Gharama ya kujenga chumba na sebule master

Gharama ya kujenga chumba na sebule master

Mi naona anaweza na inatosha kuna tecnolojia flana wanatumia kule mlandizi wanafyetua tofali za udongo zimechanganywa kidogo na cement its vry cheap na tofali bora sana....mbao za kupaua atatumia chache kama atatumia zile bati za kawaida(silver) choo shimo la nje kama laki tatu kila kitu ila liwe moja tu lile la round basi....inaatosha kaka...fanya utafiti wote kabla hujaanza usije kosea kitu ukaingia garama.
 
1- Tofali1800 @ 1000/= Tshs 1,800,000/=
2- Cement 30bags @13,500/= Tshs 405,000/=
3- Mchanga 5 lories @ 150,000/= Tshs 750,000/=
4- Chuma/Nondo 30pcs ya12mm @ 16,000/= Tshs 480,000/=
5- Zege 13.2 cubic metre @ 225,000/= Tshs 2,970,000/=
6- Labour charges = Tshs 1,000,000/=
7- Gharama nyinginezo = Tshs 500,000/=

Jumla ni 7.9...milioni


Huo ni mchanganuo wa gharama za ujenzi wa msingi tu peke yake na ikizingatiwa nyumba ni msingi usije jidanganya ukalipua ujenzi wa msingi itakugharimu sana baadae. Ok fikiria mpaka hapo...sasa tunafikia milioni 7.9
 
hiyo nyumba unaijenga ukanda upi!? ikiwa mikoa ya ukanda wa bahari jiandae bajeti hiyo ya foundation.
 
Umetumia ramani gani mkuu!!?

Chumba kimoja cha master nimetumia tofali 500 za block, bati 21, mbao 40, mifuko ya simenti 17, nondo 2, mchanga trip 4, ukijumlisha na vitu vingine vidogo vidogo kama maji, misumali, nk imetumika 3.7 mil pamoja na fundi. kwa hesabu hiyo choo hesabu yake haimo, lakni kama anajenga mbao za kwake, maji ya kwake, mawe ni ya karibu, mchanga ni wa karibu, anaweza kumaliza au kuongeza kidogo.

wamekuibia mafundi!
 
Mmmh!!! Sijui iweje, hyo hela mmmm!

inatosha kabisa kuishi mkuu, ila for final finishing utaongeza
-1.5 BOMA yaani msingi na ukuta (fundi)
- 1.4 roofing and roofing materials
- 1.5 blocks, hardcore,sand and coment
- 600,000 finishing - angalau 1 door and 1 window grill
Hii pia inategemea kiwanja kiko katika site nzuri au vp
 
ni vema ukaandaa makadrio ya majenzi sahihi yanayoendana na materials za ujenzi utakazotumia, hii itakusaidia sana ili mafundi nao wasijipimie chao kwa ulaji wa extra cost ambazo hazipo katika vipimo. tumia watalaamu wa majenzi kupata hesabu kamili kabla hujaanza kujenga, uelewe vema mchoro wako na gharama zake mpaka nyumba iishe. hapo hata ukianza kwa amamu basi unakuwa na ufahamu wapi utaendelea badae pesa ikipatikana
 
mie nilikua na gofu, nikalipaua weka bati , gypusm tiles umeme , bafu ndani kwa 6 mil

so approx apo unaweza ,,,kama una kiwanja utafanikiwa

Kabla sijajua hata ukubwa wa nyumba, haiwezekani

Weka mchanganuo wa gharama
1. Paa(mbao,bati,fundi)
2. Madirisha,milango
3. Gypsum,tiles
 
kujenga miaka hii uwe umekamilika kama ni kuziba kuta tu mbona hata vijijini kwa milioni moja tu kuta zinasimama na paa juu fresh
 
Input...chumba cha 3m kwa 3m kinaitaji tofati 288..hii kabla hujatoa tofali za madirisha na mlango, so idadi inaweza kupungua, na hii idadi haijajumlisha msingi coz msingi unategemea nature ya ground yako...

Calculation: tofali huwa na urefu wa 0.48m mpaka 0.50m..

Chukua urefu wa upande mmoja wa chumba gawanya kwa urefu wa tofali..
(3m/0.50m=6 tofali).

Kozi 12 zitaitaji tofali
( 12*6tofali=72tofali).
Kuta nne za chumba zitaitaji tofali ngapi..
(72*4= 288 tofali)..

Haya wenye input zaidi waongezee hapo...
 
Kujenga chumba na sebule ya kawaida bila mbwebwe za aluminium ,tiles unamaliza. Ila hutakuwa na shimo la choo.
Choo peke yake kuchimba, kujenga na kufunika si chini ya 3m.
 
Back
Top Bottom