Gen Z niwakumbushe jambo moja tu: Uzee unakuja haraka sana kama mafuriko

Gen Z niwakumbushe jambo moja tu: Uzee unakuja haraka sana kama mafuriko

Muda unaonekana mrefu ukiwa na miaka 18, 20 au 25. Lakini ukweli ni kwamba miaka inapita kwa kasi ajabu. Jana ulikuwa mwanafunzi, ghafla una miaka 30 unajiuliza muda ulienda wapi.

Ndiyo maana:
• Jifunze mapema
• Fanya kazi kwa bidii
• Jenga nidhamu
• Heshimu muda
•Acha masihara na maisha
•washkaji hawatakuwepo unapotaabika uzeeni!

Kwa sababu siku moja utaamka na kugundua ujana umebaki kwenye kumbukumbu tu.

Tumia ujana wako vizuri, maana uzee hausubiri mtu...na uzee usio na rasilimali za kutosha huisha kwa mateso makali zaidi.
Wote tutakufa kwanini tuna hofu sana kana kwamba tunaishi milele! Hakuna kinachodumu milele utajiri na umaskini unapita tu. Furahia maisha kadri mungu anavyokubariki maana hatujui wakati akikubariki kufiki uzee kuwa na kitu au bila kitu ni sawa tu
 
Kasi ya kutoka 30's kwenda 40's inatisha sio kidogo. 😁

Usipotia akili utajikuta upo 40's bado unakula maskani, huna kazi huna mishe, huna hata godoro. 😁
Huu ni ukweli mchungu, kuna jamaa namfahamu alichomokea 40 sasa hivi hakamatiki kawaacha mbali hata waliomtangulia kumbe alikua anaset mipango tu
 
Huu ni ukweli mchungu, kuna jamaa namfahamu alichomokea 40 sasa hivi hakamatiki kawaacha mbali hata waliomtangulia kumbe alikua anaset mipango tu
😀 kumbe bado sana hivo, basi ngoja na mimi niendelee kuset mipango tu mpaka 60s
 
Tunatishana sana aisee hakuna cha muhimu Duniani kama furaha Yako na amani ya moyo.
Ishi tu, ukitilia kila kitu maanani unachanganyikiwa! Mwingine kajilaza zake stendi na ana amani anawaanzishi uzi wa vitisho lol!
 
Back
Top Bottom