Gharama za safari na mapumziko Zanzibar

Gharama za safari na mapumziko Zanzibar

Mbavu za Mbwa

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2011
Posts
303
Reaction score
154
WanaJF!!

Ninategemea kuanza likizo ya siku 28 hivi karibuni. Katika plan yangu ninatarajia kwenda Unguja kwa mapumziko ambapo nitakaa kwa juma zima.

Msaada ninaohitaji kutoka kwenu ni huu:-
(i) Minimum na maximum ya bei ya nauli za boti
(ii) Gharama za hoteli hu-range kuanzia bei gani? Mfano, kwa mji kama Mwanza, Arusha na Dodoma, Tsh 25,000 to 30,000 unapata chumba Standard kabisa.
(iii) Gharama ya taxi (town trip) ni bei gani?
(iv) Gharama ya chakula ikoje?

Nisaidieni ili nijue kama nitamudu au lah!!!
 
Kuna Manta resort , underwater room ni us$ 900 single, us$ 1500 ukiwa na mwenza ... Kazi ni kwako
 
ImageUploadedByJamiiForums1384935097.277583.jpg

Kitu underwater bedroom, nenda kale maisha mkuu
 
Ukiwa Ngome Kongwe...nenda St. Monica room 30,000/= taxi bei poa mno kuliko dar. Kilimanjaro Boat ya Azam elfu 20.
 
ukwa na 135,000/= inakutosha wiki nzima kukaa znz ..malazi ,kunywa na kutembea sehemu mbalimbali
 
ukwa na 135,000/= inakutosha wiki nzima kukaa znz ..malazi ,kunywa na kutembea sehemu mbalimbali
Wewe usimdanganye mwenzio halafu akaja kuaibika.

135K wiki nzima? Hayo malazi tu hapo St. Monica Ngome Kongwe umeambiwa ni 30K. Kwa siku 5 tayari 150,000. Bado hujala, hujatembea, dharula, n.k.

Mi namshauri jamaa aandae kama 500K hivi kama yuko peke yake. Na kama yuko double basi kama 1M hivi.

Kumbuka haimaanishi pesa hiyo itaisha yote, lakini ni kheri ibaki kuliko kupungua.
 
Kuwa macho na ma basha wa Malindi,wale wazee nuksi tupu utawakuta macho kama mamba huku wakikukondolea macho mwanaume mwenzao! Kalale Kids Guest House iko Mtendeni Darajan ili uenjoy Zanzibar,pale hawana sheria za Uamsho isipokuwa kelele za swalaaa,swalaaa. Ukishuka chini yaani mtaani hapo ndo unakumbana na supu ya pweza! Shem unaye? Yasije kupata ya Kapuya maana supu ile huwa tunakunywa sisi wajanja halafu tunawahi mtaa wa Jozani. Kazi kwako.
 
WanaJF!!

Ninategemea kuanza likizo ya siku 28 hivi karibuni. Katika plan yangu ninatarajia kwenda Unguja kwa mapumziko ambapo nitakaa kwa juma zima.

Msaada ninaohitaji kutoka kwenu ni huu:-
(i) Minimum na maximum ya bei ya nauli za boti
(ii) Gharama za hoteli hu-range kuanzia bei gani? Mfano, kwa mji kama Mwanza, Arusha na Dodoma, Tsh 25,000 to 30,000 unapata chumba Standard kabisa.
(iii) Gharama ya taxi (town trip) ni bei gani?
(iv) Gharama ya chakula ikoje?

Nisaidieni ili nijue kama nitamudu au lah!!!


ukitaka kupumzika basi usilale hotel ya elf 30 au 40, kwani sio nzuri sana, hasa kwa zanzibar hotel ni ghali kidogo..chumba cha elf 30 sio kizuri saaaaana kwa mapumziko, kinafaa km umeenda kikazi..
unapoenda kupumzika unatakiwa upumzike kweli, na uinjoi likizo yako..sio unaenda hotel, maji hamna, au shuka mbofu mbofu, kachumba kodgoo, haina maana ni bora ukae home kwako ambako ni pazuri...

alafu wiki ni kubwa siku 3 zinatosha kabisa, zanzibar sio kubwa sana na wala hakuna masehemu meeengi ya kutembea(kwa mtizamo wangu) kwa ivo unaweza kujikuta umeboreka kama umelipia hotel kwa wiki, bora ulipie siku 3 kwanza... usiku usiache kwenda forodhani, ni pazuri kwa vyakula na kupunga upepo

nakutakia mapumziko mema, hope utakuwa na mwenzi wako..enjoy your holiday
 
ukwa na 135,000/= inakutosha wiki nzima kukaa znz ..malazi ,kunywa na kutembea sehemu mbalimbali


135,000/- kutumiwa katika wiki moja ni sawa na kuigawa hiyo hela katika mafungu 7.
So utakuwa unatumia Tsh. 19,000/- kwa siku.


Naomba nielekeze unakula wapi? Breakfast, Lunch, na dinner, kisha unalala wapi. Na je utakuwa umejifungia chumbani? au utakuwa na shughuli unasarifi bububu na kwingineko kwa kutumia usafiri gani hasa hadi hiyo 19,000 itoshe.

Kama ni hela ya kula na Mkeo ambaye unaishi naye hapo Zanzibar, basi naweza kusema hela hiyo yaweza kutosha na kubaki.

Nilidhani huu uzi unahusu wasafiri ambao wapo Unguja kwa muda mfupi. Au kuna kitu sijakielewa?

Kifupi nadhani hiyo 135,000/- ni hela ya lawalawa kwa mtu ambaye yupo Zanzibar kikazi kwa wiki akiwa mpita njia
 
Kuwa macho na ma basha wa Malindi,wale wazee nuksi tupu utawakuta macho kama mamba huku wakikukondolea macho mwanaume mwenzao! Kalale Kids Guest House iko Mtendeni Darajan ili uenjoy Zanzibar,pale hawana sheria za Uamsho isipokuwa kelele za swalaaa,swalaaa. Ukishuka chini yaani mtaani hapo ndo unakumbana na supu ya pweza! Shem unaye? Yasije kupata ya Kapuya maana supu ile huwa tunakunywa sisi wajanja halafu tunawahi mtaa wa Jozani. Kazi kwako.

Shukrani kwa ushauri. Adhana kwangu si tatizo, mi mwenyewe muislamu
 
MKUU kama unaenda kwa mapumziko kweli nakushauri usiishie stone town ! Nenda Nungwi! Kutoka stone town hadi Nungwi watakushika Dola hamsini kwa tax, kama ukipanda chai Maharage ni kwenye elfu 2500 hadi 4000!
Ukifika Nungwi kuna beach hotels nyingi, kama Amaan Bungalows, hapa kidogo ni ghali, chumba ni kuanzia dola 70 hadi 150 kwa siku, lkn kuna Nungwi in! Hapo mm ndio nafikiaga mara kwa mara. Bei zao ni mpaka dola 35 kwa night! Kama ukitaka kwenda naweza kukupatia contacts zao!
Chakula ni kuanzia elfu 9 nakuendelea inategemea na aina ya chakula!
Ukiwa huko utasahau mihangaiko yako yote wewe ni kula bata tu!
 
Mkuu ukienda zbar usiache kufika NUNGWI kule ndio wa starehe za dunia ni pazuri ajabu.unaweza kwenda kwa kukodi gari self driving au kwa hiace.
vyakula bei nzuri na hata pa kulala kutokana na hela yako.
 
Back
Top Bottom