nameless girl
JF-Expert Member
- Apr 22, 2012
- 4,195
- 2,685
MTAMBO WA MAUTI
BY: BEN R. MTOBWA
Si hilo tu, kirusi hicho, ambacho katika hali ya kawaida hakijihusishi na chembechembe nyekundu, hapa kilionekana kikizishambulia chembechembe hizo moja baada ya nyingine kwa kasi ya ajabu.
Chembechembe nyeupe kwa jina la kitaalamu T-Cells au CD4+, zina kazi maalumu ya kuhakiki kinga ya mwili na kurekebisha uharibifu wowote unaotokea. Chembechembe nyekundu ambazo, kwa kawaida, huishi siku 120 kabla ya kuharibiwa katika ini au wengu na nyingine kuchukua nafasi yake, kazi yake kubwa ni kusafirisha oksijeni mwilini. Inaaminika kuwa kiasi cha chembechembe 200,000,000 hutengenezwa na kuharibiwa kila siku. Kasi ya kirusi hiki katika kuteketeza chembechembe hizo na kuzaliana ilionyesha wazi kuwa binadamu aliyeambukizwa asingeishi zaidi ya siku tatu! Jambo ambalo liliwafanya madaktari hao bingwa watazamane kwa hofu na mshangao.
Uamuzi wa kufanya majaribio haya ulichukuliwa na uongozi wa hospitali hiyo baada ya mgonjwa wa kumi na moja, kati ya kumi na wawili walioletwa hospitalini hapo, kufa saa ishirini nan ne baadaye kama waliomtangulia. Wote walilalamika maumivu ya kichwa na homa kali. Walipopimwa damu zao zilionekana kuathiriwa na virusi vya UKIMWI, jambo ambalo si wao wala ndugu zao walioafikiana nalo. “Jana tu alikuwa mzima wa afya, leo niambiwe kuwa ana UKIMWI!” Mmoja wa ndugu wa wagonjwa hao alimaka.
Kitu kingine kilichowasukuma madaktari hao kufanya uchunguzi huo ni historia ya maradhi yao. Wote walionekana kuugua ghafla baada ya kula chakula cha aina moja katika tafrija ya arusi iliyofanyika mjini hapa. Walikuwa wamekula nyama ya kusaga ambayo baadaye waandaji wa tafrija hiyo walikana kuhusika nayo!
Awali, hospitali ilidhani kuwa wamekula sumu. Lakini vipimo vilionyesha tofauti. Vifo vyao vilitokana na shambulizi kubwa la virusi vya UKIMWI. Virusi vinavyoshambulia kwa kasi kubwa kuliko ile ya maradhi yote mengine ya mlipuko ikiwemo Ebola na hata kipindupindu.
“Mungu wangu!” Dakktari mmoja alilalamika. “Mnajua kwamba kirusi hiki kikiruhusiwa kuendelea kuishi mwaka mmoja tu baadaye nchi hii haitabakia na mtu au mnyama yeyote aliye hai?”
“Hilo liko wazi, hasa baada ya kuona kuwa kinaweza kuishi ndani ya vitu vingine kama maji na chembechembe za chakula badala ya damu pekee kama ilivyo ada!”
“Nakichukia kirusi hiki!” Daktari mwingine alisema kwa kufoka.
“Kwa hiyo, la kufanya ni lipi?”
Daktari aliyekuwa kimya muda mwingi akachangia, “Nadhani hatuna la kufanya kwa sasa, zaidi ya kupeleka sampuli hii Shirika la Afya Duniani, WHO, ili nao wathibitishe juu ya kitu hiki ambacho kimeingia katika soko la maradhi hatari.”
Waliafikiana naye.
Muda mfupi baadaye sampuli hiyo ilikuwa ndani ya kasha maalumu la DHL, ikielekea Jeneva, Uswizi.
Saa ishirini nan ne zilizofuata tayari Shirika la Afya lilirejesha majibu, likionyesha kushitushwa kwake na ‘ugonjwa huo mpya’ ambao haukuwemo katika kumbukumbu zao na ambao, ‘kwa vyovyote vile tiba yake itakuwa ngumu kutokana na kasi yake ya maambukizi.’
Madaktari bingwa waliitana tena kwa faragha na kulitafakari jibu la WHO.
“Kwa hiyo tufanye lipi?” mmoja wao aliuliza tena. “Tuitangazie nchi na dunia hii ili watu wajihadhari?”
Wenzake wawili watatu walimpinga harakaharaka. “Hilo hatuwezi kufanya. Litaleta hofu kubwa miongoni mwa wananchi,” mmoja wao alisema.
“Halafu, maadam hatujajua chanzo, tutakuwa hatujasaidia chochote.”
“Zaidi ya hayo, kazi yetu ni kutunza siri, sio kuzitoa.”
“Una maana hata Waziri wa Afya tusimwambie?” msemaji wa awali alihoji tena.
“Atatusaidia lipi kwa hili?” mwenzake alimhoji “Yeye ni mwanasiasa, si mtaalamu. Ataishia kupiga kelele majukwaani.”
Msemaji wa awali alikuwa hajaridhika, akasema, “Jamani, mnataka kuniambia tumfiche hata Rais wa Jamhuri ya Tanzania taarifa hizi?”
Kila mmoja alimtumbulia macho. Hakuna aliyemjibu.
NB: HII STORY UTAIMALIZIA UTAKAPOJIPATIA NAKALA YAKO. USIJE UKASEMA SIKUKWAMBIA.
BY: BEN R. MTOBWA
KIDOKEZO
Muhimbili, Dar es Salaama, Tanzania.
April 1, 2004
Madaktari bingwa sita, waliokubuhu katika taaluma ya tiba, waliduwaa mbele ya microscope wakishuhudia kitu ambacho hawakupata kukiona maishani mwao. Kwa muda wa dakika moja, kirusi kimoja tu cha UKIMWI kilichowekwa katika damu yenye ujazo wa milimita 3, kilikuwa tayari kimeteketeza chembechembe nyeupe 5,000 kati ya chembechembe zisizopungua 10,000 zilizokuwemo!Muhimbili, Dar es Salaama, Tanzania.
April 1, 2004
Si hilo tu, kirusi hicho, ambacho katika hali ya kawaida hakijihusishi na chembechembe nyekundu, hapa kilionekana kikizishambulia chembechembe hizo moja baada ya nyingine kwa kasi ya ajabu.
Chembechembe nyeupe kwa jina la kitaalamu T-Cells au CD4+, zina kazi maalumu ya kuhakiki kinga ya mwili na kurekebisha uharibifu wowote unaotokea. Chembechembe nyekundu ambazo, kwa kawaida, huishi siku 120 kabla ya kuharibiwa katika ini au wengu na nyingine kuchukua nafasi yake, kazi yake kubwa ni kusafirisha oksijeni mwilini. Inaaminika kuwa kiasi cha chembechembe 200,000,000 hutengenezwa na kuharibiwa kila siku. Kasi ya kirusi hiki katika kuteketeza chembechembe hizo na kuzaliana ilionyesha wazi kuwa binadamu aliyeambukizwa asingeishi zaidi ya siku tatu! Jambo ambalo liliwafanya madaktari hao bingwa watazamane kwa hofu na mshangao.
Uamuzi wa kufanya majaribio haya ulichukuliwa na uongozi wa hospitali hiyo baada ya mgonjwa wa kumi na moja, kati ya kumi na wawili walioletwa hospitalini hapo, kufa saa ishirini nan ne baadaye kama waliomtangulia. Wote walilalamika maumivu ya kichwa na homa kali. Walipopimwa damu zao zilionekana kuathiriwa na virusi vya UKIMWI, jambo ambalo si wao wala ndugu zao walioafikiana nalo. “Jana tu alikuwa mzima wa afya, leo niambiwe kuwa ana UKIMWI!” Mmoja wa ndugu wa wagonjwa hao alimaka.
Kitu kingine kilichowasukuma madaktari hao kufanya uchunguzi huo ni historia ya maradhi yao. Wote walionekana kuugua ghafla baada ya kula chakula cha aina moja katika tafrija ya arusi iliyofanyika mjini hapa. Walikuwa wamekula nyama ya kusaga ambayo baadaye waandaji wa tafrija hiyo walikana kuhusika nayo!
Awali, hospitali ilidhani kuwa wamekula sumu. Lakini vipimo vilionyesha tofauti. Vifo vyao vilitokana na shambulizi kubwa la virusi vya UKIMWI. Virusi vinavyoshambulia kwa kasi kubwa kuliko ile ya maradhi yote mengine ya mlipuko ikiwemo Ebola na hata kipindupindu.
“Mungu wangu!” Dakktari mmoja alilalamika. “Mnajua kwamba kirusi hiki kikiruhusiwa kuendelea kuishi mwaka mmoja tu baadaye nchi hii haitabakia na mtu au mnyama yeyote aliye hai?”
“Hilo liko wazi, hasa baada ya kuona kuwa kinaweza kuishi ndani ya vitu vingine kama maji na chembechembe za chakula badala ya damu pekee kama ilivyo ada!”
“Nakichukia kirusi hiki!” Daktari mwingine alisema kwa kufoka.
“Kwa hiyo, la kufanya ni lipi?”
Daktari aliyekuwa kimya muda mwingi akachangia, “Nadhani hatuna la kufanya kwa sasa, zaidi ya kupeleka sampuli hii Shirika la Afya Duniani, WHO, ili nao wathibitishe juu ya kitu hiki ambacho kimeingia katika soko la maradhi hatari.”
Waliafikiana naye.
Muda mfupi baadaye sampuli hiyo ilikuwa ndani ya kasha maalumu la DHL, ikielekea Jeneva, Uswizi.
Saa ishirini nan ne zilizofuata tayari Shirika la Afya lilirejesha majibu, likionyesha kushitushwa kwake na ‘ugonjwa huo mpya’ ambao haukuwemo katika kumbukumbu zao na ambao, ‘kwa vyovyote vile tiba yake itakuwa ngumu kutokana na kasi yake ya maambukizi.’
Madaktari bingwa waliitana tena kwa faragha na kulitafakari jibu la WHO.
“Kwa hiyo tufanye lipi?” mmoja wao aliuliza tena. “Tuitangazie nchi na dunia hii ili watu wajihadhari?”
Wenzake wawili watatu walimpinga harakaharaka. “Hilo hatuwezi kufanya. Litaleta hofu kubwa miongoni mwa wananchi,” mmoja wao alisema.
“Halafu, maadam hatujajua chanzo, tutakuwa hatujasaidia chochote.”
“Zaidi ya hayo, kazi yetu ni kutunza siri, sio kuzitoa.”
“Una maana hata Waziri wa Afya tusimwambie?” msemaji wa awali alihoji tena.
“Atatusaidia lipi kwa hili?” mwenzake alimhoji “Yeye ni mwanasiasa, si mtaalamu. Ataishia kupiga kelele majukwaani.”
Msemaji wa awali alikuwa hajaridhika, akasema, “Jamani, mnataka kuniambia tumfiche hata Rais wa Jamhuri ya Tanzania taarifa hizi?”
Kila mmoja alimtumbulia macho. Hakuna aliyemjibu.
NB: HII STORY UTAIMALIZIA UTAKAPOJIPATIA NAKALA YAKO. USIJE UKASEMA SIKUKWAMBIA.