Gen Z niwakumbushe jambo moja tu: Uzee unakuja haraka sana kama mafuriko

Gen Z niwakumbushe jambo moja tu: Uzee unakuja haraka sana kama mafuriko

N'yadikwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2014
Posts
7,988
Reaction score
12,019
Muda unaonekana mrefu ukiwa na miaka 18, 20 au 25. Lakini ukweli ni kwamba miaka inapita kwa kasi ajabu. Jana ulikuwa mwanafunzi, ghafla una miaka 30 unajiuliza muda ulienda wapi.

Ndiyo maana:
• Jifunze mapema
• Fanya kazi kwa bidii
• Jenga nidhamu
• Heshimu muda
•Acha masihara na maisha
•washkaji hawatakuwepo unapotaabika uzeeni!

Kwa sababu siku moja utaamka na kugundua ujana umebaki kwenye kumbukumbu tu.

Tumia ujana wako vizuri, maana uzee hausubiri mtu...na uzee usio na rasilimali za kutosha huisha kwa mateso makali zaidi.
 
Gen z hawana muda wakusoma maelezo mengi hayo. Watasema unaleta jangwa tu
 
Kasi ya kutoka 30's kwenda 40's inatisha sio kidogo. 😁

Usipotia akili utajikuta upo 40's bado unakula maskani, huna kazi huna mishe, huna hata godoro. 😁
 
Back
Top Bottom