Ghetto langu lilinisaliti; Mrembo akanikimbia

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,900
GHETTO LANGU LILINISALITI; MREMBO AKANIKIMBIA!

Anaandika, Robert Heriel

Vijana jijengeni! Wekeni mambo yenu Sawa kama mnataka hizi pisikali! Wanawake hawana Jema! Wengi ni materialists. Hakikisheni mnaishi sehemu nzuri na vitu vya ndani viwe vimenyooka.

Mnyamwezi kama kawaida yangu ikifika majira ya jioni nilikuwa natoka kwenda kuwinda, si unajua tena Ujana maji ya moto ya kumnyonyolea Kuku wa Sikukuu. Ilikuwa kawaida kila jioni kutoa kwenda kuwinda vitoto vya mjini virembo. Mimi nilikuwa mlevi wa warembo. Nilikuwa Teja wa pisikali, yaani nikiona tuu pisikali Roho itanipwita na sinaga kawaida ya kuutesa moyo yangu. Yaani nione pisikali alafu nisiitongoze labda sio Mimi.

Hapo nimepigilia pamba zangu. Kijana wa rika langu na Wadada WA hirimu yangu ingekuwa ngumu Sana kunikatalia. Mabinti wengi walikuwa wakijigonga na Mimi katika vitu nimejaliwa basi ni mdomo WA kuongea, Sauti iliyotulia, maneno yaliyopangika, na ujanjaujanja WA hapa na pale Kwa umri wangu uliifanya kazi ya kutongoza warembo iwe nyepesi.

Binti mmoja ambaye aliukonga moyo wangu vilivyo. Mtoto amejaliwa Sura, rangi na umbo la kushangaza. Alikuwa kaumbwa jamani! Nikasema potelea mbali! Nikamuimbisha, mtoto akanikagua kama Gari la udalali, sikujali Mimi. Aliporidhishwa tukabadilishana namba, mahusiano yakaanza. Tukapanga appointment aje Ghetto.

Siku ikafika, mrembo akafika Ghetto la Taikon. Daah! Kwa kweli ghetto liliniangusha. Yule Dada bhana ni kama nilim- disappoint.
ATI akanambia siendani na pale ninapoishi.
Akaanza kupakosoa, mara kitanda gani like, mara ninaishi kwenye kachumba kabaya, alafu vitu vimelundikana kama Stoo. Akaendelea kuisema Feni yangu, ATI Nina Feni ya kishamba, mara sabufa ya kisukuma. Yaani aliongea vitu vya ajabu sijapata kusikia.

Sikutaka kukwazika ili nisijevuruga mipango yangu ya kumchapa ili nilipize hasira zangu zote.
Nikamdanganya kuwa kuna Pesa nilikuwa nimeipata hivyo asiwaze, nikamuonyesha muamala kama laki Saba hivi. Nikamwambia hiyo hela ni mahususi ya kuliweka Sawa Ghetto langu.
Asijue hiyo Pesa ilikuwa ni ya Boom. Nikamuambia nitamtumia laki moja Kwa sababu kuna milioni mbili na nusu hivi zitaingia siku tatu zinazofuata. Nitahama pale kisha akija atafurahi mwenyewe.

Mtoto kusikia ninataka kumtumia laki moja akajisahau tena. Asijue yupo na jitu baya, Dudu liumalo lenye Roho za mizimu ya kale. Mtoto akajichanganya nami nimamgeuza mchuzi mix.

Vijana, jipangeni. Hawa Wanawake sio wamchezo mchezo. Jijengeni. Vinginevyo Watoto Wazuri mtatuachia Sisi wanyamwezi. Wazee wa Dp World.

Ijumaa Kareem

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Pesa muhimu sana, ujanja ujanja ni mzuri ila huwa unatesa na sometimea una maumivu. Pesa haina maneno meeengi anajaa mwenyewe tu

Na kadiri unavyokua mkubwa unachoka kuongeaongea.
Maneno mengi Wakati mwingine ni dalili ya utoto na uvulana.
Watu wanataka waone vitu vikifanyika.
Sio blah! Blah! Blah!

Siku hizi nimekuwa sina maneno mengi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom