mizambwa
JF-Expert Member
- Oct 8, 2008
- 4,421
- 1,792
- Thread starter
- #41
HADITHI: KIVULI CHEUSI
SEHEMU YA KUMI
TULIPOISHIA.............
Alijua sasa kilichobaki ni mke wa Raymond. Mwanamke aliyesababisha kifo cha mama yake, Bi furahiya.
"Lazima nimuanze yeye ili huyu mshenzi ajue nipo siriazi"
Moses hakufahamu kuwa hakumaliza kufuta kumbukumbu ya taswira yake ya uzee katika kichwa cha Mfaume.
Akacheka sana kwa furaha alipokuwa akitazama taarifa ya habari akiwa ndani ya bar yenye mazingira machafu katika guest aliyolala huko kigogo mburahati.
Taarifa iliyokuwa ikitangaza tukio la kuuwawa kwa kwa muhudumu wa nyumba ya kulala wageni na muuwaji akihusishwa katika matukio ya mauaji ya wasichana wawili.
ENDELEA...............
Majira ya saa 3:15 asubuhi, ndipo Andrew kiongozi wa wahudumu wa apartment aliyoichukua Moses akakosa uvumilivu. Ilipita siku moja bila mtu yeyote kufungua mlango.
"si mwanamke wake wala yeye mwenyewe" alikuwa Baraka, msaidizi wa Andrew.
"kitu cha ajabu na kushangaza zaidi, kuna harufu kali inatokea chumbani"
Haikuwa kawaida kwa Andrew kupoteza uvumilivu haraka kiasi hicho. Lakini kengele ya hatari ikagonga kichwani mwake. Kengele ya kuhisi kumetokea jambo ambalo si la kawaida. Akavunja masharti ya kazi yake.
Kazi yake haikumruhusu kuingia ndani ya nyumba endapo kuna wateja. Labda kwa ruhusa maalumu au baada ya kutoka na kwenda kufanya usafi. Harufu kali ya uvundo, ikampa wasiwasi kila mfanyakazi wa apartment hiyo.
Andrew alichukua ufunguo wa ziada, akatekenya kitasa nacho kikalegea. Harufu ikawapokea kwa kero na hali ya kutofahamu kitu gani kimetokea ndani ya nyumba hiyo. Andrew akifuatiwa na Baraka walienda moja kwa moja mpaka chumbani. Harufu ikawa nzito hata ikawafanya wazibe pua zao. Wakaingia ndani ya chumba hicho, taswira ya dimbwi dogo la damu lililoanza kukauka likataka kumkimbiza Baraka. Kutokana na kukosa uvumilivu, Baraka akaita Mama kwa sauti ya juu kama vile hakuimeza miaka thelathini na nne duniani. Kiwiliwili kilichogawanyishwa mikono na miguu yake iliyowekwa pembeni kikawaadhibu Andrew na Baraka kwa uoga. Jasho jingi likawatoka hakuna aliyemuongelesha mwenzake.
"kichwa kiko wapi?"
likawa swali la kwanza kwa Andrew tangu wafike katika chumba hicho. Baraka akaona michirizi ya damu iliyoelekea moja kwa moja mpaka kwenye friji ndogo ya chumba hicho. Yeye mwenyewe akalifungua alichokutana nacho, kikamfanya apoteze fahamu.
Dakika chache baadaye Andrew ndiye aliwaita mapolisi baada ya kumtafuta kwa muda mrefu mmiliki wa apartment hiyo McCuthbert bila mafanikio. Simu zake zote ziliita bila kupokelewa. Polisi walikuja huku Inspekta Jafari Hiza akiwemo.
Yakawa mauaji mengine ya kushitua zaidi. Tena huenda haya yalikuwa makubwa kuliko yaliyopita. Akampa taarifa rafiki yake wa karibu Vannesa. Kwa kuwa waandishi wengi walikuwepo, basi Vannesa akaendesha gari, hakika ulikuwa ni mwendo wa mwendawazimu. Dakika kumi tu zikamfikisha hapo.
Wengi walimfahamu Vannesa na walizoea kumuona kwenye matukio makubwa, haswa kama hayo. Akaondokea kuwa mwandishi aliyejulikana na askari wengi kwa kazi ya uandishi bila kufahamu kuwa kulikuwa kuna kazi kubwa zaidi ya hiyo. Wakampa njia alipotaka kupita naUshirikiano alipouhitaji.
Akaelekea moja kwa moja kwenye chumba kilichofanyika mauaji. inspekta Jafari Hiza akamkabidhi picha ya kivuli cheusi iliyokutwa ndani ya friji pamoja na kichwa
"Unasema huyu nae amekatwa kichwa?"
Vannesa alihamaki kwa mshangao wa hasira. Haikuwa kawaida kwa Vannesa kuwa katika hali hiyo. Ni nani ambaye hamjui Vannesa anayependa kucheka hata kwenye misiba? Basi leo Jafari Hiza alimshangaa.
"Naomba kukiona kichwa cha huyo msichana"
Akaletewa kichwa cha Eva. Sura ya Eva haikumpotea hata kidogo. Alikumbuka vyema alivyokuwa akimuhoji katika tukio lile la Bertha kijitonyama. Damu yake ikaanza kuchemka. Ilichemka kwa kuwa alifahamu kuwa muuaji anajua anachokifanya. Akaanza kuingiwa na hisia muuaji huyu labda si mtanzania kamili.
Mtanzania aliyezaliwa Tanzania hawezi kuwa na akili za kuua kiakili kiasi hicho.
Ushahidi wa kwanza ukawa umefutika bila kupata chochote cha maana kutoka kwake. Akamwambia Jafari
"namfahamu huyu msichana aliyeuawa"
"unamfahamu?"
Inspekta hakufahamu kabisa kama huyo ni Eva. Jafari Hiza amekuwa msahulifu katika mambo mengi sana, ndio maana akauliza tena
"ina maana tunaweza kumpata muuaji?"
"kifo chake kinazidi kutupa ugumu wa kumpata muuaji"
Vannesa akaondoka akiwa amechanganyikiwa. Kifo cha Eva kikazidi kumchanganya na kumfanya amchukie zaidi muuaji huyo. Akaelekea bar fulani aliyoipenda huko maeneo ya kinondoni. Alichoamini bila kuushitua ubongo wake kwa kinywaji kikali, basi asingekuwa sawa wala kupata chochote katika tafakuri zake.
Akaingia ndani ya bar hiyo maarufu kwa watu maarufu na kama hukuwa nazo, basi usingeweza kumudu gharama za bar hiyo. Hivyo kwa sababu hiyo, ikafanya bar hiyo ya caribean kuwa na wateja wachache waliopata huduma za hadhi yao. Vannesa akajipachika pembezoni mwa ukuta huku akitazama orodha ya vinywaji
XXXXX
Baada ya kufanya mauaji ndani ya apartment ile, Moses alitoka na kuelekea upanga siku iliyofuata mara baada ya kutoka katika guest aliyopanga kama amekurupushwa. Huko alienda moja kwa moja kwenye nyumba aliyoishi McCuthbert. Mholanzi aliyemiliki apartment nyingi hapa mjini. Moses alifahamu fika endapo askari watakuja kumuhoji McCuthebert, basi angeharibu mipango yake. Mipango ya kulipiza kisasi kwa kumtaja kuhusika na mauaji hayo ndani ya apartment yake.
Hakutaka hilo litokee.
Ndio maana akausaliti urafiki walio nao kwa muda mrefu na kumpokonya uhai wake kwa sumu kali ya nyongo ya mamba. Alitokomea huku akiwa amebadilisha muonekano alioingia nao ndani ya ofisi ya bosi huyo wa kiholanzi.
Alitafakari mengi juu ya Raymond kutokana na bugudha ya kelele kusumbua tafakuri zake, sehemu sahihi aliyoamua kwenda ikawa ni kinondoni katika bar ya Caribean. Aliupenda utulivu wa eneo lile pamoja na huduma zake. Alipofika huko akachagua sehemu pweke ambayo angekaa peke yake huku akitafakari jinsi ya kumuangamiza Raymond.
Muhudumu akaifuata orodha ya vinywaji, huku akiwa amechagua mvinyo kutoka dodoma (dompo) leo hakuhitaji kabisa kulewa. Kabla hajafanya chochote wala ajamimina funda lolote kinywani mwake. Alihisi kusimamiwa mbele yake. Alipouinua uso wake kumtazama mtu huyo hakuwa mwingine zaidi ya Vannesa....
XXXXX
ITAENDELEA!!!
SEHEMU YA KUMI
TULIPOISHIA.............
Alijua sasa kilichobaki ni mke wa Raymond. Mwanamke aliyesababisha kifo cha mama yake, Bi furahiya.
"Lazima nimuanze yeye ili huyu mshenzi ajue nipo siriazi"
Moses hakufahamu kuwa hakumaliza kufuta kumbukumbu ya taswira yake ya uzee katika kichwa cha Mfaume.
Akacheka sana kwa furaha alipokuwa akitazama taarifa ya habari akiwa ndani ya bar yenye mazingira machafu katika guest aliyolala huko kigogo mburahati.
Taarifa iliyokuwa ikitangaza tukio la kuuwawa kwa kwa muhudumu wa nyumba ya kulala wageni na muuwaji akihusishwa katika matukio ya mauaji ya wasichana wawili.
ENDELEA...............
Majira ya saa 3:15 asubuhi, ndipo Andrew kiongozi wa wahudumu wa apartment aliyoichukua Moses akakosa uvumilivu. Ilipita siku moja bila mtu yeyote kufungua mlango.
"si mwanamke wake wala yeye mwenyewe" alikuwa Baraka, msaidizi wa Andrew.
"kitu cha ajabu na kushangaza zaidi, kuna harufu kali inatokea chumbani"
Haikuwa kawaida kwa Andrew kupoteza uvumilivu haraka kiasi hicho. Lakini kengele ya hatari ikagonga kichwani mwake. Kengele ya kuhisi kumetokea jambo ambalo si la kawaida. Akavunja masharti ya kazi yake.
Kazi yake haikumruhusu kuingia ndani ya nyumba endapo kuna wateja. Labda kwa ruhusa maalumu au baada ya kutoka na kwenda kufanya usafi. Harufu kali ya uvundo, ikampa wasiwasi kila mfanyakazi wa apartment hiyo.
Andrew alichukua ufunguo wa ziada, akatekenya kitasa nacho kikalegea. Harufu ikawapokea kwa kero na hali ya kutofahamu kitu gani kimetokea ndani ya nyumba hiyo. Andrew akifuatiwa na Baraka walienda moja kwa moja mpaka chumbani. Harufu ikawa nzito hata ikawafanya wazibe pua zao. Wakaingia ndani ya chumba hicho, taswira ya dimbwi dogo la damu lililoanza kukauka likataka kumkimbiza Baraka. Kutokana na kukosa uvumilivu, Baraka akaita Mama kwa sauti ya juu kama vile hakuimeza miaka thelathini na nne duniani. Kiwiliwili kilichogawanyishwa mikono na miguu yake iliyowekwa pembeni kikawaadhibu Andrew na Baraka kwa uoga. Jasho jingi likawatoka hakuna aliyemuongelesha mwenzake.
"kichwa kiko wapi?"
likawa swali la kwanza kwa Andrew tangu wafike katika chumba hicho. Baraka akaona michirizi ya damu iliyoelekea moja kwa moja mpaka kwenye friji ndogo ya chumba hicho. Yeye mwenyewe akalifungua alichokutana nacho, kikamfanya apoteze fahamu.
Dakika chache baadaye Andrew ndiye aliwaita mapolisi baada ya kumtafuta kwa muda mrefu mmiliki wa apartment hiyo McCuthbert bila mafanikio. Simu zake zote ziliita bila kupokelewa. Polisi walikuja huku Inspekta Jafari Hiza akiwemo.
Yakawa mauaji mengine ya kushitua zaidi. Tena huenda haya yalikuwa makubwa kuliko yaliyopita. Akampa taarifa rafiki yake wa karibu Vannesa. Kwa kuwa waandishi wengi walikuwepo, basi Vannesa akaendesha gari, hakika ulikuwa ni mwendo wa mwendawazimu. Dakika kumi tu zikamfikisha hapo.
Wengi walimfahamu Vannesa na walizoea kumuona kwenye matukio makubwa, haswa kama hayo. Akaondokea kuwa mwandishi aliyejulikana na askari wengi kwa kazi ya uandishi bila kufahamu kuwa kulikuwa kuna kazi kubwa zaidi ya hiyo. Wakampa njia alipotaka kupita naUshirikiano alipouhitaji.
