Gharama za uendeshaji wa gari

HAKUNA

Senior Member
Mar 12, 2012
133
66
GHARAMA ZA UENDESHAJI WA GARI - APRIL 2012.

Watu wengi wemekuwa na mtazamo kwamba gharama ya uendeshaji wa gari linapotembea ni mafuta yanayotumika tu.

Gharama za uendeshaji wa gari zimegawanyika katika makundi 2:

1. GHARAMA ZA LAZIMA (Fixed Cost):

  • Gharama hizi hufanyika kwa mwaka:
  • Leseni ya barabarani (Road License) = Tsh. 100,000/=
  • Bima (third part insurance) = Tsh. 50,000/=
  • Ukaguzi wa gari = Tsh. 5,000/=
  • Zimamoto (Fire Sticker) = Tsh. 5,000/=
JUMLA = Tsh. 160,000/= (kwa mwaka)
KWA SIKU = Tsh. 444.44 ~ Tsh. 500/=


2. GHARAMA ZITOKANAZO NA GARI KUTEMBEA (Running Cost):


Gharama hizi zinatokana na gari kutembea, ambapo tunaweza kuangalia kwa kila kilomita (1), inagharimu kiasi gani:
  • Mafuta - Magari mengi utumiaji wa mafuta ni lita 1 kwa mwendo wa kilomita 10 - 14, inategemea na aina ya gari. Hivyo basi makadirio nitafanya kwa gari linalotumia lita 1 kwa kilomita 10. Bei ya Petrol kwa sasa ni Tsh. 2290/= kwa lita, Hivyo basi kwa kila kilomita 1 = Tsh. 229/= ~ Tsh. 230/=
  • Matengenezo (Service) - Hii hufanyika gari baada ya kutembea takribani kilomita 4000. Gari inahitaji kubadilishwa engine oil n.k. Gharama za matengenezo haya hufikia takribani Tsh.100,000/=. Hivyo basi kwa kila kilomita 1 = Tsh 25/=
  • Uchakavu (ware-out) - Gari linapotembea vipuri mbalimbali huanza kusagika/kuharibika yakiwemo matairi. Gharama hizi zinaweza kukadiriwa Tsh. 500/= kwa kilomita.
JUMLA KWA KILOMITA = Tsh. 755/=


Hivyo basi gari likitembea kilomita 10 = Tsh 7,550/= (Gharama za kutembea gari tu) + Gharama ya lazima ya siku = 500/=, itakuwa Jumla ni Tsh. 8,550/=

NB: Kwa gari ya biashara (TAXI)
>> Utahitaji malipo ya dereva kwa siku = Tsh. 10,000/=
>> Kodi

Kumbuka biashara yeyote inapaswa kupata faida isiyopungua asilimia 15% kutokana na malipo ya huduma/bidhaa.

TUNAWEZA KUPATA UWIANO WA GHARAMA ZA UENDESHAJI NA MALIPO YANAYOFANYIKA KWA HUDUMA YA TAXI NA KUANGALIA KAMA NI BIASHARA INAYOLIPA?

KWA MTAZAMO MWINGINE:

  • Kuna umuhimu wa kila Mtanzania kumiliki gari (baba na mama kila mmoja gari lake, watoto n.k), hivi tunajiuliza gharama kabla...!!!
  • Kwa nini tusiboreshe huduma za usafiri wa jamii (public transport) kuokoa fedha tunazotumia kila siku kuendesha magari.

MCHANGO ZAIDI UNAWEZA KUTOLEWA KATIKA GHARAMA ZA UENDESHAJI GARI..........!!!!!
 
asanti sana....ila naona umeongelea zaidi gari chini ya cc 1500....hebu tupe za cc juu ya hapo....
 
asanti sana....ila naona umeongelea zaidi gari chini ya cc 1500....hebu tupe za cc juu ya hapo....

Preta....nimejaribu kufanya hiyo analysis kutokana na uzoefu, kwani mimi natumia zaidi gari za chini ya cc 1500. Kama kuna ambae atakuwa na uzoefu katika magari ya uwezo wa juu bas tunaweza kushirikishana uzoefu.
 
Mchango mzuri. Umesahau parking fees karibu miji yote siku hizi zipo. Dar Shs 300.00: Morogoro Shs 200 kwa saa moja.Chukulia tuu wastani wa masaa 2 kila siku unapoingia mjini halafu ongezea kule pamoja na wale vijana wa kufuta gari na kufiuta kioo cha mbele kwa lazima.
 
Umefanya analysis nzuri lakini ungeweza pia kuangalia faida za kutumia private car ukilinganisha na public transport.
Ukienda pale posta jioni unaweza ukasubiri zaidi ya masaa mawili ndiyo upande gari, muda huo unaweza kuutumia kufanya shughuki nyingine; lakini pia private transport ni confortable and convinience na unapunguza risk ya kuibiwa vitu kama simu, pesa n.k, nenda pale Mwenge ndiyo utajua public transport ilivyo balaa!
 
Umefanya analysis nzuri lakini ungeweza pia kuangalia faida za kutumia private car ukilinganisha na public transport.
Ukienda pale posta jioni unaweza ukasubiri zaidi ya masaa mawili ndiyo upande gari, muda huo unaweza kuutumia kufanya shughuki nyingine; lakini pia private transport ni confortable and convinience na unapunguza risk ya kuibiwa vitu kama simu, pesa n.k, nenda pale Mwenge ndiyo utajua public transport ilivyo balaa!

Micha..., hapa ndipo hoja ya maboresho ya public transport inapotakiwa kuchukua nafasi yake ili kupunguza gharama za maisha.........hii nchi umasikini ni wa kujitakia............!!!, kufikiri na kutatua matatizo yanayotuzunguka limekuwa ni tatizo kumbwa......!!!!????
 
Gari ni noumaa aisee! Mtu unaweza usizione hizi gharama sababu zinakutoka wakati tofautitofauti. Ingekuta road license, bima, mafuta, service etc zinalipwa per day ungeniambia mziki wake
 
Ndio maana gari ni ghali na bila kutumia gari utatumia nn nchi yetu ndio hiyo
 
gharama za kumiliki gari kubwa sana , lakini kwa hali ya public transport ilivyo gari imekuwa kitu cha lazima...

Tatizo tz kila kitu deal, hata ikija sera ya maboresho ya usafiri wa umma, wajanja wachache watageuza deal, halafu kisifanyike kitu!!!!!
 
Tatizo la vijana wengi siku hizi wanakimbilia kununua magari (tena yenye cc kubwa) kama fashion kabla ya kukaa chini na kujiuliza kama wataweza kumudu gharama za kulitunza. Wengi wanafikiri gharama kubwa ya gari ni kwenye manunuzi wakati sio kweli. Mimi nafikiri gharama kubwa zipo kwenye uendeshaji. Kama hauna kipato cha uhakika kinachoweza kumudu hizo gharama utajikuta gari linakuongezea huzuni badala ya kukupa furaha.
 
Kuna umuhimu wa kukimbilia magari yenye cc ndogo. Lakini shida vijana hawataki hili wanataka yale makubwaaa! Ili waonekane. Jana kwenye kipindi cha The Big Story channel ya K24 wameonesha jamaa anapiga debe kwa matumizi ya Smart Car. Kigari kidogo kama kiberiti. Kuna haja ya kutumia vigari kama hivyo. Ila kwa wale wenye familia kama kijiji havitasaidia! Oups!
 
Kuna umuhimu wa kukimbilia magari yenye cc ndogo. Lakini shida vijana hawataki hili wanataka yale makubwaaa! Ili waonekane. Jana kwenye kipindi cha The Big Story channel ya K24 wameonesha jamaa anapiga debe kwa matumizi ya Smart Car. Kigari kidogo kama kiberiti. Kuna haja ya kutumia vigari kama hivyo. Ila kwa wale wenye familia kama kijiji havitasaidia! Oups!

Kwa Barabara zipi Mkuu?
 
GHARAMA ZA UENDESHAJI WA GARI - APRIL 2012.


Watu wengi wemekuwa na mtazamo kwamba gharama ya uendeshaji wa gari linapotembea ni mafuta yanayotumika tu.

Gharama za uendeshaji wa gari zimegawanyika katika makundi 2:

1. GHARAMA ZA LAZIMA (Fixed Cost):


  • Gharama hizi hufanyika kwa mwaka:
  • Leseni ya barabarani (Road License) = Tsh. 100,000/=
  • Bima (third part insurance) = Tsh. 50,000/=
  • Ukaguzi wa gari = Tsh. 5,000/=
  • Zimamoto (Fire Sticker) = Tsh. 5,000/=
JUMLA = Tsh. 160,000/= (kwa mwaka)
KWA SIKU = Tsh. 444.44 ~ Tsh. 500/=


2. GHARAMA ZITOKANAZO NA GARI KUTEMBEA (Running Cost):


Gharama hizi zinatokana na gari kutembea, ambapo tunaweza kuangalia kwa kila kilomita (1), inagharimu kiasi gani:
  • Mafuta - Magari mengi utumiaji wa mafuta ni lita 1 kwa mwendo wa kilomita 10 - 14, inategemea na aina ya gari. Hivyo basi makadirio nitafanya kwa gari linalotumia lita 1 kwa kilomita 10. Bei ya Petrol kwa sasa ni Tsh. 2290/= kwa lita, Hivyo basi kwa kila kilomita 1 = Tsh. 229/= ~ Tsh. 230/=
  • Matengenezo (Service) - Hii hufanyika gari baada ya kutembea takribani kilomita 4000. Gari inahitaji kubadilishwa engine oil n.k. Gharama za matengenezo haya hufikia takribani Tsh.100,000/=. Hivyo basi kwa kila kilomita 1 = Tsh 25/=
  • Uchakavu (ware-out) - Gari linapotembea vipuri mbalimbali huanza kusagika/kuharibika yakiwemo matairi. Gharama hizi zinaweza kukadiriwa Tsh. 500/= kwa kilomita.
JUMLA KWA KILOMITA = Tsh. 755/=


Hivyo basi gari likitembea kilomita 10 = Tsh 7,550/= (Gharama za kutembea gari tu) + Gharama ya lazima ya siku = 500/=, itakuwa Jumla ni Tsh. 8,550/=

NB: Kwa gari ya biashara (TAXI)
>> Utahitaji malipo ya dereva kwa siku = Tsh. 10,000/=
>> Kodi

Kumbuka biashara yeyote inapaswa kupata faida isiyopungua asilimia 15% kutokana na malipo ya huduma/bidhaa.

TUNAWEZA KUPATA UWIANO WA GHARAMA ZA UENDESHAJI NA MALIPO YANAYOFANYIKA KWA HUDUMA YA TAXI NA KUANGALIA KAMA NI BIASHARA INAYOLIPA?

KWA MTAZAMO MWINGINE:

  • Kuna umuhimu wa kila Mtanzania kumiliki gari (baba na mama kila mmoja gari lake, watoto n.k), hivi tunajiuliza gharama kabla...!!!
  • Kwa nini tusiboreshe huduma za usafiri wa jamii (public transport) kuokoa fedha tunazotumia kila siku kuendesha magari.

MCHANGO ZAIDI UNAWEZA KUTOLEWA KATIKA GHARAMA ZA UENDESHAJI GARI..........!!!!!
gharama ya uchakavu ya sh 500 kwa kilomita siyo sahihi kabisa.matumizi makubwa ya gari ni kwenye fuel ambayo ina account to 90% or more
 
gharama za uendeshaji wa gari - april 2012.


watu wengi wemekuwa na mtazamo kwamba gharama ya uendeshaji wa gari linapotembea ni mafuta yanayotumika tu.

gharama za uendeshaji wa gari zimegawanyika katika makundi 2:

1. Gharama za lazima (fixed cost):


  • gharama hizi hufanyika kwa mwaka:
  • leseni ya barabarani (road license) = tsh. 100,000/=
  • bima (third part insurance) = tsh. 50,000/=
  • ukaguzi wa gari = tsh. 5,000/=
  • zimamoto (fire sticker) = tsh. 5,000/=
jumla = tsh. 160,000/= (kwa mwaka)
kwa siku = tsh. 444.44 ~ tsh. 500/=


2. Gharama zitokanazo na gari kutembea (running cost):


gharama hizi zinatokana na gari kutembea, ambapo tunaweza kuangalia kwa kila kilomita (1), inagharimu kiasi gani:
  • mafuta - magari mengi utumiaji wa mafuta ni lita 1 kwa mwendo wa kilomita 10 - 14, inategemea na aina ya gari. Hivyo basi makadirio nitafanya kwa gari linalotumia lita 1 kwa kilomita 10. Bei ya petrol kwa sasa ni tsh. 2290/= kwa lita, hivyo basi kwa kila kilomita 1 = tsh. 229/= ~ tsh. 230/=
  • matengenezo (service) - hii hufanyika gari baada ya kutembea takribani kilomita 4000. Gari inahitaji kubadilishwa engine oil n.k. Gharama za matengenezo haya hufikia takribani tsh.100,000/=. Hivyo basi kwa kila kilomita 1 = tsh 25/=
  • uchakavu (ware-out) - gari linapotembea vipuri mbalimbali huanza kusagika/kuharibika yakiwemo matairi. Gharama hizi zinaweza kukadiriwa tsh. 500/= kwa kilomita.
jumla kwa kilomita = tsh. 755/=


hivyo basi gari likitembea kilomita 10 = tsh 7,550/= (gharama za kutembea gari tu) + gharama ya lazima ya siku = 500/=, itakuwa jumla ni tsh. 8,550/=

nb: Kwa gari ya biashara (taxi)
>> utahitaji malipo ya dereva kwa siku = tsh. 10,000/=
>> kodi

kumbuka biashara yeyote inapaswa kupata faida isiyopungua asilimia 15% kutokana na malipo ya huduma/bidhaa.

Tunaweza kupata uwiano wa gharama za uendeshaji na malipo yanayofanyika kwa huduma ya taxi na kuangalia kama ni biashara inayolipa?

kwa mtazamo mwingine:

  • kuna umuhimu wa kila mtanzania kumiliki gari (baba na mama kila mmoja gari lake, watoto n.k), hivi tunajiuliza gharama kabla...!!!
  • kwa nini tusiboreshe huduma za usafiri wa jamii (public transport) kuokoa fedha tunazotumia kila siku kuendesha magari.

mchango zaidi unaweza kutolewa katika gharama za uendeshaji gari..........!!!!!

good analysis
 
tatizo la vijana wengi siku hizi wanakimbilia kununua magari (tena yenye cc kubwa) kama fashion kabla ya kukaa chini na kujiuliza kama wataweza kumudu gharama za kulitunza. Wengi wanafikiri gharama kubwa ya gari ni kwenye manunuzi wakati sio kweli. Mimi nafikiri gharama kubwa zipo kwenye uendeshaji. Kama hauna kipato cha uhakika kinachoweza kumudu hizo gharama utajikuta gari linakuongezea huzuni badala ya kukupa furaha.

in cairo, more than 90% owned cars are less than 1500 cc
 
gharama ya uchakavu ya sh 500 kwa kilomita siyo sahihi kabisa.matumizi makubwa ya gari ni kwenye fuel ambayo ina account to 90% or more

Sahihi ni kiasi gani, tuko hapa kuelimishana; tupe data sahihi tuelimike....!!!
 
Back
Top Bottom