Godbless Lema katika kashfa ya kuiua CHADEMA Arusha

Godbless Lema katika kashfa ya kuiua CHADEMA Arusha

Crashwise katika uzi wa Octoba 2012 alijibu baadhi ya tuhuma hizi, majibu ambayo yanapatikana https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la...azi-print.htm. Kwa kifupi alielaza kuwaIli kuweka mambo sawa, kiwanja cha hospital iliyoahidiwa na Lema kipo Burka kilomita tatu kutoka barabara kuu na kwa sasa michoro ya hosp. inaendelea, trekta lilikabidhiwa kwa wamama wasiojiweza lakini itakuwa chini Arusha Dev Fund (ArDF).


Naye Mkurugenzi wa Afya na Elimu (ArDF) alitoa taarifa hii:
Awali ya yote napenda sana kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuweza kutujaalia uhai.
Nimeisoma na kuielewa vema mada yako ndugu Lengio, wenye kichwa cha habari “Lema katupapeli shamba alilo omba kujenga hospital ya Wazazi”.
Napenda kueleza mambo machache ambayo yatakuwa na umuhimu kwetu na taifa kwa ujumla, na hasa kuondoa uvumi huu ambao hauna tija kwa taifa na ambao umekuwa ukienezwa na watu wenye fikra mgando. Awali ya yote naomba kueleza kwamba mimi ni mmoja wa Waasisi wa Taasisi ya Maendeleo ya jimbo la Arusha mjini,(Arusha Development Foundation -ArDF) Naitwa Kamanda Magoma Jr Magoma, kwa sasa ni Mkurugenzi wa Elimu na Afya katika taasisi ya ArDF (nikiwa na jukumu kubwa la kuhakikisha tunafanikiwa kutimiza malengo ya taasisi ya ArDF katika nyanja za Afya na Elimu) si kama ambavyo mleta mada ameeleza bila kuwa na haya wala soni hata tone kwa kufanya upotoshaji wa hali ya juu bila kupima madhara yake kwa jamii kwamba “Lema katutapeli shamba alio omba kujenga hospital ya Wazazi”. Napenda nileezee historia ya awali ambayo ninahisi wanachi wengi hasa waishio nje ya Arusha hawaifahamu na wangependa kuifahamu. Mwaka 2010 katika kampeni za uchaguzi mkuu Kamanda Lema aliahidi kwamba atajenga hospitali ya mama na mtoto katika jimbo la Arusha mjini endapo atapewa dhamana ya kuliwakilisha jimbo la Arusha mjini katika bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kamanda Godbless Lema alisema “ili kuondoa adha ya huduma za afya kwa mama na mtoto, hasa ikizingatia kuwepo kwa msongamano na wagonjwa katika hostpitali ya Mkoa wa Arusha (Mount Meru) mkinichagua nitajenga hostiptali ya mama na mtoto”. Baada ya kamanda Lema kushinda alikutana na wadau wengine wa maendeleo katika jimbo la Arusha na kuamua kuanzisha Taasisi ya Maendeleo ya jimbo la arusha (ArDF). Aidha moja na malengo ya msingi ya ArDF ni kujenga hospitali ya mama na mtoto, hivyo ili kuweza kufanikisha malengo ya kujenga hospitali kiwanja ni semehu ya vitu muhimu katika utekelezaji wa ujenzi, hivyo wadau wa Maendeleo walitupatia eneo la ukubwa wa ekari tano katika eneo la Burka, na ili kuweka kumbukumbu sahihi kiwanja hicho kiko chini ya ArDF kikiwa kinasimaniwa na Mama na Mtoto Foundation (Taasisi tanzu ya ArDF) na kwamba si kweli kiwanja hicho kinamilikuwa na Kamanda Godbless Lema na wala hakijabadilishwa umiliki wake wa awali kama ambavyo ndugu Lengio atanaka kuupotosha umma. Hivyo napenda kuwajulisha kwamba alicho andika ndugu Lengio ni uongo na hali ya juu na ni uposhaji uliopiliza mipaka. Chadema ni chama chenye viongozi makini wenye lengo la dhati la kuijenga Tanzania. Aidha nichukue fursa hii kuwajulisha wanachi wa Arusha kwamba tumekuwa tukiwasiliana na wadau na wataalum wa Afya na baada ya muda tutaanza ujenzi wa Hospitali ya mama na watoto, ikisimamiwa na Mama na Mtoto Foundation. “Umoja Wetu ndio Silaha yetu”
Naomba kuwasilisha,
Asanteni Wana JF.
Kamanda Magoma Jr Magoma
(Mkurugenzi wa Elimu na Afya ArDF)
(M/Kiti Mstaafu CHADEMA Wilaya Arusha Mjini)

Hoja na viroja vya nyongeza?








Tuwekee hati ya kiwanja hapa ili kuondoa utata simple as that watu waone jina la kiwanja na hata ikibidi weka michoro kwani kuna siri gani hapa?
 
Tatizo ni kwamba wabunge wa chadema badala ya kutekeleza waliyo waahidi wananchi wanatumia muda wao mwingi kutafuta umaarufu na mwishowe itafikia 2015 hawajafanya kitu kwenye majimbo yao.
 
Mwache Kitila ana yake yanayomtosha. Hukuona katika sakata la Masalia juu ya madiwani wa Arusha?

Hivi hii ndiyo development fund pekee Tanzania? Hata kama ikiwa na ripoti ya mwaka ni kwa ajili ya nani? Hata wewe usiyehusika inakuhusu? Uliona wapi mambo hayo? Ndiyo maana wakaunda Fund. Kama ingekuwa ni kitu cha kila mtu huundi Fund ya nini? Ukiona hivyo hicho ni chombo maalum kwa ajili ya watu maalum. Kama huhusiki na hiyo Development Fund ripoti yake ya mwaka waitakiani?

Yaani sisi watanzania tunapenda kudanganywa sana. Hii Foundation inatoka wapi kwenye tuhuma za Lema? Foundation ibaki kama ilivyo na Lema aje ajibu tuhuma zake kama Lema. Thus are two things different and also are two different Legal entint
 
Hawa wanaosimamia ArDF ndio beneficiaries wa huo ufisadi, unategemea waseme nini? Kama chadema iko serious imtume Kitila akafanye uchunguzi huru Arusha juu ya hizi tuhuma.

mkuu,
Dr. Kitila anahusishwa na watu fulani humu kama na yeye ni kundi la 'masalia' kutokana na swala la madiwani Arusha. Haitakuwa vizuri kwake yeye kwenda kuchunguza kwa sababu kuna uwezekano hicho kikundi kikapiga kelele na kusema 'kesi ya mbuzi amepelekewa fisi'.

Labda Tablet ya Mheshimiwa Godbless Lema ni mbovu ndiyo maana hajatokea kutolewa ufafanusi kama afanyavyo kila mara kuhusu hii barua na viongozi wengine waandamizi bado wana hangover ya vikao vya chama.

Kwanza tumia akili ndogo tu, Development foundation gani haina ripoti ya mwaka? Anachotakiwa kufanya ni kuleta ripoti ya mwaka ya mapato na matumizi pamoja na majina na anuani za walionufaika na ArDF.

Katika maswala ya uangalizi wa pesa, lazima kuwepo transaction na report ya maandishi kuhusu mapato na matumizi. Tunafahamu jf siyo mahali ya kuonyesha mtiririko wa each transaction lakini kwa vile Chama kinasimama katika dhana ya uwazi katika utendaji na kina viongozi waandamizi katika mitandao, basi wangetolea ufafanuzi kwa hili.

WASWAHILI WANASEMA, KIMYA KINGI KINA KISHINDO.
 
hapo hakuna changamoto acha kupoteza muda mkuu.
aliyoibua hizo tuhuma anadai ni kiongozi wa chama, je, alichukua hatua gani ndani ya chama na alipewa majibu gani?
je, alishawahi kumwuliza Lema?

Hivi Mungi sanity yako iko integral kweli?
Mtu kaiandika barua ofisi ya mäkao makuu ya chama na barua yenyewe iko hapa, halafu unauliza amechukua hatua gani? Au ulitaka apigane makonde kama anavyofanya Lema?
Barua inajieleza wazi kwamba ukorofi wa Lema umeshindikana kushughulikiwa na ngazi zote walayani na mkoani ndio maana wamepeleka swala hili kwa kamati kuu.
Lete hati ya kiwanja cha kujenga hospitali tuone jina la mmiliki...
 
Mkuu, document hiyo imetoka kwenu Arusha na kusainiwa majina hayo umeyaona na imetumwa hadi makao makuu ya chadema. Mimi sijaongeza neno kwa nini unanishambulia mimi binafsi? badala ya kujibu yatokanayo na hiyo Document?

fitina zenu bahati kwetu
 
my take: Chadema isipokuwa makini umaarufu wake utapungua kutokana na migogoro mingi inayokikumba chama hicho. Mwaka 2015 si mbali jahazi linaonekana kuyumba ukilinganisha na huko nyuma. Wengi wataumia ndani ya chama hicho kwani umaarufu wa mtu unakuwa juu ya chama. Hizi tuhuma dhidi ya lema hazikijengi chama bali zinakibomoa. Arusha hali si shwari.

attachment.php

attachment.php


zaidi, angalia attachments chini
muda utafika watanzania watajua yote,kabati langu limejaa uchafu wao.nashukuru na ww umeweka huu uchafu wa yule anayyejiona malaika,wakati uchafu wa lema akiwa nccr pale arusha tumeuziba kwa muda.
Asante kwa kufunua haya machache,mm nipo bize naanda atomic bom waliloliandaa wao wenyewe kwa matukio mannne tofauti ya kutisha.kuna haja ya watanzania kuyajua sasa.
 
Tatizo ni kwamba wabunge wa chadema badala ya kutekeleza waliyo waahidi wananchi wanatumia muda wao mwingi kutafuta umaarufu na mwishowe itafikia 2015 hawajafanya kitu kwenye majimbo yao.
A time wil tell.Mbona hawa si wakwenda nao haraka,taratibu kila mmoja atawekwa wazi kwa uchafu wake.Hapa nasubiria document zinifikie muda wowote kutoka makao makuu ya chama za uozo wa CHADEMA COLLEGE pale KIBAHA.Pesa zilishatoka,Katibu mkuu akaelekeza tumboni kwake
 
muda utafika watanzania watajua yote,kabati langu limejaa uchafu wao.nashukuru na ww umeweka huu uchafu wa yule anayyejiona malaika,wakati uchafu wa lema akiwa nccr pale arusha tumeuziba kwa muda.
Asante kwa kufunua haya machache,mm nipo bize naanda atomic bom waliloliandaa wao wenyewe kwa matukio mannne tofauti ya kutisha.kuna haja ya watanzania kuyajua sasa.

lema hakuwahi kuwa Nccr..poleni kwa kuchinjwa man,ndo matunda ya undumilakuwili.,jaribu kalime huko pwani.
 
A time wil tell.Mbona hawa si wakwenda nao haraka,taratibu kila mmoja atawekwa wazi kwa uchafu wake.Hapa nasubiria document zinifikie muda wowote kutoka makao makuu ya chama za uozo wa CHADEMA COLLEGE pale KIBAHA.Pesa zilishatoka,Katibu mkuu akaelekeza tumboni kwake
mradi tu ziwe taarifa za ukweli na zisiwe za kutengeneza.
 
bado hadi 2015 tutaona mengi...unajua siku zote unapomnyoshea mwingine kidole kumbuka vidole vingine vinakunyoshea wewe................... katika chadema kuna uchafu mwingi sana kama ukitolewa humu ukweli chama hiki hakiwezi simama mbele ya watu na kusema ni chama mbadala ni bora hata ccm
 
A time wil tell.Mbona hawa si wakwenda nao haraka,taratibu kila mmoja atawekwa wazi kwa uchafu wake.Hapa nasubiria document zinifikie muda wowote kutoka makao makuu ya chama za uozo wa CHADEMA COLLEGE pale KIBAHA.Pesa zilishatoka,Katibu mkuu akaelekeza tumboni kwake
TUNTEMEKE tunasubiri nondo
 
Bila kukusahau na wewe mwenyewe mpenda madaraka lakini ni dhaifu sana hata kuliko hao uliowataja.

Ha ha haa haaaaaaaaaaaaa. Masalia wamewashika pabaya mwaka huu! Msipoabadilisha jina na kukiita chama cha Maendelo na Masalia (CHAMAMA) sijui!
 
Duh uzi unazidi kwenda post #332 hakuna mtetezi aliyetayari kubandika hati ya kiwanja,hakuna mtetezi wa kutuweka sawa tractor liko wapi linafanya nini,limewasaidia wajane wangapi (ikiwezekana waweke anwani).hakuna aliyetayari kuonyesha mchakato wa ndani wa ugombea udiwani Daraja II ulivyokwenda!.

Hakuna majibu hoja zimekosa majibu viroja vimechukuwa nafasi yake.Nilisema na nitaendelea kusema Lema hana sifa za uongozi.Ipo siku wapinzani wangu wataniita wenyewe bila kulazimishwa Nabii Ngongo.Si kwamba naichukulia barua iliyoletwa na MAMA POROJO kama kigezo cha udhaifu wa Lema hapana hii barua ni nyongeza ndogo sana ya udhaifu na uhuni wa Lema.
 
Last edited by a moderator:
Mimi huwa najiuliza kila siku je watu wanaojiita wanachadema je ni washabiki?,Wafuasi? wapenzi? au wanachama?
Hawataki kabisa kuona mtu wanaomwamini kasemwa vibaya.
Hivi hao ni malaika au ni miungu wasio na makosa?

Seriously haya mabo ya Lema yanatakiwa yatolewe ufafanuzi wa kina. La sivyo nitawaona watu wa chadema kama majuha.
 
muda utafika watanzania watajua yote,kabati langu limejaa uchafu wao.nashukuru na ww umeweka huu uchafu wa yule anayyejiona malaika,wakati uchafu wa lema akiwa nccr pale arusha tumeuziba kwa muda.
Asante kwa kufunua haya machache,mm nipo bize naanda atomic bom waliloliandaa wao wenyewe kwa matukio mannne tofauti ya kutisha.kuna haja ya watanzania kuyajua sasa.

lema hajawai kuwa nccr bali aliwai kuwa TLP na hii inadhihirisha you know nothing about Lema, hayo mabomu kila siku unasema unayaanda siku zinazidi kwenda yatalipukia uvunguni kwako.
 
Duh uzi unazidi kwenda post #332 hakuna mtetezi aliyetayari kubandika hati ya kiwanja,hakuna mtetezi wa kutuweka sawa tractor liko wapi linafanya nini,limewasaidia wajane wangapi (ikiwezekana waweke anwani).hakuna aliyetayari kuonyesha mchakato wa ndani wa ugombea udiwani Daraja II ulivyokwenda!.

Hakuna majibu hoja zimekosa majibu viroja vimechukuwa nafasi yake.Nilisema na nitaendelea kusema Lema hana sifa za uongozi.Ipo siku wapinzani wangu wataniita wenyewe bila kulazimishwa Nabii Ngongo.Si kwamba naichukulia barua iliyoletwa na MAMA POROJO kama kigezo cha udhaifu wa Lema hapana hii barua ni nyongeza ndogo sana ya udhaifu na uhuni wa Lema.

inadhihirisha kuwa husomi majibu yaliyotolewa humu, kuhusu tractor jibu limeshatolewa, kuhusu kiwanja jibu limewekwa humu ila kama wewe una hati yenye jina la lema weka tuone, tukiwaendekeza nyie kila siku mtakuja na propaganda za kutaka mpaka tuwawekee humu hadi mipango yetu ya ndani, kwa mfano: wewe usiyehusika na chama unahitaji kujua mchakato wa uchaguzi wa daraja II ili iweje??
 
Back
Top Bottom