Akaelekea moja kwa moja kwenye chumba kilichofanyika mauaji. inspekta Jafari Hiza akamkabidhi picha ya kivuli cheusi iliyokutwa ndani ya friji pamoja na kichwa
"Unasema huyu nae amekatwa kichwa?"
Vannesa alihamaki kwa mshangao wa hasira. Haikuwa kawaida kwa Vannesa kuwa katika hali hiyo. Ni nani ambaye hamjui Vannesa anayependa kucheka hata kwenye misiba? Basi leo Jafari Hiza alimshangaa.
"Naomba kukiona kichwa cha huyo msichana"
Akaletewa kichwa cha Eva. Sura ya Eva haikumpotea hata kidogo. Alikumbuka vyema alivyokuwa akimuhoji katika tukio lile la Bertha kijitonyama. Damu yake ikaanza kuchemka. Ilichemka kwa kuwa alifahamu kuwa muuaji anajua anachokifanya. Akaanza kuingiwa na hisia muuaji huyu labda si mtanzania kamili.
Mtanzania aliyezaliwa Tanzania hawezi kuwa na akili za kuua kiakili kiasi hicho.
Ushahidi wa kwanza ukawa umefutika bila kupata chochote cha maana kutoka kwake. Akamwambia Jafari
"namfahamu huyu msichana aliyeuawa"
"unamfahamu?"
Inspekta hakufahamu kabisa kama huyo ni Eva. Jafari Hiza amekuwa msahulifu katika mambo mengi sana, ndio maana akauliza tena
"ina maana tunaweza kumpata muuaji?"
"kifo chake kinazidi kutupa ugumu wa kumpata muuaji"
Vannesa akaondoka akiwa amechanganyikiwa. Kifo cha Eva kikazidi kumchanganya na kumfanya amchukie zaidi muuaji huyo. Akaelekea bar fulani aliyoipenda huko maeneo ya kinondoni. Alichoamini bila kuushitua ubongo wake kwa kinywaji kikali, basi asingekuwa sawa wala kupata chochote katika tafakuri zake.
Akaingia ndani ya bar hiyo maarufu kwa watu maarufu na kama hukuwa nazo, basi usingeweza kumudu gharama za bar hiyo. Hivyo kwa sababu hiyo, ikafanya bar hiyo ya caribean kuwa na wateja wachache waliopata huduma za hadhi yao. Vannesa akajipachika pembezoni mwa ukuta huku akitazama orodha ya vinywaji
XXXXX
Baada ya kufanya mauaji ndani ya apartment ile, Moses alitoka na kuelekea upanga siku iliyofuata mara baada ya kutoka katika guest aliyopanga kama amekurupushwa. Huko alienda moja kwa moja kwenye nyumba aliyoishi McCuthbert. Mholanzi aliyemiliki apartment nyingi hapa mjini. Moses alifahamu fika endapo askari watakuja kumuhoji McCuthebert, basi angeharibu mipango yake. Mipango ya kulipiza kisasi kwa kumtaja kuhusika na mauaji hayo ndani ya apartment yake.
Hakutaka hilo litokee.
Ndio maana akausaliti urafiki walio nao kwa muda mrefu na kumpokonya uhai wake kwa sumu kali ya nyongo ya mamba. Alitokomea huku akiwa amebadilisha muonekano alioingia nao ndani ya ofisi ya bosi huyo wa kiholanzi.
Alitafakari mengi juu ya Raymond kutokana na bugudha ya kelele kusumbua tafakuri zake, sehemu sahihi aliyoamua kwenda ikawa ni kinondoni katika bar ya Caribean. Aliupenda utulivu wa eneo lile pamoja na huduma zake. Alipofika huko akachagua sehemu pweke ambayo angekaa peke yake huku akitafakari jinsi ya kumuangamiza Raymond.
Muhudumu akaifuata orodha ya vinywaji, huku akiwa amechagua mvinyo kutoka dodoma (dompo) leo hakuhitaji kabisa kulewa. Kabla hajafanya chochote wala ajamimina funda lolote kinywani mwake. Alihisi kusimamiwa mbele yake. Alipouinua uso wake kumtazama mtu huyo hakuwa mwingine zaidi ya Vannesa....
XXXXX
ITAENDELEA!!!