Mganguzi
JF-Expert Member
- Aug 3, 2022
- 1,032
- 2,769
Karibu hapa askofu Josephat gwajima! Heri konzi Moja pamoja na furaha ! Kuliko konzi mbili pamoja na huzuni ,nakuuliza askofu wangu ndugu Josephat kwamba hulioni anguko lako Bado najua Unafahamu thamani na heshima ya kuhani wa mungu ! Mimi nauliza tu Bado tuendelee kuiamini mikono yako vichwani mwetu? Bado tuendelee kunywa mvinyo ambayo tayari imechanganywa na siasa? Nauliza tu ameenda wapi yule Josephat gwajima wa mwaka 2000? Yameenda wapi Yale maono makubwa ya kujenga mji wa mwanakondoo? Maelfu ya watu waliokuwa wanakanyagana pale kawe na ubungo hapo waendelee kuiamini mikono yako? Nauliza tu askofu wangu ! Wale ulikuwa unawatolea mapepo na kuponya magonjwa yao kwa sasa wanajua wewe ni mwanasiasa ! Ninini kimekuondoa madhabahuni na kwenda kwenye ulingo wa siasa uliojaa chuki ,visasi ,matusi na dhihaka za Kila aina ? Waumini wako wanakuona bunju unacheza singeli ! Nini kimekupata tajiri mkubwa! ....si ni wewe uliagiza trein? Si ni wewe uliagiza ndege? Si ni wewe ulikuwa unaongea na Amina chifupa kwa nguvu ya maombi ? Ninini kimekupata? Wewe unaonaje kanisa lako la 2000 ni sawa na la Leo? Najua utajikaza kisabuni lakini kiufupi Hilo nianguko kubwa sana kwako! YESU alisema toshekeni na mishahara ! Mungu wako alikunyima nini ukiwa mtumishi wake? Akija Josephat yule wa 2010 akakutana na wewe Josephat wa 2024 ! Atakupiga vibaya sana umemharibia heshima yake ! Na umemuondolea Nuru yake! Kwa nini unamfanyia hivi josephati gwajima yule asilia? Wewe ni gwajima yupi? Ok sawa ! Umeamua kuchagua mauti na kuukataa uzima? Umeamua kuchagua kumtumikia herode ? Umeamua kuchagua kuvaa utukufu wa farao !? Nimeona nikukumbushe huenda macho yako yamepofuka hayaoni ! Asante sana