Prince Naahjum_
Senior Member
- Jun 13, 2016
- 139
- 125
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 10
Lakini kipindi wakiwa wanatembea kuelekea stendi tangia pale mlango wa geto la Dullah, kulikuwa na kijana mmoja aliyeshika digital kamera ndogo akiwa kajibana kwenye kona moja ya uchochoro na akawa anawapiga picha kinyemela pasi na wao kujua hadi pale Asunta anapanda kwenye gari yake na kuondoka.
Dullah akiwa mwenye furaha wakati anarudi kuelekea getto kwake mara alishikwa bega kwa nyuma na alipogeuka alikutana na sura ya mtu asiyemfahamu.
"samahani kaka mi mgeni maeneo haya naitwa Sam naomba nikuulize samahani lakini eti njia inayotojea Tandale hospitali ni ipi hapa?"
aliuliza yule kijana.
"Nyoosha hii moja kwa moja hadi ukipita soko mbelembele kidogo ndo utakuta hospitali."
"haya poa, nashukuru ndugu yangu samahani kwa kukusumbua hivi unaitwa nani?"
"D"
alijibu kifupi Dullah huku akiondoka pasi na kujua mtu aliyekuwa anaongea nae ni nani na laiti angejua huenda angeangusha hata kasheshe (ugomvi/timbwili).
Dullah aliendelea na zake huku yule kijana nae akaendelea na safari yake ya uongoa na baada ya hatua chache alimtazama Dullah na kutikisa kichwa kumsikitikia baada ya hapo aliingia kwenye duka moja ambapo kumbe alipaki pikipiki yake kubwa aina ya Honda na kuiwaha nae kutimka zake maeneo yale.
Hakuwa mwengine yule kijana bali ni yule yule aliyekuwa anawapiga picha za mnato yeye na Asu pasi na wao wenyewe kujua.
* * * * *
((WIKI MOJA KABLA))-MASAKI
................................
Baada ya kurudi kutoka katika kuhubiri neno la Mungu tena safari hii alirejea akiwa na mgeni mkubwa ambae ni Askofu mkuu wa Kenya aliyeamua kuongozana na Pastor George kuja kutazama anapoishi na maendeleo yote ya shughuli za ibada na uchamungu ili kuzidi kudumisha urafiki wao wa kimwili na kiroho na akiwa nyumbani Pastor alibaini ukosefu wa furaha aliokuwa nao binti ake kipenzi Asunta.
Alijaribu kutafuta chanzo cha Asu kukosa furaha na haikuwa kawaida na safari zote kumkuta katika hali ile ndipo Pastor George alimpeleleza sana mkewe kwa maswali ya hapa na pale juu ya mtoto wao kukosa furaha.
"mh! baba Asu labda kutokana na kumzuia kwangu kuwa asiende mazoezini wala asitoke nyumbani mpaka urudi."
"He! kwanini sasa uliamua hivyo na sio kawaida yako, kuna tukio lolote baya alifanya?"
"Hapana mme wangu ila nilikuwa na hofu nae tangia siku ile alipoacha kwenda mazoezini na kwenda sehemu anazozijua yeye, sasa afadhali babaake ukiwepo utajua jinsi ya kumtafuta kuliko mimi mama tu."
majibu ya mama Asu Pastor aliyaelewa lakini kidogo upande mmoja alibaini lazima itakuwa Asunta alirudia abia yake ya kuchelewa nyumbani tu, na ndipo safari hii aliamua kutengeneza plani ambayo hakumshilikisha mtu yeyote kati yao zaidi ya kijana mmoja aliyekuwa anaitwa Samson ambae alikuwa mmoja wa waumini wake pale Kanisani.
Siku hiyo alimwita Sam pembeni baada ya ibada ya jumapili kuisha.
"Ewe kondoo wa bwana ulie mbele yangu."
"Ndio baba mchungaji nakusikiliza."
"Bwana amenionesha katika maono kuwa nikuteue wewe katika shughuli maalum unayopaswa kuifanya kwa siri kubwa pasi na mtu mwengine kujua zaidi yetu na bwana. je uko tayari.?"
"Niko tayari baba ila ningependa kujua shughuli gani hiyo."
"Sam, roho mtakatifu amesema nami katika maono kuwa wewe ni kijana hodari sana nami nakutuma kazi moja ya kumpeleleza binti angu kwa siri hususani kwenye safari zake nje ya nyumbani nataka uwe unamfatilia hasa nyakati za asubuhi kuanzia kesho anapokwenda mazoezini na ataporudi hakikisha uwe unampiga picha kila tukio ama sehemu anayopitia ambayo iko tofauti. je utaweza?"
"sawa baba niko tayari.. Nitaweza."
"Basi vizuri sana Sam, chukua hii namba zungumza na huyu mtu mwambie wewe ndie kijana uliyeelekezwa na Pastor uende ukaichukue hiyo pikipiki aina ya Honda. Nakuahidi Sam endapo utafanikisha vizuri zoezi hili basi hiyo pikipiki itakuwa ya kwako moja kwa moja. Neema ya bwana iwe juu yako."
"Asante sana babaa eeemen."
"basi sawa nataka ujue kuanzia kesho utapoiona ile benzi yangu mpya basi ujue huyo ni Asuna na unapaswa kuifatilia."
baada ya kumaliza maongezi na Sam Pastor alifanya ibada fupi palepale na kuachana na Sam na ndipo jioni ya siku hiyo alipoongea na mwanae na kumruhusu kuanzia kesho aanze kwenda mazoezini.
"Najua mwanangu jinsi gani umekosa furaha toka mamaako akuzuie kwenda mazoezini, nami nabatilisha kauli hiyo kuanzia leo nahitaji furaha ya mwanangu irejee mahali pake na kuanzia kesho mama utaanza kwenda kwenye mazoezi na ratiba zako zote zitakuwa wazi pia chukua funguo hizi za ile Benzi yangu kwani gari yako sasa itatumika kwenye shughuli ndogo ndogo tu za kumpeleka house girl sokoni sipendi mwanangu utembelee gari yenye matatizo."
aliongea Pastor na Asunta alifurahi mno moyoni mwake na kujua sasa atapata nafasi ya kukutana tena na Dullah bila kujua nini kinachoendelea nyuma ya Pazia.
* * * * *
Baada ya kurudi nyumbani Asunta huku akiwa mwenye mawazo kidogo lakini alijilazimisha kuonekana mtu mwenye furaha aliingia ndani na kulala huku fikra zake zote zikiwa juu ya Dullah vipi atakubali kubadili dini ili iwe njia rahisi ya kuwa nae.
Ilipotimu majira ya jioni Pastor alirejea akiwa na baba Askofu na walipokuwa sebureni wakiendelea na maongezi yao ndipo Pastor alipoiita familia yake kwa maongezi maalum.
Asunta alistuka baada ya kusikia kuna kikao tena mbele ya babaaskofu lakini alipata amani baada ya kumuona babaake akiwa ni mtu mwenye tabasamu muda wote na ndipo moyoni Asu alijua kuwa si kikao kilichomuhusu yeye kwenye makosa yake zidi ya Dullah kwani awali alihisi huenda babaake kagundua kitu.
"Mama Asunta hii ni habari njema kutoka kwa baba Askofu juu ya maendeleo ya binti yetu Asunta na katika msingi wake wa hapo baadae. Natumani hii habari ninayoisema hivi sasa itapokelewa kwa furaha na kila mmoja wetu kama jinsi ilivyotufurahisha sisi wenyewe, Habari yenyewe ni hivi, tunajua kuwa zimebaki siku mbili tu baba Askofu itapaswa arejee Nairobi sasa katika safari yake imetokea bahati naweza kusema ni bwana mwenyewe ndie amaemua kuwa baba Askofu aondoke na mwanetu Asunta kwenda kuanza masomo maalum ya kisayansi na kiroho katika chuo maalum jijini Nairobi...."
