Hadithi: Jini Mweusi

Hadithi: Jini Mweusi

SEHEMU YA 47

Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam kufuatia kupotea mfululizo kwa machangudoa katika mazingira ya kutatanisha. Taharuki kubwa inazuka kwani ndani ya kipindi kifupi tu, zaidi ya machangudoa kumi na moja wanapotea na hakuna anayejua walikopotelea.

Jambo hilo linasababisha jeshi la polisi kuingilia kati. Kinachozidi kuzua utata, wote wanapotea katika mazingira yanayofanana. Mwanaume mmoja asiyejulikana, aliyekuwa anatembelea gari la kifahari aina ya Volkswagen, aliyekuwa akienda eneo hilo usiku wa manane ndiye anayehusishwa na wote wanaopotea.

Upande wa pili, kijana aliyekuwa na mwonekano tofauti na binadamu wa kawaida, Dickson Maduhu au Zinja kama wenzake walivyokuwa wakimtania, amejiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Hisia kali za mapenzi zinasababisha kijana huyo aanze kutoka usiku na kwenda kutafuta machangudoa. Hivyo baadaye anahamishiwa Dar es Salaam.

Mara baada ya kufanikiwa kuwa DCP, Dickson anajikuta akinogewa na penzi la changudoa mmoja aitwaye Pamela, umbo lake, ngozi vinamchanganya na kujikuta akianza kumganda pasipo kujua kwamba ukaribu wake na msichana huyo ungeweza kubadilisha kila kitu.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Huo ulikuwa mwanzo wa ukaribu baina ya Dickson na changudoa Pamela. Msichana huyo mrembo ambaye alivutia kila alipomwangalia aliliteka penzi la Dickson kiasi kwamba hata alipokuwa ofisini, hakuwa akifikiria kitu chochote kile zaidi ya penzi la msichana huyo mwenye umbo lenye mvuto.

Siku zikaendelea kukatika, hakukuwa na muda wa kutulia, saa mbili ofisini pasipo Pamela zilionekana kuwa nyingi, wakati mwingine alihakikisha anafanya kazi zake haraka iwezekanavyo kisha kurudi nyumbani ambapo alimpigia simu Pamela na kuja nyumbani kwake.

Wivu ukamjaa moyoni, wakati mwingine alimlazimisha msichana huyo alale nyumbani kwake kwani kila alipokuwa naye mbali, alihisi msichana huyo kulala na wanaume wengine kitu kilichouumiza mno moyo wake, kwa jinsi alivyokuwa na mapenzi mazito kwa Pamela, kuna kipindi alisahau kabisa kwamba msichana huyo alikuwa changudoa tu ambaye alilala na mwanaume yeyote aliyekuwa na pesa.

“Vipi tena?” aliuliza Pamela, ilikuwa mchana wa saa saba, alipigiwa simu na Dickson, haikuwa kawaida kitu hicho kutokea.

“Upo wapi?”

“Nipo nyumbani, kuna nini mpenzi?” aliuliza Pamela.

“Unaweza kuja mara moja?”

“Wapi?”

“Nyumbani kwangu.”

“Kwani haupo kazini?”

“Haujanijibu swali langu, unaweza kuja?”

“Naweza. Ila kuna nini?”

“Wewe njoo, wala usiogope,” alisema Dickson na simu kukatwa.

Kichwa chake kilichanganyikiwa mno, alichokitaka mahali hapo ni kumuona msichana huyo tu kwani hakukuwa na kitu alichokuwa akipenda kama kuwa karibu na Pamela.

Hakutaka kuendelea kukaa ofisini, alichokifanya ni kuondoka na kurudi nyumbani haraka ambapo wala hazikupita dakika nyingi, Pamela akafika, moja kwa moja akampeleka chumbani na kulala naye, hata kazi aliamua kuachana nayo kwa siku hiyo kwani penzi la Pamela lilimchanganya.

****
Magreth alibadilisha ratiba yake, kila siku akawa mtu wa kutembea katika viwanja mbalimbali vya machangudoa huku lengo lake likiwa ni kuona kama angefanikiwa kumpata mteja wake aliyemkimbia katika kipindi alichomhitaji sana.

Alizunguka na kuzunguka, tena wiki nzima mpaka alipofanikiwa kupata taarifa ambazo aliamini kwamba mtu aliyekuwa akizungumziwa alikuwa huyohuyo aliyekuwa akimhitaji.

“Umesema ana BMW nyeusi?” aliuliza changudoa mmoja.

“Ndiyo! Unamfahamu?”

“Kwa kweli sijawahi kumuona, ila huyo mteja anafika sana hapa kiwanjani,” alijibu changudoa huyo.

“Nitampata vipi?”

“Kwani ni nani kwako? Mumeo?”

“Hapana! Ila ninataka kuonana naye,” alisema changudoa huyo.

Jibu pekee alilopewa ni kwamba isingewezekana kuonana na mteja huyo kwani siku hizo hakuwa akifika sana kutokana na kulipata penzi la kudumu kutoka kwa msichana mrembo aliyetokea Arusha, Pamela.

Kitu alichokitaka Magreth ni kuonana na huyo Pamela kwa kuamini kwamba angepata taarifa nyingi juu ya mwanaume huyo na hata ikiwezekana kupafahamu kwake kwani hakukuwa na mteja ambaye alimpa fedha nyingi kama mwanaume huyo ambaye mpaka katika kipindi hicho hakujua alikuwa na sura gani.

Alipofanikiwa kuonana na Pamela, akajaribu kutengeneza urafiki naye, akaanza kumzoea, kila siku mchana akawa mtu wa kwenda kumtembelea, kwa kuwa Pamela hakuwa na marafiki wengi na pia hakuwa amelizoea sana jiji, akaupokea urafiki wa Magreth pasipo kujua msichana huyo alihitaji nini.

Mpaka siku ambayo Dickson alimpigia Pamela simu na kumuita nyumbani, Magreth alikuwa pamoja naye chumbani, alichokifanya ni kumuaga kwa lengo la kwenda huko.

“Ndiyo unakwenda kuonana naye?” aliuliza Magreth.

“Ndiyo! Unataka twende wote?” aliuliza Pamela huku akionekana dhahiri kwamba alikuwa akitania.

“Hahah! Kama inawezekana! Kwani hawezi kulala na wanawake wawili?” aliuliza Magreth, naye mwenyewe alionesha kutania.

Pamela hakujibu swali hilo zaidi ya kucheka kisha kuondoka nyumbani hapo. Kwa Magreth alionekana kuwa na uhakika kwamba mwanaume huyo ambaye Pamela alikwenda kuonana naye ndiye yule ambaye alifika sana katika kiwanja chake, Sinza Mori na kumnunua, lakini ghafla akapotea na hakurudi tena.

“Atakuwa ndiye yeye tu, ni lazima nimtafute, nipajue kwake na kumrudisha mikononi mwangu,” alisema Magreth pasipo kujua mtu huyo alikuwa nani.

Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 48

Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam kufuatia kupotea mfululizo kwa machangudoa katika mazingira ya kutatanisha. Taharuki kubwa inazuka kwani ndani ya kipindi kifupi tu, zaidi ya machangudoa kumi na moja wanapotea na hakuna anayejua walikopotelea.

Jambo hilo linasababisha jeshi la polisi kuingilia kati. Kinachozidi kuzua utata, wote wanapotea katika mazingira yanayofanana. Mwanaume mmoja asiyejulikana, aliyekuwa anatembelea gari la kifahari aina ya Volkswagen, aliyekuwa akienda eneo hilo usiku wa manane ndiye anayehusishwa na wote wanaopotea.

Upande wa pili, kijana aliyekuwa na mwonekano tofauti na binadamu wa kawaida, Dickson Maduhu au Zinja kama wenzake walivyokuwa wakimtania, amejiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Hisia kali za mapenzi zinasababisha kijana huyo aanze kutoka usiku na kwenda kutafuta machangudoa. Hivyo baadaye anahamishiwa Dar es Salaam.

Mara baada ya kufanikiwa kuwa DCP, Dickson anajikuta akinogewa na penzi la changudoa mmoja aitwaye Pamela, umbo lake, ngozi vinamchanganya na kujikuta akianza kumganda pasipo kujua kwamba ukaribu wake na msichana huyo ungeweza kubadilisha kila kitu.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Magreth hakutaka kukurupuka, alitaka kufanya vitu kimyakimya, yaani kumchunguza rafiki yake mpaka pale ambapo angepata ukweli wa mambo ili ajue ni kitu gani cha kufanya.


Alijipanga, hakutaka kushtukiwa kabisa. Siku iliyofuata ambapo Pamela alirudi nyumbani, alimtembelea na kumchangamkia kama ilivyo siku nyingine, yote hayo aliyafanya kwa sababu alihitaji kufahamu mwanaume aliyekuwa akitembea naye aliishi wapi, kwani hata yeye alikuwa akimhitaji kwa sababu alikuwa bwana wake kitambo.

Alihakikisha hachezi mbali na simu ya Pamela, alijitahidi kufuatilia namna ya kutoa loki za kwenye simu kwa mtindo wa kuzungusha pattern, alipozikariri, kazi ikawa kwake kuifungua na kufanya yake.

Alimvizia Pamela alipokwenda bafuni kuoga ndiyo ukawa muda wake wa kuchukua simu yake kisha kuanza kuiangalia palepale kitandani. Alitoa loki kisha kuanza kuangalia namba zilizoingia jana usiku, muda ule ambao alitakiwa kuondoka nyumbani.

Jina alilokutana nalo lilikuwa Mapesa, akajua kwamba hiyo ndiyo namba ya huyo bwana aliyekuwa na wasiwasi naye. Alichokifanya ni kuchukua simu yake na kuangalia namba, zilikuwa za mtu yuleyule, mwanaume aliyekuwa akilala naye kwa malipo makubwa.

“Ndiye yeye!” alisema Magreth huku akiachia tabasamu pana na la kinafiki.

Huo ndiyo ukawa mwanzo wa kazi yake ya kumtafuta mwanaume huyo. Kitu cha kwanza alichokitaka ni kufahamu mahali alipokuwa akiishi, hilo wala halikuwa tatizo, kwa sababu alikuwa rafiki kipenzi wa Pamela, ndani ya siku chache tu akafahamu mahali alipokuwa akiishi mwanaume huyo, Dickson.

Kilichofuata ni kuanza kumvizia, kila siku usiku alihakikisha anakwenda nyumbani kwa mwanaume huyo, anakaa nje kwa mbali huku akimsubiri aingie nyumbani kwake kwa lengo la kwenda kuzungumza naye lakini kila siku aliambulia patupu, hakuwa akibahatika kuonana na mwanaume huyo, kwani mara nyingi alikuwa akilala hotelini na Pamela, aliporudi ilikuwa ni asubuhi.

Magreth alifuatilia kwa takriban wiki mbili ndipo siku moja akafanikiwa kuliona gari la Dickson likianza kuingia ndani ya jumba hilo la kifahari. Kwa kasi kubwa, Magreth akajitoa kule alipokuwa amejificha na kuanza kupiga hatua za haraka kuelekea lilipokuwa geti la nyumba ile, alitaka kuzungumza na mwanaume huyo.

Alipolifikia gari, kwa haraka akaenda katika mlango wa gari na kuanza kugonga kioo huku akihitaji kufunguliwa.

Dickson aliyekuwa ndani alishtuka, akaanza kujiuliza mtu huyo alikuwa nani mpaka kupata ujasiri wa kutaka kufunguliwa mlango. Kitu cha kwanza alihisi kwamba alikuwa jambazi, alipomwangalia vizuri, alikuwa msichana ambaye wala hakumfahamu vizuri kutokana na mwanga hafifu.

Kabla hajashusha kioo cha gari, akahakikisha anaangalia sehemu nyingine kama kulikuwa na watu wengine ambao alihisi ndiyo waliomtuma msichana huyo, alipoona amani imejaa, akashika bunduki yake kama tahadhari kisha kushusha kioo.

“Nikusaidie nini binti?” aliuliza Dickson, garini mwake hakukuwa na mwanga mkali. Mkono wake wa kushoto ulishikilia bunduki kisiri.

“Umenisahau mpenzi?” aliuliza Magreth, Dickson akashtuka, kwani sauti aliyoisikia haikuwa ngeni, na hata alipomwangalia vizuri msichana huyo, aligundua kwamba alikuwa Magreth.

“Mage…”

“Ndiyo mimi kipenzi. Nimekukumbuka sana,” alisema msichana huyo.

“Umepajuaje hapa?”

“Nani? Mimi? Mbona nimepajua kawaida tu.”

“Mmh!”

“Usijali mpenzi!

Kitendo cha Magreth kupafahamu alipokuwa akiishi lilionekana kuwa kosa kubwa, alijua fika kwamba mwisho wa siku msichana huyo angegundua kwamba yeye alikuwa kamanda mkuu jijini Dar es Salaam.

Alichokifanya ni kumchangamkia kisha kumchukua na kuelekea naye ndani, tena huku akihakikisha anaivaa kofia yake. Magreth alionekana kuwa na furaha mno, kitendo cha kuona kwamba mwanaume huyo amempokea kwa mapenzi motomoto, kilimfurahisha.

Akamchukua na kumpeleka ndani huku akihakikisha gari amelipaki vizuri. Alipofika humo, hakuwasha taa sebuleni, aliunganisha naye mpaka chumbani kisha akamlaza kitandani.

Alichokitaka ni kumuua msichana huyo tu. Alihitaji kuwa na amani, hakuhitaji presha, alijua fika kwamba endapo angemuacha msichana huyo basi kitu ambacho kingefuata ni aibu kubwa.

Magreth angejua kwamba nyumba ile ni ya kamanda wa jeshi la polisi na mwisho wa siku kuwatangazia watu kwamba mtu huyo alikuwa bwana wake. Alipofikiria mambo yote hayo, hakuona sababu ya msichana huyo kuendelea kuwa hai.

Alipofikishwa kitandani na kulazwa chali, alifurahi kwa kuona kwamba hatimaye alifanikiwa kumrudisha bwana wake mikononi mwake. Alijiachia kitandani pale, alijiweka vizuri tayari kwa kumkaribisha Dickson katikati ya miguu yake pasipo kujua kwamba mwanaume huyo alikuwa na vitambaa kadhaa mikononi mwake kwa ajili ya kumziba pumzi na kumuua. Hilo, Magreth hakulitambua kwa sababu ya giza.


Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 49

Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam kufuatia kupotea mfululizo kwa machangudoa katika mazingira ya kutatanisha. Taharuki kubwa inazuka kwani ndani ya kipindi kifupi tu, zaidi ya machangudoa kumi na moja wanapotea na hakuna anayejua walikopotelea.

Jambo hilo linasababisha jeshi la polisi kuingilia kati. Kinachozidi kuzua utata, wote wanapotea katika mazingira yanayofanana. Mwanaume mmoja asiyejulikana, aliyekuwa anatembelea gari la kifahari aina ya Volkswagen, aliyekuwa akienda eneo hilo usiku wa manane ndiye anayehusishwa na wote wanaopotea.

Upande wa pili, kijana aliyekuwa na mwonekano tofauti na binadamu wa kawaida, Dickson Maduhu au Zinja kama wenzake walivyokuwa wakimtania, amejiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Hisia kali za mapenzi zinasababisha kijana huyo aanze kutoka usiku na kwenda kutafuta machangudoa. Hivyo baadaye anahamishiwa Dar es Salaam.

Mara baada ya kufanikiwa kuwa DCP, Dickson anajikuta akinogewa na penzi la changudoa mmoja aitwaye Pamela, umbo lake, ngozi vinamchanganya na kujikuta akianza kumganda pasipo kujua kwamba ukaribu wake na msichana huyo ungeweza kubadilisha kila kitu.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Dickson hakuwa na hamu ya kufanya mapenzi na Magreth, alichokifikiria ni kumuua msichana huyo tu. Alimwangalia kitandani pale, kwa jinsi alivyojiachia, alijua fika kwamba endapo angeleta mchezo na kumuacha hai msichana huyo ilikuwa ni lazima aumbuke hapo baadaye.

Vitambaa vyake vilikuwa mikononi mwake, Magreth hakuwa na hofu yoyote ile, alijiweka vizuri pale kitandani huku akianza kuchojoa nguo moja baada ya nyingine.

“Come to me big dad…” (Njoo kwangu baba…) alisema Magreth kwa kutumia maneno ya mahaba. Dickson akakifikia kitanda kile na kumsogelea karibu.

Hakuwa na huruma, hiyo haikuwa mara ya kwanza kuua, alikwishawahi kufanya hivyo kabla hivyo hilo halikuwa tatizo kwake, kwa kasi ya ajabu, hapohapo akaviandaa vitambaa vile na kumfunika navyo Magreth puani na mdomoni.

Msichana huyo akaanza kukukuruka kitandani pale, akaanza kurusha mikono yake huku na kule kama mtu aliyekaribia kukata roho. Dickson hakutaka kumuacha, aliendelea kumkandamizia vitambaa vile. Kutokana na nguvu kubwa aliyokuwa nayo, Magreth akashindwa kujitoa mikononi mwa mwanaume huyo, ndani ya dakika mbili tu, nguvu zikaanza kumuisha na baada ya sekunde chache, akatulia kitandani hapo, pumzi ikakata na kufariki dunia.

“Haina jinsi Magreth…” alisema Dickson.

Alipohakikisha kwamba msichana huyo amekufa, akaelekea jikoni akachukua maji na kuyaweka kwenye bakuli kisha kurudi mle chumbani. Akachukua kitambaa na kuanza kuufuta mwili ule katika sehemu zote zilizokuwa na alama za vidole vyake.

Hakutaka kugundulika, alijua fika kwamba kama asingefanya hivyo basi ilikuwa ni lazima kugundulika kwani alama za vidole zingepimwa na uchunguzi kuanza kufanyika.

Alipoona kwamba amezifuta alama zote, akauzungushia shuka kisha kuubeba na kutoka nao nje. Alipofika nje, akaelekea katika eneo la maegesho ya magari yake, akaupakiza mwili ule ndani ya gari kisha kuondoka nao.

Hali ya hewa ilianza kubadilika, mawingu yalijikusanya angani na upepo kuanza kuvuma hali iliyoonesha kipindi kichache kijacho mvua kubwa ingeweza kunyesha.

Dickson akaenda stoo ambapo alichukua koleo na sururu kisha akaelekea ndani ya gari, kilichofuata ni kuanza safari ya kuelekea katika Msitu wa Pande huku lengo lake likiwa ni kwenda kuuzika mwili ule.

Mvua kubwa ikaanza kunyesha, Dickson hakurudi nyuma, alichotaka ni kumalizana na suala la mwili wa Magreth usiku huohuo. Kwa kuwa hakuwa na foleni usiku huo, alitumia dakika kumi tu, akaanza kuukaribia msitu huo.

“Ngoja niingie hapahapa,” alisema Dickson kisha kukata upande wa kushoto na kuingia ndani ya msitu huo.

Aliliendesha gari katika njia iliyokuwa na nyasi ndefu zilizolowanishwa na mvua iliyoendelea kunyesha. Alikwenda mbele zaidi huku taa za gari lake zikiwa full. Aliendesha mpaka alipofika katika sehemu iliyokuwa imezungukwa na miti mingi, akasimamisha gari na kuteremka huku mkononi akiwa na bunduki kwa ajili ya tahadhari.

Hakuutoa mwili kwanza, akachukua vifaa vyake na kuanza kuchimba shimo msituni pale. Hakutaka kujiamini kwamba alikuwa peke yake, muda mwingi aliangalia huku na kule ili kuona kama kulikuwa na mtu mwingine zaidi yake.

Alichukua dakika zaidi ya ishirini, shimo likakamilika, alichokifanya ni kurudi garini, akauchukua mwili wa Magreth na kwenda kuuingiza kwenye shimo lile kisha kuanza kuufukia.

****
“Unasemaje?”

“Tumeletewa taarifa ya mauaji!”

“Kutoka wapi?”

“Mbezi! Kuna taarifa kwamba inasemekana kuna mwili umefukiwa.”

“Wapi?”

“Kwenye msitu wa Pande!”

“Lini hiyo?”

“Jana usiku wakati mvua kubwa ilipokuwa ikinyesha,” ilisikika sauti ya polisi mmoja.

Polisi wa Kituo cha Polisi cha Mbezi walikuwa wakitoa taarifa kwa mkuu wa kituo hicho kwamba siku hiyo waliambiwa kwamba kulikuwa na taarifa zilizodai kwamba kuna mwili wa mtu ulikuwa umefukiwa msituni.

Taarifa hizo zikapokelewa hivyo polisi wanne waliokuwa na bunduki mikononi mwao, wakiwa ndani ya gari lao kuanza safari ya kuelekea huko walipoambiwa kwamba mwili wa mtu ulipozikwa.

Hawakuchukua dakika nyingi, wakafika katika eneo ambalo watu wengi waliingia msituni kwenda kushuhudia kile kilichokuwa kimetokea, nao wakaliingiza gari kuelekea huko.

Mbele, wakakutana na umati mkubwa wa watu ukiwa umekusanyika kwa staili ya kuzunguka kitu, walichokifanya ni kuwasogeza watu hao na kisha kuelekea pale ambapo kulionekana kama kuna kitu kimefukiwa, wakaanza kufukua.

“Kuna nini kwani?” alisikika mwanamke mmoja akiuliza.

“Nasikia kuna mwili umezikwa. Ila ni tetesi, sijui kama ni kweli,” alijibu mwanaume mmoja kwa sauti ya chini. Bado polisi waliendelea kulifukua shimo lile.
 
SEHEMU YA 50

Alijijengea heshima kubwa nchini Tanzania kutokana na utendaji kazi wake mkubwa aliokuwa akiufaya katika jeshi la Polisi nchini Tanzania. Kutokana na umahiri wake, akajikuta akipandishwa vyeo na mwisho wa siku akijikuta akiwa Kamanda Mkuu Kanda ya Dar es Salaam, DCP.

Heshima yake inakuwa kubwa, kila anayemuona anamheshimu kutokana na utendaji wake mzuri wa kazi. Pamoja na heshima zote hizo, mwanaume huyu aliyeitwa Dickson alikuwa mtu mwenye sura mbaya ambapo huko shuleni kipindi cha nyuma aliitwa kwa jina la Zinjathropus, yaani binadamu wa zamani.

Hakuwa na mchumba, hakuwa na mpenzi, alichokifanya ni kuanza kununua machangudoa. Alifanikiwa sana, alilala na wengi. Alipofika Dar es Salaam, akaendelea kulala nao ila kwa kila ambaye alimuona sura yake na kumgundua, alimuua, alitaka suala la kununua machangudoa liwe siri maisha yake yote.

Upande wa pili kuna mwanamke mrembo aitwaye Pamela, msichana huyu mwenye umbo matata amefika jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufanya kazi ya uchangudoa. Anapofika huko, kutokana na uzuri wake, anawapata wanaume wengi, anamtetemesha kila mtu, si wanaume tu, hata wanawake wenzake.

SONGA NAYO…

‘Do not cross’ (usivuke) yalikuwa maneno machache yaliyoandikwa katika viplastiki mfano wa kamba zilizozunguka sehemu hiyo ambayo kulikuwa na kazi maalum ya kufukua sehemu ambayo watu walisema kulikuwa na mwili uliofukiwa.

Polisi walikuwa bize kulifukua shimo hilo, hakukuwa na kazi kubwa kwani ardhi ililowa kwa kiasi kikubwa kutokana na mvua kubwa iliyonyesha usiku. Baada ya dakika kadhaa, wakaufikia mwili huo, wakayaweka makoleo pembeni kisha kuanza kufukua kwa mikono.

“Mungu wangu!”

Kila mmoja alishtuka, mwili wa mwanamke ukatolewa katika shimo lile, baadhi ya wanawake waliokuwa mahali hapo wakashindwa kuvumilia, wakaanza kulia, waliumia mioyo yao, kile kilichokuwa kikionekana, kilikuwa ni ukatili wa hali ya juu.

“Utoeni kabisa, hakikisheni hamgusi sehemu zile zinazotakiwa kufanyiwa uchunguzi,” alisema polisi mmoja ambaye alionekana kuwa kiongozi wa polisi waliokuwa mahali pale.

Mwili wa Magreth ukachukuliwa na kupelekwa pembeni kabisa, watu wengine hasa wanawake wakashindwa kubaki mahali hapo, wakaondoka huku wakiwa wenye nyuso za huzuni.

“Mmewapigia simu?” aliuliza kamanda.

“Akina nani?”

“Watu wa uchunguzi.”

“Ndiyo! Wamesema wanakuja mkuu!”

Zilipita dakika kumi na tano, gari jingine likafika mahali hapo, wanaume wanne waliokuwa na mavazi maalum na glavu mikononi mwao wakateremka na kuanza kupiga hatua kule kulipokuwa na polisi wale wengine ambao walikuwa na mwili wa Magreth pembeni.

Mara baada ya kuzungumza nao kidogo, wakaanza kuuchunguza mwili ule palepale, lengo lao likiwa ni kutaka kubaini alama za vidole, waliporidhika, wakaubeba na kuupandisha ndani ya gari na safari ya kuelekea hospitalini kuanza.

“Hii ni hatari sana…”alisikika polisi mmoja.

* * *
‘Mwili wa Mwanamke wakutwa Msituni’, Muuaji aibuka jijini Dar’, Dar Yageuka Machinjioni’, hivyo vilikuwa vichwa mbalimbali vya habari katika magazeti yaliyotoka siku moja baada ya mauaji ya msichana Magreth.

Kila mtu aliyeyaona magazeti yaliyokuwa na vichwa hivyo vya habari hiyo, alishtuka, si kwamba hawakuwa wakijua kama kulikuwa na mauaji ya chinichini yaliyokuwa yakiendelea bali kitendo cha kukutwa msichana mwingine akiwa ameuawa msituni ndicho kilichowashtua zaidi.

Waandishi wa magazeti hayo waliandika habari ndefu ambayo ilionekana dhahiri kwamba muuaji wa mauaji yote hayo alikuwa mtu mmoja. Walianza na taarifa ile ya kwanza kabisa, mauaji ya msichana ambaye aliuawa katika Msitu wa Pande, taarifa zilisema kwamba muuaji huyo alivalia kofia kubwa ili kuuficha uso wake.

Shuhuda pekee wa tukio lile, mzee Gombana ambaye ndiye alimuona muuaji huyo na kusema kwamba alivaa kofia kubwa, mwisho naye alikufa katika kifo kilichojaa utata mkubwa baada ya kutoka katika kituo cha polisi kutoa maelezo.

Ukiachana na mzee huyo, pia alizungumziwa msichana mwingine aliyekuwa akiishi Mwananyamala, msichana huyo ambaye alikuwa akifanya kazi katika gesti bubu moja aliuawa bafuni wakati anaoga huku vijana ambao walimuona muuaji huyo wakisema kwamba alivalia kofia kubwa ambayo iliwapa ugumu kuuona uso wake.

Muuaji alikuwa nani? Kwa nini aliua? Hayo yalikuwa maswali yaliyokuwa vichwani mwa watu wengi, hakukuwa na mtu aliyekuwa na jibu lolote lile. Watu waliendelea kujiuliza juu ya muuaji lakini bado vichwa vyao viliendelea kuwa na giza.

“Ni lazima muuaji apatikane,” alisema polisi wa Kituo cha Mbezi.

“Sawa mkuu! Tutafanya hivyo!”

Ilikuwa ni lazima taarifa hizo zifikishwe makao makuu ya polisi jijini Dar ambapo ndipo muuaji, kamanda Dickson alipokuwa. Ndani ya dakika arobaini, tayari taarifa za mauaji yale zilikuwa mezani kwa kamanda Dickson ambapo baada ya kuzisoma, akapigwa na mshtuko na kujiuliza ni kwa namna gani watu walifahamu kule alipouzika mwili ule usiku kwani aliamini kwamba hakukuwa na mtu aliyemuona.

“Ni nani alimuona muuaji akiingia msituni?” aliuliza kamanda Dickson.

“Taarifa zinasema ni wawindaji.”

“Mmh! Waliweza kumuona wakati anachimba shimo na kuufukia mwili?” aliendelea kuuliza, alitaka kupata jibu.

“Hapana ila walisema waliliona gari likiingia msituni, wao wakakimbia kujificha…”

“Baada ya hapo?”

“Gari lilipoondoka ndipo walipokwenda kuona kulikuwa na nini, wakahisi kwamba kulikuwa na mwili umefukiwa, hivyo wakatoa taarifa,” alisema polisi mmoja.

“Sawa, unaweza kwenda.”

“Asante mkuu,” alisema polisi huyo kisha kupiga saluti kama heshima, akaondoka zake. Kamanda Dickson akabaki ofisini akiwa na presha kubwa.


Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 51

Alijijengea heshima kubwa nchini Tanzania kutokana na utendaji kazi wake mkubwa aliokuwa akiufanya katika jeshi la polisi nchini Tanzania. Kutokana na umahiri wake, akajikuta akipandishwa vyeo na mwisho wa siku akajikuta akiwa Kamanda Mkuu Kanda ya Dar es Salaam, DCP.

Heshima yake inakuwa kubwa, kila anayemuona anamheshimu kutokana na utendaji wake mkubwa aliokuwa akiufanya. Pamoja na heshima zote hizo, mwanaume huyu aliyeitwa Dickson alikuwa mtu mwenye sura mbaya ambapo huko shuleni kipindi cha nyuma aliitwa kwa jina la Zinjathropus, yaani binadamu wa zamani.

Hakuwa na mchumba, hakuwa na mpenzi, alichokifanya ni kuanza kununua machangudoa. Alifanikiwa sana, alilala na wengi. Alipofika Dar es Salaam, akaendelea kulala nao ila kwa kila ambaye alimuona sura yake na kumgundua, alimuua, alitaka suala la kununua machangudoa liwe siri maisha yake yote.

Upande wa pili kuna mwanamke mrembo aitwaye Pamela, msichana huyu mwenye umbo matata amefika jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufanya kazi ya uchangudoa. Anapofika huko, kutokana na uzuri wake, anawapata wanaume wengi, anamtetemesha kila mtu, si wanaume tu, hata wanawake wenzake.

SONGA NAYO.

“Unaweza kuja nyumbani leo?” ilisikika sauti ya Dickson kwenye simu.

“Mimi?”

“Kwani nazungumza na nani mpenzi? Ndiyo! Wewe hapo.”

“Mmh! Kwa leo sidhani, kuna msiba huku.”

“Nani amefariki?””Rafiki yangu, anaitwa Magreth!”

“Pole sana aiseee. Basi sawa, nitakucheki keshokutwa,” alisema Dickson na kukata simu.

Muda huo, mwili wake ulimuwaka moto, alikuwa na hamu ya kuwa na mwanamke hata kwa saa moja tu. Mtu pekee ambaye kila siku aliuridhisha moyo wake alikuwa msichana Pamela tu.

Alimpigia simu na kumwambia kwamba asingeweza kuja kwa kuwa alikuwa kwenye msiba wa rafiki yake. Hapo ndipo Dickson alipogundua kwamba kumbe Magreth alifahamiana na Pamela.

Hakutaka kukaa nyumbani, pepo la ngono alilokuwa nalo lilimchanganya mno, alichokifanya ni kuondoka nyumbani na kwenda Ambiance ambapo aliamini kwamba angepata msichana mzuri wa kulala naye usiku wa siku hiyo.

Kama kawaida yake akaingia ndani ya gari lake na kuanza safari ya kuelekea huko kwa ajili ya kumnunua changudoa na kulala naye usiku huo. Ndani ya gari, alijiona kuchelewa kufika huko alipokuwa akielekea, aliendesha kwa kasi kubwa na ndani ya dakika ishirini, akafika Ambiance ambapo pembeni kulikuwa na wanawake wengi waliokuwa wakijiuza.

Hata kabla hajachagua yupi wa kumfuata, ghafla wasichana wanne wakasogea kule alipokuwa, walivalia mavazi tofauti, wengine taiti na wengine vimini vilivyoyaacha mapaja yao wazi.

“Ngoo… ngoo… ngoo…” kioo cha mlango wa gari kiligongwa na msichana mmoja. Akakishusha na kuwaangalia wasichana hao. Hakukuwa na aliyemfahamu kutokana na giza kubwa lililokuwa ndani ya gari.

“Karibu mpenzi…” alisema msichana mmoja huku akijinyonganyonga.

“Asante. Bei inakwendaje?”

“Kulala au show time?”

“Kulala!”

“Elfu sitini,” alisema msichana huyo.

“Nyingi sana. Mwingine?”

“Subiri kwanza kaka! Mbona hatujaelewana! Bei mazungumzo mpenzi!”

“Utapunguza hadi ngapi?” aliuliza Dickson.

Kilichokuwa kikiendelea mahali hapo ni kukubaliana kwa bei na changudoa huyo aliyesimama nje ya gari lake huku wale wengine wakiwa wamekwishaondoka kwani mwenzao huyo alichaguliwa hivyo ndiye aliyetakiwa kukubaliana bei na mteja huyo.

Baada ya dakika kadhaa, wakakubaliana na hivyo msichana huyo kutakiwa kuingia ndani ya gari na kuondoka mahali hapo, changudoa huyo akafanya hivyo.

Alivyoingia ndani ya gari, ndipo Dickson alipogundua uzuri wa changudoa huyo. Kimini alichokuwa nacho ambacho kiliishia mapajani, alipokaa kitini, kikajivuta kwa juu na kumfanya Dickson kuweweseka zaidi.

Hawakuchukua muda mrefu wakafika katika nyumba moja ya wageni iliyokuwa Manzese Midizini. Gari likasimamishwa hivyo kutakiwa kuteremka. Changudoa yule alibaki na mshangao, hakuamini kama safari yao ingeishia ndani ya nyumba hiyo.

Ilikuwa uswahilini mno ambapo bei yake isingeweza kuwa zaidi ya shilingi elfu tano. Mtu aliyekuwa amemnunua kutoka katika kiwanja chake, alionekana kuwa bwana wa haja, mwenye pesa lakini kitendo cha kupelekwa katika chumba kile, ilimshangaza.

“Tumefika!” alisema Dickson.

“Nidiyo humu?” aliuliza changudoa yule kwa mshangao.

“Ndiyo! Kwani tatizo nini?”

“Mbona unaonekana una pesa sana, au hata hili gari umeazima?”

“Hapana. Ni maamuzi tu. Unataka hela au unataka kulala kwenye kitanda cha gharama?” aliuliza Dickson, alionekana kuanza kukasirika.

“Nataka hela.”

“Kama unataka hela twendeni,” alisema Dickson.

Kwa sauti aliyoitoa, hata changudoa yule alihisi kwamba alimkosea Dickson kwa kumuoneshea ishara ambazo moja kwa moja zilionekana kama kudharauliwa, alitamani kumuomba msamaha lakini akashindwa kufanya hivyo, kama malipo yake, akaahidi kufanya kila liwezekanalo amchanganye chumbani tu.

Kofia yake haikutoka kichwani mwake, bado hakuhitaji kujulikana, kila kitu kilikuwa siri kubwa kwake, walipofika mapokezi, akalipia chumba na kwenda chumbani tayari kwa kufanya kile kilichowapeleka pale.

“Naruhusiwa kuweka masharti kama mteja?” aliuliza Dickson.

“Kama lipi?”

“Napenda kufanya gizani, sipendi taa.”

“Kweli?”

“Ndiyo!”

“Hata mimi napenda giza, hakuna tatizo,” alisema msichana huyo kwa furaha, tena huku akionekana kuchangamka sana, kwa muonekano wake tu, alionekana kuwa na kitu nyuma ya pazia, Dickson hakuelewa hilo.


Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 52

Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam kufuatia kupotea mfululizo kwa machangudoa katika mazingira ya kutatanisha. Taharuki kubwa inazuka kwani ndani ya kipindi kifupi tu, zaidi ya machangudoa kumi na moja wanapotea na hakuna anayejua walikopotelea.

Jambo hilo linasababisha jeshi la polisi kuingilia kati. Kinachozidi kuzua utata, wote wanapotea katika mazingira yanayofanana. Mwanaume mmoja asiyejulikana, aliyekuwa anatembelea gari la kifahari aina ya Volkswagen, aliyekuwa akienda eneo hilo usiku wa manane ndiye anayehusishwa na wote wanaopotea.

Upande wa pili, kijana aliyekuwa na mwonekano tofauti na binadamu wa kawaida, Dickson Maduhu au Zinja kama wenzake walivyokuwa wakimtania, amejiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Hisia kali za mapenzi zinasababisha kijana huyo aanze kutoka usiku na kwenda kutafuta machangudoa. Hivyo baadaye anahamishiwa Dar es Salaam.

Mara baada ya kufanikiwa kuwa DCP, Dickson anajikuta akinogewa na penzi la changudoa mmoja aitwaye Pamela, umbo lake, ngozi vinamchanganya na kujikuta akianza kumganda pasipo kujua kwamba ukaribu wake na msichana huyo ungeweza kubadilisha kila kitu.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Dickson akashtuka kutoka katika usingizi mzito, mwili wake ulikuwa umechoka mno, akaangalia huku na kule, alitaka kufahamu alikuwa sehemu gani kwani kwa jinsi kitanda kile kilivyokuwa, alikuwa na uhakika kwamba hapo hapakuwa nyumbani kwake.

Akayafikicha macho yake na kuiangalia sehemu hiyo, ilikuwa katika nyumba ya wageni. Kumbukumbu zake zikaanza kurudi nyuma ili ajue sababu zilizomfanya kuwa ndani ya chumba hicho.

Hapo ndipo alipokumbuka kwamba mara ya mwisho kabisa alikuwa chumbani na mwanamke, walishikana hapa na pale, kilichofuata, hakukikumbuka. Akaelekea katika suruali yake, alitaka kuona kama fedha zake zilikuwepo, hakukuta kitu, si fedha tu, hata simu yake pia haikuwepo.

Akajikuta akiuma meno kwa hasira, mwili ukaanza kumtetemeka mithili ya mtu anayesikia baridi, kwa sababu kwa mbali mwanga wa alfajiri ulishaanza kutokeza, akainuka, akavaa nguo zake na kuondoka chumbani hapo huku akiwa na kofia yake kichwani.

Hakumsalimia dada wa mapokezi, aliunganisha moja kwa moja mpaka nje, akalifuata gari lake na kuondoka huku akiwa na hasira kali dhidi ya changudoa aliyemlevya na kumuibia

Alichokitaka ni kulipa kisasi, hakutaka kumuacha changudoa huyo aendelee kuishi kwani akili yake ilimwambia kwamba kabla ya kuondoka, alimwangalia usoni na kumgundua alikuwa nani, hivyo akaenda kuwaambia marafiki zake.

Hakutaka kuona siri hiyo ikivuja, kwa hali na mali, tena kwa gharama yoyote ile ilikuwa ni lazima amuue changudoa huyo. Hakujua alifananaje, alichokikariri kutoka kwake ni miguu yake, ilikuwa imejaajaa huku kwa mbali akiwa na matege. Mbali na miguu hiyo, sura yake ilikuwa na chunusi nyingi zilizomfanya kumpendezesha sana na kumfanya avutie.

“Nitamtafuta, na nitamuua tu, si yeye, hadi marafiki zake wote ni lazima niwamalize wote kwa kuwa najua atakuwa amewaambia tu,” alisema Dickson huku akionekana kuwa mwingi wa hasira.

Alichokifanya mara baada ya kufika ofisini ni kuagiza usiku wa siku hiyo katika sehemu zote ambazo zilikuwa na machangudoa waliokuwa wakijiuza, ilikuwa ni lazima polisi waende kuwakamata na ikiwezekana wawaweke ndani na yeye mwenyewe kwenda kuwaangalia.

Polisi walishangaa sababu ya Kamanda Dickson kuamua hivyo lakini hakukuwa na mtu mwenye maswali, kwa kuwa amri ile ilitolewa na mkuu wao, ikawabidi waifuate kama walivyotakiwa.

Usiku wa usiku huo polisi wakafanya doria sehemu zote zilizokuwa na machangudoa, wengi wakakamatwa na kupelekwa vituoni, asubuhi iliyofuata Kamanda Dickson akaanza kutembelea kila kituo na kuwaangalia machangudoa hao, alipoona hakuna mbaya wake aliyekuwa akimtafuta, akaachana nao.

“Nitampata tu, ni suala la muda tu,” alijisemea Kamanda Dickson.

* * *

Kichwa cha Pamela kilikuwa na mawazo mengi, stori alizopewa kuhusu mtu mwenye gari nyeusi ambaye alikuwa akiwachukua wasichana na kwenda kuwaua ilimuogopesha.

Moyo wake ulijawa na hofu lakini hiyo haikuwa sababu iliyojitosheleza ya kumfanya asimame na kuachana na shughuli zake. Alitoka jijini Arusha mpaka Dar es Salaam kwa sababu alihitaji fedha, alijipanga na katika kipindi ambacho aliishi jijini Dar, tayari aliyaona mafanikio, hivyo kuachana na biashara ya kujiuza ilikuwa ngumu.

“Umakini ndiyo unaohitajika tu,” alijisemea.

Machangudoa wote wa Kinondoni hawakuwa watokaji, ili ufanye nao ngono ilikuwa ni lazima iwe hapohapo makaburini au ndani ya gari lako, ila si kuondoka katika eneo hilo na kwenda hotelini au sehemu nyingine.

Kwa Pamela ilikuwa tofauti, aliyatoa maisha yake sadaka, alijua kwamba wanaume wengi hawakupenda kufanya ngono makaburini kwa kisingizio cha kuogopa laana, hivyo kama na yeye angefanya kama watu wengine basi asingepata fedha, hivyo ilikuwa ni lazima kufanya kama zamani.

Machangudoa wengine walimshangaa Pamela lakini hakuonekana kujali, alihitaji kuwa na fedha, hivyo hata suala la kuuawa, aliliita ajali kazini.

Siku ya kwanza ikapita, ya pili, ya tatu mpaka wiki nzima, hali ilikuwa ni amani tele, hakuuawa wala kukutana na mtu mbaya, wote waliokuja kwake ambao walimtaka kwenda kulala naye, walikuwa watu wema mpaka kufikia hatua akahisi kwamba inawezekana stori hizo zilikuwa ni uzushi tu.

Baada ya wiki nzima kukatika, hapo ndipo akajikuta mikononi mwa polisi. Hakuwa yeye, walikuwa na machangudoa wengine wengi, walifungwa pingu na kupelekwa vituoni.

Kila mmoja alishangaa, hakukuwa na taarifa kama siku nyingine ambapo kabla ya polisi kufanya doria, waliletewa taarifa, doria ya siku hiyo ilikuwa ya ghafla sana hivyo machangudoa wengi kujikuta wakiingia mkenge.

Alilala sero na wenzake, kesho yake, hawakuachiwa bali waliambiwa wasubiri kwani Kamanda Dickson, mtu mwenye sura mbaya alikuwa akipita katika vituo vyote kwa ajili ya kuangalia idadi ya machangudoa hao kujua kama kuna muharifu aliyekuwa akimtafuta.

Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 53

Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam kufuatia kupotea mfululizo kwa machangudoa katika mazingira ya kutatanisha. Taharuki kubwa inazuka kwani ndani ya kipindi kifupi tu, zaidi ya machangudoa kumi na moja wanapotea na hakuna anayejua walikopotelea.

Jambo hilo linasababisha jeshi la polisi kuingilia kati. Kinachozidi kuzua utata, wote wanapotea katika mazingira yanayofanana. Mwanaume mmoja asiyejulikana, aliyekuwa anatembelea gari la kifahari aina ya Volkswagen, aliyekuwa akienda eneo hilo usiku wa manane ndiye anayehusishwa na wote wanaopotea.

Upande wa pili, kijana aliyekuwa na mwonekano tofauti na binadamu wa kawaida, Dickson Maduhu au Zinja kama wenzake walivyokuwa wakimtania, amejiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Hisia kali za mapenzi zinasababisha kijana huyo aanze kutoka usiku na kwenda kutafuta machangudoa. Hivyo baadaye anahamishiwa Dar es Salaam.

Baada ya kuwa DCP, Dickson anakutana na msichana aitwaye Pamela, anatokea kuvutiwa naye, anafanya naye mapenzi kwa kumnunua Kinondoni. Kupitia changudoa huyo aliyetoka Arusha, anajikuta akianza kuwaua wanawake wengi jijini Dar es Salaam.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Hawakuchukua muda mrefu wakafika kituoni, alichokifanya polisi ni kumwambia kijana yule aliyejitambulisha kwa jina la Samto ampigie simu Hadija na kumwambia maneno yoyote yale ilimradi wakutane sehemu.

Hiyo ndiyo njia ambayo ilionekana kufaa kutumika kwani vinginevyo wasingeweza kumkamata mwanamke huyo. Wakati Samto amepewa simu kwa ajili ya kumpigia Hadija, Kamanda Dickson akamzuia kwa kumwambia kwamba hakutakiwa kufanya hivyo, kwa kuwa alikwishaipata simu yake, haikuwa na haja.

“Haina haja kufanya hivyo, nilichokuwa nakitaka ni simu tu,” alisema Kamanda Dickson hali iliyomfanya kila polisi kushangaa huku wengine wakimuona kuwa na roho nzuri.

“Hakuna tatizo afande.”

“Ila ningependa kuzungumza na huyu mtu.”

“Sawa mkuu!” alisema polisi mmoja kisha kupiga saluti.

Wakamchukua Samto na kumpeleka katika chumba kimoja kilichokuwa na meza moja ndefu na viti viwili. Walipofika wakamuweka kwenye kiti kimoja na kiti kingine kukaliwa na Kamanda Dickson, polisi wote wakatoka nje.

Kamanda Dickson akabaki akimwangalia Samto huku uso wake ukionekana kuwa na hasira mno. Alivimba kiasi kwamba ubaya wa sura yake kuonekana dhahiri. Samto alimfahamu mtu aliyekuwa mbele yake, alikuwa miongoni mwa watu waliosemekana kuwa na roho mbaya, hivyo kila alivyomwangalia na kwa jinsi alivyokuwa na hasira, akajua kwamba angeweza kufanywa kitu kibaya.

“Huyo Hadija anaishi wapi?” aliuliza Dickson.

“Anaishi Kinondoni A.”

“Kama kunaelekezeka hebu nielekeze,” alisema Dickson hivyo Samto kuanza kumuelekeza.

“Sawa. Alipokuuzia simu hii alikwambiaje?”

“Alisema kwamba ilikuwa yake hivyo nisiwe na hofu na kwa sababu huwa mara nyingi nanunua vitu kwake, nilimwamini sana,” alisema Samto.

“Huwa anapatikana nyumbani muda gani?”

“Mchana huwa yupo muda wote, ila kuanzia saa moja, anatoka kwenda kwenye mishe zake.”

“Na hapo anaishi na watu wangapi?”

“Yupo na wasichana wenzake wawili, Asha na Anita, ila pia ana marafiki zake wa karibu, Mariamu na Ashura ambao wanaishi kama nyumba ya tatu kutoka hapo anapoishi,” alisema Samto.

“Sawa. Wanafanya kazi gani?”

“Wanajiuza usiku.”

“Wote hao?”

“Ndiyo!”

Kamanda Dickson hakutaka kupoteza muda, alichokifanya ni kuondoka kituoni hapo huku akitoa agizo kwamba Samto asitolewe kituoni wala asiwasiliane na mtu yeyote na kama alihitaji chakula, ilibidi kununuliwa lakini si kuruhusu kuonana na mtu yeyote yule.

Ili kuonesha kwamba alimaanisha alichokisema, akaingiza mkono mfukoni na kutoa kiasi cha shilingi elfu hamsini na kumgawia mkuu wa kituo huku akimtaka mkuu wa kituo ahusike katika ishu zote za chakula kwa Samto.

*********

“Dada samahani!” ilisikika sauti ya mwanaume mmoja kutoka katika sehemu iliyokuwa na giza hafifu, kichwani alikuwa na kofia kubwa huku akiwa amevaa shati lenye maua.

“Nani? Mimi?” aliuliza msichana huyo, kwa kumwangalia tu, wala usingeweza kujiuliza mara mbili kwamba alikuwa akifanya kazi gani, mavazi yake tu, tena kwa muda kama huo alionekana kuwa changudoa, na kama hakuwa changudoa, basi alikuwa mtu wa kujirusha kwa sana usiku.

“Ndiyo dada! Nakuhitaji mara moja.”

“Mbona gizani?”

“Jamani! Kwani kuna giza hapa? Halafu sisi wengine wenye familia zetu hatutaki kuonekana, si unajua mke akituoni usiku hakulaliki…” alisikika mwanaume huyo.

Msichana yule akajisogeza karibu na mwanaume yule ila kwa mwendo ulioonesha kuwa na hofu na uwepo wa mwanaume yule mahali pale. Alipomfikia, alijitahidi sana kumwangalia usoni ili amuone vizuri lakini kutokana na kigiza kilichokuwa mahali pale, hakuweza kumgundua.

“Nataka mechi…” alisema mwanaume huyo.

“Nani kakwambia kama najiuza?”

“Jamani! Nimebanwa mwenzako, hata kama haujiuzi, naomba tu uniridhishe mtoto wa mwanamke mwenzio, nitakupa hela yoyote uitakayo,” alisema mwanaume huyo.

“Una kilo?”

“Hiyo tu? Hakuna tatizo,” alisema mwanaume huyo, hapohapo akaingiza mkono mfukoni na kutoa kiasi cha shilingi laki moja na kumgawia msichana huyo. Alionekana kuwa na kiu ya kutaka kulala naye kwa kisingizo cha kutoka mkoani na gari la mizigo, hivyo njiani kote alikosa mwanamke wa kumkosha roho yake. Mwanaume huyo alikuwa Kamanda Dickson na mwanamke alikuwa Shamila, rafiki yake Hadija.

Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 54

Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam kufuatia kupotea mfululizo kwa machangudoa katika mazingira ya kutatanisha. Taharuki kubwa inazuka kwani ndani ya kipindi kifupi tu, zaidi ya machangudoa kumi na moja wanapotea na hakuna anayejua walikopotelea.

Jambo hilo linasababisha jeshi la polisi kuingilia kati. Kinachozidi kuzua utata, wote wanapotea katika mazingira yanayofanana. Mwanaume mmoja asiyejulikana, aliyekuwa anatembelea gari la kifahari aina ya Volkswagen, aliyekuwa akienda eneo hilo usiku wa manane ndiye anayehusishwa na wote wanaopotea.

Upande wa pili, kijana aliyekuwa na mwonekano tofauti na binadamu wa kawaida, Dickson Maduhu au Zinja kama wenzake walivyokuwa wakimtania, amejiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Hisia kali za mapenzi zinasababisha kijana huyo aanze kutoka usiku na kwenda kutafuta machangudoa. Hivyo baadaye anahamishiwa Dar es Salaam.

Baada ya kuwa DCP, Dickson anakutana na msichana aitwaye Pamela, anatokea kuvutiwa naye, anafanya naye mapenzi kwa kumnunua Kinondoni. Kupitia changudoa huyo aliyetoka Arusha, anajikuta akianza kuwaua wanawake wengi jijini Dar es Salaam.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Biashara ilikuwa mbaya kwa Shamila, alishinda katika kijiwe chake lakini wanaume siku hiyo waliadimika, hakukuwa na mwanaume yeyote aliyemfuata mpaka mishale ya saa kumi alfajiri alipoamua kurudi nyumbani kupumzika kwa kuhesabu kwamba siku hiyo aliambulia patupu.

Wakati akiwa amefika karibu na mahali alipokuwa akiishi, bahati nzuri kwake akakutana na mwanaume, aliyeonekana kuwa na hela nyingi ambaye alihitaji huduma yake kwa muda huo uliobakia.

Shamila hakutaka kulaza damu, hiyo ilionekana kuwa bahati yake, yaani kama kutembea kilometa hamsini pasipo kuuona mwembe halafu mbele unakutana na embe dodo, alichokifanya ni kuondoka na mteja huyo na kwenda naye katika gesti iliyokuwa karibu na eneo hilo.

“Unaonekana mzuri sana, ila unaweza au ndiyo utaleta usista duu?” aliuliza Kamanda Dickson kwa sauti ya kilevi kwa mbali, hakutaka kugundulika kirahisi, yaani msichana huyo ajue kwamba alikutana na mlevi.
“Usije ukakimbia wewe tu.”
“Kweli?”
“Ndiyo!”

“Basi kama ndiyo hivyo, nitakuongeza fedha, ilimradi unifikishe ninapokwenda,” alisema Dickson huku wawili hao wakipiga hatua kuelekea kwenye gesti moja iliyokuwa karibu, kwa namna walivyokuwa wakitembea ilikuwa ni rahisi sana kusema kwamba walikuwa wapenzi wa muda mrefu, kwani walishikana kimahaba.

Walipofika katika gesti hiyo, moja kwa moja wakaelekea mapokezi ambapo dada wa hapo alionekana kufahamiana sana na Shamila, wakasalimiana kwa furaha na kuomba chumba, wakapewa chumba namba ishirini na mbili.

“Si ndiyo kile chenye wavu uliochanika na kitanda chenye kelele?”
“Ndiyo! Ila wavu tulibadilisha na hata kitanda kipo poa, tulikibadilisha, tumeweka cha chuma,” alisema mhudumu.

“Kama ni hivyo sawa, leo nipo na mpenzi mpya, sitaki presha ya kitanda cha kelele,” alisema Shamila pasipo Dickson kuzungumza chochote kile.

Kwa sababu Shamila ndiye alikuwa mwenyeji, alichokifanya ni kuchukua ufunguo wa chumba hicho na kuanza kuelekea huko. Bado walikuwa wakishikana kimahaba mpaka walipofika chumbani ambapo yeye kama mteja, Dickson akahitaji kufanya mapenzi kwenye giza kwa lengo la kutokuonekana.

“Nyie wateja wa siku hizi mna masharti kama waganga…mnapenda sana kufanya mapenzi gizani kama paka,” alisema Shamila kwa sauti iliyoashiria kutania, alipomaliza kusema hayo, akampiga Dickson kibao cha mahaba kisha kuanza kuvua nguo zake.

Uso wa Dickson ulionesha tabasamu pana lakini moyo wake ulikuwa na hasira kali, hakumpenda Shamila, alimchukia kwa kudhani kwamba huyo Hadija alimwambia kuhusu yeye hivyo kupania kumuua humohumo ndani.

Shamila alijichekesha huku akizungumza maneno ya mahaba ambayo alidhani kwamba yangeingia ndani ya moyo wa Dickson na kuubadilisha hatimaye kuwa mteja wake wa kila siku hasa baada ya kubadilishana namba za simu.
“Nataka nikupe mapenzi ya kisasa baby…” alisema Shamila.
“Yapoje hayo?”

“Wewe subiri, nitakuonesha kwa nini wananiita Shamila mkia wa taa,” alijigamba msichana huyo.

Dickson alitulia tu, alibaki akimwangalia msichana huyo ambaye alionekana kupania sana usiku wa siku hiyo pasipo kujua kwamba usiku huo ndiyo ungekuwa kwisho wa kuvuta pumzi ya hii dunia.

Baada ya kumaliza manjonjo yake yote, akamsogelea Dickson pale kitandani na kulala juu yake. Dickson akamgeuza Shamila na kumuweka chini huku akileta unafiki wa kumbusu hapa na pale hali iliyomfanya msichana huyo kufumba macho kimahaba.
“Bila shaka unaitwa Shamila…” alisema Dickson, Shamila akashtuka.
“Kumbe unanifahamu?” aliuliza Shamila huku kwa mbali akionekana kushtuka.
“Ndiyo! Hadija yupo wapi?”

“Nani? Hadija? Ndiye nani?” aliuliza Shamila huku akijidai kutokumjua Hadija kwa kuhofia kuchukuliwa mteja wake.
“Haumfahamu?”
“Wala simjui kabisa.”

“Una uhakika?”
“Ndiyo! Kwanza ndiyo nini kumtajataja mtu kwenye muda kama huu jamani baby? Mbona unataka kuniumiza?” aliuliza Shamila huku akijifanya kama kutaka kulia eti kwa kuumizwa na wivu mkali.

“Na wewe si ndiye uliyetumia naye fedha zangu alizoniibia gesti? Bila shaka mlifurahi na kula bata sana kwa hela za mwanaume msiyemjua ni nani,” alisema Dickson, maneno hayo yakaanza kumtia shaka Shamila, akataka kujitoa pale kitandani, akashindwa, mikono yake ilizuiliwa vilivyo, Dickson alikuwa juu yake.

“Wewe ni nani?” aliuliza Shamila huku akiwa na hofu tele.
“Mwenye simu na fedha! Nimekuja kwa ajili ya kuwaonesha ni jinsi gani mali za mwanaume haziendi bure,” alisema Dickson, hapohapo pasipo kuchelewa akaanza kumkaba Shamila kooni.

Msichana huyo alikukuruka huku na kule, alijitahidi kuitoa mikono ya Dickson shingoni mwake lakini hakufanikiwa, alikabwa vilivyo, macho yakaanza kubadilika na mishipa ya shingo kumsimama, Dickson hakumwacha, aliendelea kumkaba kwa lengo la kumuua.

Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 55

Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam, machangudoa wengi wanaanza kuuawa katika mazingira ya kutatanisha. Hakuna anayemjua muuaji, kila changudoa anayenunuliwa na mwanaume aliyekuwa kwenye gari aina ya Volkswagen nyeusi, anauawa kikatili.

Kila mmoja anaogopa, machangudoa wengine wanaacha kujiuza, wanajifungia vyumbani mwao, ila kwa wengine ambao hawakuweza kuishi bila kufanya biashara hiyo, wanakwenda huko, bado wengine wanaendelea kuuawa.

Nyuma ya kila kitu, kuna mwanaume mmoja mwenye sura mbaya, tena akiwa ni Kamanda Mkuu wa Jeshi la Polisi Kanda ya Dar es Salaam, (DCP) Dickson ndiye ambaye anafanya mauaji hayo pasipo kugundulika.

Kazi yake ni kununua machangudoa na yeyote atakayemgundua, humuua kikatili na kuondoka zake.

Polisi wanachanganyikiwa, wanamtafuta muuaji, wanamkosa kwani anaonekana makini hasa kwenye kufuta alama za vidole vyake.
Hali ya hofu inaendelea kutanda jijini Dar es Salaam.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Kule chooni alikoingia, Happy alifungua kipochi chake na kutoa bastola ndogo tayari kwa kumuweka chini ya ulinzi Kamanda Dickson pasipo kujua kwamba mtu huyo alikuwa hatari zaidi yake.

Hakutaka kuchelewa kule, akatoka huku akijiamini kwani alikuwa na uhakika kwamba mwanaume huyo hakuwa akijua yeye alikuwa nani na chooni alikwenda kufanya nini. Akaufungua mlango kwa ajili ya kuingia chumbani, kitu kilichomshtua, ngumi moja nzito ikatua usoni mwake, akabaki akipepesuka, hapohapo akaanguka chini.

Kamanda Dickson hakutaka kuchelewa, tena alipoiona bastola ile akagundua kwamba mtu huyo alikuwa hatari na kama angemuacha basi ilikuwa lazima afe, hivyo kitu cha haraka kilichomjia kichwani, iwe isiwe ilikuwa ni lazima kumuua.

Akamsogelea pale chini kwa lengo la kukamilisha alichokitaka, kwa ustadi mkubwa kama mtu aliyepitia mafunzo ya karate, Happy akainyanyua miguu yake na kuikamata shingo ya Kamanda Dickson na kumwangusha chini.

“Kamanda…” alijikuta akiita Happy huku akionekana kuwa na mshtuko, hakuamini kile alichokiona, mkuu wake wa kazi ndiye aliyekuwa naye chumbani, tena akipambana naye kwa ajili ya kuuokoa uhai wake.

“Koh koh koh…” Kamanda Dickson alijikuta akikohoa huku akijitahidi kuiondoa miguu ya Happy ambayo iliikaba shingo yake vilivyo.

Dickson hakutaka kukubali, hakuwa tayari kuona akikamatwa kirahisi namna hiyo hivyo alichokifanya ni kujinyanyua pale chini alipokuwa, akamnyanyua Happy huku miguu ya msichana yule ikiendelea kuing’ang’ania shingo yake.

Alimbeba juujuu na kumbamiza chini kwa kuanguka naye. Sauti kubwa ya maumivu ikasikika kutoka kwa msichana huyo, hata kabla hajajua nini cha kufanya, Dickson akajisogeza pembeni, akaishika shingo yake iliyokuwa na maumivu na kuanza kukohoa mfululizo.

“Who the hell are you?” (Wewe ni nani?) aliuliza Dickson huku akimwangalia mwanamke huyo kwa macho ya mshangao, hakuamini kama kungekuwa na changudoa aliyekuwa na mbinu za kujihami namna ile.

“I don’t know, I am here to kill you,” (Sijui, nipo hapa kwa ajili ya kukuua)
Wote walisimama na kuanza kuangaliana, Happy alimwangalia kamanda wake ni kweli alimfahamu vilivyo, wakati mwingine alipokea amri kutoka kwa mkuu wake huyo na kuambiwa nini cha kufanya lakini kwa hali ilivyokuwa chumbani humo, hakukuwa na muda wa kupeana heshima tena, ulikuwa ni wakati wa hatari, wakati wa kuiokoa nafsi yake.

“Kama unataka kuniua, niue kama utaweza! Ukishindwa, nakuua wewe,” alisema Dickson huku akikunja ngumi. Hakukuwa na kingine kilichofuata zaidi ya kupigana. Kila mmoja alipitia mafunzo makali lakini kwa Dickson alionekana kuwa hodari katika kurusha ngumi mfululizo, mateke na hata ukwepaji wake ulionesha kabisa kwamba alikuwa mzuri katika kupambana tofauti na Happy.

Dakika kumi na tano zilikatika huku wakiendelea kuoneshana kazi, tena kimyakimya pasipo kuwasumbua wateja wengine waliokuwa kwenye vyumba vingine. Happy akaishiwa nguvu, akashtukia akipigwa ngumi mfululizo zilizomchanganya na kujikuta akiangukia kitandani huku uso wake ukiwa umevimba vilivyo na damu zikimtoka. Akabaki akipiga kelele tu. Akawahiwa kwa kuzibwa mdomo.

“Nyamazaaa…” alisema Kamanda Dickson kwa ukali huku akimziba mdomo.
Wakati akiwa amemtuliza pale kitandani, mara akasikia mlango ukigongwa, akajua fika kwamba mgongaji alikuwa mhudumu wa gesti ile hivyo akaufuata mlango na kuufungua, hata kuvaa kofia yake alisahau kuivaa.
“Nikusaidie nini?”

“Nimesikia kelele kaka…”
“Ndiyo! Ni kelele za mahaba… na wewe unataka?”
“Hapana! Samahani, nilifikiri mnahitaji msaada,” alisema msichana yule huku akitetemeka.

Dickson hakutaka kuzungumza sana, akaufunga mlango na kumfuata Happy kitandani pale, kilichofuatia ni kuendelea kumpiga ngumi za uso mfululizo na mwisho kabisa akainyonga shingo yake kwa kumkaba.

“Kwisha kazi…” alijisemea Dickson huku akikaa pembeni.
Alikaa kwa dakika kama kumi hivi ndipo alipokumbuka jambo moja la muhimu sana. Wakati ameufungua mlango na kuzungumza na dada wa mapokezi, hakuwa na kofia ya kuuficha uso wake na ndiyo maana dada yule alikuwa akizungumza naye huku akitetemeka, hasa baada ya kugundua alikuwa akizungumza na nani.

“Kanigundua…kanigundua…ni lazima nimuue,” alisema Dickson huku akionekana kuchanganyikiwa.

Harakaharaka akainuka kutoka pale kitandani, akaufuata mlango na kutoka. Breki ya kwanza ilikuwa mapokezi, alipofika hapo, dada huyo hakuwepo, alichanganyikiwa zaidi, akaanza kuita kwa kuhisi labda msichana huyo alikuwa sehemu, hakuisikia sauti iliyoitikia.

Huku akiangalia huku na kule, ghafla akasikia sauti za watu nje wakija, maneno aliyoyasikia ni koplo, kamanda na mkuu, mbali na maneno hayo, akasikia sauti ya msichana, akajua kwamba dada huyo wa mapokezi alikwenda kuwaita polisi, alichokifanya, akaufunga mlango wa kuingilia ndani ya gesti ile, polisi wale wakaanza kugonga kwa nguvu.

“Fungua mlango… fungua mlango kabla hatujauvunja,” alimsikia polisi mmoja ambaye alizungumza huku akiikoki bunduki yake, Dickson akabaki akiwa amesimama, hakujua ni kitu gani alitakiwa kufanya, alichanganyikiwa, hakujua kama alitakiwa kuufungua mlango au la.

Kilichomchanganya zaidi, aligundulika kama alikuwa yeye, maiti ya kule ndani ilimtia hofu kubwa, hakujua afanye nini, kwanza akasimama na kuanza kujifikiria, polisi waliendelea kugonga mlango wakitaka wafunguliwe.

“Siwezi kukamatwa kijinga…” alijisemea Dickson, kweli, kwa jinsi hali ilivyokuwa, lingekuwa jambo gumu kwa mtu kama yeye kukamatwa kizembe namna ile. Ghafla, polisi wale wakaanza kupiga teke mlango kwa lengo la kuuvunja huku yeye akiwa amesimama, tena amepigwa butwaa.

Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 56

Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam kufuatia kupotea mfululizo kwa machangudoa katika mazingira ya kutatanisha. Taharuki kubwa inazuka kwani ndani ya kipindi kifupi tu, zaidi ya machangudoa kumi na moja wanapotea na hakuna anayejua walikopotelea.

Jambo hilo linasababisha jeshi la polisi kuingilia kati. Kinachozidi kuzua utata, wote wanapotea katika mazingira yanayofanana. Mwanaume mmoja asiyejulikana, aliyekuwa anatembelea gari la kifahari aina ya Volkswagen, aliyekuwa akienda eneo hilo usiku wa manane ndiye anayehusishwa na wote wanaopotea.

Upande wa pili, kijana aliyekuwa na mwonekano tofauti na binadamu wa kawaida, Dickson Maduhu au Zinja kama wenzake walivyokuwa wakimtania, amejiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Hisia kali za mapenzi zinasababisha kijana huyo aanze kutoka usiku na kwenda kutafuta machangudoa. Hivyo baadaye anahamishiwa Dar es Salaam.

Baada ya kuwa DCP, Dickson anakutana na msichana aitwaye Pamela, anatokea kuvutiwa naye, anafanya naye mapenzi kwa kumnunua Kinondoni. Kupitia changudoa huyo aliyetoka Arusha, anajikuta akianza kuwaua wanawake wengi jijini Dar es Salaam.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Idadi kubwa ya watu ilikusanyika nje ya gesti ya Mkombothi iliyokuwa Kinondoni jijini Dar. Minong’ono ilisikika kila kona kwamba ndani ya gesti hiyo kulikuwa na msichana aliyekuwa ameuawa.

Kila mmoja aliyesikia minong’ono hiyo alishindwa kuamini hivyo watu wengi kutaka kwenda ndani kujionea wao wenyewe. Wanaume waliokuwa na nguvu ambao ndiyo walikuwa watu wa kwanza kupewa taarifa hiyo walifanya kazi ya ziada ya kuwazuia watu kuingia ndani.

Waliokuwa na simu zenye kamera, kama kawaida yao walikuwa bize kupiga picha, walitaka kuwa wa kwanza kutoa taarifa katika mitandao ya kijamii. Hakukuwa na mtu aliyekumbuka kuwapigia simu polisi, walichokifikiria kwanza kilikuwa ni mitandao ya kijamii tu.

Umati wa watu ulizidi kuongezeka huku kila mtu akiongea lake, baadhi ya wanawake waliopewa nafasi ya kwenda chumbani, waliporudi walikuwa wakilia huku wakisema kwamba mwanamke aliyeuawa kikatili alikuwa Shamila.

“Shamila!” Haiwezekani! Ni jana tu nilikuwa naye!” alisema kijana mmoja huku akionekana kutokuamini kabisa.

Jina la Shamila likaanza kusikika masikioni mwa watu. Walimfahamu msichana huyo, japokuwa alikuwa maarufu kwa kujiuza lakini alikuwa msichana wa tofauti kabisa. Alikuwa mchangamfu na aliyependa kuzungumza na kila mtu, hakuwa msichana wa majivuno, hata kwa kidogo alichokuwa nacho, alikuwa radhi kumpatia hata na mwingine.

“Ni kweli Shamila au nimemfananisha?” aliuliza jamaa mmoja.

“Ni yeye! Ni Shamila kweli!”

Pamela akafika mahali hapo, alipoambiwa kwamba Shamila alikutwa akiwa ameuawa chumbani kwake, hakuamini. Alitaka kujionea kwani usiku uliopita tu alikuwa naye Kinondoni mpaka alipoamua kuondoka kwa sababu alikosa wateja.

Akaruhusiwa kwenda ndani. Hazikuwa tetesi, kile alichokisikia ndicho alichokutana nacho ndani. Mwili wa Shamila ulikuwa kitandani, mdomoni alikuwa na alama zilizoonesha kwamba kabla ya kuuawa alitokwa sana na mapovu mdomoni.

Pamela akashindwa kuvumilia, hapohapo machozi yakaanza kumtoka, picha aliyoiona kitandani ilimsisimua sana hivyo kujikuta akitoka nje huku akilia kwa sauti.

Lilikuwa pigo kubwa kwa machangudoa wengine. Hazikupita dakika nyingi, polisi wakafika katika gesti hiyo na kuingia ndani, mtu wa kwanza kabisa kumshikilia kama mtuhumiwa namba moja alikuwa dada wa mapokezi.

“Jamani sijui chochote kile,” alisema msichana huyo.

“Sawa! Ila twende kituoni, tunataka uisaidie polisi,” alisema polisi mmoja, dada yule wa mapokezi akafungwa pingu, mwili wa Shamila ukatolewa ndani.

Watu walipouona ukitolewa, hawakuamini, wakabaki wakilia, ni kweli, mtu aliyekuwa ameuawa ndani ya chumba kile alikuwa Shamila, hivyo akaacha vilio vikubwa katika mtaa aliokuwa akiishi.

Muuaji hakujulikana, hata dada yule alipoulizwa juu ya muuaji huyo, alishindwa kumfahamu ila kitu pekee alichokisema ni kwamba mwanaume huyo alivalia kofia kubwa ya Marlboro, hivyo hakuweza kumgundua usoni.

“Alivalia kofia ya Marlboro?” aliuliza polisi kana kwamba hakuwa amesikia.

“Ndiyo!”

“Haukuweza kuuona uso wake?”

“Ndiyo afande.”

Maelezo ya dada yule yakawarudisha nyuma kabisa na kukumbuka kwamba wanawake kadhaa waliouawa kipindi cha nyuma, waliuawa na mtu huyohuyo ambaye kila siku alionekana kuvalia kofia kubwa.

Hawakujua mtu huyo alikuwa nani na kwa nini aliwaua wanawake tu. Polisi walichanganyikiwa, hawakujua pa kuanzia kwani hata nyakati za usiku walipokuwa wakitembea kama kufanya doria, walikutana na watu wengi waliovalia kofia za namna hiyo hivyo kuwa na wakati mgumu wa kumfahamu mhusika.

“Ila huyu muuaji ni nani?” aliuliza polisi mmoja, alionekana kuchoka, walizunguka sehemu kubwa jijini Dar kufanya doria lakini hakukuwa na dalili zozote zile.

“Hata mimi sifahamu! Hapa inabidi tuongeze kasi, la sivyo wanawake wengi hapa Dar watauawa,” alisema polisi mmoja.

Wakati polisi wakiendelea na doria yao, upande wa pili Kamanda Dickson alikuwa na mawazo tele, moyo wake ulianza kuridhika kutokana na kile alichokifanya, aliambiwa kwamba mbali na Hadija kulikuwa na wasichana watatu na mmoja alikuwa amekwishamuua na walibaki wawili kabla ya kumalizia na mhusika mwenyewe ambaye ni Hadija.

Usiku wa siku hiyo, alishinda akinywa pombe nyumbani kwake, kichwa chake bado kilikuwa na mawazo tele, kila kitu kilichokuwa kikiendelea, kilimchanganya sana.

Alijiona kuwa na roho mbaya lakini hakuwa na jinsi, alihitaji kuificha siri yake ili aishi kiamani na hakukuwa na kitu kingine cha kufanya kuificha siri hiyo zaidi ya kuua kama alivyokuwa akifanya.

Mara kwa mara alikuwa akiwasiliana na Pamela, japokuwa msichana huyu alikuwa changudoa lakini moyo wake ulimpenda, alikuwa radhi kwa kila kitu, kutumia kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya msichana huyo kwake halikuwa tatizo kutokana na uzuri aliokuwa nao, aliona kustahili kufanyiwa mambo yote ili awe na furaha maisha yake yote.

“Wa pili ni huyu Asha, nikimalizana naye, nahamia kwa Anita kisha kumuua Hadija mwenyewe, bila kufanya hivi, najua itakula kwangu tu,” alisema Kamanda Dickson kisha kujitupa kitandani kwake, akili yake ilichoka mno.


Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 57

Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam, machangudoa wengi wanaanza kuuawa katika mazingira ya kutatanisha. Hakuna anayemjua muuaji, kila changudoa anayenunuliwa na mwanaume aliyekuwa kwenye gari aina ya Volkswagen nyeusi, anauawa kikatili.

Kila mmoja anaogopa, machangudoa wengine wanaacha kujiuza, wanajifungia vyumbani mwao, ila kwa wengine ambao hawakuweza kuishi bila kufanya biashara hiyo, wanakwenda huko, bado wengine wanaendelea kuuawa.

Nyuma ya kila kitu, kuna mwanaume mmoja mwenye sura mbaya, tena akiwa ni Kamanda Mkuu wa Jeshi la Polisi Kanda ya Dar es Salaam, (DCP) Dickson ndiye ambaye anafanya mauaji hayo pasipo kugundulika. Kazi yake ni kununua machangudoa na yeyote atakayemgundua, humuua kikatili na kuondoka zake.

Polisi wanachanganyikiwa, wanamtafuta muuaji, wanamkosa kwani anaonekana kuwa makini hasa kwenye kufuta alama za vidole vyake. Hali ya hofu inaendelea kutanda jijini Dar es Salaam.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Pamela alibaki akitetemeka pale kitini, kila alipomwangalia mwanaume yule aliyeingia, hakuonekana kuwa na utani, muonekano wake tu ulionesha kwamba alitaka kuambiwa ukweli juu ya kilichokuwa kikiendelea, vinginevyo asingeweza kueleweka. Mwanaume huyo akakaa kwenye kiti na kuweka zile karatasi juu ya meza, macho yake akayatuliza kwa Pamela ambaye tayari kijasho chembamba kilianza kumtoka huku kwa mbali akitetemeka kama mtu aliyeanza kuhisi baridi kali.

“Unamfahamu huyu?” aliuliza mwanaume yule huku akimuoneshea Pamela picha ya Kamanda Dickson, yaani hata kumsalimia hakutaka, kwake, maswali yalikuwa muhimu zaidi ya salamu.

“Nd..iy..o..” alijibu Pamela huku akitetemeka.
“Ulishawahi kumuona wapi?”
Hapo ndipo Pamela alipoanza kuhadithia namna alivyokutana na Kamanda Dickson tangu siku ya kwanza mpaka siku ya mwisho kuachana naye. Katika kipindi chote hicho cha kuhadithia, mwanaume yule alikuwa kimya akimsikiliza, pale alipoona kulikuwa na jambo la muhimu kuandika, aliandika kwenye moja ya karatasi zake.

“Ulishawahi kumuuliza kwa nini alikuwa akificha sura yake siku za kwanza?” aliuliza mwanaume yule.“Hapana! Sikutaka kujali sana kwa kuwa nilihisi kwamba yeye ni mume wa mtu hivyo hakutaka kugundulika, sikuwa na hofu, nilichokiangalia ni fedha tu,” alijibu Pamela.

“Unahisi kwa nini aliwaua wanawake aliokuwa akiwachukua?”
“Nahisi walimgundua. Hata siku ya kwanza nilipouona uso wake akaniuliza kwa nini sikushtuka au kuogopa? Kwa kuwa sikuwa namfahamu, nikamwambia siwezi kushtuka wala kuogopa. Nahisi wale waliomgundua ndiyo aliowaua kwa kudhani siri yake ingegundulika,” alisema Pamela.

Kila swali aliloulizwa mahali pale, alijibu kiufasaha kabisa. Mahojiano hayo yalichukua zaidi ya dakika thelathini ndipo akaruhusiwa kuondoka huku akiambiwa kwamba alitakiwa kufika pale kituoni kila atakapokuwa akihitajika.

* * * *

Watu walijaa katika meza za wauza magazeti, walichokuwa wakikiona, hawakukiamini hata kidogo. Minong’ono ya hapa na pale ilikuwa ikisikika katika kila meza ya magazeti iliyokuwa imekusanya idadi kubwa ya watu.

Habari iliyokuwa imeandikwa katika magazeti hayo, ilimshtua kila mmoja, hakukuwa na aliyeamini kwamba mtu aliyekuwa akiwaua wanawake wale katika kipindi chote hicho alikuwa Kamanda Dickson, mtu aliyeheshimika na kuogopwa mno na wahalifu. Hiyo ndiyo ikawa habari ya mjini, kila gazeti lililokuwa na habari hiyo, lilinunulika na mpaka kufikia saa sita mchana, hakukuwa na gazeti lolote mitaani lililokuwa na habari kuhusu Kamanda Dickson.

Habari hiyo haikuwa peke yake bali hata uthibitisho wa picha ya gari lake likiwa nje ya gesti moja Mwananyamala ilisindikizia habari hiyo kitu kilichowafanya watu wengi kuamini kwamba kamanda huyo ndiye alikuwa muuaji wa wanawake wale. “Mimi siamini mwenzenu…” alisikika mwanamke mmoja aliyesimama mbele ya meza moja ya magazeti.

“Wewe ndiyo kama mimi! Eti Kamanda Dickson muuaji, sasa huku kuchafuana kumezidi, kwanza magazeti haya bora yafungiwe tu,” aliisema mwanaume mmoja aliyeonekana kukasirishwa mno na habari hiyo.

“Kwanza haya magazeti yafungiwe kwa kumchafua kamanda wetu, mchapakazi na anayejitolea sana, pili ni lazima jeshi la polisi liingilie kati, haiwezekani lichafuliwe kiasi hiki tena kwa habari ya kuungaunga kama hii,” aliingilia mwanaume mwingine, kila mtu aliyekuwa mahali hapo alionekana kukasirishwa na habari ile.

Mijadala iliendelea mitaani, watu walikuwa wakibishana kwamba inawezekana habari hizo zilikuwa ni za kutengenezwa kwa ajili ya kumchafua mtu fulani. Japokuwa ukweli uliandikwa gazetini lakini hakukuwa na mtu aliyeuamini, kila mmoja alihisi kwamba taarifa hizo zilikuwa kwa lengo la kumchafua kamanda huyo.

Taarifa hazikutolewa gazetini tu, ilipofika saa saba mchana, karatasi zenye picha zake zikaanza kubandikwa katika vituo mbalimbali vya daladala, mitaani kwamba Dickson alikuwa mtu hatari na yeyote ambaye angefanikisha kukamatwa kwake basi kitita cha shilingi milioni ishirini kingekuwa kama zawadi yake.

Hapo ndipo wale watu ambao hawakuamini kilichoandikwa magazetini wakaamini. Hoja zikaibuka tena, mijadala ikaanza kwenye mitandao ya kijamii, watu wengi walikuwa wakilishutumu jeshi la polisi kwa kutokulivalia njuga suala hilo mpaka pale wanawake wengi walipouawa.

“Polisi wazembe sana…” alilalamika jamaa mmoja pasipo kukumbuka kwamba mtu aliyekuwa akifanya mauaji alikuwa Kamanda Mkuu Kanda ya Dar es Salaam.

Kila mtu alizihitaji hizo milioni ishirini. Kumgundua Kamanda Dickson halikuwa jambo gumu, alijulikana kila kona, ubaya wa sura yake ulikuwa gumzo. Watu wakawa makini mitaani, wengi waliokuwa hata wakifanana naye walichukuliwa na kupelekwa kituoni. Siku ya kwanza ikapita, wananchi walikuwa makini kila kona lakini hawakuweza kumpata. Siku ya pili ikaingia, ya tatu mpaka ya nne lakini bado polisi na wananchi waliendelea kumtafuta pasipo mafanikio.

Wakati polisi wakiendelea kumtafuta kwa kufuatilia hata akaunti zake benki, wakagundua kwamba siku moja nyuma, kiasi chote cha fedha alichokuwa nacho kilihamishwa na kupelekwa katika akaunti ambayo hawakuiona, walishindwa kufahamu ni nani aliyefanya hivyo na fedha hizo zilikuwa katika akaunti ya nani.

Kama fedha zilihamishwa kisiri, ilimaanisha kwamba alikuwa sehemu. Yeye hakuwa na utaalamu wa masuala ya kompyuta, je ni nani aliyemsaidia kuhamisha fedha hizo pasipo benki kujua mahali zilipopelekwa? Mbali na hiyo, je, huyu Kamanda Dickson alikuwa wapi? Hilo ndilo swali alilojiuliza kila mtu pasipo kupata jibu.

Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 58

Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam, machangudoa wengi wanaanza kuuawa katika mazingira ya kutatanisha. Hakuna anayemjua muuaji, kila changudoa anayenunuliwa na mwanaume aliyekuwa kwenye gari aina ya Volkswagen nyeusi, anauawa kikatili.

Kila mmoja anaogopa, machangudoa wengine wanaacha kujiuza, wanajifungia vyumbani mwao, ila kwa wengine ambao hawakuweza kuishi bila kufanya biashara hiyo, wanakwenda huko, bado wengine wanaendelea kuuawa.

Nyuma ya kila kitu, kuna mwanaume mmoja mwenye sura mbaya, tena akiwa ni Kamanda Mkuu wa Jeshi la Polisi Kanda ya Dar es Salaam, (DCP) Dickson ndiye ambaye anafanya mauaji hayo pasipo kugundulika. Kazi yake ni kununua machangudoa na yeyote atakayemgundua, humuua kikatili na kuondoka zake. Polisi wanachanganyikiwa, wanamtafuta muuaji, wanamkosa kwani anaonekana kuwa makini hasa kwenye kufuta alama za vidole vyake.

Hali ya hofu inaendelea kutanda jijini Dar es Salaam.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Amani ikatoweka moyoni mwake, muda mwingi Pamela alionekana kuwa na majonzi mengi, hakuamini kile kilichokuwa kikiendelea kwamba marafiki zake, wafanyakazi wenzake wa uchangudoa walikuwa wakifa katika mazingira ya kutatanisha.

Moyo wake ulijawa hofu lakini hakutaka kujali sana, aliingia jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutafuta fedha tu na hakutaka kurudi tena Arusha pasipo kuwa na fedha. Alifanya kazi yake huku akiwa na hofu kubwa lakini hilo, alilipuuzia kwa kuamini kwamba kama siku yako ya kufa imefika, hata ufanye nini utakufa tu.

Siku hii alikuwa amejipumzisha chumbani kwake, ilikuwa majira ya saa kumi jioni. Alijisikia kuchoka, alihitaji muda mwingi wa kupumzika kabla ya usiku kuelekea katika shughuli zake kama kawaida.

Wakati akiwa hapo, akasikia simu yake ikiita, alipoangalia namba ya mpigaji, alikuwa Stella, changudoa mwenzake maeneo ya Kinondoni Makaburini. Hakujua alitaka nini, mara nyingi halikuwa jambo la kawaida kupigiwa simu muda huo kwani machangudoa wengi hupenda kulala kwa ajili ya kazi kubwa ya usiku. Alichokifanya, akaipokea.

“Shoga, unasikia kinachozungumziwa kwenye TV?” aliuliza Stella hata kabla ya salamu.

“Kituo gani?”

“Global TV.”

Haraka akachukua rimoti na kuwasha televisheni yake na kuweka kituo hicho alichoambiwa. Macho yake yakatua kwa mtu ambaye alimfahamu kabisa, alikuwa akizungumza kama Kamanda Mkuu wa Jeshi la Polisi Kanda ya Dar es Salaam, Kamanda Dickson.

Kwanza hakuamini kile alichokiona, akaisogelea televisheni na kumwangalia yule mtu aliyekuwa akizungumza kwa kuhisi labda alimfananisha, alipomwangalia, alikuwa mwenyewe.

“Kumbe ni mkuu wa polisi!” alisema Pamela kwa mshtuko, hofu ikaanza kumuingia, kijasho chembamba kikaanza kumtoka.

“Halo Pamela unamsikia huyo polisi anavyoongea?” alisikika Stella akiuliza.

“Abee..” aliitikia Pamela huku akionekana kuwa kwenye lindi la mawazo.

“Umemsikia?”

“Ndiyo!” alipojibu hivyo tu, hapohapo akakata simu.

Pamela akakosa nguvu, hakuamini kile alichokiona kwenye televisheni. Akasimama na kuanza kuzungukazunguka ndani ya chumba chake huku akiongea peke yake kama chizi. Kichwa chake kilijaa mawazo mengi, alichojiuliza ni juu ya Kamanda Dickson ambaye bado alikuwa akizungumza kwenye televisheni.

Hapo ndipo akajaribu kuvuta kumbukumbu za nyuma, siku alipokutana na Kamanda Dickson kwa mara ya kwanza. Aliikumbuka siku hiyo, alikumbuka sana kwamba alimuita ndani ya gari kulipokuwa na mwanga hafifu na kisha kumchukua tena huku kichwani akiwa na kofia.

Hapo ndipo alipopata jibu juu ya kofia ile, hakuishia hapo, alikumbuka mpaka siku walipokwenda chumbani, alipotoka kuoga na kuuona uso wake kisha kuulizwa kama alishtuka na yeye kujibu hapana.

Pia alikumbuka siku ambayo yeye na machangudoa wengine walikamatwa na polisi kisha kutupwa sero, cha kushangaza kabisa ambacho kilimwachia maswali mengi, yeye aliachwa huru pasipo kujua sababu ya polisi kufanya hivyo.

Kila kitu kikaanza kutiririka kichwani mwake, akapata majibu ya kila swali lililokuja kichwani mwake. Mbali na kufikiria hivyo, pia akaanza kukumbuka maneno ya watu wengine ambao walimuona muuaji wa machangudoa wote kwamba alikuwa mwanaume fulani aliyekuwa na kofia ya Marlboro kichwani.

Hapo pia akapata jibu kwamba inawezekana yule muuaji aliyekuwa akiwaua machangudoa alikuwa mwanaume huyohuyo, swali muhimu lililokuja kwake ni sababu za mtu huyo kuwaua watu hao zilikuwa nini? Na kama kweli yeye ndiye alikuwa muuaji, kwa nini hakumuua siku ya kwanza alipoingia naye chumbani? Kila alichojiuliza, akakosa jibu kabisa.

“Lakini inawezekana yeye ndiye huyu muuaji?” alijiuliza.

“Mmh! Hapana! Mbona mimi hakuniua? Kwa nini? Ila inawezekana kweli akawa ndiye muuaji? Siwezi kukubali hilo, hebu ngoja kwanza nimpigie simu,” alisema Pamela kisha kuchukua simu yake.

Haikuwa kazi kubwa kuipata namba ya Kamanda Dickson, aliisevu kwa jina la ‘Buzi’, alipoiona, moja kwa moja akampigia simu kwa lengo la kuzungumza naye. Simu ikaanza kuita.

Macho yake yalikuwa yakimwangalia Kamanda Dickson kwenye televisheni, aliendelea kuipiga, bado haikupokelewa na mara baada ya dakika kadhaa, Kamanda Dickson alipomaliza kuzungumza, simu haikuwa ikipatikana.

* * * *

Mara baada ya kufika kwenye nyumba ya wageni, moja kwa moja Dickson na Happy wakaingia ndani. Muda wote, Happy alikuwa kimya, moyo wake ukahisi kwamba inawezekana huyo mwanaume ndiye aliyekuwa muuaji kwani muda wote aliing’ang’ania kofia yake kuwa kichwani mwake, hakutaka kuivua.

“Usiwashe taa mpenzi…” alisema Kamanda Dickson.

“Kwa nini?”

“Napenda giza, giza ndiyo mzuka wenyewe…”

Happy akazidi kuwa na wasiwasi, mbali na kofia, pia tukio hilo likampa uhakika kwamba mwanaume huyo ndiye aliyekuwa muuaji kwani hakuona sababu ya mtu kusema kwamba hakutaka mwanga kwa kuwa alipenda giza, yaani ufanye mapenzi na mtu pasipo kumuona uso wake, lilikuwa jambo lisilowezekana.

“Ndiye yeye…” alisema Happy, akaomba ruhusa kwenda chooni kwanza, kitu kilichomshangaza Kamanda Dickson, msichana huyo alikwenda na kipochi chake huko chooni, kitu hicho kikampa maswali mengi.

“Mmh!” alijikuta akiguna, tayari machale yakamcheza, naye akajiweka sawa pasipo kujua msichana huyo alikuwa mtu hatari.


Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 59

Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam, machangudoa wengi wanaanza kuuawa katika mazingira ya kutatanisha. Hakuna anayemjua muuaji, kila changudoa anayenunuliwa na mwanaume aliyekuwa kwenye gari aina ya Volkswagen nyeusi, anauawa kikatili.

Kila mmoja anaogopa, machangudoa wengine wanaacha kujiuza, wanajifungia vyumbani mwao ila kwa wengine ambao hawakuweza kuishi bila kufanya biashara hiyo, wanakwenda huko, bado wengine wanaendelea kuuawa.

Nyuma ya kila kitu, kuna mwanaume mmoja mwenye sura mbaya, tena akiwa ni Kamanda Mkuu wa Jeshi la Polisi Kanda ya Dar es Salaam, (DCP) Dickson ndiye ambaye anafanya mauaji hayo pasipo kugundulika. Kazi yake ni kununua machangudoa na yeyote atakayemgundua, humuua kikatili na kuondoka zake. Polisi wanachanganyikiwa, wanamtafuta muuaji, wanamkosa kwani anaonekana makini hasa kwenye kufuta alama za vidole vyake.

Hali ya hofu inaendelea kutanda jijini Dar es Salaam.

Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

“Haloo… naongea na Peter Msigwama?” aliuliza Kamanda Dickson.

“Ndiyo! Wewe nani? Mbona usiku-usiku?” aliuliza Peter.

“Unazungumza na Kamanda Dickson…”

“Kumbe ni wewe mkuu! Samahani sana..”

“Usijali. Upo wapi?”

“Nyumbani…”

“Nielekeze, nataka kuja mara moja kuonana nawe…” alisema Dickson.

Kamanda Dickson alikuwa akizungumza na mtu aliyejulikana kwa jina la Peter Msigwama. Huyu alikuwa kijana mwenye uwezo mkubwa wa kuchezea kompyuta na kufanya wizi katika benki mbalimbali nchini Tanzania.

Mwaka mmoja uliopita, zaidi ya shilingi bilioni tano ziliibwa kwa njia ya kitaalamu katika Benki ya Watu iliyokuwa jijini Dar es Salaam, mkurugenzi wa benki hiyo alichanganyikiwa, hakuamini kilichotokea hali iliyomfanya kuwaambia vijana wake wa kitengo cha IT (Information Technology) waliokuwa wakihusika na mambo ya kompyuta kuhakikisha wanajua akaunti fedha hizo zilipohamishiwa.

Haikuwa kazi ndogo, ilikuwa kazi kubwa ambayo usiku na mchana watu wa kitengo hicho cha IT walikesha lakini hawakuweza kujua mahali fedha zilipohamishiwa, mtu aliyezihamisha alionekana kuwa mtaalamu wa kucheza na system.

“Vipi?” aliuliza mkurugenzi huku akionekana kuchanganyikiwa.

“Bado hatujajua ni nani,” alijibu jamaa mmoja huku akionekana kuwa bize na kompyuta yake.

Mkurugenzi hakutaka kusubiri, kiasi cha fedha kilichoibwa kilikuwa kikubwa mno akawaita wataalamu wengine kwa ajili ya kumfanyia kazi hiyo lakini majibu yalikuwa yaleyale, hawakuweza kutambua fedha hizo zilikwenda wapi.

Mtu aliyekuwa ameiba fedha hizo alikuwa Peter, aliziiba akiwa chumbani kwake huku kompyuta ya mapajani ikiwa mbele yake. Uso wake ulikuwa kwenye tabasamu pana, baada ya kusoma IT, Mississippi nchini Marekani, alirudi Tanzania na zoezi lake la kwanza kabisa ili kuona kama aliiva ilikuwa ni kuiba fedha hizo.

Utaalamu alioutumia ulikuwa ni wa hali ya juu. Mkurugenzi na uongozi mzima wa Benki ya Watu ulichanganyikiwa, hawakujua nini cha kufanya, japokuwa walitoa taarifa polisi lakini hilo halikufanikiwa kugundua fedha hizo zilitolewa na kuwekwa kwenye akaunti ipi.

“Yaani hamjajua fedha zimewekwa kwenye akaunti ipi?” aliuliza polisi mmoja.

“Hatujajua mkuu! Tumesumbuka kwa siku tatu mfululizo, hatukupata kitu,” alijibu jamaa mmoja wa kitengo cha IT.

Simu ikapigwa nchini Afrika Kusini, wataalamu wengine wanne wakashuka na kupelekwa katika benki hiyo lakini bado hali ilikuwa tete. Baada ya wiki kupita, Peter akaamua kuzirudisha fedha hizo katika benki hiyo, mkurugenzi akashusha pumzi, hakuamini kilichotokea.

Polisi hawakutulia, vichwa vyao vilisumbuka, watu wakatumwa kwa ajili ya kufanya upelelezi kugundua ni nani aliyekuwa akihusika katika wizi huo, japokuwa fedha zilirudishwa lakini bado walitaka kumfahamu mtu huyo.

Baada ya siku kumi, wakafanikiwa kumkamata Peter ambaye aliwaambia marafiki zake mchezo aliocheza ambao walimsaliti kwa kutoa taarifa polisi kisiri. Polisi walipomuona Peter hawakuamini, alikuwa kijana mdogo mno lakini kichwa chake kilikuwa na mambo makubwa.

Kama serikali, haikutaka kumpoteza kijana kama Peter, walichokifanya ni kumchukua kwa ajili ya kuisaidia serikali huku akipewa sehemu muhimu kwa ajili ya kufanyia mambo yake tofauti na wizi.

Katika kipindi alichopelekwa katika kituo cha polisi ndipo alipokutana na Kamanda Dickson, hakuamini alipomuona Peter, alipoambiwa kwamba huyo ndiye aliyehusika katika wizi wa mabilioni ya fedha kwa kutumia kompyuta yake, alibaki akishangaa. Kwa kuwa namba ya kijana huyo iliachwa ofisini kwake akaamua kuichukua.

“Huyu atanisaidia…” alisema Dickson baada ya kumkumbuka Peter.

Alipompigia simu na kuzungumza naye, akaamua kumfuata Mikocheni alipokuwa akiishi. Japokuwa ilikuwa ni usiku sana lakini hakutaka kujali, ilikuwa ni lazima kuonana naye ili aweze kuzihamisha fedha zake na kuziweka katika akaunti yake ya siri.

“Unataka nikusaidie nini mkuu?” aliuliza Peter huku akitetemeka, alimuogopa sana kamanda huyo, hakuwa mtu mzuri hata mara moja.

“Nataka kuhamisha fedha zangu zote, kutoka kwenye akaunti hii, kwenda kwenye hii,” alisema Dickson huku akimuonesha akaunti zake.

“Hakuna tatizo…”

Peter hakutaka kuuliza maswali, alichokijua ni kwamba bado mtu huyo alikuwa kiongozi wa jeshi la polisi lakini ukweli ni kwamba aliamua kutoroka na kuacha kila kitu. Peter akaingia kazini, akachukua kompyuta yake ya mapajani na kuanza kufanya kazi hiyo. Japokuwa ilikuwa ni usiku sana, hakuchoka, hakusinzia, alitaka kuhakikisha fedha zinahamishwa, kweli baada ya dakika thelathini, kiasi chote cha shilingi milioni mia mbili kikahamishwa kwenda kwenye akaunti nyingine ya siri ya Dickson. Kamanda Dickson akakenua, sasa kilichobaki ni safari ya kuelekea katika Kisiwa cha Ukerewe kujificha.

Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 60

Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam, machangudoa wengi wanaanza kuuawa katika mazingira ya kutatanisha. Hakuna anayemjua muuaji, kila changudoa anayenunuliwa na mwanaume aliyekuwa kwenye gari aina ya Volkswagen nyeusi, anauawa kikatili.

Kila mmoja anaogopa, machangudoa wengine wanaacha kujiuza, wanajifungia vyumbani mwao, ila kwa wengine ambao hawakuweza kuishi bila kufanya biashara hiyo, wanakwenda huko, bado wengine wanaendelea kuuawa.

Aliyekuwa akiua wanawake hao ni Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda ya Dar es Salaam, Dickson. Aliwaua kwa siri lakini baada ya kipindi fulani kupita, akagundulika na hivyo kuanza kutafutwa.

Kwa amehamishiwa fedha zake zote katika akaunti yake ya siri, hakuna aliyejua fedha zimehamishwaje kwani aliyefanya kazi hiyo ni mtaalamu sana katika mambo ya kompyuta, anachokifanya ni kuanza safari ya kuelekea Mwanza.


Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…

Usiku ambao taarifa zilitolewa kwamba Kamanda Dickson ndiye aliyekuwa akifanya mauaji na hivyo ilitakiwa atafutwe mpaka apatikane, polisi hawakutaka kuchelewa, walichokifanya kilikuwa ni kuimarisha ulinzi katika kila kona kuhakikisha kwamba mtu huyo havuki kwenda nje ya Jiji la Dar es Salaam.

Walichokifanya ni kuimarisha ulinzi mkali katika bandari zote kuhakikisha mtu huyo haondoki kuelekea Zanzibar au katika kisiwa chochote kile. Ulinzi wao haukuishia huko tu, pia wakahakikisha wanaimarisha ulinzi Kibamba ambapo walijua fika kwamba mtu huyo anaweza kutoroka na kuelekea katika mkoa wowote.

Ulinzi uliwekwa kila sehemu, hawakutaka kusikia mtu huyo akiondoka jijini Dar es Salaam kwenda sehemu yoyote ile kwani hata viwanja vya ndege, kote huku walihakikisha ulinzi unakuwa mkubwa, polisi wengi waliokuwa na bunduki na mbwa mikononi mwao walisimama imara wakimsubiri.

Wakati hao wakiwa wameweka ulinzi kila kona, Kamanda Dickson ndiyo kwanza alikuwa akitoka nyumbani kwa Peter ambapo tayari alikamilisha suala zima la uhamishaji fedha alilokuwa amelitaka lifanyike haraka iwezekanavyo.

Hakutaka kurudi nyumbani kwake, mpango wake mzima ulikuwa ni kutoroka na kuelekea katika Kisiwa cha Ukerewe ambapo aliamini kwamba angeishi kwa raha mustarehe huku akila maisha mpaka hapo atakapokufa. Akaondoka na kuelekea barabarani, kofia kubwa ilikuwa kichwani mwake kama kawaida, alipoiona Bajaj moja ikija kule alipokuwa, akaisimamisha.

“Hapa mpaka Kimara elfu ishirini…” alisema dereva Bajaj.
“Sawa! Twende…”
Safari ya kuelekea Kimara ikaanza mara moja. Njiani, alikuwa na mawazo mengi lakini hakutaka kujali sana, wakati huo haukuwa wa majuto tena, ulikuwa ni muda wa kufanya mambo mengine na kuangalia maisha yake ya mbele.

Kutoka hapo Mikocheni B mpaka Kimara walichukua dakika ishirini tu kufika, akamlipa dereva kiasi cha fedha alichokihitaji kisha kukaa pembezoni mwa barabara akisubiri magari makubwa ya mizigo.

Muda ulikuwa umekwenda sana, ilikuwa ni saa nane kasoro usiku, kulikuwa na baridi kali, lakini hakutaka kujali, kitu pekee alichokuwa akikihitaji ni kulikimbia Jiji la Dar es Salaam ambalo lilionekana kuwa la hatari katika maisha yake kipindi hicho.

Mawazo juu ya msichana Pamella yakaanza kurudi tena kichwani mwake, alimkumbuka msichana huyo mrembo, alijitahidi kumuonesha mapenzi ya dhati lakini kitu kilichotokea hakujua msichana huyo angelichukuliaje suala lake la kutafutwa baada ya kuwaua wanawake wengi.

“Hivi akijua itakuwaje?” alijiuliza lakini hakupata jibu lolote lile.
Wakati akiwaza hayo, akakumbuka kwamba alikuwa na namba yake ya simu hivyo alichokifanya ni kuichukua simu yake na kuanza kulitafuta jina la Pamella. Alichokuwa akikitaka ni kuzungumza naye, kumjulia hali na pia kumuomba msamaha kwa mabaya yote aliyoyafanya.

“Au nitampigia baadaye…” alisema na kuacha.
Wakati akiwa amesimama mahali hapo, kwa mbali akaliona gari kubwa aina ya Scania likija kule alipokuwa. Kwa haraka sana akasimama kutoka pale alipokaa na kusogea barabarani, kilichofuata ni kuanza kulisimamisha gari hilo kwa kupunga mkono juu, dereva akasimamisha gari hilo, hakuwa na hofu ya utekaji kwa kuwa bado alikuwa ndani ya jiji hilo.

“Nikusaidie nini? Mbona usiku sana?” aliuliza dereva huyo aliyeonekana kuwa na miaka sitini au zaidi.
“Nataka kwenda mkoani, nimefiwa rafiki yangu!”
“Umefiwa na nani?”

“Mama yangu! Tena usiku huuhuu. Naomba unisaidie swahiba…”
“Unakwenda wapi?”
“Dodoma..”

“Daah! Una bahati sana, mimi nakwenda Singida…ingia nikusaidie,” alisema dereva yule huku akifungua mlango. Dickson akaingia, kitu alichokutana nacho kwenye ‘dashboard’ ni Biblia ambayo ilimfanya kuamini kwamba mtu aliyempa lifti alikuwa Mkristo mzuri tu.

Safari ikaanza, garini, Kamanda Dickson hakutaka kuwa kimya, alikuwa mzungumzaji sana huku muda wote akijitahidi kubadilisha sauti yake na kusikika kivingine kabisa. Alimwambia dereva yule namna alivyoguswa na msiba wa mama yake kwani jinsi alivyokuwa akimlea tangu alipokuwa mtoto mpaka kipindi hicho, kwa kweli moyo wake ulimuuma sana.

Dereva yule alimwamini kwa kila alichomwambia, alichokifanya ni kumfariji na kumtia moyo kwamba hiyo yote ilikuwa ni mitihani ya dunia hivyo kama mwanaume alitakiwa kupambana mpaka pale atakaposhinda.

Kwa kipindi kifupi tu, wakazoeana, wakaanza kuzungumza kana kwamba walikutana kipindi kirefu kilichopita. Ingawa ilikuwa usiku sana lakini hakukuwa na mtu aliyetamani kulala, walibaki wakizungumza mpaka walipoingia Mbezi Mwisho.

Wakati wanatoka Mbezi Mwisho na kuanza kuelekea Kibamba, kwa mbali mbele wakaanza kuona msururu wa magari makubwa ya mizigo yakiwa yameegeshwa pembeni, hawakuelewa ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea, alichokifanya dereva yule ni kusimamisha gari lake karibu na gari jingine, akateremka na kumfuata dereva mwingine ambaye naye alisimamisha gari lake pembeni.

Kamanda Dickson hakujua kitu kilichokuwa kikiendelea, muda wote macho yake yalikuwa katika saa yake, alijiona kuchelewa, alitamani kumwambia dereva yule arudi kwani safari yake ndefu ilitakiwa kufanyika usiku kwa usiku na kama ikifika asubuhi, angekaa hotelini ambapo huko angeshinda siku nzima mpaka usiku ambapo angeendelea na safari yake.

“Kuna nini?” aliuliza Dickson wakati dereva aliporudi.
“Hawa polisi wanazingua sana, eti kuna mtu wanamtafuta…” alijibu dereva yule huku akionekana kukasirika.
“Mtu gani?”“Yule Kamanda Dickson, nasikia kavuruga, nilipata stori yake juu-juu tu usiku huu, ndiyo wanamtafuta kwa kupekua kila gari,” alijibu dereva yule pasipo kufahamu yule mtu aliyekuwa akizungumza naye ndiye aliyekuwa akitafutwa.

Moyo wa Dickson ukapiga paa, damu ikaanza kuzunguka kwa kasi mwilini mwake, hakuamini alichokisikia, hapohapo akajikuta akianza kutokwa na kijasho chembamba na wakati kulikuwa na kibaridi.

Polisi waliokuwa mahali hapo wakayaruhusu magari kusogea kule walipokuwa na gari walilokuwemo nalo likaruhusiwa, likaanza kusogea kule kulipokuwa na idadi kubwa ya polisi. Hakujua afanye nini kuwaepuka, akajikuta akianza kusali tu Mungu amuokoe na avuke salama.

Je, kitaendelea nini?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom