mireille
JF-Expert Member
- Mar 4, 2020
- 523
- 568
HAVINTISHI 1
HUSQER BALTAZAR (0657762790)
Siku moja nimekaa nyumban nikashangaa baba anakuja na shangazi pamoja na mwanaume ambae alikuwa anaonekana kama hajapishana sana na baba, “havintishi njoo tulete vinywaji”, alisema mama mara baada ya wageni kuingia ndani, nilienda nikauliza wanakunywa vinywaji gani wakaniambia kisha nikakimbia dukani kununua, lakin wakati wote huo yule mwanaume aliekuja na baba Pamoja na shangazi alikuwa ananiangalia sana, sikujal maana niliamin huenda ni rafiki yake na baba maana alikuwa anautuuzima flan hivi.
Niliporudi nikawapa vinywaji vyao, maana shangazi na mgeni waliagiza pepsi n a baba akaagiza stone tangawizi, so nikawafungulia pale kisha nikawapa na glass alafu nikaondoka zangu.
Mara mama akaniita, ikabidi nimfate chumban kwake kumsikiliza anataka kunambia nn, “havi mwanangu unataka Kwenda kuzurura na wakat huu ugeni ni wako”, akasema mama.
Wangu? Nikauliza kwa mshango maana suala la yeye kunambia ule ugeni ni wangu sikumuelewa kabisa yaan, “ndio ni ugeni wako”, akaendelea kusema mama ila kwa sauti ya kinyonge sana kana kwamba anaogopa kunambia jambo.
Ehee nambie wangu kivipi? Ikabidi na mm niulize, huyo unaemuona hapo ni mchumba wako na baba yako alishapokea posa kitambo na leo ndio ameleta mahari, akasema mama, na hapo unapomuona mwanangu anawake watatu wewe unaenda kuwa mke wa nne, akaendelea kusema mama.
Kiukweli maneno yale yamenishangaza maana nimeletewa vipi posa na hali ya kuwa mm mwenyewe sijui, na licha ya kutokujua pia sijaikubali sasa inawezekana vipi wachukue na mahari kabisa, alafu mm hata mwanaume simjui inawezekana vipi niolewe mke wan ne?, mbona natongozwaga na vijana wenzangu kila wakat na wananiambiaga wananipenda?, au baba ni kwamba hajaona vijana wenzangu?, au ndio ameshanichoka so anataka kunifukuza?, nikawaza.
“Mama mbona ni mtu mzima hivyo?”,nikauliza.mwanangu vijana ni washenzi bora mwanangu hawa ambao tayar wameshayajua maisha hawawez kukusumbua, watu wazima hawawez kukutesa, akasema mama na kiukweli sikuwa namuelewa kabisa,yaan ndio kwanza ninamiaka 18, alafu ndoa yangu ya kwanza niolewwe na mtu mwenye miaka 40 huko, sibaba yangu kabisa huyu, nikawaza, aweeee !, labda sio havintishi mm, haolewi mtu hapa., nikawaza
Hata sikubisha nikajichekesha pale mbele ya mama kisha nikamtoroka na Kwenda kuwafata mashoga zangu, alikuwa siwema, na mwanakombo, nikawapa Habari ya mambo yanayoendelea kwetu.
Usikubali …… usikubali yaan uzee ale na wazee wenzie ujana aje atake kumalizia kwako,akukome tena, siwema na mwanakombo wakasema na kidogo wakanipa nguvu.
Nafanyaje sasa?, nikawauliza ili walau wanipe mawazo ya nn cha kufanya maana kuolewa na kijitu kizima inataka moyo, kwakweli.
Mnyookee na umpe vidonge vyake, alafu tunasikia ukiolewa na mzee na wewe unazeeka shoga, usikubali kabisa, yaan akitoka pale kwenu mtafutie upenyo umcharue mpaka akome kutaka kuoa vibint vidogo, akasema siwema na mwanakombo akadakia “heheheiyaaa wanasema ng’ombe azeeki maini ila anadumaaa, usikubali kudumazwa shoga angu”, basi wote wakacheka vile vicheko vya kipashkuna na kumuambia havintishi aende akakae karibu na kwao ili kale kazee kakitoka akafate akakape vidonge vyake, na Havi kwa akili yake akakubali chap chap maana kuolewa na mtu mzima inataka moyo kwa kweli, na moyo huo havintishi hakuwa nao kabisa yaani.
Basi kweli akawa anazengea zengea kwao mpaka akamuona yule mzee anatoka akiwa na baba yake, akawafata nyuma nyuma akaona baba yake ameingia kwenye kijiwe cha kahawa na yule mzee anatembea pekee yake, akavizia afike mbali kidogo ili baba yake asije akamuona, kweli aliposogea sogea akamfata
“Shikamoo mume wangu mtarajiwa”, akasema havinitishi kitu ambacho kilimfanya yule mwanaume acheke maana nadhan hata yeye alijua fika havintishi n mdogo na hawezi kukubali kuolewa na mwanaume kama yeye, sijui hata alikuwa anatafuta nn Kwenda kuoa Watoto wadogo,ila hiki choo alichoingia ni cha Watoto yaan asipojuta kumchumbia havintishi hatakaa ajute tena.
“Mume nasikia njaa”, akasema havintishi ili apate sehemu ya kukaa kuongea na yule mwanaume, maana kwanza ni mtu mzima na pili pale mtaani wanamjua sana havintishi n mtu wa matukio wasije wakaanza kumtania bure,na yule baba akatafuta kasehemu kama kakibanda wanacho kaanga chipsi, akamwambia waende pale,na walipofika akamwambia havintishi akaagize chakula, yaan hapo ndio alipobugi mtoto wa mwalusembe huko, enzi hizo bado shamba hata chpsi hawalagi hovyo, wao ni kila siku wanakula ugali wa bada na mihogo, alafu unafika kwenye kibanda cha chips unamwambia agiza si utafariki, yaan hapo ndio utashangaa kumuona binti mrembo ana appetite ya fundi ujenzi, anakula kama anabeba zege, au anachimba mitaro.
Naomba chipsi yai mbili moja mebwedo na nyingine ikauke, hio mdebwedo utaniletea hapa mezan na kipaja cha kuku Pamoja na pepsi baridi, akasema havintishi, yule mzee ni kama hakutegemea akaanza kujichekesha chekesha, havintishi akaona nisije nikaabika nikaosheshwe vyombo hapa bure, akamwambia muhudumu nitafutie chupa yamaji iliotumika uniwekee pepsi yangu na hizo chips zote nitabeba, akashangaa yule baba akasema njoo na zege tatu na kuku nusu, alafu akamuita muhudumu akampa pesa kabisa maana alishaanza kuona huenda havintishi anamuona kama hana pesa hivi.
Ewaaaa… mambo si ndio hayo mwenzio nilikuwa naogopa kuosheshwa vyombo, sasa hapa hata ukiondoka siwi na shida yoyote maana umeshalipa, baada ya muda mfupi akaja yule muhudumu akaleta zege mbili, na kuku nusu maana moja ilikuwa bado haijawa tayar, havintishi akazisogeza zote kwake akaanza kula na yule baba alikuwa ameagiza maji tu anakunywa taratibu, kama utani havintishi alimaliza chipsi zege mbili na nusu kuku, kitu ambacho hata yule baba hakutegemea, alipomaliza sasa akaanza kumpa vidonge vyake yule mzee.
“naomba nikusalimie tena mume mtarajiwa shikamoo”,akasema havintishi mpaka yule baba akajikuta anacheka, sasa mzee wewe cha kutaka kunioa binti mdogo kama mimi ni nn, au ndio umepewa masharti ya m ganga kuwa utafut kabinti bikira, kisa chakutaka kunibemenda mtoto wa watu ni nini, akasema havintishi.
Yaan wazee wa siku hizi wa hovyo sana, yaan ujana wanakula pekee yao alafu wanaanza kutafuta Watoto wa watu wa kumaliziana nao uzee, au unaniona kama nina miaka 38 mzee, mm ni mdogo ndio kwanza form four nimemaliza mwaka jana na ndio kwanza nina miaka 18, nak ama wazaz wangu walikuwa wanaogopa kukuambia, naomba nikuambie mm kuwa sikutaki na siwez kuolewa na mwanaume mzee kama wewe, akasema Havi
Baba yako ameshakula pesa zangu, so huo uwezo wa kukataa huna, akasema yule mzee, weee kamdai nenda kamdai pesa zako, mm sio bidhaa kwamba mtu akijisikia kuninunua ananinunua tu, nakuheshimu sana maana wewe ni mtu mzima, lakin kama unataka nikukosee heshima endeleza hii ndoa, maana hata kama utafanikiwa kunioa jua utaniacha pekee yako bila kutegemea, yaan unawake watatu alafu unataka kuja kunibemenda mtoto wa mwanaume mwenzio, hovyoo……., akasema havintishi huku akiwa anaondoka na ile chipsi zege yake hakuisahau, akaibeba na kumuacha yule mzee anamuangalia (itaendelea…………….)
HUSQER BALTAZAR (0657762790)
Siku moja nimekaa nyumban nikashangaa baba anakuja na shangazi pamoja na mwanaume ambae alikuwa anaonekana kama hajapishana sana na baba, “havintishi njoo tulete vinywaji”, alisema mama mara baada ya wageni kuingia ndani, nilienda nikauliza wanakunywa vinywaji gani wakaniambia kisha nikakimbia dukani kununua, lakin wakati wote huo yule mwanaume aliekuja na baba Pamoja na shangazi alikuwa ananiangalia sana, sikujal maana niliamin huenda ni rafiki yake na baba maana alikuwa anautuuzima flan hivi.
Niliporudi nikawapa vinywaji vyao, maana shangazi na mgeni waliagiza pepsi n a baba akaagiza stone tangawizi, so nikawafungulia pale kisha nikawapa na glass alafu nikaondoka zangu.
Mara mama akaniita, ikabidi nimfate chumban kwake kumsikiliza anataka kunambia nn, “havi mwanangu unataka Kwenda kuzurura na wakat huu ugeni ni wako”, akasema mama.
Wangu? Nikauliza kwa mshango maana suala la yeye kunambia ule ugeni ni wangu sikumuelewa kabisa yaan, “ndio ni ugeni wako”, akaendelea kusema mama ila kwa sauti ya kinyonge sana kana kwamba anaogopa kunambia jambo.
Ehee nambie wangu kivipi? Ikabidi na mm niulize, huyo unaemuona hapo ni mchumba wako na baba yako alishapokea posa kitambo na leo ndio ameleta mahari, akasema mama, na hapo unapomuona mwanangu anawake watatu wewe unaenda kuwa mke wa nne, akaendelea kusema mama.
Kiukweli maneno yale yamenishangaza maana nimeletewa vipi posa na hali ya kuwa mm mwenyewe sijui, na licha ya kutokujua pia sijaikubali sasa inawezekana vipi wachukue na mahari kabisa, alafu mm hata mwanaume simjui inawezekana vipi niolewe mke wan ne?, mbona natongozwaga na vijana wenzangu kila wakat na wananiambiaga wananipenda?, au baba ni kwamba hajaona vijana wenzangu?, au ndio ameshanichoka so anataka kunifukuza?, nikawaza.
“Mama mbona ni mtu mzima hivyo?”,nikauliza.mwanangu vijana ni washenzi bora mwanangu hawa ambao tayar wameshayajua maisha hawawez kukusumbua, watu wazima hawawez kukutesa, akasema mama na kiukweli sikuwa namuelewa kabisa,yaan ndio kwanza ninamiaka 18, alafu ndoa yangu ya kwanza niolewwe na mtu mwenye miaka 40 huko, sibaba yangu kabisa huyu, nikawaza, aweeee !, labda sio havintishi mm, haolewi mtu hapa., nikawaza
Hata sikubisha nikajichekesha pale mbele ya mama kisha nikamtoroka na Kwenda kuwafata mashoga zangu, alikuwa siwema, na mwanakombo, nikawapa Habari ya mambo yanayoendelea kwetu.
Usikubali …… usikubali yaan uzee ale na wazee wenzie ujana aje atake kumalizia kwako,akukome tena, siwema na mwanakombo wakasema na kidogo wakanipa nguvu.
Nafanyaje sasa?, nikawauliza ili walau wanipe mawazo ya nn cha kufanya maana kuolewa na kijitu kizima inataka moyo, kwakweli.
Mnyookee na umpe vidonge vyake, alafu tunasikia ukiolewa na mzee na wewe unazeeka shoga, usikubali kabisa, yaan akitoka pale kwenu mtafutie upenyo umcharue mpaka akome kutaka kuoa vibint vidogo, akasema siwema na mwanakombo akadakia “heheheiyaaa wanasema ng’ombe azeeki maini ila anadumaaa, usikubali kudumazwa shoga angu”, basi wote wakacheka vile vicheko vya kipashkuna na kumuambia havintishi aende akakae karibu na kwao ili kale kazee kakitoka akafate akakape vidonge vyake, na Havi kwa akili yake akakubali chap chap maana kuolewa na mtu mzima inataka moyo kwa kweli, na moyo huo havintishi hakuwa nao kabisa yaani.
Basi kweli akawa anazengea zengea kwao mpaka akamuona yule mzee anatoka akiwa na baba yake, akawafata nyuma nyuma akaona baba yake ameingia kwenye kijiwe cha kahawa na yule mzee anatembea pekee yake, akavizia afike mbali kidogo ili baba yake asije akamuona, kweli aliposogea sogea akamfata
“Shikamoo mume wangu mtarajiwa”, akasema havinitishi kitu ambacho kilimfanya yule mwanaume acheke maana nadhan hata yeye alijua fika havintishi n mdogo na hawezi kukubali kuolewa na mwanaume kama yeye, sijui hata alikuwa anatafuta nn Kwenda kuoa Watoto wadogo,ila hiki choo alichoingia ni cha Watoto yaan asipojuta kumchumbia havintishi hatakaa ajute tena.
“Mume nasikia njaa”, akasema havintishi ili apate sehemu ya kukaa kuongea na yule mwanaume, maana kwanza ni mtu mzima na pili pale mtaani wanamjua sana havintishi n mtu wa matukio wasije wakaanza kumtania bure,na yule baba akatafuta kasehemu kama kakibanda wanacho kaanga chipsi, akamwambia waende pale,na walipofika akamwambia havintishi akaagize chakula, yaan hapo ndio alipobugi mtoto wa mwalusembe huko, enzi hizo bado shamba hata chpsi hawalagi hovyo, wao ni kila siku wanakula ugali wa bada na mihogo, alafu unafika kwenye kibanda cha chips unamwambia agiza si utafariki, yaan hapo ndio utashangaa kumuona binti mrembo ana appetite ya fundi ujenzi, anakula kama anabeba zege, au anachimba mitaro.
Naomba chipsi yai mbili moja mebwedo na nyingine ikauke, hio mdebwedo utaniletea hapa mezan na kipaja cha kuku Pamoja na pepsi baridi, akasema havintishi, yule mzee ni kama hakutegemea akaanza kujichekesha chekesha, havintishi akaona nisije nikaabika nikaosheshwe vyombo hapa bure, akamwambia muhudumu nitafutie chupa yamaji iliotumika uniwekee pepsi yangu na hizo chips zote nitabeba, akashangaa yule baba akasema njoo na zege tatu na kuku nusu, alafu akamuita muhudumu akampa pesa kabisa maana alishaanza kuona huenda havintishi anamuona kama hana pesa hivi.
Ewaaaa… mambo si ndio hayo mwenzio nilikuwa naogopa kuosheshwa vyombo, sasa hapa hata ukiondoka siwi na shida yoyote maana umeshalipa, baada ya muda mfupi akaja yule muhudumu akaleta zege mbili, na kuku nusu maana moja ilikuwa bado haijawa tayar, havintishi akazisogeza zote kwake akaanza kula na yule baba alikuwa ameagiza maji tu anakunywa taratibu, kama utani havintishi alimaliza chipsi zege mbili na nusu kuku, kitu ambacho hata yule baba hakutegemea, alipomaliza sasa akaanza kumpa vidonge vyake yule mzee.
“naomba nikusalimie tena mume mtarajiwa shikamoo”,akasema havintishi mpaka yule baba akajikuta anacheka, sasa mzee wewe cha kutaka kunioa binti mdogo kama mimi ni nn, au ndio umepewa masharti ya m ganga kuwa utafut kabinti bikira, kisa chakutaka kunibemenda mtoto wa watu ni nini, akasema havintishi.
Yaan wazee wa siku hizi wa hovyo sana, yaan ujana wanakula pekee yao alafu wanaanza kutafuta Watoto wa watu wa kumaliziana nao uzee, au unaniona kama nina miaka 38 mzee, mm ni mdogo ndio kwanza form four nimemaliza mwaka jana na ndio kwanza nina miaka 18, nak ama wazaz wangu walikuwa wanaogopa kukuambia, naomba nikuambie mm kuwa sikutaki na siwez kuolewa na mwanaume mzee kama wewe, akasema Havi
Baba yako ameshakula pesa zangu, so huo uwezo wa kukataa huna, akasema yule mzee, weee kamdai nenda kamdai pesa zako, mm sio bidhaa kwamba mtu akijisikia kuninunua ananinunua tu, nakuheshimu sana maana wewe ni mtu mzima, lakin kama unataka nikukosee heshima endeleza hii ndoa, maana hata kama utafanikiwa kunioa jua utaniacha pekee yako bila kutegemea, yaan unawake watatu alafu unataka kuja kunibemenda mtoto wa mwanaume mwenzio, hovyoo……., akasema havintishi huku akiwa anaondoka na ile chipsi zege yake hakuisahau, akaibeba na kumuacha yule mzee anamuangalia (itaendelea…………….)