Hivyo, aliwapita kama hatua mia moja na kisha kulisimamisha gari lake kando ya barabara. Huku akijifanya anakagua matairi ya gari, macho yake yalikuwa makini yakitazama kinachoendelea baina ya Inspekta Kombora na dereva wa pick up. Alimwona dereva akishuka na kuzunguka nyuma ya gari. Alihangaika kama anayetaka kulifungua sanduku hilo. Kisha, jambo la ajabu lilitokea. Joram alimwona Inspekta Kombora akipaa angani na kisha kuanguka chini kama mzoga. Alipojaribu kuinuka alipokea kipigo kingine ambacho kilimfanya apepesuke na kurudi chini huku bastola yake ikifyatuka na askari wengine walikuwa wakigalagala chini, mmoja kashikilia mbavu zake, wa pili shingo ikiwa haifanyi kazi.
Tukio hili lilifanyika kwa muda mfupi sana kiasi kwamba ilimchukua Joram Kiango nusu dakika kuelewa kinachotokea. Baada ya hapo alikuwa ameliacha gari lake na kutimka mbio kuelekea eneo la tukio. Alikimbia kwa kunyata kama chui. Alimfikia dereva huyo ghafla na kuachia teke ambalo lilitua tumboni barabara. Dereva huyo alipepesuka na kutokwa na macho ya mshangao. Hata hivyo, Joram aliporusha teke la pili lilidakwa na mguu wake kuanza kupindwa. Alitumia mguu wake wa pili kuruka tiktak ambayo ilimpata barabara dereva huyo usoni na kumfanya aanguke na kumwachia Joram ambaye aliviringika! Waliinuka kwa pamoja na kuanza kunyatiana kwa mwendo wa chui walio mawindoni. Macho yao yalitazamana. Hayakuwa macho ya kawaida. Kila mmoja aliona kitu katika macho ya mwenzie, kitu kisichoelezeka, kinachoonyesha waziwazi wao ni nani katika dunia hiyo.
Joram alihisi kupata kuyaona mahali fulani macho hayo. Macho ambayo yana dalili zote za tamaa ya kuwa kiu ya mauaji. Wapi aliyaona macho haya? Alijiuliza wakati akinyata kutafuta fursa nzuri ya kummaliza adui yake, huku akijua fika adui huyo pia anatafuta nafasi ya kumwua.
Wakati huo kikundi cha wapita njia kilikwisha wazingira, kila mmoja akiwa mdomo wazi kwa mshangao na kutoelewa kinachotukia. Dereva huyo alitazama huko na huko kisha akatia mkono wake mfukoni na kuutoa ukiwa umeshikilia tufe ambalo alilipiga chini kwa nguvu. Papo hapo ulitokea moshi mzito unaowasha zaidi ya bomu la machozi. Joram alilazimika kufumba macho huku akiruka upesi kutoka eneo hilo, kitendo ambacho kilimwokoa na pigo la judo ambalo lingemmaliza. Akiwa ameyafumba macho yake yaliyojaa machozi, huku watu wengi wakilia na kukimbia ovyo, hakuwa na uwezo wa kufanya lolote kuizuia pick up hiyo kuondoka kwa mwendo wa kasi.
‘Ninja’ aliwaza kwa mshangao. ‘Ninja Tanzania!’
Kombora alimfikiria kama Powel mwingine, kwa jinsi walivyofanana kimaumbile na kimavazi.Yeye pia alikuwa ameungua uso na sehemu mbalimbali za mikono yake. Yeye pia alikuwa na jicho moja, ingawaje lake lililoungua lilikuwa wazi nyuma ya kovu kana kwamba linaona. Badala ya mkono wa bandia yeye alikuwa na mguu mmoja wa mbao. Hilo Kombora aliligundua wakati alipoukunja kwa mikono yake yote miwili pindi akiketi chini, vinginevyo isingekuwa rahisi kugundua.
Powel aliyaona macho ya Kombora yakitembelea uso huu hadi ule kana kwamba yanadai maelezo. Kwa sauti ilelile inayocheka Powel alisema, “Watu wengi wanasema tumefanana. Wengine wanadhani tu mapacha. Lakini wanakosea sana. Hatujafanana hata kidogo. Ukishatuzoea, utagundua kuwa huyu mwenzangu ni mrefu kuliko mimi, mnene kuliko mimi.” Alipoona maelezo hayo hayajamridhisha Kombora aliongeza, “ kinachotufanya tufikiriwe ndugu ni haya masahibu yaliyotukuta, siku moja, saa moja, kwa bomu moja. Ilikuwa tufe pamoja, kwa bahati mungu alitunusuru pamoja. Tungeweza kuwa ombaomba barabarani, lakini mungu ametusaidia vilevile na kutuwezesha kuwa wafanyabiashara wakubwa duniani…”
“Hujaniambia mwenzako anaitwa nani,” Kombora alimkatiza
“Oh kweli anaitwa Philip Benjamin. Yeye ni Mkurugenzi wa Fedha” alimgeukia mwenzake huyo na kumwambia, “Philip, huyu hapa ni Inspekta Kombora bila shaka umepata kumsikia”
Philip alitikisa kichwa kukubali.
Powel aliendelea “Inspekta Kombora anadhani kuna mwizi ambaye amejificha katika jengo hili. Unadhani inawezekana Philip?”
Badala ya kujibu Philip aliangua kicheko.
“Unaona Inspekta? Unapoteza muda wako bure.”
Kombora alianza kupandwa na hasira juu ya watu hawa. Aliona wazi kuwa ama walikuwa punguani wa akili kama ilivyokuwa kwa baadhi ya viungo vyao, ama walikuwa wakimdhihaki. Akaamua kucheza mchezo waliotaka wao. Aliinuka akawashukuru na kutoka nje huku akihisi kila jicho linaloona, la kila mmoja kati yao, likiwa limemganda mgongoni huku linamcheka.
Alipanda gari na kuamuru liondoke. Baada ya kupinda kona moja alisimamisha gari na kumwamuru kachero mmoja arejee na kutafuta uwezekano wa kuilinda ofisi hiyo kwa makini bila ya yeye mwenyewe kuonekana.
11
Ilikaribia saa kumi na mbili Kombora aliporejea ofisini kwake kama mgonjwa aliyeruhusiwa kutoka hospitali baada ya kukata tamaa ya kuendelea kuishi. Alijibweteka juu ya kiti chake na kujiinamia kwa muda, mikono yake yote miwili ikiwa imekilea kichwa chake.
‘Msichana mzuri, asiye na hatia yuko mikononi mwa muuaji wa hatari, aliwaza kwa uchungu, mbele ya macho yangu mwenyewe jambazi huyohuyo ameua watu wawili wasio na hatia… Na ametoweka…mbele ya macho yangu mwenyewe. Mimi … ambaye najiita mkuu wa kikosi hiki…’ alishindwa kuendelea kufikiri. Hasira zilikuwa zimefura katika kichwa chake kiasi cha kufanya ubongo wake ukitishia kuchemka. ‘Lazima nitunze kichwa changu,’ alinong’ona kimoyomoyo huku akiiitoa mikono yake kichwani na kuipeleka mezani ambako ilirudi na faili ambalo hakulihitaji. Alilitupa mezani hapo na kuiingiza mikono mfukoni ambamo alitoka na kile kijitabu cha maelezo ya kampuni ya Kangaroo. Alikipekuapekua kwa dakika chache kabla hajainua simu na kumpigia mmoja wa wasaidizi wake, ambaye alifika mbele yake mara moja na kupiga saluti ambayo haikujibiwa.
“Fanya kila unaloweza nipate taarifa za kampuni hiyo kabla ya saa mbili,” alimwamuru akimwonyesha kijitabu hicho. “Nataka kujua imeanzishwa lini na wapi, hapa nchini imeingia lini, nani hasa mwenye kampuni hiyo, shughuli zake hasa ni zipi na kila unachoweza kupata. Zaidi, jitahidi nipate kila ambalo linaweza kupatikana juu ya wakurugenzi wake wawili walioko hapa, Paul Powel na Philip Benjamin. Tumia watu wote unaoweza kuwapata. Upo?
“Nipo afande.”
“Haya! Bado unasubiri nini zaidi?”
Amri ya pili ambayo Kombora aliitoa na kumtaka Sajin Kangura mwenyewe kuhakikisha inatekelezwa mara moja ni ile ya kupata ramani ya majengo ya Sunrise Modern Club na Kangaroo Enterprises katika muda wa saa mbili.
“Ni zaidi ya saa mbili sasa, afande. Ofisi ya Ardhi na jiji zitakuwa zimefungwa…”
“Zinaweza kufunguliwa. Kama wanaohusika hawapatikani mtafute waziri wao azifungue. Na kama hana funguo mwambie azivunje.”
“Ndiyo, afande.”
Kombora alipobaki peke yake alijaribu tena kukisoma kijitabu cha maelezo ya kampuni ya Kangaroo. Maelezo yalikuwa mengi, marefu yaliyowekwa katika mpangilio ambao ungemfanya msomaji yeyote ahisi kuwa kampuni hiyo ilikuwa moja ya makampuni makubwa sana duniani. Yalitaja matawi yake katikasehemu mbalimbali za dunia. Hata hivyo, ilimshangaza Kombora kuona kuwa anuani za matawi hayo hazikutajwa wala makao makuu, ambayo yalidaiwa kuwa yako New York, Marekani. Hali kadhalika, zaidi ya Powel na Philip, kijitabu hicho hakikuwa na jina jingine la Mkurugenzi yeyote.
Hayo yaliyoongeza mashaka ya Kombora juu ya kampuni hiyo, mashaka ambayo yalianza tangu alipowatia machoni wakurugenzi hao wawili, ambao pamoja na kutojiweza kwao hawakuonekana kuwa na lugha ya biashara hata chembe. Kwa ujumla, Kombora hakuwaona kama wafanyabiashara. ‘Kama wanafanya biashara, lazima biashara hizo zitakuwa haramu,’ aliwaza. ‘Si biashara walizoziorodhesha hapa.’
Kombora alijua ambacho angefanya kesho. Alijua kuwa angehitajika kuwataka msaada polisi wa kimataifa, Interpol, toka nchi zote ambazo Kangaroo ilizitaja kuwa ina matawi yake na kumwomba juu ya uhalali wa makampuni hayo, biashara halisi wanazozifanya na taarifa kamili za wakurugenzi wake.
Hilo lilikuwa la kesho. La leo ambalo lilikuwa likimsumbua Kombora na ambalo lisingesubiri kesho lilikuwa la kumtoa Nuru mikononi mwa Kakakuona, akiwa hai. Alitazama saa yake na kuona ikikaribia moja na nusu usiku; lakini hajapata bado jibu toka kwa watu aliowataarifu kupata taarifa za Kangaroo, jengo lao na lile la Sunrise. ‘Wako wapi hawa’ alinung’una akiinua uso wake kutazama mlangoni.
Juu ya meza yake Kombora alishukuru kuona kuwa mtu mmoja alimwekea chupa ya chai au kahawa na mayai matatu ya kuchemsha. Ndio kwanza akahisi kuwa alikuwa na njaa kali. Akavunja yai moja na kulitafuna. Yai la pili vilevile alilila kavukavu. La tatu ndilo aliloshusha kwa chai nzito ya maziwa toka katika chupa. Baadaye, aliinuka na kuukamilisha mlo wake kwa glasi mbili za maji toka katika friji yake ndogo ya ofisini. Wakati akirudi mezani simu ililia. Kombora aliinyakua na kuidaka masikioni mwake.
“Afande, Kabweka hapa.”
“Najua, uko wapi?”
“Napiga toka bandarini, nilikuwa katika kuhakikisha kama kweli hawa Kangaroo wanaingiza vitu toka nje.”
“Enhe!”
“Ni waingizaji maarufu wa vitu vya nje, Mzee, nimeona mizigo yao mingi ambayo haijatolewa. Nimeambiwa pia kuwa safari hii wamekodi meli mbili. Moja inatarajiwa kuanza kushusha mali zao wakati wowote. Ya pili haijapata nafasi ya kuingia bandarini, imetia nanga nje kidogo ya pwani.”
Hazikuwa habari nzuri sana kwa Kombora. “Ni hayo tu uliyoyapata?” Kombora aliuliza akitaka kuthibitisha kama hakukuwa na habari nzuri zaidi.
“Ndiyo mzee, lakini…”
“Lakini nini?”
“Kuna jambo moja ambalo limenitatanisha.”
“Lipi?”
“Hawa wakurugenzi wake. Idara yetu inayoshughulikia taarifa za wageni haina lolote kabisa juu ya Philip na Powel. Hakuna kinachofahamika zaidi ya kuwa ni raia wa Urusi ambao walikwenda Angola kuwasaidia wazalendo dhidi ya Wareno, wakati walipokuwa wakipigania uhuru wao. Taarifa hizo hazionyeshi maisha yao huko Urusi, waliondoka lini na walikuwa wakipigana kikosi kipi. Zinaonyesha kuwa MPLA tayari wameulizwa juu ya watu hawa na wakashindwa kutoa majibu. Wanasema kwa kuwa watu wengi vitani hupenda kutumia majina ya bandia huenda watu hao walishiriki. Urusi nako, kikosi chao cha KGBkimesema hakina majina hayo katika kumbukumbu zao.”
Kombora alimsikiliza kwa makini, “Kwa hiyo, unawafikiriaje watu hawa, Kabweka?” Kombora alimwambia.
“Nahisi kuna kitu wanaficha na kuna kitu zaidi wanafanya. Inawezekana hawa ni wanachama wa kikundi cha Mafia ambao wanajishughulisha na biashara haramu za dawa za kulevya au nyara za serikali,” alieleza na kuongeza kwa sauti ya kujiamini. “Inawezekana mzee, hawa ni maadui wa Joram Kiango.”
“Ahsante kwa mchango wako. Endelea na usikose kuniarifu kila utakapopata kitu kipya,” Kombora alisema akiitua simu chini.
Papo hapo ikaita tena. Safari hii aliyepiga alikuwa Sajin Kangura. Alikuwa akipiga toka Halmashauri ya jiji. Alimwarifu Kombora habari ambazo zilimsisimua zaidi. “Inashangaza, afande. Si wizara ya Ardhi wala jiji ambao wana nakala ya ramani ya majengo hayo yote mawili.”
“Kwanini?”
“Haieleweki. Jiji wanadai kuwa wana hakika walikuwa na nakala za majengo hayo lakini hawazioni. Hata hivyo, mmoja wa maafisa wa jiji ananieleza kuwa jengo la Sunrise lilikuwa dogo la ghorofa moja lakini liliibuka ghafla na kupanuliwa hata kabla ya kukamilisha taratibu za ujenzi. Kuwa waliingia katika mgogoro na mwenye jengo hilo ambapo baadae ulitatuliwa na akaruhusiwa kundelea.”
“Hamkuweza kumpata mwenye jengo hili awapeni ramani hiyo?” Kombora alimwuliza.
“Yeye pia yalimkuta makubwa,” Kombora aliambiwa “Inadaiwa kuwa huu mwaka wa tatu tangu alipotoweka”
“Katoweka!”
“Ndiyo, afande. Tumeambiwa kuwa bwana huyo, Fabian Kalila, ambaye alikuwa maarufu kwa ujenzi mara tu baada ya kukamilisha jengo hilo la Sunrise aliaga siku moja kuwa anakwenda Kigamboni kukagua uwanja mpya ambao ulihitajiwa kujengwa nyumba ya pili. Bwana huyo alifika hadi Ferry ambapo alionekana akizungumza na watu anaofahamiana naye.Watu waliomwona kwa mara ya mwisho walidai alipanda na kwenda ng’ambo. Lakini huko ng’ambo hakuna aliyemwona, yametolewa matangazo magazetini na maredioni lakini hazijafika taarifa zozote juu yake, wala maiti yake.”
“Naam, iko namna,” Kombora aliropoka kwa namna ya mtu anayezungumza peke yake.
Kangura alikuwa akiendelea, “pamoja na hayo, afande, tumefanya upekuzi mkubwa katika makabrasha yake yote, tumeweza kuona karibu nakala za majengo yote aliyowahi kushughulikia isipokuwa hili la Sunrise na Kangaroo. Hatukuweza kupata hata zile za majaribio.”
“Ni yeye aliyeshughulikia jengo lile pia?”
“Ndio, afande”
Kombora hakujua afanye nini zaidi. Alichanganyikiwa kupita kiasi. Kwa ujumla, hakujua kama anakwenda mbele au anarudi nyuma katika suala hilo. Alitua simu chini bila kusema neno lolote zaidi.
***
Mtu mwingine aliyekuwa jengo Fulani mtaa fulani, wa jijini hapo, baada ya kuyasikiliza maongezi hayo ya Kombora na wasaidizi wake aliitua simu yake chini taratibu. Kisha, akakichunguza chombo chake cha kunasia sauti kuona kama kilikuwa kinafanya kazi vizuri.
“Not so bad” alitamka, akitabasamu. Aliitoa kanda hiyo na kuitia mfukoni mwake. Akategesha upya chombo chake na kisha kuondoka zake toka chumbani humo, tabasamu likiwa bado usoni mwake.
***
Mtaa wa tatu toka hapa mtu mwingine alikuwa akitabasamu. Lakini hili lilikuwa tabasamu lake la kwanza kwa siku hiyo, na pengine kwa wiki hiyo. Mtu huyo aliitwa Joram Kiango.
Kama ungemtazama harakaharaka alivyoketi juu ya kochi, ndani ya chumba alichokodi katika hoteli hii ya Mawenzi usingemfikiria kabisa kuwa alikuwa na tatizo kubwa la kutisha ambalo lingetosha kabisa kumtia kichaa. Badala yake ungemwona kijana mtanashati, aliyevaa suti yake nyeusi iliyomkubali vilivyo; akiwa ameketi juu ya kochi pana glasi ya wiski ikiwa mbele yake, sigara mkono mmoja na simu mkono wa pili.
Hali hii ilimrejea joram baada ya kujiaminisha tena na tena kuwa alihitaji kutuliza kichwa chake ili kupambana kikamilifu na janga hilo. ‘wewe ni Joram Kiango’ nafsi yake ilimwambia, ‘Endelea kuwa Joram Kiango vinginevyo Nuru utampoteza na maisha yako yatapotea.’
Hakujali sana juu ya maisha yake lakini alipomkumbuka Nuru na ukatili wa watu wanaomshikilia, alituliza akili yake na kuwa Joram Kiango. Na kwa mshangao wake alikuta akili yake ikichemka kwa ukamilifu kama betri zilizochajiwa upya.
Aliwakumbuka marafiki zake wote, wa nje na ndani. Namba zao za simu teleksi na faksi ziliibuka kama chemichemi akilini mwake. Akiwa na pesa za kutosha haikumchukua muda kukifanya chumba hicho kidogo kigeuke ofisi kubwa ya mawasiliano ambayo yalitoka huku na huko.
Simu yake ya kwanza ilimwendea rafiki yake mmoja anayemiliki kampuni yake binafsi jijini. Huyu akiwa ni mtu ambaye kila kitu kwake ni biashara, alikuwa anafahamu kila mtu na kila kampuni jijini Dar es Salaam. Hivyo, Joram alipomwuliza anafahamu nini juu ya Kangaroo Enterprises rafiki yake aliangua kicheko.
“Vipi? Sioni kama jina hilo linachekesha,” Jorama alimsaliti.
“Sio jina braza, ni pesa” Sauti ilijibu toka upande wa pili.
“Pesa?”
“Pesa hazina macho,” alieleza na kuongeza “pesa, kwa kweli mara nyingine inapotea njia.”
“Sijakuelewa?” Joram alimkumbusha.
“Kwani hujawaona wakurugenzi wa kampuni hiyo?”
“Wakurugenzi gani?”
“Powel na Philip.”
“Wanakasoro gani?”
“Swali sio wana kasoro gani , ila kasoro gani hawana” kicheko “Wale mabwana ukiwaona utafikiri pacha. Wenyewe wanadai hawana undugu wowote. Ukiwaona utadhani ndio kwanza wanaibuka toka kaburini; utafikiri waliwekwa katika pipa wakachemshwa na kisha kutolewa kabla ya kukata roho. Mmoja ni nusu kipofu asiye na mkono wa pili, mwingine nadhani kiziwi na hana mkono mmoja. Kwakweli mabwana wale ni watu wa kuchekesha sana.”
“Sioni wamewezaje kupata pesa,” Joram alichochea.
Baada ya maswali mengi alibaini kuwa kampuni ya Kangaroo Enterprises ni mpya inayoongozwa na watu wasiojiweza, Paul powel na Philip Benjamin. Pamoja na kwamba kampuni hiyo ilidai inajishughulisha na mambo mengi, lakini taarifa alizozipata ni kuwa kazi kubwa ambayo kampuni hiyo imekwishafanya ni uingizaji wa pickup, bidhaa toka nje na kuzisambaza kwa wauzaji mbalimbali wa jumla jijini. Bidhaa yao kubwa, Joram aliarifiwa, ni vipodozi vya aina kwa aina, hasa kwa kina mama.
Alifahamishwa kuwa kampuni hiyo ilijenga maghara yake kando ya barabara ya Nelson Mandela katika eneo la Tabata.
Joram alimshukuru rafiki huyo na kumtaka amwarifu kila atakachokipata juu ya wakurugenzi hao wawili.
Rafiki yake mwingine alikuwa miongoni mwa vijana wa Inspekta Kombora. Kila alipopata wasaa aliwatoroka wenzake na kumdokeza Joram juu ya kila tukio. Alimfahamisha jinsi ambavyo Inspekta Kombora alikuwa taabani baada ya watu wawili wasio na hatia kuuawa mbele yake na Nuru kutoweka mbele ya macho yake. Aidha, alimfahamisha juu ya harakati zote ambazo zilifanyika kulikagua jengo hilo na majengo yote ya jirani bila mafanikio yoyote.
“Sasa hivi ukimwona mzee Kombora utadhani ana umri wa miaka mia moja, kwa jinsi alivyozeeka ghafla,” Rafiki huyo alidokeza katika maongezi hayo.
Baada ya Joram kuuliza kwa makini ukubwa wa jengo la Sunrise Modern Club, Kangaroo Enterprises zilivyojengwa ndani na nje, sehemu ambayo Kakakuona alimwua dereva wa taksi na alipomwua msichana wa mapokezi, na mengine mengi, alipatiwa majibu yote aliyoyahitaji kwa kiwango cha kuridhisha. Maelezo hayo yalifuatwa na onyo, “Joram kama unakusudia kufuata nyayo za Kakakuona, lazima ujihadhari sana. Huyu sio mtu wa kawaida. Mambo aliyoyafanya hapa ambayo nimeyaona kwa macho yangu sio mambo ya kawaida. Labda tunayoona katika filamu baada ya watu wa studio kuweka utaalamu wao. Huyu si binadamu ningekushauri ufikirie mara mbili.”
Ni hilo ambalo lilimfanya Joram atabasamu kwa mara ya kwanza siku hiyo. Yalimchekesha mengi. Moja likiwa lile la kujua kuwa nje ya maadui, ni yeye peke yake ambaye alifahamu kuwa Kakakuona hayuko duniani tena. Jingine alipoona rafiki yake huyo asivyomwelewa kikamilifu kwa kumtahadharisha kumfuata Kakakuona. Laiti angejua kuwa alikuwa tayari kumfata hadi kuzimu, na kuhakikisha akirejea na Nuru, akiwa hai au salama! Hata hivyo, Joram alimshukuru rafiki huyo na kumtaka aendelee kuwa macho.
Joram alipata msaada mkubwa zaidi toka kwa rafiki yake mmoja wa kampuni ya simu. Huyu, alimwezesha kupata moja kwa moja mawasiliano yote ya simu yaliyokuwa yakiendelea katika ofisi ya Kombora kwa kuiunganisha na laini moja ya hoteli ambayo Joram aliikodi kwa bei mbaya.
Mawasiliano hayo yalimpunguzia Joram kazi kwa kiasi kikubwa. Hakuhitaji tena kujishughulisha na uraia wa watu hao kwa wakati huo kutokana maongezi baina ya Kombora na msaidizi wake. Hakuwa na haja tena ya kutafuta ramani ya majengo hayo wala ujenzi wake kutokana na taarifa hizohizo. Hali kadhalika, asingepoteza muda wa kutafuta habari za kampuni hiyo huko nje kwani tayari ilionyesha kuwa taarifa zao sio za kweli. Zaidi, Joram hakuwa na wasiwasi juu ya Nuru kuhamishwa toka jengo hilo kwa kujua kuwa vijana wa Kombora walikuwa wakilinda doria na kumtaarifu juu ya kila tukio lililotendeka, taarifa ambazo yeye pia alikuwa akizipata.
Kitu ambacho kwa sasa kilisumbua sana akili ya Joram Kiango kilikuwa kushindwa kuoanisha maelezo juu ya maumbile ya wakurugenzi hao wa Kangaroo na mkasa huu mzima. Kama kweli ni watu wasiojiweza,wenye biashara zao halali, vipi wajihusishe na ujasusi huo wa kimachomacho? Watakuwa wanajiamini nini?
Kitendo chao cha kumteketeza Kakakuona hata kabla hajakamilisha jukumu alilopewa pia lilimtatiza. Kama wangemwua Kakakuona na kisha kumwachia Nuru angeweza kuelewa. Ingekuwa ishara ya kukubali kushindwa. Lakini kumwua Kakakuona, na kuendelea kumshikilia Nuru kwa vyovyote vile ni dalili ya kutangaza shari zaidi, shari ambayo kwa maumbile yao yalivyo, wasingeweza kuitekeleza bila msaada wa mtu mwingine mwenye uwezo na akili timamu zaidi ya Kakakuona.
Joram alihitaji kumfahamu mtu huyo kwa gharama yoyote ile kwani ni yeye tu aliyekuwa kipingamizi baina yake na Nuru. Vinginevyo, angeweza kwenda zake, mchana kweupe, na kumpokonya Nuru toka mikononi mwao.
Simu ililia. Akaipokea na kuisikiliza, kisha akaitua, haikuwa na kitu cha muhimu.
Teksi ikapata uhai. Taarifa ilitoka katika tawi moja wapo la NBC mjini hapo, ilimtajia namba ya akaunti ya Kangaroo Enterprises na kitita cha pesa kilichokuwemo. Kwa kampuni kama hiyo, bilioni moja na nusu si ela nyingi. Kilichomsisimua Joram ni habari kuwa pesa hizo ziliingia toka katika akaunti moja ya mjini New York, Marekani.
Joram aliitazama saa yake. Ilikuwa saa kumi kasoro. Aliandika ujumbe harakaharaka na kuutuma kwa faksi kwenda kwa rafiki yake mmoja mwenye kampuni ya upelelezi wa kujitegemea mjini humo, akimtaka kuichunguza akaunti hiyo kuona ina pesa kiasi gani na nani anamiliki. Ujumbe ulichukua nusu dakika kufika na baadaye kupata jibu ambalo lilimfahamisha kuwa anashughulikiwa.
Nusu saa baadaye alipata majibu ya maswali yake. Benki hiyo haikuwa na akaunti yoyote yenye jina la Kangaroo wala namba zilizotajwa si za benki hiyo.
‘Haya.’ Joram aliwaza baada ya kuisoma faksi hiyo, ambayo pia iliandikwa kwa mkono, kazi ndio kwanza inaanza! Hata hivyo, hilo alikumsumbua sana Joram. Kitendo cha kuficha ukweli wa pesa zao ni jambo la kawaida kwa wafanyabiashara kote duniani. Alipoitazama tena saa yake aligutuka kugundua kuwa imetimia saa tatu za usiku akiwa ameketi kwenye kochi hilohilo. Akiwa si mtu wa kuketi alifurahi kuona usiku umeingia. Kwake giza ni mali, giza ni uhai; hali ambayo alihitaji sana.
Akavuta kabati na kutoa vifaa vyake vyote muhimu alivyokuwa ameviandaa kwa safari yake ya Zanzibar; bastola moja, visu viwili, funguo zake Malaya, bomu moja la mkono alilolitengeneza mwenyewe na vikorokoro vingine vingi. Vyote alivifutika katika mifuko ya siri baada ya hapo alichukua kitita cha pesa na kukifutika mifukoni. Kabla ya kutoka alitegesha chombo cha kupokelea simu ambazo angepigiwa. Wakati akikamilisha kufanya hivyo, simu iliyomwunga na redio call ya Kombora ilipata uhai. Joram akainua chombo cha kusikilizia na kulitegesha sikio lake.
“Ni mimi afande koplo Shomari. Bado nilikuwa nikilinda ofisi ya Kangaroo ninamashaka kuna kitu wanafanya mzee…”
“Kitu gani?”
“Ni sanduku kubwa ambalo linatosha kupakia watu watatu wazima. Sioni kwanini mzigo huo usafirishwe saa hizi…”
“Nisubiri nakuja.” Sauti ya Kombora ilisikika. “Usiache mzigo huo ukupotee machoni. Kadhalika, usiruhusu wajue kuwa unawatazama.”
“Sawa, afande…”
Jibu hilo la mwisho halikumfikia Joram. Alikuwa tayari amekwisha funga mlango na kukimbia hadi nje ambako alimwomba dereva wa teksi bubu moja, aina ya Toyota Corolla, aliyekuwa amepaki nje ya hotel hiyo, amwazime gari. Ili mtu huyo asiwe na shaka Joram alimkabidhi laki tano. “Nikirudisha gari salama laki mbili zako, laki tatu utanirejeshea,” alimwambia baada ya kumwelekeza namba ya chumba chake na kumtajia jina lake la bandia.
Dakika tano baadaye gari hilo likawa limepaki jengo moja toka ilipo ofisi ya Kangaroo, boneti ikiwa imefunguliwa huku dereva wake akihangaika, mara achungulie ndani ya injini mara aingie ndani na kujaribu kuwasha, mara ajitie kulisukuma. Lakini wakati wote huo macho yake yalikuwa yakiangalia kwa umakini kila kinachoendelea katika ofisi hiyo.
Utulivu wake na jinsi alivyokuwa akiitazama saa yake mara kwa mara vilimfanya Joram aanze kuhisi kuwa chochote kilichomo ndani ya sanduku hilo hakikuwa na thamani yoyote kama alivyotarajia. Hakuamini kama Nuru alikuwa ndani ya sanduku hilo. Badala yake alihisi kuwa zilikuwa zinafanyika njama za kuwaita polisi nje ya eneo hilo ili aweze kuhamishwa kwa utulivu zaidi.
Wakati Joram alipokuwa akiwaza hayo, aliona gari ya Inspekta Kombora likifika katika eneo hilo. Lilikuwa Rangerover lenye namba za kiraia. Lilijipitisha katika eneo hilo kama ambalo halina shughuli yoyote na jengo hilo, kwa mwendo wa taratibu na kutokomea mitaani.
Kana kwamba dereva wa pickup yenye ‘mzigo’ alikuwa akisubiri ishara hiyo, aliingia ndani ya gari lake na kulitia moto. Alifuata barabara ya UWT na baadaye kuingia ya Morogoro. Dakika mbili baadaye Joram aliona gari ya Kombora, likiwa na watu wawili zaidi, waliovaa sare za polisi wakilifuata gari hilo.
Joram alisita kabla ya kuamua kulifuata gari hilo au la. Lakini, shingo upande alilifanya gari lake Lionekane kama limepona, akaliwasha na kuyafuata magari ambayo yalikuwa yakitokomea mbele yake.
Saa hizo, magari yakiwa yamepungua barabarani, haikumchukua muda kuyapata magari hayo. Aliacha magari mawili, moja likiwa daladala yamtenganishe na Kombora ambalo lilikuwa nyuma ya ile pickup. Waliipata kariakoo wakaivuka jangwani na kuingia magomeni ambapo pia waliinuka hadi Manzese.
Wakati wakikaribia kiwanda cha urafiki, Joram alimwona Inspekta Kombora akilipita gari hilo na kisha kulisimamisha kwa mkono. Liliposimama yeye na wenzake wawili, bastola zikiwa wazi mikononi, walishuka na kumfuata dereva wa pickup hiyo.
“Una nini ndani ya sanduku…? Joram alimsikia Kombora akiuliza alipokuwa akiwapita taratibu.
Asingeweza kusimama hapo. Hivyo, aliwapita kama hatua mia moja na kisha kulisimamisha gari lake kando ya barabara. Huku akijifanya anakagua matairi ya gari, macho yake yalikuwa makini yakitazama kinachoendelea baina ya Inspekta Kombora na dereva wa pick up. Alimwona dereva akishuka na kuzunguka nyuma ya gari. Alihangaika kama anayetaka kulifungua sanduku hilo. Kisha, jambo la ajabu lilitokea. Joram alimwona Inspekta Kombora akipaa angani na kisha kuanguka chini kama mzoga. Alipojaribu kuinuka alipokea kipigo kingine ambacho kilimfanya apepesuke na kurudi chini huku bastola yake ikifyatuka na askari wengine walikuwa wakigalagala chini, mmoja kashikilia mbavu zake, wa pili shingo ikiwa haifanyi kazi.
Tukio hili lilifanyika kwa muda mfupi sana kiasi kwamba ilimchukua Joram Kiango nusu dakika kuelewa kinachotokea. Baada ya hapo alikuwa ameliacha gari lake na kutimka mbio kuelekea eneo la tukio. Alikimbia kwa kunyata kama chui. Alimfikia dereva huyo ghafla na kuachia teke ambalo lilitua tumboni barabara. Dereva huyo alipepesuka na kutokwa na macho ya mshangao. Hata hivyo, Joram aliporusha teke la pili lilidakwa na mguu wake kuanza kupindwa. Alitumia mguu wake wa pili kuruka tiktak ambayo ilimpata barabara dereva huyo usoni na kumfanya aanguke na kumwachia Joram ambaye aliviringika! Waliinuka kwa pamoja na kuanza kunyatiana kwa mwendo wa chui walio mawindoni. Macho yao yalitazamana. Hayakuwa macho ya kawaida. Kila mmoja aliona kitu katika macho ya mwenzie, kitu kisichoelezeka, kinachoonyesha waziwazi wao ni nani katika dunia hiyo.
Joram alihisi kupata kuyaona mahali fulani macho hayo. Macho ambayo yana dalili zote za tamaa ya kuwa kiu ya mauaji. Wapi aliyaona macho haya? Alijiuliza wakati akinyata kutafuta fursa nzuri ya kummaliza adui yake, huku akijua fika adui huyo pia anatafuta nafasi ya kumwua.
Wakati huo kikundi cha wapita njia kilikwisha wazingira, kila mmoja akiwa mdomo wazi kwa mshangao na kutoelewa kinachotukia. Dereva huyo alitazama huko na huko kisha akatia mkono wake mfukoni na kuutoa ukiwa umeshikilia tufe ambalo alilipiga chini kwa nguvu. Papo hapo ulitokea moshi mzito unaowasha zaidi ya bomu la machozi. Joram alilazimika kufumba macho huku akiruka upesi kutoka eneo hilo, kitendo ambacho kilimwokoa na pigo la judo ambalo lingemmaliza. Akiwa ameyafumba macho yake yaliyojaa machozi, huku watu wengi wakilia na kukimbia ovyo, hakuwa na uwezo wa kufanya lolote kuizuia pick up hiyo kuondoka kwa mwendo wa kasi.
‘Ninja’ aliwaza kwa mshangao. ‘Ninja Tanzania!’
