Prince Naahjum_
Senior Member
- Jun 13, 2016
- 139
- 125
- Thread starter
- #81
SEHEMU YA 43
["Unasema Chinedu mwanangu Asu anaaa...?!"]
aliuliza tena Pastor George baada ya kukaa kwa dakika nzima akitetemeka midomo pindi alipokuwa anafikiria cha kujibu na kujikuta anauliza mithili ya kwamba alivyoambiwa awali hakusikia.
[["Mwanao Asunta kipindi tunafanya ile mudawa tulikosea kitu moja ambayo hatukukijua nacho ni Mimba. Na tatizo itakuja ule upendo aliokuwa nao Asunta sambamba na mudawa tuliyoifanyia kazi zote zimeingia tumboni kwa kiumbe ambaye ana damu ya mutu yule tumemrogea Asunta amsahau na sasa muunganiko wa yule mutoto ndio unamrudishia fahamu mwanao na kujiuliza maswali, na atavyozidi kuiona sura ya yule kijana ndivyo habari itapozidi kutumwa kwenye memory za mutoto ambae nae atamsababishia mamaake kumuonesha vile vyote vilivyojificha juu ya yule mtu aliyemfikiria, na hapo hadi ulichokifanya kitakuwa wazi kwenye maono ya mwanao."]]
maneno ya Chinedu kwa njia ya simu yalizidi kukichanganya kichwa cha Pastor George na kubaki na bumbuwazi kusikia kumbe ujauzito aliokuwa nao mwanae ni wa yule adui yake mkubwa manywele?
Na si kwamba ni ya Fredy kama alivyodhani...!
["Yaani Mimba ya yule mshenzi hasidi wa maendeleo ya mwanangu?"]
aliuliza kwa ghabhabu Pastor George mithili ya kwamba alikuwa haongei kwa simu.
[["Usifoke George ndio hivyo ilivyo, sasa unachotakiwa wewe kuamua jinsi ya kufanya ili Asu asipate muda wa kumfikiria au kumuona iwe kwenye picha au live"]]
["Huyu afe tuu, Fanya mpango Chinedu ua kabisa manywele hili"]
[["hahahahahaaa George kumuua huyu ni kumuua na mwanao pia kwani endapo akisikia habari za kufariki kwake akiwa bado hajajifungua jua nstuko ataoupata yule mtoto utamfanya aruke mfurulizo tumboni na kumkosesha hewa na nguvu mwanao na lazima afe tu"]]
jibu la Chinedu lilizidi kumchanganya George asijue sasa wamfanyeje Dullah kwani ni kweli atapofariki lazima Asu atasikia na yote imechochewa na umaarufu ule wa Dullah ulioanza kuonekana siku baada ya siku akiwa nchini Kenya.
["Chinedu, naomba nisaidie jinsi ya kufanyaaaa"]
[["sawa George, Hapa nitachofanya ni kumtengeneza VUNJESHA ambae ataenda kumshughulikia katika kazi yake onayosababisha kusikiwa na Asunta muda mwingi na ataenda kuugulia kwao hadi Asu atapojifungua sasa hapo ndipo tunamaliza muchezooo hahahaha']]
ushauri wa Chinedu uliungwa mkono moja kwa moja na Pastor George na baada ya kufika ule muafaka waliagana na kukata simu.
"Mwana izaya huyuuu, Dunga dunga... Kamdunga mwanangu Mimba ya pili??!!"
alijiongelea kwa uchungu Pastor George huku akisimama kujiandaa kutoka mule chumbani.
* * * *
NAIROBI - KENYA
________________
Furaha mara dufu ilirejea katika familia ya Dullah mara baada ya Ilham kurejewa na akili zake za kawaida mara aliporuhusiwa kule kwa mganga na kuhamia kwenye nyumba ile nzuri waliyokuwa wanaishi ambayo ilikodiwa na Tusker fc kwa niaba ya star wao Dullah.
Ilham aliona kama ndoto maisha yale ambapo kila siku walikuwa wanakula vyakula vizuri, wanavaa vizuri na mambo kwenda raha mustarehe.
Sala na maombi ya mama Dullah yalianza kujibu kwa kuonesha dariri za wazi wazi kwamba Ilham anampenda sana Roja na Roja anampenda sana Ilham ila tatizo kila mtu alikuwa anahofia kumuanza mwenzake kutokana na heshima iliyokuwepo baina yao.
Roja alimuheshimu sana mama Dullah na kutokana na urafiki wake mkubwa na Dullah ilifika wakati alijifikiria kama Ilham anamchukulia sawa na kakaake tu, kumbe hata Ilham nae alikuwa na hisia hizo na kuogopa kumtamkia Roja akichukulia kutokana na urafiki wao na kakaake Dullah basi hata na yeye Roja anamchukulia kama mdogo ake tu.
