Hadithi: Mpangaji

"MPANGAJI 01
Hakuna mpangaji yoyote ambaye alikuwa anafahamu asili ya Yule mpangaji mwenzao, hata jina lake la ‘sele’ wapo waliosema halikua jina lake halisi, lakini yote kwa yote Sele kama unavyoweza kusema alikua mpangaji wa kudumu wa mzee Mhina, miaka ilikatika na sio mzee Mhina wala wapangaji ama watoto wake walijua kazi halisi ya Sele,
Wapo waliosema sele alijihusisha na kazi ya kuzibua vyoo huko mjini mbali na hapo, wengine walisema sele Alikuwa mtu wa ‘kitengo” na kama ilivyo kawaida ya wabongo basi wengine walizua kuwa sele ni jahili mzoefu,
Kwanza Sele asingetoka nje ya chumba chake bila kuitwa, na kwakuwa chumba chake kilikua ni selfu basi huwezi kujua kama sele yupo ndani au ametoka,"


Nimekumbuka Mwanzo wa story ya Bigi ya Steve.....


Naweka kambi rasmi hapaa!!

Wapii Tayukwa Lovelovie Bantu Lady Kalpana baby zu Kigi Makasi Tyrone Kaijage mmash Restless Hustler Unforgettable Mafian cartel mtzmweusi mshaisoma hii storee???
Tumeshawasili dyadya...
 
MPANGAJI 03

Sele hakukaa hata kidogo aliondoka zake mara tu baada ya kumuacha Ester pale kwao,
Sasa Ester alizunguukwa na wapangaji wote waliokuwepo wakitaka awaeleze kuhusu Sele,
“hivi anaongea kabisa, halafu anacheka?” aisha alidakia
“jamani Sele ni mwanaume mzuri tu kama walivyo wanaume wote, yaani sijui nisemeje ni binadamu kabisa!” alisema ester sasa alishachoka kufanya mahojiano ambayo kwa uono wake yeye haukuwa na kichwa wala miguu,
“haya tuambie mlikula nini, kawhiyo Sele pia anakula kabisa!” aliuliza mama Mwajuma!
“hahahaha jamani mama, eti anakula, kwahiyo bado mnaamini Sele ni Zimwi, sijui jini huko..” alisema ester akiingia ndani
“na mizigo yote hii mwanangu umemaliza mshahara wako huko!” alisema mama mwajuma
“hapo vitu vingi kaninunulia Sele” alisema Ester sasa akiangalia hotpot lilipo ili achukue chakula
“mh makubwa haya jamani!”alisema mama Mwajuma sasa akimtafutia maji ya kunawa mwanae

Ndani ya muda mfupi Sele alizoeana kabisa na Ester na sasa unaweza kuwakuta wamekaa nyuma ya nyumba usiku wakipiga soga huku wakicheka kabisa, hata hivyo Sele alikataa kata kata kumueleza chochote kuhusu maisha yake pamoja na Ester kujinasibu kumuelezea hadithi zake za mahusiano yaliyopita na maisha ya shule kwa ujumla , Sele hakuthubutu kumueleza chochote,
Na sasa waliweza kubadilishana namba za simu na siku nyingine wangechati mpaka usiku wa manane,
Baada ya sikukuu ya Pasaka sasa Ester alipaswa kuondoka kurudi kazini kwake lindi , Tayari mkuu wake wa shule alishampigia kumkumbusha umuhimu wa kurejea mapema,
Hivyo siku hiyo Ester alitumia muda wake kwenda kariakoo kununua vitu baadhi alivyodhani vingemfaa , aliwaza na kuwazua akaona atafute zawadi ndogo kwa ajili ya Sele na hivyo akaingia duka moja la kuuza simu na kununua simu janja aina ya Tecno F2.

“bila shaka Sele atafurahi kuwa na simu hii janja, na nitakuwa namtumia picha zangu nay eye ananitumia zake nikiwa Lindi” aliwaza Ester.
Alirudi nyumbani na kuandaa mizigo yake tayari kwa safari kesho yake, baada ya kumaliza alitoka nje kwenda kumsubiri rafiki yake Sele ambaye alifika kwa wakati kabisa,
“yaani umejuaje kunisubiri hapa!” alisema Sele akiwa na bashasha kweli kweli,
“ah yaani acha tu wewe mwanaume una kismati maana hata sijui kwanini nimekuzoea hivi” alisema Ester bila kujielewa
“nisubiri basi hapa nikaweke mizigo then nitakukuta hapa nje!” alisema Sele akiingia ndani
“mh yaani mpaka naondoka sijaingia chumbani kwako Kaka sele Jamani!” alisema Ester akipiga hatua kumfuata Sele,
“HAPANAA!!” alifoka Sele , mpaka mwenyewe akashangaa na kurudi nyuma kwa ester kuomba radhi,
“nisamehe Ester, kwakweli hakuna mtu ataingia chumbani kwangu , nasikitika nimekufokea nisubiri tu nakuja” alisema Sele akiingia ndani haraka
“nitaingia hiki chumba Sele, kama sio leo basi kesho!” alijisemea Ester akimsubiri Sele atoke
Sele alitoka baada ya dakika chache tu kisha wakasogea kwenye msingi wa nyumba ambao ulikua haujaisha na kukaa kupiga Story,
“yeah kama nilivyokuambia kesho nasepa Sele nitakumisi sana!” alisema Ester kwa uchungu kidogo
“yeah, ndio hivyo kazi ni muhimu sana Ester inabidi uende mimi mwenyewe nitakumisi ujue, wengine wananitenga mara waniite zimwi, siijui jinni.. hahahaha!” alisema sele akimalizia na kicheko
“hahaha yaani nakuambia kabla hatujaonana nilikua naambiwa sana habari zako , ila kumbe mtu mwenyewe wala hata hauko hivyo,” alisema Ester akilala kwenye mabega ya Sele
“hahaha mawazo yao tu, sema unajua maisha ya Dar kila mtu na hamsini zake kwahiyo nadhani watu wako bize sana kutafuta riziki ndio maana wananifikiria vibaya!” alisema Sele
“kaka Sele nimekuletea Zawadi hii” alisema akitoa ile simu kwenye box lake na kumkabidhi Sele,

“loh asante sana Ester kwa smartphone hii” alisema Sele akiichukua
“ooh asante kwa kushukuru, ndio sasa nikiwa Lindi nitakuwa nakupigia video call, nakutumia picha na video zangu Sele!” alisema Ester kwa furaha
“sikiliza ester mimi situmii mtandao wowote wa kijamii” alisema Sele kwa upole huku mkono mmoja akiwa ameuweka begani kwa Ester
“sele unasema kweli?” Ester alihamaki akimtazama Sele machoni hakuamini kabisa maneno haya yanatoka kwa kijana mwenye umri wa miaka 30-33 hivi
“yaani hutumii facebook, insta, whatsapp?” aliuliza Ester na Sele aliatingisha kichwa tu kuashiria anakubaliana nae..
“basi ni kweli kuna tatizo Sele!” alisema Ester sasa akitoa kitambaa chake kwenye suruali aliyokua amevaa akifuta machozi na kisha akasimama na kuondoka kurudi ndani
“rudi ester” Sele alijaribu kumuita lakini tayari Esta alishawahi kulifikia geti kurudi ndani
“nilijua tu atachemka, mimi ni Zimwi kweli!” alijisemea Sele akipiga ngumi kwenye mchanga kwa hasira alijisikia vibaya sana kuagana na esta katika hali ile esta alirudi ndani na kukimbilia Chumbani kwake alijikuta akilia bila sababu mpaka yeye mwenyewe akawa anajishangaa
“Triiiiia” simu yake ilitingishika kuashiria ujumbe mfupi uliingia
Aliufungua na kusoma ulitoka kwa sele
“NINA ZAWADI YAKO PIA TAFADHALI UJE UICHUKUE”
Esta aliwaza kama aende ama abaki lakini baadae alijiona mpumbavu kulia mbele ya mtu ambaye hata hakuwa na mahusiano yoyote
Alijikaza kisabuni na kutoka nje na kumkuta sele akiwa ameshikilia begi dogo hivi la wastani
“hii zawadi yako Esta” alisema akimkabidhi kisha akageuka kurudi chumbani kwake!
“na hili begi, mbona kama kuna uzito humu?” aliuliza esta,
“bhana ni zawadi yako vyote pamoja na begi” alisema Sele akitabasamu kisha akaendelea na hatua zake kadhaa kuingia kwake,
Esta bado alikua na shauku ya kujua ndani ya begi kulikua na nini, hivyo aliangalia huko na huko kuhakikisha hakuna mtu pale nje kisha akaingia ndani na kufungua lile begi..
Ndani kulikua na komputa mpakato mpya kabisa aina ya apple ikiwa katika makaratasi yake
“whaaat” Esta aliweka ile komputa kitandani huku akiwa haamini, hakujua kama afurahi ama la, haraka alichukua Simu yake ana kuingia mtandaoni na kwenda kwenye google kisha akatafuta “apple sx400 min series price” bila hiyana google wakamletea $1,100 , alijaribu kubadili pesa hizo na kuweka kwenye pesa ya Tanzania na kukuta ni zaidi ya million mbili!
“yaani huyu Sele ananinulia mimi zawadi ya million mbili?, sele huyu katika nyumba ya kupanga ya kawaida tu?” Sasa akili yake ilimwambia huyu “sele” sio mtu wa kawaida kama alivyokuwa anamchukulia,
Aliwaza na kuwazua kisha akaona ngoja acheze huu mchezo
Alichuchukua simu yake na kuandika ujumbe mfupi kwa sele
“asante sana kwa zawadi dear ila nina ombi moja”
Kisha akutuma kwa sele , baada ya muda mfupi yake simu yake ilitoa ishara kuwa ujumbe ule umepokelewa na hivyo akasubiri jibu
“yap karibu” sele alijibu
“naomba sana kesho unisindikize hadi ubungo tafadhali sana, naomba sana kesho usiende kabisa kazini” aliutuma ujumbe huo kwa sele
“Esta nilishapanga hilo nisingekuacha uende mwenyewe best” alijibu sele kisha wakaagana
Kila mmoja aliwaza kuhusu mwenzake
Badala ya furaha Sele alijikuta machozi yakimtoka, alienda kwenye sanduku lake ambalo alikuwa ameliweka kwenye kabati ya nguo,
Alitoa bahasha kadhaa kisha akatoa picha mbili aliziangalia muda mrefu huku machozi yakimtoka
‘nipe Baraka zako , nipe Baraka zako!” alisema huku machozi yakimtoka akiwa ameshikilia zile picha,
Sele sasa hakuweza kutazama zile picha zaidi alizirudisha na na kisha akaenda bafuni alifungulia maji tu yakimwagikia mwilini na mwishowe akagundua kuwa alikuwa hajavua nguo zake kumbe


Mambo yanazidi kunoga lol!!

Ester na Sele on the line 1 and 2!!

Ngoja tuone 🙇
 
"‘wewe ni mzee Lota, una watoto wanne , watatu wa kike na mdogo wa mwisho wa kiume, Yule ni Aisha na mumewe Mkude, Yule ni mama Mama Mwajuma na mume wake Ngoda, pale ni Isa , kule ni John na hapa ni kaka Ephraim na mke wake mama Joan’"


Sele nyookkoo

Pozi lazima ziliwaisha hapa

Aaliyyah kuna story ya Sele hukuu!!
Kati ya sehemu zilizonifurahisha sana kwenye hadithi ni hapa....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom