Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,744
- 25,445
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 35
Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam kufuatia kupotea mfululizo kwa machangudoa katika mazingira ya kutatanisha. Taharuki kubwa inazuka kwani ndani ya kipindi kifupi tu, zaidi ya machangudoa kumi na moja wanapotea na hakuna anayejua walikopotelea. Jambo hilo linasababisha jeshi la polisi kuingilia kati. Kinachozidi kuzua utata, wote wanapotea katika mazingira yanayofanana. Mwanaume mmoja asiyejulikana, aliyekuwa anatembelea gari la kifahari aina ya Volkswagen, aliyekuwa akienda eneo hilo usiku wa manane ndiye anayehusishwa na wote wanaopotea.
Upande wa pili, kijana aliyekuwa na mwonekano tofauti na binadamu wa kawaida, Dickson Maduhu au Zinja kama wenzake walivyokuwa wakimtania, amejiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Hisia kali za mapenzi zinasababisha kijana huyo aanze kutoka usiku na kwenda kutafuta machangudoa. Hivyo baadaye anahamishiwa Dar es Salaam.
Mara baada ya kufanikiwa kuwa DCP, Dickson anaendelea na tabia yake ya kununua machangudoa pasipo watu kufahamu kwamba yeye ndiye aliyekuwa amefanya mauaji ya msichana aliyeuawa siku kadhaa zilizopita.
Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…
Mzuka wa kufanya mapenzi ulikwishampanda Dickson, alimchukua changudoa yule na kumvuta kitandani pale, akili yake ilichanganyikiwa, umbo zuri na ngozi nyororo aliyokuwa nayo msichana yule ilizidi kumhamasisha kufanya naye mapenzi mle chumbani.
“Subiri kwanza,” alisema msichana yule.
“Kuna nini?”
“Mbona una haraka?”
“Sasa si tumelipia short time, tufanye fasta,” alisema Dickson, hata sauti aliyoitoa chumbani hapo ilionesha ni jinsi gani alikuwa kwenye mhemko mkubwa wa kufanya mapenzi. Dickson hakutaka kusikia kitu chochote kile, alichokuwa akikitaka ni kufanya mapenzi tu. Mapigo yake ya moyo yalikuwa yakidunda kwa kasi, damu ilizunguka kwa kasi mno, kilipita kipindi kirefu kufanya mapenzi kabla ya siku hiyo, ule mzuka wa wiki mbili zote alikuwa nao ulimzidi nguvu.
Alimchojoa changudoa nguo zake katika haraka ambayo hata yeye mwenyewe aliishangaa, alipomaliza, akamlaza kitandani. Katika kila kitu alichokuwa akikifanya mahali hapo hakutaka kugundulika kama alikuwa Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, kila alipomgeuza huku na kule, alihakikisha kwamba mwanga wa taa iliyokuwa nje haimpigi usoni mwake.
Walitumia muda huo vilivyo, baada ya saa mbili baadaye, kila mmoja alikuwa hoi, Dickson alibaki akimwangalia changudoa yule huku hata hamu ya kuendelea hakuwa nayo kabisa.
“Kiasi gani?”
“Unataka unilipe ipi? Ya mpaka asubuhi au short time?” aliuliza changudoa yule.
“Mpaka asubuhi japokuwa nataka kuondoka.”
“Laki moja na nusu.”
“Hakuna tatizo.”
Dickson akaivuta suruali yake na kutoa pochi yake ambapo akaifungua na kuanza kuhesabu fedha zake. Hakukuwa na hela ndogo, noti zote zilizokuwa ndani ya pochi ile zilikuwa ni elfu kumi tu, hivyo akazihesabu mpaka zilipofika kiasi hicho akamgawia msichana yule.
“Laki moja na nusu hii?” aliuliza msichana yule.
“Ndiyo!”
“Mmmh! Usije ukawa umenipiga changa la macho, ngoja niwashe taa nizihakikishe,” alisema msichana yule huku akisimama kitandani pale. Dickson akamshika mkono.
“Baby...”
“Abee kipenzi!”
“Huniamini?”
“Kwenye suala la fedha, hautakiwi kumuamini mtu, hata shemasi tu anaiba sadaka kanisani” alijibu msichana yule.
“Siwezi kukufanyia mchezo huo, niamini kipenzi. Kwanza hebu andika namba yako hapa,” alisema Dickson, aliamua kuliingizia suala la namba kwani hakutaka changudoa yule aendelee kuweka msisitizo wake juu ya kuwasha taa ile.
Dickson akafanikiwa kumlaghai msichana yule na mwisho wa siku hakuweza kabisa kuwasha taa ile kitu kilichomfurahisha sana Dickson. Mpaka alipoamua kuondoka na kumuachia changudoa yule fedha za kutosha zaidi, wakaahidiana kwamba kuanzia siku hiyo angekuwa mteja wake, yaani kuhusu suala la fedha hakutakiwa kuwa na wasiwasi kabisa.
Kila siku usiku Dickson alipokuwa akifika Sinza Mori, hakutaka kumchukua msichana mwingine zaidi ya huyohuyo aliyejitambulisha kwa jina la Magreth, ila awapo kazini alipenda sana kuitwa Mage. Uwepo wa Dickson ukawa gumzo mahali hapo, machangudoa wengi wakamfahamu kama mwanaume aliyekuwa akija na gari jeusi, kila walipoliona usiku mahali hapo, walijua fika kwamba alifika mahali hapo kwa ajili ya kumchukua Magreth, hivyo hawakutaka kumuingilia.
Katika kipindi cha wiki mbili, Magreth hakuweza kugundua kwamba yule mtu aliyekuwa akimchukua kila usiku alikuwa Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam. Siku zikaendelea kukatika, kutokana na fedha alizokuwa akizipata Magreth, akawa changudoa aliyekuwa na maendeleo kuliko yeyote mahali hapo.
“Niitie Magreth...” alisema Dickson, kama kawaida alikuwa amefika Sinza Mori kwa ajili ya kumchukua Magreth na kuondoka naye kama kawaida yake.
“Hajafika!” alijibu msichana mmoja aliyevalia kimini.
“Amekwenda wapi?”
“Hajafika. Anaumwa tumbo!”
“Sawa! Asante.”
“Hutaki huduma?”
“Nataka, ila kama ye....”
“Hata mimi naweza kukupa huduma, tena zaidi ya huyo Mage,” alisema msichana huyo.
“Kweli?”
“Kweli kabisa.”
“Basi ingia twende nikaone,” alisema Dickson.
Kutokuwepo kwa Magreth hakukuwa na tatizo lolote lile, alichokuwa akikitaka mahali hapo ni kufanya mapenzi tu, hakujali chochote kile, akamchukua msichana yule na kuanza kuondoka naye mpaka kwenye gesti bubu ya Chenchebe iliyokuwa maeneo ya Mwananyamala. Walipofika, wakateremka na kuingia ndani pasipo dada wa mapokezi kuhoji sana kwani alikuwa mteja wake ambaye hakuwahi hatakumuona uso, alimzoea mno na hata wakati mwingine aliachiwa kiasi fulani cha fedha.
“Nataka unionyeshee ulichonacho sasa,” alisema Dickson. “Usijali,” alisema msichana yule, akakifuata kitanda na kuanza kujinyonganyonga maungo yake, alipomaliza akazivua nguo zake na Dickson kumfuata pale kitandani.
“Anza na kifua changu kwanza,” alisema msichana yule, kwa haraka pasipo kuuliza chochote Dickson akafanya kama alivyoambiwa pasipo kujua kwamba huo ulikuwa mtego mkubwa, msichana yule alitaka kumlevya na madawa ya usingizi aliyoyapaka kifuani.
Je, nini kitafuatia?
Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam kufuatia kupotea mfululizo kwa machangudoa katika mazingira ya kutatanisha. Taharuki kubwa inazuka kwani ndani ya kipindi kifupi tu, zaidi ya machangudoa kumi na moja wanapotea na hakuna anayejua walikopotelea. Jambo hilo linasababisha jeshi la polisi kuingilia kati. Kinachozidi kuzua utata, wote wanapotea katika mazingira yanayofanana. Mwanaume mmoja asiyejulikana, aliyekuwa anatembelea gari la kifahari aina ya Volkswagen, aliyekuwa akienda eneo hilo usiku wa manane ndiye anayehusishwa na wote wanaopotea.
Upande wa pili, kijana aliyekuwa na mwonekano tofauti na binadamu wa kawaida, Dickson Maduhu au Zinja kama wenzake walivyokuwa wakimtania, amejiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Hisia kali za mapenzi zinasababisha kijana huyo aanze kutoka usiku na kwenda kutafuta machangudoa. Hivyo baadaye anahamishiwa Dar es Salaam.
Mara baada ya kufanikiwa kuwa DCP, Dickson anaendelea na tabia yake ya kununua machangudoa pasipo watu kufahamu kwamba yeye ndiye aliyekuwa amefanya mauaji ya msichana aliyeuawa siku kadhaa zilizopita.
Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…
Mzuka wa kufanya mapenzi ulikwishampanda Dickson, alimchukua changudoa yule na kumvuta kitandani pale, akili yake ilichanganyikiwa, umbo zuri na ngozi nyororo aliyokuwa nayo msichana yule ilizidi kumhamasisha kufanya naye mapenzi mle chumbani.
“Subiri kwanza,” alisema msichana yule.
“Kuna nini?”
“Mbona una haraka?”
“Sasa si tumelipia short time, tufanye fasta,” alisema Dickson, hata sauti aliyoitoa chumbani hapo ilionesha ni jinsi gani alikuwa kwenye mhemko mkubwa wa kufanya mapenzi. Dickson hakutaka kusikia kitu chochote kile, alichokuwa akikitaka ni kufanya mapenzi tu. Mapigo yake ya moyo yalikuwa yakidunda kwa kasi, damu ilizunguka kwa kasi mno, kilipita kipindi kirefu kufanya mapenzi kabla ya siku hiyo, ule mzuka wa wiki mbili zote alikuwa nao ulimzidi nguvu.
Alimchojoa changudoa nguo zake katika haraka ambayo hata yeye mwenyewe aliishangaa, alipomaliza, akamlaza kitandani. Katika kila kitu alichokuwa akikifanya mahali hapo hakutaka kugundulika kama alikuwa Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, kila alipomgeuza huku na kule, alihakikisha kwamba mwanga wa taa iliyokuwa nje haimpigi usoni mwake.
Walitumia muda huo vilivyo, baada ya saa mbili baadaye, kila mmoja alikuwa hoi, Dickson alibaki akimwangalia changudoa yule huku hata hamu ya kuendelea hakuwa nayo kabisa.
“Kiasi gani?”
“Unataka unilipe ipi? Ya mpaka asubuhi au short time?” aliuliza changudoa yule.
“Mpaka asubuhi japokuwa nataka kuondoka.”
“Laki moja na nusu.”
“Hakuna tatizo.”
Dickson akaivuta suruali yake na kutoa pochi yake ambapo akaifungua na kuanza kuhesabu fedha zake. Hakukuwa na hela ndogo, noti zote zilizokuwa ndani ya pochi ile zilikuwa ni elfu kumi tu, hivyo akazihesabu mpaka zilipofika kiasi hicho akamgawia msichana yule.
“Laki moja na nusu hii?” aliuliza msichana yule.
“Ndiyo!”
“Mmmh! Usije ukawa umenipiga changa la macho, ngoja niwashe taa nizihakikishe,” alisema msichana yule huku akisimama kitandani pale. Dickson akamshika mkono.
“Baby...”
“Abee kipenzi!”
“Huniamini?”
“Kwenye suala la fedha, hautakiwi kumuamini mtu, hata shemasi tu anaiba sadaka kanisani” alijibu msichana yule.
“Siwezi kukufanyia mchezo huo, niamini kipenzi. Kwanza hebu andika namba yako hapa,” alisema Dickson, aliamua kuliingizia suala la namba kwani hakutaka changudoa yule aendelee kuweka msisitizo wake juu ya kuwasha taa ile.
Dickson akafanikiwa kumlaghai msichana yule na mwisho wa siku hakuweza kabisa kuwasha taa ile kitu kilichomfurahisha sana Dickson. Mpaka alipoamua kuondoka na kumuachia changudoa yule fedha za kutosha zaidi, wakaahidiana kwamba kuanzia siku hiyo angekuwa mteja wake, yaani kuhusu suala la fedha hakutakiwa kuwa na wasiwasi kabisa.
Kila siku usiku Dickson alipokuwa akifika Sinza Mori, hakutaka kumchukua msichana mwingine zaidi ya huyohuyo aliyejitambulisha kwa jina la Magreth, ila awapo kazini alipenda sana kuitwa Mage. Uwepo wa Dickson ukawa gumzo mahali hapo, machangudoa wengi wakamfahamu kama mwanaume aliyekuwa akija na gari jeusi, kila walipoliona usiku mahali hapo, walijua fika kwamba alifika mahali hapo kwa ajili ya kumchukua Magreth, hivyo hawakutaka kumuingilia.
Katika kipindi cha wiki mbili, Magreth hakuweza kugundua kwamba yule mtu aliyekuwa akimchukua kila usiku alikuwa Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam. Siku zikaendelea kukatika, kutokana na fedha alizokuwa akizipata Magreth, akawa changudoa aliyekuwa na maendeleo kuliko yeyote mahali hapo.
“Niitie Magreth...” alisema Dickson, kama kawaida alikuwa amefika Sinza Mori kwa ajili ya kumchukua Magreth na kuondoka naye kama kawaida yake.
“Hajafika!” alijibu msichana mmoja aliyevalia kimini.
“Amekwenda wapi?”
“Hajafika. Anaumwa tumbo!”
“Sawa! Asante.”
“Hutaki huduma?”
“Nataka, ila kama ye....”
“Hata mimi naweza kukupa huduma, tena zaidi ya huyo Mage,” alisema msichana huyo.
“Kweli?”
“Kweli kabisa.”
“Basi ingia twende nikaone,” alisema Dickson.
Kutokuwepo kwa Magreth hakukuwa na tatizo lolote lile, alichokuwa akikitaka mahali hapo ni kufanya mapenzi tu, hakujali chochote kile, akamchukua msichana yule na kuanza kuondoka naye mpaka kwenye gesti bubu ya Chenchebe iliyokuwa maeneo ya Mwananyamala. Walipofika, wakateremka na kuingia ndani pasipo dada wa mapokezi kuhoji sana kwani alikuwa mteja wake ambaye hakuwahi hatakumuona uso, alimzoea mno na hata wakati mwingine aliachiwa kiasi fulani cha fedha.
“Nataka unionyeshee ulichonacho sasa,” alisema Dickson. “Usijali,” alisema msichana yule, akakifuata kitanda na kuanza kujinyonganyonga maungo yake, alipomaliza akazivua nguo zake na Dickson kumfuata pale kitandani.
“Anza na kifua changu kwanza,” alisema msichana yule, kwa haraka pasipo kuuliza chochote Dickson akafanya kama alivyoambiwa pasipo kujua kwamba huo ulikuwa mtego mkubwa, msichana yule alitaka kumlevya na madawa ya usingizi aliyoyapaka kifuani.
Je, nini kitafuatia?