Gavana wa Kenya amjibu Rais Magufuli kuhusu kukamata mifugo, asema uongozi wake ni aibu kwa Afrika Mashariki

Huyu gavana bila shaka atakuwa shoga weziwe wanambokowa .na a mshukuru mungu weke yupo mbali nasi
 
Wanajisumbua tu wafuate sheria na mipaka ya nchi. ova
Wale wanyarwanda wanafuata sheria za mipaka?

Wamasai wana-move all over East n' Central Africa bila vibali all those years.
Je hao intarahamwe from Rwanda nao wako hivyo au?

Kule Tabora, Geita, Kagera, Kigoma, Rukwa,Katavi wamejaa haswa nani anawafuatilia?


Kigoma, Kagera, Chato, Rukwa wapo wanafuga Mang'ombe yao mengi nani alishawauliza?
 
Unaijua katiba inayomuongoza? Nitajie kifungu alichokivunja ama kukikiuka. Taja pia amekikiukaje, nami nitakujibu kupitia hiyohiyo katiba.
Katiba yetu inatoa haki ya kukusanyika na kujieleza. Je ni kifungu gani cha katiba iliyomruhusu kupiga marufuku mambo hayo?! Pili ni kifungu gani cha katiba, inayomuelekeza kufanya matumizi nje ya budget iliyoidhinishwa na bunge ?!!
 
Na bado, tunatafuta mbinu ya kuhamisha mlima kilimanjaro usionekane upo kenya
 
Balozi wetu pale Kenya Mh Pindi Chana na mwenzake Kenya Foreign Secretary Mh Amina Mohamed wameshamaliza mtafaruku maana Diplomasia yetu aaaah bado hovyo sana
 
bora kampa fact uyu mtu mabavu yake ni aibu kwa Tz jamii za kimasai n ndugu wayback
 
Gavana wa Kaunti ya Kajiado Joseph Ole Lenku amekosoa kauli ya Rais Magufuli kuwa Tanzania sio shamba la kufugia mifugo.

Ameelezea jamii ya Wamasai upande wa Kenya na Tanzania wamekuwa na uhusiano mwema na kuwa kama kaka na dada na wamekuwa wakisaidiana kwa miaka mingi

Amesema kuna ng'ombe wengi kutokaTanzania wapo Kenya na uongozi wake umekua aibu sana kwa Afrika Mashariki kwa sababu ushirikiano uliokuwepo umeleta manufaa kwa pande zote mbili na kutumia mabavu kukamata mifugo imewaumiza watanzania na ni vyema ajue hilo

Ameongeza kujifanya unakuja na kifua mbele hakuna mahali atapeleka kifua mbele na umasikini wake ila hawatalipiza kwa Wamasai wa Tanzania waliopo Kenya kwa kuwa sio kosa lao



Huyo gavana nimwehu hii ni tz tumeandaa sehemu yakufugia kwaajili ya mifugo yetu wenyewe walijenga sehemu yao yote na kuongeza mifugo wakitegemea malisho kwetu jpm hapo upo sawa aungwe mkono lazima atakae pinga hili akapimwe akili nimwehu kushinda mwehu
 
bora kampa fact uyu mtu mabavu yake ni aibu kwa Tz jamii za kimasai n ndugu wayback
Udugu hauondoi mipaka wewe umeweka chakula kwa ajili ya wanao ghalani baadae anakuja ndugu yako ameshindwa kupangilia vyakwake anakuja kwako bilakuuliza wala kuomba utasema muache avuruge nindugu ukijuwa kufanya hivyo kutauwa watoto wako?
 
Kuna jamaa mmoja wa Kenya aliongea kwa simanzi sana, alisema "Jamani Magufuli kipenzi cha Mungu kweli ameruhusu vifaranga wasiokua na hatia kuchomwa moto? Si angewapa hata wananchi masikini wafuge kuku wapate pesa ama chakula kama aliona kuwarudisha Kenya haiwezekani? Ni kitu gani anacho zaidi ya marais watangulizi wake au marais wengine popote duniani? Very sad!" Jamaa alionesha kuumizwa sana na maamuzi ya kiongozi huyo pande hizi.
Kama vilikua na mqgonjwa je?
 
Ungewahi kuwa mfugaji usinge comment upuuzi huu. Kiangazi hakuna maji wala nyasi, wanyama wanakufa huku ukiwatazama Utafanya je?! Unazungumza kwa kuwa umezoea maisha ya mjini ya kuhemea.

Wafugaji na wakulima maisha yao hutegemea sana hali ya hewa. Na majirani hao hutegemeana zaidi kuliko hiyo mipaka. Wangefukuzwa na mali zao, kuliko kuwadhulumu na kuingiza pesa hazina !!
Kama sheria inasema wataifishwe hakuna namna lazima nchi iishimiwe vinginevyo watajua rais wao ndio anatawala mpaka huku
 
Ukiachilia mbali wamasai, wapo watanzania wengi wanafanya kazi na kuishi Kenya.Kenya tumepokelewa vizuri tu. Ushahidi soko la mitumba Nairobi- Gikomba watanzania wengi. Magu kuwa mungwana.
Mlivyoenda huko kenya si mlifuata na kutii sheria zao? Why wao hawataki kutii sheria zetu?
 
Ww acheni ushabiki wa kirofa, vile vifaranga vilikuwa na vimelea vya magonjwa ya ndege kwahiyo viachwe tu!!! Kama hujui jambo sio lazima uzungumze, utaumia na kesi isiyokuhusu
 
Hivi walishindwa kuwapiga fine tu kidogo dhidi ya kuwanyang'anya mifugo yao? Wamezaliwa lini hawa viongozi? Uhasama wa mifugo hata ulivyoisha mimi sikuamini watu walikuwa wanapoteza maisha hakuna mifano sasa unarudishwa awamu hii ya tano dadeki ugomvi dhidi ya kenya Ni upuuzi hizo ng'ombe zina gharama kuzitunza and then anazibeba kiraini zote. .. haya yetu macho
Wapigwe mnada tu wamevunja sheria wamekula nyasi zetu waharibu ardhi yetu wamekata miti yetu kwaukweli asari nikubwa
 
Tatizo ni watu kufanya mambo kwa mihemuko tu bila kufahamu chochote kuhusiana na historia hii..
Wamaasai wa kenya na tanzania huwezi kuwatenga wala kuwatofautisha kwa lolote lile, ule mpaka ulichorwa tu na ni wa kufikirika kwani wengi wao hata hawautambui
Sisi hatutaki kuwatenga hao wamaasai ila ambacho hatutaki ni wao kuleta mifugo yao kuja kuilishia kwetu,na ili kukomesha hilo ngombe wote tunawapiga chapa then tukute ngombe ambayo chapa ni mali yetu,hapa kwetu tu mifugo hairuhusiwi kutoka kijiji kimoja kwenda kingine bila kibali sembuse wa nchi nyingn?
 
Sisi hatutaki kuwatenga hao wamaasai ila ambacho hatutaki ni wao kuleta mifugo yao kuja kuilishia kwetu,na ili kukomesha hilo ngombe wote tunawapiga chapa then tukute ngombe ambayo chapa ni mali yetu,hapa kwetu tu mifugo hairuhusiwi kutoka kijiji kimoja kwenda kingine bila kibali sembuse wa nchi nyingn?
Lumumba katika ubora wako! Povu la nini wakati anaongea na rais wako?
 
Back
Top Bottom