Design hii ya wanawake wanastahili kutorokwa kwenye bill

BabaMorgan

JF-Expert Member
Dec 18, 2017
4,050
10,490
Sometimes nakubaliana na baadhi ya wanaosema Mwanamke hapaswi kuonewa huruma kutokana na tabia zake za ubinafsi.

Kuna mwanamke ameomba tukutane tusalimiane kwa mtazamo wangu ni kuwa amenimiss anahitaji kuniona tupeane salamu then kila mtu ataendelea na ratiba zake nikapigia pamba zangu kawaida shati nyepesi, crazy jeans na chini Crocs very simple ila good looking bajeti ya nauli niliweka elfu kumi lengo ni kama kuna matumizi mengine yataongezeka basi yasizidi hiyo hela ila kwa tahadhari nikatoka na elfu thelathini mfukoni.

Picha linaanza nimepanda daladala nimemuomba konda mapema anishushe kituo x maana sipajui nikapitilizwa vituo vitatu tayari bajeti yangu ikaanza kuvurugika ikabidi nipande Bodaboda kurudi kituo nilichopitishwa.

Nimefika kituo husika nakuta binti yupo vizuri kapendeza kimsingi ni mrembo tunasalimiana ananiambia ana njaa anataka kwenda kula kitimoto na ugali kwa mazingira tuliyopo mimi ni mgeni nikamuuliza vipi tunaenda wapi wanapouza hicho kitimoto ananiambia mimi nakufuata wewe kwa tathmini ya haraka tulipo kuna mabaa ya gharama kwa elfu 30 yangu nikaona nitakuja kuaibika so nikamwambia twende mitaa ya kwetu lengo akatae tuachane palepale au akubali ili tukifika mitaa ya ghetto iwe mtelemko kumpeleka gheto kula tunda kimasihara.

Tunaanze safari ya kuelekea home ground tunapita kwa wamachinga anadai nimnunulie pafyumu nikamkazia nikamwambia nitakuletea kama gift siku nyingine tunapanda usafiri maana ni magari mawili tulipo mpaka mitaa ninayoishi.

Tumefika wanapouza kitimoto ikabidi niagize nusu lengo waandae pale ili gheto tuende kutoa dongo akaanza kutoa maagizo jinsi anavyotaka kiandaliwe wakati tunasubiria kitimoto nikamwita muhudumu atupe viwanyaji mi nikaagiza zangu maji yeye sasa akaanza kuagiza vinywaji ambavyo bahati nzuri havikuwepo maana vingekuwepo ingekuwa hasara kwangu.

Wakati tunapiga stori akaanza habari za kuwa anataka kuhama kwao kodi na vitu vya ndani alishapata je mimi kama mimi nitamchangia nini? Nikaona ili tatizo bora liishie hapahapa hakuna haja ya kwenda ghetto ingawa nilikuwa natamani mapaja yake tumemaliza kula anadai nirequest Bolt kucheki nauli ya Bodaboda elfu kumi na mimi kwenye 30 yangu nimebakiwa na elfu kumi na tano na kwa vyovyote vile inabidi nibaki na ten la kuanzia maisha kesho maana sijui michongo itaendaje.

Nikampa elfu tano anadai ndogo haiwezi mfikisha kwao nikamwambia twende nyumbani maana hapa sina hela nyingine anakataa anasema basi ataenda kwa kuunganisha magari.

Sasa design ya hawa wanawake wasiojali kuhusu financial status ya mtu ni wabaya sana maana mimi licha ya kupendeza ila muonekano wangu unaonyesha kuwa naishi maisha magumu maana mwenyewe nikijiangalia kwenye kioo najiona nimebaki mifupa tuu.

Wewe dada nimekuheshimu na nimeona aibu kukufanyia ubaya sababu sina roho mbaya ila ukiendelea na utaratibu huo ipo siku utayatimba kwa wahuni ndio utajua hujui.
 
Wapo kibao hao mamwehu sio wachache ni wengi wengi wengi ukijichanganya wanakuacha mifupa mitupu Dawa yao ni mikausho mikali ukimwambia Sina ni Sina tena kwa herufi kubwa usimchekee hutaki tembea hela zinatafutwa we unataka watu wazimwage ovyo kengele
 
Pole.

Kwa uchumi uliouelezea unatakiwa ukwepe outings zitakuliza.
Sure nimekosa mpaka usingizi maana pesa yangu naipata kwa tabu sana afu inakuja kupotea kipuuzi sana maana leo nimepoteza karibia 50000 kwa wanawake.

Ni kama kuna kapepo ambako hakataki nisonge mbele yaani nikishika pesa simu za vizinga vya mademu zinaanza najikuta nishatuma hela baada ya hapo ni majuto tu.
 
Sure nimekosa mpaka usingizi maana pesa yangu naipata kwa tabu sana afu inakuja kupotea kipuuzi sana maana leo nimepoteza karibia 50000 kwa wanawake.

Ni kama kuna kapepo ambako hakataki nisonge mbele yaani nikishika pesa simu za vizinga vya mademu zinaanza najikuta nishatuma hela baada ya hapo ni majuto tu.
wanakuendesha kwa kuwa bado hujakua

Ukikua wala hawatakusumbua hata kidogo
 
Aisee hapo tatizo , sema unatokaje na demu wa aina hio na bajeti ya 30k, mademu wa namna hio kama huna hela mbinu unampanga aje getto kwako na unamwambia kabisa kuna 15k, Akija unainyumbulisha wee kisha una mpa chake anasepa.Demu anajiuza ila umehangaika na hata kuila hujaila.
 
Na hapo mwisho umekosea kumchukia

Ukiwa hivyo utachukia wengi

Kwenye outings me ndo anatoa pesa, hali ya wewe kukosa pesa imekufanya uwe sehemu ya tatizo
Wewe nani amekukaririsha hizi concepts za kwamba kwenye outings me ndio hutoa Pesa alieiprogram hio kwenye kichwa chako ni nani? Yaan wewe una bajeti yako alafu mtu mwingine anakuja kufanya kufuru wewe unasema eti me sijui kufanyaje?

Umeelewa Moral of the Story? Ameshakwambia akiokota Zombie nini hujaelewa? Au haujanisoma story vizuri? Nyinyi ndio mkipigwa masikio yakatoka damu mnaliaga vibaya sana ukanga kabisa
 
Demu anajiuza ila umehangaika na hata kuila hujaila.
Ndio kuendana na Story jamaa aliokota Malaya hio ni bila kupingwa na lengo la Malaya yoyote ni kukukomesha Malaya hana huruma na wewe lengo akupukutishe ubakie mtupu uende hujamla hio ndio furaha yake alafu siku nyingine ukijichanganya tena anakupiga alafu hupewi chini yeye ni kukukamua tu ukileta habari za kugonga chini anapiga danadana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom