Goba ni uswazi iliyochangamka ni Manzese ama Tandale ya miaka 30 ijayo

The Assassin

JF-Expert Member
Oct 30, 2018
4,355
17,321
Wikiendi iliyopita, Jumamosi na Jumapili nilipata wasaa wa kutembea Goba kwa sehemu kubwa kwa sababu nilikua na ndugu yangu ambae katoka huko mkoani anataka kiwanja na kujenga Dar.

Ndugu yangu kafika hapa tayari alishachagua eneo analolitaka kua ni Goba, basi tukatafta madalali na kuanza kuzungukia viwanja, kuanzia makongo, Goba Senta, Goba Kulagwa, Goba Kilalata kwa awadhi, ostabei na sehemu nyingine nyingi.

Baada ya mizunguko ya siku 2 ndio nikagundua kwamba Goba ni Uswahilini kwenye nyumba za kisasa.

Kwa maana kwamba Goba haijapangiliwa kabisa. Goba kuna nyumba kali na za kisasa sana ila hakujapangwa, nyumba nzuri ila zimejegwa zigzaga, hakuna mitaa iliyonyooka.

Miaka 30 ijayo Goba itakua kama Manzese ya sasa ama Tandale, itakua uswazi.

Ni wakati sasa Serikali inapaswa kuingilia hii biashara ya upimaji na uuzaji ardhi. Hua najiuliza hivi viongozi wetu wakienda huko ulaya hawaoni wenzetu miji yao ilivyopangwa? Mbona huku kwetu wanaacha mambo yanakua hovyo hivi?

Ni hayo tu wakuu.
 
Kama watu wanaweza kujenga nyumba Kali wanashindwa nini kukubaliana kuacha miguu kadhaa Kwa ajili ya barabara....Hii nchi kwenye suala la kupanga miji ukiachia serikali utaumia, naona serikali hasa halmashauri haziwazi kabisa kupanga miji.
 
Miaka 30 n mingi sana mkuuu.n hapo mbelee tu miaka michache patakuwa hapatamanikii maaana Raia n wengi sana wanakimbilia goba ..

Karibu nikupe kiwanjaa njia ya makongo mkuu kipo njian kbs na huduma zt zipo ..
 
Goba na milima yake kuanzia Kayuni mpaka huko tegeta A. Kama ingepangiliwa vizuri ikapimwa ingekuwa kama Beverly hills, Capetown RSA, Lavington Nairobi, Cite El nasr Au Menzah VI Tunis au Cairo New city Egypt, Cocody Abidjan Ivorycoast.

Hakuna raha kama mitaa inaelekea milimani halafu nyumba zimepangana. Sijui Nyerere alisahau wapi kuongoza upimaji ardhi na makazi maana yeye peke yake ndio alikuwa na akili za kuona miaka 100 mbele.

Ukitaka kujua nyerere alikuwa na akili angalia ardhi aliyowapimia na kuwapa TPA, Tazara, TRC wangekuwa hawa viongozi wa sasa wasingekuwa na akili ya kuacha ardhi kubwa leo gsm anafaidi eneo la tazara, azam anafaidi eneo la TPA, TRC. Hii kambi ya Lugalo enzi za mwalimu ilikuwa inaanzia mwenge mpaka mto mbezi bondeni kawe yote haikuwepo.
 
Goba na milima yake kuanzia Kayuni mpaka huko tegeta A. Kama ingepangiliwa vizuri ikapimwa ingekuwa kama Beverly hills, Capetown RSA, Lavington Nairobi, Cite El nasr Au Menzah VI Tunis au Cairo New city Egypt, Cocody Abidjan Ivorycoast.

Hakuna raha kama mitaa inaelekea milimani halafu nyumba zimepangana. Sijui Nyerere alisahau wapi kuongoza upimaji ardhi na makazi maana yeye peke yake ndio alikuwa na akili za kuona miaka 100 mbele.

Ukitaka kujua nyerere alikuwa na akili angalia ardhi aliyowapimia na kuwapa TPA, Tazara, TRC wangekuwa hawa viongozi wa sasa wasingekuwa na akili ya kuacha ardhi kubwa leo gsm anafaidi eneo la tazara, azam anafaidi eneo la TPA, TRC. Hii kambi ya Lugalo enzi za mwalimu ilikuwa inaanzia mwenge mpaka mto mbezi bondeni kawe yote haikuwepo.
Tegeta A mbona pako vizuri,mpka goba mpakan
 
Ni maeneo machache sana hapa Dar ambayo mipango miji walizingatia upimaji wa viwanja kwa mpangilio na kuacha barabara pana inayoweza kupata njia ya magari, watembea kwa miguu na mitaro ya maji taka

Kuna baadhi ya maeneo ukipita hapa Dar nyumba ni za kawaida lakini ukiangalia mipango miji walivyopangilia panapendeza machoni. Barabara pana nyumba zimefuatana vizuri
 
Back
Top Bottom