Godbless Lema: Kesho narudi bungeni!

Godbless Lema: Kesho narudi bungeni!

unajua ccm mnafikiri eti wananchi wanawapongeza kumbe tunawaonea huruma mnavyopotea njia. nashauri badilisheni nafasi ya uspika hali ni tete upande wenu
 
ukivuta bang hata maramoja ni tatizo sasa hawa wameifanya bang kuwa ni chakula chao

Pole umekalia wamevuta bangi... inaonyesha huna hoja ya msingi... toa kifungu gani alichotumia naibu spika kuwaadhibu... shame on you... mnatumika tumika tu kama condoms... Njaa mbaya sana.
 
Sifa binafsi wamachinga arusha shida kibao amekalia mwongozo wa spika
Msemakweli hapa si maneno matupu mnayobwabwaja hapa bali ni pale octoba 2015 ndipo hasira za watanzania zitakapopelekwa kwenye masanduku ya kura. Hapo ninyi CCM mtaomba milima iwaangukie au ardhi ifunguke mkimbilie humo.
 
Nimemsikia Mbunge lema kupitia taarifa ya habari ya ITV ya saa 2 usiku huu akisema kuwa kesho anarudi bungeni licha ya amri ya naibu spika kuwazuia kuingia bungen kwa siku 5.

Mbunge Lema alikuwa akihojiwa na ITV sambamba na wabunge wengine waliosimamishwa kuhudhuria vikao vya bunge.Mmoja wao alikuwa mh.Tundu Lissu aliesema hakuna kanuni ya bunge inayoweka ukomo wa mtu kuomba utaratibu na kwamba maamuzi ya naibu spika hayakuwa sahihi.Wengi wao waliohojiwa wamelaumu uamuzi huo.

Binafsi nashindwa kuamini nilichokisika labda kama nimesikia vibaya maana najiuliza kama hizo kanuni za bunge zitamruhusu kweli kurudi bungeni?

Kwakweli wabunge wa CHADEMA wananyanyaswa sana na kiti cha spika!

Makamanda vumilieni kwani msitarajie ushindi rahisi bila watu kupita katika kipindi kigumu.

Hata hivyo,naibu spika anapaswa kutafakari athari za kukosa michango ya wabunge hao ndani ya bunge kwa siku hizo 5.Maamuzi haya ya jaziba hayana tija kwa watanzania badala yake ni hasara kwa Taifa.
alichosema lema ni kuwa hizo siku tano ni sawa na siku moja, maana alisema kuna watu waliwahi kufungwa miaka 27 jela!
 
(samahani wakuu kama nimetoka nje ya mada)
Nijuavyo mimi kazi ya Ubunge inategemea kuchaguliwa kila baada ya miaka mitano, kwa hiyo mtu hawezi kulazimisha na ndio maana wanakuwa na professional zingine mbadala.
Sasa swali langu ni hili:
- Mh. Tundu Lissu ni Mwanasheria na wakili kwa hivyo asipochaguliwa (tuseme 2015) anaingia mahakamani,
- Je, Mh. Job Ndugai professional yake ni nini na alikuwa akifanya nini kabla ya hapo?

Majibu haya yanaweza kutuongezea mwanga juu ya kilichotokea na kinachoendelea
 
bangi zinamsumbua tumewachoka badala kujadili shida za wananchi mmekalia kuonekana sifa za kishenzi,pumbafuuuu chadomo

Pumbaf ni wewe mwenye mtindio wa ubongo usiyejua unachokiandika, nyau we! masaburi mkubwa we!
 
ccm wamezoea kusinzia na kuzomea bungeni,wanacdm wako makini kutetea hoja za msingi,kwa ulev wa cheo cha uspika,hawaoni alama za nyakati,imebuma
 
Vipi mbona Lema hajatinga mjengoni? Kama alivyoahidi jana mwenye taarifa tafadhali atujuze
 
Tundu Lissu na wenzake walioomba utaratibu yaani "Point of Order" hawakuwa na kosa lolote kwani Kanuni ya Bunge ibara ay 65(1)(c) inasema hivi:

{Isipokuwa tu kwa idhini ya Spika, Mbunge yeyote hataruhusiwa kusema zaidi ya mara moja juu ya hoja, ila tu kama anasema kuhusu utaratibu}

Hivyo, Lema, Lissu na wenzake hawajavunja kanuni yoyote na anayepaswa kuwajibika ni Job Ndugai kwani video imeonyesha wazi kuwa amezuia point of order wakati hana mamlaka hayo.
UNAWEZA UKAWA SAHIHI SANA... lakini ki-staarabu inaonyesha wazi jinsi wabunge wa CDM walivyo wakorofi kwa kupania INTENTIONALLY kuvuruga mchango wa NCHEMBA. mbona mnyika,lema na lissu walitoa michango yao(tena yenye kejeli na matusi) lakini wabunge wa CCM walivumilia mpaka wakamaliza michango yao!!!???
CDM hakuna utamaduni wa kuvumilia mashambulizi na hivyo kukosa sifa ya kuwa chama cha siasa. mnataka kuvuna mazao ambayo hata mbegu hazijaanza kuchipua.. mngekibadilisha chama chenu kiwe NGO ya kukutanisha akina MANGI kila mwisho wa wiki na kunywa mbege.. siasa ni wito na hakuna mwenye wito miongono mwenu na hata yule mmoja ZZK mmefnikiwa kumbadilisha kutoka kuwa mwanasiasa sasa amekuwa mwanaharakati kama wenzie
 
Mungu hajasinzia ! ! Lema haendi kwa Mganga ila Hua Anjibiwa Maombi Maana Anabahati kuchagua upande wa haki.
Kumbuka mungu hali CHAPATI
 
Vipi mbona Lema hajatinga mjengoni? Kama alivyoahidi jana mwenye taarifa tafadhali atujuze

ndugu yangu weeee aende wapi huyo mchovu, wafuasi wa cdm wamezoea kudanganywa na vijikelele vya kwenye media na walivyowepesi kuamini uongo sasa hapa ukiwaambia jamaa jana kaudanganya umma watabisha, spika ni mamlaka, fyata kabisaaa, arudi tena ITV kuwaambia ataingia tena kesho
 
Wanajf,jana usiku nilipata nafasi ya kwenda kuangalia tarifa ya habari ya saa 2 usiku katika ukumbi wa chuo, wanafunzi walikua ni wengi sana na wnapenda sana kuanaglia tarifa ya habari ya ITV.

Nilishangazwa sana pale GODBLESS LEMA alivyo sema kesho narudi bungeni, ukumbi mzima ulisimama na kushangilia. Ndipo nilipo amini kuwa CHADEMA ni chaguo la MUNGU.

MUNGU ibariki TANZANIA, MUNGU ibariki CHADEMA.
 
Back
Top Bottom