"BABAA!!"
Almanusura Asunta azimie kwa taarifa hizi na kujikuta anamkatisha babaake kwa kumwita ghafra huku akiwa ametahayuri hadi baba Askofu alishangaa.
"Vipi tena Asunta mwanangu mbona unatustua mama."
aliongea Pastor George na kumgutusha Asunta ambae alidhani alipayuka moyoni mwake tu kumbe alitoa sauti iliyomstua kila mtu.
"Babaa.. Baba Askofu Siamini kwa kweli nashukuru sana kwa nafasi hii nzuri ya kipekee lakini.."
"Lakini nini tena Asunta mwananguu!"
alimkatisha tena Pastor George na Asunta kubaki kimya akishindwa kuelezea sababu yake iliyomfanya atie 'lakini' katika maneno yake.
"Baba Askofu kama unavyoona mwenyewe na jinsi nilivyokwambia kuwa habari hizi tutapomwambia Asunta mwanangu kwa jinsi ninavyomjua anavyopenda elimu ya kisayansi na mazingira ya kiroho aliyokulia lazima furaha yake itapitiliza na hatoamini hahahahaaaa Ubarikiwe sana mwanangu Asunta"
aliongezea Pastor George maneno yaliyozidi kumchoma na kumkata maini Asunta na ilibidi atabasamu tu japo moyoni mwake alikuwa anaumia na alihisi huenda ile ni mbinu mbadala aliyoamua kuitumia babaake ili kuzidi kumtenganisha na kipenzi chake Dullah ambae alishamwambia kuwa hataki kulisikia jina kama hilo tena.
"ha ha ha Neema ya bwana izidi kuing'arisha nyumba hii Pastor George."
"Ameeen baba Askofu."
"Lakini binti ako niliona kama bado alitaka kuzungumza.! Eti Asunta umefurahishwa na habari hii mpaka katika moyo wako?"
aliuliza baba Askofu swali ambalo lilimfanya Asunta achelewe sekunde kadhaa kulijibu baada ya kutokea vita vikali baina ya moyo wake na akili zake. Akili zilimtuma akubali kuwa amefurahi ili atunze heshima ya babaake na maneno yake yazidi kuaminiwa na Askofu lakini moyo ulimkatalia na kumwambia aongee ukweli tu kuwa hajafurahishwa ili aeke abaki na uaminifu wake mbele ya Dullah.
"Asunta mwanangu baba Askofu si anakuuliza wewe?"
alidakia mamaake na kumstua tena Asunta
"Eeeh.. eeh ndio baba Askofu nimefurahishwa, nimefurahishwa sana baba Askofu Nimefurahi kwa kweli Mungu akubariki sana baba."
aliamua kuzilidhisha akili zake Asunta huku akiuchoma sindano ya maumivu moyo wake lakini hakuwa na jinsi yote yale aliyafanya kwa lengo la kulinda heshima ya wazazi wake mbele ya baba Askofu.
"hahahaa Umeona baba Askofu yaani hapo ninavyomjua Asunta mwanangu ndio ushampeleka kwenye mawazo ya huko chuo hahaha"
alifurahi Pastor George huku akimuangalia Asunta na walipokutana macho kwa macho jicho la Pastor George lilionesha alama ya hasira tofauti na sauti na uso wake na hii aliigundua Asunta na kuamini kuwa ile ni palni tu ya babaake.
"Vizuri sana mwanangu Asunta"
"Asante baba Askofu"
alijibu na kuonesha tabasamu bandia Asunta lililomuaminisha baba Askofu japo kwa upande wa moyo wa Pastor George na mkewe walijua wazi kuwa mtoto wao hajapendezewa hata kidogo na safari ile lakini hawakuwa na jinsi ilibidi tu wamsafirishe ili izidi kuwa heri na salama baina yake na kijana huyo wa kiisilaamu.
* * * *
ITAENDELEA
Lakini kipindi wakiwa wanatembea kuelekea stendi tangia pale mlango wa geto la Dullah, kulikuwa na kijana mmoja aliyeshika digital kamera ndogo akiwa kajibana kwenye kona moja ya uchochoro na akawa anawapiga picha kinyemela pasi na wao kujua hadi pale Asunta anapanda kwenye gari yake na kuondoka.
Dullah akiwa mwenye furaha wakati anarudi kuelekea getto kwake mara alishikwa bega kwa nyuma na alipogeuka alikutana na sura ya mtu asiyemfahamu.
"samahani kaka mi mgeni maeneo haya naitwa Sam naomba nikuulize samahani lakini eti njia inayotojea Tandale hospitali ni ipi hapa?"
aliuliza yule kijana.
"Nyoosha hii moja kwa moja hadi ukipita soko mbelembele kidogo ndo utakuta hospitali."
"haya poa, nashukuru ndugu yangu samahani kwa kukusumbua hivi unaitwa nani?"
"D"
alijibu kifupi Dullah huku akiondoka pasi na kujua mtu aliyekuwa anaongea nae ni nani na laiti angejua huenda angeangusha hata kasheshe (ugomvi/timbwili).
Dullah aliendelea na zake huku yule kijana nae akaendelea na safari yake ya uongoa na baada ya hatua chache alimtazama Dullah na kutikisa kichwa kumsikitikia baada ya hapo aliingia kwenye duka moja ambapo kumbe alipaki pikipiki yake kubwa aina ya Honda na kuiwaha nae kutimka zake maeneo yale.
Hakuwa mwengine yule kijana bali ni yule yule aliyekuwa anawapiga picha za mnato yeye na Asu pasi na wao wenyewe kujua.
* * * * *
((WIKI MOJA KABLA))-MASAKI
................................
Baada ya kurudi kutoka katika kuhubiri neno la Mungu tena safari hii alirejea akiwa na mgeni mkubwa ambae ni Askofu mkuu wa Kenya aliyeamua kuongozana na Pastor George kuja kutazama anapoishi na maendeleo yote ya shughuli za ibada na uchamungu ili kuzidi kudumisha urafiki wao wa kimwili na kiroho na akiwa nyumbani Pastor alibaini ukosefu wa furaha aliokuwa nao binti ake kipenzi Asunta.
Alijaribu kutafuta chanzo cha Asu kukosa furaha na haikuwa kawaida na safari zote kumkuta katika hali ile ndipo Pastor George alimpeleleza sana mkewe kwa maswali ya hapa na pale juu ya mtoto wao kukosa furaha.
"mh! baba Asu labda kutokana na kumzuia kwangu kuwa asiende mazoezini wala asitoke nyumbani mpaka urudi."
"He! kwanini sasa uliamua hivyo na sio kawaida yako, kuna tukio lolote baya alifanya?"
"Hapana mme wangu ila nilikuwa na hofu nae tangia siku ile alipoacha kwenda mazoezini na kwenda sehemu anazozijua yeye, sasa afadhali babaake ukiwepo utajua jinsi ya kumtafuta kuliko mimi mama tu."
majibu ya mama Asu Pastor aliyaelewa lakini kidogo upande mmoja alibaini lazima itakuwa Asunta alirudia abia yake ya kuchelewa nyumbani tu, na ndipo safari hii aliamua kutengeneza plani ambayo hakumshilikisha mtu yeyote kati yao zaidi ya kijana mmoja aliyekuwa anaitwa Samson ambae alikuwa mmoja wa waumini wake pale Kanisani.
Siku hiyo alimwita Sam pembeni baada ya ibada ya jumapili kuisha.
"Ewe kondoo wa bwana ulie mbele yangu."
"Ndio baba mchungaji nakusikiliza."
"Bwana amenionesha katika maono kuwa nikuteue wewe katika shughuli maalum unayopaswa kuifanya kwa siri kubwa pasi na mtu mwengine kujua zaidi yetu na bwana. je uko tayari.?"
"Niko tayari baba ila ningependa kujua shughuli gani hiyo."
"Sam, roho mtakatifu amesema nami katika maono kuwa wewe ni kijana hodari sana nami nakutuma kazi moja ya kumpeleleza binti angu kwa siri hususani kwenye safari zake nje ya nyumbani nataka uwe unamfatilia hasa nyakati za asubuhi kuanzia kesho anapokwenda mazoezini na ataporudi hakikisha uwe unampiga picha kila tukio ama sehemu anayopitia ambayo iko tofauti. je utaweza?"
"sawa baba niko tayari.. Nitaweza."
"Basi vizuri sana Sam, chukua hii namba zungumza na huyu mtu mwambie wewe ndie kijana uliyeelekezwa na Pastor uende ukaichukue hiyo pikipiki aina ya Honda. Nakuahidi Sam endapo utafanikisha vizuri zoezi hili basi hiyo pikipiki itakuwa ya kwako moja kwa moja. Neema ya bwana iwe juu yako."
"Asante sana babaa eeemen."
"basi sawa nataka ujue kuanzia kesho utapoiona ile benzi yangu mpya basi ujue huyo ni Asuna na unapaswa kuifatilia."
baada ya kumaliza maongezi na Sam Pastor alifanya ibada fupi palepale na kuachana na Sam na ndipo jioni ya siku hiyo alipoongea na mwanae na kumruhusu kuanzia kesho aanze kwenda mazoezini.
"Najua mwanangu jinsi gani umekosa furaha toka mamaako akuzuie kwenda mazoezini, nami nabatilisha kauli hiyo kuanzia leo nahitaji furaha ya mwanangu irejee mahali pake na kuanzia kesho mama utaanza kwenda kwenye mazoezi na ratiba zako zote zitakuwa wazi pia chukua funguo hizi za ile Benzi yangu kwani gari yako sasa itatumika kwenye shughuli ndogo ndogo tu za kumpeleka house girl sokoni sipendi mwanangu utembelee gari yenye matatizo."
aliongea Pastor na Asunta alifurahi mno moyoni mwake na kujua sasa atapata nafasi ya kukutana tena na Dullah bila kujua nini kinachoendelea nyuma ya Pazia.
* * * * *
Baada ya kurudi nyumbani Asunta huku akiwa mwenye mawazo kidogo lakini alijilazimisha kuonekana mtu mwenye furaha aliingia ndani na kulala huku fikra zake zote zikiwa juu ya Dullah vipi atakubali kubadili dini ili iwe njia rahisi ya kuwa nae.
Ilipotimu majira ya jioni Pastor alirejea akiwa na baba Askofu na walipokuwa sebureni wakiendelea na maongezi yao ndipo Pastor alipoiita familia yake kwa maongezi maalum.
Asunta alistuka baada ya kusikia kuna kikao tena mbele ya babaaskofu lakini alipata amani baada ya kumuona babaake akiwa ni mtu mwenye tabasamu muda wote na ndipo moyoni Asu alijua kuwa si kikao kilichomuhusu yeye kwenye makosa yake zidi ya Dullah kwani awali alihisi huenda babaake kagundua kitu.
"Mama Asunta hii ni habari njema kutoka kwa baba Askofu juu ya maendeleo ya binti yetu Asunta na katika msingi wake wa hapo baadae. Natumani hii habari ninayoisema hivi sasa itapokelewa kwa furaha na kila mmoja wetu kama jinsi ilivyotufurahisha sisi wenyewe, Habari yenyewe ni hivi, tunajua kuwa zimebaki siku mbili tu baba Askofu itapaswa arejee Nairobi sasa katika safari yake imetokea bahati naweza kusema ni bwana mwenyewe ndie amaemua kuwa baba Askofu aondoke na mwanetu Asunta kwenda kuanza masomo maalum ya kisayansi na kiroho katika chuo maalum jijini Nairobi...."
"BABAA!!"
Almanusura Asunta azimie kwa taarifa hizi na kujikuta anamkatisha babaake kwa kumwita ghafra huku akiwa ametahayuri hadi baba Askofu alishangaa.
"Vipi tena Asunta mwanangu mbona unatustua mama."
aliongea Pastor George na kumgutusha Asunta ambae alidhani alipayuka moyoni mwake tu kumbe alitoa sauti iliyomstua kila mtu.
"Babaa.. Baba Askofu Siamini kwa kweli nashukuru sana kwa nafasi hii nzuri ya kipekee lakini.."
"Lakini nini tena Asunta mwananguu!"
alimkatisha tena Pastor George na Asunta kubaki kimya akishindwa kuelezea sababu yake iliyomfanya atie 'lakini' katika maneno yake.
"Baba Askofu kama unavyoona mwenyewe na jinsi nilivyokwambia kuwa habari hizi tutapomwambia Asunta mwanangu kwa jinsi ninavyomjua anavyopenda elimu ya kisayansi na mazingira ya kiroho aliyokulia lazima furaha yake itapitiliza na hatoamini hahahahaaaa Ubarikiwe sana mwanangu Asunta"
aliongezea Pastor George maneno yaliyozidi kumchoma na kumkata maini Asunta na ilibidi atabasamu tu japo moyoni mwake alikuwa anaumia na alihisi huenda ile ni mbinu mbadala aliyoamua kuitumia babaake ili kuzidi kumtenganisha na kipenzi chake Dullah ambae alishamwambia kuwa hataki kulisikia jina kama hilo tena.
"ha ha ha Neema ya bwana izidi kuing'arisha nyumba hii Pastor George."
"Ameeen baba Askofu."
"Lakini binti ako niliona kama bado alitaka kuzungumza.! Eti Asunta umefurahishwa na habari hii mpaka katika moyo wako?"
aliuliza baba Askofu swali ambalo lilimfanya Asunta achelewe sekunde kadhaa kulijibu baada ya kutokea vita vikali baina ya moyo wake na akili zake. Akili zilimtuma akubali kuwa amefurahi ili atunze heshima ya babaake na maneno yake yazidi kuaminiwa na Askofu lakini moyo ulimkatalia na kumwambia aongee ukweli tu kuwa hajafurahishwa ili aeke abaki na uaminifu wake mbele ya Dullah.
"Asunta mwanangu baba Askofu si anakuuliza wewe?"
alidakia mamaake na kumstua tena Asunta
"Eeeh.. eeh ndio baba Askofu nimefurahishwa, nimefurahishwa sana baba Askofu Nimefurahi kwa kweli Mungu akubariki sana baba."
aliamua kuzilidhisha akili zake Asunta huku akiuchoma sindano ya maumivu moyo wake lakini hakuwa na jinsi yote yale aliyafanya kwa lengo la kulinda heshima ya wazazi wake mbele ya baba Askofu.
"hahahaa Umeona baba Askofu yaani hapo ninavyomjua Asunta mwanangu ndio ushampeleka kwenye mawazo ya huko chuo hahaha"
alifurahi Pastor George huku akimuangalia Asunta na walipokutana macho kwa macho jicho la Pastor George lilionesha alama ya hasira tofauti na sauti na uso wake na hii aliigundua Asunta na kuamini kuwa ile ni palni tu ya babaake.
"Vizuri sana mwanangu Asunta"
"Asante baba Askofu"
alijibu na kuonesha tabasamu bandia Asunta lililomuaminisha baba Askofu japo kwa upande wa moyo wa Pastor George na mkewe walijua wazi kuwa mtoto wao hajapendezewa hata kidogo na safari ile lakini hawakuwa na jinsi ilibidi tu wamsafirishe ili izidi kuwa heri na salama baina yake na kijana huyo wa kiisilaamu.
* * * *
ITAENDELEA