Gazeti la Al-Huda lafanya uchochezi

Gazeti la Al-Huda lafanya uchochezi

Status
Not open for further replies.
Sitaki kuamini kama kuna siku itafika kutaja kanisa au msikiti ni udini..!!! Hii aibu ya wapi..?kwa hiyo kesho ikitokea muislam kasimama kataja habari ya msikiti atakua anahubiri udini..?
 
Mojawapo ya kazi za kanisa ni kuwafundisha watu wawe huru na utumwa wa dhambi ni sawa na chadema inavyofanya
inawaambia mafisadi ukweli na wanaojitambua wanahama chama.Ndicho alichokuwa anamaanisha Msigwa

Kazi za Kanisa zinafana na kazi za Chadema?
 
Waandishi wanajua vizuri Msigwa alimaanisha nini Ila wameamua kwa Maksudi kupotosha kauli Ili kupata attention na kuboost biashara
 
Wewe ndo umepotea kabisa na pengine wewe ni miongoni mwa waandishi wa gazeti hili!!

Unauliza amejuaje kama Msigwa alimaanisha hicho alichokisema mleta mada!?

Wewe hujui kusoma au kusikia na kisha ukapata mantiki (logic) ya kilichosemwa au kilichosikika?

Kama wana natatizo ya tafsiri ya mantiki kama uliyonayo wewe, hata km wangemsikia kasema "CHADEMA ni kama maji....,...................." wasingeelewa na wangekuja na tafsiri potofu tu ili mradi tu nia na lengo lao ovu litimie!!

Kubali tu ndugu yangu, gazeti hili limechemka na kujishushia hadhi na nadhani wana malengo ovu/baya nyuma yake especially kwa Msigwa mwenyewe na chama chake!

Hakuna namna nyingine unavyoweza kusema dhidi ya hili gazeti zaidi ya alichokiona mleta mada, and I agree with him/her!

Nakushukuru kwa kunikinga na mvua ya mawe inayonishukia! Naitwa John Peter M
 
Mojawapo ya kazi za kanisa ni kuwafundisha watu wawe huru na utumwa wa dhambi ni sawa na chadema inavyofanya
inawaambia mafisadi ukweli na wanaojitambua wanahama chama.Ndicho alichokuwa anamaanisha Msigwa
Fisadi dawa yake jela kama kina Yona kauli ya Mchungaji Msigwa ipo wazi wala haitaji maelezo period.
 
Hili gazeti linatoka nchi gani...msaada tafadhali
Gazeti la Mwananchi ili hapa soma.

Chadema ni kanisa la wokovuAkizungumzia taarifa hizo, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa alikifananisha chama hicho na kanisa ambalo kwa kawaida halikatai mtu, bali linawapokea wenye dhambi na kuwaongoza kufanya toba.“Chadema ni kama kanisa, hakataliwi mtu, tunahubiri habari njema ya wokovu, ukija hapa unatubu unaendelea kufanya kazi,” alisema Mchungaji Msigwa.
 
Kilichoandikwa kwenye gazeti ndicho kilichotamkwa na Msigwa nawe unakiri,sasa umechanganyikiwa nini? Gazeti limenukuu kila moja atachukua maneno hayo atachanganya na akili zake kisha ataewa, nakushangaa unayetaka kila mmoja aelewe kama wewe. Wapo ambao wana uelewa mzuri wa kupima athari ya kauli zinazotolewa na zinavyopokelewa na hadhira.
 
Democracy kwenye nchi iliyojaa wajinga ni bure kabisa. Nawasikitikia wanaokubaliana na maandishi haya
 
Udini na ukabila utaipeleka ccm kuzimu mwaka huu
 
Magazeti zaidi ya kumi yameandika hii habari au nikuwekee?

Haina maana yoyote kwa sbb wote wenye akili tulishaelewa na tunaelewa what Rev Msigwa meant tofauti na Gazeti hili lilivyoipa tafsiri kauli hiyo!

Otherwise labda km unataka tuanze kubishana kwa jambo ambalo halina maana wala kutusaidia kwa namna yoyote ile!
 
mbona mnataka kumsemea msigwa?

Mwenyewe kasha sema chadema ni kanisa, wanahubiri wokovu. kitu gani kisicho eleweka hapo? mbona kiswahili chepesi kabisa hicho au hamjui maana ya kanisa???

Thank you bro.

Watu wa ajabu sana hawa, wamezidi ubishi, sijui wanabisha nini, everything is clear.
 
Mtu anaposema "ni kama" wasomi wenzangu mnaelewa sio actual thing ni namna ya kujenga ulinganishaje ambao kimantiki sio sawa na kinachozungumzwa, mi nadhani hawo wahariri walikua na yao pia
 
Mungu aturehemu watanzania na tuendelee kuishi kwa umoja na upendo pamoja na tofauti zetu za imani.
 
Fisadi dawa yake jela kama kina Yona kauli ya Mchungaji Msigwa ipo wazi wala haitaji maelezo period.
Mafisadi na majambazi wamejaa huko ccm akina Chenge,Ngeleja,Tibaijuka ,Lowasa n.k mmeshindwa kuwapeleka mahakamani?
 
The Boss

Rais Kikwete ni Muislamu amewasaidia nini waislamu hadi anaondoka madarakani!? Hilo gazeti linaonekana linatumia plan B baada ya ile plan A ya Mizengo Pinda kuwatumia waislam kwa kuwahadaa na Mahakama ya kadhi kufanikisha ushindi wa CCM!

Tunajua waandishi wengi wa habari wanakadi za CCM si vibaya, lakini hii style inayotumika kuchafua Chadema hapo maana yake wanajichanganya wenyewe, kwakuwa bahati mbaya sana CCM mgombea wao ni mkristo anaitwa John Pombe Magufuli kwahiyo mnatuambia nini!?

Hii ni nchi yetu sote hampaswi kuturudisha nyuma tuchelewe kujadili upuuzi wenu huu wa udini baadaye mtahamia kwenye ukabila mwisho ukanda! Shame on you!

Asante sana kiongozi
 
Last edited by a moderator:
Gazeti limeripoti kama alivyosema Mchungaji wa Chadema Msigwa.

Kasema kweli Chadema ni kama Kanisa.

Sasa hapo unalishambulia gazeti kwa kosa gani, wewe umejuaje kama Mchungaji Msigwa alikuwa hana maana hiyo.

Wewe nani kakwambia kuwa msigwa anafanya kazi ya uchungaji cdm?, mbona humsemi mchungaji rwakatale kuwa ni mchungaji wa ccm?wacha hizo
 
Gazeti la Mwananchi ili hapa soma.

Chadema ni kanisa la wokovuAkizungumzia taarifa hizo, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa alikifananisha chama hicho na kanisa ambalo kwa kawaida halikatai mtu, bali linawapokea wenye dhambi na kuwaongoza kufanya toba."Chadema ni kama kanisa, hakataliwi mtu, tunahubiri habari njema ya wokovu, ukija hapa unatubu unaendelea kufanya kazi," alisema Mchungaji Msigwa.

Sawa kabisa!

Sasa tatizo la kauli hiyo ni nni kwani kwako wewe na wenzako pamoja na hawa wa gazeti?

Je, si kweli kwamba hizo ndizo kazi za kanisa? Au kosa hapo ni kulinganisha CHADEMA na ufanyaji kazi wa kanisa wa kuwakubali watu wakosefu, wenye dhambi na kuwaelekeza kutubu na kisha kuanza kuishi maisha mapya?

Au ndani ya misikiti waislamu huwa wanahubiri nini jamani? Chuki na kuwakataa wakosefu?

Je, ni makosa kusema ACT Wazalendo au chama chochote cha siasa hata CCM au CHADEMA ni kama uislamu au msikiti vile ambao haumukatai mtu yeyote ili mradi mtu anakuja na kutubu dhambi zake na kuanza kuishi maisha mapya, matakatifu yaliyojengwa ktk misingi ya dini hiyo?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom