HADITHI: Mtoto wa Pastor

HADITHI: Mtoto wa Pastor

SEHEMU YA 5

Upande wa pili alionekana Asunta akijitahidi kuendeesha gari kwa speed sana ili aweze kuwahi ubungo na kugeuka kurudi nyumbani kwani alishahisi kuwa anatafutwa kwenye simu kwa kuwa alikuwa nyuma ya muda kwa zaidi ya masaa mawili na kwa kuwa haikuwa kawaida yake na alivyowaelewa wazazi wake walivyo juu yake alihisi tu lazima watakuwa wamepata wasiwasi tayari.

Alilifikia geti la kuingilia mule ndani na alipokuwa anapaki gari yake alishangaa kuiona gari aliyopenda kutembelea babaake ikiwa eneo lile na zaidi kilichomuaminisha ni baada ya kumuona dereva wa babaake akiwa kasimama nje ya ile gari na hata nae alipoiona gari ya Asunta alitabasam na kumuashilia kuwa akipaki aende.

"Mh! mbona leo kivumbi, sijui kaja na baba!"
Alijisemea moyoni Asunta na mapigo kuanza kumuenda kasi na aliposhuka kwenye gari kumfata yule dereva na baada ya kusalimiana kabla hajauliza chochote moyo ulimripuka mara baada ya kusikia sauti ya babaake sambamba na mwalimu wake wakijia pale walipo.

"Si huyu hapa Asunta!!? aaah mwanangu nini kimekupata tena"
Aliongea kwa taharuki Pastor George na kumsogelea Asunta ambae alikosa cha kujibu harakaharaka kwani aliogopa sana kumdanganya babaake lakini pia alijua si vyema wala si busara kumwambia mzazi wake kuwa alikuwa na mwanaume huko atokapo ambae wanapendana.

Hali ile ilimfanya Asunta abaki amejiinamia kichwa huku akivunjavunja vidole na ndipo Pastor George alipofika jirani yake tu alimuekea mwanae mikono kichwani na kuanza kumuombea palepale.

"......Baba naomba katika jina la Yesu vunja na teketeza nguvu zote na mapepo mabaya yanayoanza kumnyemerea bint yangu... Jehova nakutumaini wewe baba ingia na uusafishe moyo wa bint angu Asunta umuondolee hofu ya kumficha shetani na kuogopa kusema ukweli ... Naamuru sasa katika Jina la Yesu Kristo alie haaaii.... Nateketeza na kuchoma nguvu zote za giza na ushawishi wa shetani ... ktk jina la Yesu nasema Asante baba maana najua kazi yako unaenda kuifanya sasa.. aashgamaloga bbautih a ngghikjhhgaamaa... Aaamen.."

Aliomba hadi Asunta nae alijikuta anafumba macho na baada ya maombi yale alimuamuru aingie kwenye gari wageuze kurudi nyumbani kwani hayo mengine watayazungumza watapofika nyumbani.

Aliendeesha gari Asunta huku akijua fika sasa kimenuka na babaake aliheshimu tu mazingira ya pale ndio maana hakumsema sana lakini vilevile moyo wake ulifurahi kuwa ktk mahusiano na Dullah japo alijua hawezi kumwambia yeyote kwa muda ule mpaka hapo baadae taratibu zitapofatwa.

Walifika nyumbani na kweli kama alivyowazia Asunta baabaake alikuwa bado kakasilika mno.

"Haya mama twambie ulikuwa wapi"

Aliuliza pastor George baada ya kueka kikao cha dharula na kumwita mkewe sambamba wamuhoji na kumsikiliza biti yao Asunta wapi alipokuwa na kwanini amechelewa.
Asunta alibaki tumbo joto akifikiri aanzie wapi amalizie wapi ili awalidhishe wazazi na ndipo kwa haraka ilimjia mbinu kichwani na kuamua kuitumia.

"Naomba mnisamehe sana wazazi wangu lakini nilipokuwa njiani asubuhi naelekea mazoezini Vero alinipigia na kunambia anaumwa hivyo nilijikuta napitiliza mpaka kwao kwanza kumuona na kwa bahati mbaya simu ilizima chaji na nikasahau kuichaji ndio maana sikuwataarifu mapema"

Alijitetea Asunta kwa kutunga uongo wa pale pale lakini Pastor George alikuwa na mbinu sana za kumsoma mwanae pindi aongeapo kweli.

"Ahaa kwa hiyo ulipitia kwa Vero, vipi ulimkuta?"
"Ee nilimkuta baba"
"anaendeleaje?"
"hali yake si nzuri sana ila hajambo."

"oke sawa, mama Asunta chukua simu ya Asunta ichomeke chaji tumpigie Vero sasa hivi"
Kauli ile ya kuwa apigiwe Vero ilisababisha moyo wa Asunta kulipuka na kuanza kuhofia zaidi jinsi Vero atavyomponza kwani walikuwa na siku kadhaa hawakuonana pia hakumpigia simu kumpanga kwa jambo lile alilolitunga.

"Asunta mwanangu, ninavyokutazama tu roho mtakatifu ananionesha kuwa unachokisema sio cha kweli.. hebu kuwa muwazi kwani huoni kama ni aibu na dhambi kubwa kusema uongo tena mbele ya wazazi wako?"

Aliongea tena Pastor George maneno yaliyomchoma kidogo Asunta na kujikuta anapata kigugumizi kwani alihofia mno kusema ukweli mapema ile pia alihofia kuendelea kung'ang'aniza uongo wake kwani aliamini endapo atapigiwa kweli Vero basi ataumbuka.

Alifikilia mno na kubaki kainama bila kusema chochote hali iliyozidi kumuimanisha Pator George kile akisemacho na moyoni alijikuta anahuzunika kidogo Pastor na kubaki wanatazamana na mkewe wakisemezana kwa macho wamfanyeje mtoto wao kipenzi kwani walimpenda mno na hawakuwa tayari apotee mapema ile na walishamuekea mikakati mizuri sana ya baadae ili asije kuwa tegemezi.

Akiwa bado katulia Asunta safari hii mamaake alimsihi na kumuomba aseme ukweli tu wala asiogope kwani wao ni wazazi wake hivyo asiwaogope wala asiwafiche kitu.

Ndipo alipoinua uso wake Asunta na kumuangalia mamaake kipenzi aliyemzoea kama rafiki pia kwa vile walivyoishi na kupewa uhuru wa mawazo na kujadili mambo muda mwingi ya kimaisha pamoja.

Safari hii Asunta alipiga moyo konde na kutaka kuongea kitu lakini kabla hajafanya hivyo mara simu yake iliyokuwa imechomekwa kwenye chaji na ilishawashwa muda kwa dhumuni la kumpigia Vero ghafra iliita na ndipo mamaake alipoitazama kwenye kusoma jina la aliyekuwa anapiga na kumuangalia mwanae kwa mshangao kisha akamkabidhi simu yake.

"Nani huyo anaempigia?"
Aliuliza Pastor George akiitilia mashaka simu ile kuhusiana na safari ya mwanae.
na mara baada ya Asunta kuiangalia jina lililotokea kwenye Screen liliseviwa My D.

Moyo ulimripuka sana Asunta hasa pale babaake alipomfokea pindi alipositasita kuipokea ile simu.

"Pokea basi uzungumze na huyo mtu, tena uweke Loud speeker..!"

Alifoka Pastor George na kunyanyuka hali iliyomtisha zaidi Asunta na kujua sasa akizembea atapigwa vibao kwani alimuelewa vizuri pia babaake japo hakuwahi kumpiga mara kwa mara lakini sifa zake za ugomvi hapo zamani na kutopenda ujinga alishahadithiwa na mamaake na kumtahadhalisha kuwa licha ya babaake kuwa mtumishi mzuri wa mungu lakini hasira zinapomzidi sana huwa anabadilika mno.

Kwa hofu kubwa Asunta alikielekeza kidole gumba sehemu ya batani ya kijani ya simu yake na kuipokea.

"Hallow baby, samahani ushafika nyumbani? naomba nikwambie kitu Asunta mamy... ukweli tangia tumeachana mida ile mpaka sasa nahisi ubongo wangu umeganda na kushindwa kuingiza vitu vipya nikitafakari hivi hiki kilichotokea ni ndotooo au ni picha halisi?!! Haloo.. Halooooooo .. Asunta halooo!!!?"

Naam ilikuwa ni sauti ya maneno ya Dullah kutokea simuni pindi ilipoekwa loud speeker baada ya kupokelewa na yalisikiwa vizuri na kila mmoja si Asunta, mamaake wala Pastor George huku Asunta akiwa kaganda bila ya kujibu chochote hadi Dullah alipoamua kukata simu baada ya kuona upande wapili kimya kimeshamiri.

Alisimama Pastor George na kuanza kufoka huku Asunta akibaki amejiinamia analia kwa kwikwi pale chini na kuomba msamaha kwa wazazi wake kwani tayari siri yote ilishabumbuluka na hakuwa na jipya tena.

"Umeonaa!!? umesikia mama Asunta ujinga wa mwanao.!!! na haya ndio mazoezi mapya aliyoanza siku hizi, mazoezi ya kuidhalilisha na kuitia nuksi nyumba yangu takatifu.

Asunta mwanangu kwanini unataka kututia aibu hivi? Eee Yesu baba muokoe huyu mwana kondoo wako hapa chini na unipe moyo wa uvumilivu nisije kumvunja heee!! Mwanangu Asunta!? mafundisho yoooootee kanisani imekuwa bure? sasa hivi ushakuwa baby wa mtu..!? nilichotaka usome mwanangu au kama hutaki kusoma fine naomba unijibu ukweli wote kabla sijaondoka kuhusu huyo aliyepiga simu.

Maana aibu sitaki kuikaribisha ndani ya nyumba yangu, unataka mume?? sema ifatwe sheria twende ngazi kwa ngazi sio hivyo unavyoenda wewee mwananguuu Aaaaagh"
Aliwaka sana Pastor George hadi mate yalikuwa yanamtoka mdomoni kutokana na hasira na kupanua mno mdomo kipindi anafoka.

"Naomba mnisamehe sana wazazi wangu ila sikupanga kuwaficha kabisa nilikuwa nasubiri muda rasmi ufike niwaambie habari hizi"

"Utuambie wewe ndie mshenga?.. hebu acha ujinga wako kama unataka kuolewa na umepata mtu uliyempenda mama sawaaa ila kwa masharti na vigezo vya roho mtakatifu mwenye kuleta amani na utulivu ndani ya nyumba, kwanza huyo mtu wako uliyepanga kutwambia habari zake si ndio huyo aliyepiga simu?

"Ndio."
"Anaitwa nani..?"
"Dullah baba"

"Dullah Dullah Dullaaaah!! okeeeei yaani Abdallah!!?!!.. Eee bwana Yesu ulie mbinguni, mbona shetani anamuandama kiasi hiki binti angu?!!

sasa sikiliza Asunta mimi naondoka ila kuanzia muda huu sahau kabisa juu ya huyo Shetani asije kukupoteza. na Sitotaka tena kumsikia mtu kama huyo ndani ya nyumba yangu takatifu. Nadhani umenisikia mama Asunta..

Amani ya bwana iwe nawe'
Aliongea kwa hasira Pastor George baada ya kulitafakali jina la Dullah na kugundua kirefu chake kisha akatoka na kuingia chumbani kulipokuwa begi lake na kutoka nje ambapo tayari msafara wa magari mawili kutoka kanisani kwao ulikuwa unamsubiri kwaajili ya kumpeleka uwanja wa ndege kwa safari yake jijini Nairobi.

Kwa upande wa Asunta hakuelewa kwanini babaake ameongea maneno yale na kwa hasira vile na baada ya kutoka na kuondoka Asunta alirudi ndani na kujifungia chumbani kwake na kuanza kulia kwa uchungu hadi mlango wa chumba chake ulipofunguliwa na hakuwa mwengine aliyeingia bali ni mamaake kipenzi ambae alikuwa mpole sana na mwenye busara pia.


ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 6





"Mwanangu Asunta usilie mama... usijali babaako kaongelea hasira tu."
"Hasira gani mama, babaa alichosema ndicho anachomaanisha.."
"hamna mwanangu mimi namfahamu sana babaako.. usilie basi, kwani huyo kijana ni yupi na anaishi wapi?"
"Ukimuona nadhani utamkumbuka mama"
"hee! nitamkumbuka?! kwani nilishawahi kumuona wapi?"
Aliuliza kwa mshangao mama Asunta
"ukimuona utakumbuka tu mama"
"okeee au Rymond yule mliosoma wote?"
"hapana mama ila naomba nikuulize swali kwanini baba amekuwa mkali zaidi baada ya kumtajia jina la Dullah?"
"Mmmmh!! sina hakika ila nahisi ni kwa sababu Abdallah ni jina la kiislam na kwa imani yetu tena kutoka kwenye familia iliyobarikiwa kama hii haitawezekana binti etu kumpoteza mahala tofauti na sisi....kwani hukuwahi kumuuliza dini gani huyo kijana"
"sijawahi mama ila nampenda sana sidhani kama dini inaweza kuwa tatizo kivilee."
"Mmh!! basi nakushauri kwanza umuulize mapemaa tujue kwani ninavyomjua babaako hata mimi mwenyewe pia napenda uolewe mwanangu lakini si na muislam, ongea nae huyo jamaa yako umuulize na ikiwa ni kweli muislam na anakupenda mshauri abadili dini aungane nasi kanisani apewe baraka na mafundisho kwa muda ndipo taratibu nyengine zifate."
"Mmh! mama.. kama akikataa je nami nampenda?"
"akikataa itakuwa sio riziki yako na bwana atakuletea mume mwengine bora kwasababu hata uking'ang'ania vipi hakuna atakayekuruhusu uolewe na muislam tena ukizingatia babaako ni mtumishi mkubwa wa mungu.."
Aliongea mama yule na kunyanyuka mara baada ya kuona sasa mwanae kaacha kulia na kuanza kurejea katika hali ya kawaida. alifungua mlango na kumuacha ajipumzishe kwanza lakini kichwani mwake Asunta alibaki bado na maswali mengi na kutokana na shauku na msukumo wa damu kuongeza kasi kidogo pindi alipokuwa anazidi kufikiria ndipo aliposhusha pumzi kwa nguvu na kuchukua simu yake alibinya haraka haraka sehemu ya simu zilizoingia na kubinya namba ya Dullah huku mapigo ya moyo yakizidi kumuenda mbio simu ilipokuwa inaita upande wa pili huku zaidi alifikiria ni vipi Dullah angejibu pindi atapomuuliza swali lile aliloambiwa na mamaake la udini na kama kweli akiwa muislam atakubali kubadili dini? na kwa jinsi alivyompenda hakuwa tayari kabisa Asunta moyoni mwake kukubali kumkosa Rasta yule.

"Hallooo.. halooow"
Ilisikika sauti ya Dullah upande wa pili punde tu ilipopokelewa ile simu huku Asunta akiwa na mawazo lundo alijikuta anababaika hata jinsi ya kuanza kuongea.
"Hallow baby Asunta vipi mamy kwema?'"
"Kwema D, samahani naomba nikuulize kitu."
"Kitu gani tena baby cha kukufanya hadi utangulize samahani kabla ya kuniuliza eeh, kuwa huru mi ni mfano wa samaki uliyemkuta anatapatapa baada ya mto kukaukiwa maji nawe ukamuokota na kumtia kwenye beseni lako la maji, kuwa huru mamy niulize mpaka uchoke usiseme samahani."
Maneno ya Dullah yalimfanya Asunta atabasamu mwenyewe na kuendelea.
"Eti D, wewe ni dini gani."
"Aaagh!! kumbe kaswali kenyewe ndio hako? ushasikia Dullah.. Yaani Abdallah mjukuu wa sheikh Kombo. mimi ni Muislamu pure kabisa mamy, vipi kwani mbona umeniuliza hivyo.!!"
"Mh!! ngoja nakuja huko sasahivi tuongee vizuri."
Alishusha pumzi Asunta na kukata simu huku mapigo yake ya moyo yalibadilika ghafra baada ya kusikia kuwa Dullah alikuwa muislam.

'Vipi Asunta mbona hivyo!"
"Hapana mama wacha tu niende nikaongee nae huko huko kuliko kumuuliza kwenye simu"
"Hee!! we una wazimu? yaani sasa hivi hapa umetoka kusemwa harafu unataka kwenda huko huko, babaako akipiga kukuulizia je?"
"Aaaagh, mamaa we mwambine nimelala tu"
"Umelala? kwa hiyo unanifundisha kudanganya ktk mambo ya kipuuzi si ndio.. na babaako unamjua mtu wa magutu endapo akirudi ghafra. haya nakuomba rudi ndani hamna kutoka kwenda popote"
Aliongea mama Asunta kwa ukali kidogo na kumnyong'onyesha kabsa Asunta ambae awali alijua mamaake ngemruhusu tu kutokana na jinsi alivyomzoea lakini alishangaa kuona anaekewa msimamo na vizuizi vya kutoka.

Alikaa kwenye sofa na kuanza kulia taratibu kwa kwikwi kwa takribani dakika ishirini ambapo hata mamaake sasa alianza kumuonea huruma na kuamua kumruhusu ila kwa sharti tu asichelewe kurudi na awe makini.
"Vpi utatumia gari yangu au utaenda nayo ileile yako"
Aliuliza mama Asunta ktk hali ya kum bembeleza na kumfariji mwanae.
"hapana mama sitatumia gari yoyote zaidi naomba dereva anisindikize tu hapo mbele nitachukua taxi"
"He! Asunta mwanangu mbona unapenda usumbufu, kwanini umeamua hivyo"
"Agh, basi tu mama, nahofia nisije kuonekana na watu wa baba au pengine hata mwenyewe atakuwa bado hajavuka nje ya jiji kwa hiyo atapoiona gari itakuwa nongwa"
"hapo sasa nimekuelewa mwanangu haya ila naomba usichelewe mama, hebu nisubiri kwanza"
Aliongea mama Asunta na kupandisha juu ambapo aliporudi alimpa mwanae kiasi cha pesa takribani laki mbili na nusu.
"Haya hii utaongezea kwenye nauli yako mamaa eeh"
"haya Asante mamy baadae"
Waliagana na kutoka nje ambapo alimuamuru dreva na kumsogeza mpaka maeneo ya stendi za daladala kulipokuwa na parking ya taxi na kujitoma ndani ya Taxi ambapo gharama yake ilikuwa elfu ishirini tu mpaka tandare kwa tumbo.
Kichwani akiwa na wazo moja na shauku ya kutaka kujua Dullah atakubaliana na msimamo wa wazazi wake kwa kubadili dini.?

* * * * *

Huku akiwa anapiga mluzi Dullah aliendelea kupiga deki chumbani kwake na kufanya usafi wa hapa na pale na kupanga vitu vizuri kwaajili ya kueka mandhali nzuri kujiandaa na ugeni alioutarajia kuupokea muda si mrefu.

Baada ya kuridhishwa na usafi alioufanya Dullah alitoka nje na kuelekea dukani ambapo alinunua chupa ya air fresh na kurejea na kupulizia kila kona ya kuta ya chumba chake na kuleta manukato mazuri mule ndani na kumfanya aachie tabasamu zito na kujituliza kitandani kusubiria simu ya huyo mgeni wake.

Baada ya Muda akiwa amekaa kitandani mala alianza kusikia matone ya mvua yakichombweza bati taratibu na punde simu yake iliita alipoangalia hakuwa mwengine bali Asunta.
"Hee, nambie baby"
"Poa D, njoo unichukue nipo stend hapa tulipoachana asubuhi"
"Dakika sifuri baby nitakuwa hapo"
Aliongea D na kukurupuka kitandani kutoka nje ambapo hali ya hewa ilikuwa ime change huku wingu zito likiwa limetanda angani na manyunyu yaliendelea kudondoka.
Alifika stend na kumkuta mgeni wake akiwa anamsubiria kwa shauku walisalimiana kwa kupeana mikono na taratibu wakaanza kuelekea mahala alipoishi Dullah, wakiwa wameanza kukata vichochoro tu mara manyunyu yaliongeza kasi na ndipo mvua kubwa sasa ilianza kunyesha na kusababisha kuwaloanisha wote wawili na hawakuwa na mwamvuli wowote.
Asunta hakujua kabisa kukazana kwa kuhofia kuteleza hali iliyomfanya na D kwenda mwendo uleule sambamba na mpaka walipofika na kuingia ndani wote walikuwa wamelowana chapachapa vitu pekee vilivyosalimika ni simu na pesa ambavyo viliekwa kwenye mkoba wa Asunta ambao ulikuwa hauingizi maji kwa jinsi ulivyotengenezwa.

Alibaki amesimama Asunta pindi tu alipoingia ndani na kushindwa kusogea sehemu yoyote huku midomo ikimcheza na meno kugongana gongana kwa ule mtetemo wa baridi lililosababishwa na kuloana kwake.
Suruali ile nyepesi ya kitambaa aliyovaa iling'ang'ana kwenye ngozi na kunata sambamba na nyama raini za mapaja kutokana na kulowana hali iliyomcholesha kila kitu na kuanza kumpa wakati mgumu Dullah hasa alipomuangalia sehemu za kifuani mara baada ya chuchu zake miba kijichora na kuonekana vizuri zikiwa ndani ya kiblauz cheupe kilichonakshiwa mapambo frani furan ya kumeremeta.
Na kwa kuwa D nae alikuwa ameloa chapa chapa alishindwa kusogea kitandani wala kumkaribisha mgeni wake akae zaidi aliamua kuchukua taulo na kumkadhi Asunta kwani hakuwa na nguo nyengine yoyote pana zaidi ya shuka na kwa upande wake hakuona soni alichojoa t shet na suruali yake na kubaki na bukta kisha kuchukua baadhi ya nguo chafu na kujikaushia hizo mwilini mwake huku akimtazama Asunta aliebaki ameganda kwa aibu na kushindwa aanzie wapi licha ya kwamba alikuwa na D ambae ni mpenzi wake mpya lakini swala la kusaula mbele yake muda mfupi vile halikumjengea picha nzuri kichwani mwake Asunta.

"Samahani D naomba suruali yako yoyote na furana then nielekeze bafuni."
"haha Asunta baby hata nisikufiche kwanza bafu lipo nje zaidi ya hatua ishilini pili halijaezekwa hivyo hata ukitoka utakuwa hakuna ulichofanya utarudi umelowa tena chapa chapa"
Aliongea D na kumfanya Asunta azidi kosa jipya na alipomuangalia Dullah akiwa tumbo wazi aliweza mshuhudia kwa mara ya kwanza jinsi kifua chake kilivyojichora vizuri kwa mazoezi pamoja na tumbo lake lililoeka michilizi ya kukatika kimazoezi.
"Fumba macho basi D.."
Aliongea kwa sauti raini Asunta kwa aibu kwani hakuwa na jinsi tena ilibidi ageukie pembeni kwa ukutani na kuanza kuchojoa blauz yake huku akiwa kajiziba na taulo ili kuyaficha mautamu yake akiwa kampa mgongo D kisha taratibu alianza kuchojoa suruali yake lakini kutokana na vile umbile lake lilivyo na kwa jinsi alivyolifunga taulo kuzuia sehemu zake za juu kwenye maziwa ililifanya taulo kuzidi kuwa fupi hasa wakati alipoinama kumalizia kuvua suruali na kumuachia video ya bure D aliesimama nyuma yake akimuangalia na kumfanya Njomba Nchumali kuanza kuweweseka na kutingisha bukta ya D hasa alipoyaona mapaja mazuri ya Asunta na ktk hali ya kuhangaika na kujificha ficha hasa nae Asunta alipohisi maumbile yake nyuma yanaonekana na kulifungua taulo kwa juu ili alishushe tena chini kidogo pindi alipokuwa anamalizia kuvua mguu wa pili wa suruali yake ghafra kwa bahati mbaya taulo lote lilidondoka na kuacha mambo yote hadhalani na alipogeuka kuliokota hakuamini alipomuona D akiwa ameshikilia paipu yake iliyokuwa imetuna ipasavyo ndani ya bukta.

"Aaaah! jamani D nini tenaa?"
Aliuliza Asunta pindi alipoona D wazimu wa muda mrefu wa kitanga ulipoanza kumzonga kichwani na kupiga hatua pale alipo Asunta huku macho yake yakiwa yamebadilika na kuwa mekundu mithili ya mtu aliyekula ganja (bangi) kete ishirini pekeake.
"Asunta"
Aliita Dullah kwa sauti ambayo Asunta hakuwahi kuisikia, sauti iliyomaanisha kuhitaji kitu na wakati huo alikuwa kasimama jirani kabisa na Asunta aliyeegemea ukuta akimshangaa D kubadilika hisia ghafra vile na kabla Asunta hajafanya chochote Dullah alimkamata kwa kumshika sehemu ya mashavu na kuuinua uso wa Asunta aliyekuwa kauinamisha akiona aibu hata kuutazama uso wa Dullah na wakati huo mvua bado ilikuwa inapiga bati kwa wingi sana.
"Asunta naomba unitazame usiogope baby, amini mimi na wewe tumeunganishwa na mungu mwenyewe na hali hii iliyotokea haimaanishi mimi nina tamaa tu nawewe la hasha bali nakupenda sana tena inawezekana nikawa nakupenda zaidi yako na si kwa sababu una pesa ila ni sababu una moyo mzuri. Naomba ukunjue moyo wako tunapokuwa pamoja na ujisikie amani zaidi juu yangu.. Mvua hii naamini imekuwa baraka na alama aliyotutunuku mungu ktk mapenzi yetu naomba tuitumie baraka hii vizuri na ibaki kuwa shahidi wetu kama itatokea mmoja wetu kumsariti mwenzake hapo baadae.."
Aliongea Dullah huku akitumia ufundi wake wa kitanga na kumpelekea mdomo Asunta na kuunganisha mdomo wake na kwa ufundi aliokuwa nao D kipindi mikono ya Asunta ilikuwa ikilazimisha kuishusha mikono yake iliyokuwa mashavuni mwake huku vidole vya mwisho vya Dulla vikiwa vimeziba kwenye tundu za masikio ya Asunta na vidole gumba vikabinya taya ya Asunta na hapo ndipo Asunta mwenyewe alijikuta anaachia lipsi alizozibana na kumrahisishia Dullah kuupenyeza ulimi wake mdomoni mwake na kubadilishana mate taratiibu na ndipo alipoitoa mikono na kuikamata mikono ya Asunta viganja kwa viganja.
Asikwambie mtu Dullah hakuwa fundi uwanja wa nje tu wenye mashabiki, bali alikuwa fundi pia hadi kwenye uwanja mdogo wa ndani usiokuwa na shabiki yeyote kwani kwa jinsi alivyoanza kumpiga chenga ndogo ndogo Asunta hadi akabadilisha hisia zote alizokuja nazo awali na kumpandisha nae mapepo yake ya muda mrefu.
"aaaaasssss jamani D baaa..oooosss..baasiii...aaaah"
Aligugumia Asunta wakati huo D alibadilika na kumfanya asunta kama kitoto cha paka kilichozaliwa muda mfupi kwa jinsi alivyokuwa anamrambaramba mwili mzima na alipofika maeneo ya ikulu alianza kumfanyia vituko ambavyo Asunta hakuwa hata kuota kama vipo na hadi kufikia Asunta anatolewa kufuri lake na kupandishwa machinjioni pasi na kujitambua hadi alipohisi Njomba Nchumari wa Dullah anasongomeka bichwa lake kwenye kitundu kilichohifadhi asali yake isiyokwisha.
Vitu vya Dullah kwenye mambo yale ni ngumu sana kuvisimulia labda ukutane na Asunta umuombe akudokeze walau kiduchu! lakini kwa ufupi Dullah alikuwa fundi wa kale kamchezo na kumpagawisha Asunta kutoa vilio mfululizo ndani silio vilivyobeba hisia nzito, vilio vya usiniache,nakupenda,sikuachi,siamini na kadhalika hadi Dullah anapata gori la kwanza tayari Asunta alishajifunga mengine matatu na hadi mechi inamalizika matokeo yalikuwa Asunta Nne Dullah Mbili.

* * * * * *

ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 6





"Mwanangu Asunta usilie mama... usijali babaako kaongelea hasira tu."
"Hasira gani mama, babaa alichosema ndicho anachomaanisha.."
"hamna mwanangu mimi namfahamu sana babaako.. usilie basi, kwani huyo kijana ni yupi na anaishi wapi?"
"Ukimuona nadhani utamkumbuka mama"
"hee! nitamkumbuka?! kwani nilishawahi kumuona wapi?"
Aliuliza kwa mshangao mama Asunta
"ukimuona utakumbuka tu mama"
"okeee au Rymond yule mliosoma wote?"
"hapana mama ila naomba nikuulize swali kwanini baba amekuwa mkali zaidi baada ya kumtajia jina la Dullah?"
"Mmmmh!! sina hakika ila nahisi ni kwa sababu Abdallah ni jina la kiislam na kwa imani yetu tena kutoka kwenye familia iliyobarikiwa kama hii haitawezekana binti etu kumpoteza mahala tofauti na sisi....kwani hukuwahi kumuuliza dini gani huyo kijana"
"sijawahi mama ila nampenda sana sidhani kama dini inaweza kuwa tatizo kivilee."
"Mmh!! basi nakushauri kwanza umuulize mapemaa tujue kwani ninavyomjua babaako hata mimi mwenyewe pia napenda uolewe mwanangu lakini si na muislam, ongea nae huyo jamaa yako umuulize na ikiwa ni kweli muislam na anakupenda mshauri abadili dini aungane nasi kanisani apewe baraka na mafundisho kwa muda ndipo taratibu nyengine zifate."
"Mmh! mama.. kama akikataa je nami nampenda?"
"akikataa itakuwa sio riziki yako na bwana atakuletea mume mwengine bora kwasababu hata uking'ang'ania vipi hakuna atakayekuruhusu uolewe na muislam tena ukizingatia babaako ni mtumishi mkubwa wa mungu.."
Aliongea mama yule na kunyanyuka mara baada ya kuona sasa mwanae kaacha kulia na kuanza kurejea katika hali ya kawaida. alifungua mlango na kumuacha ajipumzishe kwanza lakini kichwani mwake Asunta alibaki bado na maswali mengi na kutokana na shauku na msukumo wa damu kuongeza kasi kidogo pindi alipokuwa anazidi kufikiria ndipo aliposhusha pumzi kwa nguvu na kuchukua simu yake alibinya haraka haraka sehemu ya simu zilizoingia na kubinya namba ya Dullah huku mapigo ya moyo yakizidi kumuenda mbio simu ilipokuwa inaita upande wa pili huku zaidi alifikiria ni vipi Dullah angejibu pindi atapomuuliza swali lile aliloambiwa na mamaake la udini na kama kweli akiwa muislam atakubali kubadili dini? na kwa jinsi alivyompenda hakuwa tayari kabisa Asunta moyoni mwake kukubali kumkosa Rasta yule.

"Hallooo.. halooow"
Ilisikika sauti ya Dullah upande wa pili punde tu ilipopokelewa ile simu huku Asunta akiwa na mawazo lundo alijikuta anababaika hata jinsi ya kuanza kuongea.
"Hallow baby Asunta vipi mamy kwema?'"
"Kwema D, samahani naomba nikuulize kitu."
"Kitu gani tena baby cha kukufanya hadi utangulize samahani kabla ya kuniuliza eeh, kuwa huru mi ni mfano wa samaki uliyemkuta anatapatapa baada ya mto kukaukiwa maji nawe ukamuokota na kumtia kwenye beseni lako la maji, kuwa huru mamy niulize mpaka uchoke usiseme samahani."
Maneno ya Dullah yalimfanya Asunta atabasamu mwenyewe na kuendelea.
"Eti D, wewe ni dini gani."
"Aaagh!! kumbe kaswali kenyewe ndio hako? ushasikia Dullah.. Yaani Abdallah mjukuu wa sheikh Kombo. mimi ni Muislamu pure kabisa mamy, vipi kwani mbona umeniuliza hivyo.!!"
"Mh!! ngoja nakuja huko sasahivi tuongee vizuri."
Alishusha pumzi Asunta na kukata simu huku mapigo yake ya moyo yalibadilika ghafra baada ya kusikia kuwa Dullah alikuwa muislam.

'Vipi Asunta mbona hivyo!"
"Hapana mama wacha tu niende nikaongee nae huko huko kuliko kumuuliza kwenye simu"
"Hee!! we una wazimu? yaani sasa hivi hapa umetoka kusemwa harafu unataka kwenda huko huko, babaako akipiga kukuulizia je?"
"Aaaagh, mamaa we mwambine nimelala tu"
"Umelala? kwa hiyo unanifundisha kudanganya ktk mambo ya kipuuzi si ndio.. na babaako unamjua mtu wa magutu endapo akirudi ghafra. haya nakuomba rudi ndani hamna kutoka kwenda popote"
Aliongea mama Asunta kwa ukali kidogo na kumnyong'onyesha kabsa Asunta ambae awali alijua mamaake ngemruhusu tu kutokana na jinsi alivyomzoea lakini alishangaa kuona anaekewa msimamo na vizuizi vya kutoka.

Alikaa kwenye sofa na kuanza kulia taratibu kwa kwikwi kwa takribani dakika ishirini ambapo hata mamaake sasa alianza kumuonea huruma na kuamua kumruhusu ila kwa sharti tu asichelewe kurudi na awe makini.
"Vpi utatumia gari yangu au utaenda nayo ileile yako"
Aliuliza mama Asunta ktk hali ya kum bembeleza na kumfariji mwanae.
"hapana mama sitatumia gari yoyote zaidi naomba dereva anisindikize tu hapo mbele nitachukua taxi"
"He! Asunta mwanangu mbona unapenda usumbufu, kwanini umeamua hivyo"
"Agh, basi tu mama, nahofia nisije kuonekana na watu wa baba au pengine hata mwenyewe atakuwa bado hajavuka nje ya jiji kwa hiyo atapoiona gari itakuwa nongwa"
"hapo sasa nimekuelewa mwanangu haya ila naomba usichelewe mama, hebu nisubiri kwanza"
Aliongea mama Asunta na kupandisha juu ambapo aliporudi alimpa mwanae kiasi cha pesa takribani laki mbili na nusu.
"Haya hii utaongezea kwenye nauli yako mamaa eeh"
"haya Asante mamy baadae"
Waliagana na kutoka nje ambapo alimuamuru dreva na kumsogeza mpaka maeneo ya stendi za daladala kulipokuwa na parking ya taxi na kujitoma ndani ya Taxi ambapo gharama yake ilikuwa elfu ishirini tu mpaka tandare kwa tumbo.
Kichwani akiwa na wazo moja na shauku ya kutaka kujua Dullah atakubaliana na msimamo wa wazazi wake kwa kubadili dini.?

* * * * *

Huku akiwa anapiga mluzi Dullah aliendelea kupiga deki chumbani kwake na kufanya usafi wa hapa na pale na kupanga vitu vizuri kwaajili ya kueka mandhali nzuri kujiandaa na ugeni alioutarajia kuupokea muda si mrefu.

Baada ya kuridhishwa na usafi alioufanya Dullah alitoka nje na kuelekea dukani ambapo alinunua chupa ya air fresh na kurejea na kupulizia kila kona ya kuta ya chumba chake na kuleta manukato mazuri mule ndani na kumfanya aachie tabasamu zito na kujituliza kitandani kusubiria simu ya huyo mgeni wake.

Baada ya Muda akiwa amekaa kitandani mala alianza kusikia matone ya mvua yakichombweza bati taratibu na punde simu yake iliita alipoangalia hakuwa mwengine bali Asunta.
"Hee, nambie baby"
"Poa D, njoo unichukue nipo stend hapa tulipoachana asubuhi"
"Dakika sifuri baby nitakuwa hapo"
Aliongea D na kukurupuka kitandani kutoka nje ambapo hali ya hewa ilikuwa ime change huku wingu zito likiwa limetanda angani na manyunyu yaliendelea kudondoka.
Alifika stend na kumkuta mgeni wake akiwa anamsubiria kwa shauku walisalimiana kwa kupeana mikono na taratibu wakaanza kuelekea mahala alipoishi Dullah, wakiwa wameanza kukata vichochoro tu mara manyunyu yaliongeza kasi na ndipo mvua kubwa sasa ilianza kunyesha na kusababisha kuwaloanisha wote wawili na hawakuwa na mwamvuli wowote.
Asunta hakujua kabisa kukazana kwa kuhofia kuteleza hali iliyomfanya na D kwenda mwendo uleule sambamba na mpaka walipofika na kuingia ndani wote walikuwa wamelowana chapachapa vitu pekee vilivyosalimika ni simu na pesa ambavyo viliekwa kwenye mkoba wa Asunta ambao ulikuwa hauingizi maji kwa jinsi ulivyotengenezwa.

Alibaki amesimama Asunta pindi tu alipoingia ndani na kushindwa kusogea sehemu yoyote huku midomo ikimcheza na meno kugongana gongana kwa ule mtetemo wa baridi lililosababishwa na kuloana kwake.
Suruali ile nyepesi ya kitambaa aliyovaa iling'ang'ana kwenye ngozi na kunata sambamba na nyama raini za mapaja kutokana na kulowana hali iliyomcholesha kila kitu na kuanza kumpa wakati mgumu Dullah hasa alipomuangalia sehemu za kifuani mara baada ya chuchu zake miba kijichora na kuonekana vizuri zikiwa ndani ya kiblauz cheupe kilichonakshiwa mapambo frani furan ya kumeremeta.
Na kwa kuwa D nae alikuwa ameloa chapa chapa alishindwa kusogea kitandani wala kumkaribisha mgeni wake akae zaidi aliamua kuchukua taulo na kumkadhi Asunta kwani hakuwa na nguo nyengine yoyote pana zaidi ya shuka na kwa upande wake hakuona soni alichojoa t shet na suruali yake na kubaki na bukta kisha kuchukua baadhi ya nguo chafu na kujikaushia hizo mwilini mwake huku akimtazama Asunta aliebaki ameganda kwa aibu na kushindwa aanzie wapi licha ya kwamba alikuwa na D ambae ni mpenzi wake mpya lakini swala la kusaula mbele yake muda mfupi vile halikumjengea picha nzuri kichwani mwake Asunta.

"Samahani D naomba suruali yako yoyote na furana then nielekeze bafuni."
"haha Asunta baby hata nisikufiche kwanza bafu lipo nje zaidi ya hatua ishilini pili halijaezekwa hivyo hata ukitoka utakuwa hakuna ulichofanya utarudi umelowa tena chapa chapa"
Aliongea D na kumfanya Asunta azidi kosa jipya na alipomuangalia Dullah akiwa tumbo wazi aliweza mshuhudia kwa mara ya kwanza jinsi kifua chake kilivyojichora vizuri kwa mazoezi pamoja na tumbo lake lililoeka michilizi ya kukatika kimazoezi.
"Fumba macho basi D.."
Aliongea kwa sauti raini Asunta kwa aibu kwani hakuwa na jinsi tena ilibidi ageukie pembeni kwa ukutani na kuanza kuchojoa blauz yake huku akiwa kajiziba na taulo ili kuyaficha mautamu yake akiwa kampa mgongo D kisha taratibu alianza kuchojoa suruali yake lakini kutokana na vile umbile lake lilivyo na kwa jinsi alivyolifunga taulo kuzuia sehemu zake za juu kwenye maziwa ililifanya taulo kuzidi kuwa fupi hasa wakati alipoinama kumalizia kuvua suruali na kumuachia video ya bure D aliesimama nyuma yake akimuangalia na kumfanya Njomba Nchumali kuanza kuweweseka na kutingisha bukta ya D hasa alipoyaona mapaja mazuri ya Asunta na ktk hali ya kuhangaika na kujificha ficha hasa nae Asunta alipohisi maumbile yake nyuma yanaonekana na kulifungua taulo kwa juu ili alishushe tena chini kidogo pindi alipokuwa anamalizia kuvua mguu wa pili wa suruali yake ghafra kwa bahati mbaya taulo lote lilidondoka na kuacha mambo yote hadhalani na alipogeuka kuliokota hakuamini alipomuona D akiwa ameshikilia paipu yake iliyokuwa imetuna ipasavyo ndani ya bukta.

"Aaaah! jamani D nini tenaa?"
Aliuliza Asunta pindi alipoona D wazimu wa muda mrefu wa kitanga ulipoanza kumzonga kichwani na kupiga hatua pale alipo Asunta huku macho yake yakiwa yamebadilika na kuwa mekundu mithili ya mtu aliyekula ganja (bangi) kete ishirini pekeake.
"Asunta"
Aliita Dullah kwa sauti ambayo Asunta hakuwahi kuisikia, sauti iliyomaanisha kuhitaji kitu na wakati huo alikuwa kasimama jirani kabisa na Asunta aliyeegemea ukuta akimshangaa D kubadilika hisia ghafra vile na kabla Asunta hajafanya chochote Dullah alimkamata kwa kumshika sehemu ya mashavu na kuuinua uso wa Asunta aliyekuwa kauinamisha akiona aibu hata kuutazama uso wa Dullah na wakati huo mvua bado ilikuwa inapiga bati kwa wingi sana.
"Asunta naomba unitazame usiogope baby, amini mimi na wewe tumeunganishwa na mungu mwenyewe na hali hii iliyotokea haimaanishi mimi nina tamaa tu nawewe la hasha bali nakupenda sana tena inawezekana nikawa nakupenda zaidi yako na si kwa sababu una pesa ila ni sababu una moyo mzuri. Naomba ukunjue moyo wako tunapokuwa pamoja na ujisikie amani zaidi juu yangu.. Mvua hii naamini imekuwa baraka na alama aliyotutunuku mungu ktk mapenzi yetu naomba tuitumie baraka hii vizuri na ibaki kuwa shahidi wetu kama itatokea mmoja wetu kumsariti mwenzake hapo baadae.."
Aliongea Dullah huku akitumia ufundi wake wa kitanga na kumpelekea mdomo Asunta na kuunganisha mdomo wake na kwa ufundi aliokuwa nao D kipindi mikono ya Asunta ilikuwa ikilazimisha kuishusha mikono yake iliyokuwa mashavuni mwake huku vidole vya mwisho vya Dulla vikiwa vimeziba kwenye tundu za masikio ya Asunta na vidole gumba vikabinya taya ya Asunta na hapo ndipo Asunta mwenyewe alijikuta anaachia lipsi alizozibana na kumrahisishia Dullah kuupenyeza ulimi wake mdomoni mwake na kubadilishana mate taratiibu na ndipo alipoitoa mikono na kuikamata mikono ya Asunta viganja kwa viganja.
Asikwambie mtu Dullah hakuwa fundi uwanja wa nje tu wenye mashabiki, bali alikuwa fundi pia hadi kwenye uwanja mdogo wa ndani usiokuwa na shabiki yeyote kwani kwa jinsi alivyoanza kumpiga chenga ndogo ndogo Asunta hadi akabadilisha hisia zote alizokuja nazo awali na kumpandisha nae mapepo yake ya muda mrefu.
"aaaaasssss jamani D baaa..oooosss..baasiii...aaaah"
Aligugumia Asunta wakati huo D alibadilika na kumfanya asunta kama kitoto cha paka kilichozaliwa muda mfupi kwa jinsi alivyokuwa anamrambaramba mwili mzima na alipofika maeneo ya ikulu alianza kumfanyia vituko ambavyo Asunta hakuwa hata kuota kama vipo na hadi kufikia Asunta anatolewa kufuri lake na kupandishwa machinjioni pasi na kujitambua hadi alipohisi Njomba Nchumari wa Dullah anasongomeka bichwa lake kwenye kitundu kilichohifadhi asali yake isiyokwisha.
Vitu vya Dullah kwenye mambo yale ni ngumu sana kuvisimulia labda ukutane na Asunta umuombe akudokeze walau kiduchu! lakini kwa ufupi Dullah alikuwa fundi wa kale kamchezo na kumpagawisha Asunta kutoa vilio mfululizo ndani silio vilivyobeba hisia nzito, vilio vya usiniache,nakupenda,sikuachi,siamini na kadhalika hadi Dullah anapata gori la kwanza tayari Asunta alishajifunga mengine matatu na hadi mechi inamalizika matokeo yalikuwa Asunta Nne Dullah Mbili.

* * * * * *

ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 07


"Asunta, Asunta, Asunta baby amka basi tule Asunta.."
Alikuwa ni Dullah akimuamsha Asunta aliyepitiwa na usingizi mzito kwa muda mrefu toka wamalize mechi na Asunta alionekana kuchoka mno na hapo alijigeuza kwa uchovu na kumtazama D usoni kwa macho maregevu.
"Niekee maji ya kuoga kwanza mume wangu"
Aliongea kwa sauti ya uchovu mno Asunta nae D alinyanyuka fasta na kufanya vile ambapo baada ya kurudi na kumtoa Asunta kumpeleka bafuni wakati huo mvua ilikuwa ishaacha kunyesha.
"Heee, shoga umemuona rasta leo?"
"Mmh!! nakwambiaa!! "
"heeeeheeee... Kaogeeee"
Yalikuwa ni maneno ya umbea toka kwa videmu vya mtaa ule pindi walipomuona Dullah akimtoa Asunta kumpeleka bafuni.
Asunta almanusura azimie kwa mstuko baada ya kutoka nje na kuona kumbe ilishakuwa usiku.
"Haaa!! D saa ngapi saivi?"
"Bado mapema tu baby saa tatu kasoro"
"Tatu Kasorooo! Yesu wanguuu D umeniponza sana leo mamaaa..."
Alipagawa Asunta na kujikuta anarudi kwanza ndani badala ya kwenda bafuni ambapo alikimbilia kwenye mkoba wake na kutoa simu ambayo ilionesha kuwa na missed call 16 toka kwa mamaake na msg 8 na kabla hajazifungua simu ilianza kuita na safari hii lilitokea jina 'MY DADDY' hapo alibaki anaitazama simu huku mwili mzima ukimtetemeka kwa hofu.

"D umeona sasa daah!!"
aliongea Asunta huku akipigapiga mikono kwenye mapaja yake na kurusha vidole utadhani amechanwa viganja na kiwembe huku akiishia kuitazama ile simu pasi na kuipokea mpaka ikakatika na kuanza kuita kwa mara ya pili.
"Kwani nani anaekupigia"
"Baba Dullah.. Daah! najuta mimi sijui hata nitaanzia wapi! daah.."
"Sikia baby usiogope wala usichanganyikiwe utadhani umekutwa na kichwa cha albino kwenye mkoba wako hebu tulia kwanza nihadithie kidogo ulivyotoka na kuaga nyumbani kisha nijue tunafanyaje"
"D, haisaidii chochote jamani mi nimelazimisha tu kutoka afu daah, kwaheri acha niende tu nitajua mbele kwa mbele"
"Asunta vipi wewe? hivi unajua kama umejifunga taulo tu, sasa unaendaje"
aliongea Dullah na kumkumbusha Asunta aliyebeba mkoba wake kwaajili ya kuondoka huku akiwa amejisahau kama alikuwa na taulo tuu mara alipotoka awali kwa dhumuni la kwenda kuoga.
Baada ya kujitazama na kuamini kumbe alikuwa hajavaa ndipo Asunta alipoghairi hata kuoga kwenyewe na kuchukua nguo zake ambazo alisahau kama zililowa chapachapa na hakubeba nguo yoyote ya akiba.
"Dah! mbona mikosi sasa Dullah nitavaaje nguo hizi zimelowa kiasi hiki?"
"Mi nakushauli Asunta kwanza pokea simu kuwatoa wasiwasi wazazi"
Aliongea Dullah mara baada ya simu kuanza kuita tena.
"Harafu niwambieje..!"
"Waambie wasiwe na wasi upo salama kabisa na utaporudi ndio utaongea nao vizuri"
"weeweweweeee Dullah tatizo humjui babaangu na hujui jinsi gani alivyo"
"sasa unadhani vipi Asu wangu nipe basi niongee nae mie"
"hahahaaa usinifanye nicheke wakati nimechanganyikiwa D, wacha tu nivae hivi hivi potelea mbali"
alikata shauli Asunta na kuanza kuzivaa zile nguo licha ya kuwa zilikuwa mbichi na ndipo Dullah alipomzuia.
"Sikia baby, kiafya tumefundishwa shule japo ya msingi kuwa tusivae nguo zilizolowa sasa siweze kuvumilia kipenzi changu yakupate maladhi kwa ajili ya nguo mbichi. nakuomba vaa hizi"
alinena Dullah na kufungua mfuko wake mkubwa wa rambo ambapo alihifadhi nguo zake na kutoa suruali moja aliyoitenga kwa safari pamoja na tishet ya jezi ya Chelsea na kumkabidhi Asunta huku akiwa amempigia magoti kwa heshima kubwa.
Alijikuta anatabasam mwenyewe Asu mtoto wa Pastor George kwa vituko vya Dullah na kupokea zile nguo kisha kuzivaa licha ya kwamba suruali ilishindwa kumkaa vizuri kutokana na kuwa ya kiume lakini ile tishrt ya chelsea ilimpendeza vizuri sana na baada ya kuwa tayari alimuomba Dullah amsindikize stendi ya Taxi.
"Asu bwana, ushasikia wapi Tandale uswahilini kuna stendi ya taxi! labda hospitali kule au barabarani kubahatisha lakini zaidi hapa ni bajaj na bodaboda."
"sawa D twende lakini daaah! naona hata aibu hivi nilivyovaa ila kwakuwa za baby wangu rasta nitazieka kuwa kumbukumbu ya siku hii ndani kwangu maana kila nitavyozitazama nitakumbuka mvua na......"
alisita Asunta kisha kumtazama Dullah aliyekuwa anatabasamu muda wote huku akiwa haamini moyoni kama kweli yeye ndie aliyefaidi mautamu ya tunda zuri la mtoto mzuri Asunta.

Walifika stend ya bajaji ambapo Asunta aliamini kuwa Dullah angeishia hapo lakini ajabu kwake alishangaa kuona D nae kapanda kwenye ile bajaji na kumuamuru dereva awapeleke huko Masaki.
" Yesu wangu Ha! D kwani tunaenda wote?!!"
"Ndio, we ulidhani nitakuacha usiku huu uzulule pekeako?"
"aaah!! hapana D hivyo utaniongezea matatizo kwa kweli we ungebaki tu mi ntafika mwenyewe."
"Asu, mwenzio kudanganya siwezi kwani naamini siku zote ukweli una nguvu ya muda mrefu kuliko uongo pia siogopi kusema ukweli japo najua unauma."
"sasa Dullah unataka kunambia unataka kufika mpaka kwetu?"
"Ndio manaake hii inaitwa mguu kwa mguu hadi mlangoni kwenu nikukabidhi ukiwa salama usalimini."
"Weeee, Dullah acha utani kabisa nakuomba usije kufanya kitu kama hiko utajieka pabaya pia itakuwa rahisi sana kunikosa, wazazi wangu ni wakali sana na hawapendi ujinga hasa baba."
"sasa Asu mama, kama kukufikisha kwenu ukiwa salama ndio nitaonekana nimefanya ujinga!!?"
"hapana sio hivyo unavyodhani."
"Kumbe"
"Basi tuu"
Alishindwa kuongea zaidi Asu baada ya kuona D amekazia uzi msimamo wake wa kumfikisha mpaka kwao huku kwa upande wa moyoni Asunta alijua kama atathubutu kufika na Dullah nyumbani kwao usiku ule basi balaa litazidi mara mbili na lilivyotakiwa kuwa.
Lakini kwa upande wa Dullah moyoni alijisikia faraja na kuona kitakuwa kitendo cha kishujaa sana endapo atathubutu kumfikisha Asunta mpaka kwao kabisa akiwa salama usalimini usiku ule.
Asunta alimuelekeza vizuri njia dereva yule ambae alionekana kuwa mgeni maeneo ya masaki mpaka pale alipofika kwenye Jumba moja la kifahari lililokuwa na geti jekundu ambalo Dullah alilikumbuka vizuri kwani siku chache nyuma waliwahi kuwa pale na Fred walipoenda kuuza vyombo.
Baada ya bajaji kusimama pale Dullah alimwambia mwenye bajaji amsubirie pale pale nje akiwa D bado na msimamo wake wa kumfikisha hadi ndani ya geti Asunta hadi ahakikishe anaingia kabisa chumbani kwake kulala na mida hiyo tayari ilikuwa saa tano usiku ambapo pia Asunta sasa alianza kutumia mbinu za kumzuia Dullah asiingie ndani ili balaa litalienda kuwaka limuwakie mwenyewe kwani alihisi huenda babaake amepata dharula amerudi.
Wakiwa wanaendelea kubishana pale nje ghafra walistuliwa pindi geti lilipofunguliwa na walichokiona mbele yao kilistua nafsi zao wote wawili yaani Dullah na Asunta.


* * * * * *
((MASAA 7 YALIYOPITA)) - MASAKI -


Akiwa amekaa juu kabisa ghorofani kwenye sehemu maalum iliyotengenezwa kwaajili ya kupumzika na kupigwa na upepo wa bahari huku pembeni yake kukionekana glasi yenye juice ya parachichi, mama Asunta alianza kupata wasiwasi baada ya kuona mwanae anazidi kuchelewa na tayari ilikuwa saa kumi na moja jioni ndipo alipoamua kumpigia simu na kukuta ikiita muda mrefu pasi na kupokelewa na hata aliporudia mara ya pili ikawa hivyohivyo ndipo alipoamua kumtumia ujumbe mfupi wa maneno kumuulizia alipo ambao nao haukujibiwa mpaka ikafika saa kumi na mbili hapo sasa raha ya kuendelea kuwa kule juu akipulizwa upepo ilimtumbukia nyongo mama Asu na kuendelea kumpigia simu mwanae na kutuma meseji bila kujibiwa chochote na kuzidi kupata wasiwasi.
"Mh!! masikini mwanangu nini kimemkuta tena"
aliwaza yule mama na kutelemka chini kisha kumuulizia mfanya kazi yule wa kike kama aliongea na Asunta toka ameondoka ambapo nae alikanusha kutoongea nae.
Akiwa bado haelewi huku akizidi kuchanganyikiwa ndipo simu yake iliita na alipoiangalia akijua mwanae moyo ulimstuka kidogo baada ya kugundua ni mumewe na kuhofia endapo angemuulizia Asunta atajibu nini, alifikiria kidogo na kupiga moyo konde kisha akaipokea.
"Haloo mume wangu... Eee nakusikia, waoo vipi hali ya hewa huko....si hatujambo...tunamshukuru bwana....haya....nitamwambia ila alitoka na Vero ndo wamenipigia wako njiani wanarudi... haya nawe pia bwana awe nanyi ktk kazi za utumishi..amen."
Alimaliza maongezi na mumewe na hapo ndipo alipomtumia msg tano akimsisitiza mwanae kuwa endapo atapigiwa na babaake aseme yuko na Vero na si vinginevyo lakini hadi inafika saa mbili msg hata moja haikujibiwa huku simu alikuwa kapiga mpaka vidole vikaanza kuuma pasi na kupokelewa na hapo ndipo alipomuamuru dereva wake watoke kuangalia jinsi ya kumtafuta Asunta kwani haikuwa kawaida yake kurudi usiku alihisi huenda kapatwa matatizo.
Walihangaika mpaka kwa kina Vero na hata walipofika na kuwagongea siku hiyo Vero pia alikuwapo na alishangazwa na habari za Asunta.
"Kwani ina maana Vero humjui huyo mtu mwenyewe."
"Mh! mama Asunta hajawahi kunambia habari hizo mbona?"
"sasa nyinyi ndio marafiki ina maana hata mambo yenu hamuambiani.?"
"tunaambiana mama ila hilo mi silijui."
"Heee!!!"
Alizidi kudata mama Asunta baada ya kuhisi sasa kuna asilimia kubwa mwanae akawa amepatwa matatizo makubwa sana na kujikuta anakata shauli na kukubaliana na mama Vero pamoja na Vero mwenyewe kuwa wakatoe taarifa polisi kwa msaada zaidi na ndipo walipofika polisi ikiwa tayari saa Nne za usiku na baada ya kutoa maelezo na kutokana na mpelelezi mmoja kumfahamu vizuri Pastor George aliamua kulisimamia yeye faili lile na kumchukua askali mwenzake mmoja kwanza kwenda mpaka walipoishi kina Asunta kuanza shughuli zao huko.


ITAENDELEA
 
Hadithi nzuri unajitahidi lakini fupi sana unakata utamu kati kati....
na hao polisi ndo ushamuharibia dulla ujue!!
 
SEHEMU YA 07


"Asunta, Asunta, Asunta baby amka basi tule Asunta.."
Alikuwa ni Dullah akimuamsha Asunta aliyepitiwa na usingizi mzito kwa muda mrefu toka wamalize mechi na Asunta alionekana kuchoka mno na hapo alijigeuza kwa uchovu na kumtazama D usoni kwa macho maregevu.
"Niekee maji ya kuoga kwanza mume wangu"
Aliongea kwa sauti ya uchovu mno Asunta nae D alinyanyuka fasta na kufanya vile ambapo baada ya kurudi na kumtoa Asunta kumpeleka bafuni wakati huo mvua ilikuwa ishaacha kunyesha.
"Heee, shoga umemuona rasta leo?"
"Mmh!! nakwambiaa!! "
"heeeeheeee... Kaogeeee"
Yalikuwa ni maneno ya umbea toka kwa videmu vya mtaa ule pindi walipomuona Dullah akimtoa Asunta kumpeleka bafuni.
Asunta almanusura azimie kwa mstuko baada ya kutoka nje na kuona kumbe ilishakuwa usiku.
"Haaa!! D saa ngapi saivi?"
"Bado mapema tu baby saa tatu kasoro"
"Tatu Kasorooo! Yesu wanguuu D umeniponza sana leo mamaaa..."
Alipagawa Asunta na kujikuta anarudi kwanza ndani badala ya kwenda bafuni ambapo alikimbilia kwenye mkoba wake na kutoa simu ambayo ilionesha kuwa na missed call 16 toka kwa mamaake na msg 8 na kabla hajazifungua simu ilianza kuita na safari hii lilitokea jina 'MY DADDY' hapo alibaki anaitazama simu huku mwili mzima ukimtetemeka kwa hofu.

"D umeona sasa daah!!"
aliongea Asunta huku akipigapiga mikono kwenye mapaja yake na kurusha vidole utadhani amechanwa viganja na kiwembe huku akiishia kuitazama ile simu pasi na kuipokea mpaka ikakatika na kuanza kuita kwa mara ya pili.
"Kwani nani anaekupigia"
"Baba Dullah.. Daah! najuta mimi sijui hata nitaanzia wapi! daah.."
"Sikia baby usiogope wala usichanganyikiwe utadhani umekutwa na kichwa cha albino kwenye mkoba wako hebu tulia kwanza nihadithie kidogo ulivyotoka na kuaga nyumbani kisha nijue tunafanyaje"
"D, haisaidii chochote jamani mi nimelazimisha tu kutoka afu daah, kwaheri acha niende tu nitajua mbele kwa mbele"
"Asunta vipi wewe? hivi unajua kama umejifunga taulo tu, sasa unaendaje"
aliongea Dullah na kumkumbusha Asunta aliyebeba mkoba wake kwaajili ya kuondoka huku akiwa amejisahau kama alikuwa na taulo tuu mara alipotoka awali kwa dhumuni la kwenda kuoga.
Baada ya kujitazama na kuamini kumbe alikuwa hajavaa ndipo Asunta alipoghairi hata kuoga kwenyewe na kuchukua nguo zake ambazo alisahau kama zililowa chapachapa na hakubeba nguo yoyote ya akiba.
"Dah! mbona mikosi sasa Dullah nitavaaje nguo hizi zimelowa kiasi hiki?"
"Mi nakushauli Asunta kwanza pokea simu kuwatoa wasiwasi wazazi"
Aliongea Dullah mara baada ya simu kuanza kuita tena.
"Harafu niwambieje..!"
"Waambie wasiwe na wasi upo salama kabisa na utaporudi ndio utaongea nao vizuri"
"weeweweweeee Dullah tatizo humjui babaangu na hujui jinsi gani alivyo"
"sasa unadhani vipi Asu wangu nipe basi niongee nae mie"
"hahahaaa usinifanye nicheke wakati nimechanganyikiwa D, wacha tu nivae hivi hivi potelea mbali"
alikata shauli Asunta na kuanza kuzivaa zile nguo licha ya kuwa zilikuwa mbichi na ndipo Dullah alipomzuia.
"Sikia baby, kiafya tumefundishwa shule japo ya msingi kuwa tusivae nguo zilizolowa sasa siweze kuvumilia kipenzi changu yakupate maladhi kwa ajili ya nguo mbichi. nakuomba vaa hizi"
alinena Dullah na kufungua mfuko wake mkubwa wa rambo ambapo alihifadhi nguo zake na kutoa suruali moja aliyoitenga kwa safari pamoja na tishet ya jezi ya Chelsea na kumkabidhi Asunta huku akiwa amempigia magoti kwa heshima kubwa.
Alijikuta anatabasam mwenyewe Asu mtoto wa Pastor George kwa vituko vya Dullah na kupokea zile nguo kisha kuzivaa licha ya kwamba suruali ilishindwa kumkaa vizuri kutokana na kuwa ya kiume lakini ile tishrt ya chelsea ilimpendeza vizuri sana na baada ya kuwa tayari alimuomba Dullah amsindikize stendi ya Taxi.
"Asu bwana, ushasikia wapi Tandale uswahilini kuna stendi ya taxi! labda hospitali kule au barabarani kubahatisha lakini zaidi hapa ni bajaj na bodaboda."
"sawa D twende lakini daaah! naona hata aibu hivi nilivyovaa ila kwakuwa za baby wangu rasta nitazieka kuwa kumbukumbu ya siku hii ndani kwangu maana kila nitavyozitazama nitakumbuka mvua na......"
alisita Asunta kisha kumtazama Dullah aliyekuwa anatabasamu muda wote huku akiwa haamini moyoni kama kweli yeye ndie aliyefaidi mautamu ya tunda zuri la mtoto mzuri Asunta.

Walifika stend ya bajaji ambapo Asunta aliamini kuwa Dullah angeishia hapo lakini ajabu kwake alishangaa kuona D nae kapanda kwenye ile bajaji na kumuamuru dereva awapeleke huko Masaki.
" Yesu wangu Ha! D kwani tunaenda wote?!!"
"Ndio, we ulidhani nitakuacha usiku huu uzulule pekeako?"
"aaah!! hapana D hivyo utaniongezea matatizo kwa kweli we ungebaki tu mi ntafika mwenyewe."
"Asu, mwenzio kudanganya siwezi kwani naamini siku zote ukweli una nguvu ya muda mrefu kuliko uongo pia siogopi kusema ukweli japo najua unauma."
"sasa Dullah unataka kunambia unataka kufika mpaka kwetu?"
"Ndio manaake hii inaitwa mguu kwa mguu hadi mlangoni kwenu nikukabidhi ukiwa salama usalimini."
"Weeee, Dullah acha utani kabisa nakuomba usije kufanya kitu kama hiko utajieka pabaya pia itakuwa rahisi sana kunikosa, wazazi wangu ni wakali sana na hawapendi ujinga hasa baba."
"sasa Asu mama, kama kukufikisha kwenu ukiwa salama ndio nitaonekana nimefanya ujinga!!?"
"hapana sio hivyo unavyodhani."
"Kumbe"
"Basi tuu"
Alishindwa kuongea zaidi Asu baada ya kuona D amekazia uzi msimamo wake wa kumfikisha mpaka kwao huku kwa upande wa moyoni Asunta alijua kama atathubutu kufika na Dullah nyumbani kwao usiku ule basi balaa litazidi mara mbili na lilivyotakiwa kuwa.
Lakini kwa upande wa Dullah moyoni alijisikia faraja na kuona kitakuwa kitendo cha kishujaa sana endapo atathubutu kumfikisha Asunta mpaka kwao kabisa akiwa salama usalimini usiku ule.
Asunta alimuelekeza vizuri njia dereva yule ambae alionekana kuwa mgeni maeneo ya masaki mpaka pale alipofika kwenye Jumba moja la kifahari lililokuwa na geti jekundu ambalo Dullah alilikumbuka vizuri kwani siku chache nyuma waliwahi kuwa pale na Fred walipoenda kuuza vyombo.
Baada ya bajaji kusimama pale Dullah alimwambia mwenye bajaji amsubirie pale pale nje akiwa D bado na msimamo wake wa kumfikisha hadi ndani ya geti Asunta hadi ahakikishe anaingia kabisa chumbani kwake kulala na mida hiyo tayari ilikuwa saa tano usiku ambapo pia Asunta sasa alianza kutumia mbinu za kumzuia Dullah asiingie ndani ili balaa litalienda kuwaka limuwakie mwenyewe kwani alihisi huenda babaake amepata dharula amerudi.
Wakiwa wanaendelea kubishana pale nje ghafra walistuliwa pindi geti lilipofunguliwa na walichokiona mbele yao kilistua nafsi zao wote wawili yaani Dullah na Asunta.


* * * * * *
((MASAA 7 YALIYOPITA)) - MASAKI -


Akiwa amekaa juu kabisa ghorofani kwenye sehemu maalum iliyotengenezwa kwaajili ya kupumzika na kupigwa na upepo wa bahari huku pembeni yake kukionekana glasi yenye juice ya parachichi, mama Asunta alianza kupata wasiwasi baada ya kuona mwanae anazidi kuchelewa na tayari ilikuwa saa kumi na moja jioni ndipo alipoamua kumpigia simu na kukuta ikiita muda mrefu pasi na kupokelewa na hata aliporudia mara ya pili ikawa hivyohivyo ndipo alipoamua kumtumia ujumbe mfupi wa maneno kumuulizia alipo ambao nao haukujibiwa mpaka ikafika saa kumi na mbili hapo sasa raha ya kuendelea kuwa kule juu akipulizwa upepo ilimtumbukia nyongo mama Asu na kuendelea kumpigia simu mwanae na kutuma meseji bila kujibiwa chochote na kuzidi kupata wasiwasi.
"Mh!! masikini mwanangu nini kimemkuta tena"
aliwaza yule mama na kutelemka chini kisha kumuulizia mfanya kazi yule wa kike kama aliongea na Asunta toka ameondoka ambapo nae alikanusha kutoongea nae.
Akiwa bado haelewi huku akizidi kuchanganyikiwa ndipo simu yake iliita na alipoiangalia akijua mwanae moyo ulimstuka kidogo baada ya kugundua ni mumewe na kuhofia endapo angemuulizia Asunta atajibu nini, alifikiria kidogo na kupiga moyo konde kisha akaipokea.
"Haloo mume wangu... Eee nakusikia, waoo vipi hali ya hewa huko....si hatujambo...tunamshukuru bwana....haya....nitamwambia ila alitoka na Vero ndo wamenipigia wako njiani wanarudi... haya nawe pia bwana awe nanyi ktk kazi za utumishi..amen."
Alimaliza maongezi na mumewe na hapo ndipo alipomtumia msg tano akimsisitiza mwanae kuwa endapo atapigiwa na babaake aseme yuko na Vero na si vinginevyo lakini hadi inafika saa mbili msg hata moja haikujibiwa huku simu alikuwa kapiga mpaka vidole vikaanza kuuma pasi na kupokelewa na hapo ndipo alipomuamuru dereva wake watoke kuangalia jinsi ya kumtafuta Asunta kwani haikuwa kawaida yake kurudi usiku alihisi huenda kapatwa matatizo.
Walihangaika mpaka kwa kina Vero na hata walipofika na kuwagongea siku hiyo Vero pia alikuwapo na alishangazwa na habari za Asunta.
"Kwani ina maana Vero humjui huyo mtu mwenyewe."
"Mh! mama Asunta hajawahi kunambia habari hizo mbona?"
"sasa nyinyi ndio marafiki ina maana hata mambo yenu hamuambiani.?"
"tunaambiana mama ila hilo mi silijui."
"Heee!!!"
Alizidi kudata mama Asunta baada ya kuhisi sasa kuna asilimia kubwa mwanae akawa amepatwa matatizo makubwa sana na kujikuta anakata shauli na kukubaliana na mama Vero pamoja na Vero mwenyewe kuwa wakatoe taarifa polisi kwa msaada zaidi na ndipo walipofika polisi ikiwa tayari saa Nne za usiku na baada ya kutoa maelezo na kutokana na mpelelezi mmoja kumfahamu vizuri Pastor George aliamua kulisimamia yeye faili lile na kumchukua askali mwenzake mmoja kwanza kwenda mpaka walipoishi kina Asunta kuanza shughuli zao huko.


ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 08


Mara baada ya lisaa limoja walikuwa washamaliza tafiti zao za awali chumbani kwa Asunta wale askali wawili sambamba na Vero na mama Asunta ambae dakika hizo alishindwa kuyazuia machozi huku akiwazia mumewe atakuwaje atapopata taarifa zile..!
Wakiwa wanaagana na wale askali waliokuwa wanamsihi pia mama mchungaji asilie na alale kwa amani tu kwa kumuhakikishia bint ake atapatikana akiwa salama salimini na wakiwa wanaongea ndipo waliposikia mlio wa bajaji kwa nje ikisimama na waliposikilizia walisikia sauti ya Asunta akibishana na mtu swala la kuingia ndani na hapo ndipo walipofungua geti na kuwashuhudia uso kwa uso Asunta na Dullah.

"Yesu wanguuuu..!!!! Asuntaa?"
alihamaki mama Asunta na wakati huo huo wale polisi haraka walimkamata Dullah huku yule dereva bajaji wakimkosa baada ya kutimua bajaji yake kwa spidi ya hatari na kumuacha mteja wake aliyekuwa anamsubiri katika kasheshe zito.
"Kaa chini tuliaa Mjinga wee."
alichimba biti (alimtia hofu) afande mmoja aliyemkwida na kumpiga ngwala Dullah wakati huo yule mwengine alimshika mkono Asunta na kumsogezea kule kwa mamaake.
"sasaa Afandeee mbona unanivamia, unanipiga na kunitusi? kipi nimekosa?"
"Peleka huko Mibangi yako tena kelele kabisa usije nipandisha hasira zaidi nikakunyofoa nyofoa minywele yako."
Bado yule afande alizidi kumuwakia Dullah wakati huo yule polisi mwengine alikuwa anamtuliza Asunta na kuongea na mamaake aliyebaki katahayuri akimtazama mara mbilimbili mwanae sambamba na Dullah ambae alikuwa anachezea virungu kimtindo pale pembeni ya geti.

"Mama mchungaji kama nilivyokutaarifu awali na ndivyo ilivyokuwa, nilikwambia usiwe na wasiwasi sasa nadhani umeamini nami nakusikiliza unataka tumfanyeje huyu mpuuzi mwenye rasta, tumvunje miguu au tumpoteze kabisa aache kusumbua watu."
"Jamaniii naomba muacheniii huyo si mtu m baya kanisindikiza tuu"
alijitahidi kutetea Asunta baada ya kusikia kauli ya yule afande wakati huo ilishatoka amri kuwa mlinzi ampeleke ndani Asu huku nyuma yake akifuatiwa na Verombamba na yule house girl.
"Jamani askali mi kikubwa nilikuwa nataka nimpate mwanangu ila huyu kijana naomba msimfanye kitu kwanza nimuulize, Eti kijana wewe ndie Dullah?"
aliongea mama mchungaji na kusogea pale alipokwidwa D.
"Ndio mama mimi ndie Dullah. shkamoo mama"
"Yesu wangu!! wewe si uliwahi kuja na Fred hapa kuleta vyomboa au..?"
alitaharuki zaidi yule mama baada ya kusogea na kumuangalia vizuri Dullah.
"Ndio mama, ndie mimi nilikuja na Fred kuuza vyombo."
bila hofu wala wasi Dullah alijibu bila kujua kuwa majibu yake yalizidi kumchefua mama mchungaji.
"Yaani we kijana hivi kusoma hujui, hata picha huoni? mbona unataka kutuharibia mtoto! Mungu wangu sijui mwanangu kakumbwa na nini hadi kwenda kujitafutia balaa hili... Eti nini kimekuleta labda ungenambia."
"Mama mimi ni mtoto wa kimasikini kweli tena sana lakini kilichonikutanisha na Asunta si pesa bali ni moyo, na kilichonileta hapa ni kuhakikisha anakuwa salama na sio kumuacha mwenyewe nikihofia angeweza patwa tatizo mamaangu. lakini ukweli Nampenda sana Asu nae ananipenda pia na kama kumfikisha salama ndio kosa langu niko radhi niendelee kuadhibiwa."
"Umeliona mama Mchungaji hili lijamaa linakupotezea muda wa kupumzika tu, acha tukalitie adabu si umeona linaongea mibangi tuu"
alidakia afande yule aliyemkwida Dullah.
"Sawa bwana Dullah nimekusikia nakupongeza kwa kuonesha confident mbele yangu ila nina imani kama angekuwepo baba Asu naamini hata uwezo wa kunyanyua huo mdomo usingekuwa nao. Ila mi nakutahadhalisha kijana achana na mwanangu Asunta na kuanzia leo usahau kabisa kwani hatuhitaji matatizo na wewe wala sikuhukumu chochote nakuomba na nakuonya."
"Nimekusikia mama ila kiukweli mdomo wangu unaweza kuwa tayari kusema hivyo lakini moyo wangu kumbuka hauwezi kusema mama na Asu ndie yuko moyoni mwangu"
Kauli ya Dullah alijiponza na kushushiwa vilungu mfurulizo akichangiwa na wale maafande na baada ya kuwa hoi D huku msimamo wake wa kumpenda Asunta ukibaki pale pale ndipo yule mama aliposogea pembeni na afande mmoja na kuongea nae kisha Dullah alipigwa pingu na kuingizwa kwenye gari waliyoenda nayo pale wale askali na safari ya kituoni ilianza.

* * * * * *

"Asu rafikiangu kwanini unajidhalilisha hivyo? yaani hebu ona leo ulivyokuwa daah!"
ilikuwa ni sauti ya Vero akiwa anamuongelesha Asunta aliekuwa bado analia wakiwa kitandani.
Kauli ya Vero ilimuudhi sana Asunta na kumtazama kwa hasira rafikiake na kulala huku akiwa kajifunika mwili mzima.
"Naomba msiniongeleshe kitu niacheni "
aliongea Asunta na hata mamaake alipoingia ndani na kumkuta katika hali ile aliamua kumuacha akiamini asubuhi angeongea nae vizuri muda ambao akili ya Asunta itakuwa imetulia.

..............
< UPANDE WA PILI >
_________________

Alionekana Dullah akiwa kafungwa kwenye selo maalum akipewa mateso huku akiulizwa kama ataacha kumfatilia mtoto wa mchungaji lakini msimamo wa ajabu wa Dullah ulibaki palepale kuwa Asunta anaishi moyoni mwake na moyo hauwezi kusema.
Kauli zile ziliwafanya wale askali kumzidishia mateso mpaka alfajiri ambapo D alikuwa ametepweta mwili mzima
Kwa bahati nzuri yule mama mchungaji aliwapa hela wale maaskali kuwa wamtishe tu wasimpeleke kokote kwa kuhofia pia habari zile zisije kuvuja na mfikia Pastor George aliyekuwa Nairobi kwa kipindi hiko.
Asubuhi yake Dullah alitolewa na kuruhusiwa kuondoka huku akipewa onyo kwa mara nyengine kuwa aachane na mtoto wa mchungaji.
alichechemea bila kujibu kitu mpaka getto kwake ambapo kila aliyekutana nae aligeuka na kumshangaa kwa jinsi alivyoonekana shati yake ikiwa imechanwa na alipasuliwa sehemu za kichwani lakini moyoni mwake bado hakujutia Dullah kupigwa kwaajili ya Asunta aliona ni bora kuliko angemuacha aondoke mwenyewe harafu akapatwa matatizo njiani usiku ule.


* * * * * *

Zilipita siku mbili toka Dullah apatwe majanga yale huku muda wote simu ya Asunta haikupatikana wala hakupata ujumbe wowote kutoka kwa Asu. Hali hii ilimtia upweke na mawazo D asijue nini cha kufanya kwani ndio kwanza moyo wake ulianza kupenda na hakuwa tayari kuwa mbali na Asunta.
Siku hiyo ikiwa ndio ilikuwa siku yake ya kwanza kuanza kupasha mwili alfajiri tangu alipoumizwa na wale polisi.
Dullah akiwa anakimbia uwanjani mawazo yake yote bado yalibaki kwa Asunta na hata baada ya wiki kupita alipokuwa anaenda mazoezini kiwango chake kilionekana kushuka ghafra hadi mascout wa vilabu mbali mbali vya ligi kuu waliokuwa wanaenda kumchunguza uwezo wake mara baada ya mechi ile ya kirafiki alivyowafanya simba lakini walishangaa kuona kiwango chake kikiwa cha kawaida sana tu hali iliyowaaminisha kuwa siku ile alivyocheza na simba bahati ya mtende tu ilimdondokea.

Upweke wa bila kuwa na Asunta ulizidi kuitesa nafsi ya Dullah na kila siku alipiga namba ya Asunta bila kumpata na kutuma meseji ambazo wmishoe zilirudi hapo alijikatia shauli na kuamua liwalo na liwe lazima aende hukohuko kwa kina Asu kwani aliamini ukweli hudumu kuliko kukaa kiuongo na kuiumiza nafsi yake.

Baada ya masaa machache alifika maeneo ya Masaki na hatimae akawa mbele ya mjengo wa kina Asunta na kubonyeza kengele ambapo alitoka mlinzi.
"aag, Bob marley nikusaidie nini mwana"
"Naomba niitie Asunta ndugu yangu mwambie D yuko nje "
"Kha! we si ndio ulirushwa rushwa mabuti juzijuzi tu hapa? mwanangu naona sasa unataka kupigwa risasi za kichwa... hivi hujioni ulivyo? hahahahaa Duh!! we kweli zuzu"
kauli ile ya yule mlinzi ilimkera sana Dullah kwa kuitwa zuzu kwa kisa tu kumpenda Asu na kujikuta anaanza mzozo na yule mlinzi kwa kubishana pale nje.
"ndugu yangu sisi sote wanaume tena hali zetu hazitofautiani sana kwanini sasa unanitusi namna hii..?"
"sio nakutusi ailee, wenzako wanaokuwaga na marasta wanakuwa wapole wao wanacheza na vijiti tu kuitafuta amani, sasa wewe unaecheza na watoto wa watu unachotafuta nini kama sio kifo"
"sasa hata nikifa we kitakuuma nini?"
"akha,,! kiniume nini na kwetu hatuna hata ndugu mmoja marasta labda ningeumia kwa kukufananisha nae. man narudia tena we sepa tu."
sauti ile ya juu ya mlinzi ilimfanya Asu ambae kumbe alikuwa eneo la nje kwenye bustani akiwa kakaa akijilazimisha kusoma kitabu cha story za mtoto wa Becker ili kimpunguzie mawazo mazito aliyokuwa nayo ndipo alistuka kuona mlinzi muda wote akiwa katika hali ya kubishana na mtu aliyekuwa nje ya geti na kumfanya asogee jirani zaidi kuona kulikoni pale getini.
"We Octa, nani huyo?"
aliita na kuulizia Asu wakati huo huo ujumbe mfupi wa maneno uliingia kwenye simu yake kipindi akipiga hatua nae kuelekea getini ambapo alipoufungua alikuta umetumwa na mamaake aliyeenda na watu kadhaa wa kanisa kwenda kumpokea mumewe aliyekuwa narudi siku hiyo baada ya safari ya siku kadhaa alipokwenda kuhubiri neno la mungu Kenya. Ujumbe ulisomeka hivi..
'''' Kuweni tayari tayari tunakaribia hapo tupo na baba Askofu kutoka Nairobi pia mwambie mlinzi akae jilani na geti ''''

Alipomaliza kuisoma ile meseji alikuwa amefika pale getini na alipoangalia kwa nje hakuamini macho yake kumuona Dullah ambapo kama watoto walijikuta wote wanakumbatiana mbele ya mlinzi na kupeana mabusu motomoto.
"Mmmhmh.. D nakuomba we nenda tu, mi nimenyeng'anywa kila kitu ila nakuahidi nitafanya kila liwezekanalo nitakuja tu.."
aliongea Asunta huku akimvutia Dullah kwa nje na kumsihi asipoteze muda pale.
"Lakini Asu...."
"D naomba nisikilize pia niamini we ondoka sasa hivi tena ukikaa zaidi itakuwa balaa ambalo halijawahi tokea, wee nenda Dullah.."
alisisitiza Asu na Dullah kishingo upande alianza kupiga hatua kuondoka huku Asu na mlinzi wakiwa wanamuangalia pale getini lakini mara muda ule ule kwenye kona mbele yake ulionekana msafara wa gari za kisasa tatu uliom beba Pastor George na watumishi wengine wa mungu ukiingia maeneo yale.


ITAENDELEA
 
Story yako nzuri isipokuwa inakosa msisimko, radha na maudhui kwa sababu ya kutoiweka katika mtiririko mmoja.
 
SEHEMU YA 09


Dullah alisimama pembeni na kuzipisha zile gari ambazo hakuweza kuona waliokuwapo ndani yake kutokana na tinted zilizofungwa kwenye vioo vya gari zile zote tatu na kuzisindikiza kwa macho mpaka alipoona zinasimama na kuingia kwenye geti lililokuwa linafunguliwa pale kwa kina Asunta.
Na hapo ndipo alipogundua bila shaka ni wazazi wa Asunta na ndio maana Asu alimsihi sana awahi kuondoka nae haraka aliamua kukunja nyuma ya ile fensi kulipokuwa na barabara ya lami na kutoweka kwa mwendo wa haraka sana maeneo yale.

"Mama Asu, kama nimemuona kijana mmoja mchafu akitokea maeneo haya yetu, au we hukumuona?"
aliuliza Pastor George akiwa ndani ya gari pindi walipokuwa wanaingia getini.
"Aag! baba Asu nawe? si muokota makopo yule anapitaga pitaga hapa akielekeaga kule beach wanapouza maji na soda."
alizuga mama Asu na kumpoteza kwenye mstali mumewe licha ya kuwa ukweli mama Asu alimgundua kuwa yule kijana ni yuleyule anayemsumbua mwanae lakini hakutaka kabisa swala lile mumewe ajue.
"ahaa, Kumbe. Mi nilijua Octa kaanza kuleta marafiki wake wa ajabu ajabu."
aliamini Pastor na muda huo tayari gari zilisimama ndani ya parking ya mjengo ule na kushuka huku wakilakiwa na wanakwaya wachache waliokuwa wanasubiri pale sebureni ambao Asunta hakuungana nao awali na kuamua kukaa nnje kujiriwaza kwa kusoma kitabu ili kutuliza mawazo kabla hajaonana na Dullah pale getini.

* * * * *

Baada ya Dullah kumuona Asunta na kuuridhisha moyo wake ambao ulikuwa hauna amani awali baada ya kupoteza mawasiliano, siku hiyo alipokuwa uwanjani majira ya jioni ambapo kulikuwa na mechi ya kirafiki baina ya club ambayo alikuwa anafanyia mazoezi ya Tandale fc na club iliyopanda ligi kuu msimu huo ya Becker Sport.
Akiwa mwenye furaha sana Dullah wakati anapasha na wenzake huku moyo wake ukiamini lazima atamuoa Asu hasa kwa jinsi alivyopokelewa nae na kupigwa busu mwanana aliamini kuwa si yeye pekee aliyekuwa anaumia kumbe hata Asu nae alikuwa anampenda sana.

Furaha na uchangamfu aliokuwa nao Dullah ulijulikana na kila mtu hadi kocha na mashabiki wa Tandale walimpigia makofi na kumshangilia sana huku wakijua ana mzuka na furaha kutokana na kuanzishwa kwenye mechi ile zidi ya club ambayo ilikuwa inakuja juu kwa kasi ya umeme club ya Becker fc.
Lakini ukweli ulibaki kichwani mwake mwenyewe Dullah na mara baada ya refarii kupuliza kipyenga tu siku hiyo mpila ulipoanza Dullah alionesha kiwango cha hali ya juu tofauti na siku kadhaa zilizopita na kila alipogusa mpira shangwe zito na miluzi ilisikika huku wengi wa watu waliokuwa wanamtazama hawakuamini kabisa.
"Aaaagh! Ku*a**ake Rastaa Hafaiiiiii oyoooo Rasta ukitoka nione nina kete zako kumi na nanasi zima hapaaa....ndioo Muongezeee, agh! mtie kofii.. weee Rastaaa weeee.."
Ilikuwa ni sauti ya shabiki maarufu mkeleketwa wa Tandale fc bwana Chidy Ng'ole huku akiwa anazunguka pembeni ya uwanja na kuhamasisha mashabiki wenzake washangilie kwa nguvu huku akipagawishwa sana na vitu alivyokuwa anavifanya Dullah muda ule wa mchezo baada ya kumpiga tobo kiungo tegemeo wa club ya Becker fc na kuwatoka mabeki wengine wawili ambapo sasa alionekana Dullah akikimbiza mpila huku mbele kukiwa kumebaki beki mmoja na kipa tu.
Ni ufundi wa hali ya juu aliouonesha Dullah uwanjani mara baada ya kumdanganya beki kama anampiga chenga kisha akatoa pasi maridadi kwenye njia iliyokutwa vizuri na mshambuliaji mwenzake wa Tandale fc na kufunga kiulaini kabisa na kuongeza shangwe na vifijo uwanjani.
"Daah! huyu Rasta si ndio yule wa simba hadi nasikia John aliramba nyasi za tipi mara baada ya kutingishwa na kuanguka kama gunia?"
"Haswaa, ndie huyu si unaona vitu anavyofanya."
"Daah! ujue hazina kama hizi hadimu sana"
"tena sana bosi hatuhitaji kabisa kumuacha tandale mtu kama huyu atakuja kuharibu kiwango chake kwa kuendekeza bangi"
"kweli kabisa."
Yalikuwa ni mazungumzo ya meneja wa club ya Mtibwa suger ya Morogoro ambao walikuwa mabingwa watetezi wa ligi kuu msimu huo ulioisha pindi nao walipokuwa uwanjani pale wakiangalia ile mechi na kilichowavuta zaidi ni kutaka kumuona huyo mchezaji ambae habari zake zilivuma baada ya kuwafunga simba magoli mawili huku akimnyanyasa beki tegemeo wa simba na Taifa staz bwana John.

Hakuishia hapo Dullah alizidi kuonesha uwezo wake na mpaka kipyenga cha mwisho kinapulizwa matokeo yalikuwa tandale fc gori tatu ambapo mbili alifunga Dullah na moja alitengeneza yeye na kwa upande wa Becker fc walifunga magoli mawili hivyo Tandale waliibuka kifua mbele.
Sio siri siku hiyo Dullah alikuwa na furaha sana na kila gori alilofunga moyoni mwake alilituma kama zawadi kwa kipenzi chake Asu.
Siku hiyo pesa alizotunzwa na mahabiki baada ya mechi zilikuwa nyingi sana na walipoachana usiku mara baada ya kurudi nyumbani huku viongozi wa Tandale fc wakimuahidi kumpa mkataba na kumsajili moja kwa moja, alipofika ndani alitulia kitandani na kuanza kuzihesabu zile noyi alizokuwa nanzo ambazo alitunzwa kule uwanjani na alipomaliza kuzihesabu alitabasamu na kutoamini kuona ilikuwa ni laki mbili na sabini na tano elfu.
alichukua simu na kuwapigia nyumbani kijijini kwao huko muheza na kuzungumza na mamaake ambae alishawatumia simu siku chache za nyuma na kumuelezea kuwa amepata kazi na mpenzi wanaependana sana na anataraji kuja kumuoa huku akimuahidi mamaake kuwa siku moja atakwenda nae huko kijijini wamuone.
Mara baada ya Dullah kuongea na mamaake alielekea tena bafuni kuoga na aliporudi ndani alijibwaga kitandani kwa furaha na kulala.


* * * * * * *


Usiku huo Dullah alilala usingizi mzuri sana wenye ndoto tam tam za mafanikio kwenye mapenzi yake na Asunta.
Alifajiri na mapema kama kawaida yake Dullah alinyanyuka na kuvaa jezi zake na kuelekea mazoezini na kuanza kupasha viungo kama ilivyo desturi yake na ilipofika majira ya saa mbili kasoro alipokuwa anarudi getto alipoishi nyuma yake kulikuwa na watu wawili waliokuwa wanaenda kule alipokuwa anaenda na alipokatisha kutaka kuingia alipoishi ndipo wale watu walimwita na kujitambulisha kwake.
"Habari ndugu, naitwa Atanas mwenzangu anaitwa Rama sisi ni scout wa club ya mtibwa suger na ujio huu ulikuwa wako kabisa"
"sawa karibuni. Mi naitwa Dullah."
"Asante sana bwana Dullah sasa kuna bahasha yako hapa kaa tulia utaisoma nakuielewa kisha tutafanya mawasiliano."
aliongea yule bwana aliyejitambulisha jina la Atanasi na kumpatia Dullah mfuko mmoja wa khaki na kuaga kisha kuondoka ambapo Dullah alipokuwa ndani kwake baada ya kuufungua alishangaa kukuta bahasha mbili moja iliwa na barua kutoka kwenye club ya mtibwa na nyengine ilikuwa na viburungutu viwili vya pesa ambapo kabla hajasoma barua alihesabu kwanza pesa na kukuta kila kiburungutu kimoja kilichokuwa na noti za elfu tano tano kilikuwa na jumla ya kiasi cha shilingi laki tano na jumla ya viburungutu vile viwili ilikuwa ni milioni moja.
Alishusha pumzi na kuifungua ile barua na alipoanza kuisoma ilikuwa inamuelekeza atumie zile pesa kama nauli ya kwenda Manungu Morogoro wiki ileile kukutana na club ile ambayo waliridhishwa na kiwango chake na walipenda wajumuike nae.
ndani yake walimuhakikishia watamsainisha mkataba mnono na watampa nyumba ya kuishi huko Moro endapo tu atakubali kutia sahihi kwenye mkataba wa kujiunga nao Mtibwa sugar.
Chini kabisa alikuta kumeandikwa namba za simu na majina ya scout wale waliojitambulisha nje pamoja na anuani ya timu na meneja.
"hawa kweli wajinga, yaani mi niache kuwa jilani na mtu nimpendae nizidi kutengeneza maelewano zaidi eti niende huko polini afu nimpoteze jumla kizembe Asu wangu.. hahaha hii haitotokea."
alijisemea kimoyo moyo Dullah na kuchukua simu yake kisha kupiga zile namba na simu iliita ilipopokelewa tu alimuomba yule scout aje tena pale alipo waongee.
Na kweli kumbe wale mascout hawakuwa mbali kabisa muda mfupi tu walifika na kumgongea Dullah ambapo alipotoka na alichokuwa anaongea wote walimshangaa.
"Vipi kwani Rasta mbona unarudisha sasa hii bahasha."
"Jamani chukueni tu bahasha yenu kila kitu mlichoeka kipo vilevile kama hamuamini hakikisheni basi, ila ndio hivyo mimi nimeridhika na club niliyopo hata kama haichezi ligi kuu. sitoweza kwenda popote Ahsante."
"Aagh! lakini Rasta maisha haya ujue!! afu bahati hizi haziji mara mbili."
"Nimekuelekeza ndugu sihitaji bahati hiyo na isipokuja mara ya mbili ndo itakuwa vizuri kwangu kama hujui."
aliongea Dullah na kurudi ndani kisha kukomea mlango kabisa.
wale jamaa walibaki wanatazamana na yule mwengine aliamua kumgongea Dullah ambapo alipotoka tena alijaribu kumsihi lakini Dullah msimamo wake ulibaki pale pale na kufunga tena mlango.
Hawakumuelewa hata kidogo.
"atakuwa tayari kashakula nyama ya simba huyu ama karamba koni si bure tuondoke."
aliongea Rama na kumsihi mwenzake waondoke wakiamini huenda aliwakatalia baada ya kujiwa na watu wa club ya simba ama ile ya Azam.
lakini ukweli ulibaki pale pale ndani ya moyo wa Dullah alikataa kwenda Moro kujiunga na Mtibwa kwa hofu ya kumpoteza Asunta kwani hakuwa na mawasiliano nae zaidi ya pale anapoishi kuwa ndio nembo pekee Asu anaweza kuitumia kukutana nae na alishamuahidi hivyo kuwa angekuja.
Akiwa kwenye mawazo mazito pale kitandani huku akiuwazia ujasiri uliomkumba na kuzikataa zile hela ilihali alikuwa masikini na aliacha kazi kipindi hiko, mara mlango uligongwa tena na aliamua kunyamaza kwa kujua kuwa bado wale watu wanataka kumshawishi.
Alikereka zaidi baada ya mlango kuzidi kugongwa na kufungua kwa hasira.
"NIMESHAWAAMBIA SITA........AAAH ASUNTAAAAAAA"
alianza kufoka akiwa anafungua mlango lakini hakuamini alipotazama nje na kumuona aliyekuwa anagonga hakuwa mwengine bali kivuli cha moyo wake binti mrembo Asunta.
Alifurahi nusura moyo wake utoke nje ya kifua umkumbatie Asunta kumuonesha jinsi gani amefurahi.
"vipi D jamani mbona hivyo.?"
aliuliza Asu lakini D hajajibu chochote zaidi alimkumbatia kwa furaha Asu na kum beba juu juu.
"haaaa, jamani D utaniangusha mwenzioo!"
aliingia nae ndani na kumshusha huku akiwa bado haamini macho yake Dullah.
"Kwa kweli siamini hata kidogo kama nimuonaye mbele yangu ndie yule malaika wa poozo la moyo wangu daah! Asu baby hivi ni kweli ama naota?"
"Kweli D wala sio ndoto hata mimi nimefurahi kukukuta na nimejiiba mazoezini kwani leo ndio niliruhusiwa kwa mara ya kwanza kwenda mazoezini na nimemdanganya ticha kuwa sijisikii vizuri ili tu nije kwako kwa maongezi maalum."
"Yapi tena Asu mama."
"Ni hivi Dullah mi nakupenda sana tena sana ila kuna tatizo moja ambalo kama hutokuwa makini unaweza kunikosa D"
"Lipi hilo jamani Asu wangu?"
"Kuhusu dini Dullah, najua we muislam na mimi mkristo pia wazazi wangu wameshanionya kuwa hawatakuwa tayari niolewe na muislam kwa hiyo nakuomba D kama vipi niwaambie upo tayari kubadili dini ili iwe njia rahisi ya mimi na wewe kuoana na kuishi pamoja."
"Uuuphhhhhhh..." alishusha pumzi Dullah na kumuangalia usoni Asunta.
"Asu wangu, mi sidhani kama dini ndo tatizo la mimi na wewe kuwa pamoja ila ukweli kwamba sitoweza kubadili dini hata mara moja wala nawe sitokuja kukulazimisha ubadili dini mpaka nafsi yako mwenyewe itapotaka kwa hiyo sidhani wala siamini kama dini linaweza kuwa tatizo ila nahisi pesa ndo inaweza kuwa tatizo."
aliongea Dullah maneno ambayo yalimfanya Asu aanze kuuona ugumu wa moyo wa Dullah juu ya imani yake.
"Lakini D si unanipenda na unanihitaji."
"Haswaaaaa"
"sasa si ukubali tu"
"Nikubali? nikubali kubadili dini....hahaaa Asu hayo ni masuala tofauti kabisa na kukupenda hayo maswala ya imani naomba tuyaache mi sijakupendea dini yako mimi nimekupenda wewe kama wewe."
"sasa tutaoanaje?"
"Tutaoana tu Asu wenyewe wazazi watapohakikisha tunapendana watatukubalia tuu"
aliongea Dullah lakini Asu alionekana kutopendezwa na mawazo ya Dullah.
"sawa D sasa mi naondoka."
"Mh! Asu mbona mapema hivyo baby tulipoteana hatujazungumza zaidi juu kwa juu unaondoka?"
"hapana D saivi baba yupo natakiwa niwahi nyumbani kama nilivyoaga mazoezini"
"sawa baby twende nikupeleke"
alijibu Dullah na kunyanyuka kisha kwa pamoja walitoka mpaka barabarani ambapo safari hii Asu alikuja kwa gari yake mwenyewe na aliipaki pale stendi.


ITAENDELEA



PRINCE NAAHJUM ALSINA
0652691819
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom