MVUMBUZI
JF-Expert Member
- Jan 8, 2011
- 5,182
- 2,330
Mafarisayo, na wakuu wa Kiyahudi waliwahi mpelekeaYesu mwanamke aliyekamatwa akizini ili amuhukumu. Yesu akawasikiliza akauliza ana tatizo gani wakasema wamemkamata akizini na wanataka amhukumu kwa sheria za Kiyahudi. Yesu akaandika maandishi ardhini kwa kidole kisha akasimama na kuwaambia" ASIYEKUWA NA DHAMBI MIONGONI MWENU NA AWE WA KWANZA KUMPIGA KWA MAWE". Kilichotokea ni kwamba kila mmoja alianza mbele kuanzia mdogo hadi mkubwa na kumwacha yule mwanamke peke yake. Hapa nina maana gani wana JF? wote wanaojidai kutaka kutoa data za Lema ili tu aonekane mhalifu ni wanafiki wakubwa na in essence hawajui watendalo. Nasema hivi kwa sababu hebu kila mmoja ajitazame kwa uaminifu katika nafsi yake kama ni msafi kiasi gani. Kwa mfano Mungu akisema asiye na dhambi aje hapa na kama ukija wakati unajua una dhambi hakika utakufa then kaa pembeni utazame ni wangapi wataenda kujitakia matatizo. Binadamu hatuko safi kiasi cha kushabikia mwenzako kuitwa mwizi namna hiyo kwani kama wewe siyo Mzinzi basi ni mdokozi, na kama siyo mwasherati basi mwongo au mrushi au mwenye tamaa, husuda au wivu au ubakaji, au ushoga, au ubasha n.k. Lazima tujue watu wa namna hiyo wote hawafai kuongoza wenzao ila kutokana na ukweli kwamba hakuna mtu ambaye hana kasoro hata moja basi tunachagua wale ambao ni afadhali kuliko wenzao. Lema inawezekana aliwahi husishwa na hayo mambo huko mwanzo kutokana na ujana ila kwa sasa amekuwa ameacha. Zaidi sana ni nani aliyeko kwenye uongozi wa nchi hii tunaweza kum single out kuwa hana dosari yoyote ya kitabia?
Kama tuna uhakika wa hilo swali na tunajua kuwa tu safi na watakatifu basi tuendelee kumjadili Lema.
Nina uhakika kila mmoja wwetu akichimbwa sawasawa na kujadiliwa basi tutajikuta wengine hatutafikia hata nusu ya uadilifu wa Lema.
Kama tuna uhakika wa hilo swali na tunajua kuwa tu safi na watakatifu basi tuendelee kumjadili Lema.
Nina uhakika kila mmoja wwetu akichimbwa sawasawa na kujadiliwa basi tutajikuta wengine hatutafikia hata nusu ya uadilifu wa Lema.
