Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,808
- 59,326
Kwa nnavyoelewa mimi neno ''gubu'' hua linatumika kuongelea ile hali ya mtu kukumbushia makosa au kutosahau kwa maana nyingine.Wanaosemwa kwa kua na gubu mara nyingi ni wanawake.Wanaume hawachoki kabisa kuongelea ni kiasi gani hawapendelei/hawafurahishwi na hii tabia.
Binafsi sipendi hilo neno kwasababu halitendei haki watu wanaokosewa kila mara alafu akijaribu kukuonyesha kwamba hata jana ulifanya vile vile unaanza kukwambia ana gubu!!!Kama ambavyo unapomuomba mtu msamaha unategemea na unataka kusamehewa ndivyo ambavyo na wewe unatakiwa usirudie makosa.Ukikosa tena unaomba msamaha na unayemwomba ana haki ya kukuonyesha ni jinsi gani unaabuse msamaha anaokupa kila mara.
Ni kweli kwamba binadamu hatujakamilika ndo maana tunakosa na kukosa tena na tena....kwa hayo hayo mapungufu ndo inashindikana kusahau kabisa yaliyopita na kukumbushana mara kwa mara.
Naamini kwamba jana inajenga leo....ulichokosea jana unajifunza ili usirudie tena leo....ulichofanya jana kama ni kizuri kinafanikisha furaha ya leo nk.Hata swala la mafanikio....ukikumbuka kitu kilichokuangusha jana ni rahisi zaidi kukikwepa mbeleni kwahiyo watu wakubali kusemwa na kukumbushwa pale inapobidi maana safari ya mabadiliko ndivyo inavyoanza...KWA KUKUMBUKA!!!!
Ila katika kila kitu kunahitajika kiasi.Don't exaggerate things....kidogo acha kibaki kua kidogo!!!
Binafsi sipendi hilo neno kwasababu halitendei haki watu wanaokosewa kila mara alafu akijaribu kukuonyesha kwamba hata jana ulifanya vile vile unaanza kukwambia ana gubu!!!Kama ambavyo unapomuomba mtu msamaha unategemea na unataka kusamehewa ndivyo ambavyo na wewe unatakiwa usirudie makosa.Ukikosa tena unaomba msamaha na unayemwomba ana haki ya kukuonyesha ni jinsi gani unaabuse msamaha anaokupa kila mara.
Ni kweli kwamba binadamu hatujakamilika ndo maana tunakosa na kukosa tena na tena....kwa hayo hayo mapungufu ndo inashindikana kusahau kabisa yaliyopita na kukumbushana mara kwa mara.
Naamini kwamba jana inajenga leo....ulichokosea jana unajifunza ili usirudie tena leo....ulichofanya jana kama ni kizuri kinafanikisha furaha ya leo nk.Hata swala la mafanikio....ukikumbuka kitu kilichokuangusha jana ni rahisi zaidi kukikwepa mbeleni kwahiyo watu wakubali kusemwa na kukumbushwa pale inapobidi maana safari ya mabadiliko ndivyo inavyoanza...KWA KUKUMBUKA!!!!
Ila katika kila kitu kunahitajika kiasi.Don't exaggerate things....kidogo acha kibaki kua kidogo!!!