Usher-smith MD
JF-Expert Member
- Jul 7, 2015
- 9,504
- 12,176
Kaanza na Mwenge
Bwana baba wa mbingun awe nanyi wapendwa katika kristo.
Kama kichwa cha habali kinavyosomeka tupeane kinachoendelea kutoka kwa Gwajima
Leo katika mahubiri yake alikuwa akizungumzia swala la uchawi wa kufungwa kutooana (kuinamishwa) kazungumzia mengi hasa mali tulizonazo kuanzia maziwa, mito, mbuga lakini tunalia pia migodi ya dhahabu kuwa tumefungwa hatuoni.
Ana sema anauliza kwanini mwenge unakimbizwa nchi nzima mtaa kwa mtaa unamaana gani? Je unazunguka kutulaza? (Kutuloga)
Anataka aupige ila akijibiwa ndo ataupiga vizuri.
Sasa lengo la kuanzishwa mpka leo unakimbizwa kufanya nini na kwa gharama kubwa? Kwanini wasiukimbize toka mwenge hadi posta tena live kwenye tv na radio si inatosha?
Huu mwenge sio unatuinamisha watanzania tusione?
Kunanini kwenye mwenge?
Kama Magufuli kaanza na madini na hili litamshindaje? Maana usiku huwa watu hukutana kwa maovu tupu na hasara kwa taifa.
HahahahaHuyo awahubirie waumini wake namba gani ya kwenda Mbinguni na kurithi ufalme wa Mbinguni sio vijembe na udaku wa Tandale na Manzese uwanja wa fisi.
Kama ana hamu na siasa aachane na Dini aingie kwenye kuvuana mataulo na chupi kwenye siasa maana huko utachambuliwa mpaka unakolala!!
Sikuhizi naona kuna raisi mkuu na rais msaidiziGwajima kuwavua mataulo wanaomchokoza
Dar es Salaam. Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amewatahadharisha wanaomchokoza akisema ni sawa na mtu anayeanzisha ugomvi huku akiwa amevaa taulo.
Akihubiri leo, Gwajima amesema wakiendelea atawavua mataulo ili jamii iwaone.
Bila kufafanua kuhusu kauli hiyo, Gwajima amesema hawezi kunyamaza wakati watu wanaendelea kumfuata fuata.
"Leo nitakwapua mataulo ya watu,"amesema huku akishangiliwa na waumini wake.
Madini
Dar es Salaa,. Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amesema ni muhimu madini yasichimbwe hadi itakapowekwa mashine za kuchenjua makinikia.
Akizungumza kwenye ibaada kanisani kwake leo Askofu Gwajima amesema, "Tusiogope kushtakiwa Magufuli(Rais John) piga marufuku makinikia kusafirishwa nje."
"Madini yaliyopo Tanzania ni zaidi ya 300 lakini bado tuna umaskini tumelogwa na nani."
Vipi yale mapepo aliyotuma kwenda kwa Rc Makondo alifikia wapi? Je hayo mapepo anayahifadhi kanisani mwake au anatembea nayo?Leo katika mahubiri yake alikuwa akizungumzia swala la uchawi wa kufungwa kutooana (kuinamishwa) kazungumzia mengi hasa mali tulizonazo kuanzia maziwa, mito, mbuga lakini tunalia pia migodi ya dhahabu kuwa tumefungwa hatuoni.
Ana sema anauliza kwanini mwenge unakimbizwa nchi nzima mtaa kwa mtaa unamaana gani? Je unazunguka kutulaza? (Kutuloga)
Anataka aupige ila akijibiwa ndo ataupiga vizuri.
Sasa lengo la kuanzishwa mpka leo unakimbizwa kufanya nini na kwa gharama kubwa? Kwanini wasiukimbize toka mwenge hadi posta tena live kwenye tv na radio si inatosha?
Huu mwenge sio unatuinamisha watanzania tusione?
Kunanini kwenye mwenge?
Kama Magufuli kaanza na madini na hili litamshindaje? Maana usiku huwa watu hukutana kwa maovu tupu na hasara kwa taifa.