howard
Senior Member
- Feb 21, 2011
- 188
- 28
Wanajamvini nilikuwa naangalia taarifa ya habari Channel 10 kuhusu sakata la dodoma nillkichokiona kwa Lema ni kuwa huyu ni mtu jasiri. Mkuu wa mkoa anasema "kuanzia sasa wanasiasa hawaruhusiwi kwenda vyuoni na kufanya shughuli za kiasiasa kwa kuwa wanasababisha vurugu na ndio maana wanafunzi wa UDOM wamejaa pale na kuletya vurugu". Lema akahojiwa akasema na "yeye hatasimama kwenda kwenye vyuo kwa kuwa si dhambi ataenda vyuo vingi tu hakuna sheria yoyote anayovunja kuongea na wanafunzi na mazingira anayoongea ni yale aliyokuwepo mkuu huyo wa mkoa ingawa watu wa TV hawakuonyesha mkuu huyo wa mkoa alikuwa wapi. anasema alikwenda UDOM kuwaambia wanafunzi waje kutoa mawazo yao kwa kuwa mswada umeandikwa kwa kiingereza na wale ni wasomi wanajua wanachangia nini. Nikasema hivi huyu jamaa akipewa uongozi wa aina yoyote sehemu anayoisimamia itakuwaje, Namkubali sana huyu jamaa ktk kuwakilisha hisia zake.Mungu amlinde