SEHEMU YA MWISHO
Akatembea kwa kasi hadi alipokifikia kituo cha
mafuta cha BP.
Habari yako dada.
Nzuri nikusaidie nini?
Naweza kumpata Samson Masanja.
Mh. Wiki ya pili sasa Samson kalazwa katika
Hospitali ya Amana.
Unaweza kunielekeza chumba alicholazwa?
Ukiingia pale Receiption uliza VIP wakikuelekeza
nenda chumba namba 9 ndiko alikolazwa.
Akaondoka huku akimshukuru yule dada.
* * *
DUKA LA VIFAA VYA HOSPITALI. Maandishi hayo
yalimvutia Vero ambaye moja kwa moja aliingia
mle dukani.
Hili shilingi ngapi? Aliuliza huku akishika koti
jeupe la hospitali.
Elfu kumi na tano. Alijibu yule muuzaji huku
akilitoa lile koti kwa mti maalum.
Nipatie hilo. Alisikika huku akitoa kiasi
alichoambiwa.
Akaliweka kwenye mfuko wake kisha akaondoka.
Baada ya nusu saa alikuwa maeneo ya Ilala.
Akaingia moja kwa moja pale hospitali. Akatembea
moja kwa moja hadi mapokezi.
Habari dada.
Salama nikusaidie nini?
Naomba unielekeze VIP.
VIP ni huku (huku akinyoosha kidole) lakini kwa
sasa huruhusiwi kwa sababu huu si muda wa
kuona wagonjwa. Alijibu yule dada wa mapokezi
ambaye kabla ya kufika Vero alikuwa anasinzia
pale dirishani.
Vero akaondoka pale dirishani na kuelekea upande
alioelekezwa. Bila kujali onyo alilopewa. Yule dada
wa mapokezi hakumwangalia Vero wakati anaingia
kule viliko vyumba vya VIP. Hakuingia moja kwa
moja. Akaingia chooni na kuvaa koti lile jeupe ili
asiweze kusumbuliwa kwani korido ilikuwa ndefu
mpaka kukifikia chumba namba 9.
Alipishana na manesi wawili ambao walionekana
kuwa busy huku wakitoka chumba kilekile
alichotaka kuingia. Akaingia mle chumbani.
Chumba kilikuwa na vitanda viwili lakini mgonjwa
alikuwa mmoja.
Samson. Aliita Vero
Mgonjwa dhaifu aliitika kwa sauti yenye
mikwaruzo.
Nani. Aliuliza mgonjwa huku akikohoa.
mimi ni Vero unanikumbuka?
Sogea nikuone macho yangu hayaoni mbali.
Vero akasogea karibu na mgonjwa.
Umenikumbuka? Aliuliza Vero huku akianza
kuingiwa na huruma kutokana na hali ya samson
Masanja.
Bado.
Unamkumbuka mama Pili, yule mama wa
Buguruni ambaye alikuwa anafuga machangudoa?
Aliuliza huku huruma aliyokuwa nayo ikianza
kupotea. Akamuona mgonjwa akishtuka kidogo.
Sina muda wa kupoteza mimi ni mmoja wa watu
ambao kwa kutumia fedha zako uliweza
kutuambukiza virusi, Nimekuja kuchukua roho
yako. Kwani hustahili kifo cha kiungwana kama hiki
cha hospitali. Alimaliza na kuchomoa kisu chake
chenye mpini mwekundu.
*****
Alikuwa anakaribia kupatwa na wazimu kwa
mshituko alioupata baada a kifo cha Fredi.
Veronika alikuwa amekamatwa. HUYU
ANAYEFANYA MAUAJI NI NANI? Lilikuwa swali
lisilojibika. Alifungua tena tepu ndogo ambayo
ilikuwa imerekodiwa wakati makachero wanamuhoji
Veronika.
Nimeshindwa sasa kama munataka kunua niueni
tu
.. Alifoka Vero kwenye kinasa sauti kile.
Akasimama na kuanza kuzunguka zunguka huku
akikuna kichwa chake.
Ni muda huu ambao akili yake ilikuwa kama
imerudi. Akaanza kumkumbuka mkewe Vick na
mama yake. Alishangaa kugundua kuwa siku zote
hizo hakupata hata fursa ya kujiuliza wako wapi.
Upweke uliotawala kwenye nyumba yake ulimfanya
atokwe na machozi mara kadhaa.
UKO WAPI MAMA. Aliwaza huku akimkumbuka
mama yake mzazi, mama ambaye alikuwa na
huruma ya kweli mama ambaye aliyatoa maisha
yake kwa ajili ya manufaa ya mwanae. Alianza
kutokwa na machozi baada ya kuikumbuka familia
yake.
Akakumbuka kuwa mkewe alikuwa mjamzito.
Amejifungua? Au ameolewa na mwanaume
mwingine? Akainama pale mezani. Upweke ulikuwa
unamsulubu fikra zikarudi nyuma akakumbuka jinsi
alivyomfokea mkewe mpaka akaamua kutoroka.
Aliowathamini wote wamerudi mchangani.
Wakati akiwa kwenye dimbwi la mawazo simu yake
ikaanza kuita. Akaitazama ile namba akazidi
kuchanganyikiwa. Namba ya marehemu Lucy ndiyo
iliyoingia.
Hallow habari Inspekta.
Ongea unachotaka kuongea.
Bila salamu?
Haya nzuri ongea.
Nataka ufahamu kuwa mimi ni muuaji mwenye
huruma kama mama yako mzazi. Kama una
kumbukumbu mama yako aliwahi kwenda mahali
kumuokoa dada ambaye alikuwa anakaribia
kuambukizwa virusi vya ukimwi na mumewe. Hivyo
kwa kufuata moyo nzuri wa mama yako na mimi
napenda kumuokoa huyo dada munayemshikilia
hapo. Moja napenda utambue kuwa mimi ndiyo
Vero, pili naona kazi zenu hamfanyi kitaalamu hivi
askari wakubwa kama nyinyi mnashindwa
kuoanisha alama za vidole za mtu munayemshuku
na zile zilizoko kwenye visu, huyo dada
mnamuonea tu kama unakumbuka vizuri siku ya
tukio ulipishana na mwendawazimu ambaye ndio
mimi, pia napenda kukufahamisha kuwa tayari
nimemaliza kazi kwa mtu wa mwisho nenda
chumba namba 9 upande wa VIP katika hospitali
ya Amana.
Simu ilikatwa Inspekta akainua simu yake ya
mezani. Akiwa amechanganyikiwa kabisa
akampigia kachero Dadi kasweyaga.
Hallow vipi afande. Ilisikika simu upande wapili
kuna mauaji mengine Amana.
Tumeshapata taarifa na maiti yake pamoja na ile
ya Fredi zote ziko hospitali ya Taifa ya Muhimbili
nilikuwa nakuja kukupa taarifa.
Halafu naomba huyo Vero aachiwe nafikiri
mahojiano na aina ya matukio yanayotokea
hahusiki kabisa. Alimaliza Inspekta kisha
akaegemea kiti chake tena.
Akili yake ilifanya kazi kuliko uwezo wake wa
kawaida. Swali moja alilojiuliza ni kuhusu muuaji
ambaye ameweza kutoa historia ya maisha ya
mama yake siku za nyuma. Huyu mtu ni nani na
anataka nini. Hilo ni swali lililopita katika kichwa
cha Inspekta. Akatoa simu yake akajaribu kupiga
katika namba za Lucy. Simu ilikuwa
inaita.Hatimaye ikapokelewa.
Enhe. Iliuliza sauti kwa dharau kidogo.
Nataka kujua ni kwanini umefanya mauaji mengi
kiasi hicho?
Kwa kuwa muda wangu wa kuishi umekwisha
nitakufahamisha kila kitu.
Tutaonana vipi?
Unakumbuka vizuri pale ulipokulia?
Una maanisha nini?
Unaikumbuka ile nyumba ya mbagala ambayo
ilikuwa ya marehemu baba yako?
Ndiyo nakumbuka vizuri.
Tukutane pale saa 12.30 Jioni.
Sawa. Simu ikakatwa.
* * *
Huku hofu ikiwa imeutawala moyo wake Inspekta
alitembea Taratibu kuelekea eneo walilokubaliana
kukutana. Alipapasa mfuko wake wa kushoto.
Bado bastola yake ilikuwepo. Alikuwa amedhamiria
kuua ingawa alijiuliza sana kwa nini muuaji
ametaka wakutane eneo lile. Siku hii hakuvaa sare
zake za kazi. Alipofika eneo lile la kihistoria kwake
akashangaa kuona jinsi lilivyochakaa huku likiwa
limezungukwa na majumba makubwa ya kisasa.
Nyumba yao ilikuwa imeanguka upande mmoja.
Alipoangalia vizuri ndipo akashtuka baada ya
kuwaona mabinti wawili waliokuwa wamekaa
kwenye gogo lile la mnazi ambalo alikuwa
anapenda kukaa miaka mingi iliyopita.
karibu. sauti tulivu ya Vero ilimkaribisha.
Ulikuwa mshtuko wa mwaka. Asingeweza
kumsahau Vero kwani alifanana sana na mama
yake mzazi. Aliyemshangaa pale ni yule binti
mwingine ambaye alifanana na mkewe Vick.
Vero. Unafanya nini hapa? Aliuliza Inspekta huku
akionekana wazi kuchanganyikiwa na kusahau
dhamira yake ya kumuua muuaji.
Baba, si unamtaka muuaji. Niko mbele yako
nifanye utakacho lakini kabla ya yote naomba
nikusimulie kila kitu kuhusu mauaji yale. Huku
machozi yakimtoka akasimama na kuanza
kumsimulia Inspekta.
.. kutokana na ile sumu mama yangu aliishi
siku chache hatimaye akapoteza maisha akaniacha
mimi, Sara na bibi yetu ambaye alipoteza maisha
kutokana na kuzidiwa na homa za mara kwa mara
ambazo zilisababishwa zaidi na ukosefu wa
chakula bora. Baba tazama hayo makaburi
.
Inspekta akaangalia kule alikoelekezwa kidole. Ndio
kwanza akagundua kuwa kulikuwa na makaburi
mawili. Hilo la kwanza ni la mama yangu Vick
ambaye alikupenda akayapigania maisha yako kwa
nguvu zake zote lakini ukamtesa na kumnyanyasa
na hilo la pili ni la mama yako mzazi, amekufa
hata mazishi yake hujahudhuria
. Narudia tena
mimi ndio muuaji na sababu zangu nishakueleza.
Sara na Inspekta walikuwa wanamwaga machozi.
Sara alikuwa analia kwa kuliona kaburi la mama
yake. Inspekta alikuwa analia kutokana na mjeledi
aliopigwa katika maisha yake.
Baba sioni tena thamani ya kuendelea kuishi mimi
ni muathirika yanipasa kumfuata mama na bibi,
naomba umtunze huyo sara
.
Hapana mwanangu usiniache peke yangu
.
Inspekta alilia kama mtoto mdogo huku
akimbembeleza Vero ambaye alikuwa ameshika
kisu mkononi.
Hapana Vero mwanangu usifanye hivyo dawa ya
ukimwi ishagunduliwa mwanangu. Alibembeleza
Inspekta huku akimnyooshea mkono mwanawe
asithubutu kujiua.
Dada utaniacha na nani kama utakufa. Sara naye
alilia akimbembeleza dada yake asijiue.
Usijali Sara nimekufikisha mbele ya baba yako
atakutunza mimi naondoka.
Veroooooooooo. Aligumia Sara kwa uchungu
wakati akimshuhudia dada yake akididimiza kisu
kifuani kwake mwenyewe.
Damu ziliruka zikarukia kwenye blauzi nyeupe ya
Sara. Vero alikuwa anakata roho huku
akimwangalia mdogo wake kwa macho yaliyojaa
huruma. Sara aliinama pale alipolala dada yake na
kumshikilia mabegani huku akilia kwa uchungu.
Kwanini dada, kwa nini ufe. Aliendelea kulalamika
Vero.
Inspekta naye aliendelea kulia kwa sauti kubwa.
Huku akimwangalia mwanae alivyokuwa anakata
roho. Sara. Aliita Vero. Nakk
..kk..mh
.
Haijulikani alitaka kuongea nini akakata roho.
MWISHO