Gharama ya kujenga chumba na sebule master

Gharama ya kujenga chumba na sebule master

Mkuu ile ilikuwa 2015 enzi za JK sasa kuna JPM hesabu zingine fyekelea mbali hesabu iliyopo ni kula lipa ada ya mtoto bas
Ha ha ha ha pole mkuu,kama unatumia formula: Kula 4 + Kodi 3 + shule 5 + usafiri 3=15 badili na iwe: Kula 2 + Kodi 1 + Shule 2 + usafiri 1 + ujenzi 9 =15,kwa kuanzia jenga nyumba ya kawaida mfano iwe na; chumba 1,sebule,jiko na choo ndani.
 
Nina kampuni ya ujenzi naomba unitafute nikupe ushauri wa kiufundi nicheki Dm.
 
Kutosha au kutokutosha itategemea mambo matatu:

1. Ukubwa wa nyumba
2. Finishing ya nyumba
3. Jeografia ya eneo unapojenga

Ukubwa wa jengo utakupa kiwango cha material, kadiri inavyokuw kubwa ndio kadiri gharama inavyoongezea

Finishing ya jengo hii inaathiri sana gharama amini kwamba kuna jiko na choo hio hela haitoshi so itategemea sana finishing yako ipoje

Jeografia ya eneo unalojenga itakwambia gharama za kusafirisha material, upatikanaji wa material, bei za material, aina ya ujenzi kama ni msingi mrefu au mfupi, na uchumi wa eneo husika utakupa gharama ya fundi.

Ila muhimu wewe anza tu kama umeamua kujenga
 
Back
Top Bottom