Na hata walivyokuwa wanapiga story mbalimbali na kucheka pamoja kila mtu alikuwa na hisia zake moyoni mwake lakini kwa utu uzima wa mama Dullah alibaini kuwa kuna kitu akilini mwao hasa kwa mwanae Ilham.
Baada ya mwezi mwengine kuisha wakati wakiwa mapomziko ambapo iliwabidi Dullah na Roja kusafiri hadi Tanzania mara baada ya kupigiwa upatu na Clouds fm, hatimae wote waliitwa kwa mara ya kwanza kwenye kikosi cha timu ya Taifa kwenye michuano ya kukata tiketi kucheza kombe la Dunia.
Ilikuwa ni habari njema kabisa kwao na ya furaha kwa kuingia kwenye historia ya kuitwa timu ya Taifa jambo ambalo kila mchezaji alilitamani kwani anapoonesha kiwango bora na timu ya Taifa anakuwa amelitangaza taifa lake.
"Hili ni tukio kubwa sana Dullah ona mwenyewe ratiba ilivyowekwa daah! mechi ya kwanza wiki mbili zijazo harafu mzee tunapanda dege hadi Nigeria?"
aliongea Roja mara baada ya kila mchezaji aliyeitwa kupewa kijitabu kidogo cha ratiba nzima ya mechi za makundi kuingia katika mtoano wa kuzipata timu za taifa 5 ambazo zitaiwakilisha Afrika katika michuano ile mikubwa kabisa katika ngazi ya mpira wa miguu.
Timu ya Tanzania maarufu kama Taifa Starz wao walieka Kambi Bagamoyo mkoani Pwani wakijiandaa na safari ambayo ilikuwa inawakutanisha na timu ya Nigeria iliyokuwa kundi moja na wao.
Mbali ya kuwa Dullah na Roja walikuwa na umaarufu lakini bado umaarufu wao haukusambaa kwa wananchi wote wapenda michezo zaidi ya wale wachache waliobahatika kuwaona uwanjani.
Hata ile siku ya siku ilipofika na timu ya Taifa ya Tanzania ilipoondoka kwenda jijini Lagos kukutana na moja ya timu ngumu ya Nigeria na watu walijua kuwa Tanzania wanachokifata kule ni kipigo tu kutokana na kuachwa mbali katika viwango vya ubora wa kisoka kwa mujibu wa Fifa.
Lakini manaojua wanasema mpira ni dakika tisini ndio zinazoamua, na kwa mara ya kwanza Dullah pamoja na Roja waliweza kuchanganyika na watu maarufu waliowajua kabloa toka wanacheza Tandale na humo D alukutana na John beki kisiki wa Simba mbae aliijua vizuri habari ya Dullah mara baada ya kuangushwa kwa vyenga zaidi ya mara mbili.
***********
Maneno ya Mbwiga na Shafii kuhusu uwezo wa ajabu wa Dullah kupitia Clouds fm radio ndio yaliwahamasisha watu wengi kukaa kwenye mabanda ya video siku hiyo kuangalia mtanange mkali ambao walijua kuwa timu yao kushinda si rahisi kutokana na kuzidiwa kila idara tangia kipindi cha kwanza hadi kinamalizika walikuwa washafungwa goli moja kwa bila.
Kipindi cha pili kilianza huku Tanzania safari hii wakijitahidi kushambulia ili wapate goli lakini hadi dakika ya 80 mambo yalizidi kuwa magumu kutengeneza nafasi ya ushindi japo kipa wa Tanzania alifanya jitihada nyingi sana hadi wanigeria walishangaa kwa jinsi alivyokuwa anaokoa magoli ya wazi kabisa.
Kocha alikata shauri na kuamua kumuingiza Rastaman Dullah kwa mara ya kwanza ili akajaribu na yeye bahati yake baada ya mshambuliaji tegemeo wa Tanzania kuuniana hapo ndipo jicho la kila mtanzania lilipoganda kwenye tv kumuangalia kwa umakini huyo mchezaji aliyesifiwa wiki nzima kupitia clouds baada ya kuitwa na kocha wa timu ya Taifa kwa mara ya kwanza.
Na kweli Dulla baada ya kuingia ile ilipofika dakika ya 87 alifanya vitu vya ajabu sana pindi timu yao ilipokuwa inashambuliwa na mpira ulipookolewa na kuja kwake akiwa zaidi ya mita sitini na gori la timu pinzani, alianza kukimbia na mpira na kuwachambua kama karanga wachezaji sita wa Nigeria waliokuwa mbele yake huku uwanja mzima ukiwa umesimama hadi Rais wa Nigeria ambae alikuwa mgeni rasmi siku hiyo ya mechi nae alisimama na kustaajabu na si kwa uwezo ule pakee aliouonesha Dullah... Bali ni baada ya kuwachenga wachezaji sita na alipotokea goli kipa nae alimpiga chenga ya maudhi na hatimae kubaki yeye na goli lakini chaajabu na kushangaza Dullah alipotaka kuupiga ule mpira alisita na kusimama ghafra mbele ya macho ya watu zaidi ya elfu arobaini walimshuhudia Rasta wa Tanzania akishindwa kuipatia point muhimu timu yake ya Taifa na kuuganda kwa sekunde kadhaa na kuanguka mzima mzima bila kusukumwa wala kuguswa na yeyote
Kipa wa Nigeria aliwahi na kuukimbilia mpira uliokuwa unaelekea gorini taratibu na kuudaka kabla wachezaji wengine pamoja na madaktari wa timu ya Tanzania hawajakimbilia uwanjani pindi refa alipopuliza kipenga cha kuusimamisha mchezo kutokana na kudondoka ghafra kwa Dullah.
"Aaaaaagggggg... Rooojaaaaaa Nakufaaaa aaaagggg"
alipiga kelele Dullah pindi madaktari na wachezaji wenzake walipofika pale alipodondokea kutaka kujua nini kimemkumbuka lakini hawakuweza kwa kuona jeraha kwa macho wala uvimbe zaidi ya kuhisi kuwa mguu ule wa kushoto ambao ndio alikuwa anautumia sana Dullah kuuchezea mpira, ulikuwa unamletea maumivu makali ukiwa umekakamaa huku ukivibrate mithili ya simu mbovu ya kichina.
Kadri madaktari walivyomshika ule mguu kuangalia harakaharaka tatizo ili wampatie huduma ya kwanza ndivyo Dullah alivyozidi kupiga kelele huku akimwita Roja ambae alikuwa hajaingizwa kabisa kucheza siku hiyo lakini pindi alipomuona rafiki ake akidondoka ghafra yeye nae alikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kufika pale alipodondoka Dullah huku akiwa na wasiwasi mkubwa.
Kutokana na sheria za michezo ilibidi Dullah abebwe kwenye machera ili akatibiwe vizuri nje ya uwanja kupisha kipute kiendelee na hapo ndipo kocha wa Tanzania alipomuamuru Roja achukue nafasi ya rafiki ake aliyekuwa anatolewa huku akipiga sana kelele za maumivu makali hadi kila mchezaji na aliyekuwepo pale uwanjani walimuonea huruma na wengine walijikuta wakitokwa machozi wakiwa hawaelewi nini kimemkumba mchezaji yule aliyeingia muda mfupi tu na kuonesha vitu hadimu sana kwa kuwachachafya wachezaji saba tegemeo wa Nigeria lakini yakamkuta mazito yasiyojulikana yalipotokea..!! hii iliwashangaza wengi sana na si kwa wale tu waliokuwa uwanjani bali hadi waliokuwa wanafatilia mtinange ule kupitia tv hususani wananchi wa Tanzania walijikuta wanaghadhibika sana na kuwalaani wanaigeria wakiami kuwa ule ulikuwa uchawi tu walioutega gorini si kweli kabisa eti nyonga imestuka kama ambavyo wachambuzi wa Spersport walivyokuwa wanasema muda mfupi baada ya kuwa wanalirudia rudia lile tukio kwa karibu na kiminyato jinsi alivyoanguka Dullah.
Jopo la madaktari wa Nigeria waliungana na wenzao wa Tanzania ili kumsaidia Dullah pale nje na kumfunga ule mguu huku wakimpulizia dawa mbalimbali za kutuliza maumivu na kulegeza nyonga ambapo ajabu hakukuonekana hata dariri kama alikuwa anapata nafuu zaidi ya kulalamika kuwa maumivu yanazidi na hapo ndipo walipoamua kumpakia kwenye gari ya wagonjwa iliyokuwa pale uwanjani kwaajili ya dharula na haraka safari ya kumpeleka hospitali ilianza ili akachunguzwe kitaalam zaidi ule mguu wake umepatwa na nini..(?)
* * * *
WIKI MBILI KABLA - NIGERIA
__________________________
Pastor George kwa mara nyengine tena alifunga safari ya kwenda kukutana na Chinedu kwa ajili ya kumaliza suala lile waliloongea juu ya Dullah na Asunta na hii ilimchochea mno kwenda kule kule Nigeria mara baada ya kusikia kwenye vyombo vya habari juu ya uteuzi wa kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania baada ya kuongezwa majina mapya kwa mara ya kwanza na kulisikia jina la adui wa moyo wake Dullah likiwa ni miongoni mwa majina ya wachezaji walioongezwa kwa mara ya kwanza.
Aliwasiliana na Chinedu kama kawaida baada ya kufika walielekea kule kwenye makazi ya Chinedu na kuanza mambo yao kwenye chumba kile cha kichawi kama ilivyo desturi yao na Pastor kuanza kunuia anachotaka afanywe Dullah ili iwe njia rahisi ya kutoonekana machoni mwa mwanae hadi ajifungue na ndipo wammalize kabisa.
"Wakuu, nataka huyu kijana mwenye manywele pindi atapokuja na wenzake kwaajili ya kucheza huo mpira hapa kwenye ardhi hii yenu tukufu basi mumtie adabu kwa kumpa adhabu itayomfanya imlaze kitandani ashindwe kutembea hadi mwanangu Asunta atapojifungua ndipo mumpeleke kabisa kuzimu...."
aliongea Pastor George huku akiwa kashika kile kimdori cha maajabu na baada ya kumaliza nia yake ile alimkabidhi kile kimdori Chinedu ambae nae alifanya yake kimaajabu ndipo moshi ukaanza kufuka na kutengeneza tena kifungu kama cha tv pale juu ya chumba na mara ilisikika sauti iliyokuwa inaongea lugha ambayo Pastor hakuielewa zaidi ya Chinedu ambae alikuwa anamtafsiria na kisha moshi ule ukatoweka kwa kurudi moja kwa moja kwenye kile kimdori.
"Hahahahaaaa Mutume Joji wewe ni mutu ya bahati sanaaa, hahaha aa Habari iko muzuri kabisaaaaaa, misiku si mingi akifika hapa Lagosi jua hatorudi kama alivyokujaaa. Huyu ambae metoka zugumza hapa ni Jini mukubwaaaa sanaaaaaaaaaa saaaaanaaaa, naye atamfanyia muchezo mudogo sana hahahahaaaaaa"
aliongea kwa kujiamini Chinedu na kufurahi pamoja na Pastor George ambae habari zile ziliukuna sawia moyo wake na kuisubiri hiyo siku kwa hamu kubwa sana.
*******
Siku ya mechi ilifika ambapo kwa upande wa Pastor George alikuwa tayari amerejea nyumbani Tanzania akindelea kujitangaza na kujichukulia umaarufu mkubwa kuwa yeye ni nabii mpya mwenye upako mkubwa baada ya kutokewa na Yesu usiku na kum bariki ili kupitia yeye awasaidie na binaadam wengine wenye shida.
Hakuwa na aibu wala soni Pastor George pindi awapo jukwaani akijinadi kuwa yeye ni miongoni mwa wabora katika kizazi cha mwisho mwisho.
Na baada ya mizunguko siku ile ambayo alikuwa anaisubiri kwa hamu sana usiku wake majira ya saa moja ilipotimu alikaa sebuleni na watoto wake wale wawili wa kiume waliokuwa wapo likizo baada ya kuwa muda mwingi wanakuwa boarding shuleni.
Hata watoto wake wenyewe walishangaa siku hiyo kuona baba yao akiwa na 'mzuka' (shauku) sana kuangalia mpira siku hiyo baina ya Nigeria na Tanzania huku wakijua fika kuwa baba yao hakuwa mpenzi kabisa na mpira hata ukimwambia awataje wachezaji watano wa timu ya taifa alikua hawajui lakini hawakujua siku hiyo kulikoni yeye kuwa mtu wa kwanza kufatilia matangazo yale ya mpira tokea saa moja kasoro usiku wakati mechi husika ilikuwa ni saa moja na nusu?
Hata mkewe siku hiyo aliona maajabu na kubaki anacheka.
"Hee! mume wangu naona na wewe leo unaonesha uzalendo?"
"hahaaa si unajua sisi watakatifu macho yetu yanaweza kuwa neema muda mwengine kuwatazama vijana wa nyumbani wanaolitangaza taifa."
alijinasibu Pastor George lakini ukweli ulibaki moyoni mwake juu ya kile kilichomsukuma kuiangalie ile Mechi.
Na kweli baada ya Dullah n=kuingia na kufanya vitu vya ajabu vilivyowafurahisha wanae kwa jinsi alivyokuwa anawachambua wachezaji wa Nigeria lakini mara aliposhindwa kufunga na kuanguka wote walistuka kusikia ukelele wa furaha uliomtoka ghafra Pastor George pale sebuleni.
"Weeeeweeeeeeeeeeeeeeee.."
ITAENDELEA
["Unasema Chinedu mwanangu Asu anaaa...?!"]
aliuliza tena Pastor George baada ya kukaa kwa dakika nzima akitetemeka midomo pindi alipokuwa anafikiria cha kujibu na kujikuta anauliza mithili ya kwamba alivyoambiwa awali hakusikia.
[["Mwanao Asunta kipindi tunafanya ile mudawa tulikosea kitu moja ambayo hatukukijua nacho ni Mimba. Na tatizo itakuja ule upendo aliokuwa nao Asunta sambamba na mudawa tuliyoifanyia kazi zote zimeingia tumboni kwa kiumbe ambaye ana damu ya mutu yule tumemrogea Asunta amsahau na sasa muunganiko wa yule mutoto ndio unamrudishia fahamu mwanao na kujiuliza maswali, na atavyozidi kuiona sura ya yule kijana ndivyo habari itapozidi kutumwa kwenye memory za mutoto ambae nae atamsababishia mamaake kumuonesha vile vyote vilivyojificha juu ya yule mtu aliyemfikiria, na hapo hadi ulichokifanya kitakuwa wazi kwenye maono ya mwanao."]]
maneno ya Chinedu kwa njia ya simu yalizidi kukichanganya kichwa cha Pastor George na kubaki na bumbuwazi kusikia kumbe ujauzito aliokuwa nao mwanae ni wa yule adui yake mkubwa manywele?
Na si kwamba ni ya Fredy kama alivyodhani...!
["Yaani Mimba ya yule mshenzi hasidi wa maendeleo ya mwanangu?"]
aliuliza kwa ghabhabu Pastor George mithili ya kwamba alikuwa haongei kwa simu.
[["Usifoke George ndio hivyo ilivyo, sasa unachotakiwa wewe kuamua jinsi ya kufanya ili Asu asipate muda wa kumfikiria au kumuona iwe kwenye picha au live"]]
["Huyu afe tuu, Fanya mpango Chinedu ua kabisa manywele hili"]
[["hahahahahaaa George kumuua huyu ni kumuua na mwanao pia kwani endapo akisikia habari za kufariki kwake akiwa bado hajajifungua jua nstuko ataoupata yule mtoto utamfanya aruke mfurulizo tumboni na kumkosesha hewa na nguvu mwanao na lazima afe tu"]]
jibu la Chinedu lilizidi kumchanganya George asijue sasa wamfanyeje Dullah kwani ni kweli atapofariki lazima Asu atasikia na yote imechochewa na umaarufu ule wa Dullah ulioanza kuonekana siku baada ya siku akiwa nchini Kenya.
["Chinedu, naomba nisaidie jinsi ya kufanyaaaa"]
[["sawa George, Hapa nitachofanya ni kumtengeneza VUNJESHA ambae ataenda kumshughulikia katika kazi yake onayosababisha kusikiwa na Asunta muda mwingi na ataenda kuugulia kwao hadi Asu atapojifungua sasa hapo ndipo tunamaliza muchezooo hahahaha']]
ushauri wa Chinedu uliungwa mkono moja kwa moja na Pastor George na baada ya kufika ule muafaka waliagana na kukata simu.
"Mwana izaya huyuuu, Dunga dunga... Kamdunga mwanangu Mimba ya pili??!!"
alijiongelea kwa uchungu Pastor George huku akisimama kujiandaa kutoka mule chumbani.
* * * *
NAIROBI - KENYA
________________
Furaha mara dufu ilirejea katika familia ya Dullah mara baada ya Ilham kurejewa na akili zake za kawaida mara aliporuhusiwa kule kwa mganga na kuhamia kwenye nyumba ile nzuri waliyokuwa wanaishi ambayo ilikodiwa na Tusker fc kwa niaba ya star wao Dullah.
Ilham aliona kama ndoto maisha yale ambapo kila siku walikuwa wanakula vyakula vizuri, wanavaa vizuri na mambo kwenda raha mustarehe.
Sala na maombi ya mama Dullah yalianza kujibu kwa kuonesha dariri za wazi wazi kwamba Ilham anampenda sana Roja na Roja anampenda sana Ilham ila tatizo kila mtu alikuwa anahofia kumuanza mwenzake kutokana na heshima iliyokuwepo baina yao.
Roja alimuheshimu sana mama Dullah na kutokana na urafiki wake mkubwa na Dullah ilifika wakati alijifikiria kama Ilham anamchukulia sawa na kakaake tu, kumbe hata Ilham nae alikuwa na hisia hizo na kuogopa kumtamkia Roja akichukulia kutokana na urafiki wao na kakaake Dullah basi hata na yeye Roja anamchukulia kama mdogo ake tu.
Na hata walivyokuwa wanapiga story mbalimbali na kucheka pamoja kila mtu alikuwa na hisia zake moyoni mwake lakini kwa utu uzima wa mama Dullah alibaini kuwa kuna kitu akilini mwao hasa kwa mwanae Ilham.
Baada ya mwezi mwengine kuisha wakati wakiwa mapomziko ambapo iliwabidi Dullah na Roja kusafiri hadi Tanzania mara baada ya kupigiwa upatu na Clouds fm, hatimae wote waliitwa kwa mara ya kwanza kwenye kikosi cha timu ya Taifa kwenye michuano ya kukata tiketi kucheza kombe la Dunia.
Ilikuwa ni habari njema kabisa kwao na ya furaha kwa kuingia kwenye historia ya kuitwa timu ya Taifa jambo ambalo kila mchezaji alilitamani kwani anapoonesha kiwango bora na timu ya Taifa anakuwa amelitangaza taifa lake.
"Hili ni tukio kubwa sana Dullah ona mwenyewe ratiba ilivyowekwa daah! mechi ya kwanza wiki mbili zijazo harafu mzee tunapanda dege hadi Nigeria?"
aliongea Roja mara baada ya kila mchezaji aliyeitwa kupewa kijitabu kidogo cha ratiba nzima ya mechi za makundi kuingia katika mtoano wa kuzipata timu za taifa 5 ambazo zitaiwakilisha Afrika katika michuano ile mikubwa kabisa katika ngazi ya mpira wa miguu.
Timu ya Tanzania maarufu kama Taifa Starz wao walieka Kambi Bagamoyo mkoani Pwani wakijiandaa na safari ambayo ilikuwa inawakutanisha na timu ya Nigeria iliyokuwa kundi moja na wao.
Mbali ya kuwa Dullah na Roja walikuwa na umaarufu lakini bado umaarufu wao haukusambaa kwa wananchi wote wapenda michezo zaidi ya wale wachache waliobahatika kuwaona uwanjani.
Hata ile siku ya siku ilipofika na timu ya Taifa ya Tanzania ilipoondoka kwenda jijini Lagos kukutana na moja ya timu ngumu ya Nigeria na watu walijua kuwa Tanzania wanachokifata kule ni kipigo tu kutokana na kuachwa mbali katika viwango vya ubora wa kisoka kwa mujibu wa Fifa.
Lakini manaojua wanasema mpira ni dakika tisini ndio zinazoamua, na kwa mara ya kwanza Dullah pamoja na Roja waliweza kuchanganyika na watu maarufu waliowajua kabloa toka wanacheza Tandale na humo D alukutana na John beki kisiki wa Simba mbae aliijua vizuri habari ya Dullah mara baada ya kuangushwa kwa vyenga zaidi ya mara mbili.
***********
Maneno ya Mbwiga na Shafii kuhusu uwezo wa ajabu wa Dullah kupitia Clouds fm radio ndio yaliwahamasisha watu wengi kukaa kwenye mabanda ya video siku hiyo kuangalia mtanange mkali ambao walijua kuwa timu yao kushinda si rahisi kutokana na kuzidiwa kila idara tangia kipindi cha kwanza hadi kinamalizika walikuwa washafungwa goli moja kwa bila.
Kipindi cha pili kilianza huku Tanzania safari hii wakijitahidi kushambulia ili wapate goli lakini hadi dakika ya 80 mambo yalizidi kuwa magumu kutengeneza nafasi ya ushindi japo kipa wa Tanzania alifanya jitihada nyingi sana hadi wanigeria walishangaa kwa jinsi alivyokuwa anaokoa magoli ya wazi kabisa.
Kocha alikata shauri na kuamua kumuingiza Rastaman Dullah kwa mara ya kwanza ili akajaribu na yeye bahati yake baada ya mshambuliaji tegemeo wa Tanzania kuuniana hapo ndipo jicho la kila mtanzania lilipoganda kwenye tv kumuangalia kwa umakini huyo mchezaji aliyesifiwa wiki nzima kupitia clouds baada ya kuitwa na kocha wa timu ya Taifa kwa mara ya kwanza.
Na kweli Dulla baada ya kuingia ile ilipofika dakika ya 87 alifanya vitu vya ajabu sana pindi timu yao ilipokuwa inashambuliwa na mpira ulipookolewa na kuja kwake akiwa zaidi ya mita sitini na gori la timu pinzani, alianza kukimbia na mpira na kuwachambua kama karanga wachezaji sita wa Nigeria waliokuwa mbele yake huku uwanja mzima ukiwa umesimama hadi Rais wa Nigeria ambae alikuwa mgeni rasmi siku hiyo ya mechi nae alisimama na kustaajabu na si kwa uwezo ule pakee aliouonesha Dullah... Bali ni baada ya kuwachenga wachezaji sita na alipotokea goli kipa nae alimpiga chenga ya maudhi na hatimae kubaki yeye na goli lakini chaajabu na kushangaza Dullah alipotaka kuupiga ule mpira alisita na kusimama ghafra mbele ya macho ya watu zaidi ya elfu arobaini walimshuhudia Rasta wa Tanzania akishindwa kuipatia point muhimu timu yake ya Taifa na kuuganda kwa sekunde kadhaa na kuanguka mzima mzima bila kusukumwa wala kuguswa na yeyote
Kipa wa Nigeria aliwahi na kuukimbilia mpira uliokuwa unaelekea gorini taratibu na kuudaka kabla wachezaji wengine pamoja na madaktari wa timu ya Tanzania hawajakimbilia uwanjani pindi refa alipopuliza kipenga cha kuusimamisha mchezo kutokana na kudondoka ghafra kwa Dullah.
"Aaaaaagggggg... Rooojaaaaaa Nakufaaaa aaaagggg"
alipiga kelele Dullah pindi madaktari na wachezaji wenzake walipofika pale alipodondokea kutaka kujua nini kimemkumbuka lakini hawakuweza kwa kuona jeraha kwa macho wala uvimbe zaidi ya kuhisi kuwa mguu ule wa kushoto ambao ndio alikuwa anautumia sana Dullah kuuchezea mpira, ulikuwa unamletea maumivu makali ukiwa umekakamaa huku ukivibrate mithili ya simu mbovu ya kichina.
Kadri madaktari walivyomshika ule mguu kuangalia harakaharaka tatizo ili wampatie huduma ya kwanza ndivyo Dullah alivyozidi kupiga kelele huku akimwita Roja ambae alikuwa hajaingizwa kabisa kucheza siku hiyo lakini pindi alipomuona rafiki ake akidondoka ghafra yeye nae alikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kufika pale alipodondoka Dullah huku akiwa na wasiwasi mkubwa.
Kutokana na sheria za michezo ilibidi Dullah abebwe kwenye machera ili akatibiwe vizuri nje ya uwanja kupisha kipute kiendelee na hapo ndipo kocha wa Tanzania alipomuamuru Roja achukue nafasi ya rafiki ake aliyekuwa anatolewa huku akipiga sana kelele za maumivu makali hadi kila mchezaji na aliyekuwepo pale uwanjani walimuonea huruma na wengine walijikuta wakitokwa machozi wakiwa hawaelewi nini kimemkumba mchezaji yule aliyeingia muda mfupi tu na kuonesha vitu hadimu sana kwa kuwachachafya wachezaji saba tegemeo wa Nigeria lakini yakamkuta mazito yasiyojulikana yalipotokea..!! hii iliwashangaza wengi sana na si kwa wale tu waliokuwa uwanjani bali hadi waliokuwa wanafatilia mtinange ule kupitia tv hususani wananchi wa Tanzania walijikuta wanaghadhibika sana na kuwalaani wanaigeria wakiami kuwa ule ulikuwa uchawi tu walioutega gorini si kweli kabisa eti nyonga imestuka kama ambavyo wachambuzi wa Spersport walivyokuwa wanasema muda mfupi baada ya kuwa wanalirudia rudia lile tukio kwa karibu na kiminyato jinsi alivyoanguka Dullah.
Jopo la madaktari wa Nigeria waliungana na wenzao wa Tanzania ili kumsaidia Dullah pale nje na kumfunga ule mguu huku wakimpulizia dawa mbalimbali za kutuliza maumivu na kulegeza nyonga ambapo ajabu hakukuonekana hata dariri kama alikuwa anapata nafuu zaidi ya kulalamika kuwa maumivu yanazidi na hapo ndipo walipoamua kumpakia kwenye gari ya wagonjwa iliyokuwa pale uwanjani kwaajili ya dharula na haraka safari ya kumpeleka hospitali ilianza ili akachunguzwe kitaalam zaidi ule mguu wake umepatwa na nini..(?)
* * * *
WIKI MBILI KABLA - NIGERIA
__________________________
Pastor George kwa mara nyengine tena alifunga safari ya kwenda kukutana na Chinedu kwa ajili ya kumaliza suala lile waliloongea juu ya Dullah na Asunta na hii ilimchochea mno kwenda kule kule Nigeria mara baada ya kusikia kwenye vyombo vya habari juu ya uteuzi wa kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania baada ya kuongezwa majina mapya kwa mara ya kwanza na kulisikia jina la adui wa moyo wake Dullah likiwa ni miongoni mwa majina ya wachezaji walioongezwa kwa mara ya kwanza.
Aliwasiliana na Chinedu kama kawaida baada ya kufika walielekea kule kwenye makazi ya Chinedu na kuanza mambo yao kwenye chumba kile cha kichawi kama ilivyo desturi yao na Pastor kuanza kunuia anachotaka afanywe Dullah ili iwe njia rahisi ya kutoonekana machoni mwa mwanae hadi ajifungue na ndipo wammalize kabisa.
"Wakuu, nataka huyu kijana mwenye manywele pindi atapokuja na wenzake kwaajili ya kucheza huo mpira hapa kwenye ardhi hii yenu tukufu basi mumtie adabu kwa kumpa adhabu itayomfanya imlaze kitandani ashindwe kutembea hadi mwanangu Asunta atapojifungua ndipo mumpeleke kabisa kuzimu...."
aliongea Pastor George huku akiwa kashika kile kimdori cha maajabu na baada ya kumaliza nia yake ile alimkabidhi kile kimdori Chinedu ambae nae alifanya yake kimaajabu ndipo moshi ukaanza kufuka na kutengeneza tena kifungu kama cha tv pale juu ya chumba na mara ilisikika sauti iliyokuwa inaongea lugha ambayo Pastor hakuielewa zaidi ya Chinedu ambae alikuwa anamtafsiria na kisha moshi ule ukatoweka kwa kurudi moja kwa moja kwenye kile kimdori.
"Hahahahaaaa Mutume Joji wewe ni mutu ya bahati sanaaa, hahaha aa Habari iko muzuri kabisaaaaaa, misiku si mingi akifika hapa Lagosi jua hatorudi kama alivyokujaaa. Huyu ambae metoka zugumza hapa ni Jini mukubwaaaa sanaaaaaaaaaa saaaaanaaaa, naye atamfanyia muchezo mudogo sana hahahahaaaaaa"
aliongea kwa kujiamini Chinedu na kufurahi pamoja na Pastor George ambae habari zile ziliukuna sawia moyo wake na kuisubiri hiyo siku kwa hamu kubwa sana.
*******
Siku ya mechi ilifika ambapo kwa upande wa Pastor George alikuwa tayari amerejea nyumbani Tanzania akindelea kujitangaza na kujichukulia umaarufu mkubwa kuwa yeye ni nabii mpya mwenye upako mkubwa baada ya kutokewa na Yesu usiku na kum bariki ili kupitia yeye awasaidie na binaadam wengine wenye shida.
Hakuwa na aibu wala soni Pastor George pindi awapo jukwaani akijinadi kuwa yeye ni miongoni mwa wabora katika kizazi cha mwisho mwisho.
Na baada ya mizunguko siku ile ambayo alikuwa anaisubiri kwa hamu sana usiku wake majira ya saa moja ilipotimu alikaa sebuleni na watoto wake wale wawili wa kiume waliokuwa wapo likizo baada ya kuwa muda mwingi wanakuwa boarding shuleni.
Hata watoto wake wenyewe walishangaa siku hiyo kuona baba yao akiwa na 'mzuka' (shauku) sana kuangalia mpira siku hiyo baina ya Nigeria na Tanzania huku wakijua fika kuwa baba yao hakuwa mpenzi kabisa na mpira hata ukimwambia awataje wachezaji watano wa timu ya taifa alikua hawajui lakini hawakujua siku hiyo kulikoni yeye kuwa mtu wa kwanza kufatilia matangazo yale ya mpira tokea saa moja kasoro usiku wakati mechi husika ilikuwa ni saa moja na nusu?
Hata mkewe siku hiyo aliona maajabu na kubaki anacheka.
"Hee! mume wangu naona na wewe leo unaonesha uzalendo?"
"hahaaa si unajua sisi watakatifu macho yetu yanaweza kuwa neema muda mwengine kuwatazama vijana wa nyumbani wanaolitangaza taifa."
alijinasibu Pastor George lakini ukweli ulibaki moyoni mwake juu ya kile kilichomsukuma kuiangalie ile Mechi.
Na kweli baada ya Dullah n=kuingia na kufanya vitu vya ajabu vilivyowafurahisha wanae kwa jinsi alivyokuwa anawachambua wachezaji wa Nigeria lakini mara aliposhindwa kufunga na kuanguka wote walistuka kusikia ukelele wa furaha uliomtoka ghafra Pastor George pale sebuleni.
"Weeeeweeeeeeeeeeeeeeee.."
ITAENDELEA