Hadithi: Jini Mweusi

Hadithi: Jini Mweusi

SEHEM YA 15

Ananogewa na mchezo huo kiasi cha kuwamtumwa wa ngono, anaendelea na mchezohuo mpaka anapoingia mwaka wa tatu chuoni hapo. Msichana mdogo aliyekuwa akisomamwaka wa kwanza chuoni hapo, Neema,anatokea kumpenda Dickson, jambo ambalohalijawahi kumtokea. Hata hivyo , msichana huyo hayupo tayarikuanza kufanya mapenzi na Dickson , jambolinalosababisha kijana huyo aende tenakununua machangudoa bila kujua kuwa Neemaalikuwa akimfuatilia kwa nyuma .

Kwa macho yake anamshuhudia Dickson akinunua changudoa, jambo linalomuumiza sana.

Je , nini kitafuatia? SONGA NAYO

Baada ya Neema kumshuhudia kwa machoyake mwenyewe, Dickson akinunua changudoana kuelekea naye gesti , alijisikia maumivumakali mno ndani ya moyo wake. Licha yakujipa moyo kwamba afadhali ameujua ukwelimapema, bado maumivu makali yaliendeleakumtesa kiasi cha kuamua kuondoka kabisaeneo hilo, huku machozi yakimtoka.Akaelekea barabarani kwa lengo la kuvukaBarabara ya Shekilango ili atafute usafiri wakumrudisha chuoni, huku mawazo mengiyakizidi kukitesa kichwa chake, akawa anahisikama amebeba jiko la mkaa kichwani mwake .Machozi yakawa yanaendelea kumtoka nakuulowanisha uso wake mzuri.

Hata alipokuwa anavuka barabara ,hakukumbuka kuangalia magari huku na kulekabla ya kuvuka, akajikuta ameingiabarabarani huku akiendelea kulia kwauchungu.Penzi la Dickson lilimtesa mno , upandemwingine akawa anajilaumu kwamba kamamchana wa siku hiyo angekubali kufanyamapenzi na Dickson, huenda hayo yote yasingetokea.“ Lakini mimi sijawahi kufanya mapenzi nanimejiwekea nadhiri kwamba sitampa ruhusa mwanaume yeyote auguse mwili wangumpaka nitakapo …” Neema aliendelea kuwazalakini kabla hajamalizia, alishtukia honi kalizikipigwa upande wake wa kushoto, alipogeuka, gari dogo la kifahari, Toyota MarkX tayari lilishamfikia mwilini.

Licha ya dereva kujitahidi kufunga breki kali,gari hilo lilimgonga Neema na kumrusha mita kadhaa juu , akadondoka katikati ya lami nakusababisha taharuki kubwa eneo hilo.***Baada ya kukidhi haja zake, Dickson alitokaharakaharaka kwenye chumba cha gestialichoingia na changudoa yule kamailivyokuwa kawaida yake. Kwa kuwa kaziiliyomleta alishaimaliza, hakutaka kuendeleakukaa eneo hilo.

Akawa anaondoka kwa lengo la kuvuka barabara na kuchukua usafiri wa kumrudishachuoni lakini ghafla alipoikaribia barabara ,alishtushwa na umati wa watu uliokuwaumekusanyika barabarani huku watu wenginewengi wakikimbilia eneo hilo.“ Kuna nini kimetokea pale ?” Dickson alimuuliza mmoja kati ya watu wengi waliokuwa wanakimbilia eneo hilo.“ Amegonga mtu! Daah , sijui kama ataponayule dada , ” alisema mtu huyo huku akizidishamwendo, Dickson naye akaongeza mwendompaka mahali mtu aliyegongwa alipokuwaameangukia.“ Ooh my God! Neema , what happened to you?”(Mungu wangu ! Neema, nini kimekutokea?)“ Mnafahamiana?” Patrick Buzohela, mwandishimahiri kutoka Kituo cha Runinga cha GlobalTV , alimhoji Dickson huku akimsogezea‘ maikrofoni ’ mdomoni, mwandishi mwingineakiwa makini kuchukua picha za video kwaajili ya kurusha kwenye runinga hiyo.“ Ni mwanachuo mwenzangu, tunasoma nayeChuo Kikuu cha Dar es Salaam, ” alisemaDickson kwa sauti ya juu huku akiwasukumawatu wote na kwenda mpaka pale chinimsichana huyo alipokuwa ameangukia, damu nyingi zikimtoka puani, mdomoni na kwenyemajeraha mengi aliyoyapata .

Patrick na mwenzake waliendelea kuchukuapicha za tukio hilo kwa umakini mkubwa,wakawa wanarekodi kila kitu kilichokuwakinaendelea pamoja na kuwahoji baadhi yamashuhuda wa ajali hiyo .Bila kujali chochote, Dickson alimuinua nakuanza kuomba msaada kwa mtu yeyotemwenye usafiri ili wamkimbize hospitali .Bahati nzuri , gari lililomgonga halikuwa limeharibika sana, dereva akashuka hukuakitetemeka na kukubali kumkimbizahospitalini .Kwa kuwa askari wa usalama barabaranihawakuwa mbali na eneo hilo, walifika na kuchukua taarifa zote muhimu kishawakaruhusu mgonjwa akimbizwe hospitalini .Dickson akiwa kwenye siti ya nyuma ya garihilo, alimpakata Neema ambaye damu nyingizilikuwa zikiendelea kumvuja nakumlowanisha kijana huyo mwilini lakinimwenyewe hakujali.

Muda mfupi baadaye, tayari walikuwawamewasili kwenye Hospitali yaMwananyamala ambapo waliteremka nakupokelewa na wahudumu waliomlazamsichana huyo kwenye kitanda chamagurudumu na kumkimbiza wodini. Tayarigiza lilishaanza kuingia. Dickson akawasaidia mpaka walipofika kwenyemlango wa wodi ya wagonjwa mahututiambapo hakuruhusiwa kuingia. Msichana huyoambaye alishapoteza fahamu kuanzia mudauleule aliogongwa na gari , aliingizwa wodiniambapo madaktari walianza kuhangaikakuokoa maisha yake.“ Mgonjwa ni nani yako?”“ Ni mwanachuo mwenzangu. ”“ Mnasoma wapi?”“ Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ” alisemaDickson wakati akitoa maelekezo kwa mtualiyekuwepo mapokezi, kwa ajili ya kuandaafaili la mgonjwa. Baada ya kumaliza kutoamaelezo hayo , Dickson ambaye damu nyingizilizokuwa zimemvujia kwenye nguo zakezilikuwa zimeanza kukauka, alienda kukaakwenye benchi lililokuwa jirani na wodi yawagonjwa mahututi.

Tayari Kituo cha Runinga cha Global TVkilikuwa kikiirusha habari ya mwanachuo huyo kugongwa na gari na kueleza kila kitukilichokuwa kinaendelea mpaka muda huo .Watu wengi, wakiwemo wanachuo wenzakewakasikia taarifa hiyo na kuanza kukusanyanakuelekea hospitalini. Maswali mengi yaliyokosa majibu yaliendeleakupita kwenye kichwa cha Dickson, akiwahaelewi ilikuwaje mpaka Neema akafika eneohilo na kupata ajali mbaya kiasi hicho.Aliendelea kujiuliza maswali mengi ambayohakuna hata moja alilopata jibu lake.“ Au alikuwa ananifuatilia nini? Lakini haiwezekani, alijuaje kwamba nimekuja huku?” alijiuliza lakini akajipa moyo mwenyewe.

Aliendelea kukaa kwenye benchi hilo kwamuda mrefu mpaka baadaye aliposhtukiaviongozi wa serikali ya wanachuo na baadhiya wahadhiri wakija kwa wingi hospitalinihapo.“ Kumetokea nini Zinja ?”“ Neema kapata ajali mbaya , amegongwa nagari. ”“ Neema yupi ? Yule mwanachuo wa mwaka wakwanza mliyekuwa mmekaa naye jana wakatiwa chakula cha jioni ?”“ Ndiyo huyohuyo ,” alijibu Dickson nakuinamisha kichwa chake chini. Maswalialiyokuwa anaulizwa na wanachuo wenzakeyalizidi kumtia uchungu na kusababishamachozi yaanze kumlengalenga. Muda mfupi baadaye, mlango wa wodi yawagonjwa mahututi ulifunguliwa, watu wotewakasimama wakiwa na shauku kubwa yakusikia chochote juu ya hali ya mwanachuo mwenzao.

Je, nini kitafuatia?
 
SEHEM YA 16

Ananogewa na mchezo huo kiasi cha kuwamtumwa wa ngono, anaendelea na mchezohuo mpaka anapoingia mwaka wa tatu chuonihapo. Msichana mdogo aliyekuwa akisomamwaka wa kwanza chuoni hapo, Neema,anatokea kumpenda Dickson, jambo ambalohalijawahi kumtokea .Hata hivyo , msichana huyo hayupo tayarikuanza kufanya mapenzi na Dickson , jambolinalosababisha kijana huyo aende tenakununua machangudoa bila kujua kuwa Neemaalikuwa akimfuatilia kwa nyuma . Kwa machoyake anamshuhudia Dickson akinunuachangudoa, jambo linalomuumiza sana .Anapoteza umakini na kujiingiza barabaranibila kuangalia magari, jambo linalosababishaagongwe vibaya.

Je , nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Baada ya Neema kumshuhudia kwa machoyake mwenyewe, Dickson akinunua changudoana kuelekea naye gesti , alijisikia maumivumakali mno ndani ya moyo wake. Licha yakujipa moyo kwamba afadhali ameujua ukwelimapema, bado maumivu makali yaliendeleakumtesa kiasi cha kuamua kuondoka kabisaeneo hilo, huku machozi yakimtoka. Akaelekea barabarani kwa lengo la kuvuka Barabara ya Shekilango ili atafute usafiri wakumrudisha chuoni, huku mawazo mengiyakizidi kukitesa kichwa chake, akawa anahisikama amebeba jiko la mkaa kichwani mwake. Machozi yakawa yanaendelea kumtoka nakuulowanisha uso wake mzuri .

Wanachuo wengi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Mlimani) waliendelea kufurika kwenyeHospitali ya Mwananyamala baada ya kuonataarifa ya habari ya dharura (breaking news) kupitia Kituo cha Runinga cha Global TV .Wakiwa nje ya wodi ya wagonjwa mahututialiyolazwa msichana huyo aliyepata ajalimbaya ya kugongwa na gari, mara mlangoulifunguliwa, madaktari wawili wakatokawakionekana kuwa na haraka sana. Wanachuo wote wakasimama , wakiwa nashauku kubwa ya kutaka kujua hali yamwenzao.“ Bado hali siyo nzuri, tunafikiria kumkimbizaMuhimbili, ” alisema daktari aliyekuwa amevaliakoti jeupe, shingoni akiwa na kifaa chakupimia mapigo ya moyo au kwa kitaalamu Stethoscope.

Kauli hiyo ilimnyong’ onyeza kila mmoja kwaniilivyoonekana hali ya mgonjwa ilikuwa mbayasana. Muda mfupi baadaye, gari la kubebeawagonjwa (ambulance) liliwasili eneo hilo nakupelekwa mpaka jirani kabisa na mlangomkubwa wa kuingilia kwenye wodi hiyo .Manesi kwa kushirikiana na madaktari, wakasaidiana kumtoa msichana huyo kutokakwenye wodi ya wagonjwa mahututi nakumpakiza kwenye gari la kubebea wagonjwa.Gari hilo likaondoka kwa kasi huku likiwalimewashaa taa zote na lilipotoka eneo lahospitali hiyo, lilianza kupiga ving ’ ora .

Ilibidi viongozi wa serikali ya wanachuowaitane na kuwakusanya wanachuo wotewaliokuwa wamefurika hospitalini hapo ,wakawasihi kwamba ni vyema wakarejeachuoni na wachache kati yao wataendakuwawakilisha kufuatilia hali ya mgonjwa.“ Muda umeshaenda sana na giza linazidikutanda kila mahali , nashauri nyote mrejeechuoni halafu sisi viongozi wenu na baadhi yarafiki zake wa karibu tutaelekea Muhimbilikufuatilia kinachoendelea . Nawaomba wotemuwe wavumilivu katika kipindi hiki kigumu,”rais wa serikali ya wanachuo, aliwaambiawenzake.Japokuwa kila mmoja alikuwa na shauku yakutaka kwenda Muhimbili, maelezo hayo yakiongozi wao yaliwafanya wanachuokukubaliana na kilichosemwa.

Safari ya kurejea chuoni ikaanza huku kila mmojaakizungumza lake, wengi wakimuonea hurumamsichana huyo kwa kilichotokea.Wengine walikuwa wakihoji alikuwa akitokeawapi mpaka apate ajali hiyo kwani kulikuwa naumbali mrefu kutoka chuoni mpaka eneokulipotokea ajali, Sinza Afrika Sana. “ Halafuilikuwaje mpaka Zinja naye afike eneo la tukioharaka kwenda kutoa msaada ? Au walikuwapamoja?” mwanachuo mmoja alihoji wakatiwakirejea chuoni. Hakuna aliyekuwa na majibuya kilichotokea.

Viongozi wa serikali ya wanachuo na watuwengine wachache, akiwemo Dicksonwalielekea Muhimbili ambapo mpakawanawasili, tayari mgonjwa alikuwa akiendeleakupatiwa matibabu kwenye wodi ya wagonjwamahututi .“ Amepata madhara makubwa kwenye uti wamgongo na fuvu la kichwa , tunaendeleakuchunguza kwa kina ukubwa wa madharahayo na kutafuta njia ya kumsaidia lakini kazihaitakuwa nyepesi, ” alisema Dokta Innocent Nzunda wakati akizungumza na Dicksonpamoja na wenzake walioongozana nao kutokaHospitali ya Mwananyamala.“ Msaidieni dokta apone, niko chini ya miguuyenu, ” alisema Dickson huku akilia kamamtoto mdogo , wenzake wakawa na kazi yakumbembeleza. Hakuna kitu ambacho hakuwatayari kuona kinatokea kama Neema kupotezamaisha .

Alitamani na yeye angekuwa daktari ili aingiemwenyewe wodini kwani alihisi madaktari haohawajitumi ipasavyo kumsaidia mpenzi wakehuyo. Bado alikuwa akiendelea kujiuliza maswali mengi yaliyokosa majibu kuhusumazingira ya ajali yenyewe. Hakujua Neema alikuwa akitoka wapi mpakaakapata ajali hiyo mbaya , bado akili nyinginezilikuwa zikimtuma kuamini kwamba huenda msichana huyo alikuwa akimfuatilianyumanyuma na alishuhudia wakati Dicksonakimnunua changudoa na kuingia naye gestina huenda ndiyo sababu iliyomfanya Neemaakose umakini na kujikuta akigongwa na gari.“ Hapana! Haiwezi kuwa hivyo, haiwezekani , ”Dickson alizungumza kwa sauti ya juu nakuwafanya wenzake waliokuwa pembeni yakewamshangae. “ Nini hakiwezekani Dickson?” mmoja wao alimuuliza , ikabidi avunge kwambaalikuwa akimaanisha haiwezekani Neem aapoteze maisha .“ Usiwe na wasiwasi sana , yupo kwenyemikono salama, si unaona jinsi madaktariwanavyopishana kuingia na kutoka kwenyewodi aliyolazwa? Cha msingi ni kuendele kumuombea kwa Mungu, ” alisema kiongoziwao lakini bado Dickson alionekana kuendeleakuwaza kwa uchungu, machozi yakimtoka nakuulowanisha uso wake.

.Dakika kadhaa baadaye, Dokta Nzunda alitoka wodini na kuwasogelea akina Dickson, naowakainuka pale walipokuwa wamekaa kila mmoja akionekana kuwa na shauku kubwandani ya moyo wake kutaka kusikia daktarihuyo atasema nini.“ Jamani hali siyo nzuri sana, mwenzenu amevunjika uti wa mgongo na pia damuimevujia ndani ya fuvu la kichwa chake,tunamuandaa kwa ajili ya upasuaji mkubwautakaofanyika usiku huuhuu , mzidi kumuombea kwa Mungu wakati na sisitukitimiza majukumu yetu, ” alisema Dokta Nzunda. Kauli hiyo ilikuwa sawa na mkuki ndani yamoyo wa Dickson, japokuwa hakuwa akijuachochote kuhusu mambo ya kitabibu lakini maelezo ya daktari huyo yalitosha kumfanya ajue kwamba kazi ya kuokoa maisha ya msichana huyo haikuwa nyepesi.

Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 17

kununua machangudoa bila kujua kuwa Neemaalikuwa akimfuatilia kwa nyuma . Kwa machoyake anamshuhudia Dickson akinunuachangudoa, jambo linalomuumiza sana .Anapoteza umakini na kusababisha agongwena gari na kupoteza fahamu. Anapelekwahospitali hali yake ikiwa mbaya sana .

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

“ Jamani hali siyo nzuri sana, mwenzenuamevunjika uti wa mgongo na pia damuimevujia ndani ya fuvu la kichwa chake,tunamuandaa kwa ajili ya upasuaji mkubwautakaofanyika usiku huuhuu , mzidikumuombea kwa Mungu wakati na sisitukitimiza majukumu yetu , ” alisema DoktaNzunda aliyekuwa akisimamia matibabu yamsichana huyo.Kauli hiyo ilikuwa sawa na mkuki ndani yamoyo wa Dickson, japokuwa hakuwa akijuachochote kuhusu mambo ya kitabibu lakinimaelezo ya daktari huyo yalitosha kumfanyaajue kwamba kazi ya kuokoa maisha ya msichana huyo haikuwa nyepesi.

Palepale Dickson alipiga magoti na kuinuamikono juu kama ishara ya mtu anayeomba ,akafumba macho yake na kuanza kusalikimyakimya, akimuomba Mungu aoneshemiujiza yake kwa kumnusuru Neema na kifokwani hali yake ilishakuwa tete.Japokuwa watu walianza kumshangaa, hukuwengine wakihisi anaelekea kuchanganyikiwa ,mwenyewe hakujali, aliendelea kusali hukumachozi yakimtoka kwa wingi.“ Dickson, unahitaji kwenda kupumzikakidogo. ”“ Siwezi kupumzika wakati Neema yupomahututi, nitakaa hapahapa mpaka nionemwisho wake. ”“ Tazama nguo ulizovaa zimekaukia damukibao, kwa nini usiende mara moja chuonijapo ukaoge na kubadilisha nguo ? Atakuwasawa si unaona madaktariwanavyomhangaikia?” kiongozi wa serikali yawanachuo alikuwa akijaribu kumtuliza Dicksonau Zinja kama wengi walivyozoea kumuitalakini ilikuwa ni sawa na kazi bure.

Muda mfupi baadaye, mlango wa wodi yawagonjwa mahututi ulifunguliwa, manesikadhaa wakatoka wakiwa wanasukuma kitandachenye magurudumu huku Neema akiwa juuyake, majeraha makubwa aliyoyapata yakiwayamefungwa na bandeji .Bado hakuwa na fahamu hata kidogo. Dicksonambaye bado alikuwa amepiga magoti ,harakaharaka aliinuka na kukimbilia kulemanesi walikokuwa wanaelekea hukuakiendelea kulia kwa uchungu .“ Usiondoke Neema, unaniacha na nanijamani ?” Dickson alisema huku akilia, machozina kamasi vikimtoka mfululizo.“ Kaka tafadhali tunaomba utupe nafasi tufanyekazi yetu, kulia hakusaidii chochote kwa sasa, ”alisema nesi mmoja huku walinzi waliokuwapembeni nao wakianza kumsogelea Dickson.

Alitii alichoambiwa, kitanda chamagurudumu kikaendelea kusukumwa mpakakwenye wodi iliyokuwa na maneno makubamlangoni yaliyosomeka THEATRyakimaanisha chumba cha upasuaji. Milangoikafunguliwa, wakaingia kisha ikafungwa .Muda mfupi baadaye, madaktari kadhaawalionekana wakitembea harakaharakakuelekea kwenye chumba cha upasuaji hukumanesi wengine wakiwa wamebeba vifaambalimbali kwa ajili ya upasuaji.

Kila mmoja alikuwa katika pilikapilika za kuhakikishamsichana huyo anapatiwa matibabu ya uhakika haraka iwezekanavyo ili kunusurumaisha yake.Tangu madaktari hao na manesi waingiekwenye chumba cha upasuaji, muda uliendeleakuyoyoma kwa kasi bila mlango kufunguliwa wala mtu yeyote kutoka au kuingia ndani yachumba hicho cha upasuaji. Kwa muda wote huo, Dickson alikuwa amekaanje, mita chache kutoka kwenye mlango wakuingilia ndani ya wodi hiyo, akiendelea kusalina kumuomba Mungu wake aoneshemiujiza . Japokuwa kwa kipindi kirefu alikuwaamempa kisogo Mungu wake , akiwaameshasahau hata mara ya mwisho kwendakanisani ilikuwa ni lini, kipindi kigumualichokuwa anapitia kilimfanya akumbukekuwa kumbe Mungu yupo na ana uwezo wakufanya hata yale ambayo kwa akili za kibinadamu hayawezekani.

Baada ya takribani saa sita kupita, ndipo kwamara ya kwanza mlango wa wodi hiyoulipofunguliwa, kitanda cha magurudumukikatolewa huku manesi kadhaa wakikisukuma,wakionesha kuchoka mno.“ Anaendeleaje? Amezinduka? Nesi…amepona?” maneno mfululizo yalikuwa yakimtoka Dickson, akihangaika kama kukuanayetaka kutaga. Nesi mmoja alimjibu kwamba asiwe na wasiwasi kwani kazi imekamilika lakini bado mgonjwa hakuwa amerejewa na fahamu zake. Kidogo moyo wa Dickson ulitulia, akawaanawasindikiza kwa macho manesi hao wakati wakiendelea kukisukuma kitanda ambacho Neema alikuwa amelazwa juu yake, akiwa ameunganishwa na mashine ya kupumulia na kutundikiwa dripu iliyokuwa ikiendelea kushuka mishipani mwake kwa kasi. Alirudishwa mpaka kwenye wodi ya wagonjwa mahututi ambako aliendelea kutibiwa chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari.

Hata hivyo ,licha ya madaktari kufanya kilakilichowezekana siku hiyo , bado msichanahuyo hakuweza kurejewa na fahamu. Siku ya kwanza ikapita, Neema akiwa badoanapumulia mashine ndani ya wodi yawagonjwa mahututi , siku ya pili nayo ikapitahali ikiwa bado vilevile. Mwisho Dicksonakawa hana ujanja zaidi ya kukubali kurudichuoni kupumzika kwani kwa zaidi ya saa 48, hakupata muda wa kupumzika hata kidogo.

Akaondoka kwa shingo upande huku badoakiendelea kumuomba Mungu wake aoneshemiujiza kwa kumzindua msichana huyo kutokakwenye usingizi wa mauti. Hakukaa sanachuoni, akarejea tena hospitalini ambako badohali ilikuwa ileile, Neema alikuwa amelala tukitandani, akiwa hajui chochote kilichokuwakinaendelea kwenye ulimwengu wa kawaida.
 
SEHEMU YA 18

Jioni moja msichana huyo anaamuakumfuatilia Dickson na kwa macho yakeanamshuhudia akinunua changudoa. Mshtukoanaoupata , unasababisha apoteze umakini nakujikuta akigongwa na gari linalomjeruhivibaya na kukimbizwa hospitalini , hali yakeikiwa mbaya mno . Madaktari wanajaribukumsaidia lakini kazi haiwi nyepesi.

Je, ninikitafuatia? SONGA NAYO…

Siku ya kwanza ilipita , hali ya Neema ikiwabado ni tete, akiendelea kupumulia mashinendani ya wodi ya wagonjwa mahututi kwenyeHospitali ya Taifa ya Muhimbili . Hata siku yapili ilipowadia , bado hali ya msichana huyohaikuwa ya kuridhisha.Mwisho Dickson akawa hana ujanja zaidi yakukubali kurudi chuoni kupumzika na kwendakubadilisha nguo kwani kwa zaidi ya saa 48,hakupata muda wa kupumzika hata kidogo. Akaondoka kurudi chuoni kwa shingo upandehuku bado akiendelea kumuomba Mungu wakeaoneshe miujiza kwa kumzindua msichanahuyo kutoka kwenye usingizi wa mauti.

Hakukaa sana chuoni, akarejea tena hospitaliniambako bado hali ilikuwa ileile, Neema alikuwaamelala tu kitandani , akiwa hajui chochotekilichokuwa kinaendelea kwenye ulimwenguwa kawaida. Wazazi wa msichana huyo walikuwa kwenyewakati mgumu zaidi kwani hakuna aliyekuwatayari kuona mtoto wao huyo wa kipekeeanapoteza maisha .Kwa kuwa kiuchumi walikuwa na uwezomkubwa, walianza kujadiliana na baadhi yandugu wa karibu juu ya kufanya taratibu zakumsafirisha msichana huyo kwenda nchiniIndia kwani kwa hali ilivyokuwa, isingekuwarahisi kutibiwa na kupona nchini Tanzania .“ Kijana kwani wewe una uhusiano gani namwenetu? Unaonekana kuguswa sana natangu mimi nije nakuona upo tu hapahospitalini, ” mwanaume mmoja aliyekuwa nasura inayofanana na Neema, alimuuliza Dickson baada ya kumkuta amekaa kwenyebenchi lililokuwa nje ya wodi aliyokuwaamelazwa msichana huyo.

Dickson alibabaika kidogo kwani alijua kuwalazima huyo anayezungumza naye ni baba wamsichana huyo au ndugu yake wa karibu kwajinsi walivyokuwa wakifanana sura.“ Mimi ni rafiki yake wa karibu, naitwaDickson. ”“ Oooh! Wewe ndiye Dicksonuliyekuwa wa kwanza kumtambua baada yakupata ajali?”“ Ndiyo mimi mzee . ”“ Sisi kama familia tunakushukuru sana kwawema wako uliouonesha . Muda mrefu nilikuwanamtafuta mtu aliyemsaidia mwanangu, walasikujua kama ni wewe. Mimi ndiye baba mzaziwa Neema, ” alisema mzee huyo na kushikanamikono na Dickson kaendelea kumshukuru na kumueleza kuwasura yake haikuwa ikifanana na moyo wakipekee aliokuwa nao. Mwisho akamuelezakuhusu uamuzi ambao wao kama wanafamiliawalikuwa wameufikia, wa kumsafirishamsichana huyo mpaka nchini India kwamatibabu zaidi kwani vipimo vilioneshaalikuwa na matatizo makubwa kwenye utiwake wa mgongo na kichwani .“ Tupo kwenye maandalizi ya mwisho yakumpeleka India, endeleeni kutuombea, ”alisema mzee huyo na kabla hajahitimishamazungumzo yake na Dickson, alikuja kuitwana daktari mmoja waliyeongozana naye mpakaofisini kwake.Japokuwa Dickson alikuwa anaomba usiku namchana msichana huyo apone , alitamaniaendelee kutibiwa hapohapo ili iwe rahisikwake kuendelea kumuona lakini hakuwa naujanja, akajiinamia huku machozi yakiendeleakumtoka.

Maandalizi ya kumsafirisha Neema kwendanchini India kwa matibabu yalizidi kupambamoto , Dickson akawa anafuatilia kila hatua,ikiwa ni pamoja na kuwapa taarifa wanachuowenzake ili wapate nafasi ya mwisho yakumuona msichana huyo kabla hajasafirishwa.Baada ya taarifa kuwafikia wanachuo wenzake, kwamba msichana huyo alikuwa mbionikusafirishwa kwenda nchini India, waliendakwa wingi hospitalini hapo kumuangalia. Bado Neema hakuwa amerejewa na fahamu, hakuwaakimtambua mtu yeyote aliyekuwa akiingiawala kutoka kwenye wodi aliyokuwaamelazwa. Hali aliyokuwa nayo iliwaliza wanachuowenzake wengi ambao baadhi walikuwa wakishindwa kuyazuia machoziyasizilowanishe nyuso zao.

Wanachuo waliendelea kumiminika kwa wingi chuoni hapo mpaka ikabidi uongozi wa hospitali uingilie kati na kuwataka kuanza kuingia kwa awamu ili kuruhusu shughuli nyingine kuendelea hospitalini hapo.Wazazi wake nao waliendelea kuhangaika nabaada ya muda mfupi , tayari maandaliziyalikuwa yameshakamilika, ikiwa ni pamoja nakupata nafasi kwenye ndege maalum iliyokuwana chumba maalum cha kuhudumia wagonjwakwa ajili ya safari ya kuelekea nchini India.

Hakukuwa na cha kusubiri tena , gari lakubebea wagonjwa liliandaliwa, Neemaakatolewa wodini chini ya uangalizi wamadaktari na manesi wengi na kuingizwandani ya gari hilo la kubebea wagonjwa.Daktari mmoja aliyechaguliwa kusafiri pamojana mgonjwa ili kuendelea kumhudumia wakatindege ikiwa angani , naye tayari alishakuwaamejiandaa, wakaingia pamoja na wazazi wamsichana huyo kwenye gari hilo.Gari likawashwa na kuanza kuondokahospitalini hapo kuelekea uwanja wa ndegehuku wanachuo wengi waliokuwa wakisomapamoja na msichana huyo wakiwawanashuhudia kila kilichokuwa kinaendelea ,wengine wakitokwa na machozi ya uchungu.

Hali ilikuwa mbaya zaidi kwa Dickson ambayemuda wote alikuwa akilia kama mtoto mdogona kusababisha macho yake yabadilike rangina kuwa mekundu huku yakiwa yamevimba .“ Jikaze Dickson, ukilia sana utakuwaunamkufuru Mungu wako, piga moyo kondena tuendelee kumuombea kwa Mungu ataponatu, ” mwanachuo mmoja aliyekuwa akikaachumba kimoja na Dickson alimfariji kijanahuyo ambaye alionekana kuumia sana ndaniya moyo wake .Baada ya kutoka kwenye eneo la hospitali ,gari lililokuwa limembeba Dickson lilianzakupiga ving ’ ora kwa nguvu na kusababishamagari mengine yapishe njia. Likazidikuchanja mbuga kuwahi uwanja wa ndege .Baada ya dakika kadhaa, tayari gari hilolilikuwa limeshawasili Uwanja wa Ndege waKimataifa wa Julius Nyerere ambapo garililisogea mpaka kwenye mlango maalum wakuingilia uwanjani hapo .

Kwa kuwa tayari wahudumu wa uwanja huowalikuwa na taarifa juu ya mgonjwa huyo,walisaidiana kumteremsha kwenye gari, babayake akaenda kukamilisha taratibu zote zakiusalama kisha akapelekwa moja kwa mojakwenye ndege kubwa ya IndianAirways. Akaingizwa mpaka kwenye chumbamaalum na kulazwa huku yule daktariakiendelea kumhudumia .
 
SEHEMU YA 19

Jioni moja , msichana huyo anamfuma Dicksonkwa macho yake akinunua changudoa nakuingia naye gesti. Mshtuko anaoupata,unasababisha apoteze umakini na kujikutaakigongwa na gari linalomjeruhi vibaya.Anakimbizwa hospitalini lakini hali inazidikuwa mbaya . Wazazi wa msichana huyowanaamua kumsafirisha kwenda nchini India.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Gari la kubebea wagonjwa lilikuwa likipigaving ’ ora kwa nguvu huku taa zote zikiwazimewashwa , likawa linachanja mbuga kwakasi kuelekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifawa Julius Nyerere. Muda mfupi baadaye, tayarililikuwa limewasili kwenye uwanja huo ambapolilisogea mpaka kwenye mlango maalum wakuingilia uwanjani hapo .Kwa kuwa tayari wahudumu wa uwanja huowalikuwa na taarifa juu ya mgonjwa huyo, walisaidiana kumteremsha kwenye gari, babayake akaenda kukamilisha taratibu zote zakiusalama ambapo baada ya tiketi na hati zakusafiria za wote waliokuwa wakisafirikukaguliwa, msichana huyo alipelekwa mojakwa moja kwenye ndege kubwa ya IndianAirways.

Akaingizwa mpaka kwenye chumba maalumna kulazwa huku yule daktari akiendelea kumhudumia. Muda mfupi baadaye, ndege hiyo ilianza kujongea taratibu kuelekea kwenye njia za kurukia, ikazidi kuongeza kasi huku injini zake kubwa zikitoa muungurumo mkubwa, baadaye ikapaa na kuiacha ardhi ya Tanzania. Ikawa inapasua mawingu kuelekea nchini India huku msichana Neema bado akiwa kwenyehali yake ya kutojitambua.* * *“ Jikaze Dickson, ukilia sana utakuwa unamkufuru Mungu wako, atakuwa sawa tu, madaktari wa India wanasifika kwa ufanisi nahakuna kinachoweza kuwashinda , tuendeleekumuombea kwa Mungu, ” rafiki yake Dickson waliyekuwa wakikaa naye chumba kimoja ,alimbembeleza mwenzake baada ya kumuona akiwa kwenye hali mbaya sana kihisia.

Muda wote alikuwa akilia tu, hata chakulahakutaka kula wala hakutaka kwenda darasanikujisomea, ungeweza kudhani amepokeahabari za msiba wa mama au baba yake kwajinsi alivyokuwa na huzuni.Licha ya jitihada kubwa za kumbembelezakufanyika , bado Dickson au Zinja aliendeleakulia muda wote, macho yake ya kutishayakazidi kuwa mekundu na kuzidi kumfanyaawe na mwonekano wa ajabu .

Kama ndiyo ungemuona kwa mara ya kwanza ,ungeweza kudhani ni mnyama mkali wamwituni anayekaribia kusababisha madharamakubwa kwa binadamu.* * *Ndege kubwa ya Indian Airways iliendeleakupasua mawingu kwa kasi kubwa, ikikatizajuu ya Bahari ya Hindi kuelekea nchini Indiaambako msichana Neema alipangwakupelekwa kwenye Hospitali ya Apollo jijiniMumbai kwa matibabu .“ Mabibi na mabwana, ahsanteni kwa kuchaguakusafiri na ndege ya Shirika la Indian Airways ,muda mfupi baadaye, tutakuwa tukitua kwenyeUwanja wa Ndege wa Kimataifa wa ChatrapatiShivaji jijini Mumbai , India , tafadhali abiriawote mnaombwa kufunga mikanda wakatindege ikijiandaa kutua, ahsanteni sana , ” sautinyororo ya mhudumu wa kike wa ndegeilisikika ikiwataarifu abiria wote kilichokuwakinaendelea .

Abiria wakaanza kufunga mikanda kamawalivyoelekezwa, msichana Neema ambayealikuwa kwenye chumba maalum akiendeleakupewa uangalizi wa karibu na daktarialiyesafiri naye kutoka jijini Dar es Salaam, naye alifungwa mikanda maalum iliyokuwakwenye kitanda chake.Muda mfupi baadaye, ndege ilianza kuinamaupande wa mbele na kuanza kushuka chinikwa kasi, ikaendelea kufanya hivyo kishaikatingishika kidogo na kurudi kwenye usawawake kuashiria kwamba tayari ilishatua kwenyeardhi ya Jiji la Mumbai .

Ilikimbia kwa kasi na baadaye ikaanzakupunguza mwendo kabla ya kusimamakabisa mbele ya jengo kubwa lililokuwa namaandishi yaliyosomeka Chatrapati ShivajiInternational Airport, Mumbai .Baada ya kusimama kabisa, milangoilifunguliwa ambapo magari yenye ngaziyalisogezwa kisha abiria wakaanza kuteremka.Wahudumu wa ndege pamoja na wale wauwanja huo , walisaidiana kuteremsha kitandacha matairi ambacho juu yake alikuwaamelazwa msichana Neema akiwa hajitambuikabisa.Baada tu ya kuteremshwa, wahudumu haowalianza kukisukuma kitanda hicho kwa kasikuelekea kwenye mlango maalum wa kutokeakwani tayari taarifa zake zilishakuwepouwanjani hapo .

Wazazi wake pamoja nadaktari aliyekuwa akimhudumia, wao wakawawanakimbia kuelekea kwenye mlango wakawaida wa kuingilia sehemu ya ukaguzi .Wakawa abiria wa kwanza kukaguliwa ambapobaada ya taratibu zote za kiusalamakukamilika , walitoka mpaka nje ambapowaliwakuta madaktari wengine wawilinamanesi wawili waliokuwa wamevalia sare zaHospitali ya Apollo, wakiwa kwenye harakatiza kumpakiza mgonjwa kwenye ambulanceiliyokuwa na maandishi makubwa ubavuniyaliyosomeka Apollo Hospital , Mumbai.Muda mfupi baadaye, ambulance hiyoiliondoka kwa kasi uwanjani hapo, huku taazote zikiwa zimewashwa na ving ’ ora vikipigakelele kwa nguvu, magari mengine yakawayanaipisha kama sheria za usalama barabaranizinavyosema .

Watu wengine waliosalia pale uwanjani ,walipanda kwenye gari jingine ambalo nalolilikuwa na maandishi ubavuni yaliyosomekaApollo Hospital , Mumbai na kuondoka kwakasi kuelekea kule ambulance ile ilikoelekea.Kila mmoja alikuwa kimya kabisa ndani yagari, wazazi wake wakawa wamejiinamia chinihuku kila mmoja akiendelea kumsaliakimyakimya binti yao huyo ili aamke kutokakwenye usingizi wa mauti aliokuwa amelala .Dakika kadhaa baadaye, tayari walikuwawamewasili kwenye Hospitali ya Apollo, Mumbai ambapo gari la wagonjwa alilokuwaamepakizwa Neema , lilipitiliza moja kwa mojampaka sehemu iliyokuwa na maandishimakubwa ukutani yaliyosomeka ‘ EmergencyPatients’ yakimaanisha sehemu ya kupokeleawagonjwa wa dharura.Taratibu za kumpokea msichana huyo zikaanza kufanyika ambapo muda mfupi baadaye, tayari alikuwa ameingizwa kwenye wodi ya wagonjwa mahututi, madaktari bingwa zaidi ya wanne wakaanza kazi ya kumfanyia upya vipimo kubaini alikuwa na tatizo gani.

Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 20

Jioni moja, msichana huyo anamfuma Dicksonakinunua changudoa, mshtuko anaoupataunasababisha muda mfupi baadaye agongwena gari . Matibabu yake hayawi mepesi , haliinayolazimu asafirishwe kwenda India.

Je, ninikitafuatia? SONGA NAYO

Baada ya ndege kubwa ya Indian Airwayskuwasili kwenye Uwanja wa Ndege waKimataifa wa Chatrapati Shivaji jijini Mumbai,India , msafara kutoka nchini Tanzaniauliokuwa umemsafirisha msichana Neema kwamatibabu, ulipokelewa na timu ya madaktarina wauguzi kutoka Hospitali ya Apollo .Harakaharaka akapakizwa kwenye gari lakubebea wagonjwa na safari ya kuelekeakwenye hospitali hiyo ikaanza . Dakika kadhaabaadaye, tayari walikuwa wamewasili kwenyeHospitali ya Apollo , Mumbai , Neemaakapokelewa na kulazwa kwenye kitanda chamagurudumu na kukimbizwa kwenye wodi yawagonjwa mahututi .

Madaktari bingwa zaidi ya wanne wakaanzakazi ya kumfanyia upya vipimo kubaini alikuwana tatizo gani . Akafanyiwa vipimo vyotekuanzia X - Ray, MRI (Magnetic ResonanceImaging), CT Scan (Computerized TomographyScan) na vingine vingi ambavyo madaktariwaliona vinafaa kutoa majibu ya uhakika yakilichokuwa kinamsumbua .Kutokana na ubora wa vifaa vyote vya kupimiawagonjwa vilivyokuwepo hospitalini hapo,muda mfupi tu baadaye, tayari majibu yoteyalikuwa yametoka.

Jopo la madaktariwaliopewa jukumu la kumtibu likakutanakuyajadili majibu ya vipimo vyotealivyochukuliwa .“ She got severe injuries in her spinal cord ,vertebrae and the skull. ” (Amepata majerahamakubwa kwenye uti wake wa mgongo, pingilina fuvu la kichwa)“ What? Ooh my God. ” (Niniii ? Mungu wangu )mmoja kati ya madaktari waliokuwawakijadiliana kuhusu matokeo ya msichanahuyo, alijikuta akishindwa kuzizuia hisia zake.Alielewa vizuri athari za madhara aliyokuwaameyapata. Daktari wa awali aliyekuwa akiwasomeawenzake matokeo hayo, Siddharth Shivam ,aliendelea kutoa ufafanuzi wa kitaalamu kwawenzake.

“ The bundle of nerves that extenddownward from the spinal cord which is called Cauda Equina are injured too ,” (Neva zake zafahamu zinazopita kwenye uti wa mgongokutokea kichwani kuelekea kiunoni ziitwazoCauda Equina nazo zimejeruhiwa pia ) alisemadaktari huyo, kila mmoja akashusha pumzindefu kwani kazi iliyokuwa mbele yao haikuwanyepesi.Kwa maelezo hayo, jambo ambalo lilikuwa nilazima limtokee msichana huyo ilikuwa nikuendelea kupoteza fahamu kwa kipindi kirefu,mwili kupooza na kupoteza uwezo wa kuinukakitandani, kuhisi, kuona, kukumbuka walakuzungumza chochote.

Kila mmoja alionekanakumsikitikia msichana huyo kwani alikuwabado mdogo kustahili mateso makubwa kiasihicho.“ Administer her with analgesics ,Acetaminophen 3cc syringe thrice a day andconnect her to effective Oxygen pumpingmachine while we prepare ourselves forsurgery as soon as possible . ”(Mchomeni sindano ya kupunguza maumivu, Acetaminophen sentimita tatu za ujazo, maratatu kwa siku na muunganisheni na mashineya Oxygen yenye nguvu wakati tukijiandaakumfanyia upasuaji haraka iwezekanavyo) alisema Dokta Shivam, harakaharaka manesiwakatii walichoambiwa huku wakizingatiamaelekezo aliyowapa kwamba msichana huyohakutakiwa kutingishwa au kugeuzwa kwanamna yoyote ili kuzuia uti wake wa mgongousizidi kupata madhara zaidi.

Neema ambaye hakuwa na fahamu hatakidogo, alichomwa sindano ya kuzuiamaumivu kisha akabadilishiwa mashine yaOxygen na kuwekewa nyingine yenye nguvuzaidi. Jopo la madaktari waliopaswakumshughulikia mgonjwa huyo, wakaingiakwenye chumba maalum kuelekezana nini chakufanya kwani hali ya mgonjwa wao ilikuwaikihitaji umakini wa hali ya juu, vinginevyomaisha ya msichana huyo yalikuwa hatarini.

Baada ya kuelekezana kwa zaidi ya saa tatukwa nadharia, huku wakitumia vipimo vyamsichana huyo kuoneshana nini cha kufanyana kugawana majukumu ya kila mmoja pindiwatakapoingia kwenye chumba cha upasuaji ,hatimaye madaktari hao wakiongozwa nadaktari bingwa wa mifumo ya fahamu(neurosurgeon ), Dk . Shivam walitoka nakuelekea kwenye vyumba vya maandalizi .Manesi nao wakamtoa Neema kwa tahadharikubwa kutoka kwenye wodi ya wagonjwamahututi na kupelekwa kwenye wodi ya kisasaya upasuaji. Muda mfupi baadaye, madaktariwote walikuwa tayari wameshaingia kwenyewodi hiyo , manesi nao wakawa wanapiganavikumbo huku na kule kuhakikisha vifaa vyotemuhimu vilivyokuwa vinahitajika , vipo sehemuyake.Kwa muda wote huo, wazazi wa Neemawalikuwa nje wakiendelea kumuomba Munguwao atende miujiza.

Licha ya uwezo mkubwawa kifedha waliokuwa nao, Neema ndiyealiyekuwa mtoto wao wa kipekee na hakunaaliyekuwa tayari kuona anapoteza maishawakati uwezo wa kumsaidia walikuwa nao.“ Wakishindwa hapa India ni bora hata tusafirinaye kuelekea Uingereza , lazima mwananguapone , ” alisema baba mzazi wa msichanahuyo huku akimbembeleza mkewe ambayemuda wote alikuwa akisali huku akilia kwauchungu.Muda mfupi baadaye, madaktari waliianza kazingumu na ya hatari ya kumfanyia upasuajimsichana huyo, kuanzia kwenye fuvu lakichwa mpaka kwenye uti wa mgongo ambaovipimo vilionesha kwamba umeathirika zaidikuliko sehemu nyingine .* * *Wakati hayo yakiendelea nchini India ,Tanzania hali ilikuwa mbaya sana kwaDickson.

Hakutaka kula wala kuingia darasani ,bado moyo wake ulikuwa na majonzimakubwa kuhusu kilichomtokea Neema,msichana pekee aliyetokea kumpenda nakumuonesha mapenzi ya dhati licha ya surana mwonekano wake wa kutisha uliosababishawengi wamuogope. Juhudi za wanachuo wenzake pamoja nauongozi wa serikali ya wanafunzi wa ChuoKikuu cha Dar es Salaam alichokuwa akisomeakujitahidi kumrudisha kwenye hali yake yakawaida, zilionekana kugonga mwamba ,mwisho kila mmoja akaamua kumuachiamwenyewe.

Itaendelea...
 
SEHEM YA 21

Akinunua changudoa, mshtuko anaoupataunasababisha muda mfupi baadaye agongwena gari . Matibabu yake hayawi mepesi , haliinayolazimu asafirishwe kwenda India ambakojopo la madaktari linaingia kazini kuokoamaisha ya msichana huyo.Upande wa pili, Dickson anaoneshakuchanganywa mno na kilichotokea , kiasi chakupoteza hamu ya kufanya jambo lolote.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Siku zilizidi kusonga mbele huku Dickson auZinja akiendelea kuteseka ndani ya moyo wakekutokana na hali aliyomuona nayo mara yamwisho Neema . Hata hivyo, kama wahengawasemavyo kwamba hakuna daktari mzurikama muda , kadiri siku zilivyokuwa zinazidikusonga mbele ndivyo majeraha aliyokuwanayo Dickson ndani ya moyo wake yalivyozidikupungua.

Akaanza kuona kama kila kilichotokea kilikuwani kitu cha kawaida na kilitokea kwa sababumaalum. Ule uchangamfu wake ukaanzakurudi taratibu, akaanza upya kuhudhuriadarasani na kushirikiana na wenzake kwenyemambo mbalimbali kama ilivyokuwa kawaidayake kabla Neema hajapatwa na ajali mbayaya kugongwa na gari.Mara chache alizokuwa anamkumbuka Neema ,alikuwa akijisikia vibaya ingawa hali haikuwambaya kama ilivyokuwa mara ya kwanza. Kwakipindi kirefu, alikuwa akiendelea kupiganamba ya simu ya baba yake Neema aliyopewa siku walipokutana Hospitali yaMuhimbili kabla Neema hajasafirishwa kwendaIndia lakini mara zote, namba hiyo haikuwaikipatikana hewani .* * *Jopo la madaktari kadhaa , wakiongozwa nadaktari bingwa wa mifumo ya fahamu(neurosurgeon ), Dk . Siddharth Shivamwaliendelea na kazi ngumu ya kumfanyiaupasuaji msichana mdogo, Neema , ndani yaHospitali ya Apollo , Mumbai nchini India.

Kazi haikuwa nyepesi kwani maeneoaliyokuwa ameathirika , hasa kwenye uti wamgongo, kulikuwa na mishipa mingi yafahamu ambayo ilihitaji umakini wa hali ya juukatika kuishughulikia kwani hitilafu yoyoteambayo ingetokea wakati wa upasuaji huoingeweza kuhatarisha maisha ya msichanahuyo mdogo , jambo ambalo hakuna aliyekuwatayari kuona linatokea.Baada ya takribani saa nane, hatimayemsichana huyo alitolewa kwenye chumbahicho cha upasuaji , akiwa amepandikizwavyuma maalum kwenye uti wake wa mgongokwa ajili ya kushikilia pingili za mifupa mpakazitakapojiunga na kuwa kama awali. Kutokana na aina ya upasuaji wenyewe ,manesi walipewa angalizo la kuhakikisha kuwamsichana huyo hatingishiki hata kidogo,akafungwa kwa mikanda maalum kwenyekitanda hicho na kusukumwa taratibu kuelekeakwenye wodi ya wagonjwa mahututi ambakoalilazwa .

Siku zilizidi kusonga mbele huku Neema akiwabado hajarejewa na fahamu zake. Hakuwa nauwezo wa kufanya jambo lolote, kila kitualisaidiwa na mashine maalum alizokuwaameunganishwa nazo pale kitandani kwake,kuanzia kula , kupumua mpaka kutoa hajandogo na kubwa. Alikuwa kwenye usingizi mzito wa kifo, akiwahaelewi chochote kilichokuwa kikiendeleakatika ulimwengu wa kawaida. Wazazi wakekamwe hawakumkatia tamaa, kila siku wakawawanamuombea kwa Mungu hukuwakihakikisha anapatiwa kila kitu kilichokuwakinahitajika kwenye matibabu yake.

Baada ya kulala kitandani akiwa hana fahamukwa zaidi ya miezi miwili, huku kila sikumadaktari wakiendelea kumfanyia uchunguziwa karibu kuonesha maendeleo ya afya yake,hatimaye jioni moja msichana huyo alifumbuamacho, jambo lililoamsha shangwe kubwa kwawazazi wake.“ Siamini macho yangu , siamini mume wangu, ”alisema mama mzazi wa msichana huyo hukuakimkumbatia mumewe kwa nguvu, akitokwana machozi mengi. Kuzinduka kwa Neemakulikuwa ni zaidi ya miujiza .Madaktari ambao nao walikuwa wakihangaikausiku na mchana bila kupata hata muda wakupumzika , walipongezana sana kwa kitendocha msichana huyo kurejewa na fahamu zake. Wakawa wanaendelea kumfanyia vipimombalimbali lakini baadaye wakagundua kituambacho hakikuwafurahisha sana.

Licha ya msichana huyo kuzinduka lakinivipimo vilionesha kwamba itamchukua mudamrefu kurudi kwenye hali yake ya kawaidakwani uti wake wa mgongo ulikuwa ukiponakwa kasi ndogo sana .Jambo hilo lilimaanisha kwamba angechelewasana kurejewa na fahamu zake, kuwa nauwezo wa kuinuka mwenyewe kitandani nauwezo wa kuzungumza kama ilivyokuwamwanzo kabla hajapata ajali hiyo .Baada ya majadiliano ya muda mrefu nawazazi wa msichana huyo, walikubalianakwamba kwa sababu itamchukua muda mrefumsichana huyo kupona, ni bora warudi nayenyumbani ambako daktari maalum atakuwaakifuatilia maendeleo yake na kuwasiliana namadaktari hao moja kwa moja nchini India.

Lengo la kufanya hivyo ilikuwa ni kupunguzagharama na kumuepusha msichana huyo asijeakapata magonjwa mengine kwa kuendeleakukaa zaidi hospitalini hapo. Wazazi wakewalikubaliana na ushauri huo wa kitaalamu nakwa sababu tayari walikuwa na daktari waowaliyesafiri naye kutoka nchini Tanzaniaambaye aliondoka mara tu baada ya upasuajiwa msichana huyo kukamilika , waliwasiliananaye wakiwa hukohuko nchini India .Daktari huyo akapewa maelekezo na wenzakewaliokuwa nchini India juu ya namna yakumshughulikia mgonjwa huyo.

Baada yamakubaliano kufikiwa, taratibu za kurejeanchini Tanzania zilianza kufanywa, hukuhospitali hiyo ikigharamia mambo mengi, ikiwemo usafiri wa kumpeleka mpaka uwanjawa ndege na gharama za kitabibu kwa mudawote wa safari mpaka msichana huyoatakapowasili nchini Tanzania. Safari ilianza kutoka hospitalini hapo ambapokutokana na wazazi wa msichana huyo kukaamuda mrefu wakimuuguza mtoto wao, walishazoeana na madaktari na manesi , watuwengi walishikwa na huzuni kutokana nakuondoka kwao, wakawasindikiza nakuwatakia kila la heri katika maendeleo yamtoto wao.

Neema akapakizwa kwenye ‘ ambulance ’ nakupelekwa mpaka Uwanja wa Ndege waKimataifa wa Chhatrapati Shivaji jijini Mumbai.Kwa kuwa tayari tiketi za ndege na taratibuzote za usafiri zilishakamilika, hawakukaa sanauwanjani hapo , Neema akapitishwa kwenyelango maalum akiwa kwenye kitanda chamagurudumu huku akiwa amefungwa mikandamaalum ya kumzuia asitingishike. Akapelekwa moja kwa moja mpaka kwenyendege ambako alipelekwa kwenye chumbamaalum na kuwekwa chini ya uangalizimaalum. Abiria wengine nao wakapanda ,wakiwemo wazazi wake na muda mfupibaadaye, ndege kubwa ya Shirika la Indian Airways ikapaa kuelekea nchini Tanzania .

Je, nini kitafuatia?
 
SEHEM YA 22

Upasuaji mkubwa unafanyika lakini bado haliya msichana huyo inaonesha kulegalega .Baadaye madaktari wanashauriana na wazaziwake kumrudisha nyumbani Tanzaniakuendelea na matibabu akiwa nyumbani .

Je , nini kitafuatia? SONGA NAYO…


Baada ya taratibu zote kukamilika, Neemaalipelekwa moja kwa moja mpaka kwenyendege ambako aliingizwa kwenye chumbamaalum na kuwekwa chini ya uangalizimaalum wa daktari. Abiria wengine naowakapanda, wakiwemo wazazi wake na mudamfupi baadaye, ndege kubwa ya Shirika laIndian Airways ikapaa kuelekea nchini Tanzania.“ Sitaki mtu yeyote ajue kinachoendeleakuhusu mtoto wetu, si unajua tena mambo ya Kiswahili , wanaweza kummalizia bure !” mamamzazi wa Neema alimwambia mumewewakiwa angani, wakati ndege waliyopandaikiendelea kupasua mawingu kuelekea nchiniTanzania. Kwa jinsi alivyokuwa anampenda mkewe, alikubaliana naye na kwa pamoja wakafikiamuafaka kwamba watakapofika nchiniTanzania, kila kitu kitafanyika kwa usirimkubwa.

Baada ya kusafiri saa nyingi angani ,hatimaye waliwasili kwenye Uwanja wa Ndegewa Kimataifa wa Julius Nyerere ambapo Neema alipokelewa na daktari wake ambayealikuja na gari maalum la kubebea wagonjwauwanjani hapo akiwa sambamba na dereva .Msichana huyo akashushwa kwenye ndegekwa tahadhari ya hali ya juu, akiwa amefungwakwa mikanda maalum kwenye kitandaalichokuwa amelala juu yake, akatolewataratibu mpaka nje na kupakizwa kwenye garila kubebea wagonjwa lililokuwa limeandaliwakwa ajili yake. Akasafirishwa kwa umakini mkubwa mpakaMasaki, yalipokuwa makazi ya familia yake.

Kwa kuwa tayari baba yake alishafanyamawasiliano na wafanyakazi wake waliokuwanchini Tanzania tangu akiwa India , kila kitukilikuwa kimeshaandaliwa .Akaingizwa mpaka kwenye chumba maalumkilichokuwa kimetengenezwa maalum kwa ajiliya kumhudumia Neema , kikiwa na vifaa vyotemuhimu kama chumba cha wagonjwamahututi hospitalini .Kwa jinsi mpango wa kumsafirishaulivyofanywa kwa siri kubwa, ni watuwachache sana waliokuwa na taarifa kwambamsichana huyo tayari amesharejea nyumbanikwao. Kila kitu kiliendelea kufanyika kwa usirimkubwa huku akiendelea kupatiwa matibabuna daktari wake ndani ya chumba hicho.***Siku zilizidi kusonga mbele huku Dickson auZInja akiendelea na masomo yake.

Zile hisiachungu kuhusu Neema zilizidi kupungua kadirisiku zilivyokuwa zinayoyoma na sasa alikuwana uwezo wa kusoma vizuri kama zamani .Mara chache alizokuwa akimkumbuka Neema ,alikuwa akijaribu kupiga namba za simu zababa yake lakini hazikuwa zikipatikana, akawana imani kubwa kwamba bado wapo kwenyematibabu nchini India .Siku moja jioni, alijaribu tena kupiga nambaya simu ya baba yake Neema ambapo katikahali ambayo hakuitegemea, simu hiyo ilianzakuita . Mapigo ya moyo wake yakawayanamuenda mbio huku akiwa na shaukukubwa ya kusikia taarifa juu ya maendeleo yaNeema.“ Haloo !” sauti nzito ya mwanaume ilisikikabaada ya simu kupokelewa.

Huku akitetemeka,Dickson alimwamkia mwanaume huyo ambayebila hata kuuliza alijua ni baba yake Neema .Jambo la kwanza baada ya salamu , ilikuwa nikumuuliza kuhusu maendeleo ya Neema .Hata hivyo , tofauti na alivyotegemea , mzazihuyo wa Neema alimjibu kwa kifupi kwambayeye hajui chochote kwa sababu amerejeaTanzania na Neema bado anaendelea kutibiwanchini India. Akamwambia kwa muda huoalikuwa na kazi nyingi hivyo aulizwe sikunyingine .Kwa kuwa tayari Dickson alishakuwa na akiliza kiutu uzima , alielewa tafsiri ya majibu yamzee huyo kwamba hakuwa akipendakuulizwa habari kuhusu mwanaye.

Alijisikiavibaya sana ndani ya moyo wake lakinihakuwa na cha kufanya , akaamua kupigamoyo konde na kuendelea na masomo .Siku zilizidi kuyoyoma, Dickson au Zinja kamawanachuo wenzake walivyokuwa wamezoeakumuita, akawa anaendelea na masomo nahatimaye , alihitimu Shahada ya Kwanza yaSheria . Kwa kuwa ndoto zake za siku nyingizilikuwa ni kuingia jeshini , aliamua kutimizandoto zake ambapo alirudi nyumbani kwaowakati akiendelea kufanya maandalizi yakujiunga na mafunzo ya jeshi la polisi. Miezi michache baadaye, Dickson alipatanafasi ya kujiunga na Chuo cha Mafunzo yaPolisi Moshi (CCP). Baada ya maandalizi yotekukamilika, alisafiri mpaka mkoani Kilimanjarokilipokuwa chuo hicho na kwenda kuripoti .

Akaungana na wanachuo wengine wengikuyaanza mafunzo ya kijeshi.Awali alipata shida sana kwani tayarialishazoea kukutana kimwili na machangudoamara kwa mara lakini sheria za jeshinizilikuwa kali mno kiasi kwamba hakupata hataupenyo wa kufanya mchezo huo aliouzoea.Njia pekee aliyokuwa anaitumia kukidhi hajazake, ikawa ni kujichua kama alivyokuwaakifanya kipindi alichokuwa anasomasekondari. Hata hivyo, hata nafasi ya kufanya mchezohuo pia ilikuwa ikipatikana kwa mbinde sanakwani muda mwingi alikuwa akibanwa naratiba ya jeshini ambapo kila siku walikuwawakiamshwa alfajiri na mapema na kuanzakucheza kwata kwa saa nyingi mfululizo.

Baada ya hapo, walikuwa wakipata kifunguakinywa kisha kuendelea na mazoezi mengineikiwemo kupanda Mlima Kilimanjaro hukumgongoni kila mtu akiwa na begi lenye mawemazito, mazoezi ambayo ama kwa hakikayalikuwa yakimchosha sana.Muda pekee waliokuwa wakipumzika ilikuwa nikuanzia saa nne za usiku ambapo sikunyingine alikuwa akishindwa kufanya mchezohuo kutokana na jinsi alivyokuwa anachokakwa msoto wa kutwa nzima jeshini. Siku zilizidi kusonga mbele , hatimaye mweziwa kwanza ukaisha, Dickson akiwa badoanaendelea na mafunzo ya kijeshi. Hata hivyo ,hamu ya kukutana kimwili na mwanamkeiliendelea kumsumbua , ikafika kipindi akawaanafanya makosa ya kizembe kwa sababu yaakili yake kufikiria jambo hilo kupitakiasi .“ Lazima leo nitoroke niende uraiani kutafutamwanamke wa kuipooza nafsi yangu, siwezikuishi maisha haya, nimechoka kuvumilia , ”aliwaza Dickson jioni moja wakiwa kwenyemazoezi ya kulenga shabaha .

Je, nini kitafuatia?
 
SEHEM YA 23

Upasuaji mkubwa unafanyika lakini bado hali ya msichana huyo inaonesha kulegalega . Baadaye madaktari wanashauriana na wazazi wake kumrudisha nyumbani Tanzania kuendelea na matibabu akiwa nyumbani.
Upande wa pili, hatimaye Dickson au Zinja anafanikiwa kuhitimu chuo na baada ya hapo anaenda kujiunga na Chuo cha Polisi mjini Moshi, Kilimanjaro lakini usiku mmoja, uzalendo unamshinda na kuamua kutoroka chuoni kwenda mitaani kutafuta machangudoa.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Muda mfupi baadaye , Dickson alikuwa kama alivyotoka kwenye tumbo la mama yake , ndani ya chumba cha gesti akiwa na changudoa , akamsogelea mwanamke huyo ambaye naye alimalizia kutoa nguo yake ya mwisho , wakakumbatiana lakini kabla hawajafanya chochote, wote wawili walishtuka baada ya kusikia mlango wa chumba walichokuwemo ukigongwa kwa nguvu.
“ Nani!”
“ Fungua, ” sauti ya zaidi ya wanaume sita ilisikika kutokea nje ya chumba cha gesti ambacho Dickson au Zinja alikuwa ndani na mwanamke huyo anayefanya biashara haramu ya kujiuza , aliyemnunua muda mfupi uliopita kwenye mtaa maarufu kwa biashara hiyo , Majengo, Moshi mkoani Kilimanjaro.

“ Mungu wangu , ” alisema Dickson baada ya kufunua pazia kidogo na kuchungulia nje ambapo alishuhudia kundi la wanaume , wengine wakiwa na silaha za jadi, wakiwa wameuzingira mlango wa chumba alichokuwa amejifungia na mwanamke huyo .“ Kwani kuna nini?” mwanamke huyo aliuliza huku naye akisogelea dirishani hapo, wote wakiwa kama walivyotoka kwenye matumbo ya mama zao.

“ Yeleuwiiii, mume wangu! Mume wangu ametufumania, ” alisema mwanamke huyo kwa lafudhi ya wenyeji wa mkoa huo .“ Mume wako ? Kwani wewe umeolewa ?”

“ Ndiyo nimeolewa lakini mume wangu huwa anasafiri halafu haniachii pesa za matumizi ndiyo maana huwa nakuja kujiuza , ” alisema mwanamke huyo huku akionesha dhahiri hofu kubwa aliyokuwa nayo ndani ya moyo wake .
Kwa kasi ya ajabu, Dickson alikimbilia nguo zake, akazivaa huku mlango ukiendelea kugongwa kwa nguvu .
“ Tunahesabu mpaka tatu , usipofungua tunavunja mlango, ” sauti ya mwanaume mmoja aliyeonekana kuwa na mamlaka kuliko wenzake ilisikika, wakati Dickson akimalizia kuvaa nguo zake.

Kufumba na kufumbua, mlango wa chumba hicho cha gesti ulivunjwa, wanaume wenye hasira wakavamia huku kila mmoja akipiga kelele za ‘mgoni !’ Mgoni ! Mwizi wa wake za watu leo amepatikana !’ “ Jamani mimi sikujua ka …” Dickson alijaribu kujitetea lakini ilikuwa sawa na kazi bure, ngumi nzito ilitua kwenye uso wake, sauti yake ikamezwa na watu hao ambao tayari walishamtia mikononi na kuanza kumshushia kipigo kwa kumgombania kama mpira wa kona .

Yule mwanamke alipata upenyo na kutoroka , akamuacha Dickson peke yake akiendelea kuchezea kichapo kutoka kwa wanaume hao walioonesha kumpania kwelikweli. Japokuwa alikuwa ameiva kwa mafunzo ya kijeshi , hakutaka kuyatumia kumjeruhi yeyote kwani alikuwa anajua fika kwamba ni kosa kisheria .

Hata hivyo , alipoona hali inaanza kuwa mbaya kwake , hakuwa na namna zaidi ya kujitetea. Kwa kasi ya ajabu akafungua mkanda wa kijeshi aliokuwa ameuvaa kiunoni na kuanza kuwatawanya watu hao ambao walishaonesha nia ya kumdhuru kutokana na jinsi walivyokuwa wanampiga kwa hasira kama mwizi.

“ Ana mkanda wa jeshi, jamani klumbe ni mwanajeshi…” alisema mwanaume mmoja baada ya kukoswakoswa na mkanda huo lakini alikuwa ameshachelewa kwani Dickson alishapandisha hasira zake , ndani ya sekunde chache tu , tayari alikuwa amefanikiwa kuwaangusha watu wote waliokuwa ndani ya chumba hicho, huku kila mmoja akiwa amejeruhiwa vibaya.

Wakati anataka kukimbia, mmoja kati ya wale wanaume aliyefanikiwa kutoka nje ya chumba cha gesti , alimnyooshea upinde uliokuwa na mshale wenye sumu , akamtaka kusalimu amri vinginevyo atamjeruhi vibaya. Kwa kasi ya ajabu, Dickson aliurusha ule mkanda wake na kumpiga nao mwanaume huyo kichwani, akadondoka chini na kupiga kelele zilizowakusanya watu wengi. Dickson hakuwa na ujanja zaidi ya kuanza kutimua mbio, akakimbia na mita chache mbele, alipotelea kwenye mashamba ya migomba na kuendelea kutimua mbio kuelekea kambini.
Dakika kadhaa baadaye, tayari alishawasili kambini, akapitia kwenye njia ileile aliyoitumia kutorokea na kutambaa mpaka ndani ya eneo la jeshi, huku mwili mzima akiwa amechafuka vibaya kutokana na kuanguka mara kadhaa wakati akikimbia kwenye mashamba ya migomba.

Ebwana vipi mbona umechafuka kiasi hicho?” askari mmoja ambaye naye alikuwa mafunzoni kama Dickson , alimuuliza swali ambalo hakulitegemea baada ya kumkuta amejibanza kwenye korido ya mabweni yao , akitafuta njia ya kuingia bila kugundulika na wakufunzi wao. “ Nilikuwa shambani, ” Dickson alidanganya huku akijitahidi mwenzake huyo asimuone usoni. Hatimaye akafanikiwa kuingia mpaka ndani ambapo alienda kubadilisha nguo, akaenda kuoga kisha akaenda kuziloweka nguo hizo bafuni na kuzifua usiku huohuo ili kupoteza ushahidi.

Kesho yake asubuhi , wananchi kadhaa waliwasili kwenye kambi hiyo ya jeshi , huku wengi wakionesha kuwa na majeraha makubwa miilini mwao . Wakaomba kukutana na mkuu wa chuo hicho aliyekuwa akisifika kwa ukali kiasi cha wanachuo kumtungia jina la Pilipili Kichaa. Baada ya kuwasilikiza malalamiko yao pamoja na kupokea kidhibiti kilichoachwa eneo la tukio na mhusika, cha mkanda wa jeshi uliokuwa umetapakaa damu , mkuu huyo wa chuo aliomba kwanza apewe muda wa kutafakari. Akakaa ndani ya ofisi yake na kutulia kwa dakika kadhaa. Kawaida yake, alikuwa akikasirika sana anacheka mwenyewe kabla ya kuanza kuchukua hatua kali.

Alipoinuka, aliamuru wanajeshi wote waliokuwa mafunzoni ambao asubuhi hiyo walikuwa wakiendelea na mazoezi, kuacha kila kitu walichokuwa wanakifanya na kuelekea ‘Assembly Square’ , eneo maarufu lililokuwa likitumika kwa mikusanyiko ya kusikiliza matangazo . Kutokana na jinsi alivyokuwa amekunja sura, kila mtu akajua kazi ipo siku hiyo.

Je, nini kitafuatia?
 
SEHEM YA 24

Upande wa pili, hatimaye Dickson au Zinja anafanikiwa kuhitimu chuo na baada ya hapo anaenda kujiunga na Chuo cha Polisi mjini Moshi, Kilimanjaro lakini usiku mmoja, uzalendo unamshinda na kuamua kutoroka chuoni kwenda mitaani kutafuta machangudoa ambapo anasababisha mtafaruku mkubwa .

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Baada ya kupata malalamiko hayo , mkuu wa chuo cha polisi alipandwa na hasira kali, akainuka na kuamuru askari wote waliokuwa mafunzoni ambao asubuhi hiyo walikuwa wakiendelea na mazoezi, kuacha kila kitu walichokuwa wanakifanya na kuelekea ‘Assembly Square’ , eneo maarufu lililokuwa likitumika kwa mikusanyiko na kusikiliza matangazo . Kutokana na jinsi alivyokuwa amekunja sura, kila mtu akajua kazi ipo siku hiyo.

Mkuu huyo wa chuo cha mafunzo ya polisi alianza kwa kuwataka watu wote kukaa kwenye mistari kwa ajili ya gwaride la utambuzi . Bila kueleza chochote , alitoa ishara ambapo wanaume zaidi ya wanne , wote wakiwa na majeraha sehemu mbalimbali za miili yao, walitoka kwenye ofisi kuu na kuelekea mpaka pale ‘ Assembly ground’ . Akaanza kuwapitisha kwenye mistari waliyokuwa wamejipanga askari hao waliopo mafunzoni huku akiwahimiza kumtazama kila mmoja kwa umakini ili kumbaini aliyefanya tukio lililochafua mno taswira ya chuo hicho .

Dickson aliyekuwa miongoni mwa askari waliokuwa wamepanga mstari kwa ajili ya gwaride hilo la utambuzi , alikuwa akitetemeka kwa hofu kubwa kwani ni yeye peke yake ndiye aliyekuwa akijua kila kitu kilichokuwa kinaendelea.
“ Eeh Mungu wangu, onesha miujiza yako , ” Dickson alisema huku akiendelea kutetemeka. Japokuwa hakuwa mhudhuriaji mzuri wa nyumba za ibada, siku hiyo alitamani Mungu amfanyie muujiza wowote kwani kwa jinsi alivyokuwa akimfahamu mkuu wao wa chuo , alijua moto utawaka.

Kila alipokumbuka kwamba katika purukushani hiyo kofia yake ilianguka na kusababisha watu wote waione sura yake halisi , alizidi kuishiwa nguvu, akajua lazima atanaswa .Ukaguzi mkali uliendelea huku askari wengi wakongwe wakirandaranda huku na kule kuhakikisha hakuna anayetoroka eneo hilo la ukaguzi .
“ Huyu hapa, ni yeye kabisa. ” “ Ndiyo mwenyewe , sura yake ni hiihii , anafanana na binadamu wa kale, ” wanaume wawili kati ya wale wanne walisema kwa sauti ya juu na kuungwa mkono na wenzao , askari wengi wakamzunguka Dickson huku mkuu wa chuo hicho, akimtazama akiwa ni kama haamini.

Siku zote alikuwa akimchukulia Dickson kama kijana mpole , asiyependa kujichanganya na wenzake na mwenye staha kubwa lakini kumbe haikuwa hivyo , akabaki anamtazama huku jazba zake zikionekana waziwazi .
“ Siyo mimi, wananisingizi …” alisema Dickson lakini kabla hajamalizia kauli yake hiyo , alipigwa mtama na mmoja wa askari aliyekuwa na mwili mkubwa , akadondoka chini kama mzigo, puuuh!

“ Mkanda wako wa kijeshi uko wapi ?” alisema mkuu wa chuo hicho huku akimkagua vizuri Dickson.
“ Nimeibiwa, ” alisema Dickson , kauli iliyozidi kumpandisha hasira mkuu huyo wa chuo . Siku zote hakuna kitu alichokuwa anakichukia kama mtu kushindwa kukiri kosa. Hata hivyo , Dickson hakuwa mwepesi kukiri kosa kwa sababu kwa askari kukubali kirahisi namna hiyo , ulikuwa ni udhaifu mkubwa kutokana na mafunzo waliyokuwa wanapewa .
“ Unaujua huu mkanda?” kiongozi huyo alisema huku akimuonesha Dickson mkanda ulioletwa na wananchi hao kama ushahidi , ukiwa na damu zilizokaukia. Dickson aliutazama ule mkanda kisha akainama chini.

“ Mpelekeni Guantanamo, ” alisema mkuu huyo wa chuo hicho akimaanisha Dickson apelekwe kwenye gereza maalum la jeshi lililokuwa likisifika kwa kutoa adhabu kali na mateso ya hali ya juu kwa wote wanaobainika kuvunja sheria za chuo hicho.

Kitendo hicho kilionesha kumkasirisha mno mkuu huyo wa chuo , mikunjo ikazidi kuongezeka kwenye uso wake . Akawapeleka wale walalamikaji mpaka ofisini kisha akarudi na kuanza kuzungumza na wanachuo wa chuo hicho cha kijeshi .

Akawaeleza jinsi tukio zima lilivyokuwa na akaahidi kumchukulia hatua kali Dickson kwa alichokifanya kwani mbali na kuwasababishia maumivu makubwa raia wasio na hatia, pia alikuwa amechafua sifa ya chuo hicho mbele ya jamii kwa kuonesha kwamba askari wanaofundishwa hapo, hawana maadili ndiyo maana wanafikia hatua ya kwenda kufanya mapenzi na wake za watu mitaani.

Baada ya kumaliza kuzungumza kwa ukali , mkuu huyo wa chuo aliondoka akiwa na askari wengine kadhaa na kuelekea mpaka kwenye gereza la jeshi lililopewa jina la Guantanamo kwa ajili ya kwenda kumshughulikia Dickson .
Huku nyuma , askari wengine waliruhusiwa kuendelea na majukumu yao ambapo kila mmoja alianza kucheka kutokana na tukio lililofanywa na Dickson . Wengi walimuonea huruma kwani walijua mateso atakayoenda kukutana nayo Guantanamo, hayaelezeki .

Baada ya kufikishwa Guantanamo , Dickson alianza kuteswa vikali kwa kuchapwa mijeledi akilazimishwa aeleze ukweli wa kilichotokea. Haikuwa kazi nyepesi lakini kwa kuwa kulikuwa na watalaamu waliobobea katika kazi ya kuwatesa binadamu wenzao , hatimaye Dickson alikiri baada ya kuwa ameteswa sana. Baada ya kukiri, alitolewa Guantanamo mwili wote ukiwa umechakaa kwa mateso, akapelekwa mpaka ofisi kuu, damu nyingi zikimvuja kila sehemu ambapo alilazimishwa kukiri mbele ya waathirika juu ya makosa aliyoyafanya.

Huku akiugulia maumivu makali , Dickson aliwaomba radhi wote aliowajeruhi na kueleza kwamba wakati anakutana na mwanamke huyo , hakujua kama ni mke wa mtu bali alidhani ni changudoa. Watu hao walikubali kumsamehe lakini wakataka kila mmoja alipwe fedha za matibabu ambapo Dickson hakuwa na ujanja zaidi ya kukubali.

“ Chuo kitakusaidia kuwalipa lakini itabidi hizo fedha zikatwe kwenye ada yako , ” alisema mkuu wa mafunzo ambaye alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa ndani ya ofisi hiyo wakisikiliza mashtaka.Baada ya makubalianao hayo , watu wote wanne walilipwa fedha za matibabu kisha wakaondoka wakiwa wameridhika, kazi ikabakia kwa Dickson ambapo alikuwa na kesi ya pili ya kujibu .

“ Kwa nini ulitoroka chuoni na kwenda kufanya ufuska uraiani?” aliuliza mkuu wa chuo , Dickson akawa hana majibu zaidi ya kugugumia kwa maumivu makali, akaamrisha arudishwe tena Guantanamo na kufungiwa kwa siku saba kisha baada ya hapo, atalazimika kufanya kazi ngumu atakazopangiwa na viongozi wake na atakuwa chini ya uangalizi maalum kwa kipindi chote atakachokuwepo chuoni hapo.

Japokuwa Dickson alikuwa na roho ngumu, alishindwa kuyazuia machozi yasiulowanishe uso wake wakati akikokotwa na askari kurudishwa Guantanamo huku viungo vyote vya mwili wake vikimuuma sana kutokana na mateso makali . Akaingizwa kwenye gereza hilo la jeshi na kufungiwa, mateso yakaendelea
 
SEHEM YA 25

Upande wa pili, hatimaye Dickson au Zinja anafanikiwa kuhitimu chuo na baada ya hapo anaenda kujiunga na Chuo cha Polisi mjini Moshi, Kilimanjaro lakini usiku mmoja, uzalendo unamshinda na kuamua kutoroka chuoni kwenda mitaani kutafuta machangudoa, jambo linalomgharimu sana kwani anapewa adhabu kali sana inayomfanya ajute.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Siku saba zilikatika Dickson au Zinja kama wengi walivyokuwa wanamuita kutokana na sura yake kufanana na binadamu wa kale (Zinjathropus), akiendelea kuteseka ndani ya gereza la chuo cha polisi almaarufu Guantanamo kutokana na makosa makubwa aliyokuwa ameyafanya ya kutoroka chuoni na kwenda kununua changudoa mitaani na kujikuta akisababisha vurugu kubwa baada ya kufumaniwa.

Maumivu aliyokuwa anayasikia mwili mzima yalimfanya ajiapize kuwa kamwe hatarudia tena kufanya upuuzi kama alioufanya kwani ilikuwa ni lazima kila asubuhi aje kuamshwa kwa mijeledi kisha kufanyishwa kazi ngumu ndani ya gereza hilo, hali iliyomfanya aijutie sana nafsi yake. “ We kenge amka , vaa nguo zako adhabu yako ya kukaa humu imeisha, ” askari mmoja aliyekuwa amevalia magwanda, alimwambia Dickson huku akimtupia magwanda waliyokuwa wanavaa chuoni hapo, Dickson akajikongoja na kusimama, akavaa nguo hizo na kutoka mpaka nje.

Kutokana na kukaa kwenye giza kwa siku zote hizo, macho yake yalikuwa ni kama yamepigwa na upofu kwenye mwanga wa jua , ikamlazimu kukaa kwa zaidi ya dakika kadhaa ndipo alipoanza kuona vizuri, akaongozwa na yule mwanajeshi mpaka kwenye ofisi ya mkuu wa chuo ambapo alitakiwa kuandika barua maalum ya kukiri makosa yake yote kwa maandishi na kueleza kwamba hatarudia tena. “ Hiki ulichokiandika hapa ndicho kitakachotumika kukuhukumu endapo utarudia tena makosa yako, baada ya kumaliza kifungo chako adhabu inayofuata ni kazi ngumu, utapasua kuni kwa ajili ya kupikia chakula cha wanachuo wote kwa muda wa wiki nzima.

“ Pia utapalilia ekari tatu za shamba la migomba la chuo na utapasua mawe ili kupata vifusi vitatu vikubwa kwa ajili ya ujenzi wa majengo mapya , ” alisema mkuu huyo wa chuo huku akionesha kutokuwa na hata chembe ya masihara.
Baada ya kumaliza kumsomea adhabu anazotakiwa kuzifanya , mkuu huyo wa chuo alimuonesha Dickson sehemu maalum ya kusaini kuonesha kwamba amekubali adhabu hizo.

Aliposaini, Dickson aliruhusiwa kwenda bwenini kuoga na kujiweka kwenye hali ya usafi , tayari kwa kuendelea na shughuli nyingine za chuoni hapo ikiwa ni pamoja na kutekeleza adhabu alizopangiwa.Kwa wiki kadhaa mfululizo , Dickson aliendelea kupata msoto wa nguvu wakati akitekeleza adhabu alizopangiwa. Hata ile hamu ya kukutana kimwili na wanawake iliyokuwa inamsumbua , ilimuisha kabisa kwani kila siku alikuwa akilala hoi bin taaban na kuamshwa alfajiri na mapema kama ilivyokuwa kawaida ya chuoni hapo.

Mpaka alipomaliza adhabu alizopangiwa, mwili wake ulikuwa umepungua uzito kwa kiasi kikubwa , akawa ameshika adabu na kujiapiza kuwa ni bora aendelee kuteseka na hisia za kimapenzi kuliko kufanya upuuzi wa kutoroka tena kwenda mitaani. Mafunzo yakaendelea huku Dickson akiwa amenyooka kitabia . Kila alipokuwa akizidiwa na hamu ya kukutana kimwili na mwanamke, alikuwa akienda kumaliza haja zake kwenye mabafu ya chuo hicho kwa kujichua mpaka alipokidhi haja zake.

“ Nikirudi uraiani watanikoma, nitalipiza hizi taabu ninazonipata, ” alijisemea Dickson wakati akijichua bafuni . Kutokana na mazoea yake ya kujichua mara kwa mara , huku wakati mwingine akipiga kelele bafuni , wenzake waliokuwa wakisoma naye walikuwa wakimcheka sana na kumtania mara kwa mara. Kwa kuwa alishazoea kutaniwa tangu akiwa mdogo, hakujali kitu , akaendelea na tabia yake hiyo ya ajabu mpaka alipohitimu mafunzo ya upolisi. Wakafanyiwa sherehe kubwa chuoni hapo na kutunukiwa vyeti na nishani zao , tukio ambalo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama wa Tanzania. Hatimaye wakatunukiwa vyeti na nishani mbalimbali, huku wanachuo waliong ’ara katika kada mbalimbali , nao wakitunukiwa tunu mbalimbali. Kutokana na tukio alilolifanya Dickson miezi kadhaa nyuma , hakupata tuzo yoyote zaidi ya cheti na nishani.

Kwa kuwa kulikuwa na uhaba wa maafisa wa jeshi la polisi , Dickson na wenzake wengi walipata ajira ya moja kwa moja katika Jeshi la Polisi. Dickson akapangiwa kwenye mji mdogo wa Tunduma, kwenye mpaka kati ya Tanzania na Zambia. Siku kadhaa baadaye, askari wote walikuwa tayari wamesharipoti kwenye vituo vyao vya kazi, Dickson na wenzake kadhaa wakaripoti Tunduma ambapo walipokelewa kijeshi kwa kupigiwa saluti kisha wakapangiwa majukumu ya kila mmoja.

Siku hiyohiyo aliyoripoti kazini, Dickson hakulaza damu , baada ya kupanga vitu vyake kwenye nyumba aliyopewa, alivaa nguo za kiraia na kuingia barabarani, akatafuta mwenyeji mmoja na kumuuliza mahali anakoweza kupata machangudoa.
“ Ukivuka mpaka na kwenda upande wa kule Zambia, Nakonde kuna wanawake wazuri sana wanajiuza , kama utanilipia na mimi twende nikupeleke, ” alisema kijana mdogo aliyekuwa akifanya biashara ya kuuza maji barabarani , Dickson akamwambia yupo tayari kumlipa .

Kwa kuwa hakukuwa na umbali mrefu kutoka hapo walipokuwa kuelekea Nakonde, Zambia , walitembea kwa miguu na kuvuka mpaka unaozitenganisha nchi hizo mbili kwenye sehemu maarufu ya Custom na kuingia upande wa pili, wakatembea kwa miguu na dakika kadhaa baadaye, tayari walikuwa wamewasili Nakonde. Kijana huyo akampeleka moja kwa moja mpaka eneo maarufu liitwalo Zesco ambapo walikatiza mitaa na kutokea kwenye nyumba moja kubwa ya kifahari, iliyokuwa na wanawake wengi wazuri waliokuwa wamekaa kibarazani. Wanawake hao waliokuwa wamevalia kihasarahasara, walipowaona tu Dickson na mwenzake, waliwachangamkia na kuanza kuwazungumzisha Kiwemba , lugha kubwa inayozungumzwa nchini Zambia . “ Watshani boizi , kulichi kung ’anda, ” ( mambo zenu kina kaka, habari za nyumbani) walisema wanawake hao huku wengine wakiinuka haraka kuwafuata Dickson na mwenzake .

“ Bwino, kung ’anda kulichete! Tulefwaya sevisi, ” (Nzuri, za nyumbani salama, tunataka huduma) alijibu kijana huyo aliyeonekana kuielewa vyema lugha hiyo , wanawake hao wakawazunguka, wengine wakawa wanawamwagia mvua ya mabusu huku wengine wakiwavuta kuelekea ndani, Dickson akawa anameza mafunda ya mate mfululizo , kama fisi aliyeona lundo la mifupa.
 
SEHEMU YA 26

Anaendelea na masomo chini ya uangalizi mkali na hatimaye anahitimu na kupangiwa kituo cha kazi katika mji mdogo wa Tunduma, uliopo kwenye mpaka wa Tanzania na Zambia.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

aada ya kusafiri kwa muda mrefu, hatimaye Dickson au Zinja na wenzake waliokuwa wamepangiwa kwenda kuripoti katika Kituo cha Polisi cha Tunduma, waliwasili kwenye mji huo mdogo na kupokelewa vizuri na wenyeji wao kisha kila mmoja akapangiwa majukumu pamoja na kuoneshwa nyumba ya kuishi.

Siku hiyohiyo, Dickson hakutaka kulaza damu, kwa jinsi alivyokuwa akijisikia hamu ya kukutana kimwili na mwanamke, aliona kama hawezi kufika kesho yake, akaingia mitaani na kukutana na kijana mmoja aliyekubaliana naye ampeleke kwenye sehemu anazoweza kupata machangudoa.

Wakavuka mpaka na kuingia nchi jirani ya Zambia, kwenye Mji wa Nakonde alikoelekezwa kwamba ndiyo kuna machangudoa wazuri, akaongozana na kijana huyo mpaka kwenye mtaa maarufu wa Zesco na hatimaye wakatokezea kwenye nyumba nzuri iliyokuwa na wanawake wengi waliovalia kihasarahasara. Kwa kuwa mwenzake alikuwa akiielewa Lugha ya Kiwemba ambayo ndiyo iliyokuwa inatumika sana nchini humo, alifanikiwa kuzungumza na wanawake hao na kuwaeleza shida yao, wakawagombania kama mpira wa kona na kuingizwa ndani.

Muda mfupi baadaye, Dickson na mwenzake walikuwa wakielea kwenye ulimwengu tofauti kabisa, huku Dickson akionesha kufurahia sana alichokuwa anakifanya, hasa ukizingatia jinsi alivyokuwa anabanwa kwa sheria kali kipindi alipokuwa jeshini. Baada ya kukidhi haja zao na kulipa gharama walizotajiwa, waliaga na kuondoka huku Dickson akionesha kunogewa mno na mchezo huo. Njiani akawa na kazi ya ziada ya kukariri mitaa na njia ili siku nyingine awe anaenda peke yake.

Mpaka Dickson anarejea kwenye nyumba yake mpya, tayari ilishatimia saa moja za usiku, akaenda kuoga na kupumzika kwani tangu afike hakupata hata muda wa kupumzika. Akawa ameyaanza maisha mapya huku akionesha kuufurahia sana mji wa Tunduma. Kesho yake asubuhi, alienda kuripoti kazini kwa mara ya kwanza, akapangiwa kukaa kaunta na askari wenzake wakati akielekezwa kazi mbalimbali anazotakiwa kuwa anazifanya kila siku kituoni hapo.Mchana, alichukuliwa na askari wenzake na kuingia kwenye difenda, wakawa wanazunguka na askari wenzake sehemu mbalimbali za mji huo mdogo lakini uliochangamka sana kibiashara.

Alitembezwa mitaa yote, kuanzia Maporomoko, Mwaka, Black Market, Tukuyu, Majengo mpaka Majengo Mapya kisha wakarejea kituoni, ikiwa tayari imeshatimia saa kumi na moja jioni, akakamilisha taratibu za kawaida na kuruhusiwa kwenda kwenye nyumba yake, iliyokuwa jirani na kituo hicho kwa ajili ya mapumziko. Japokuwa hakuna aliyeweza kumuonesha dhahiri, askari wenzake na watu wote waliokuwa wakikutana na Dickson, walikuwa wakionesha mshangao kwa jinsi sura yake ilivyokuwa mbaya.Alipofika nyumbani kwake, alibadilisha nguo na kuvaa za kiraia, akavaa kofia yake kubwa iliyokuwa inaziba sehemu kubwa ya uso wake na kutoka, akaianza safari ya kuelekea Nakonde huku akiwa makini kuhakikisha hapotei.

Akafanikiwa kuvuka mpaka na kuingia Nakonde bila tatizo, akachanja mitaa na hatimaye akatokea Zesco na kunyoosha moja kwa moja mpaka kwenye nyumba ya wale machangudoa ambapo walipomuona tu, walimchangamkia kwani walikuwa wanamkumbuka. Tatizo likawa namna ya kuelewana naye kwani hakuwa akijua Kiwemba, akalazimika kutumia Kiingereza, kwa bahati nzuri wengi walionekana kumuelewa alichokuwa anakisema, akamchagua mmoja aliyekuwa anamtaka na kuingia naye mpaka kwenye vyumba vya ndani, wakamalizana kisha Zinja akalipa fedha na kuondoka zake.

Huo ndiyo ukawa mchezo wake, ikawa kila siku jioni ni lazima avuke mpaka na kuelekea Nakonde kutafuta machangudoa ambao kila siku alikuwa akiwabadilisha kama nguo, leo akitoka na mnene, kesho anamtaka mwembamba, keshokutwa akitoka na mfupi siku inayofuatia anatoka na mrefu!

Siku alizokuwa anaingia shifti za usiku, alikuwa anapata sana shida ambapo asubuhi na mapema baada ya kutoka kazini, ilikuwa ni lazime avuke mpaka. Hayo ndiyo yakawa maisha yake.Hata hivyo, kipato alichokuwa anakipata kutokana na kazi yake ya upolisi, hakikuwa kinamtosha kwa matumizi ya aina hiyo kwani ukiachilia mbali kwenda kununua machangudoa, ilikuwa ni lazima pia ale na kufanya mambo mengine mengi ambayo yote yalihitaji fedha.
Upande wa kazi, japokuwa alikuwa mgeni, alianza kupata umaarufu mkubwa kutokana na jinsi alivyokuwa mahiri wa kupambana na matukio ya uvunjifu wa amani, huku alama yake kubwa ikiwa ni sura yake mbaya ambayo hata akicheka alikuwa akionekana kama analia.

Vijana wakorofi wa Tunduma, waliokuwa wakisifika kwa matukio mbalimbali ya uvunjifu wa amani, wakambatiza kwa jina la Afande Sura Mbaya, huku wengi wakionekana kumchukia kutokana na umakini wake awapo kazini. Hata hivyo, kutokana na uhitaji mkubwa wa fedha kwa ajili ya kwenda kununua machangudoa, Dickson alijikuta akianza kutoka nje ya mstari, akaanza tabia ya kupokea rushwa ndogondogo kutoka kwa wahalifu aliokuwa anawakamata, lengo lake likiwa ni kuhakikisha kila siku hakosi kwenda kuopoa changudoa.

Siku moja, akiwa amepangwa zamu ya usiku, wakiwa mitaani ndani ya gari la polisi, walishtushwa na milio mfululizo ya risasi zilizokuwa zinamiminwa kuelekea kwenye gari walilokuwemo, vioo vyote vikapasuliwa pamoja na matairi huku risasi zikiendelea kurindima, ikabidi askari wote watumie mafunzo yao kunusuru maisha yao yaliyokuwa hatarini.
Wakajirusha kwa ufundi mkubwa mpaka nje ya gari lakini haikusaidia kitu, risasi ziliendelea kufyatuliwa kwa kasi ya ajabu.

ITAENDELEA
 
SEHEM YA 27

Ananogewa na mchezo huo kiasi cha kuwa mtumwa wa ngono . Baadaye Dickson au Zinja anahitimu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kwenda kujiunga na Chuo cha Polisi mjini Moshi, Kilimanjaro. Anapohitimu anapangiwa kwenda kufanya kazi katika mji mdogo wa Tunduma, uliopo kwenye mpaka wa Tanzania na Zambia. Baada ya mafanikio makubwa, anahamishwa kikazi na kuelekea Dar es Salaam, huko, kama alivyofanya sehemu nyingine, napo anaendelea na mchezo wake kama kawaida.

Je , nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Ilisikika milio mingi ya risasi kutoka katika Benki ya Dar es Salaam iliyokuwa maeneo ya Ubungo . Watu wengi waliokuwa karibu na eneo hilo wakaanza kukimbia kuyaokoa maisha yao , wanawake walikuwa wakipiga kelele huku wengine wakilala chini ili wasiweze kupigwa na risasi hizo.

Hakukuwa na utulivu hata mara moja, milio ile ya risasi ambayo ilisikika kutoka ndani ya benki ile ikawapelekea polisi waliokuwa karibu na benki hiyo kufika eneo la tukio huku wakiwa na bunduki zao mikononi .Benki ya Dar es Salaam ilikuwa imevamiwa na majambazi watano waliokuwa na bunduki zenye nguvu mikononi mwao. Kila mtu aliyekuwa ndani ya benki ile aliamriwa kulala chini na kutoangalia kitu kilichokuwa kikiendelea.

“ Weka fedha haraka dada, usiniangalie usoni, mimi siyo mjomba wako , ” alisema jambazi mmoja kwa sauti yenye utetemeshi mkubwa iliyomtisha dada huyo na kufanya kama alivyoagizwa.
Ndani ya dakika kadhaa, polisi waliendelea kuongezeka karibu na eneo hilo. Kila aliyejaribu kuingia ndani, alipigwa risasi, damu zikatapaa katika eneo la nje ya benki hiyo .

Hakukuwa na polisi aliyetaka kuingia ndani, kila mmoja aliona hatari iliyokuwa mbele yake, waliyapenda maisha yao, hivyo hawakuwa radhi kuona wakipigwa risasi na kufariki dunia na wakati walikuwa na familia zao. Wala hazikupita dakika nyingi , Inspekta wa polisi , Dickson akafika eneo la tukio huku akiwa ametangulizana na baadhi ya polisi . Alichokifanya ni kuteremka ndani ya gari na kuanza kuwafuata polisi wenzake ambao walimwambia kile kilichokuwa kikiendelea.

Hiyo, kwake ilionekana kuwa kazi ndogo , alichokifanya, akachukua bastola ndogo, akaiweka kiunoni mwake na kisha kuanza kuufuata mlango wa benki ile . Kila polisi akaogoppa, alimshangaa Dickson kwani hakukuwa na mtu aliyekuwa radhi kuusogelea mlango ule ambapo ndani yake, risasi ziliendelea kurushwa kila wakati. Alipoona ameukaribia mlango ule, akajibanza pembeni ukutani na kisha kuitoa bunduki yake na kuishikilia. Polisi wote waliokuwa wakimwangalia , walishangaa , hawakujua Inspekta wao alipata wapi ujasiri kiasi kile , alichokifanya ni kuanza kuupiga risasi mlango ule wa vioo mpaka kioo chote kilipovunjika . “ Pigeni risasi mfululizo , ” aliwaambia polisi wake.

Risasi zilipigwa mfululizo kuelekea ndani ya benki ile , zaidi ya risasi hamsini zikapigwa hali iliyowafanya majambazi wale kujificha. Hiyo ilikuwa nafasi pekee kwa Inspekta Dickson , kama ninja mwenye mafunzo makubwa , akarukia ndani ya benki ile ambapo majambazi walikuwa wamejificha na bunduki zao.

Alipotua ndani tu , kwa kasi ya ajabu, akaanza kuwamiminia risasi majambazi wale ambao kwa ghafla sana walimuona kama mzimu kutokana na uharaka wake wa kuingia ndani ya benki ile. Kazi ilikuwa kubwa lakini ndani ya dakika moja tu , majambazi wote watano walikuwa chini , damu zilikuwa zikiwatoka hali iliyomaanisha kwamba jengo lilikuwa salama.
Hilo likawa tukio jingine kubwa ambalo alikuwa amelifanya Inspekta Dickson. Taarifa juu ya umahiri wake zikatangazwa , serikali ikajivunia kuwa na polisi kama yeye hivyo kupandishwa cheo na kuwa Naibu Kamishina wa Polisi ( DCP) kwa Mkoa wa Dar es Salaam.
* * *
Pamoja na umahiri wake wa kupambana na majambazi lakini bado Dickson hakuachana na tabia yake ya kuendekeza kununua machangudoa mitaani na kwenda nao hotelini kufanya nao ngono . Aliyazoea maisha hayo tangu Tunduma hivyo kuachana nayo ilikuwa kazi ngumu mno. Siku zikaendelea kukatika, kama kawaida yake , kila siku usiku alikuwa akienda sehemu wanawake walipokuwa wakijiuza na kumchukua mwanamke mmoja kisiri na kuondoka naye .
Hakutaka kujulikana kutokana na umaarufu wake. Kila kitu alichokuwa akiendelea kukifanya, alikifanya kisiri mno.
“ Mpaka asubuhi nitakufanyia elfu hamsini , ” alisema changudoa mmoja, alikuwa akizungumza na mteja wake aliyevalia kofia ambaye hakutaka kuteremka garini, DCP Dickson.

“ Ingia twende , ” alisema Dickson na msichana yule kuingia . Safari yao ikaishia ndani ya hoteli moja ya kifahari ambapo akaingia ndani na msichana yule. Kitu cha kwanza kabisa kukifanya , alifanya kila liwezekanalo kuhakikisha taa haiwashwi , hilo halikuwa na tatizo kwani alichokihitaji changudoa yule ni hela yake tu.

Walifanya mapenzi kwa zaidi ya masaa matatu, walipomaliza, msichana yule akasimama na kuifuata swichi ya taa ya chumba kile . Alitaka kuuona uso wa mwanaume huyo aliyempa haki yake mpaka kuridhika , akawasha taa na DCP Dickson kushtuka kutokana na mwanga mkali. “ Aaah! Dickson. ..!!” msichana yule alijikuta akisema huku akiwa na mshtuko mkubwa, Dickson akamwangalia mwanamke yule , naye akahofia kwa kuona aligundulika . Akabaki akiwa ameduwaa tu.

ITAENDELEA
 
SEHEM YA 28

Kwa upande wa kazi , Dickson anaendelea kujituma kadiri ya uwezo wake , jaribio la kutaka kumuua linashindikana na muda mfupi baadaye, anafanikiwa kuzima jaribio kubwa la ujambazi kwenye benki , hali inayosababisha apandishwe tena cheo na kufikia ngazi ya DCP. Hata hivyo , michezo yake ya kununua machangudoa anaendelea nayo .

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Baada ya kukidhi haja za mwili wake, DCP Dickson au Zinja kama alivyokuwa akifahamika tangu akiwa chuoni, alijitupa kitandani huku akionesha kuchoka sana kutokana na kazi nzito aliyotoka kuifanya . Ghafla akashtuka taa ya chumba cha gesti aliyokuwa amelala na mwanamke huyo ikiwashwa, jambo ambalo lilimfanya ashtuke mno, akajua siri yake imefichuka. Mshtuko alioupata ulisababisha mwanamke yule ambaye bado alikuwa amesimama pembeni ya swichi kushtuka, akamtaza vizuri Dickson na kujikuta akipigwa na butwaa.

“ Haaa ! Dickson ?” alisema mwanamke huyo kwa mshtuko mkubwa baada ya kugundua kuwa mwanaume aliyekuwa amelala naye , alikuwa kiongozi mkubwa kwenye jeshi la polisi. Kutokana na jinsi mwanamke huyo alivyoshtuka, almanusra atoke nje bila nguo lakini Dickson alimuwahi na kuchomoa funguo na kuificha . “ Nisamehe, nisamehe , ” alisema mwanamke huyo kwa hofu huku akihisi kwamba huenda kiongozi huyo wa jeshi la polisi alikuwa anataka kumkamata na kumfungulia mashtaka kwa kujihusisha na biashara ya uchangudoa. Kwake aliamini haiwezekani kabisa Dickson akawa ni mteja wa kawaida kwani kwa hadhi aliyokuwa nayo , aliamini lazima ana familia yake.

“ Wala sina nia mbaya na wewe , tafadhali usiogope, ” alisema Dickson kwa sauti ya chini kwani kwa jinsi mwanamke huyo alivyoonesha kushtuka, angeweza hata kupiga kelele za kuomba msaada , Dickson akawa anaendelea kumbembeleza na kumtoa wasiwasi.

Ilimchukua muda mrefu sana mwanamke huyo kutulia, japokuwa hiyo ilikuwa mara yake ya kwanza kuonana uso kwa uso na Dickson, kila kukicha alikuwa akimuona kwenye runinga na kwenye magazeti au wakati mwingine kusikia habari zake kwenye redio jinsi alivyokuwa shujaa wa kupambana na ujambazi na vitendo vingine vya uvunjifu wa amani .
Akawa anamtazama kwa hofu huku mapigo ya moyo wake yakimuenda mbio kwani ukiachilia mbali vyeo alivyokuwa navyo Dickson, sura yake pia ilikuwa inatisha sana . Dickson akaendelea kumbembeleza kwa muda mrefu mpaka akatulia.

“ Unaniahidi hutamwambia mtu yeyote kwamba usiku wa leo umelala na mimi?” Dickson alimuuliza mwanamke huyo ambaye harakaharaka alitingisha kichwa kukubali. Japokuwa aliahidi kuitunza siri hiyo , ndani ya moyo wake alikuwa na hofu kubwa kwamba siri ile itavuja na kumsababishia fedheha kubwa na pengine kusababisha afukuzwe kazi kabisa.
Japokuwa makubaliano yao ilikuwa ni kulala mpaka alfajiri na mapema , Dickson aliamua kubadilisha mawazo , akainuka na kuanza kuvaa nguo zake , akamwamuru mwanamke huyo naye kuvaa nguo zake.

“ Tunaenda wapi ?”
“ Nataka tuhame gesti , sidhani kama hapa panatufaa, ” alisema Dickson huku akilazimisha tabasamu kwenye uso wake . Akamuahidi mwanamke huyo kumuongeza fedha kutoka shilingi elfu hamsini walizokuwa wamekubaliana awali mpaka shilingi laki moja, jambo lililomfanya mwanamke huyo kukubali kirahisi . Wakaongozana mpaka nje ya gesti waliyoingia huku Dickson akiwa ameshusha kofia na kuziba sura yake ili isiwe rahisi kwa mtu yeyote kumtambua, wakatoka mpaka kwenye gari lake ambapo Dickson alimfungulia mwanamke huyo mlango wa gari , naye akaingia upande wa pili na kuondoa gari taratibu mpaka alipoingia kwenye barabara ya lami.

“ Tunaelekea wapi?”
“ Kuna hoteli moja nzuri sana ipo Mbezi Beach inaitwa Ichenjezya Resort, nadhani itatufaa sana , ” alisema Dickson huku akibadilisha gia kwenye gari lake na kuzidi kuchanja mbuga.Walipofika Mwenge, Dickson alisimamisha gari pembeni kidogo ya stendi ya kuelekea Tegeta , akamwambiamwanamke huyo amsubiri kidogo anaenda kununua vinywaji. Ili kuhakikisha kwamba hamkimbii, Dickson alipoteremka garini alibonyeza rimoti ya gari na ‘kuiloki’ milango yote.

Dakika chache baadaye, alirejea akiwa na vinywaji viwili mkononi , kimoja kikiwa kimeshafunguliwa . Akamkabidhi mwanamke huyo kile kinywaji kilichokuwa kimefunguliwa kisha na yeye akafungua cha kwake huku akiwasha gari . Muda mfupi baadaye, tayari walikuwa kwenye barabara ya lami, wakichanja mbuga kuelekea Mbezi. Tofauti na awali , safari hii Dickson alionesha kuchangamka sana, akawa anamsemesha mwanamke huyo mambo mbalimbali huku akimsisitiza kunywa kinywaji chake mpaka amalize. Baada ya kunywa mafunda kadhaa, mwanamke huyo alianza kulalamika kwamba anasikia usingizi mzito.

Dickson akamtegulia siti na kumwambia apumzike, wakifika atamuamsha . Dakika chache baadaye , alikuwa hajitambui kwa usingizi, Dickson akaachia tabasamu pana na kuzidi kukanyaga mafuta , gari likawa linakimbia kwa spidi 120 huku akiwa makini kuhakikisha hakuna mtu anayemfuatilia. Saa nane za usiku juu ya alama, Dickson alikuwa akichepuka kutoka kwenye barabara kuu, eneo la Madale na kuifuata barabara ya vumbi iliyokuwa inaelekea kwenye Msitu wa Pande, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Kwa muda wote huo, mwanamke huyo alikuwa akiendelea kukoroma, akiwa haelewi kabisa kilichokuwa kinaendelea.

Je, nini kitafuatia?
 
SEHEM YA 29

Anapohitimu anapangiwa kwenda kufanya kazi katika mji mdogo wa Tunduma, uliopo kwenye mpaka wa Tanzania na Zambia . Baada ya mafanikio makubwa, anahamishwa kikazi na kuelekea Dar es Salaam , huko , kama alivyofanya sehemu nyingine, napo anaendelea na mchezo wake kama kawaida.

Kwa upande wa kazi , Dickson anaendelea kujituma kadiri ya uwezo wake , jaribio la kutaka kumuua linashindikana na muda mfupi baadaye, anafanikiwa kuzima jaribio kubwa la ujambazi kwenye benki , hali inayosababisha apandishwe tena cheo na kufikia ngazi ya DCP. Hata hivyo , michezo yake ya kununua machangudoa anaendelea nayo huko.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Tabasamu pana lilikuwa usoni mwa Dickson, aliendelea kuendesha gari lile kwa kasi kuelekea msituni. Kichwa chake kilikuwa na mawazo mengi, alijua kwamba alikuwa akienda kufanya kitu kibaya kwa mtu asiyekuwa na hatia yoyote ile lakini hakuwa na jinsi. Hakutaka suala lake la kununua machangudoa lijulikane, alitaka liendelee kuwa siri katika maisha yake yote. Alizidi kuliendesha gari lile kwa dakika kadhaa na ndipo alipofika sehemu ambayo aliiona kuwa nzuri kufanya kile alichotaka kukifanya.

Akasimamisha gari na kuteremka, akaelekea nyuma ya gari ambapo akafungua buti na kisha kutoa koleo kisha kuelekea sehemu iliyokuwa na udongo laini na kuanza kuchimba . Haikuwa kazi nyepesi lakini alitakiwa kumalizana nayo haraka sana . Aliendelea kuchimba shimo kubwa ambapo alitumia zaidi ya dakika arobaini , lilipokamilika akalifuata gari lake na kumchukua mwanamke yule ambaye bado alikuwa akikoroma.

“ Ni lazima nimuue, haina jinsi , ” alijisemea , akambeba mwanamke yule na kuelekea naye kule kulipokuwa na shimo kubwa. Alipomfikisha , akamtumbukiza shimoni na yeye mwenyewe kuingia . Moyo wake ulikwishabadilika, hakuwa katika hali ya ubinadamu , alikuwa mnyama wa kutisha asiyekuwa na masihara hata mara moja. Alichokifanya mara baada ya kuingia shimoni ni kuanza kumpiga mwanamke kichwani kwa kutumia koleo lake. Alimpiga na kumsababishia jeraha kubwa, damu ikaanza kuvilia ndani ya ubongo wake na haikuchukua muda mrefu , mapigo ya moyo ya mwanamke yule yakasimama, akawa amefariki dunia palepale shimoni.

Dickson akatoka na kuangalia huku na kule kuona kama kulikuwa na mtu aliyekuwa akimuona kwani kwa mbali tayari mwanga ulianza kuonekana, alfajiri ilianza kuingia . Hakutaka kupoteza muda , alitaka kufanya kila kitu haraka hivyo akaanza kuufukia mwili ule. “ Saa kumi na moja hii , ngoja nifanye haraka, ” alisema huku akiiangalia saa yake .
Hakuchukua muda mrefu , akamaliza. Alichokifanya ni kushindilia sehemu ile huku akichukua baadhi ya majani na kuyaweka juu ya shimo lile , alipoona kila kitu kipo vizuri, akaingia ndani ya gari lake na kuondoka mahali hapo huku akiwa na amani moyoni mwake .
* * *
Japokuwa Dickson aliamini kwamba alikuwa peke yake na hakukuwa na mtu yeyote yule aliyekuwa akimuona, lakini ukweli ni kwamba kulikuwa na mzee mmoja, mwindaji ambaye alikuwa amejificha katikati ya miti akiangalia kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Mzee huyu aliyeitwa Gombana alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakiingia katika Msitu wa Pande kila siku alfajiri kwa ajili ya uwindaji wa wanyama wadogo. Siku hiyo ambayo aliamini kwamba angeweza kupata chochote kile , aliingia lakini kitu cha ajabu ni kwamba akakuta kitu cha tofauti kabisa.

Mbele yake , umbali kama wa hatua hamsini aliliona gari limesimama , kwanza akashtuka, haikuwa kawaida kabisa kulikuta gari ndani ya msitu huo . Akaogopa sana , akatamani kukimbia kwani moyo wake ulijua kwamba inawezekana gari lile lilikuwa la majambazi hivyo kumfanyia kitu kibaya, ila kila alivyotaka kufanya hivyo, moyo wake ulisita. Alichokifanya mara baada ya kufikisha hatua ishirini kabla ya kulifikia gari lile ni kujificha, akamuona mwanaume mmoja akiubeba mwili wa mwanamke na kuutumbukiza shimoni kisha kuanza kuufukia. Mzee Gombana hakuamini alichokuwa akikiona, alitamani kupiga simu polisi ili aweze kuwafahamisha juu ya kile kilichokuwa kikiendelea lakini hakuwa na simu.

Alibaki akimwangalia mtu yule aliyekuwa bize na kazi yake . Kwa kuwa hakujua ni kwa namna gani angeweza kufikisha taarifa zile kwa polisi , alichokifanya ni kukariri namba za gari lile tu ambazo aliamini kwamba zingekuwa msaada mkubwa kwake katika kutoa taarifa juu ya kile kilichokuwa kimetokea. Mpaka gari linaondoka mahali hapo, alikuwa na uhakika kwamba taarifa ambayo angeitoa polisi ingekuwa ya uhakika iliyokuwa na ushahidi wa kutosha.

Mzee Gombana hakutaka kumwambia mtu yeyote yule juu ya kile kilichokuwa kimetokea , alikifanya kuwa siri mpaka asubuhi iliyofuata akajiandaa kwenda katika kituo cha polisi kwa ajili ya kutoa taarifa juu ya kile alichokuwa amekiona .
“ Vipi mume wangu ?” aliuliza mkewe .
“ Safi tu .”
“ Mbona upo hivyo ?”
“ Nipo vipi ?”
“ Hujiaminiamini .”
“ Nipo kawaida tu , usihofu, ” alimwambia mke wake. Hakutaka kitu hicho kijulikane kwa mtu yeyote yule, alikifanya kuwa siri kubwa mpaka ilipofika saa tatu asubuhi, muda ambao alianza kuelekea katika kituo hicho kwa ajili ya kutoa taarifa juu ya kile kilichokuwa kimetokea .
 
SEHEMU YA 30

Hali ya sintofahamu inazuka jijiniDar es Salaam kufuatia kupoteamfululizo kwa machangudoa katikamazingira ya kutatanisha . Taharukikubwa inazuka kwani ndani yakipindi kifupi tu, zaidi yamachangudoa kumi na mojawanapotea na hakuna anayejuawalikopotelea.Jambo hilo linasababisha jeshi lapolisi kuingilia kati. Kinachozidikuzua utata , wote wanapotea katikamazingira yanayofanana .Mwanaume mmoja asiyejulikana,aliyekuwa anatembelea gari lakifahari aina ya Volkswagen ,aliyekuwa akienda eneo hilo usikuwa manane ndiye anayehusishwana wote wanaopotea.Upande wa pili , kijana aliyekuwa namwonekano tofauti na binadamuwa kawaida, Dickson Maduhu auZinja kama wenzake walivyokuwawakimtania, amejiunga na ChuoKikuu cha Dar es Salaam.

Hisia kaliza mapenzi zinasababisha kijanahuyo aanze kutoka usiku nakwenda kutafuta machangudoa.Ananogewa na mchezo huo kiasicha kuwa mtumwa wa ngono.Baadaye Dickson au Zinjaanahitimu Chuo Kikuu cha Dar esSalaam na kwenda kujiunga naChuo cha Polisi mjini Moshi ,Kilimanjaro.Anapohitimu anapangiwa kwendakufanya kazi katika mji mdogo waTunduma, uliopo kwenye mpaka waTanzania na Zambia. Baada yamafanikio makubwa, anahamishwakikazi na kuelekea Dar es Salaam,huko, kama alivyofanya sehemunyingine , napo anaendelea namchezo wake kama kawaida .Kwa upande wa kazi, Dicksonanaendelea kujituma kadiri yauwezo wake , jaribio la kutakakumuua linashindikana na mudamfupi baadaye , anafanikiwa kuzimajaribio kubwa la ujambazi kwenyebenki, hali inayosababishaapandishwe tena cheo na kufikiangazi ya DCP. Hata hivyo, michezoyake ya kununua machangudoaanaendelea nayo huko.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Tabasamu pana lilikuwa usonimwa Dickson, aliendeleakuendesha gari lile kwa kasikuelekea msituni. Kichwa chakekilikuwa na mawazo mengi, alijuakwamba alikuwa akienda kufanyakitu kibaya kwa mtu asiyekuwa nahatia yoyote ile lakini hakuwa najinsi.Hakutaka suala lake la kununuamachangudoa lijulikane, alitakaliendelee kuwa siri katika maishayake yote. Alizidi kuliendesha garilile kwa dakika kadhaa na ndipoalipofika sehemu ambayo aliionakuwa nzuri kufanya kile alichotakakukifanya.Akasimamisha gari na kuteremka,akaelekea nyuma ya gari ambapoakafungua buti na kisha kutoakoleo kisha kuelekea sehemuiliyokuwa na udongo laini nakuanza kuchimba.

Haikuwa kazinyepesi lakini alitakiwakumalizana nayo haraka sana .Aliendelea kuchimba shimo kubwaambapo alitumia zaidi ya dakikaarobaini, lilipokamilika akalifuatagari lake na kumchukuamwanamke yule ambaye badoalikuwa akikoroma .“Ni lazima nimuue, haina jinsi, ”alijisemea , akambeba mwanamkeyule na kuelekea naye kulekulipokuwa na shimo kubwa .Alipomfikisha , akamtumbukizashimoni na yeye mwenyewekuingia. Moyo wakeulikwishabadilika, hakuwa katikahali ya ubinadamu , alikuwamnyama wa kutisha asiyekuwa namasihara hata mara moja. Alichokifanya mara baada yakuingia shimoni ni kuanzakumpiga mwanamke kichwani kwakutumia koleo lake.

Alimpiga nakumsababishia jeraha kubwa ,damu ikaanza kuvilia ndani yaubongo wake na haikuchukuamuda mrefu, mapigo ya moyo yamwanamke yule yakasimama ,akawa amefariki dunia palepaleshimoni.Dickson akatoka na kuangaliahuku na kule kuona kama kulikuwana mtu aliyekuwa akimuona kwanikwa mbali tayari mwanga ulianzakuonekana, alfajiri ilianza kuingia.Hakutaka kupoteza muda, alitakakufanya kila kitu haraka hivyoakaanza kuufukia mwili ule .“Saa kumi na moja hii , ngojanifanye haraka,” alisema hukuakiiangalia saa yake. Hakuchukua muda mrefu,akamaliza. Alichokifanya nikushindilia sehemu ile hukuakichukua baadhi ya majani nakuyaweka juu ya shimo lile ,alipoona kila kitu kipo vizuri,akaingia ndani ya gari lake nakuondoka mahali hapo huku akiwana amani moyoni mwake.*

* *Japokuwa Dickson aliaminikwamba alikuwa peke yake nahakukuwa na mtu yeyote yulealiyekuwa akimuona , lakini ukwelini kwamba kulikuwa na mzeemmoja, mwindaji ambaye alikuwaamejificha katikati ya mitiakiangalia kila kitu kilichokuwakikiendelea.Mzee huyu aliyeitwa Gombanaalikuwa miongoni mwa watuwaliokuwa wakiingia katika Msituwa Pande kila siku alfajiri kwa ajiliya uwindaji wa wanyama wadogo.Siku hiyo ambayo aliaminikwamba angeweza kupatachochote kile, aliingia lakini kitucha ajabu ni kwamba akakuta kitucha tofauti kabisa. Mbele yake, umbali kama wa hatuahamsini aliliona gari limesimama,kwanza akashtuka, haikuwakawaida kabisa kulikuta gari ndaniya msitu huo. Akaogopa sana, akatamani kukimbia kwani moyowake ulijua kwamba inawezekanagari lile lilikuwa la majambazihivyo kumfanyia kitu kibaya, ilakila alivyotaka kufanya hivyo, moyo wake ulisita. Alichokifanya mara baada yakufikisha hatua ishirini kabla yakulifikia gari lile ni kujificha, akamuona mwanaume mmojaakiubeba mwili wa mwanamke nakuutumbukiza shimoni kishakuanza kuufukia.

Mzee Gombanahakuamini alichokuwa akikiona ,alitamani kupiga simu polisi iliaweze kuwafahamisha juu ya kilekilichokuwa kikiendelea lakinihakuwa na simu .Alibaki akimwangalia mtu yulealiyekuwa bize na kazi yake . Kwakuwa hakujua ni kwa namna ganiangeweza kufikisha taarifa zile kwapolisi, alichokifanya ni kukaririnamba za gari lile tu ambazoaliamini kwamba zingekuwamsaada mkubwa kwake katikakutoa taarifa juu ya kilekilichokuwa kimetokea .Mpaka gari linaondoka mahalihapo, alikuwa na uhakika kwambataarifa ambayo angeitoa polisiingekuwa ya uhakika iliyokuwa naushahidi wa kutosha.

Mzee Gombana hakutaka kumwambia mtu yeyote yule juu yakile kilichokuwa kimetokea ,alikifanya kuwa siri mpakaasubuhi iliyofuata akajiandaa kwenda katika kituo cha polisi kwa ajili ya kutoa taarifa juu ya kilealichokuwa amekiona.“Vipi mume wangu ?” aliulizamkewe.“Safi tu.”“Mbona upo hivyo?”“Nipo vipi?”“Hujiaminiamini .”“Nipo kawaida tu, usihofu,”alimwambia mke wake .Hakutaka kitu hicho kijulikane kwamtu yeyote yule , alikifanya kuwasiri kubwa mpaka ilipofika saatatu asubuhi, muda ambao alianza kuelekea katika kituo hicho kwa ajili ya kutoa taarifa juu ya kilekilichokuwa kimetokea.

Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 31

Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam kufuatia kupotea mfululizo kwa machangudoa katika mazingira ya kutatanisha. Taharuki kubwa inazuka kwani ndani ya kipindi kifupi tu, zaidi ya machangudoa kumi na moja wanapotea na hakuna anayejua walikopotelea.

Jambo hilo linasababisha jeshi la polisi kuingilia kati. Kinachozidi kuzua utata, wote wanapotea katika mazingira yanayofanana. Mwanaume mmoja asiyejulikana, aliyekuwa anatembelea gari la kifahari aina ya Volkswagen, aliyekuwa akienda eneo hilo usiku wa manane ndiye anayehusishwa na wote waliopotea.

Upande wa pili, kijana aliyekuwa na mwonekano tofauti na binadamu wa kawaida, Dickson Maduhu au Zinja kama wenzake walivyokuwa wakimtania, amejiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Hisia kali za mapenzi zinasababisha kijana huyo aanze kutoka usiku na kwenda kutafuta machangudoa.

Ananogewa na mchezo huo kiasi cha kuwa mtumwa wa ngono. Baadaye Dickson au Zinja anahitimu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kwenda kujiunga na chuo cha polisi mjini Moshi, Kilimanjaro.

Anapohitimu anapangiwa kwenda kufanya kazi katika mji mdogo wa Tunduma, uliopo kwenye mpaka wa Tanzania na Zambia. Baada ya mafanikio makubwa, anahamishwa kikazi na kuelekea Dar es Salaam, huko, kama alivyofanya sehemu nyingine, napo anaendelea na mchezo wake kama kawaida.

Kwa upande wa kazi, Dickson anaendelea kujituma kadiri ya uwezo wake, jaribio la kutaka kumuua linashindikana na muda mfupi baadaye, anafanikiwa kuzima jaribio kubwa la ujambazi kwenye benki, hali inayosababisha apandishwe tena cheo na kufikia ngazi ya DCP.

Hata hivyo, michezo yake ya kununua machangudoa anaendelea nayo. Anapoona amemnunua changudoa na kugunduliwa, anamuua na kumzika msituni.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Alitembea kwa harakaharaka, moyoni alikuwa na kimuemue cha kusema kile kilichokuwa kimetokea msituni ambacho hakutaka mtu yeyote yule afahamu zaidi ya polisi wao na kisha kuwaambia juu ya lile gari aliloliona msituni kwani namba zake alikuwa nazo kichwani. Alichukua zaidi ya dakika kumi ndipo alipofika kituoni huku akiwa anahema kwa nguvu na kijasho chembamba kikimtiririka. Jambo lililowashangaza polisi wale.

“Karibu. Unataka nini?” aliuliza polisi aliyekuwa kaunta mara baada ya salamu.
“Nimekuja kutoa taarifa.”
“Taarifa gani?”
“Ya mauaji,” alijibu mzee Gombana.
“Hebu njoo huku,” alisema polisi yule huku akimvuta ndani ya chumba kidogo kwa ajili ya mahojiano marefu kwani taarifa ya mauaji haikuwa ndogo. Polisi waliokuwa wamemsikia ambao walikuwa karibu na kaunta ile, nao wakaelekea ndani. Hawakujua kama taarifa aliyoileta mzee huyo ilikuwa ni ya mauaji yaliyofanywa na kamanda wao.

“Umesema umeleta taarifa ya mauaji, si ndiyo?” aliuliza mkuu wa kituo hicho.
“Ndiyo!”
“Wapi?”
“Kule msituni.”

Alichokifanya mzee Gombana ni kuanza kuhadithia kilichokuwa kimetokea kule porini, aliwaambia kwamba alimuona mtu akiwa amefika msituni akiwa na gari, baada ya kusimama aliitoa maiti moja na kuizika katika shimo kubwa alilokuwa amelichimba.

Kila polisi aliyesikia taarifa ile alishtuka, walijaribu kumuuliza mzee huyo mara mbilimbili kama alikuwa na uhakika na kile alichokuwa amekisema, akawaambia kwamba alikuwa na uhakika na wangefika mpaka katika eneo hilo.

Hawakutaka kuendelea na mahojiano ndani ya chumba kile, walichokifanya ni kutoka, wakachukua gari lao, difenda, polisi wanne waliokuwa na bunduki wakaingia garini na safari ya kuelekea huko msituni kuanza.

Walichukua dakika arobaini mpaka kufika katika msitu huo ambapo wakaanza kuingia ndani zaidi. Dereva hakuendesha gari kwa mwendo wa kasi kutokana na miti mingi iliyokuwepo hali iliyosababisha ukosefu wa barabara ya magari.
“Wapi?” aliuliza polisi mmoja.

“Kule mbele mkuu! Nyie twendeni tu,” alisema mzee Gombana na hivyo dereva kuliendesha gari kuelekekea mbele zaidi.
Waliendelea kwenda mbele mpaka walipofika sehemu moja iliyoonekana kuwa na uwazi mkubwa, hapo ndipo mzee Gombana alipotaka gari lisimamishwe na kuegeshwa pembeni kwani hiyo ndiyo ilikuwa sehemu alipomuona Dickson akimzika mwanamke na kuondoka zake.

Kwa jinsi eneo lile lilivyokuwa, hawakuwa na shaka kwamba muda mchache uliopita sehemu hiyo ilichimbwa na kufukiwa, walichokifanya polisi wale ni kuchukua makoleo yaliyokuwa garini na kuanza kufukua lile shimo.
“Bila shaka huyu mzee yupo sahihi kabisa, humu kutakuwa na maiti, si unaona udongo unavyoonesha?” alisema polisi mmoja huku wengine wakiendelea kufukua lile shimo.

Kazi haikuwa ndogo, japokuwa walikuwa wengi lakini walipata kazi kubwa kulifukua lile shimo. Mzee Gombana alisimama pembeni, alikuwa akifuatilia kila kitu kilichokuwa kikiendelea mahali hapo huku moyoni akimuomba Mungu mwili wa mtu huyo ukutwe ili aweze kuaminika kwa taarifa aliyoitoa.

Baada ya dakika kadhaa, makoleo yao yakaanza kudunda mwilini mwa maiti na kugundua kwamba tayari walikuwa wameifikia, hivyo wakayatupa makoleo yao pembeni na kuanza kutoa mchanga kwa kutumia mikono.
“Ni msichana!” alisema polisi mmoja na hivyo kusaidiana kuutoa mwili ule.

Kila mmoja akapigwa na mshtuko, alionekana kuwa msichana mrembo wa sura na umbo, kila mtu aliyemwangalia alishindwa kuelewa kipi kilichotokea katika maisha yake mpaka huyo mtu aliyemuua na kumzika aliamua kufanya hivyo.
Walichokifanya ni kuubeba mwili ule na kuondoka nao kwa ajili ya uchunguzi wa kujua ni kitu gani kilisababisha kifo chake hata kabla ya kuzikwa. Hawakutaka kumuacha mzee Gombana, bado alihitajika kwa ajili ya kuisaidia polisi juu ya kile kilichokuwa kimetokea.

“Kuna chochote unachokikumbuka kuhusu muuaji?” aliuliza mkuu wa polisi.
“Ndiyo! Nililiona gari lake!”
“Aina gani? Unazijua namba zake?”
“Ndiyo! Nakumbuka kila kitu.”

“Safi sana, ngoja tufike kituoni kwanza,” alisema polisi yule. Hawakutaka kuendelea kubaki pale, walichokifanya ni kuanza kuelekea katika kituo chao kwa ajili ya mahojiano zaidi na mzee Gombana ambaye alitakiwa kutaja kila kitu alichokuwa amekiona, likiwemo suala la namba za gari ambalo kwao lilionekana kuwa muhimu.

Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 32

Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam kufuatia kupotea mfululizo kwa machangudoa katika mazingira ya kutatanisha. Taharuki kubwa inazuka kwani ndani ya kipindi kifupi tu, zaidi ya machangudoa kumi na moja wanapotea na hakuna anayejua walikopotelea.

Jambo hilo linasababisha jeshi la polisi kuingilia kati. Kinachozidi kuzua utata, wote wanapotea katika mazingira yanayofanana. Mwanaume mmoja asiyejulikana, aliyekuwa anatembelea gari la kifahari aina ya Volkswagen, aliyekuwa akienda eneo hilo usiku wa manane ndiye anayehusishwa na wote wanaopotea.

Upande wa pili, kijana aliyekuwa na mwonekano tofauti na binadamu wa kawaida, Dickson Maduhu au Zinja kama wenzake walivyokuwa wakimtania, amejiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Hisia kali za mapenzi zinasababisha kijana huyo aanze kutoka usiku na kwenda kutafuta machangudoa. Hivyo baadaye anahamishiwa Dar es Salaam.

Mara baada ya kufanikiwa kuwa DCP, Dickson anajikuta kwenye wakati mgumu mara baada ya kumnunua changudoa, walipokuwa hotelini na kugundulika na changudoa yule kwamba ni yeye, anaamua kumuua na mwili kwenda kuuzika porini. Wakati anauzika, kulikuwa na mzee ambaye aliona kila kilichoendelea.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Dickson alikuwa na furaha tele kwani alijua huo ndiyo ungekuwa mwanzo wa kuficha siri juu ya kile kilichokuwa kimetokea msituni. Hakutaka ajulikane na mtu yeyote kama yeye ndiye aliyehusika na mauaji ya msichana yule kisha kumzika msituni.

Mzee Gombana alikuwa na furaha tele, kwake kuwa mikononi mwa Dickson kulimpa faraja na kuona alikuwa kwenye mikono iliyo salama. Garini, mzungumzaji mkubwa alikuwa yeye, alimhadithia namna alivyomuona mwanaume huyo akiutoa mwili kutoka garini kisha kuuzika katika shimo alilokuwa amelichimba.

“Kuna watu katili sana aiseee, nilishuhudia kila kitu mkuu, yaani mpaka nikatetemeka,” alisema mzee Gombana
“Ni lazima tuhakikishe anakamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria,” alisema Dickson huku akiendesha gari.
Bado furaha ilikuwa moyoni mwake, hakuamini kama kazi ingekuwa nyepesi namna ile, alichokuwa akikifikiria kichwani mwake kwa wakati huo ni kumuua mzee Gombana tu ili ile siri iendelee kuwa siri.

Alimshukuru Mungu kwani kile ambacho mzee Gombana alikiona kule msituni, hakutoa ushahidi wa kutosha kuhusiana na lile gari hivyo kuona kwamba hiyo ndiyo ilikuwa nafasi ya kumnyamazisha milele.

Hakutaka kuwa na presha, kwa kuwa tayari alikuwa ameaminika vya kutosha, alichokifanya ni kuelekea ofisini kwake ili huko ndiyo uwe mwanzo wa kufanya kile alichotaka kukifanya. Wakati wakiwa wamefika Manzese Tip Top, Dickson akalipaki gari lake pembeni kisha kuteremka.

Akaanza kuelekea katika duka la dawa ambapo akanunua dawa za mafua, piriton. Akazichukua na kuondoka dukani hapo kurudi garini pasipo kuzungumza chochote, mzee Gombana hakusema kitu, alinyamaza huku kwa kumwangalia alionekana kuwa mtu mwenye furaha tele.

“Samahani! Mafua yananisumbua mno,” alisema Dickson na kuingia garini.
“Pole sana mkuu.”
“Asante.”

Akaingia ndani ya gari na safari kuendelea. Hawakuchukua dakika nyingi wakaingia katika jengo la makao makuu ya polisi ambapo wakateremka na kuanza kuelekea ndani huku kila polisi aliyekutana naye, alipiga saluti kama kumpa heshima.

Walipofika ofisini, akamwambia mzee Gombana akae kitini kwa lengo la kuzungumza naye. Ila kabla ya mazungumzo hayo kuanza, akainuka, akaelekea nje ya ofisi ile ambapo alichukua zile dawa za priton, akazisagasaga kisha kuchukua sumu aina ya phenomenon yenye makali ya kuua hapohapo na kuiweka kwenye kikombe ambacho alitaka kumuwekea kahawa mzee Gombana.

Kwa sababu phenomenon ilikuwa miongoni mwa sumu zilizoua kwa haraka sana mara ziingiapo mwilini mwa binadamu, alichokifanya ni kupunguza makali yake na dawa ya piriton ambayo nayo aliisaga na kuiweka ndani ya kile kikombe kisha kurudi ofisini.

Aliporudi ofisini, akachukua chupa ya kahawa na kuimimina katika vikombe viwili na kumgawia mzee yule kikombe kilichokuwa na kahawa yenye sumu na kuanza kunywa. Dickson akafurahi, kitendo cha mzee yule kunywa kahawa ile kikamuoneshea kwamba alikuwa mshindi juu ya kilichokuwa kimetokea, hivyo alijiona kushinda vita kubwa na nzito iliyokuwa mbele yake.

“Kwenye maisha nimejifunza mengi mno,” alisema Dickson.
“Umejifunza nini mkuu?”
“Unapokuwa kiongozi ni lazima uwe mnyenyekevu pia. Siku kama ya leo huwa sipendi niandaliwe kahawa, ninapenda kuandaa mwenyewe, ninapenda kuwaoneshea watu wengine jinsi kiongozi unavyotakiwa kuwa,” alisema Dickson huku akitoa tabasamu.

“Wewe ni kiongozi bora, jinsi ulivyo, ukarimu wako na matendo yako ni vitu viwili tofauti. Wengine wanakuona una roho mbaya sana, ila tangu nimekutana nawe, hakika umekuwa tofauti na nilivyokuwa nikifikiria,” alisema mzee Gombana.

“Ninapokuwa kazini huwa ninauvaa mwili wa kazini, huwezi kwenda kupambana na majambazi huku uso wako ukiwa na tabasamu pana, unatakiwa kubadilika, uso uwe kwenye muonekano wa kikazi. Ninapofanya vitu kwa ujasiri na kuingia kazini huku nikionekana mwenye hasira, wengi wanafikiri nipo hivyo, ila nipo tofauti,” alisema Dickson huku tabasamu pana likiwepo usoni mwake.

Hawakuzungumza mengi kwani tayari alijua kwamba ile sumu iliyoingia mwilini mwa mzee Gombana ingeweza kufanya kazi muda wowote ule. Alichokifanya ni kumshukuru mzee huyo kwa ushirikiano wake huku akimtaka kwenda na yeye kuendelea na kazi.

Mzee Gombana akasimama kisha kuondoka ofisini hapo huku akiwa ameiacha ile namba ya gari aliloliona msituni ambalo ndilo lilikuwa gari la Dickson aliyekuwa Mkuu wa Polisi Kanda ya Dar es Salaam. Kwa Dickson, ilikuwa ni furaha tele.
*****
“Vipi tena mbona unaonekana hivyo?” aliuliza Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Mbezi.
“Kuna taarifa mbaya mkuu!” alijibu polisi mmoja.
“Mbona unanitisha! Taarifa ipi?”
“Yule mzee kafariki jana usiku.”

“Mzee yupi?”
“Yule aliyeleta taarifa juu ya lile gari porini. Amekufa baada ya kulalamika maumivu makali ya tumbo.”
“Unasemaje?”
”Ndiyo hivyo mkuu!”
Mkuu wa kituo cha polisi akachanganyikiwa.

Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 33

Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam kufuatia kupotea mfululizo kwa machangudoa katika mazingira ya kutatanisha. Taharuki kubwa inazuka kwani ndani ya kipindi kifupi tu, zaidi ya machangudoa kumi na moja wanapotea na hakuna anayejua walikopotelea.

Jambo hilo linasababisha jeshi la polisi kuingilia kati. Kinachozidi kuzua utata, wote wanapotea katika mazingira yanayofanana. Mwanaume mmoja asiyejulikana, aliyekuwa anatembelea gari la kifahari aina ya Volkswagen, aliyekuwa akienda eneo hilo usiku wa manane ndiye anayehusishwa na wote wanaopotea.

Upande wa pili, kijana aliyekuwa na mwonekano tofauti na binadamu wa kawaida, Dickson Maduhu au Zinja kama wenzake walivyokuwa wakimtania, amejiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Hisia kali za mapenzi zinasababisha kijana huyo aanze kutoka usiku na kwenda kutafuta machangudoa. Hivyo baadaye anahamishiwa Dar es Salaam.

Mara baada ya kufanikiwa kuwa DCP, Dickson anajikuta kwenye wakati mgumu mara baada ya kumnunua changudoa, walipokuwa hotelini na kugundulika na changudoa yule kwamba ni yeye, anaamua kumuua na mwili wake kwenda kuuzika porini. Wakati anauzika, kulikuwa na mzee ambaye aliona kila kilichoendelea.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Taarifa iliyofika kituoni ilimshtua kila polisi aliyeisikia kwamba shahidi waliyekuwa wakimtegemea kuwaambia juu ya gari lile lililokuwa msituni kufariki dunia ghafla nyumbani kwake.

Mkuu wa kituo hicho hakutaka kubaki ofisini, haikuwa taarifa nzuri hata kidogo kwani viongozi wake walitaka kufahamu kila kitu akiwemo Dickson ambaye alihusika katika kifo cha shahidi huyo, mzee Gombana.

Ofisini hakukukalika tena, alichokifanya ni kuondoka ofisini hapo kuelekea nyumbani kwa marehemu. Hakwenda peke yake, alikuwa na polisi kadhaa ambao wote kwa pamoja walichanganyikiwa kwa kilichokuwa kimetokea.
“Haiwezekani, hapa kuna kitu,” alisema mkuu wa kituo.

“Kweli mtu anaweza kufariki ghafla? Tena kwenye kipindi tunachomuhitaji sana?” aliuliza polisi mmoja huku akimwangalia mkuu wake usoni.
“Haiwezekani, hapa kuna kitu, subiri tufike.”

Japokuwa barabara ilikuwa mbaya lakini dereva hakujali, aliendesha kwa mwendo wa kasi huku wakitaka kufika msibani hapo haraka iwezekanavyo. Kitu cha kwanza walichokuwa wakihitaji ni kuuchunguza mwili wake kwani waliamini hakikuwa kifo cha kawaida, kulikuwa na mtu aliyekuwa amemuua mzee Gombana kwa kutaka kuficha siri juu ya kile kilichokuwa kimetokea kule msituni.

Bado muuaji wa msichana yule na mzee Gombana aliwachanganya, hawakujua ni nani aliyekuwa nyuma ya mauaji yale, walichokuwa wakikifanya ni kuhakikisha muuaji anapatikana haraka iwezekanavyo hata kabla wakuu wao hawajachukua uamuzi mbaya.

Hawakuchukua muda mrefu wakafika msibani hapo, hata kabla gari halijasimamishwa, kama makomandoo, polisi wale wakaruka, watu wote waliokuwa msibani wakashangaa, hawakujua sababu iliyowafanya polisi hao wafike msibani hapo huku wakiwa na bunduki mikononi, amani iliyokuwepo ikaanza kupotea.

Hawakuzungumza na mtu yeyote yule, walichokifanya ni kuingia ndani na kuonana na wafiwa ambapo wakazungumza nao na kuwaambia kwamba kabla ya mwili kuzikwa ilikuwa ni lazima ufanyiwe uchunguzi ili kuona kama ulijeruhiwa sehemu yoyote au kulikuwa na kitu kingine kilichosababisha kifo chake.

Hawakuwa na jinsi, japokuwa walipanga kufanya mazishi yake siku hiyo ikabidi waahirishe ili polisi wafanye kazi yao. Mpaka siku iliyofuatia, majibu ya uchunguzi yakatolewa na kuonesha kwamba mzee Gombana alikufa baada ya kunywa sumu iitwayo Phenomenon iliyokuwa na nguvu ya kummaliza mtu kwa haraka mno.
“Nani alimnywesha?”

“Hatujui, labda tumuulize mkewe,” alisema polisi mmoja.
Hawakutaka kuchelewa, bado akili zao hazikuwa sawa mpaka pale ambapo wangehakikisha kwamba kila kitu kinajulikana siku hiyo, walichokifanya ni kurudi tena nyumbani ambapo huko wakakutana na mke wa marehemeu na kuanza kuzungumza naye.
 
SEHEMU YA 34

Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam kufuatia kupotea mfululizo kwa machangudoa katika mazingira ya kutatanisha. Taharuki kubwa inazuka kwani ndani ya kipindi kifupi tu, zaidi ya machangudoa kumi na moja wanapotea na hakuna anayejua walikopotelea.

Jambo hilo linasababisha jeshi la polisi kuingilia kati. Kinachozidi kuzua utata, wote wanapotea katika mazingira yanayofanana. Mwanaume mmoja asiyejulikana, aliyekuwa anatembelea gari la kifahari aina ya Volkswagen, aliyekuwa akienda eneo hilo usiku wa manane ndiye anayehusishwa na wote wanaopotea.

Upande wa pili, kijana aliyekuwa na mwonekano tofauti na binadamu wa kawaida, Dickson Maduhu au Zinja kama wenzake walivyokuwa wakimtania, amejiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Hisia kali za mapenzi zinasababisha kijana huyo aanze kutoka usiku na kwenda kutafuta machangudoa. Hivyo baadaye anahamishiwa Dar es Salaam.

Mara baada ya kumnunua changudoa wa kwanza na kumgundua, Dickson akamuua na kumzika msituni. Baadaye, kuna mzee alimuona lakini kabla hajatoa ushahidi, akaamua kumuua. Siri imebaki kuwa siri. Baada ya wiki moja na nusu kupita tangu amuue changudoa yule, Dickson amerudi tena kununua mwanamke kwa ajili ya kulala naye usiku kucha.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Dickson alibaki akimwangalia changudoa yule kimahaba, tayari uchu wa kufanya naye mapenzi ulikwishampanda. Vazi alilovaa, sketi fupi ambayo iliishia mapajani mwake ilimuacha hoi, kila alipokuwa akiyaangalia mapaja yake, akili yake ilichanganyikiwa mno.

Kilipita kipindi cha wiki moja na nusu tangu mara ya mwisho kumnunua changudoa ambaye mwisho wa siku aliamua kumuua kutokana na kumuona usoni na kugundua kwamba alikuwa yeye, tangu siku hiyo mpaka siku aliyosimama na msichana huyo, hakuwa amelala na msichana yeyote yule.

“Ingia basi twende,” alisema Dickson.
“Twende wapi?”
“Hotelini.”

“Mimi nataka tutumie hoteli ile pale,” alisema msichana yule huku akiinyooshea kidole Hoteli ya Maradava iliyokuwa pembeni ya eneo hilo.
“Jamaniiiii...”
“Ndiyo! Tena ile ni bei chee”
“Za bei rahisi si nzuri, mimi nataka ile iliyokuwa ya gharama, si unaona hata gari langu linaongea mimi ni mtu wa aina gani,” alisema Dickson huku akijisifia.

Msichana yule alibaki njia panda, ni kweli alikuwa na shida ya kuhitaji hela lakini kwenda mbali na mwanaume kwake lilionekana kuwa tatizo kubwa. Kwa kipindi cha wiki nzima stori za rafiki yao ambaye alikutwa amefukiwa porini ziliwatisha, wasichana wengi waliogopa kutoka na mwanaume yeyote yule kwenda naye hotelini, kwa jinsi alivyokuwa Dickson, msichana yule alijawa na hofu.

“Unajua kuna kitu kilitokea wiki moja na nusu iliyopita ndiyo maana hatutaki kwenda mbali na sehemu hii,” alisema msichana yule huku akionekana kuwa na hofu.
“Kama unaogopa, basi sawa haina noma,” alisema Dickson, akapandisha kioo cha gari, akaliwasha kwa lengo la kuondoka.

Biashara haikuwa ya uhakika sana, mara baada ya mwanamke yule kuona kwamba mteja wake alikuwa siriazi kuondoka mahali hapo, akakipigapiga kioo kisha Dickson kukiteremsha na kuanza kumsikiliza.
Kipindi chote hicho changudoa yule hakujua kama mtu aliyekuwa akizungumza naye alikuwa Kamanda wa Kanda ya Dar es Salaam kutokana na giza lililokuwemo ndani ya gari ambalo halikuruhusu uso wake kuonekana kwa urahisi.
“Subiri kwanza!”

“Nisubiri nini na wakati unaniletea pozi?”
“Naomba unisikilize kwanza!”
“Wewe sema!”
“Niongezee hamsini! Tutalala mpaka asubuhi!”
“Daah! Sawa! Haina noma! Ingia twende!”

Changudoa yule akazunguka upande wa pili. Alipopita mbele ya gari lile na taa kummulika, umbo lake lilionekana vizuri machoni mwa Dickson, alikuwa msichana mrembo aliyeumbika, msichana aliyekuwa na nyonga zilizoweza kumtia matatani mwanaume yeyote yule. Dickson akameza mate kwa uchu, kila alipomwangalia, jinsi alivyotembea na umbo lake kutingishika vilivyo, alijikuta akipagawa mno. Alipoufikia mlango, akaufungua na kuingia ndani. Dickson akashusha pumzi ndefu.

“Kumbe huwa kunakuwa na wasichana warembo hivi!” alisema Dickson huku akiachia tabasamu.
“Kwani hujawahi kuchukua msichana huku?”
“Ndiyo! Hii ni mara ya kwanza.”
“Wazuri tupo, kama vipi tutabadilishane namba za simu ili tuwe tunashtuana,” alisema msichana yule.
“Hakuna tatizo!”

Dickson hakutaka kuendelea kubaki mahali hapo, alichokifanya ni kutekenya ufunguo kisha kuliondoka gari. Kadiri walivyokuwa wakiendelea kusonga mbele ndivyo uchu wa kufanya mapenzi ulivyozidi kumshika. Ndani ya gari kulikuwa na mwanga hafifu ambao haukumfanya changudoa yule kumuona Dickson usoni, gari lilizidi kwenda na wala hakuwa na shida ya kumuona kwani kitu alichokuwa akikitaka ni fedha tu na si kitu kingine. Njiani, Dickson alijipa uchangamfu mkubwa, alitawala mazungumzo kwa kipindi kirefu mno, alihitaji changudoa huyo amzoee ili hata watakapofika chumbani kusiwe na tatizo lolote lile. Hiyo wala haikuwa shida, walizungumza mno kiasi kwamba ilionesha kama walikwishakutana tangu miaka mitatu iliyopita.

Baada ya dakika kumi, gari likaanza kuingia katika nyumba ya wageni ya Chenchebe iliyokuwa Mwananyamala jijini Dar es Salaam. Alijua kwamba alikuwa na fedha nyingi lakini kwa kuwa alikuwa kamanda wa jeshi la polisi na kujulikana mno, kwenda hotelini aliona ni lazima angejulikana kutokana na umakini uliokuwepo kwenye hoteli nyingi, hivyo alichoamua ni kutumia gesti bubu.

Huko hakukuwa na uchunguzi, pamoja na kofia yake kubwa aliyoivaa, akalipia kisha kuelekea chumbani huku akiwa amekishikilia kiuno cha changudoa huyo. Walipoufikia mlango wa chumba hicho, wakaingia ndani, kama kawaida hakutaka taa iwashwe, mwanga hafifu uliokuwa ukitoka kwenye taa ya nje, uliwatosha mno.
“Huwa sipendi taa kabisa,” alisema Dickson.

“Kumbe wewe kama mimi, sipendi pia,” alijishaua msichana yule maneno yaliyoonekana kuwa uongo ila alitaka kuwa naye pasipo kujua sababu ya mwenzake kutopenda mwanga wa taa. Hapohapo akamshika kiuno na kumvutia kitandani.


Je, nini kitafuatia?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom