Gazeti la Al-Huda lafanya uchochezi

Gazeti la Al-Huda lafanya uchochezi

Status
Not open for further replies.
Msigwa yeye ni mchungaji
na anajua tuhuma zipo za CHADEMA kuwa chama cha wakristo
hata kama hizo tuhuma si za kweli na za kutunga
hakupaswa kuwa reckless na kuanza kuita CHADEMA kanisa

Mifano ipo mingi ya kufikisha ujumbe

Kutumia mifano ya aina hiyo ni ama uzembe au kiburi na kutokujali kina nani hawatapendezwa
Chenga kidogo tu inakupoteza hata wewe .?Iam not expecting you to be a cheap man like this as the issue is very trivial.Kosa ni kusema tu CDM ni kama kanisa..ok je angeandika ni kama msikiti hilo gazeti lingeandika wakristo hawana lao kwenye chama?yaani hilo tu aah ina maana hata ule uwezo wakutafakari na pengine kupuuzia mambo madogo na kuyatafsiri ktk upotoshaji linawashinda.Au ulitaka ataje nyumba zote za ibada ili mufurahi?Je hizo tuhuma za udini ni za kweli au ni zile mbinu chafu zinazotumiwa na hao manyag`au.Nikukumbushe tu akili za kuambiwa changanya na za kwako.
Hivi akipita mtu anatangaza jamani twende msikitini kusali utasema amewabagua,hakuwajali wasiokuwa wa dini hiyo!
 
Haina maana yoyote kwa sbb wote wenye akili tulishaelewa na tunaelewa what Rev Msigwa meant tofauti na Gazeti hili lilivyoipa tafsiri kauli hiyo!

Otherwise labda km unataka tuanze kubishana kwa jambo ambalo halina maana wala kutusaidia kwa namna yoyote ile!

Bahati mbaya hawaelewi kuwa adui yao mkubwa ni CCM, badala tumjadili huyo tunaanza kuparurana hapa!
 
waache wafu wawazike wafu wenzao! Al-huda endelea wewe unawajua wafu wenzako uliowaandikia! Kweli waislamu wanaingiliwa hata huyu mwenye akilu kama hizi ni kiongozi wa kiislamu hata siamini! Waislamu wenye ufahamu mzomeeni huyo....
 
Msigwa yeye ni mchungaji
na anajua tuhuma zipo za CHADEMA kuwa chama cha wakristo
hata kama hizo tuhuma si za kweli na za kutunga
hakupaswa kuwa reckless na kuanza kuita CHADEMA kanisa

Mifano ipo mingi ya kufikisha ujumbe

Kutumia mifano ya aina hiyo ni ama uzembe au kiburi na kutokujali kina nani hawatapendezwa
Ni vigumu akili ndogo kuelewa wazo la akili kubwa!!!
 
watanzania hawatakiwi kuwa wapuuzi kwa kuendeshwa na magazeti ya kipumbavu kama hili
 
Nimefadhaishwa sana na gazeti la Al-Huda litokalo kila wiki toleo na.523 SHAWWAL1436 la tar23-29, Julai 2015 Uk wa mbele limepambwa na maneno.

Msigwa: CHADEMA kama kanisa
*Asema wanahubiri habari ya wokovu
*Wanachama waislamu sasa mashakani

Kimsingi kauli hizo ni za kichochezi dhidi ya waislam na wakristo! Ifahamike kuwa Mchungaji Msigwa(Mbunge wa Iringa) alitoa kauli hiyo kifalsafa kumkaribisha Lowassa ndani ya Chadema! Msigwa alisema "...CHADEMA ni kama kanisa, hakataliwi mtu, tunahubiri habari njema ya wokovu, unatubu unafanyakazi!"

Mimi siyo msemaji wa Msigwa lakini nimekerwa na gazeti hilo kwa sababu kauli ya Msigwa haikulenga kutugawa Wanachama wa CHADEMA kwa misingi ya kidini! Ni kama kauli ya Tundu Lissu alipotamka kuwa "...John Pombe Magufuli na kabila lake la MaCCM..." hakulenga kuwa kuna kabila la MaCCM!

Kwahiyo siyo kweli kuwa msigwa alimaanisha CHADEMA ina wafuasi wa kikristo pekee!

Naomba mamlaka husika iingilie kati! Mungu Ibariki Tanzania!
Ukiandika vitu vya kiwango hicho katika gazeti linalisomwa na watu wenye akili unajidhalilisha na kudhalilisha gazeti lako na kufanya watu wenye akili walidharau.
 
Ni vigumu akili ndogo kuelewa wazo la akili kubwa!!!

kweli! Ukiona mtu mwenye afya njema anaendeshwa na gazeti la udaku kisa lina jina la kiarabu anafikiri ni hadithi. Hapa naziona akili ndogo wala hakuna ccm hapa!
 
Haina haja ya kumuuliza Msingwa anamaanisha nini (alikuwa anaongea Kiswahili sio Kichina). Ya nini kumuuliza tena? Yeye kisha sema Chadema ni kama kanisa tena kwa lugha fasaha kabisa ya Kiswahili.

Punguzeni ushabiki usio na mantiki. Angalieni tafsiri ya moja kwa moja ktk Kiingereza, hapa ipi sahihi: Chadema is a church au Chadema is like a church?

Vv


Hawa viumbe wa ajabu sana mchungaji wao kasema Chadema ni kama Kanisa kakiri mweyewe halafu analalamikia gazeti.
 
Nyinyi akili zenu zilivyo ndogo Ramadhani Madabida anazijuwa vyema .

Jana tu BBC imereport kwamba wana chapisho la kitabu cha quran chapisho kongwe zaidi la miaka zaidi 1000 mapovu yanawatoka wakati contents ni zilezile.

Tena bunge la katiba walisahau kupendekeza kuwe na viti maalum vya waislamu bungeni, watu wa ajabu sana nyinyi.

Matola nina wasiwasi na akili zako zipo timamu?
 
Sitaki kujiingiza katika mjadala wa kidini kwani kufanya hivyo ni kupoteza muda. Hata hivyo ni lazima isemwe wazi kwamba mwenye kosa hapa ni Msigwa. Kwenye siasa usitegemee watu wafasri ulimaanisha nini. Ni lazima uwe as clear as possible ili usiwape wapinzani wako political ammunition dhidi yako. Tena ishu sensitive kama ya dini kwenye taifa kama letu ni big no! Msigwa angekuwa mwanasiasa makini angerudi mara moja na kutoa ufafanuzi alimaanisha nini hasa alipotoa kauli hiyo. Japo mi ni Mgalatia lakini kwa hili gazeti hili mnalionea tu. Muda ungalipo. Na ili kukata mzizi wa fitina Msigwa arudi mara moja na kutoa ufafanuzi wa kauli yake alimaanisha nini. This is Politics 101 hasa linapokuja suala la political crisis management.
 
ama kweli hasira, ulevi na utoto husema kweli hapa naona watu wanafumuka kwelikweli baada ya hasira,
 
Sitaki kujiingiza katika mjadala wa kidini kwani kufanya hivyo ni kupoteza muda. Hata hivyo ni lazima isemwe wazi kwamba mwenye kosa hapa ni Msigwa. Kwenye siasa usitegemee watu wafasri ulimaanisha nini. Ni lazima uwe as clear as possible ili usiwape wapinzani wako political ammunition dhidi yako. Tena ishu sensitive kama ya dini kwenye taifa kama letu ni big no! Msigwa angekuwa mwanasiasa makini angerudi mara moja na kutoa ufafanuzi alimaanisha nini hasa alipotoa kauli hiyo. Japo mi ni Mgalatia lakini kwa hili gazeti hili mnalionea tu. Muda ungalipo. Na ili kukata mzizi wa fitina Msigwa arudi mara moja na kutoa ufafanuzi wa kauli yake alimaanisha nini. This is Politics 101 hasa linapokuja suala la political crisis management.
 
Mimi nipo timamu ndio maana nimekuliiza wewe upo timamu? Maana hata mtu akikosea hupendi kusema ukweli kwa sababu ya mahaba
 
Vipi ni fahari zaidi kati ya kutukaribisha mjini then mkawa watumwa wetu??

Akina Tambaza wameacha miji wakakimbilia maporini leo mswahili anaweza miliki uwanja oysterbay??

Waswahili ni duni siku zote...

Ndugu yangu oysterbay yaleo kuna oysterbay tena?
Oystaerbay ya leo ni bar kwenda mbele na ndani ya majumba kumejaa ng'ombe na mbuzi na hata nguruwe.
Magrosary na maduka kila kona ya oystaerbay.
Kelele za mabar na dada poa kila kona.
Zamani ulikuwa ukienda oystaerbay ilikuwa unaona tofauti ya maeneo mengine.
Shoping center ilikuwa 1 tu morogoro store leo kila nyumba ina biashara mbele.
Hakunatofauti na kko.
Hakuna tena ule uzuri wa oystaerbay.
 
Nimefadhaishwa sana na gazeti la Al-Huda litokalo kila wiki toleo na.523 SHAWWAL1436 la tar23-29, Julai 2015 Uk wa mbele limepambwa na maneno.

Msigwa: CHADEMA kama kanisa
*Asema wanahubiri habari ya wokovu
*Wanachama waislamu sasa mashakani

Kimsingi kauli hizo ni za kichochezi dhidi ya waislam na wakristo! Ifahamike kuwa Mchungaji Msigwa(Mbunge wa Iringa) alitoa kauli hiyo kifalsafa kumkaribisha Lowassa ndani ya Chadema! Msigwa alisema "...CHADEMA ni kama kanisa, hakataliwi mtu, tunahubiri habari njema ya wokovu, unatubu unafanyakazi!"

Mimi siyo msemaji wa Msigwa lakini nimekerwa na gazeti hilo kwa sababu kauli ya Msigwa haikulenga kutugawa Wanachama wa CHADEMA kwa misingi ya kidini! Ni kama kauli ya Tundu Lissu alipotamka kuwa "...John Pombe Magufuli na kabila lake la MaCCM..." hakulenga kuwa kuna kabila la MaCCM!

Kwahiyo siyo kweli kuwa msigwa alimaanisha CHADEMA ina wafuasi wa kikristo pekee!

Naomba mamlaka husika iingilie kati! Mungu Ibariki Tanzania!




Acha kulalamika huo ndio ukweli wenyewe,huyo mch.Msigwa kwanini asitumie sentensi ambayo haionyeshi kuwagawa watu?
Mambo mnayojadiliana nyuma ya pazia wezenu kina msigwa wanajisahau wanayasema !! Tutasike mengi mwaka huu!
 
Vipi ni fahari zaidi kati ya kutukaribisha mjini then mkawa watumwa wetu??

Akina Tambaza wameacha miji wakakimbilia maporini leo mswahili anaweza miliki uwanja oysterbay??

Waswahili ni duni siku zote...

ooh,twendeni kwa joshua nigeria,akatupe urais.

eti wasomi,joshua na urais wa Tanzania wapi na wapi?.
ameshindwa kumpa urais jocyce banda ama goodluck jonathan akupe wewe kwa uwezo upi?.
mshaona kina salum ahmed salumu,shen,bilali wanapapatikia urais utadhani ndo kila kitu.
jk akipewa urais na joshua?.
halafu wanavaa mkanda nje na kujisifia usomi wa degree fake za ndalichako
 
Kwa staili hii ccm itaendelea kuwa madarakani milele. Viongozi lazima wachunge kauli zao na nyie wapambe wa vyama humu jf lazima mchunge points zenu na sio kupayuka tu maana inajenga chuki miongoni mwenu. Dini zenyewe zimeletwa hizi ila nyie ndo mnataka kutoana roho.
 
Huwa napata mashaka sana na CHADEMA nikiangalia comments za wafuasi wake kindaki ndaki, Mzito Kabwela, Okwi Bobab Sunzu, Nicholas n.k, maana ndio wanaoongoza ktk kukashifu uislam na waislam kwa ujumla, napenda na navutiwa mno na sera za hiki chama but kwa mambo kama haya mmhh....!!!!


Mzito kabwela na Nicholas sio watu wazuri kwa maslahi ya chadema ni heri wajiweke pembeni na chadema ili wana jf wanaopenda kujiunga na chadema wasipate Shaka kutokana na comments zao hasa linapokuja swala la udini. Wapiga kura ni waislam na wakristo jitahidi kutoegemea upande wowote kama ww ni mwanasiasa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom