Tendwa ampiga `kijembe` Liundi
2009-01-03 12:00:40
Na Simon Mhina
Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini, John Tendwa, amesema kama ni kweli mtangulizi wake, George Liundi anaishi maisha ya dhiki, basi anavuna alichokipanda.
Akizungumza na Nipashe jijini Dar es Salaam jana, Tendwa alisema Liundi ambaye ni Msajili wa kwanza wa vyama vya siasa nchini na ambaye pia aliwahi kushika nyadhifa kubwa serikalini, kama alishindwa kujijengea maisha bora wakati huo, hivi sasa `atajiju`.
Akifafanua, Msajili huyo alisema ukifuatilia historia ya Liundi tangu nchi ipate Uhuru, utakuta ameshika nyadhifa kubwa ambazo zilimfanya apokee mshahara mkubwa, ambao ungemfanya ajijenge kimaisha bila hata `kuchukua chake mapema`.
``Mfanyakazi yeyote unapokuwa kazini, sio tu unalipwa mshahara, lakini pia kuna pensheni, Liundi alikuwa afisa wa juu sana serikalini.
Anaposema ana shida ananishangaza mno. Anapotoa madai kama hayo, anataka na wale waliokuwa makarani kwenye ofisi alizofanyia kazi nao wasemeje?`` Alihoji.
Tendwa alisema hatma ya mfanyakazi yeyote, inategemea sana alivyokuwa anatumia mshahara wake na marupurupu wakati akiwa kazini na kujiwekea akiba ya uzeeni.
``Sasa kama mshahara wako ulikuwa unaumaliza, lazima utapata shida. Ukiwa madarakani, unatakiwa kipato chako ukitumie vema, unatakiwa kujipanga ukijua kuwa kuna leo na kesho ukishastaafu unaubeba msalaba wako mwenyewe, vinginevyo waswahili wanasema `utajiju` hakuna wa kukusaidia,`` alisema.
Aliongeza: ``hivi sasa hata akitokea malaika, siamini kama atakuwa na nafasi nzuri ya kumsaidia Liundi kimaisha kushinda fursa ambayo Mwenyezi Mungu alimpa miaka yote,`` alisema.
Alipoulizwa kama ofisi yake inaweza kumsaidia `chochote`Liundi kwa wakati huu, Tendwa aliangua kicheko huku akisema maisha ni sawa na msichana ambaye mvulana anatakiwa amtongoze mwenyewe.
Alisema mkongwe huyo hakuona mbali, kwa vile alitakiwa atafute kiwanja sehemu nzuri kama Kibamba, Mbezi maeneo ambayo huenda aliyakataa kwa vile yalionekana kuwa shamba.
Tendwa alisema kwa kutambua hilo, ndio maana yeye amejijengea maisha yake mazuri na kamwe hategemei kuwa na dhiki ndogo ndogo hata atakapostaafu.
``Mimi ninaishi Kibamba, nimejenga zinga la nyumba, nimeweka marumaru kwa vile nahusudu usafi, kila mtu ana mapenzi na mambo anayopenda kuyapa umuhimu, kwa hiyo huyo ambaye hana nyumba nzuri, huenda alikuwa hapendi mambo hayo,`` alijigamba.
Aliongeza: ``nina shamba kubwa lenye mifugo na mimea mingi. Nikiwa nyumbani, nakula machungwa niliyopanda mwenyewe, na mimi navuna nilichopanda,`` alisema.
Hata hivyo, alifafanua kuwa, mali alizonazo ni halali kabisa na kwamba hajadokoa chochote toka serikalini.
SOURCE: Nipashe
2009-01-03 12:00:40
Na Simon Mhina
Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini, John Tendwa, amesema kama ni kweli mtangulizi wake, George Liundi anaishi maisha ya dhiki, basi anavuna alichokipanda.
Akizungumza na Nipashe jijini Dar es Salaam jana, Tendwa alisema Liundi ambaye ni Msajili wa kwanza wa vyama vya siasa nchini na ambaye pia aliwahi kushika nyadhifa kubwa serikalini, kama alishindwa kujijengea maisha bora wakati huo, hivi sasa `atajiju`.
Akifafanua, Msajili huyo alisema ukifuatilia historia ya Liundi tangu nchi ipate Uhuru, utakuta ameshika nyadhifa kubwa ambazo zilimfanya apokee mshahara mkubwa, ambao ungemfanya ajijenge kimaisha bila hata `kuchukua chake mapema`.
``Mfanyakazi yeyote unapokuwa kazini, sio tu unalipwa mshahara, lakini pia kuna pensheni, Liundi alikuwa afisa wa juu sana serikalini.
Anaposema ana shida ananishangaza mno. Anapotoa madai kama hayo, anataka na wale waliokuwa makarani kwenye ofisi alizofanyia kazi nao wasemeje?`` Alihoji.
Tendwa alisema hatma ya mfanyakazi yeyote, inategemea sana alivyokuwa anatumia mshahara wake na marupurupu wakati akiwa kazini na kujiwekea akiba ya uzeeni.
``Sasa kama mshahara wako ulikuwa unaumaliza, lazima utapata shida. Ukiwa madarakani, unatakiwa kipato chako ukitumie vema, unatakiwa kujipanga ukijua kuwa kuna leo na kesho ukishastaafu unaubeba msalaba wako mwenyewe, vinginevyo waswahili wanasema `utajiju` hakuna wa kukusaidia,`` alisema.
Aliongeza: ``hivi sasa hata akitokea malaika, siamini kama atakuwa na nafasi nzuri ya kumsaidia Liundi kimaisha kushinda fursa ambayo Mwenyezi Mungu alimpa miaka yote,`` alisema.
Alipoulizwa kama ofisi yake inaweza kumsaidia `chochote`Liundi kwa wakati huu, Tendwa aliangua kicheko huku akisema maisha ni sawa na msichana ambaye mvulana anatakiwa amtongoze mwenyewe.
Alisema mkongwe huyo hakuona mbali, kwa vile alitakiwa atafute kiwanja sehemu nzuri kama Kibamba, Mbezi maeneo ambayo huenda aliyakataa kwa vile yalionekana kuwa shamba.
Tendwa alisema kwa kutambua hilo, ndio maana yeye amejijengea maisha yake mazuri na kamwe hategemei kuwa na dhiki ndogo ndogo hata atakapostaafu.
``Mimi ninaishi Kibamba, nimejenga zinga la nyumba, nimeweka marumaru kwa vile nahusudu usafi, kila mtu ana mapenzi na mambo anayopenda kuyapa umuhimu, kwa hiyo huyo ambaye hana nyumba nzuri, huenda alikuwa hapendi mambo hayo,`` alijigamba.
Aliongeza: ``nina shamba kubwa lenye mifugo na mimea mingi. Nikiwa nyumbani, nakula machungwa niliyopanda mwenyewe, na mimi navuna nilichopanda,`` alisema.
Hata hivyo, alifafanua kuwa, mali alizonazo ni halali kabisa na kwamba hajadokoa chochote toka serikalini.
SOURCE: Nipashe